Kamanda wa polisi mkoa wa Arusha,  Liberatus Sabas 

Na Veronica Kazimoto – MAELEZO

Jeshi la Polisi mkoani Arusha limekanusha taarifa ya kuachiwa huru kwa mtuhumiwa wa ujangili  Bw. Frank William Silangei maarufu kwa jina la “Ojung’s Mwarusha” mkazi wa Ngaramtoni Kibaoni iliyotolewa na gazeti moja la kila wiki.  

Akizungumza katika mahojiano kwa njia ya simu na Idara ya habari MAELEZO leo jijini Dar es Salaam, Kamanda wa polisi mkoa wa Arusha Liberatus Sabas amesema kuwa mtuhumiwa huyo mwenye umri wa miaka 32  hivi sasa yuko mahabusu na taratibu za kumfikisha  mahakamani zinaendelea kufanyika.

Kamanda Sabas ameeleza kuwa  mtuhumiwa  Silangei hajaachiwa huru kama ilivyoripotiwa na gazeti  hilo linalotoka kila Alhamis katika ukurasa wake wa kwanza na wa pili na kuongeza kuwa Jeshi la Polisi mkoani humo liko makini katika kutekeleza majukumu yake.

“Si kweli hajaachiwa, natamani ungekuwa hapa Arusha nikakupeleka mahabusu ukamuona mtuhumiwa kwa macho yako”, amesema Kamanda Sabas.

Kamanda Liberatus Sabas amesema Serikali kupitia Jeshi la Polisi  itaendelea na jitihada zake za kuhakikisha kuwa vitendo vyote vya ujangili vinatokomezwa na yeyote atakayehusika na vitendo hivyo atachukuliwa hatua za kisheria.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 16, 2013

    Mie nasema hivi, tunataka kuona amani na utulivu Arusha inasisitizwa na wahalifu woote wanao vuruga Arusha ambayo hapo awali ilikuwa tulivu sana, watu tukienda teka maji saa mbili usiku bila woga ila sasa ikipita saa kumi na mbili unaogopa kuvamiwa au kulipuliwa risasi na majangili!!! kwakweli jeshi la police mkoani Arusha tunawaomba muendelee kuwa bana wahalifu mpaka wakome kabisa. Fagia woote kabisa watuachie Arusha yeetu. Mungu awabariki sana Jeshi la Police, mkuu wa mkoa na wananchi woote kwa ujumla.

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 16, 2013

    Naomba Kamanda wa jeshi, mkuu wa mkoa wa Arusha na wana nchi woote tushirikiane kwa nguvu zoote ili kuwaondoa majambazi woote wanachafua jiji la Arusha!! kwakweli Arusha hii ya sasa hivi haifurahishi kabisa, matendo ya kijambazi na wezi wametanda kila kona mjini Arusha!! Police wachapeni woote wanao vuruga amani na mkuu wa mkoa simama Imara kabisa usikubali kuyumbishwa na wana nchi watajeni woote wanao leta tabia za uhalifu jijini humu. Msiwafiche.

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 17, 2013

    Na polisi wenyewe watambuane ni wepi waharifu na wepi waadilifu. Maana tunaweza kujidanganya kuwa jeshi la polisi linajitahidi kudhibiti lakni linashindwa labda kutokana na wahalifu kuwa ndani ya jeshi hilo kama tunavyosikia.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...