Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii,Mtwara na Lindi

Mamlaka ya Mawasiliano Kanda ya Mashariki (TCRA) imetoa Msaada wa Vitu mbalimbali katika Kituo cha Raha Leo mkoani Mtwara, Shule ya Sekondari WAMA Sharaf mkoani Lindi pamoja Kituo cha Wazee Wasiojiweza mkoa huo wa Lindi kwa ya ajili ya kushiriki Idd inayotarajiwa kufanyika kesho.

Msaada huo waliotoa TCRA ni Mchele,Unga wa Ngano, Mbuzi pamoja na mafuta ya kula ikiwa kwa sikukuu na kuendelea baada ya sikukuu. 

Akizungumza wakati wa Kukabidhi misaada hiyo Kaimu Mkuu wa Kanda ya TCRA Mhandisi Ikuja Jumanne amesema kuwa Msaada huo ni kuajili ya watoto hao kushiriki sikukuu ya Idd kwani hakuna sababu Kama mamlaka kuacha jamii isiokuwa na uwezo kushindwa kushiriki sikukuu ya Idd.

Jumanne amesema kuwa wao wameandaa vitu huku wakitambua vituo na shule mahitaji mengi hivyo watafanyia Kazi changamoto zingine wakati mwingine. Aidha amesema kuwa watoto na wazee watambue wanaangaliwa kwa ukaribu ndio maana wamejitoa katika misaada hiyo. 

Akipokea msaada Msimamizi wa Kituo cha EAGT Raha Leo mkoani Mtwara Caroline Mkuwele amesema kuwa msaada huo umekuja kwa muda mwafaka na kufanya watoto washiriki sikukuu ya Idd na muda mfupi kutokana na msaada huo. 

Mkuwele amesema kuwa TCRA wamejitoa kwa nguvu zote ikiwa na kuona raha Leo wana uhitaji wa msaada. "Mmetoka mbali hadi kutufikia sisi wana Mtwara kwa kweli mmeonyesha moyo wenu unajali jamii katika utatuzi wa baadhi ya changamoto licha ya kuwepo kwa sikukuu ya Idd"amesema Mkuwele.

Nae Mkurugenzi wa Kituo cha Kulelea Wazee Wasiojiweza Simon Mnnimbo amesema kuwa TCRA inatambua watu wenye changamoto na kutaka wadau wengine waige hasa wa watu waliopembezoni.

Kwa upande wa Mwalimu wa Sekondari ya WAMA Sharaf Samson Massawa amesema kuwa TCRA amewaongoza kwa kuona Shule ya WAMA wanauhitaji wa Chakula kwa ajili ya Watoto hao kwani wapo shule na wametoka katika familia zisizo na uwezo pamoja wengine kuwa wajane.
 Picha ya pamoja ya Wafanyakazi wa TCRA Kanda ya Mashariki  wakiwa picha ya pamoja na watoto wa Kituo cha EAGT Raha Leo mkoani Mtwara.
 Kaimu Mkuu wa Kanda ya Mashariki wa TCRA Mhandisi Ikuja Jumanne akikabidhi msaada kwa msimamizi wa Kituo cha EAGT Raha Leo mkoani Caroline Mkuwele kwa ajili sikukuu ya Idd.
 Msimamizi wa Kituo cha EAGT Raha Leo mkoani Mtwara Caroline Mkuwele akitoa neno la Shukurani mara baada y ya kupokea msaada kutoka TCRA Kanda ya Mashariki.
 Vyakula Vya Msaada katika Kituo cha EAGT Raha Leo mkoani Mtwara.
 Msimamzi wa Kituo cha EAGT Raha Leo mkoani Mtwara Caroline Mkuwele akiomba na watoto Mara baada ya kupokea Msaada kutoka Kanda ya Mashariki ya TCRA
 Kaimu Mkuu wa Kanda ya Mashariki wa TCRA Mhandisi Ikuja Jumanne akitoa msaada wa vyakula katika Shule ya Sekondari ya WAMA Sharaf kwa ajili ya Sikukuu ya Idd.
 Wanafunzi wa WAMA Sharaf wakisikiliza neno kutoka TCRA
 Kaimu Mkuu wa Kanda ya Mashariki wa TCRA Mhandisi Ikuja Jumanne akizungumza katika Kituo cha EAGT Raha Leo  mkoani Mtwara.
 Shule ya Sekondari WAMA Sharaf Lindi wakiwa katika picha ya pamoja na watendaji wa TCRA Kanda ya Mashariki

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...