Kampuni ya mabingwa wa vifaa vya kielektroniki Haier wamefanya mkutano wa uzinduzi wa bidhaa za viyoyozi (AC) katika ukumbi wa Hyatt regency, the kilimanjaro hotel, jijini Dar es Salaam mnamo tarehe 19.04.2024.

Mkutano huo ulihudhuriwa na wadau na watumiaji wa bidhaa za kielekroniki wakiwemo wataalam mbalimbali wa ujenzi, wasanifu majengo, wafanyabiashara wa vifaa vya kilektroniki, taasisi mbalimbali za kiserikali na wafanyakazi wa makampuni ya GSM GROUP pamoja na Haier.

Kampuni ya Haier iliingia rasmi ubia na kampuni ya GSM GROUP mnamo mwanzoni mwa mwaka 2023. Kwa kipindi hiki chote, kampuni ya Haier ikishirikiana na GSM GROUP imekuwa ikihakikisha inaleta bidhaa ambazo zina tija sokoni. ‘Tangu uanzishwaji wa kampuni ya Haier, Tanzania, tumekuwa tukijitahidi kuangalia matakwa ya soko na kuhakikisha tunaboresha huduma na ufanisi wa bidhaa zetu kwa watumiaji’ Alisema haya meneja biashara, Bw. Ibrahim Kiongozi.

Sambamba na uzinduzi huo wageni waalikwa walipata nafasi ya kujionea bidhaa hizo mpya na kupata mafunzo mafupi kwa ajili ya matumizi ya vifaa hivyo. ‘Sifa kubwa za bidhaa hizi za AC ni mfumo wake imara na wa kisasa unaosababisha matumizi kidogo ya umeme pamoja na uwezo mkubwa wa utendaji kazi katika kutoa hali ya ubaridi kwa haraka.’ Aliongezea Meneja mkuu kutoka Haier, Bw. Leon Liuchi.

Ushirikiano wa makampuni ya GSM Group na Haier unaleta tija katika ukuaji wa uchumi wa nchi kutokana na mapato na ajira mbali mbali zinazotolewa. ‘Katika kuhakikisha kwamba GSM GROUP ikishirikiana na Haier inaungana na juhudi za kukuza uchumi wa Tanzania chini ya uongozi wa Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania, Mh. Dkt Samia Suluhu Hassan, tunajitahidi kushiriki katika shughuli mbali mbali za kijamii zikiwemo udhamini wetu katika michezo kupitia timu mbali mbali za mpira wa miguu kama Young Africans Sports Club (Yanga), Coastal Union, Singida Fountain Gate na Ihefu’ Alisisitiza, Mkurugenzi Mkuu wa Makampuni ya GSM Group, Mr. Benson Mahenya.

Vile vile katika mkutano huo, wageni waalikwa walipata fursa ya kujishindia bidhaa za jokofu (fridge) pamoja na kiyoyozi (AC).

Uongozi wa makampuni ya GSM GROUP na Haier ulitoa shukrani kwa wadau mbali mbali walioshiriki pamoja na kuahidi kuendeleza ubunifu kwa matoleo ya mbeleni ya bidhaa za kielektroniki Tanzania. Vilevile Haier imethibitisha kuongeza mpango kazi katika kuhakikisha upatikanaji wa bidhaa hizo mikoa yote ya Tanzania.
Bw. Mohamed Ally, mkurugenzi wa miradi wa kampuni ya GSM Tanzania (kushoto) akimkabidhi zawadi ya Kiyoyozi mmoja wa wadau wa vifaa vya kielektroniki vya Haier



Kutoka kushoto Bw. Yang, meneja masoko Haier Africa Bw. Kevin, meneja wa bidhaa za rejareja Haier Africa Bw. Mohamed Ally, Mkurugenzi wa miradi wa kampuni ya GSM Tanzania,Mkurugenzi mkuu wa makampuni ya GSM GROUP, Bw. Benson Mahenya (katikati) Bw. Bai, meneja wa bidhaa za AC Bw. Ibrahim Kiongozi, meneja biashara wa Haier Tanzania Bw. John Nguya, mkuu wa biashara kitengo cha GSM Property.


-Yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Na Mwandishi Wetu

BARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), limewaonya watu wanaojenga miradi bila kupata Cheti cha Tathmini ya Mazingira EIA kwenye baraza hilo kwamba wanakabiliwa na faini ya shilingi milioni kumi.

