Meneja Masoko wa Kampuni ya Parimatch Levis Paul akizungumza machache mara baada ya Kuzinduliwa kwa Msimu wa tatu wa Shindano la Bingwa ambapo msimu huo Kampuni hiyo ikiwa wadhamini wakuu wa shindano.
 Meneja programu wa shindano la Bingwa Ombeni Phiri akieleza namna Shindano hilo litakavyoshirikisha Mikoa mitano ambayo ni Arusha,Mbeya,Mwanza,Dodoma pamoja na Dar es Salaam.
Meneja Masoko wa Kampuni ya Startimes David Malisa akizungumza na Wanahabari Leo Aprili 24,2024  Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam  wakati wa Uzinduzi wa Msimu wa tatu wa Shindano la Bingwa ambapo amewataka wateja wa Kisimbuzi cha Startimes kulipia kifurushi ili kuendelea kuona shindano hilo kupitia Tv3

SHINDANO la Mtindo wa Maisha (Life style) Kwa Vijana wenye ushawishi Mitandaoni ( BINGWA ) Msimu wa tatu umezundiliwa rasmi Vijana Mikoani wapewa nafasi .

Akizungumza na Wanahabari Leo Aprili 24,024 Ukumbi wa Serena Hoteli Jijini Dar es Salaam wakati wa kuzindua Shindano hilo kwa Msimu wa tatu Meneja wa Shindano hilo Ombeni Phiri amesema Shindano hilo limewapa fursa Vijana wengi mitandaoni kubadilisha maisha kutokana na fursa mbalimbali ambazo wamekuwa wakizipata na hivyo kulazimika Shindano hilo kuendelea kuwepo ambapo msimu huo wa tatu umekuwa wa kitofauti zaidi.

"Misimu miwili imekuwa yenye Mafanikio makubwa zaidi na Vijana wengi wa mitandao kuonesha Maisha yao halisi wanapokuwa kwenye mjengo huo hivyo kwa Msimu huu watatu Umepewa nguvu na Kampuni ya Kubashiri ya Parimatch ili kumsukuma Mshindi huyo kufanya vitu vikubwa zaidi Pape Shindano linapomalizika

Msimu Mpya wa tatu wa show ya Bingwa itatembelea Mikoa mitano kwa ajili ya kutafuta Vijana wengine ambapo maoni mengi yamekuwa yakiwafikia Vijana wakihitaji kushiriki Shindano hilo.

"Msimu wa tatu umefanya Maboresho mbalimbali ikiwemo ongezeko la Mikoa mitano ya washiriki ikiwemo Arusha, Dodoma,Mwanza, Mbeya pamoja na kitovu chenyewe Dar es Salaam.

Pia ameeleza kuwa usahili kila Mkoa utachukua washiriki 10 kila Mkoa na kufatia mchujo katika App ya Startimes (Startimes On) ambapo washiriki 08 watatoka Dar hivyo kukamilisha Jumla ya watakaoingia ndani ya nyumba washiriki 24 huku zawadi ya Mshindi kugharimu zaidi ya Milioni 35 za Kitanzania.

Kwa Upande wake Meneja Masoko wa Kampuni ya Startimes David Malisa amesema Msimu wa tatu utaendelea kuwapa fursa vijana zaidi na Atakaeibuka Mshindi Kampuni ya Startimes itaweza kumpa Ubalozi.

Aidha amewapongeza Kampuni ya Parimatch kuona haja ya kuwapa Moyo Vijana hao wenye ushawishi Mitandaoni kukuza vipaji vyao.

Pia amewataka wateja kulipia vifurushi cha Uhuru elfu 23000 ili kuweza kuona shindano hilo kupitia Tv3 ndani ya King'amuzi cha Startimes.

Nae Meneja Masoko wa Parimatch Levis Paul ameeleza sababu ya Kampuni hiyo kuishika mkono Shindano hilo la " Bingwa".

"Sababu ya Parimatch kuungana na Msimu wa tatu wa Shindano la bingwa ni kutokana na shindano hilo Kuhusisha Vijana na Kauli mbiu ikibeba Jumba la Washindi ambapo Kampuni yetu inalenga zaidi kutafuta Washindi walipo kwa kupitia ubashiri."

