TANGAZO KWA UMMA


TAARIFA KUHUSU UTHIBITISHAJI WA NYARAKA

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki inapenda kuufahamisha Umma kwamba, kuanzia tarehe 20 Mei, 2019 malipo yoyote Kwa Wizara yanafanyika kwa njia ya Kielektroniki kupitia mfumo wa GOVERNMENT ELECTRONIC PAYMENT GATEWAY (GePG).

Hivyo, wateja wote watakao hitaji kufanya malipo ya uthibitisho wa nyaraka mbalimbali zikiwemo; vyeti vya talaka, ndoa, kuzaliwa, Kifo n.k wanapaswa kabla ya kufanya malipo yoyote kuwasiliana na ofisi za Wizara kupitia vituo vyake vilivyopo Dodoma, Dar es salaam na Zanzibar ili kupatiwa ‘Control Number’ ili kufanikisha malipo husika kupitia Akaunti ya Benki ya CRDB. 

Wateja wanaoleta nyaraka hizo kwa uthibitisho, wanaendelea kukumbushwa pia kukamilisha hatua muhimu kabla ya kupatiwa ‘Control Number’ ikiwemo kupelekwa kwanza katika Mamlaka na Taasisi husika zilizotoa vyeti/nyaraka hizo ili vihakikiwe na kuthibitishwa. 

UMMA WOTE UNAOMBWA KUZINGATIA RAI KWAMBA, MALIPO YOYOTE YATAKAYOFANYIKA KINYUME NA MAELEKEZO BAADA YA TANGAZO HILI, HAYATOPOKELEWA 

Imetolewa na:
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...