Hayo yamesemwa leo Aprili 19,1024 katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam na msosholojia wa Baraza hilo Suzan Chawe alipokuwa akizungumza kwenye ufunguzi wa maonyesho ya kumbukumbu ya miaka 60 ya Muungano

Maonyesho hayo yamefunguliwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Hemed Abdulla.

Suzan amesema NEMC imekuwa ikifanya kaguzi za mara kwa mara na wale wanaokutwa wamejenga miradi bila EIA wamekuwa wakitozwa faidi inayofikia hadi shilingi milioni kumi

Amesema NEMC imekuwa ikiendesha kampeni ya elimu kwa umma kuhusu umuhimu wa EIA kwa wanaojenga miradi kabla ya kufanya kaguzi na kuwatoza faini.

"Mfano unaweza kukuta mtu anajenga kituo cha mafuta kwenye makazi ya watu jambo ambalo ni hatari kama ikitokea dharura tunaweza kupoteza maisha ya watu kwa hiyo tunasisitiza umuhimu wa EIA kabla ya kuanza shughuli za ujenzi," amesema Suzan

Amesema kwa miaka 60 ya Muungano NEMC inajivunia mambo mengi ikiwemo kupigania ustawi wa mazingira kwa kuhakikisha miti mingi inapandwa na kulindwa.

Suzan amesema Baraza limefanya maboresho ya mifumo yake ya mapito ya taarifa za tathmini na kaguzi za athari kwa mazingira kwa kuimarisha miundombinu ya TEHAMA kulingana na matakwa ya mfumo wa serikali mtandao.

Amesema NEMC inasimamia miradi inayofanya tathmini ya athari kwa mazingira kwa njia ya kielektroniki kupitia usajili wa mtandaoni njia ambayo inamuwezesha mwekezaji kuanzisha mchakato wa kupata cheti cha EIA kupitia mfumo wa usimamizi wa mradi ( Project Management System).

"Kabla ya kufanya usajili wa mradi mwekezaji anatakiwa kuhakikisha mawazo ya wadau yamepatikana kuhusu utekelezaji wa mradi kwenye eneo husika" amesema Suzan.

 

Maofisa wa BARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), wakihudumia watu waliofika leo kwenye viwanja vya mnazi mmoja Dar es Salaam kwenye maonyesho ya miaka 60 ya ya Muungano. Maonyesho hayo yamefinguliwa leo Aprili 19,2024 na Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar, Hemed Abdulla


NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID, KIGOMA

JAJI Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Profesa Ibrahim Hamisi Juma, amesema Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inasema lengo la vyombo vyote vya dola ni ustawi wa wananchi.

Mhe. Jaji Mkuu, ameyasema hayo mjini Kigoma Aprili 19, 2024, wakati akifungua  Kikao Kazi kati ya Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Mahakama ya Tanzania na Watendaji wa Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA) mjini Kigoma lengo kuu likiwa ni kujenga uelewa wa Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi.

“WCF ni Mfuko unaogusa ustawi wa wananchi, kwasababu unaweza kuwa unamtegemea mama, kaka, bahati mbaya akapata ajali akafariki, hapa ustawi wa familia unaweza kutoweka, kama hakuna Mfuko unaoweza kubeba hilo jukumu, kwa hivyo huu Mfuko ni muhimu mno mno.” Amebainisha Mhe. Profesa Juma.

Aidha Mhe. Profesa Juma amehimiza umakini na uadilifu katika utekelezaji wa sheria hiyo ya Fidia kwa Wafanyakazi.

“Ukosefu wa umakini, udanganyifu vyote vimechangia kuua mifuko ambayo ilikuwa na malengo mazuri sana. Tusipokuwa waangalifu, mfuko huu wa WCF vile vile unaweza kukumbana na tatizo hili. Tukielewa vizuri mantiki ya kuanzishwa mfuko huu tutaufanya uwe endelevu na himilivu,” amesema.

Aidha Mhe. Jaji Mkuu ameipongeza WCF kwa kupiga hatua kubwa katika matumizi ya TEHAMA katika utekelezaji wa majukumu yake na kukumbusha umuhimu wa mifumo ya taasisi za umma kusomana ili kurahisisha utoaji wa huduma.

