Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo akizungumza wakati wa kikao na ujumbe kutoka mashirika ya kimataifa yasiyo ya kiserikali ya The Pew Charitable Trusts (PEW) na Wetlands International (WI) kwa lengo la kuainisha fursa zilizolopo kwenye uhifadhi wa maeneo ya fukwe, Aprili 17, 2024 jijini Dodoma.
Mkurugenzi wa Shirika la The Pew Charitable Trusts (PEW) Bw. Simon Reddy akifafanua jambo wakati wa kikao na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo Aprili 17, 2024 jijini Dodoma.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa Shirika la The Pew Charitable Trusts (PEW) Bw. Simon Reddy (kushoto) na Bi. Julie Mulonga kutoka Wetlands International (WI) kwa lengo la kuainisha fursa zilizolopo kwenye uhifadhi wa maeneo ya fukwe, Aprili 17, 2024 jijini Dodoma.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo amesema Serikali itaendelea kufungua milango kwa wadau wenye nia ya kuchangia katika hifadhi endelevu ya mazingira.


Amesema hayo wakati wa kikao na ujumbe kutoka mashirika ya kimataifa yasiyo ya kiserikali ya The Pew Charitable Trusts (PEW) na Wetlands International (WI) kwa lengo la kuainisha fursa zilizopo kwenye uhifadhi wa maeneo ya fukwe, Aprili 17, 2024 jijini Dodoma.


Dkt. Jafo amewashukuru wadau hao kwa kutambulisha mradi huo hususan katika eneo la mifumo ya ikolojia ya mikoko na nyasi bahari kwa faida za kutunza bioanuai na kukabiliana na athari mabadiliko ya tabianchi.


Amesema taarifa za kitafiti zitakazotokana na mradi huo zitasaidia katika maandalizi ya taarifa ya nchi kuhusu mchango wa kitaifa wa kupunguza gesi joto duniani (NDC).


Tutambue Tanzania imedhamiria kupunguza uzalishaji wa gesijoto kwa asilimia 30 hadi 35 ifikapo mwaka 2030, hivyo mchango wenu utasaidia katika eneo hilo,“ amesema Dkt. Jafo huku akiwahakikishia kuwa Serikali kupitia Ofisi ya Makamu wa Rais itaendelea kuwapa ushirikiano mkubwa ili kufika malengo katika kuhakikisha mazingira yanahifadhiwa vizuri na kuwa endelevu.


Awali Mkurugenzi wa PEW Bw. Simon Reddy ameelezea mkakati wa shirika hilo katika kushirikiana na WI kutekeleza mradi huo katika maeneo ya Tanzania Bara na Zanzibar.


Ameomba ushirikiano kutoka serikalini ili kufikia malengo katika kuhakikisha utekelezaji wa mradi unakuwa wa mafanikio kama unavyotekelezwa katika nchi zingine.


Pia, Bi. Julie Mulonga kutoka WI shirika hilo limejikita zaidi katika kusaidia katika kuendeleza hifadhi pamoja na kurejesha uoto wa asili hapa nchini. 


Amesema tangu walipoanza shughuli zao wametoa mchango wao katika kupitia mpangokazi wa kuendeleza maeneo ya mikoko hususan katika Delta ya Rufiji.


Kikao hicho kimewahusisha wataalamu kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais pamoja na Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC).






KAMPUNI ya sukari ya kilombero imetangaza ushiriki wake katika kutoa msaada wa kibinadamu kwa jamii inayoishi wilaya ya Kilombero, ambayo imeathiriwa vibaya na matukio ya mafuriko yanayoendelea nchini kote yaliyo sababishwa na mvua kubwa.

Hafla hii ya utoaji msaada imefanyika katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kilombero, ambapo kampuni imetoa mchango wa tani sita za mahitaji muhimu ya chakula, ikiwa ni pamoja na maharage, unga wa mahindi, na mchele. Mchango huu unatarajiwa kusaidia zaidi ya kaya 500 zilizoathiriwa na mafuriko.

Wakati wa kukabidhi mchango huo, wenye thamani ya Shilingi za Tanzania milioni 15, Bwana Victor Byemelwa, Meneja wa Mawasiliano na Uhusiano na Wadau wa Kampuni ya Kilombero Sugar, Amesema msaada huo ni sehemu ya Programu ya Misaada ya Maafa ya kampuni. "Kilombero Sugar inaahidi kujali ustawi wa jamii yetu. Mchango wa leo unadhihirisha utayari na uadilifu wetu kwa jamii tunayoihudumia. Tumetoa msaada kwa zaidi ya familia 500, Kwa kulenga mahitaji yanayohitajika kwa haraka zaidi.

