Nchi wanachama za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (Southern African Development Community-SADC) zimempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa maono yake katika usimamizi na uhifadhi wa misitu miombo hasa katika kuhama kutoka kwenye matumizi ya nishati ya kuni na mkaa kuelekea nishati safi ifikapo mwaka 2030.

Kauli hiyo imetolewa leo Aprili 18,2024 na Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) katika Mkutano wa Kimataifa unaohusu Misitu ya Miombo jijini Washington DC nchini Marekani.

“Kikubwa nchi zimeweza kumpongeza Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa namna ambavyo amekuwa akitoa maelekezo mbalimbali kwetu sisi kama Wizara na Sekta katika kuhakikisha kwamba misitu ya miombo inalindwa kwa nguvu kubwa, na kwa namna ambavyo amechukua uamuzi thabiti wa kuhakikisha kwamba inapofika mwaka 2030 zaidi ya asilimia 80 ya wananchi watakuwa wameachana na matumizi wa kuni na mkaa na watakuwa wamejielekeza katika nishati safi ya kupikia” Mhe. Kairuki amesisitiza.

Amesema kuwa misitu ya miombo nchini Tanzania na katika ukanda wa kusini imekuwa ikikabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo uharibifu wa misitu ambao unasababishwa na ukataji wa miti usiozingatia sheria, taratibu na kanuni, moto, kilimo cha kuhamahama, uharibifu wa vyanzo vya maji na mabadiliko ya tabia nchi.

Aidha, amefafanua kuwa kupitia mkutano huo, wadau mbalimbali wameanza kuonesha nia ya kusaidia mpango wa utekelezaji wa Azimio la Maputo la mwaka 2022 kuhusu ulinzi na uendelezaji wa misitu ya miombo.

Amesema lengo la Mkutano huo ni kuona namna ya kuendeleza Azimio la Maputo katika kulinda na kuendeleza Misitu ya Miombo ambapo takribani asilimia 93 ya misitu ya Tanzania ni miombo ambayo pamoja na mambo mengine, inatunza wanyamapori , vyanzo vya maji na huduma nyingine za kijamii.

Naye, Kamishna Uhifadhi wa Wakala ya Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Prof. Dos Santos Silayo amesema kuwa kupitia mkutano huo nchi za SADC zimekuwa na majadiliano kuhusu kutafuta namna ya kushirikiana baina ya nchi hizo na wadau mbalimbali wa maendeleo katika kupata rasilimali fedha na kukuza ujuzi na utaalamu kwa ajili ya kusaidia uhifadhi wa misitu hiyo.

Ameongeza kuwa kongamano hilo limehitimishwa na hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Watu wa Msumbiji, Mhe. Filipe Nyusi ambapo amesisitiza umuhimu wa nchi hizo kushirikiana katika kubadilishana taarifa , kukabiliana na masuala ya uharibifu wa mifumo ya ikolojia ya miombo hususan biashara haramu za mazao ya misitu na wanyamapori katika ukanda wa SADC.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Idara ya Misitu na Nyuki, Wizara ya Maliasili na Utalii, Bw. Deusdedith Bwoyo amesema kuwa mkutano huo umekuwa ni wa kipekee na muhimu ambapo nchi 11 zimebaini kuwa umoja ni nguvu na kwamba kila nchi haiwezi kusimamia kwa ufanisi mkubwa misitu yake na hivyo, zimekutana na kujadili kwa pamoja changamoto za misitu ya miombo na namna ya kuunganisha nguvu na kutafuta rasilimali fedha katika usimamizi na uendelezaji wake kwa faida ya kizazi cha sasa na vijavyo.
Rais wa Jamhuri ya Watu wa Msumbiji, Mhe.Filipe Jaciton Nyusi akizungumza katika Mkutano wa Kimataifa kuhusu usimamizi endelevu wa misitu ya miombo  jijini Washington DC nchini Marekani leo Aprili 18,2024.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) (kulia) akiwa na baadhi ya Mawaziri wa nchi za SADC katika Mkutano wa Kimataifa kuhusu usimamizi endelevu wa misitu ya miombo jijini Washington DC nchini Marekani leo Aprili 18,2024.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) akizungumza katika Mkutano wa Kimataifa kuhusu usimamizi endelevu wa misitu ya miombo  jijini Washington DC nchini Marekani leo Aprili 18,2024.
Rais wa Jamhuri ya Watu wa Msumbiji, Mhe. Filipe Jaciton Nyusi (katikati) akifuatilia mawasilisho kuhusu misitu ya miombo kutoka kwa wawakilishi wa nchi za SADC katika Mkutano wa Kimataifa kuhusu usimamizi endelevu wa misitu ya miombo  jijini Washington DC nchini Marekani leo Aprili 18,2024. Kushoto kwake ni Waziri wa Ardhi na Mazingira wa Msumbiji, Mhe.Ivete Maibaze na Balozi wa Umoja wa Afrika nchini Marekani, Mhe. Hilda Suka-Mafdze (kulia).

Baadhi ya washiriki wa mkutano kutoka nchi mbalimbali wakipiga makofi baada ya kikundi cha burudani cha ngoma za asili kutumbuiza katika Mkutano wa Kimataifa kuhusu usimamizi endelevu wa misitu ya miombo uliofanyika jijini Washington DC nchini Marekani leo Aprili 18,2024.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii, Mhe. Timotheo Mnzava (Mb) na baadhi ya washiriki wakifuatilia Mkutano wa Kimataifa kuhusu usimamizi endelevu wa misitu ya miombo uliofanyika jijini Washington DC nchini Marekani leo Aprili 18,2024.

Na Mwandishi Wetu,Dodoma

WAENDESHA bodaboda jijini Dodoma wametakiwa kuithamini kazi yao na kujijali wenyewe ili kuondoa dhana iliyojengeka kuwa kundi hilo limekuwa likivunja sheria za usalama barabarani.