Paul ameeleza wao kama Parimatch wanatambua kuwa Washiriki wanahitaji kukaa siku 70 ambapo kila kitu kinahitaji uwezeshwaji kuanzia Malazi na vitu mbalimbali hivyo Tv3 na Startimes peke wanahitaji nguvu ya ziada ya kuendesha Shindano hilo hivyo sisi tumeona tuongeze nguvu hiyo kwa msimu huu wa tatu."

Pia amefafanua zaidi kuwa Wana amini kuwa chapa ya Kampuni hiyo ipo sehemu na sahihi hivyo kudhamini shindano hilo itaongeza na kujiweka kwenye nafasi nyingine nzuri zaidi ya kujitangaza kama Kampuni.

Serikali kupitia Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) imesema kuwa ina lengo la kuboresha maisha ya wananchi wa tarafa hiyo kwa kuwaelimisha na kuwahamisha wananchi waliojiandikisha kuhama kwa hiyari kwenda Kijiji cha Msomera Handeni Mkoani Tanga na maeneo mengine nchini.

Akizungumza na wananchi wa tarafa ya Ngorongoro kwa nyakati tofauti katika zoezi la uelimishaji, uhamaishaji na uandikishaji kaimu meneja wa Uhusiano kwa Umma wa mamlaka hiyo Hamis Dambaya amesema zoezi la kuwaelimisha wananchi hao litaendelea ili kuhakikisha kila mkazi wa tarafa ya Ngorongoro anahama kwa hiyari. 

Amewaeleza wananchi hao kwamba serikali haina nia mbaya kwa kuwashawishi kuhama kutoka ndani ya hifadhi kwani inatambua kuwa iwapo wananchi hao watakubali kuhama wataweza kuboresha maisha yao katika maeneo mbalimbali watakayoamua kuelekea sambamba na kulinda usalama wao kutokana na uwepo wa matukio ya wanyama wakali ndani ya hifadhi. 

“Mnaishi katika mazingira magumu hasa kutokana na kukosa uhuru wa kuingia na kutoka ndani ya hifadhi, kuhofia Wanyama wakali ambao wamekuwa hatari kwa mifugo na baadhi ya wananchi, serikali imefanya uamuzi sahihi wa kuwahamasisha ili kuwa na Maisha bora na huru nje ya hifadhi,”alisema bwana Dambaya.

Bwana Dambaya amesisitiza kuwa serikali imejipanga vizuri katika kuhakikisha kila mwananchi anayekubali kuhama kwa hiyari kutoka ndani ya hifadhi anapata stahiki zake zote za kisheria ikiwemo kitita cha shilingi milioni kumi wanaohamia msomera na shilingi Milioni kumi na tano wanaohamia maeneo mengine ambapo fedha hizi zinatolewa kama motisha na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan.

Amewataka wananchi hao kuachana na propaganda za baadhi ya wanasiasa na wanaharakati wasiowatakia mema kwa kuwashawishi kuendelea kubaki ndani ya hifadhi huku wao na familia zao wakiishi katika miji mbalimbali nchini na kufanya shughuli zao katika mazingira magumu.

“Msihadaike na watu wenye nia ovu wanaowashawishi mbaki ndani ya hifadhi, hameni kwa hiyari kuelekea katika Kijiji cha Msomera na maeneo mengine ambayo huduma za kijamii zimeboreshwa kwa mustakabali wenu na vizazi vyenu”,alisema bwana Dambaya.

Katika ziara hiyo ya tarafa ya Ngorongoro timu ya uhamasishaji imeweza kutembelea kaya mbalimbali katika Kijiji cha Naiyobi, Kapenjiro na endulen ambapo wananchi kadhaa walielimishwa na kukubali kuhama kwa hiyari na kuamua kujiandikisha.





Na Mathias Canal

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan ametoa Bilioni 66 kwa ajili ya kuanza urejeshaji wa miundombinu ya barabara zilizoharibika nchini.

Fedha hizo tayari zimegawanywa kwa mameneja wa TANROADS mikoa yote iliyoathirika kwa ajili ya kufanya kazi kwa haraka usiku na mchana ili kurekebisha kadhia zilizozikumbumba barabara kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha nchini.

Akizungumza jana Jijini Arusha mara baada ya kukagua Barabara ya Afrika Mashariki (Arusha bypass) iliyoharibiwa na mvua hizo, Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS) Mha. Mohamed Besta amesema kuwa kutokana na udharula huo tayari Rais Samia ametoa fedha za matengenezo ya miundiombinu hiyo ambazo zimeshapelekwa katika Mikoa yote Nchini.