Zaidi ya hayo, Bwana Byemelwa amewahimiza wadau wengine kuunga juhudi za serikali za kusaidia jamii zilizoathiriwa na mafuriko ya hivi karibuni,Pia amesisitiza umuhimu wa hatua za pamoja dhidi ya mabadiliko ya hali ya hewa. Hii ikithibitisha tena dhamira ya Kampuni ya Kilombero Sugar kwa uhifadhi wa mazingira.

Mheshimiwa Bwn. Dunstan Kyobya, Ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Kilombero, amekiri umuhimu wa kupata msaada huo kwa wakati: Amesema "Jamii yetu imeathirika sana na mvua inayoendelea, hivyo michango iliyotolewa na hawa ndugu zetu Kilombero sugar tunaithamini sana." Ameongeza kuwa msaada huu unatokana na ushirikiano thabiti kati ya serikali na sekta binafsi katika kushughulikia masuala muhimu.

Bwn. Kyobya amefichua kuwa idadi ya kaya zilizoathiriwa na mafuriko inafikia 1,500, ambapo ameeleza kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Mlimba imeathirika hasa maeneo ya Utengule na Masagati. Amesisitiza dharura ya msaada wakati juhudi zinaendelea kurejesha miundombinu katika hali yake kabla ya maafa.

Bwana Hassan Abdallah, ambaye ni mkazi wa eneo la Msagati pia muathirika wa tukio hilo amesema kuwa. "Mafuriko yaliharibu kila kitu, yakiiacha familia yangu na mimi bila makazi. Tumepokea msaada kutoka kwa serikali na mashirika kama vile Kilombero Sugar, Kwakweli msaada huu umetusaidia kupunguza mateso tuyayopitia katika kipindi kigumu.

Kilombero Sugar Company Ltd imeendeleza ahadi yake kwa jamii kwa kutenga rasilimali kwa Programu yake ya Misaada ya Maafa, ili kupunguza athari za maafa ambayo yanaweza kuathiri maeneo inayohudumia.


By Manish Jangra, Country Head, Samsung Electronics Tanzania

If you ask me to name the most common electrical appliance that Tanzanians had at home over the past two decades, I will tell you that it was the television.

You might be surprised, but that's largely the reality compared to the current situation where almost every household activity is done with a home appliance.

If you asked anyone during that time why they didn’t buy an electric stove, kettle, refrigerator, washing machine, blender, or air conditioner, they would tell you that it was a luxury to have them and that they increased electricity expenses, thus the cost of living.

But the situation has changed significantly; many people are considering different ways to simplify their daily lives, by doing multiple things within a short time.

According to Statista, in 2024, revenue in the household appliances market in Tanzania reached 3.03 billion US dollars. This market is estimated to grow annually by 5.54% (CAGR 2024-2028).

By 2024, online sales are expected to contribute 1.1% of all revenue in the household appliances market in Tanzania. In addition, the household appliances market is expected to experience a growth of 3.9% in 2025.

This is a good sign for the growth and increase in the use of home appliances, which has for many years, been advocated for by manufacturing and distribution companies of electrical appliances.

Tanzania is among the fastest-growing economies in the continent, and proper utilization of production time is a non-debatable issue now. According to the World Bank, on Tanzania’s economic outlook, the update shows the economy has been resilient, growing by 5.2% in 2023, compared to 4.6% in 2022. And the growth for 2024 is projected at 5.6%.

It is now common to find many Tanzanian families no longer using charcoal and wasting time preparing breakfast. The presence of home appliances such as kettles and stoves has simplified and saved the time that used to be wasted in the morning. For example, several years ago, a mother or housemaid had to wake up very early to prepare breakfast for the children before school. But now, it only takes about 10 minutes because there are appliances to facilitate it.

Also, I remember in the past when it would take people the whole day to do laundry, and if you had a large family, the task could take even two days or be postponed until the following week. It was a cause of suffering for mothers or housemaids because it would take them the whole day, leaving them with indescribable exhaustion yet other household chores awaited them.