Hayo yameelezwa na Polisi Kata wa Kata wa Kata ya Uhuru jijini Dodoma, alipokuwa akitoa mada katika semina ya mafunzo kwa bodaboda iliyoandaliwa na Shirika la Amend Tanzania kwa kushika na Ubalozi wa Uswisi nchini.

Mafunzo hayo ya naendelea jijini Dodoma ikiwa na awamu ya pili kutolewa katika Jiji hilo.

Amesema kumekuwapo na dhana kuwa, waendesha bodaboda wengi hawazingatii sheria za usalama barabarani, hivyo kuhatarisha maisha yao, abiria wanaowabeba na usalama wa vyombo vyao.

Kwa mujibu wa polisi Kata huyo, mafunzo wanayo yatoa ni muhimu kwa kuwa yanawawezesha bodaboda kufahamu usalama wao na jinsi ya kuvimudu vyombo wanavyoviendesha wawapo barabarani.

Kwa upande wake Ofisa Mtendaji wa Kata ya Uhuru Fatma Amri anasema mafunzo hayo kwa kiasi kikubwa yanawasaidia vijana katika Kata yake kujitambua na kuzingatia sheria wanapoendesha vyombo vya moto.

Amewasisitiza bodaboda waliopata mafunzo hayo kuhakikisha waafanyia kazi elimu waliyopewa kwa kuzingatia na kuzitekeleza kikamilifu sheria za usalama barabarani.

Kupitia mafunzo hayo waendesha bodaboda hao walielimishwa kuhusu huduma ya kwanza na umuhimu wake, pia usalama wao katika maeneo yao ya kazi.

Mfunzo hayo ambayo yanatolewa kwa ufasdhili wa Ubalozi wa Uswisi yamefanyika kwa bodaboda kuingia darasani na kwa njia ya vitendo kwa lengo la kuwajengea uwezo maofisa usafishaji wote watakaohudhuria mafunzo hayo.



Na Janeth Raphael -MichuziTv -Dodoma

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Raisi Mipango na Uwekezaji Mhe Prof. Kitila Mkumbo amesema kuwa hatua ya kwanza kujipima katika maendeleo ni kuwa na usalama wa chakula na wakati tumeungana na Zanzibar usalama wa chakula ulikuwa asilimia 60 huku lengo la nchi ni kujitosheleza kwa asilimia 100 na kuwa na akiba lakini kwasasa Nchi jna usalama wa chakula kwa asilimia 124.

Waziri Prof.Mkumbo ameyasema hayo Jijini Dodoma katika mkutano wake na Wanahabari wakati akielezea mafanikio ya Wizara hii kuelekea Maadhimisho ya miaka 60 ya Muungano wa Tanzania.

Na kuongeza kuwa hatua ya pili ni katika ustawi wa na Nchi kwa kuzungatia mambo ya msingi ya kibinadamu ikiwemo chakula,mavazi na malazi ambayo nayo tumepiga hatua.

"Hatua ya kwanza kujipima katika maendeleo ni kuwa na usalama wa chakula. Wakati ule tumeungana, usalama wa chakula ulikuwa asilimia 60 huku lengo la nchi ni kujitosheleza kwa chakula kwa asilimia 100 na kuwa na akiba. Kwa sasa nchi ina usalama wa chakula kwa asilimia 124".

"Hatua ya pili kujipima katika maendeleo ni ustawi wa watu na nchi kwa kuangalia mambo ya msingi ya kibinadamu ikiwemo chakula, mavazi na malazi ambayo nayo tumepiga hatua kubwa".

Sambamba na hayo Waziri amesema kuwa yaliyopo ni kuwa ifikapo 2025 wastani wa umri wa kuishi kwa Watanzania uwe ni 68 japo kwa Sensa ya watu na makazi mwaka 2022 wastani wa kuishi ni miaka 66. Tukilinganisha wakati tunapata Uhuru ilikuwa ni wastani wa miaka 32.

"Wakati tunapata Uhuru, umri wa kuishi kwa Mtanzania ilikuwa wastani wa miaka 32, mwaka 2000 umri wa kuishi ukasogea hadi wastani wa miaka 52. Tamaa yetu ifikapo mwaka kesho 2025 wastani wa kuishi uwe miaka 68. Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022, wastani wa kuishi ni miaka 66".

Kwa upande wa Elimu amesema kwa mwaka 2000 nchini Tanzania kiwango cha kuandikisha wanafunzi kilikuwa asilimia 69 lakini ya maendeleo ya taifa ya kwama 2025 ni kufikia asilimia 100 ya uandikishaji.

"Mambo matatu ya kufanya kukuza ustawi wa binadamu ni kumpa binadamu elimu ili aweze kuishi vizuri ambapo mwaka 2000 nchini Tanzania, kiwango cha kuandikisha wanafunzi kilikuwa asilimia 69. Kwa malengo tuliyojiwekea kwenye Dira ya Maendeleo ya Taifa ya mwaka 2025, ni kufikia asilimia 100 ya uandikishaji wa wanafunzi ambapo hadi sasa tumevuka malengo, tupo asilimia 108.5".

"Kuhusu suala la kwenda sekondari, mnamo mwaka 1964 ilikuwa asilimia 5, mnamo mwaka 2000, watoto waliofanikiwa kufika sekondari kutoka shule za msingi ilikuwa chini ya asilimia 20. Lengo letu ifikapo mwaka 2025, tuwe tumefika asilimia 48. Kwa takwimu za hivi sasa, tupo asilimia 70".

"Dira ya Maendeleo ya Taifa inayokuja, tutahitaji elimu ya msingi Tanzania iwe kwa Watanzania wote na wote lazima kufika sekondari kwa asilimia 100".

"Eneo la pili la kukuza ustawi wa binadamu ni afya hasa kwenye eneo la mama na mtoto, na la tatu ni maji ambapo wakati tunapata uhuru, uwepo wa maji vijijini ulikuwa chini ya asilimia 15 na mwaka 2000 ilikuwa asilimia 32. Kwa sasa ni asilimia 77".