“Ifike mahala mfanyakazi anapowasilisha madai yake WCF, mfumo mzima uwe unaelewa kwamba mfanyakazi fulani amepata ajali kazini au amefariki. Mifumo ya serikali ikiweza kutambuana pia itasaidia sana kuziba mianya ya udanganyifu.” Alisisitiza.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini, Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Bw. Emmanuel Humba, amemuhakikishia Mhe. Jaji Mkuu kwamba Mfuko unaendeshwa kwa ufanisi mkubwa na umepata mafanikio makubwa katika kutekeleza malengo yake.

“Malipo ya fidia kwa Wafanyakazi yameongeza kutoka TZS 3.88 bilioni Kwa mwaka 2016/2017 hadi kufikia TZS 23.58 bilioni kwa mwaka 2022/2023. Hili ni ongezeko kubwa la malipo ya fidia kulinganisha na kiasi cha TZS 250 milioni zilizokuwa zikilipwa na Waajiri kwa mwaka kabla ya kuanza Mfuko.” Amefafanua Bw. Humba.

Aidha, michango ya Waajiri iliyokusanywa imeongezeka kutoka TZS 68.40 bilioni Kwa mwaka 2015/2016 hadi kufikia TZS 86. 48 bilioni kwa mwaka 2022/2023, amesema Bw. Humba.

“Faida inayotokana na uwekezaji ya fedha zilizobaki baada ya kulipa mafao imeongezeka kutoka TZS 1.60 bilioni Kwa mwaka 2015/2016 hadi kufikia TZS 102.43 bilioni kwa mwaka 2022/2023, lakini pia   thamani ya Mfuko imeongezeka kutoka TZS 65.68 bilioni Kwa mwaka 2015/2016 hadi kufikia TZS 602.78 bilioni kwa mwaka 2022/2023.” Amefafanua.

Kuhusu ustahamilivu wa Mfuko katika kutekeleza majukumu yake, Mwenyekiti huyo wa Bodi amesema kuwa tathmnini ya uhai na uendelevu wa Mfuko iliofanywa na Shirika la Kazi Duniani (ILO) inaonesha kwamba Mfuko unauhimilivu (Sustainability) kwa kipindi cha miaka 30 kuanzia mwaka wa tathmini 2022/2023.

Akizungumzia kuhusu nia ya kikao kazi hicho, Bw. Humba alibainisha kuwa pamoja na kwamba jukumu la kulipa fidia limekasimiwa kwenye Mfuko, Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi imeweka utaratibu na vyombo vya kushughulikia madai ya wanufaika pale wanapokuwa hawajaridhika na fidia iliyolipwa au maamuzi ya Mfuko yanayokinzana na matarajio yao.

Akifafanua zaisdi alisema, Sheria inamtambua Waziri Mwenye dhamana ya masuala ya kazi kuwa ni Mamlaka ya kwanza ya rufaa dhidi ya uamuzi wa Mfuko na Mahakama Kuu Divisheni ya Kazi kuwa Mamlaka ya mwisho ya rufaa.

“Kutokana na hitaji hili muhimu la kisheria, Bodi ya Wadhamini ya WCF, Menejimenti ya Mfuko pamoja na Watendaji wa Mahakama Kuu Divisheni ya Kazi waliona kuna hitaji la kufanya vikao kazi kwa lengo la kubadilisha uzoefu, kujenga uelewa wa pamoja na kubainisha maeneo ya sheria yanayohitaji maboresho kwa lengo la kuongeza ufanisi katika kutekeleza Sheria hiyo.” Alisema.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Dkt. John Mduma ameeleza kuwa ushirikiano baina ya Mfuko na Mahakama ni muhimu kwa vile kuna maeneo mengi ambayo Mfuko unakutana na Mahakama katika utekelezaji wa majukumu yake.

“Sisi kama WCF shughuli zetu hazikamiliki bila ya uwepo wa shughuli za Mahakama. Kwa mfano katika kushughulikia masuala yanayohusu mirathi, Mfuko hutegemea maamuzi ya Mahakama.” Alisema Dkt. Mduma.

Awali, akizungumza kabla ya kumkaribisha Jaji Mkuu kufungua Kikao Kazi hicho, Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Divisheni ya Kazi, Mhe. Dkt. Yose Mlyambia alisema kuwa kumekuwa na vikao kazi vitano ambavyo vimefanyika baina ya Mahakama, WCF na Watendaji wa Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA) huko Bagamoyo, Mwanza, Arusha, Songea na Kigoma.