Laundry has become easier due to the existence of modern machines with great capacity and user friendliness. One prepares for laundry by making minimal preparations, leaving time for other activities.

In summary, home appliances complement many tasks, and provide time to enjoy other activities that wouldn't have been possible simultaneously. For example, it was difficult to find time for family outings and enjoyment in the past due to the whole day spent doing chores.

These developments have largely been attributed to the increased penetration and consumption of electricity in the country. According to the Tanzania eCooking Market Assessment Report conducted by the Modern Energy Cooking Services (MECS) in 2022, Tanzania has made significant progress in electricity penetration in recent years, more than doubling between 2010 and 2020 from 15% to 40%.

The government has ambitious plans for expanding electricity access and increasing production capacity, aiming for nearly 6000 MW to be added by 2026, 65% of which will be from renewable resources.

With these efforts, the fear that many customers have had in previous years will no longer be a challenge because the increase in production and access to electricity will go hand in hand with a decrease in costs. Thus, purchases and use of home appliances will further increase and reach many Tanzanians nationwide.

When discussing the use of household electrical appliances, modern technologies like AI to manage and control devices remotely will undoubtedly be included.

Manufacturers and distributors of home appliances have thought further ahead in simplifying people's daily activities. For example, with so much going on, how do you remember to turn off your home appliances? With technologies like the 3D Map View feature, first unveiled by Samsung Electronics Co., Ltd at CES 2024 and now available in all countries with SmartThings access, you can now manage their usage remotely hassle-free.

If you are among those who are afraid of having many home appliances due to electricity usage and think it's luxurious, I urge you to abandon that old-fashioned mindset.

Think about the convenience and time you'll save every day by making minimal preparations and doing other things you think are impossible.



NA EMMANUEL MBATILO, MICHUZI TV

ONGEZEKO la fedha shilingi Trilioni 10 kwenye bajeti ya Wizara ya Tamisemi imeibua matumaini kwa Wanaharakati wa masuala ya kijinsia ambapo wanatarajia itakwenda kutoa chachu ya kuinua ushiriki wa wanawake katika masuala ya uongozi na kuwaepusha na vitendo vya ukatili, unyanyasaji na kuwaondolea mazingira magumu wakati wa uchaguzi.

Hayo yamesemwa leo April 17,2024 katika Semina za Jinsia na Maendeleo (GDSS) ambazo zimekuwa zikifanyika kila Jumatano na kuwakutanisha wadau mbalimbali wa Jinsia katika viwanja vya TGNP- Mtandao Jijini Dar es Salaam.

Akizungumza wakati wa semina, Muwasilishaji Bw.Iddi Mziray amesema wamehoji kuhusiana na urejeshwaji wa mikopo ya asilimia 10 iliyoondolewa mwaka uliopita kutokana na changamoto za marejesho endapo mifumo iliyowekwa na serikali itawasaidia kujibu changamoto za wanawake wa chini ambao ndio walengwa.

"Kulikuwa na changamoto za msimu uliopita kwa wanawake, vijana na walemavu walichukua mikopo bila elimu,je mifumo hii tuliyonayo itakwenda kutatua masuala hayo na ya vikundi hewa". Amesema Mziray.

Aidha Mziray ameeleza kuhusiana na suala la miundombinu ya shule ambapo wanatarajia ongezeko la matundu vyoo pamoja na sehemu za kubadilishia taulo za kike na fedha kwa ajili ya taulo hizo ambapo wameona bajeti haijalizungumzia suala hilo moja kwa moja na tamanio lao ni kutengwa fedha kwa ajili ya masuala hayo.

Kwa Upande wake Mdau wa masuala ya kijinsia Bw.Mophat Mapunda amelipongeza bunge kupitisha Sheria ya unyanyasaji wa kijinsia kama kosa katika uchaguzi,ambapo amedai kuwa katika kanuni za uchaguzi ambazo zinatarajiwa kupitishwa hivi karibuni hazijaonesha namna ambavyo zitampa kipaumbele mwanamke.

Aidha Mapunda ameiomba serikali kuhusiana na fedha iliyotengwa kwa lengo la kutoa elimu ya masuala ya uchaguzi,iwe inakidhi kuwezesha wanawake kushiriki katika zoezi hilo ili kuongeza usawa na kuondoa suala la mfumo dume ambalo limetawala kwa jamii kubwa.

