Mkurugenzi
Mtendaji wa Makampuni ya ASAS,Salim Abri akizungumza na wakazi wa mji wa
Iringa na vitongoji vyake waliojitokeza kwenye semina ya kamata fursa
twenzetu.ASAS amejitolea kiasi cha shilingi milioni tano kwa ajili ya kusaidia
vikundi vitakavyoamua kutumia fursa ya kulima vitunguu na kuendelea kuwa
wajasiliamali katika fursa mbalimbali.
Mdau mkubwa wa michezo
nchini Fredrick Mwakalebela naye alipata wasaa wa kuzungumza na wakazi wa
Iringa na kutoa kiasi cha shilingi milioni moja kwa ajili ya kuwawezesha wakazi
wa mkoa huo watakaoweza kutumia fursa ya rasilimali zilizopo mkoani hapo.
Mwakilishi kutoka NSSF Makao
Makuu Salim Khalfan, akizungumzia Fursa kwa upande wa NSSF wanavyoweza kuitumia
wakazi wa Iringa katika kupata mikopo itakayowawezesha kujikwamua kimaisha.
Mkurugenzi
wa vipindi na
uzalishaji wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba akihitimisha semina ya
Kamata fursa twenzetu mepema leo mchana ndani ya mkoa wa Iringa.
Baadhi ya wakazi wa Mkoa wa Iringa wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikitolewa kwenye semina ya Fursa kwa vijana iliyofanyika kwenye ukumbi wa Chuo cha Mtakatifu Dominic mjini Iringa,ambapo watu mbalimbali wamepata fursa ya kujua namna ya kutumia sasilimali zilizopo mkoni humo kwa ajili ya kujikwamua kimaisha.PICHA ZAIDI BOFYA MICHUZIJR.BLOGSPOT.COM

Baadhi ya wakazi wa Mkoa wa Iringa wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikitolewa kwenye semina ya Fursa kwa vijana iliyofanyika kwenye ukumbi wa Chuo cha Mtakatifu Dominic mjini Iringa,ambapo watu mbalimbali wamepata fursa ya kujua namna ya kutumia sasilimali zilizopo mkoni humo kwa ajili ya kujikwamua kimaisha.PICHA ZAIDI BOFYA MICHUZIJR.BLOGSPOT.COM






Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...