Helikopta ikitua katika uwanja ulio jirani na nyumbani kwa Mchungaji Ambilikile Mawsapile, kijijini Samunge, jana. Mfanyabiashara Hans Macha, alikodi Helikopta hiyo kwa ajili ya kuipeleka familia yake, akiwamo Mama yake mzazi. Picha na Muhidin Sufiani

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 37 mpaka sasa

  1. hahaha..yaani huyu haponi maana ameruka foleni..so amevunja masharti mchungaji aliyoyatoa juzi..hapa ni kama anawaonea wengine wasikuwa na uwezo huo

    ReplyDelete
  2. jamani ina maana wabongo wote wanamaradhi mbona kunatisha? Haya babu dili hilo weka kila kichwa elfu 10.je kuna alopona hizo dawa?

    ReplyDelete
  3. Katika Biblia tunasoma pia kuwa Mungu alimfunulia Yakobo (Israel)kuwa watakuja watu toka mbali, wa kila kabila, na kila taifa kukusujudu. Simshangai huyo Babu Mnyakyusa mzaliwa wa Tukuyu Mbeya akifuatwa na watu toka pande zote za nchi Loliondo. Ni ufunuo wa Kibiblia. Ndagaa! Kyala akutulege fijo Mchungaji Ambilikileee!

    ReplyDelete
  4. muda sio mrefu tutaona run way imechongwa ili private jet toka mbali ziweze kutua kwa babu na kupata dozzi yake kama kawaida,wewe ukija na ndege,baiskeli,boti,punda,machera uwe na jero tu(Tsh 500)ili uweze pata matibabu yako.kazi ipo loliondo mwaka huu.Mbona hatuoni vingora vya wakubwa au wanakuja kimya kimya?

    ReplyDelete
  5. Tunakushukuru sana Mzee wetu wa Loliondo kwa kazi unayoifanya cha zaidi tunamshukuru sana Mungu kwa kusikia kilio cha wanadamu na kumtuma mtume wake aitende kazi ya uponyaji. Hatuna cha kukupa zaidi ya asante Mungu wetu. Nasi wanadamu tunatakiwa tupunguze maovu na msujudu Mungu kwa baraka zake kwetu.

    ReplyDelete
  6. Dah!hii kali amakweli babu kafunika kwa kikombe.Inaonekana hii dawa ni dili, kwani how come watu wanakomaa by any means ili kufika kwa babu.Ila bado naishaangaa serikali kwanini wasifanye utafiti wa kisayansi kujua ni kwavi inatibu.

    ReplyDelete
  7. Tafadhali nisaidie namna ya kupata helkopta hii. Nipate mawasiliano either na Hans Macha au wenye helkopta yao.

    ReplyDelete
  8. YESU ALISEMA ASIYE MGONJWA HAITAJI TABIBU. WEWE ULIYE MZIMA MSHUKURU MUNGU. WAACHE WAGONJWA WAKAPOKEE UPONYAJI. SHETANI HAWEZI KUPONYA. ANAYEPONYA NI MUNGU TU. WANAOBEZA WAKUMBUKE METHALI - USITUKANE WAKUNGA. NA WENGINE WAKASEMA KABLA HUJAFA HUJAUMBIKA. NYINYI MNAOKASHFU OMBENI MUENDELEE KUWA NA AFYA. MUNGU MBARIKI MCHUNGAJI

    ReplyDelete
  9. Fantastic Hans....treat your Mum, God will always be with you.

    ReplyDelete
  10. KILA MWENYE PUMZI YA MUNGU APUMUAYE KWA NEEMA BILA KUWA NA MARADHIO YOYOTE, INAMPASA KUMSHUKURU MUNGU SANA KWA WEMA WAKE KWA SABABU WEWE SI BORA SANA KULIKO WENGINE. NA KILA MWENYE PUMZI YA MUNGU NLAKINI ANAYO MARADHI, BASI INAMPASA KUMUONA TABIBU ALIYELETWA NA MUNGU ILI KUYATIBU MAGONJWA YAKO NA USIPUUZE! TIBA NI KWA AJILI YAKO..
    MWOMBEENI SANA MTOTO WA HUYU WA MNYONGE (BABU)AMBAYE MUNGU ALIMTOA KATIKA UZAO WA DAUDI ILI AWAONDOLEE WATU SHIDA ZAO P0AMOJA NA MARADHI YAO.

    ReplyDelete
  11. HII DAWA NI KWELI INAPONYESHA MIE MWENYEWE NIMESHUHUDIA>HII NI ZAWADI TOKA KWA MUNGU

    ReplyDelete
  12. Anon wa Thur March 17, 09:16:00 AM 2011 - Nakupa hongera sana ujumbe wako ni mzito na mzuri hivyo basi wadau aliye mzima akae kimya atuache wagonjwa lakini kumbukeni shilingi ina pande mbili na hugeuka.

