BARAZA la Madiwani katika Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba Mkoani Kagera limewasimamisha kazi Watendaji sita wa Halmashauri kupisha uchunguzi wa upotevu na ubadhirifu wa milioni 851 za mfuko wa barabara, Mfuko wa Afya, na Mfuko wa Jimbo zilizotumika bila kufuata utaratibu na kanuni za wa fedha.
Watendaji hao sita waliosimamishwa katika kikao cha Baraza la Madiwani cha tarehe 28.01.2016 walihusika na ubadhilifu wa fedha hizo kwa kuzitumia bila kufuata kanuni, taratibu na sheria za kuomba idhini ya kuhamisha vifungu vya fedha au kubadilisha matumizi yake kutoka fungu moja kwenda fungu lingine.
Aidha, taarifa ya Kamati hiyo iliwasilishwa mbele ya Mkuu wa Mkoa, Baraza la Madiwani, Watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba, Kamati ya Ulinzi na Usalaama ya Mkoa na Wilaya Januari 27 mwaka huu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...