Waziri amemaliza kwa kusema kuwa Tuna mengi ya kujivunia katika muungano, tumefanikiwa kuzikabili na kuzitatua changamoto zilizojitokeza. Serikali imejidhatiti kupambana na changamoto zitakazojitokeza ambazo zitatishia muungano wetu.


NA EMMANUEL MBATILO

VYUO Vikuu vina jukumu kubwa la kuwa injini ya ubunifu na ugunduzi kwani ni kitovu cha uzalishaji wa maarifa, ambapo tafiti bora za masuala mbalimbali ya kijamii, kiuchumi na kisayansi hufanywa na mawazo ya mabadiliko huzaliwa.

Hata hivyo, ili mawazo haya yaweze kuzaa matunda, lazima yatafsiriwe vizuri kwenye mahitaji halisi ya taifa na dunia kwa ujumla kupitia ushirikiano na washirika wa sekta mbalimbali na viwanda.

Ameyasema hayo Aprili 18, 2024 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania, Prof. Joseph Ndunguru wakati akifungua Maadhimisho ya Tisa ya Wiki ya Utafiti na Ubunifu ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Ngazi ya Chuo Kishiriki Cha Elimu Mkwawa mkoani Iringa.

Amesema sekta mbalimbali na viwanda, kwa upande mwingine, huleta rasilimali muhimu, utaalamu, na changamoto halisi ambazo makundi yote mawili (yaani wanataaluma na wataalam kwenye viwanda) wana wajibu wa kuzijadili na kutafuta suluhisho.

"Kwa kushirikiana na vyuo vikuu, viwanda hupata maarifa yenye mitazamo mpya kwenye uendeshaji wa viwanda. Hivyo basi, ushirikiano wa wanataaluma na wataalam kwenye viwanda husaidia kuziba pengo kati ya nadharia na mazoezi, kugeuza dhana za kufikirika kuwa suluhisho halisi la changamoto kwenye taifa na ulimwengu kwa ujumla". Amesema Prof. Ndunguru.

Aidha Prof. Ndunguru ameipongeza Menejimenti ya Chuo kwa kuendelea kutenga fedha kila mwaka ili kugharamia shughuli za utafiti na ubunifu kwa wafanyakazi wake.

Vilevile amewapongeza kukamilisha ujenzi wa Maabara ya Biolojia na mipango mbalimbali mliojiwekea kwenye ujenzi wa miundombinu kupitia Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi (HEET).

"Ujenzi wa maabara na majengo mengine kupitia mradi huu vitasaidia kuendelea kuboresha tasnia ya utafiti hapa chuoni na kukiwezesha Chuo Kishiriki cha Elimu Mkwawa kuendelea kusaidia katika utatuaji wa changamoto mbalimbali ambazo zinalikabili Taifa letu ili kuweza kusukuma mbele gurudumu la maendeleo na kufikia uchumi wa viwanda". Amesema

Pamoja na hayo amesema kuwekeza kwenye miundombinu ya utafiti, kukuza ujuzi wa mbinu za ujasiriamali, pamoja na kusisitiza ujuzi wa teknolojia ya kisasa miongoni mwa wanafunzi wetu.

"Mambo haya yatasaidia kukuza utamaduni kwa wanafunzi wetu kudadisi vitu na hatimaye kuchochea ubunifu na uvumbuzi kupitia tafiti mbalimbali". Ameeleza Prof. Ndunguru.

Kwa upande wake Kaimu Rasi wa Chuo Kishiriki cha Elimu Mkwawa, Prof. Deusdedit Rwehumbiza amesema ujenzi wa maabara ya biolojia umekamilika na Chuo kimeshakabidhiwa maabara hiyo na imeanza kutumika.

Amesema Maabara hiyo imekisaidia Chuo kuongeza nafasi kwa wanafunzi na wafanyakazi kufanya majaribio mengi ya kisayansi.

"Maabara hii inawasaidia wanataaluma wetu pamoja na wanafunzi kufanya tafiti na kujifunza kwenye mazingira rafiki. Tunaishukuru sana Serikali kwa kutusaidia kukamilisha upanuzi wa maabara hii". Amesema Prof. Rwehumbiza.

Pia amesema kuwa Chuo kimefanikiwa kukamilisha ujenzi wa jengo la ofisi ya masuala anuwai (Gender Diversity) ambalo litakisaidia Chuo kuongeza ufanisi katika kukabiliana na changamoto zinazohusisha unyanyasaji wa kijinsia wakati wa utekelezaji wa shughuli za msingi za Chuo, zikiwemo shughuli za utafiti na ubunifu.

Hata hivyo amesema kuwa Chuo kimesaini mkataba wa ujenzi wa mabweni mawili ya wanafunzi yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 300 kila moja, na ujenzi wa maktaba ya Chuo yenye uwezo wa kuchukua watumiaji 1,500 tofauti na maktaba iliyopo ambayo ina uwezo wa kuchukua watumiaji 500.

"Kukamilika kwa mabweni ya wanafunzi kutakisaidia Chuo kutoa huduma ya malazi kwa wanafunzi 1,750 (30.1%) kutoka wanafunzi 1,150 (19.8%) wanaopata huduma hiyo kwa sasa". Amesema

Sanjari na hayo amesema kuwa ujenzi wa maktaba mpya utakisaidia Chuo kuwa na uwezo wa kuchukua jumla ya watumiaji 2000 ambao ni 33.3% ya idadi ya wanafunzi na wafanyakazi wa Chuo wapatao 6,000 ikilinganishwa na maktaba iliyopo ambayo uwezo wake ni 8.3%.



Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo akizungumza wakati wa kikao na ujumbe kutoka mashirika ya kimataifa yasiyo ya kiserikali ya The Pew Charitable Trusts (PEW) na Wetlands International (WI) kwa lengo la kuainisha fursa zilizolopo kwenye uhifadhi wa maeneo ya fukwe, Aprili 17, 2024 jijini Dodoma.
Mkurugenzi wa Shirika la The Pew Charitable Trusts (PEW) Bw. Simon Reddy akifafanua jambo wakati wa kikao na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo Aprili 17, 2024 jijini Dodoma.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa Shirika la The Pew Charitable Trusts (PEW) Bw. Simon Reddy (kushoto) na Bi. Julie Mulonga kutoka Wetlands International (WI) kwa lengo la kuainisha fursa zilizolopo kwenye uhifadhi wa maeneo ya fukwe, Aprili 17, 2024 jijini Dodoma.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo amesema Serikali itaendelea kufungua milango kwa wadau wenye nia ya kuchangia katika hifadhi endelevu ya mazingira.


Amesema hayo wakati wa kikao na ujumbe kutoka mashirika ya kimataifa yasiyo ya kiserikali ya The Pew Charitable Trusts (PEW) na Wetlands International (WI) kwa lengo la kuainisha fursa zilizopo kwenye uhifadhi wa maeneo ya fukwe, Aprili 17, 2024 jijini Dodoma.


Dkt. Jafo amewashukuru wadau hao kwa kutambulisha mradi huo hususan katika eneo la mifumo ya ikolojia ya mikoko na nyasi bahari kwa faida za kutunza bioanuai na kukabiliana na athari mabadiliko ya tabianchi.


Amesema taarifa za kitafiti zitakazotokana na mradi huo zitasaidia katika maandalizi ya taarifa ya nchi kuhusu mchango wa kitaifa wa kupunguza gesi joto duniani (NDC).


Tutambue Tanzania imedhamiria kupunguza uzalishaji wa gesijoto kwa asilimia 30 hadi 35 ifikapo mwaka 2030, hivyo mchango wenu utasaidia katika eneo hilo,“ amesema Dkt. Jafo huku akiwahakikishia kuwa Serikali kupitia Ofisi ya Makamu wa Rais itaendelea kuwapa ushirikiano mkubwa ili kufika malengo katika kuhakikisha mazingira yanahifadhiwa vizuri na kuwa endelevu.


Awali Mkurugenzi wa PEW Bw. Simon Reddy ameelezea mkakati wa shirika hilo katika kushirikiana na WI kutekeleza mradi huo katika maeneo ya Tanzania Bara na Zanzibar.


Ameomba ushirikiano kutoka serikalini ili kufikia malengo katika kuhakikisha utekelezaji wa mradi unakuwa wa mafanikio kama unavyotekelezwa katika nchi zingine.


Pia, Bi. Julie Mulonga kutoka WI shirika hilo limejikita zaidi katika kusaidia katika kuendeleza hifadhi pamoja na kurejesha uoto wa asili hapa nchini. 


Amesema tangu walipoanza shughuli zao wametoa mchango wao katika kupitia mpangokazi wa kuendeleza maeneo ya mikoko hususan katika Delta ya Rufiji.


Kikao hicho kimewahusisha wataalamu kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais pamoja na Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC).






KAMPUNI ya sukari ya kilombero imetangaza ushiriki wake katika kutoa msaada wa kibinadamu kwa jamii inayoishi wilaya ya Kilombero, ambayo imeathiriwa vibaya na matukio ya mafuriko yanayoendelea nchini kote yaliyo sababishwa na mvua kubwa.

Hafla hii ya utoaji msaada imefanyika katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kilombero, ambapo kampuni imetoa mchango wa tani sita za mahitaji muhimu ya chakula, ikiwa ni pamoja na maharage, unga wa mahindi, na mchele. Mchango huu unatarajiwa kusaidia zaidi ya kaya 500 zilizoathiriwa na mafuriko.

Wakati wa kukabidhi mchango huo, wenye thamani ya Shilingi za Tanzania milioni 15, Bwana Victor Byemelwa, Meneja wa Mawasiliano na Uhusiano na Wadau wa Kampuni ya Kilombero Sugar, Amesema msaada huo ni sehemu ya Programu ya Misaada ya Maafa ya kampuni. "Kilombero Sugar inaahidi kujali ustawi wa jamii yetu. Mchango wa leo unadhihirisha utayari na uadilifu wetu kwa jamii tunayoihudumia. Tumetoa msaada kwa zaidi ya familia 500, Kwa kulenga mahitaji yanayohitajika kwa haraka zaidi.

Zaidi ya hayo, Bwana Byemelwa amewahimiza wadau wengine kuunga juhudi za serikali za kusaidia jamii zilizoathiriwa na mafuriko ya hivi karibuni,Pia amesisitiza umuhimu wa hatua za pamoja dhidi ya mabadiliko ya hali ya hewa. Hii ikithibitisha tena dhamira ya Kampuni ya Kilombero Sugar kwa uhifadhi wa mazingira.

Mheshimiwa Bwn. Dunstan Kyobya, Ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Kilombero, amekiri umuhimu wa kupata msaada huo kwa wakati: Amesema "Jamii yetu imeathirika sana na mvua inayoendelea, hivyo michango iliyotolewa na hawa ndugu zetu Kilombero sugar tunaithamini sana." Ameongeza kuwa msaada huu unatokana na ushirikiano thabiti kati ya serikali na sekta binafsi katika kushughulikia masuala muhimu.

Bwn. Kyobya amefichua kuwa idadi ya kaya zilizoathiriwa na mafuriko inafikia 1,500, ambapo ameeleza kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Mlimba imeathirika hasa maeneo ya Utengule na Masagati. Amesisitiza dharura ya msaada wakati juhudi zinaendelea kurejesha miundombinu katika hali yake kabla ya maafa.

Bwana Hassan Abdallah, ambaye ni mkazi wa eneo la Msagati pia muathirika wa tukio hilo amesema kuwa. "Mafuriko yaliharibu kila kitu, yakiiacha familia yangu na mimi bila makazi. Tumepokea msaada kutoka kwa serikali na mashirika kama vile Kilombero Sugar, Kwakweli msaada huu umetusaidia kupunguza mateso tuyayopitia katika kipindi kigumu.