Mhandisi Besta amesema kuwa tayari kazi inaendelea katika maeneo yote nchini na fedha hizo zinaratibiwa na vitengo maalumu vya dharula vilivyopo TANROADS pamoja na ofisi za mikoa.

Ameongeza kuwa kutokana na tathimini iliyofanyika mpaka sasa zaidi ya Shilingi Bilioni 250 zinahitajika kwa ajili ya ukarabati wa miundombinu ya Barabara kuu za Mikoa yote Nchini ambazo zimeharibika vibaya kutokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha sehemu mbalimbali nchini.

Amesema kuwa kuna baadhi ya maeneo kama Kanda ya Ziwa na Nyanda za juu kusini mwa Nchi mvua zimeendelea kunyesha tangu mwezi Oktoba mwaka jana, na sasa unaelekea mwezi wa saba na mvua bado zinaendelea kunyesha.

“Tunamshukuru Mhe Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwani ametupatia shilingi bilioni 66 ambazo tumezisambaza katika Mikoa yote ambapo mameneja wote wa Mikoa wamepewa kutokana na hali ya dharura ya Mkoa husika’’ ameeleza

Naye Meneja wa TANROADS Mkoa wa Arusha Mhandisi Regnald Massawe amesema Mkoa huo umetengewa kiasi cha shilingi bilioni 2.5 kwa ajili ya kazi hizo za dharura na matengenezo ya kurejesha miundombinu hiyo yanaendelea kufanyika kwa kasi.







MKUTANO wa 5 wa Harvard Kennedy School China umefanyika katika Shule ya Harvard Kennedy Usiku wa tarehe 21, Pang Xinxing, Mwenyekiti wa Startimes Group, alialikwa kuhudhuria mtandaoni.

Aidha Lengo Mkutano huo ni kujenga daraja la mawasiliano kati ya China na ulimwengu, kutoa jukwaa rafiki na wazi kwa majadiliano kati ya academia ya kimataifa, serikali, biashara, na viongozi wa jamii.

Kauli mbiu ya mkutano huu ilikuwa "Uaminifu na Ushirikiano," ukiwa na vikao tisa vinavyojadili mada kama "Mahusiano ya Marekani na China," "Uchumi wa Dunia na Uchumi wa China," "Utawala wa Dunia wa Akili Bandia," "China na Kusini Mashariki mwa Asia," "China na Mashariki ya Kati," "China na Afrika," "China na Amerika Kusini," miongoni mwa mengine.

Hafla hiyo ilialika Xie Feng, Balozi wa China nchini Marekani, Graham Allison, mwanzilishi wa Shule ya Harvard Kennedy Graham Allison, Dean Xue Lan wa Chuo Kikuu cha Tsinghua cha Schwarzman, pamoja na wawakilishi kutoka kwa sekta za kisiasa, biashara, na kitaaluma za nchi zote mbili, zaidi ya wanafunzi na wanachama 300 wa fakulteti wa Harvard, na zaidi ya wanafunzi 300 wa Kichina wanaosoma nchini Marekani.

Kupitia mawasiliano na ushirikiano, mkutano ulilenga kupata njia za pamoja za maendeleo.

Kama mwanzilishi wa kampuni inayoongoza ya televisheni ya kidigitali barani Afrika, Pang Xinxing, Mwenyekiti wa Startimes Group, alitoa hotuba mtandaoni katika kikao cha "China na Afrika: Matarajio ya Baadaye," akishiriki safari ya kuanzishwa, kukua, na maendeleo ya biashara ya Afrika ya Startimes Group na washiriki.

Tangu kuanzishwa kwake, imekuwa kikihusika sana katika uga wa utangazaji, televisheni, na vyombo vya habari vipya.


Mwenyekiti Pang Xinxing alitambulisha: "Nchini China, StarTimes imepitia mchakato mzima wa maendeleo ya televisheni ya waya ya Kichina, kutoka kutokuwepo hadi kuwepo, kutoka analogia hadi kidijitali, ikawa msanidi wa mfumo na mtoa teknolojia mwenye athari kubwa katika tasnia ya redio na televisheni ya Kichina."

Barani Afrika, kuanzia kupata leseni ya kwanza ya uendeshaji wa televisheni ya kidigitali nchini Rwanda mwaka 2007, baada ya miaka karibu ishirini ya uendeshaji na maendeleo, "StarTimes imesimamisha jukwaa la usambazaji wa mtandao linalofunika nchi 45 na watu bilioni 1.2 katika Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara.

