Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii
HALMASHAURI ya Wilaya ya Mkuranga imekuja na mpango kabambe wa mfumo wa tehama ambao utaweza kusaidia mawasiliano kati ya Wananchi Wadau na Halmashauri zote nchini.

Hayo yameleezwa na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Mhandisi Mshamu Munde alipokuwa akiwasilisha mpango huo kwa wajumbe wa Mkutano wa 33 wa Jumuiya ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(ALAT) unaondelea jijini Dar es Salaam.
Munde amesema kuwa mfumo huo ambao unafahamika kama ELGA ambao unafanana kabisa na kama mfumo wa E.Gov ambapo mfumo huu utasaidia kufanya kazi kwa uraisi.

“sisi kama Halmashauri ya Mkuranga tunataka mfumo huu uweze kusambaa nchi nzima hili Halmashauri ziweze kufanya mawasiliano ya kibiashara kwa uraisi na kuwawezesha wananchi wake” amesema Mhandisi Munde

Munde ameongeza kuwa kama Halmashauri zote zitafanikiwa kutumia mfumo huu zitasaidia katika kuinua uchumi wa Viwanda kama anavyosema Mh Rais.
Anasema umefika wakati sasa kwa wakurugenzi wa Halmashauri zote kutumia mfumo huu hiliwaweze kusaidia kuinua uchumi wa Tanzania.
 Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga, Mhandisi Mshamu Munde  akizungumza na wajumbe wa Mkutano wa 33 wa Jumuiya ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(ALAT ) Juu ya mpango wa matumizi ya teknolojia ya huduma kwa njia ya mtandao ELGA.
 Wajumbe wa Mkutano wa 33 wa  Jumuiya ya Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa uliofanyika jijini Dar es Salaam.
 Wajumbe wa Mkutano wa 33 wa  Jumuiya ya Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa uliofanyika jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...