Na Sultani Kipingo
Ushindi kwa Ujerumani ulitegemewa, ukizingatia Ureno  ni kama kwamba timu ya mtu mmoja – Ronaldo. Lakini ukweli ni kwamba isingekuwa hivyo baada ya Pepe kuoneshwa kadi nyekundu katika kipindi cha kwanza. Ila mechi hii haikuwa ni juu ya Pepe, na wala haikuwa ya Miroslav Klose, na hata haikuwa juu ya Cristiano Ronaldo. Mechi yote hii ilikuwa juu ya Thomas Muller.
 Mshambuliaji huyu wa Ujerumani tayari ameshaanza mbio kuelekea kwenye mstari wa mwisho wa mfungaji bora wa michuano, baada ya kupiga mabao matatu (hat trick), na kuendelea kuinyanyasa Ureno na Ronaldo wao muda wote wa mchezo.

Hakika michuano hii ya Kombe la Dunia huko Brazil imekuwa ni ya kuvutia hadi sasa. Na mechi ya Ujerumani na Ureno ilisemwa kuwa mtanange wa mwaka. Na Ilikuwa hivyo kwa Ujerumani kuondoka na ushindi wa mabao 4-0

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 17, 2014

    Ujerumani wameshinda, Hongera, lakini mimi nawaonea huruma kama hawana haya wanapoona video ya mshambuliaji wao Muller cheating.Football is played by the rules, so if someone is prepared to cheat by acting like a baby so that the opponent is sent off, where is fair play? Pepe ni mpumbavu,hana haki ya kumgusa mchezaji mwingine kwa hasira, lakini Muller alikuwa na nia moja tu, nayo ni kumdanganya refa. FIFA waangalie video na kumnyoa nywele Muller

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...