Alibainisha kuwa jumla ya Viongozi na watumishi 290 wameshiriki katika Vikao Kazi hivyo, wakiwemo Majaji 70, Naibu Wasajili 33, Watendaji 11, Wadau 48, Tume ya Usuluhishi na Uamuzi 32 na zaidi ya watumishi wa Mahakama 96.

JAJI Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Profesa Ibrahim Hamisi Juma, akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao kazi baina ya WCF, Mahakama na CMA mjini Kigoma Aprili 19, 2024
JAJI Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Profesa Ibrahim Hamisi Juma, akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao kazi baina ya WCF, Mahakama na CMA mjini Kigoma Aprili 19, 2024
Kikao kikiendelea
Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini, Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Bw. Emmanuel Humba, akieleza mafanikio mbalimbali ambayo Mfuko umeyapata tangu kuanzishwa kwake
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Dkt. John Mduma, akieleza jinsi Mfuko unavyotekeleza kwa vitendo Tunu (Core value) ya Ushirikiano na taasisi zingine ikiwemo Mahakama.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Divisheni ya Kazi, Mhe. Dkt. Yose Mlyambia, akkeleza matokeo ya vikao kazi hivyo katika kuboresha Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi.
Baadhi ya washiriki wakifuatilia hotuba ya ufunguzi wa kikao kazi hicho.
Baadhi ya washiriki wakifuatilia hotuba ya ufunguzi wa kikao kazi hicho.
Mkurugenzi wa Huduma za Tathmini WCF, Dkt. Abdulsalaam Omar, yaya aliwasilisha mada iliyoelezea mambo mbalimbali ikiwemo jinsi tathmini za ulemavu zinavyofanyika ikiwa ni seehemu ya mchakato wa kulipa fidia.
Mkurugenzi wa Uendeshaji WCF, Bw, Anselim Peter, yeye aliyoa mada kuhusu uendeshaji wa shughuli za Mfuko, ikiwa ni pamoja na utaratibu wa kuwasilisha madai.
Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Sheria, WCF, Bw. Abrahamu Siyovelwa, akitoa mada kuhusu Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi.
Kamishna wa Kazi, Bi. Suzan Mkangwa akiwa ni miongoni mwa viongozi walioshiriki katika kikao hicho.







Na Mwandishi Wetu
MAKAMU wa Pili wa Rais wa Zanzibar Hemed Suleiman Abdulla ametoa wito kwa wananchi wa Tanzania kuendelea kuulinda Muungano.

Hayo ameyasema leo Aprili,19,2024 jijini Dar es Salaam katika maonesho ya Taasisi za kimuungano ambapo amesema kuwa huwezi kuutenganisha umoja wa Watanzania wale wa Visiwani na Bara kwa kuwa tayari watu hawa wameungana kwa damu.

"Tangu enzi za wazee wetu watu wa visiwani wanaishi bara, wameoa bara wamejukuu bara hivyo hivyo wa bara wanaishi na wale wa bara wanaishi visiwani wameona, wamejukuu watu hawa huwezi kuwatenganisha" alisema Makamu wa pili wa Rais.

Amesema kuwa amefarijika kuona maonesho yaliyoandaliwa na Taasisi za kimuungano na kuwataka wananchi kufika kwenye maonesho hayo ili kujifunza zaidi kuhusu muungano.

Amesema kuwa Muungano umeimarika zaidi husasani kwenye huduma za kijamii na uchumi "kauli mbiu ya mwaka huu tumeimarika na tumeshikamana kwa maendeleo ya taifa letu tutaendelea umoja wetu, Muungano wetu ".

Amesema kuimarika kwa mahusiano kumetoa fursa kwa wafanyabiasha wa pande zote mbili kuwekeza katika nyanja mbambali.

Ametoa wito wa kuulinda Muungano ili kuitunza Tunu hiyo muhimu iliyotimiza miaka 60 .

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Khamis Hamza Khamis amemhakikishia Makamu wa Pili wa Rais kuw muungano upo salama.
"Sisi wanadar es Salaam tunayomengi ya kuzungumzia kuhusu Muungano na haya maendeleo yanayoonekana hapa ni zao la Muungano."

