Juma lililopita limekuwa ni la huzuni kwa wanabiafra na tasnia ya mchezo wa mbio za pole pole (jogging) mkoa wa Dar es Salaam kwa ujumla. mwanzo mwa juma tulipokea taarifa ya msiba wa mke wa katibu Mkuu wa Temeke Jogging (Rasmi) ndugu Togocho ambapo mazishi yalifanyika maeneo ya kurasini Mivinjeni. Vilabu kadhaa vya jogging viliendelea kuonesha umoja kwa kushiriki kwenye msiba huo na mingine.
Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Biafra Henry Maseko (mwenye shati jeupe) akitoa nasaha kwenye msiba wa mke wa ndugu Togocho

Siku ya Jumatano wanachama wa Biafra kundi la watoto Mtoro Elvis na kaka yake Jimmy Elvis (pichani chini)  nao walifiwa ni bibi yao mlezi ambapo mazishi yalifanyika huko Mlandizi mkoa wa Pwani. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...