IMG_9901
Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC) Juliet Kairuki akizungumza na wageni waalikwa wakati wa uzinduzi rasmi wa Ripoti ya Uwekezaji ya Dunia ya Mwaka 2013 ambayo imejikita kiundani zaidi kuangalia muunganiko wa Mahusiano ya Kibiashara na Uwekezaji Duniani.
Bi. Kairuki amesema Tanzania imeweza kupata Uwekezaji mara dufu katika maeneo ya Mafuta na Utafiti wa Gesi Asilia katika kusukuma pato la taifa kuongeza ajira na kupambana na umaskini.
Ameongeza Muunganiko wa Biashara na uwekezaji umepata mwamko mkubwa sana kutoka kwenye makampuni makubwa duniani na umeleta fursa kwa nchi maskini na zinazoendelea kama Tanzania kuwa na uhusiano mzuri kiuchumi na nchi zilizoendelea. Uzinduzi huo umefanyika leo jijini Dar kwenye ukumbi wa mikutano wa Shirika la Kazi Duniani (ILO). Picha na Zainul Mzige.
IMG_9892
Baadhi ya wageni waalikwa kutoka taasisi mbalimbali na mabalozi wakifuatilia uzinduzi rasmi wa ripoti hiyo ya Uwekezaji Duniani.
IMG_9876
Mkuu wa Masuala ya Ufundi Ushirikiano na Huduma wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Biashara (UNCTAD) Manuela TORTORA akizungumzia umuhimu wa sera za nchi za Uwekezaji kuhakikisha zinatoa fursa ya ajira na kupunguza umaskini katika nchini zinazoendelea.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...