Uongozi wa Chuo kikuu cha Sokoine cha kilimo SUA umewafuturisha wanajumuia wa kiislamu wa SUA chuoni hapo.

Lengo la futari  hiyo  ni kuwakutanisha pamoja Wafanyakazi na wanafunzi chuoni hapo ili kubadilishana mawazo,kufahamiana  na kujenga mahusiano bora miongoni mwao.

Hafla hiyo ilijumuisha viongozi mbalimbali wa BAKWATA Mkoa ambao walipata nafasi ya kuzungumza na kuelezea maana nzima ya Funga na umuhimu wa elimu kwa Waislamu.
 Mwenyekiti wa Jumuiya wa Waislamu SUA Anaitwa Profesa Wahab  Kimaro akitoa neno katika wanajumuiya namna alivyoagiza Mtume Mohammad kuhusiana na Mwezi Mtukufu wa Ramadhan
 Imam wa Msikiti wa SUA, Said Msuya akitoa mawaidha wakati wa Futari iliyoandaliwa na Chuo  Kikuu Cha Kilimo cha Sokoine kwa ajili ya wanajumuiya wa wakiislaam wa Chuo hicho.
Makamu wa Mkuu wa Chuo Profesa  Raphael Chibunda(Mwenye Kanzu Nyeupe katikati Mbele) Akifurahia jambo na Viongozi wa BAKWATA mkoa wakati viongozi mbalimbali wakitoa salamu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...