Naye, Mwanaharakati wa Jinsia Bi.Mtumwa Nindi ambaye ni mlemavu ameiomba serikali kuwapatia elimu ili wanufaike na mikopo ya asilimia 10 ambapo ameeleza kuwa mfumo huo wa porto ambao umeundwa kwa ajili ya huduma hiyo hawatambui jinsi.ya kuutumia.

TGNP kupitia semina za Jinsia na Maendeleo imekuwa ikitoa mafunzo kwa Wanaharakati namna yakupambana ili kuwa na bajeti yenye mlengo wa kijinsia ambayo itasaidia kuunda usawa kwa jinsia zote katika masuala ya fursa za uongozi pamoja na mgawanyo wa rasilimali,na umiliki wa Mali.








Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango akiagana na Waziri wa Fedha, Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango - Zanzibar, Dkt. Saada Mkuya Salum pamoja na viongozi wengine wa Shirikisho la Taasisi za Wakaguzi wa Ndani Afrika (AFIIA) mara baada ya kufungua Mkutano wa 10 wa Shirikisho hilo unaofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC).
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango akionesha tuzo aliyokabidhiwa na Shirikisho la Taasisi za Wakaguzi wa Ndani Afrika (AFIIA) wakati wa Mkutano wa 10 wa Shirikisho hilo unaofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC). Kushoto ni Waziri wa Fedha Ofisi ya Rais Fedha-Zanzibar, Dkt. Saada Mkuya Salum na kulia ni Rais wa Chama cha Wakaguzi wa Ndani Tanzania, Dkt. Zelia Njeza.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango akikabidhiwa tuzo na Rais wa Chama cha Wakaguzi wa Ndani Tanzania, Dkt. Zelia Njeza iliyotolewa na Shirikisho la Taasisi za Wakaguzi wa Ndani Afrika (AFIIA) wakati wa Mkutano wa 10 wa Shirikisho hilo unaofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC).

Waziri wa Fedha na Mipango Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dkt. Saada Mkuya akiteta jambo na pamoja Mkaguzi Mkuu wa Ndani (IAG), Bw. Benjamini Magai na viongozi wengine wa Shirikisho la Taasisi za Wakaguzi wa Ndani Afrika (AFIIA) mara baada ya kufunguliwa kwa Mkutano wa 10 wa Shirikisho hilo unaofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC).
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akiwa katika picha na Kamati ya maandalizi ya Mkutano wa 10 wa Shirikisho la Taasisi za Wakaguzi wa Ndani Afrika (AFIIA) unaofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC) Pamoja na wajumbe wengine wa mkutano.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango, akiwa katika picha ya pamoja na watoa mada pamoja na baadhi ya washiriki wa Mkutano wa 10 wa Shirikisho la Taasisi za Wakaguzi wa Ndani Afrika (AFIIA) unaofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC) mara baada ya kufungua mkutano.
Mhasibu Mkuu wa Serikali, Bw. Leornad Mkude (kushoto), akisikiliza hotuba ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa 10 wa Shirikisho la Taasisi za Wakaguzi wa Ndani Afrika (AFIIA) unaofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC).
Mkurugenzi wa Idara ya Mipango, Wizara ya Fedha, Bw. Moses Dulle (wa kwanza kiti cha pili) na Mkaguzi Mkuu wa Ndani Msaidizi Bw. Mwanika Semroki, wakisikiliza mada zilizokuwa zinatolewa wakati wa Mkutano wa 10 wa Shirikisho la Taasisi za Wakaguzi wa Ndani Afrika (AFIIA) unaofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC).


Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Rasilimali watu Wizara ya Fedha Bw. Lisius Mwenda, (wa kwanza kulia), akifuatilia hotuba ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa 10 wa Shirikisho la Taasisi za Wakaguzi wa Ndani Afrika (AFIIA) unaofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC).

(Picha na Kitengo cha Mawasiliano, Wizara ya Fedha)

Na Mwandishi Wetu,Rufiji

Wananchi walioathiriwa na mafuriko wilayani Rufiji wameiona thamani na umuhimu wa uwepo wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania - TAWA baada ya leo Aprili 16, 2024 kupokea misaada mbalimbali kutoka kwa taasisi hiyo yenye thamani ya shillingi millioni 20 ikiwemo tani 6.4 za unga wa sembe, Kilo 666 za maharage na magodoro 186.