Imekuwa kampuni pekee inayotoa huduma za video ndefu za kulipia katika mikoa inayozungumza Kiingereza, Kifaransa, na Kireno barani Afrika kwa wakati mmoja.

Imesimamisha mfumo wa uzalishaji wa yaliyomo kupitia ujumuishaji wa programu, tafsiri ya programu, na uzalishaji wa programu, sasa ikipeperusha seti 830 za vituo vya televisheni vya Kiafrika vya kimsingi, vituo vilivyoendeshwa na StarTimes, na vituo vya kimataifa kwenye jukwaa katika lugha zaidi ya kumi kwa matangazo ya 24 masaa kwa siku.


Imesimamisha mfumo kamili wa masoko na mfumo wa huduma baada ya mauzo, ikiwa ni pamoja na maduka zaidi ya 200 na maduka ya urahisi zaidi ya 30,000, na imeunda wafanyikazi wa 4,000."
Aliyaeleza: "StarTimes imekuwa ikifanya uwekezaji endelevu katika tasnia ya habari ya Afrika na kutoa mchango wake katika digitalization na habari za jamii ya Kiafrika," ikiwa ni pamoja na kuvunja monopolies za tasnia, kukuza upanuzi wa televisheni ya kidigitali barani Afrika, kupunguza kwa kiasi kikubwa vikwazo vya uwekezaji na teknolojia kwa vyombo vya habari vya televisheni vya eneo hilo, kukuza utajiri na maendeleo ya vyombo vya habari vya Kiafrika vya eneo hilo, kuandaa mashindano ya kudubu lugha za Kiafrika ili kuchagua na kutoa mafunzo kwa vipaji vya kudubu vya eneo hilo, kuanzisha vituo vya kudubu katika makao makuu ya StarTimes na mahali pengine barani Afrika kukuza urithi na maendeleo ya utamaduni wa Kiafrika wa eneo hilo, na zaidi.


Leo, StarTimes imekuwa chapa inayojulikana sana barani Afrika Katika ushirikiano unaongezeka kati ya China na Afrika leo, uendeshaji wa StarTimes barani Afrika unaingia kwenye kipindi cha mavuno. Mwenyekiti Pang Xinxing alibainisha, "Kwa kina cha ushirikiano wa kiuchumi na biashara kati ya China na Afrika na kuongezeka kwa usaidizi kwa miundombinu ya nishati barani Afrika na mashirika kama Benki ya Dunia, umeme barani Afrika unazidi kuwa wa kawaida.

Kadiri inavyoendelea, muongo ujao bila shaka utakuwa muongo wa upanuzi wa vituo vya kidigitali (vya akili) vya nyumbani barani Afrika. Tuna imani kamili katika maendeleo ya uchumi wa Kiafrika!"
Mwenyekiti Pang xing xing wa  StarTimes Group akitoa hotuba kwenye mkutano) Mkutano wa Harvard Kennedy School China, ulioanzishwa na Chama Kikuu cha Harvard Kennedy Greater China, unazingatia maendeleo ya uchumi, siasa, na utamaduni wa China na nchi za nje
(Washiriki wakisikiliza hotuba na kujadiliana na Mwenyekiti Pang)
Startimes Group ilianzishwa mwaka 1988 na kina historia ya miaka 35.

Na Mwandishi wetu

Matumizi ya Mfumo wa kuwezesha uratibu wa shughuli za uandaaji wa vikao mbalimbali vya bodi na menejimenti katika Halmashauri na Taasisi za Umma. (e-Board), umetajwa kurahisisha uendeshaji wa vikao na kupunguza gharama za maandalizi katika halmashauri ya Manispaa ya Ilemela jijini Mwanza.

Akizungumza kuhusu mfumo huo ofisini kwake jijini Mwanza, Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya Manispaa ya Ilemela Bi. Ummy Mohammed Wayayu, amesema kuwa kabla ya halmashauri hiyo kuanza kutumia mfumo wa e-Board mwaka 2023, fedha nyingi zilikuwa zinatengwa katika ununuzi wa shajara,wino na vifaa vingine kwa ajili ya vikao vya madiwani na menejimenti.