Amesema kuwa muingiliano wa biashara umekuwa mkubwa watu wanafanya shughuli zao na wanatembea kila upande wa Muungano bila kuwa na hati kusafiria "Utawaona wapo Darajani kule Zanzibar utawaona Kariakoo hapa Dar es salaam huwezi kuwatofautisha".

Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Mhandisi Cypran Luhemeja
,amesema Muungano huu umetupa fursa za kibishara na za kujamii "wengine tumepata fursa ya kuchanganya damu kwa maana tumeoa Zanzibar"
Amesema kuwa uchumi umekuwa kutokana kuchagizwa na ushirikiano wa kibiashara.

Amesema kuwa tayari Serikali ya Jamhuri imeshughulikia changamoto takribani zote za muungano.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla akifungua Maonesho ya Biashara Miaka 60 ya Muungano katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo Aprili 19, 2024.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Khamis Hamza Khamis akitoa salamu wakati wa Maonesho ya Biashara Miaka 60 ya Muungano katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo Aprili 19, 2024 ambapo mgeni rasmi alikuwa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla.
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Mhandisi Cyprian Luhemeja akitoa neno la ukaribisho wakati wa ufunguzi wa Maonesho ya Biashara Miaka 60 ya Muungano katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo Aprili 19, 2024 ambapo mgeni rasmi alikuwa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla.
Washiriki mbalimbali wakifuatilia ufunguzi wa Maonesho ya Biashara Miaka 60 ya Muungano katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo Aprili 19, 2024 ambapo mgeni rasmi alikuwa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla.





Geneva, Uswisi
TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imechaguliwa kuwa Makamu wa Rais wa Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) inayosimamia uangazi, miundombinu na mifumo ya taarifa za hali ya hewa (WMO Commission for Observation, Infrastructure and Systems - IN

FCOM). Katika uchaguzi huo Tanzania iliwakilishwa na Mkurugenzi wa Miundombinu na Huduma za Ufundi, TMA, , Dkt. Pascal Waniha.

Dkt. Waniha amechaguliwa katika nafasi hiyo tarehe 18 Aprili, 2024 katika uchaguzi wa viongozi wa Tume ya INFCOM uliofanyika katika Mkutano wa tatu wa Tume hiyo (Third Session of the WMO Commission for Observation, Infrastructure and Systems- INFCOM-3)”, unaoendelea katika makao makuu ya WMO, Geneva- Uswisi tarehe 15 hadi 19 Aprili, 2024.

Uchaguzi wa Tume ya INFCOM umefanyika kufuatia muda wa viongozi waliokuwa madarakani kumaliza muda wao ambapo viongozi hao walichanguliwa mwaka 2021 na waliongoza Tume ya INFCOM katika kipindi cha miaka minne (2020/21 – 2023/24). Uongozi wa juu wa Tume ya INFCOM unaundwa na Rais wa Tume akisaidiana na Makamu watatu wa Rais. Wagombea katika nafasi ya Makamu wa Rais walikuwa wanne (4), kutoka Tanzania, Czech, Hong Kong-China na India. Katika kinyang’anyiro hicho zilihitajika nafasi tatu na viongozi wapya waliochaguliwa ni Rais wa Tume hiyo, Bw. Michel Jean (Canada) ambaye anaendelea katika nafasi yake, na Makamu wa Rais ambao ni Dkt. Pascal Waniha (Tanzania), Dk. Chan Pak Wai (Hong Kong, China) na Dkt. Jan Danhelka (Jamhuri ya Czech).

Tume ya INFCOM ni mojawapo ya mihimili mikuu mitatu inayounda Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO). Mihimili hiyo ni: (1) Tume inayosimamia uangazi, miundombinu ya hali ya hewa na mifumo ya Taarifa za Hali ya Hewa (Commission for Observation, Infrastructure and Systems - INFCOM); (2) Tume inayosimamia Matumizi ya Taarifa za Hali ya Hewa (Commission for Weather, Climate, Hydrological, Marine and Related Environmental Services and Applications - SERCOM) na Bodi ya Utafiti (Research Board). Dkt. Waniha atakuwa miongoni mwa viongozi wapya wa Tume ya INFCOM watakaoiongoza Tume hiyo katika kipindi cha miaka minne (2024- 2028).