Kwa niaba ya Kamishna wa Uhifadhi wa TAWA akimkabidhi misaada hiyo Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe. Abubakari Kunenge, Kamishna Msaidizi mwandamizi Abraham Jullu amesema TAWA imeguswa na janga la mafuriko lililowapata majirani na wadau namba moja wa uhifadhi wananchi wa Rufiji ambao wamehusika kwa kiasi kikubwa kulinda rasilimali za Hifadhi ya Selous na hivyo imelazimika kuwashika mkono.

Jullu amesema tangu changamoto hii ya mafuriko imejitokeza TAWA ilifika kwa haraka na kuongeza nguvu kwa kutoa kikosi cha Askari 24 ili kusaidia katika zoezi la uokozi ikiwa ni pamoja na kutoa elimu ya mbinu za kujikinga na madhara yatokanayo na wanyamapori wakali na waharibifu hususani mamba na viboko kwa jamii ambapo mpaka sasa TAWA imetoa elimu hiyo kwa wananchi wapatao 4,225 na bado inaendelea na zoezi hilo.

Sanjari na hilo, TAWA imetoa boti moja lenye uwezo wa kubeba jumla ya watu 15 ili kusaidia katika shughuli za uokozi zinazoendelea wilayani humo.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe. Abubakari Kunenge amemshukuru Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kupeleka misaada mbalimbali kupitia Serikali na Chama Cha Mapinduzi tangu wilaya hiyo ipate changamoto hiyo ya mafuriko.

Pia amewashukuru Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TAWA Mej. Jen. (Mstaafu) Hamis Semfuko na Kamishna wa Uhifadhi wa TAWA Mabula Misungwi Nyanda kwa maamuzi ya haraka waliyoyafanya kupeleka misaada hiyo kwa wananchi wa Rufiji kwa wakati.

Mkuu huyo wa Mkoa ameendelea kuishukuru TAWA kwa msaada wa boti kwa ajili ya kufanya shughuli za uokozi na ushiriki wao wa ujumla katika zoezi la uokozi kwa kushirikiana na vyombo mbalimbali vya dola na kukiri kuwa wananchi wa Rufiji wanaona thamani na umuhimu wa uwepo wa Taasisi hiyo Mkoani Pwani.

Licha ya kuishukuru TAWA, Mkuu wa wilaya ya Rufiji Meja Edward Gowele amesema TAWA imekuwa na mahusiano na mashirikiano mazuri kati yake na uongozi wa wilaya yake ndio maana imekuwa rahisi kwao kuitikia wito wa kutoa msaada kufuatia janga lililoikumba wilaya hiyo.
 

Mkuu wa Mkoa wa Pwani  Abbakari  Kunenge alizungumza wakati wa kupokea msaada kutoka TAWA kwa ajili walioarhiriwa na mafuriko Rufiji na Kibiti.

 

Picha za makabidhiano ya msaada uliotolewa na TAWA.

 

Matukio ya picha mara baada ya kukabidhiana  msaada.

*Kikao cha kugushi walipeleka hazina ajili ya hiyo bajeti

Na Chalila Kibuda,Michuzi Blog

Fedha zilizobadilishwa matumizi bila kuidhinishwa na mamlaka husika na utumiaji wa nyaraka za kubadili matumizi ya udanganyifu kiasi cha Sh. bilioni 4.88

Ukaguzi ulibaini kwamba mamlaka nne za serikali za mitaa zilibadilisha matumizi ya kiasi cha Sh.bilioni 4.88bila kupata idhini kutoka kwa mamlaka husika, zikiwamo Baraza la Madiwani na Waziri wa Fedha.

Halmashauri iliyobanika katika ripoti ya CAG kati ya hizo ni Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe mkoani Katavi ilipanga kutumia bajeti ya kiasi cha Sh.bilioni 7.06 kwa
ajili ya kulipa mishahara hata hivyo, bajeti hiyo ilibadilishwa kwa
kuongeza kiasi cha Sh.bilioni 2.07. Kati ya kiasi kiasi hicho kilichotengwa Sh.bilioni 1.61 tu ndizo zilizotumika.

Pia ukaguzi ulibaini nyaraka za mihutasari ya kikao cha kamati ya fedha, mipango na uongozi kilichofanyika tarehe 5 Juni 2023 zilighushiwa na kuwasilishwa Hazina kwa ajili yakuombakibali cha kubadili vifungu vya bajeti ya mishahara, ingawa kikaohicho hakikufanyika kama inavyoelezwa kwenye.