Kilombero Sugar Company Ltd imeendeleza ahadi yake kwa jamii kwa kutenga rasilimali kwa Programu yake ya Misaada ya Maafa, ili kupunguza athari za maafa ambayo yanaweza kuathiri maeneo inayohudumia.


By Manish Jangra, Country Head, Samsung Electronics Tanzania

If you ask me to name the most common electrical appliance that Tanzanians had at home over the past two decades, I will tell you that it was the television.

You might be surprised, but that's largely the reality compared to the current situation where almost every household activity is done with a home appliance.

If you asked anyone during that time why they didn’t buy an electric stove, kettle, refrigerator, washing machine, blender, or air conditioner, they would tell you that it was a luxury to have them and that they increased electricity expenses, thus the cost of living.

But the situation has changed significantly; many people are considering different ways to simplify their daily lives, by doing multiple things within a short time.

According to Statista, in 2024, revenue in the household appliances market in Tanzania reached 3.03 billion US dollars. This market is estimated to grow annually by 5.54% (CAGR 2024-2028).

By 2024, online sales are expected to contribute 1.1% of all revenue in the household appliances market in Tanzania. In addition, the household appliances market is expected to experience a growth of 3.9% in 2025.

This is a good sign for the growth and increase in the use of home appliances, which has for many years, been advocated for by manufacturing and distribution companies of electrical appliances.

Tanzania is among the fastest-growing economies in the continent, and proper utilization of production time is a non-debatable issue now. According to the World Bank, on Tanzania’s economic outlook, the update shows the economy has been resilient, growing by 5.2% in 2023, compared to 4.6% in 2022. And the growth for 2024 is projected at 5.6%.

It is now common to find many Tanzanian families no longer using charcoal and wasting time preparing breakfast. The presence of home appliances such as kettles and stoves has simplified and saved the time that used to be wasted in the morning. For example, several years ago, a mother or housemaid had to wake up very early to prepare breakfast for the children before school. But now, it only takes about 10 minutes because there are appliances to facilitate it.

Also, I remember in the past when it would take people the whole day to do laundry, and if you had a large family, the task could take even two days or be postponed until the following week. It was a cause of suffering for mothers or housemaids because it would take them the whole day, leaving them with indescribable exhaustion yet other household chores awaited them.

Laundry has become easier due to the existence of modern machines with great capacity and user friendliness. One prepares for laundry by making minimal preparations, leaving time for other activities.

In summary, home appliances complement many tasks, and provide time to enjoy other activities that wouldn't have been possible simultaneously. For example, it was difficult to find time for family outings and enjoyment in the past due to the whole day spent doing chores.

These developments have largely been attributed to the increased penetration and consumption of electricity in the country. According to the Tanzania eCooking Market Assessment Report conducted by the Modern Energy Cooking Services (MECS) in 2022, Tanzania has made significant progress in electricity penetration in recent years, more than doubling between 2010 and 2020 from 15% to 40%.

The government has ambitious plans for expanding electricity access and increasing production capacity, aiming for nearly 6000 MW to be added by 2026, 65% of which will be from renewable resources.

With these efforts, the fear that many customers have had in previous years will no longer be a challenge because the increase in production and access to electricity will go hand in hand with a decrease in costs. Thus, purchases and use of home appliances will further increase and reach many Tanzanians nationwide.

When discussing the use of household electrical appliances, modern technologies like AI to manage and control devices remotely will undoubtedly be included.

Manufacturers and distributors of home appliances have thought further ahead in simplifying people's daily activities. For example, with so much going on, how do you remember to turn off your home appliances? With technologies like the 3D Map View feature, first unveiled by Samsung Electronics Co., Ltd at CES 2024 and now available in all countries with SmartThings access, you can now manage their usage remotely hassle-free.

If you are among those who are afraid of having many home appliances due to electricity usage and think it's luxurious, I urge you to abandon that old-fashioned mindset.

Think about the convenience and time you'll save every day by making minimal preparations and doing other things you think are impossible.



NA EMMANUEL MBATILO, MICHUZI TV

ONGEZEKO la fedha shilingi Trilioni 10 kwenye bajeti ya Wizara ya Tamisemi imeibua matumaini kwa Wanaharakati wa masuala ya kijinsia ambapo wanatarajia itakwenda kutoa chachu ya kuinua ushiriki wa wanawake katika masuala ya uongozi na kuwaepusha na vitendo vya ukatili, unyanyasaji na kuwaondolea mazingira magumu wakati wa uchaguzi.

Hayo yamesemwa leo April 17,2024 katika Semina za Jinsia na Maendeleo (GDSS) ambazo zimekuwa zikifanyika kila Jumatano na kuwakutanisha wadau mbalimbali wa Jinsia katika viwanja vya TGNP- Mtandao Jijini Dar es Salaam.

Akizungumza wakati wa semina, Muwasilishaji Bw.Iddi Mziray amesema wamehoji kuhusiana na urejeshwaji wa mikopo ya asilimia 10 iliyoondolewa mwaka uliopita kutokana na changamoto za marejesho endapo mifumo iliyowekwa na serikali itawasaidia kujibu changamoto za wanawake wa chini ambao ndio walengwa.

"Kulikuwa na changamoto za msimu uliopita kwa wanawake, vijana na walemavu walichukua mikopo bila elimu,je mifumo hii tuliyonayo itakwenda kutatua masuala hayo na ya vikundi hewa". Amesema Mziray.

Aidha Mziray ameeleza kuhusiana na suala la miundombinu ya shule ambapo wanatarajia ongezeko la matundu vyoo pamoja na sehemu za kubadilishia taulo za kike na fedha kwa ajili ya taulo hizo ambapo wameona bajeti haijalizungumzia suala hilo moja kwa moja na tamanio lao ni kutengwa fedha kwa ajili ya masuala hayo.