“Kwa mwaka tulikuwa tunatumia takribani shilingi milioni 200 hadi 300 katika maandalizi ya uendeshaji wa vikao, lakini kwa sasa gharama hizo hatuna tena kwakuwa tunatumia mfumo huu wa e-Board, ambao umetusaidie kupeleka fedha hizo katika mambo mengine ya muhimu katika halmashauri,” alisema Bi.Ummy.

Aliongeza kuwa, mfumo wa e-Board umesaidia kupunguza gharama za kudurufu taarifa mbalimbali na badala yake zinapakiwa kwenye mfumo na madiwani wanapakuwa na kuendelea kuzifanyia kazi.

Licha ya mfumo huo kusaidia katika kupunga gharama, Mkurugenzi huyo amesema kwamba mfumo wa e-Board umesaidia katika upigaji wa kura za siri katika uchaguzi wa Wenyeviti wa Kamati pamoja na uchaguzi wa Mstahiki Meya.

“Hapo awali usiri katika chaguzi hizo ulikuwa mdogo sana, lakini kwa sasa tunatumia mfumo hivyo kura zinakuwa za siri na kila mtu ndani ya nafsi anajua amemchagua nani,” alifafanua.

Aidha, Bi Ummy aliongeza kuwa mfumo wa e-Board unawasaidia madiwani kushiriki katika kila kikao hata wanapokuwa nje ya halmashauri hiyo kwa kutumia vishkwambi ambavyo vimewezeshwa matumizi ya mfumo huo na kugawiwa kwa kila diwani.

Kwa upande wake Mstahiki Meya wa Halmashauri hiyo Mheshimiwa Renatus Mulunga, alisema kuwa mfumo wa e-Board umewasaidia madiwani kuendesha vikao vyao kwa ufanisi ili kuboresha huduma za wananchi wa Ilemela.

“Nina miaka 25 kwenye udiwani, huko nyuma ilikuwa lazima ujaze gari mafuta kwa ajili ya kusambaza makarabrasha, lakini kupitia mfumo wa e-Board kila diwani anapata taarifa na makabrasha yake popote alipo kupitia mfumo na kuanza kuyafanyia kazi,” alisema Bw. Mulunga.

Mhe.Mulunga alitoa rai kwa halmashauri nyingine ambazo bado hazijaanza kutumia mfumo wa e-Board, kufanya ziara halmashauri ya Manispaa ya ilemela ili zikajifunze au kuwasiliana na Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA), ili zipate uelewa kuhusu mfumo huo.

Naye Mkuu wa Kitengo cha TEHAMA wa Halmashauri ya Ilemela Bw.Isaack Tanguye, alisema kwamba halmashauri hiyo ilianza kutumia mfumo wa e-Board baada ya kupata malalamiko kuhusu gharama kubwa za uandaaji wa vikao.

Alisema kwamba baada ya malalamiko hayo kuwa mengi, kitengo chake kiliamua kuwasiliana na e-GA kuomba mfumo wa e-Board, na baadaye walianza kuwajengea uwezo Madiwani pamoja na Menejimenti ya halmashauri hiyo ili kuanza kufanya vikao vyao kidijiti.

Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela ndiyo halmashauri ya kwanza kuanza kutumia mfumo huu wa e-board kati ya halmashauri 184 nchini, mfumo huu umesanifiwa na kutengenezwa na Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA).

KAMPUNI ya Tanzania(TBL) imedhamiria kuwasaidia wakulima nchini kwa kutambua uwezo wao wa kulisha watu, viwanda, na biashara katika ukanda huu kupitia mikataba ya wakulima iliyoimarishwa.

TBL walifanya hafla ya kushirikisha wadau jana ili kupitia, kuthibitisha na kuwasilisha mapendekezo kwa Serikali ya Tanzania ili kuwezesha mipango ya kimkataba na masoko yenye umuhimu kuwezesha fedha na uwekezaji kwa wakulima na miundombinu ya kilimo na ugavi, hususani nafaka na mazao mengine. ngano, alizeti, soya, nk).

Msukumo wa ushirikiano huo ni kwamba licha ya uwezekano wa Tanzania kuwa kapu la chakula la kikanda na kuwaunganisha wakulima na viwanda vya ndani na vya kikanda vya mazao kwa ajili ya uongezaji thamani na usindikaji, changamoto za uwezo ndani na kando ya mnyororo wa ugavi zinapunguza hili kutokea.