Hii ni kinyume na Kifungu Na.41(2) cha Sheria ya Bajeti, [Sura ya 439], ambacho kinaeleza kwamba ofisa masuuli hatabadilisha matumizi ya fedha endapo fedha hizo zinapaswa kuhamishwa kwenda kwa mtu au kwa taasisi zingineza serikali.


Maombi ya kubadilisha matumizi ya fedha yanapaswa kuambatishwa na taarifa inayoelezea kikamilifu sababu za ukosefu wa fedha zilizoidhinishwa awali. Baada ya kujadiliwa na kamati ya fedha mipango na uongozi, maombi hayo huwasilishwa kwa Baraza la Madiwani kwa ajili ya kuidhinishwa.


Pia, Kifungu cha 41(1&2) cha Sheria ya Bajeti, [Sura ya 439], kinaruhusu
ofisa masuuli, kwa idhini ya waziri, kubadili matumizi kutoka kwenye
matumizi yaliyoidhinishwa.

Hata hivyo, Ofisa masuuli hatabadili matumizi ya fedha katika mazingira yafuatayo ambapo fedha zimetengwa kwa ajili ajili ya kazi maalum fedha zilizotengwa kwa ajili  ya kuhamishwa kwenda kwa mtu au taasisi zingineza serikali fedha zilizotengwa kwa ajili ya matumizi ya shughuli zinazohusiana  na maendeleo fedha zilizotengwa kwa ajili ya mishahara kwenda kwenye matumizi mengine yasiyo ya mishahara na uhamishaji wa fedha mwingineo unaweza kusababisha ukiukwaji wa kanuni za kifedha.
NA EMMANUEL MBATILO, MICHUZI TV

WIZARA ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imeahidi kusimamia na kutekeleza ipasavyo utolewaji wa elimu ya masuala ya fedha kwa wanafunzi wa elimu ya juu ili taifa liweze kuwa na wataalam bobezi wa masuala ya kifedha.

Kauli hiyo imetolewa leo Aprili 17, 2024 Jijini Dar es salaam na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe.Omary Kipanga wakati akifungua warsha ya siku tatu kwa viongozi wa vyuo mbalimbali nchini ili kujadili mitaala ya elimu ya fedha kwa wanafunzi wa elimu ya juu huku ukiratibiwa na Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Amesema suala la elimu ya fedha kwa jamii ni muhimu kwa maendeleo ya nchi hivyo ni vyema elimu hiyo ikafika kwa jamii Ili watanzania waweze Kupata elimu ya masuala ya fedha.

Aidha Naibu Waziri Kipanga amesema serikali ya awamu ya sita imedhamiria kujenga uelewa wa masuala ya fedha kwa jamii.

“Wizara tutahakikisha elimu ya fedha inafundishwa katika mfumo wa elimu nchini hivyo twende kwa haraka kuhakikisha vijana ambao ni sehemu ya jamii nchini wanakuwa na uelewa wa masuala ya fedha hivyo natarajia wakuu wa vyuo mtabeba uelewa huo muhimu kwa vyuo vyetu nchini,” amesema Mhe. Kipanga.
.
Pamoja na hayo amesema kuwa BoT, itaendelea kusimama na vyuo na taasisi za elimu na Wizara ya Elimu katika kuhakikisha dhana ya elimu hiyo inakuwa endelevu na inafundishwa katika ngazi za jamii hata katika elimu zisizo rasmi.

Hata hivyo ameviagiza vyuo vikuu kushirikiana na BoT kufanya tathmini ya utekelezaji wa mpango huo ili kuboresha mbinu na nyenzo za kufikisha ujumbe huo kwa jamii.

“Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ipatiwe taarifa ya tathmnini mtakazofanya ili itusaidie katika kufanya maamuzi, serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan imedhamiria kujenga uelewa wa masuala ya fedha kwa jamii,” amesema.

Kwa upande wake Naibu Gavana Benki Kuu ya Tanzania Bi. Sauda Msemo amebainisha kuwa lengo la kutoa elimu ya fedha kwa Vijana wa kitanzania wanaosoma elimu ya juu ni kuwawezesha kupata ujuzi na uzoefu wa matumizi ya fedha.

