Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii

NAIBU Meya wa Manispaa ya Ilala na Diwani wa Vingunguti, Omary  Kumbilamoto amesema maisha ya watu wa vingunguti na uchumi wao inategemea pesa za biashara ya mbuzi.

Akizungumza na wakazi wa Vingunguti katika mkutano wa hadhara wa kueleza mambo aliyofanya ndani ya mwaka mmoja Kumbilamoto ametaja kuwa bila ya mbuzi vingunguti itakuwa maskini.

“nimejitahidi kutatua tatizo la wafanya biashara wa mbuzi ambao walitakiwa wahamishwe kupelekwa Pugu kwa kuangalia maslahi na vipato vya wakazi wa Vingunguti kuwa biashara hiyo itabaki vingunguti na itaendelea kama kawaida". amesema  Kumbilamoto.

Katika kipindi cha mwaka mmoja ambapo lengo lilikuwa kutoa shukrani, Kumbilamoto hakusahau Nyanja nyingine nyeti ikiwemo nyanja ya Afya ambapo alijitahidi kuwapatia Ambulance moja katika Hospitali ya Vingunguti ambayo ameahidi kuwa  mali ya wakazi wa  eneo hilo.

Pia hakuacha Elimu ambapo alisaidia shule ya Sekondari Miembeni kuchangia kupatikana kwa Umeme, hivyo wanafunzi kusoma bila matatizo , mambo mengine ambayo ameyagusia na kuyatolea ufafanuzi  ni pamoja na Sekta ya michezo, alitoa Mashine mbili za kufulia mashuka katika Hospitali hiyo, aliweza kushugulikia bomoa bomoa  na haki ya wafanyabiashara katika machinjio ambapo damu ilikuwa inapotea kwa wenye haki hawapati haki hiyo hivyo yeye amelishughulikia na limekaa sawa.
Naibu meya wa Manispaa ya Ilala na Diwani wa Vingunguti, Omary Kumbilamoto akiwa amekalia Cherahani mara baada ya kuikabidhi kwa kikundi cha wajasiliamali wa mtaa wa ukombozi vingunguti.
Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala na Diwani wa Vingunguti, Omary Kumbilamoto akihutubia wakazi wa vingunguti katika mkutano wa hadhara.
Mwanamuziki wa muziki wa Taarabu ,Fatma Mcharuko akitoa burudani katika mkutano huo.
wakazi wa vingunguti wakifatilia mkutano huo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...