    ReplyDelete
  13. Jana nilikuwa naongea na daktari hapa Duke University, Marekani, akaniambia kwa vile wanasafari ya kwenda KCMC mwezi ujao itabidi wajiandae kwa ajili ya uchunguzi zaidi. Na mimi nimesisitiza kuwa kuna dawa inaponya magonjwa ya hatari.

    Niko huku napiga debe kwa ajili ya watu kuja kufanya uchunguzi, unaweza ukakuta Babu anajengewa Loliondo World Hospital in Arusha, Tanzania, East Africa

    ReplyDelete
  14. wewe unaesema wameruka mstari nani kakwambia hapo wanatua sasa unataka watue kwenye foleni. Watu wengine mtumie akili kabla ya ku comment kwanza inatua eneo la wazi then wanaenda kupanga foleni kama wengine walivyopanga akitua penye watu panga likiwakata je? Common sense is not common to everybody

    ReplyDelete
  15. WATU WALIOKUNYWA DAWA YA BABU NA KUPONA WAJITOKEZE KUTOA UKWELI KWANI MPAKA SASA NI MAELFU WALIOKUNYWA ILA MAJIBU NI MACHACHE,KWANI KUNA WASIO NA IMANI ILI WAWEZEKUAMINI NA PUPATA MSAADA HUO.KUNA FISADI MMOJA ROSTAM AZIZ ANADAI HIYO DAWA SIO YA KWELI HEBU JITOKEZENI ILI AWAJIBIKE NA KUJIUZURU UBUNGE KWA HILI FISADI TUMELICHOKA NA LINATAKA KUWADANGANYA WATU ILI WASIPONE.
    MDAU

    ReplyDelete
  16. Haya bwana Macha, Inaonekana ni wachagga tu watakaoweza kupata huduma kwanza.

    ReplyDelete
  17. salaleeeeeee duh mpaka helikopta duh ila babu anatibu asikwambie mtu ndg yangu looooooooo

    ReplyDelete
  18. Kwanza kabisa ndg watanzania wenzangu tumshukuru mungu kwa muuijza huu aliotuletea huyu mpendwa wetu babu asante mungu. napemda kusema machache kuhusu mchungaji mwingira na kakobe wake nyie ni wezi mbele ya watu na mungu mnawaibia waumini wenu kwa kuchukua mishahara yao vitu vyao kwa faida zenu wenyewe.

    huo ni wivu nyie hamna mpya ni wadanganyifu tu tumewashtukia hatuji tena kwenye makanisa yenu igeni mfano wa babu pesa kidogo matibabu makubwa. Ndg wananchi wenzangu msiwasikilize kakobe na mwingira hawa ni matapeli tu wa kutupwa. asante babu

    ReplyDelete
  19. kudadeki....

    ReplyDelete
  20. Hivi jamani hebu niambieni ,kweli kuna mtu anaweza thibitisha na kutoa ushuhudaa???? kwamba .....kuna mtu ambaye ni HIV positive,nikimaanaisha vipimo vya hospitali vimeonyesha then kaenda kwa Ambilikile a.k.a Bubu kupata kikombe....baada ya siku kadhaa kaenda kupima na hospitali na akawa Negative????

    ReplyDelete
  21. ingelikuwa vizuri sana kama babu ange shirikiana na serekali kuchkua takwimu ya maradhi waliyokuwa nayo watu. si lazima waweke wazi maradhi gani japo kwa namba tu. kumbe watanzania ni rahisi kupigwa limbwata. kiasi tutulie kwa kila baya tunalofanyiwa....tumeshakata tamaaa sasa wacha tunywe hayo maji ya "bwana" tuzidi kutulia.

    ReplyDelete
  22. jamani naombeni msaaada kokudi helikopta bei gani??nataka kumkodishia mama yangu..

    ReplyDelete
  23. huyo annon hapo juu vipi??eti ni wachagga tuu wataokaoweza kupata huduma,kwani babu anatibu wachagga pekeyake..acha ujinga wewe

    ReplyDelete
  24. HIVI NYIE MNAOJIFANYA MNAJUA DINI...WEWE UNAWEZA KUAMINI HUYU NI NABII/MTUME.

    NDIO MAANA TANZANIA WATU WANANUNUA VIUNGO VYA BINADAMU WAKITEGEMEA KUPONA AU KUPATA UTAJIRI...SHAME ON YOU!!! HUYO NI MGANGA SIO NABII/MTUME KAMA ANAVYODAI..FUNGUA BIBILIA AU KURANI UTAJUA MAANA YA MTUME NA MTUME WA MWISHO DUNIANI. HIVI VITABU VINAZUNGUMZIA WATU WATAOJIDAI NI MITUME NK. MTUME ATAYEREJEA KABLA YA KIAMA NI YESU (NABI ISA) HAKUNA NABI MWINGINE

    ReplyDelete
  25. WADANGANYIKA....