Amesema takwimu ya Sensa ya Watu na Makazi mwaka 2022 inaonesha takribani watu asilimia 34.5 ni vijana walio na umri kati ya miaka 15-35 hivyo ili kuleta tija na ufanisi katika masuala ya uchumi ujuzi na uzoefu wa masuala ya fedha ni moja ya sifa muhimu kufikia azma hiyo.

Ameeleza kuwa elimu ya fedha kwa Watanzania kutachochea maendeleo kwa kuongeza utumiaji rasmi wa huduma za fedha na kuwawezesha watu wengi kuwa na uwezo wa kufanya maamuzi sahihi ya kifedha na kuendesha shughuli zao kwa ufanisi kukuza uchumi kwa ujumla.

Bi. Sauda mesema elimu kwa vijana wa vyuo vikuu itawasaidia kuweka akiba, kupanga bajeti na kufanya uamuzi wa masuala ya fedha kwa kuzingatia viashiria hatarishi na kuelewa taasisi mbalimbali zinazotoa huduma za fedha ili kufanya maamuzi sahihi ya fedha ili waitawale.

” Tunatarajia kujenga ‘displine’ ya fedha kupitia elimu ya fedha kwani watakuwa na uwezo wa kutawala fedha sio fedha kuwatawala vijana hao,” amesema.

Pia amesema BoT kwa kushirikiana na wadau wengine wa Baraza la Huduma Jumuishi za Fedha, imetoa muongozo na mtaala wa elimu ya fedha kwa wakufunzi ambao utatumika na taasisi za elimu ya juu kwa kuwafundisha watoa huduma za elimu ya fedha kuwafikia wananchi wote walio nje mfumo wa elimu.

“Tayari tumeingia makubaliano na baadhi ya taasisi zaa elimu katika mtaala huo wa kufunzi wa fedha na tulioingia nao makubaliano ni Chuo Kikuu cha Iringa, Zanzibar, Chuo Kikuu cha Usimamizi wa Fedha(IFM) na Chuo cha Benki Kuu ya Tanzania ,” ameseama.

Katika warsha hiyo imebainishwa kuwa elimu ya fedha inapaswa kumfikia kila mmoja ili aweze kuwa na nidhamu katika matumizi ya pesa lakini kuepuka kuingia kwenye sitofahamu ambayo inawakuta wengi hasa wanapokwenda kwenye taasisi za mikopo.
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe.Omary Kipanga akizungumza wakati akifungua warsha ya siku tatu kwa viongozi wa vyuo mbalimbali nchini ili kujadili mitaala ya elimu ya fedha kwa wanafunzi wa elimu ya juu huku ukiratibiwa na Benki Kuu ya Tanzania (BoT). Hafla hiyo imefanyika leo Aprili 17, 2024 katika ukumbi wa BoT Jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe.Omary Kipanga akifungua warsha ya siku tatu kwa viongozi wa vyuo mbalimbali nchini ili kujadili mitaala ya elimu ya fedha kwa wanafunzi wa elimu ya juu huku ukiratibiwa na Benki Kuu ya Tanzania (BoT). Hafla hiyo imefanyika leo Aprili 17, 2024 katika ukumbi wa BoT Jijini Dar es Salaam.


 Naibu Gavana Benki Kuu ya Tanzania Bi. Sauda Msemo akizungumza wakati wa ufunguzi wa warsha ya siku tatu kwa viongozi wa vyuo mbalimbali nchini ili kujadili mitaala ya elimu ya fedha kwa wanafunzi wa elimu ya juu huku ukiratibiwa na Benki Kuu ya Tanzania (BoT). Hafla hiyo imefanyika leo Aprili 17, 2024 katika ukumbi wa BoT Jijini Dar es Salaam.


Viongozi wa Vyuo Vikuu mbalimbali nchini wakiwa kwenye ufunguzi wa warsha ya siku tatu kwa viongozi wa vyuo mbalimbali nchini ili kujadili mitaala ya elimu ya fedha kwa wanafunzi wa elimu ya juu huku ukiratibiwa na Benki Kuu ya Tanzania (BoT). Hafla hiyo imefanyika leo Aprili 17, 2024 katika ukumbi wa BoT Jijini Dar es Salaam.

(PICHA ZOTE NA EMMANUEL MBATILO)
MBUNGE wa Jimbo la Nanyamba Abdallah Chikota,akichangia mjadala wa bajeti ya Ofisi ya Rais TAMISEMI 2024/25 bungeni jijini Dodoma.