Kwa Upande wake Mdau wa masuala ya kijinsia Bw.Mophat Mapunda amelipongeza bunge kupitisha Sheria ya unyanyasaji wa kijinsia kama kosa katika uchaguzi,ambapo amedai kuwa katika kanuni za uchaguzi ambazo zinatarajiwa kupitishwa hivi karibuni hazijaonesha namna ambavyo zitampa kipaumbele mwanamke.

Aidha Mapunda ameiomba serikali kuhusiana na fedha iliyotengwa kwa lengo la kutoa elimu ya masuala ya uchaguzi,iwe inakidhi kuwezesha wanawake kushiriki katika zoezi hilo ili kuongeza usawa na kuondoa suala la mfumo dume ambalo limetawala kwa jamii kubwa.

Naye, Mwanaharakati wa Jinsia Bi.Mtumwa Nindi ambaye ni mlemavu ameiomba serikali kuwapatia elimu ili wanufaike na mikopo ya asilimia 10 ambapo ameeleza kuwa mfumo huo wa porto ambao umeundwa kwa ajili ya huduma hiyo hawatambui jinsi.ya kuutumia.

TGNP kupitia semina za Jinsia na Maendeleo imekuwa ikitoa mafunzo kwa Wanaharakati namna yakupambana ili kuwa na bajeti yenye mlengo wa kijinsia ambayo itasaidia kuunda usawa kwa jinsia zote katika masuala ya fursa za uongozi pamoja na mgawanyo wa rasilimali,na umiliki wa Mali.








Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango akiagana na Waziri wa Fedha, Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango - Zanzibar, Dkt. Saada Mkuya Salum pamoja na viongozi wengine wa Shirikisho la Taasisi za Wakaguzi wa Ndani Afrika (AFIIA) mara baada ya kufungua Mkutano wa 10 wa Shirikisho hilo unaofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC).
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango akionesha tuzo aliyokabidhiwa na Shirikisho la Taasisi za Wakaguzi wa Ndani Afrika (AFIIA) wakati wa Mkutano wa 10 wa Shirikisho hilo unaofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC). Kushoto ni Waziri wa Fedha Ofisi ya Rais Fedha-Zanzibar, Dkt. Saada Mkuya Salum na kulia ni Rais wa Chama cha Wakaguzi wa Ndani Tanzania, Dkt. Zelia Njeza.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango akikabidhiwa tuzo na Rais wa Chama cha Wakaguzi wa Ndani Tanzania, Dkt. Zelia Njeza iliyotolewa na Shirikisho la Taasisi za Wakaguzi wa Ndani Afrika (AFIIA) wakati wa Mkutano wa 10 wa Shirikisho hilo unaofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC).

Waziri wa Fedha na Mipango Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dkt. Saada Mkuya akiteta jambo na pamoja Mkaguzi Mkuu wa Ndani (IAG), Bw. Benjamini Magai na viongozi wengine wa Shirikisho la Taasisi za Wakaguzi wa Ndani Afrika (AFIIA) mara baada ya kufunguliwa kwa Mkutano wa 10 wa Shirikisho hilo unaofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC).
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akiwa katika picha na Kamati ya maandalizi ya Mkutano wa 10 wa Shirikisho la Taasisi za Wakaguzi wa Ndani Afrika (AFIIA) unaofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC) Pamoja na wajumbe wengine wa mkutano.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango, akiwa katika picha ya pamoja na watoa mada pamoja na baadhi ya washiriki wa Mkutano wa 10 wa Shirikisho la Taasisi za Wakaguzi wa Ndani Afrika (AFIIA) unaofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC) mara baada ya kufungua mkutano.
Mhasibu Mkuu wa Serikali, Bw. Leornad Mkude (kushoto), akisikiliza hotuba ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa 10 wa Shirikisho la Taasisi za Wakaguzi wa Ndani Afrika (AFIIA) unaofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC).
Mkurugenzi wa Idara ya Mipango, Wizara ya Fedha, Bw. Moses Dulle (wa kwanza kiti cha pili) na Mkaguzi Mkuu wa Ndani Msaidizi Bw. Mwanika Semroki, wakisikiliza mada zilizokuwa zinatolewa wakati wa Mkutano wa 10 wa Shirikisho la Taasisi za Wakaguzi wa Ndani Afrika (AFIIA) unaofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC).


Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Rasilimali watu Wizara ya Fedha Bw. Lisius Mwenda, (wa kwanza kulia), akifuatilia hotuba ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa 10 wa Shirikisho la Taasisi za Wakaguzi wa Ndani Afrika (AFIIA) unaofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC).

(Picha na Kitengo cha Mawasiliano, Wizara ya Fedha)

Na Mwandishi Wetu,Rufiji

Wananchi walioathiriwa na mafuriko wilayani Rufiji wameiona thamani na umuhimu wa uwepo wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania - TAWA baada ya leo Aprili 16, 2024 kupokea misaada mbalimbali kutoka kwa taasisi hiyo yenye thamani ya shillingi millioni 20 ikiwemo tani 6.4 za unga wa sembe, Kilo 666 za maharage na magodoro 186.

Kwa niaba ya Kamishna wa Uhifadhi wa TAWA akimkabidhi misaada hiyo Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe. Abubakari Kunenge, Kamishna Msaidizi mwandamizi Abraham Jullu amesema TAWA imeguswa na janga la mafuriko lililowapata majirani na wadau namba moja wa uhifadhi wananchi wa Rufiji ambao wamehusika kwa kiasi kikubwa kulinda rasilimali za Hifadhi ya Selous na hivyo imelazimika kuwashika mkono.

Jullu amesema tangu changamoto hii ya mafuriko imejitokeza TAWA ilifika kwa haraka na kuongeza nguvu kwa kutoa kikosi cha Askari 24 ili kusaidia katika zoezi la uokozi ikiwa ni pamoja na kutoa elimu ya mbinu za kujikinga na madhara yatokanayo na wanyamapori wakali na waharibifu hususani mamba na viboko kwa jamii ambapo mpaka sasa TAWA imetoa elimu hiyo kwa wananchi wapatao 4,225 na bado inaendelea na zoezi hilo.