    ReplyDelete
  26. Nilikuwepo alikuwa jamaa toka Kenya. Watu tunapona. Mimi nilikuwa na sukari kwa zaidi ya miaka 10 na cliniki yangu ilikuwa kwa Dr Abbas Kariakoo. Nimekunywa dawa jumanne tarehe 15.03.2011 na mpaka leo sijanywa dawa yoyote na nimepima sukari baada ya kula na kunywa nikakuta 9.9 mm/dl. Nawashauri wanaopuuza tiba hii waache maana sisi tuliokuwa wagonjwa tunamwomba MUNGU awape watu hawa moja ya magonjwa haya ili wajue ni nini kuwa na ugonjwa usio na tiba wala kinga. Naomba waliopona wajitokeze kutoa ushahidi ili wanaodhihaki tiba hii waaibike.

    ReplyDelete
  27. Jami mimi bado ni tomaso...Aliyepona aje atuambie...Na si kupona BP, Malaria au kisukari...Nataka nione aliyekua HIV+ na sasa ni HIV-...

    Halafu huyu baba ni myakyusa ilikuaje aende huko Loliondo...Au ndio mizizi ipo huko?

    Watu waambiane ukweli kuliko kupoteza hela hivi kwenda huko...

    na babu hajatoa neno kuhusu jinsi ya hela ya usafiri wa huko? hiyo hela ikipatikana kwa ufisadi mtu anapona au la? Watu wataiba mahela manake najua hela ya kwenda kuhiji ni lazima uipate kihalali la sivyo utakiona ukienda huko...

    ReplyDelete
  28. Shuhuda nyingi tumeziskia na aliye na imani na babu na aende hazuiwi kama anapata kibali toka kwa mungu wake.na tusipende kuhoji haya kama unaumwa kimya kimya inuka kapate kikombe.ila cha muhimu mwamini mungu zaidi kuliko mwanadamu.mungu wetu ni mungu mwenye wivu.amtegemeaye mwana huyo amelaaniwa maandiko yanasema.so msifu na kumtukuza mungu kwa atakachokukirimia.

    ReplyDelete
  29. HII NI SHIRK KUBWA. JAMANI WATANZANIA ZINDUKENI. SHIRK NI MBAYA

    ReplyDelete
  30. ndio hiyo ni shirki kubwa.yeye kama kweli anatibu kwa nini asiruhusu wasiojiweza wapelekewe dawa?analazima akupe palepale dawa unywe?asikudanganye mtu,dawa ni qur'an peke yake.

    ReplyDelete
  31. babu kweli yuko juu. Mungu baba namshukru kwa kazi aliyompa BABU NAKUOMBEA UZIDI KUWA NA NGUVU ZA KUHUDUMIA WATU WA MUNGU.

    ReplyDelete
  32. huyo babu ni muongo na maji yake machafu wewe fikilia ukiumwa homa ukwanya dozi kamili utapona hata usipoamini huyo mjinga anaweka imani mbele ili asirudiwe kudaiwa na wagonjwa wasiopona na anasema mungu kamuotesha. Mungu hatibu kwa mzizi Mungu hutibu kwa Neno.? na sirikari ya tanzania lina angaria huyo fisadi mganga anataperi watu au viongozi wa chama cha majambazi. ccm wamo

    ReplyDelete
  33. Wapendwa watu wa Tanzania sasa actually watu wasio na uwezo na wenye uwezo watibiwa na kupona kila siku. Je mnahitaji shuhuda nyingi kiasi gani ili muamini? Mtu anapoenda kupata dawa anaomba Mungu apone sio ili akufurahishe ili uamini kutokuamini kwako. Kwa wale waliopata ujasiri wa kutoa shuhuda zao it is a blessing lakini nafikiri kabisa jiwekeni katika position ya mgonjwa hata tu kwa sekunde chache, mtu anaomba Mungu amponye awe mzima. ukibahatika kushiriki furaha yake jinsi alivyopona ni vizuri lakini kama ameamua kumrudishia tu Mungu wake utukufu pia it is ok. Wewe kama huumwi usiwakataze na kudiscourage wenzako wasiende kwa babu ina maana unapenda wao waendelee kuteseka na kuumwa? Naamini unapenda wapone waache wakapone basi. Asanteni.

    ReplyDelete
  34. AnonymousMay 11, 2011

    tusubiri after kama miezi sita kama hamjaona watu wamekua machizi. kwani hospitali ni za nini if this is the case wazifunge na watu wawe refered to babu. wake up tanzanians tunarudi kwenye ujima

    ReplyDelete
  35. AnonymousJune 08, 2011

    Mungu na ashukuriwe kwa kuwatendea waja wake muujiza..... amini na utapona.

    ReplyDelete
  36. JAMANI NIMESIKIA ETI BABU KAGEUKA NYOKA NA KAKIMBILIA POLINI HABARI ZIMEZAGAA HUKU KENYA...VIPI ZINA UKWELI?

    ReplyDelete
  37. Nilienda kwa babu na mume wangu mwezi wa julai lakini sukari bado inatusumbua labda kama dawa hiyo inachukua muda mrefu kufanya kazi mwilini. Asante

    Mukumbwa

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...