Na Mwandishi Wetu, DODOMA

MBUNGE wa Jimbo la Nanyamba Abdallah Chikota amempongeza Mhe. Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa kuanzisha kongani ya viwanda vya kubangua korosho mkoani Mtwara.

Alitoa pongezi hizo jana bungeni jijini hapa wakati wa mjadala wa bajeti ya Ofisi ya Rais TAMISEMI 2024/25, alisema kongani hiyo itasaidia uzalishaji wa ajira kwa wakazi wa mkoa huo.

“Tunamshukuru Rais kwa mradi wa umwagiliaji wa Arusha chini, ujenzi wa viyuo vya afya vitatu, mradi wa TACTIC, ujenzi wa stendi mpya ya mabasi na ujenzi wa barabara ya lami kilomita tano,” alisema Chikota.

Alimpongeza Waziri wa Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mohamed Mchengerwa na Manaibu Waziri wake kwa uchapakazi wao na kushughulikia hoja za wabunge.

Hata hivyo, alisema jimboni kwake yapo matatizo yanayohisiana na miundombinu ambapo mbali na kuupungeza Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini (TARURA) alisema wakala huo unakabiliwa na upungufu wa Wahandisi wa barabara.

Alisema meneja wa TARURA katika jimbo lake anahudumia wilaya tau ambazo ni Masnispaa ya Mtwara, Halmashauri ya Mtwara na Halmashauri ya Mji wa Nanyamba.

Alipendekeza kuwa TAMISEMI ipewe kibali maalum cha kuajiri Wahandisi wa barabara kwaajili ya kupelekwa wilayani.

Alisema upungufu wa watumishi pia upo katika sekta ya afya ambapo katika mkoa wa Mtwara kuna upungufu wa 6.088 waliopo ni 2,153 ambao ni upungufu wa asilimia 65.

Katika sekta ya elimu alisema kuna upungufu wa walimu ambapo aliishauri TAMISEMI kuhakikisha inatoa kibali cha walimu 300 kuajiriwa katika Halmashauri ya Nanyamba.

Alisema mapato ya serikali za mitaani madogo na vyanzo vingi si vya ukakika na vichache vilivyopo havisimamiwi vizuri.

“Halmashauri nyingi zinategemea ushuru wa mazao kama chanzo muhimu cha mapato yake. Vyanzo vingi vya uhakika vipo serikali kuu,” alisema Chikota.

Alisema kwasababu wizara imetenga Zaidi ya Sh. Bilioni 190 kwaajili ya ununuzi wa magari ya viongozi basi Mkuu wa Wilaya ya Mtwara anunuliwe gari jipya kwasababu lililopo halimwezeshi kutimiza majukumu yake vizuri.

MAADHIMISHO ya Sherehe za Mei Mosi Kitaifa kwa Mwaka 2024 yanatarajiwa kufanyika Jijini Arusha katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid na Mgeni Rasmi atakuwa Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Aprili 17, 2024 Jijini Arusha, Rais wa TUCTA, Tumaini Nyamhokya amesema maadhimisho hayo yataenda sambamba na michezo mbalimbali ya Mei mosi itakayofunguliwa rasmi siku ya Jumamosi tarehe 20 Aprili 2024 na Wazri wa Kazi, Vijana Ajira na Watu wenye Ulemavu Mhe. Deogratious Ndejembi.

Amesema Maadhimisho hayo yameratibiwa na Vyama vyote 13 vinavyounda Shirikisho la vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) ambavyo ni; - CHODAWU, COTWU (T), CWT, DOWUTA, RAAWU, TALGWU, TAMICO, TASU, TEWUTA, TRAWU, TPAWU, TUGHE na TUICO.

"TUCTA imeshirikiana na vyama vyote vilivyo nje ya TUCTA vilivyojitokeza katika maandalizi haya ya Sherehe za Mei Mosi ambayo yatakuwa ya aina yake". Amesema

Pamoja na hayo amewahimiza Wafanyakazi wote waliopo Mkoa wa Arusha na Mikoa ya Jirani kujumika kwa pamoja siku ya kilele cha maadhimisho ya Mei mosi Kitaifa ili kusherekea kwa pamoja na kuienzi siku hiyo muhimu kwa wafanyakazi Duniani.








Top News