Sanjari na hilo, TAWA imetoa boti moja lenye uwezo wa kubeba jumla ya watu 15 ili kusaidia katika shughuli za uokozi zinazoendelea wilayani humo.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe. Abubakari Kunenge amemshukuru Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kupeleka misaada mbalimbali kupitia Serikali na Chama Cha Mapinduzi tangu wilaya hiyo ipate changamoto hiyo ya mafuriko.

Pia amewashukuru Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TAWA Mej. Jen. (Mstaafu) Hamis Semfuko na Kamishna wa Uhifadhi wa TAWA Mabula Misungwi Nyanda kwa maamuzi ya haraka waliyoyafanya kupeleka misaada hiyo kwa wananchi wa Rufiji kwa wakati.

Mkuu huyo wa Mkoa ameendelea kuishukuru TAWA kwa msaada wa boti kwa ajili ya kufanya shughuli za uokozi na ushiriki wao wa ujumla katika zoezi la uokozi kwa kushirikiana na vyombo mbalimbali vya dola na kukiri kuwa wananchi wa Rufiji wanaona thamani na umuhimu wa uwepo wa Taasisi hiyo Mkoani Pwani.

Licha ya kuishukuru TAWA, Mkuu wa wilaya ya Rufiji Meja Edward Gowele amesema TAWA imekuwa na mahusiano na mashirikiano mazuri kati yake na uongozi wa wilaya yake ndio maana imekuwa rahisi kwao kuitikia wito wa kutoa msaada kufuatia janga lililoikumba wilaya hiyo.
 

Mkuu wa Mkoa wa Pwani  Abbakari  Kunenge alizungumza wakati wa kupokea msaada kutoka TAWA kwa ajili walioarhiriwa na mafuriko Rufiji na Kibiti.

 

Picha za makabidhiano ya msaada uliotolewa na TAWA.

 

Matukio ya picha mara baada ya kukabidhiana  msaada.

*Kikao cha kugushi walipeleka hazina ajili ya hiyo bajeti

Na Chalila Kibuda,Michuzi Blog

Fedha zilizobadilishwa matumizi bila kuidhinishwa na mamlaka husika na utumiaji wa nyaraka za kubadili matumizi ya udanganyifu kiasi cha Sh. bilioni 4.88

Ukaguzi ulibaini kwamba mamlaka nne za serikali za mitaa zilibadilisha matumizi ya kiasi cha Sh.bilioni 4.88bila kupata idhini kutoka kwa mamlaka husika, zikiwamo Baraza la Madiwani na Waziri wa Fedha.

Halmashauri iliyobanika katika ripoti ya CAG kati ya hizo ni Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe mkoani Katavi ilipanga kutumia bajeti ya kiasi cha Sh.bilioni 7.06 kwa
ajili ya kulipa mishahara hata hivyo, bajeti hiyo ilibadilishwa kwa
kuongeza kiasi cha Sh.bilioni 2.07. Kati ya kiasi kiasi hicho kilichotengwa Sh.bilioni 1.61 tu ndizo zilizotumika.

Pia ukaguzi ulibaini nyaraka za mihutasari ya kikao cha kamati ya fedha, mipango na uongozi kilichofanyika tarehe 5 Juni 2023 zilighushiwa na kuwasilishwa Hazina kwa ajili yakuombakibali cha kubadili vifungu vya bajeti ya mishahara, ingawa kikaohicho hakikufanyika kama inavyoelezwa kwenye.

Hii ni kinyume na Kifungu Na.41(2) cha Sheria ya Bajeti, [Sura ya 439], ambacho kinaeleza kwamba ofisa masuuli hatabadilisha matumizi ya fedha endapo fedha hizo zinapaswa kuhamishwa kwenda kwa mtu au kwa taasisi zingineza serikali.


Maombi ya kubadilisha matumizi ya fedha yanapaswa kuambatishwa na taarifa inayoelezea kikamilifu sababu za ukosefu wa fedha zilizoidhinishwa awali. Baada ya kujadiliwa na kamati ya fedha mipango na uongozi, maombi hayo huwasilishwa kwa Baraza la Madiwani kwa ajili ya kuidhinishwa.


Pia, Kifungu cha 41(1&2) cha Sheria ya Bajeti, [Sura ya 439], kinaruhusu
ofisa masuuli, kwa idhini ya waziri, kubadili matumizi kutoka kwenye
matumizi yaliyoidhinishwa.

Hata hivyo, Ofisa masuuli hatabadili matumizi ya fedha katika mazingira yafuatayo ambapo fedha zimetengwa kwa ajili ajili ya kazi maalum fedha zilizotengwa kwa ajili  ya kuhamishwa kwenda kwa mtu au taasisi zingineza serikali fedha zilizotengwa kwa ajili ya matumizi ya shughuli zinazohusiana  na maendeleo fedha zilizotengwa kwa ajili ya mishahara kwenda kwenye matumizi mengine yasiyo ya mishahara na uhamishaji wa fedha mwingineo unaweza kusababisha ukiukwaji wa kanuni za kifedha.
NA EMMANUEL MBATILO, MICHUZI TV

WIZARA ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imeahidi kusimamia na kutekeleza ipasavyo utolewaji wa elimu ya masuala ya fedha kwa wanafunzi wa elimu ya juu ili taifa liweze kuwa na wataalam bobezi wa masuala ya kifedha.

Kauli hiyo imetolewa leo Aprili 17, 2024 Jijini Dar es salaam na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe.Omary Kipanga wakati akifungua warsha ya siku tatu kwa viongozi wa vyuo mbalimbali nchini ili kujadili mitaala ya elimu ya fedha kwa wanafunzi wa elimu ya juu huku ukiratibiwa na Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Amesema suala la elimu ya fedha kwa jamii ni muhimu kwa maendeleo ya nchi hivyo ni vyema elimu hiyo ikafika kwa jamii Ili watanzania waweze Kupata elimu ya masuala ya fedha.