Dkt. Waniha ni Mtaalamu mbobezi wa hali ya hewa katika eneo la utabiri wa hali ya hewa kwa kutumia modeli (Climate Modelling and Numerical Weather Prediction -NWP) kwa takribani miaka 29, ambapo ametoa mchango mkubwa katika fani ya hali ya hewa ndani na nje ya Tanzania hususan katika WMO kupitia vikosikazi mbalimbali vya kuboresha miundombinu na huduma za hali ya hewa. Kuchaguliwa kwake katika nafasi hii ni muhimu kwa Tanzania na Afrika kwa ujumla ikizingatiwa kuwa nchi nyingi za Afrika zina changamoto ya upungufu wa miundombinu na teknolojia ya miundombinu ya hali ya hewa. Miundombinu ya hali ya hewa ni muhimu katika kupima na kufuatilia mienendo ya mifumo ya hali ya hewa na kukabiliana na changamoto ya mabadiliko ya hali ya hewa na tabianchi.
Mzee Baraka Meneja Mauzo Drafco Group Ltd wa pili kutoka kulia akikabidhi taulo za kike kwa Dkt. Robert Magoma Kaimu Mganga Mkuu hospitali ya rufaa ya Amana Ilala jijini Dar es Salaam ambapo amepokea taulo (Baby Cheeky, Cuidado na Pinotex) kutoka kampuni ya Drafco Group Limited, Pia kampeni ya kuelimisha wanawake na watoto namna ya matumizi ya Taulo za watoto, akina mama na wagonjwa wenye mahitaji maalum ilifanyika kwa siku tano na kufungwa Aprili 19 , 2024 kulia ni Dkt. Idda Luhanga Mkurugenzi wa Premature Babies Organization.


Picha ya pamoja mara baada ya makabidhiano ya taulo (Baby Cheeky, Cuidado na Pinotex) kwa ajili ya matumizi ya wagonjwa, wazazi pamoja na watoto.


Dr. Robert Magoma Mganga Mkuu Amana akitoa shukurani zake baada ya kupokea msaada huo.


Dr. Idda Luhanga mkurugenzi wa Premature Babies Ogarnization akizungumza katika makabidhiano hayo


Mzee Baraka Meneja Mauzo Drafco Group akizungumza katika hafla hiyo ya kufunga mafunzo hayo na makabidhiano ya taulo za kike kwa akina mama na watoto kwenye hospitali ya Rufaa ya Amana Ilala jijini Dar es Salaam.


KAMPUNI ya Drafco Group kwa kushirikiana na kampuni ya Premature Babies leo Aprili 19, 2024 wameadhimisha cha kilele cha programu ya siku tano ya Dipper Care ambayo ilianza rasmi Aprilin15, 2024 ambayo ilikuwa na malengo ya kuelimisha jamii kuhusu matumizi sahihi ya taulo kwa watoto, Wanawake na wagonjwa wenye.Uhitaji maalumu.

Akizungumza na waandishi wa habari jiini Dar es Salaam leo Aprili, 2024, katika hafla ya kukabidhi msaada wa taulo za kike Meneja Mauzo Drafco Group, Mzee Baraka akizungumza wakati akifunga kampeni ya siku tano ya Diaper Care, kuelimisha wanawake na watoto namna ya matumizi ya taulo (Baby Cheeky, Cuidado na Pinotex) za kike na kukabidhi taulo hizo kwa ajili ya wagonjwa na wazazi kwenye hospitali ya Amana Ilala jijini Dar es Salaam. Amesema kuwa tangu kuanzishwa kwa kampuni hiyo wamekuwa wakishirikiana na serikali kwa uchangia maendeleo ya uchumi wa taifa kwa kutumia sekta ya afya.

"Mama, Dada zetu mna nafasi kubwa sana kusaidia jamii kuweza kutumia bidhaa hizo ambazo matumizi ya bidhaa hizo humsaidia mtumiaji kuwa huru, salama na kuwa mwenye furaha wakati wote." Ameeleza

Amesema wametoa elimu kwa watu zaidi ya 700 wajawazito, watoa huduma wa hospitali, ndugu wa wagonjwa waliopo hospitali ikiwa ni pamoja na kuwapatia dipper watoto njiti na wagonjwa wenye uhitaji maalumu wote waliopo hospitali.

Pia amesema kuwa umefanikiwa kugawa taulo zenye thamani ya shilingi milioni tano na elfu sabini (5,070,000).

Pia kampuni hizo zitawakomboa wagonjwa wanne walioshindwa kulipa gharama za matibabu katika hospitali ya Rufaa ya Amana.

Pia mewakabidhi bidhaa ya taulo katoni 25 ambazo ni sawa na 35780 zenye thamani ya milioni 2,500,000/=

Kwa Upande wa mkurugenzi wa Premature Babies Ogarnization Dkt. Idda Luhanga akingumza katika makabidhiano hayo amesema kuwa wamewafikia anawake zaidi ya 200 wanaohudhuria Kliniki katika hospitali ya Amana na kutoa elimu namna ya kukabiliana na kujiepusha na kupata mtoto kabla ya muda.

"Kwa kutoa elimu hiyo tunaweza kukabiliana na kuzaa watoto njiti na kuweza kupunguza vifo vya watoto wa chini ya miaka mitano."

Kwa Upande wa Kaimu Mganga Mkuu hospitali ya Rufaa ya Amana Dkt. Robert Magoma akitoa shukurani zake baada ya kupokea msaada huo na kuomba kwa kampuni nyingine waweze kushirikiana kutoa misaada ya kibinadamu.

"Mmefanya kazi kubwa sana na mmefanya kazi ya ubinadamu Mungu awabariki, awazidishie moyo wa kujitolea isiwe kwa hospitali yetu tuu."
Taasisi ya Victoria Foundation kwa kushirikiana na Orica Tanzania inatekeleza mradi wa hatua kwa hatua uitwao Binti Ng'ara, kwa ajili ya kumsaidia mtoto wa kike kupata taulo za kike za kumuwezesha Binti aweze kwenda shule wakati wote hasa wa siku zake za Hedhi.

Katika hafla ya Ugawaji wa Taulo hizo uliofanyika katika viwanja vya shule ya Sekondari Nyankumbu Tarehe 18 April, Mgeni Rasmi alikua ni Afisa Elimu Sekondari Cassian Luoga akimuwakilisha katibu Tawala Mkoa wa Geita. Hafla hiyo ilihudhuliwa na viongozi mbalimbali akiwemo Mkurugenzi wa Orica Tanzania, Asha Mambo, Kaimu Mkurugenzi Taasisi ya Victoria Foundation Steven T. Mruma, Mkurugenzi na Mzalishaji wa Taulo za Kike za Palesa Sherie De Wity kutoka Nchini Afrika kusini, Maafisa Elimu wa ngazi mbalimbali , Muwakilishi wa Dawati la Jinsia Kutoka Jeshi la Polisi Afande Christina Katana pamoja na Walimu na Wanafunzi kutoka shule sita za Wilaya Ya Geita Mji.

Taulo hizo za kike zitawanufaisha Jumla ya wasichana 2500 kutoka Shule 25 za mkoa wa Geita kutoka katika Wilaya zote Sita ambapo box moja la taulo za kike linaweza kutumiwa na Mwanafunzi kwa muda wa miaka mitano kwakua Taulo hizo zinaweza kufuliwa na kutumika tena (Re usable), Zilizotengenezwa na kampuni ya Palesa Pads kutoka nchini Africa ya Kusini.

Akizungumza katika hafla hiyo ya ugawaji Mgeni Rasmi Cassian Luoga aliwashukuru Orica Tanzania kwa kufadhili mradi wa Binti Ng'ara chini ya Taasisi ya Victoria Foundation na kuomba wadau wengine wajitokeze kwa wingi ili kusaidia kutatua kabisa tatizo la wasichana kukosa vipindi vya Darasani kutokana na kukosa taulo za kike hasa wakati wakiwa katika hedhi.

Nae Mkurugenzi Wa Orica Tanzania Asha Mambo aliahidi kuendelea kushirikiana na Serikali pamoja na Taasisi zisizo za serikali kukabaliana na changamoto mbalimbali zinazowakabili mabinti.

Akitoa shukrani kwa niaba ya Mkurugunzi wa Victoria, 'Vicky Kamata',Maneja wa Miradi wa Taasisi hiyo Ndugu Steven T. Mruma aliwashukuru Orica Tanzania kwa Ufadhili wa Mradi, na Uongozi wa Mkoa wa Geita kwa ushirikiano mkubwa walioutoa wakati wote wa utekelezaji wa Mradi huo.







Top News