Aidha Naibu Waziri Kipanga amesema serikali ya awamu ya sita imedhamiria kujenga uelewa wa masuala ya fedha kwa jamii.

“Wizara tutahakikisha elimu ya fedha inafundishwa katika mfumo wa elimu nchini hivyo twende kwa haraka kuhakikisha vijana ambao ni sehemu ya jamii nchini wanakuwa na uelewa wa masuala ya fedha hivyo natarajia wakuu wa vyuo mtabeba uelewa huo muhimu kwa vyuo vyetu nchini,” amesema Mhe. Kipanga.
.
Pamoja na hayo amesema kuwa BoT, itaendelea kusimama na vyuo na taasisi za elimu na Wizara ya Elimu katika kuhakikisha dhana ya elimu hiyo inakuwa endelevu na inafundishwa katika ngazi za jamii hata katika elimu zisizo rasmi.

Hata hivyo ameviagiza vyuo vikuu kushirikiana na BoT kufanya tathmini ya utekelezaji wa mpango huo ili kuboresha mbinu na nyenzo za kufikisha ujumbe huo kwa jamii.

“Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ipatiwe taarifa ya tathmnini mtakazofanya ili itusaidie katika kufanya maamuzi, serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan imedhamiria kujenga uelewa wa masuala ya fedha kwa jamii,” amesema.

Kwa upande wake Naibu Gavana Benki Kuu ya Tanzania Bi. Sauda Msemo amebainisha kuwa lengo la kutoa elimu ya fedha kwa Vijana wa kitanzania wanaosoma elimu ya juu ni kuwawezesha kupata ujuzi na uzoefu wa matumizi ya fedha.

Amesema takwimu ya Sensa ya Watu na Makazi mwaka 2022 inaonesha takribani watu asilimia 34.5 ni vijana walio na umri kati ya miaka 15-35 hivyo ili kuleta tija na ufanisi katika masuala ya uchumi ujuzi na uzoefu wa masuala ya fedha ni moja ya sifa muhimu kufikia azma hiyo.

Ameeleza kuwa elimu ya fedha kwa Watanzania kutachochea maendeleo kwa kuongeza utumiaji rasmi wa huduma za fedha na kuwawezesha watu wengi kuwa na uwezo wa kufanya maamuzi sahihi ya kifedha na kuendesha shughuli zao kwa ufanisi kukuza uchumi kwa ujumla.

Bi. Sauda mesema elimu kwa vijana wa vyuo vikuu itawasaidia kuweka akiba, kupanga bajeti na kufanya uamuzi wa masuala ya fedha kwa kuzingatia viashiria hatarishi na kuelewa taasisi mbalimbali zinazotoa huduma za fedha ili kufanya maamuzi sahihi ya fedha ili waitawale.

” Tunatarajia kujenga ‘displine’ ya fedha kupitia elimu ya fedha kwani watakuwa na uwezo wa kutawala fedha sio fedha kuwatawala vijana hao,” amesema.

Pia amesema BoT kwa kushirikiana na wadau wengine wa Baraza la Huduma Jumuishi za Fedha, imetoa muongozo na mtaala wa elimu ya fedha kwa wakufunzi ambao utatumika na taasisi za elimu ya juu kwa kuwafundisha watoa huduma za elimu ya fedha kuwafikia wananchi wote walio nje mfumo wa elimu.

“Tayari tumeingia makubaliano na baadhi ya taasisi zaa elimu katika mtaala huo wa kufunzi wa fedha na tulioingia nao makubaliano ni Chuo Kikuu cha Iringa, Zanzibar, Chuo Kikuu cha Usimamizi wa Fedha(IFM) na Chuo cha Benki Kuu ya Tanzania ,” ameseama.

Katika warsha hiyo imebainishwa kuwa elimu ya fedha inapaswa kumfikia kila mmoja ili aweze kuwa na nidhamu katika matumizi ya pesa lakini kuepuka kuingia kwenye sitofahamu ambayo inawakuta wengi hasa wanapokwenda kwenye taasisi za mikopo.
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe.Omary Kipanga akizungumza wakati akifungua warsha ya siku tatu kwa viongozi wa vyuo mbalimbali nchini ili kujadili mitaala ya elimu ya fedha kwa wanafunzi wa elimu ya juu huku ukiratibiwa na Benki Kuu ya Tanzania (BoT). Hafla hiyo imefanyika leo Aprili 17, 2024 katika ukumbi wa BoT Jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe.Omary Kipanga akifungua warsha ya siku tatu kwa viongozi wa vyuo mbalimbali nchini ili kujadili mitaala ya elimu ya fedha kwa wanafunzi wa elimu ya juu huku ukiratibiwa na Benki Kuu ya Tanzania (BoT). Hafla hiyo imefanyika leo Aprili 17, 2024 katika ukumbi wa BoT Jijini Dar es Salaam.


 Naibu Gavana Benki Kuu ya Tanzania Bi. Sauda Msemo akizungumza wakati wa ufunguzi wa warsha ya siku tatu kwa viongozi wa vyuo mbalimbali nchini ili kujadili mitaala ya elimu ya fedha kwa wanafunzi wa elimu ya juu huku ukiratibiwa na Benki Kuu ya Tanzania (BoT). Hafla hiyo imefanyika leo Aprili 17, 2024 katika ukumbi wa BoT Jijini Dar es Salaam.


Viongozi wa Vyuo Vikuu mbalimbali nchini wakiwa kwenye ufunguzi wa warsha ya siku tatu kwa viongozi wa vyuo mbalimbali nchini ili kujadili mitaala ya elimu ya fedha kwa wanafunzi wa elimu ya juu huku ukiratibiwa na Benki Kuu ya Tanzania (BoT). Hafla hiyo imefanyika leo Aprili 17, 2024 katika ukumbi wa BoT Jijini Dar es Salaam.

(PICHA ZOTE NA EMMANUEL MBATILO)

Top News