Changamoto hizi kwa kiasi kikubwa husababishwa na upatikanaji mdogo wa fedha na mitaji kwa wakulima, hasa kwa ajili ya uzalishaji wa kilimo, na kwa ajili ya uwekezaji wa miundombinu ya kilimo ili kuongeza tija na kupunguza hasara baada ya kuvuna.

Mpangilio unaopendekezwa wa kilimo cha mkataba unaohimizwa na ushirikiano hutoa kushughulikia mtaji na upatikanaji wa vikwazo vya kifedha na kuwaingiza wakulima zaidi na wasiochukua katika mipango ya kilimo cha mkataba, kuwezesha uwekezaji wa ugavi, na kuongeza nafaka na uzalishaji mwingine wa mazao.

Mnyororo wa thamani wa shayiri nchini Tanzania unatoa jaribio la kwanza la uboreshaji wa mpango wa kilimo cha kandarasi kama ilivyowezeshwa na ushirikiano huo.

Zao hilo linakabiliwa na ukuaji mkubwa wa mahitaji kutoka kwa TBL ambayo inapanua kiwanda chake cha kutengeneza kimea mkoani Kilimanjaro ambacho kitaongeza mahitaji hadi tani 32 kwa mwaka kutoka kwa usambazaji wa sasa wa tani 3.5 kwa mwaka (ukuaji wa karibu wa 10X).

Kwa sasa sekta hii inakabiliwa na changamoto mbalimbali, zikiwemo za uzalishaji mdogo na uwekezaji, ubora usio thabiti, uratibu hafifu baina ya wahusika, ushiriki mdogo wa wakulima, uhaba wa ardhi inayofaa, utafiti na miundombinu duni, mipangilio dhaifu ya mikataba na changamoto za uagizaji wa bidhaa nje ya nchi.

Mfumo wa kimkataba unaopendekezwa unatumika kama suluhu la sekta kama "chombo" muhimu cha kuwezesha sekta hiyo kukidhi mahitaji ya soko yanayoongezeka.

Ili kusaidia kutekeleza majaribio ya shayiri ya kimea, tukio hilo pia liliidhinisha mkakati kwa watendaji wa sekta ya shayiri ili kukidhi mahitaji ya soko la 10X kwa kutumia mfumo uliopendekezwa wa kimkataba.

Majukumu, majukumu na hatua zinazohusiana zinazokubalika zitafafanua "mkataba wa shayiri" au mpango wa utekelezaji kwa wadau wa sekta ambao utatumika kama msingi wa maendeleo zaidi na uboreshaji kupitia ushirikiano unaoendelea.

Tukio hilo ni nyongeza ya warsha ya siku nne ya kubuni iliyowakutanisha wataalam na watendaji ili kuandaa mfumo wa kuboresha kilimo cha mkataba na mkakati wa kukidhi mahitaji ya shayiri.

Timu ya kubuni suluhisho ilijumuisha wawakilishi kutoka wizara za serikali, mashirika, mamlaka za udhibiti, taasisi za fedha na vyama. Huu ni ushirikiano wa kwanza wa namna hii kuimarisha mifumo ya kilimo cha mkataba nchini Tanzania na unatoa thamani na athari kwa washirika na wadau:

Michelle Kilpin ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Bia Tanzania, alisema, “Haja ya TBL kutafuta shayiri ndani ya nchi inaendana na maendeleo ya soko nchini Tanzania ambayo yatawezesha kuongeza uzalishaji wa tani 3,500 za shayiri hadi kufikia karibu tani 20,000 za shayiri kutoka kwa wakulima wengi iwezekanavyo.

"Hata hivyo, kuegemea kutoka kiasi cha sasa hadi kiasi kinacholengwa kutahitaji mabadiliko katika mipangilio ya uuzaji ili kuwezesha uwekezaji katika ubora na uwezo wa mnyororo wa ugavi, kwa kutumia zana za kidijitali kuongeza ufanisi na uwazi, upatikanaji wa fedha kwa wakulima na wengine katika msururu wa ugavi, na ushirikishwaji na uendelevu.”

*Ni katika kutoa vitambulisho Kwa idadi kubwa ya wananchi

Na Chalila Kibuda,Michuzi TV

Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) imesema kuwa katika miaka 60 Muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar mamlaka imepata mafanikio ya kutoa Vitambulisho Kwa idadi kubwa.

Hayo ameyasema Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano Godfrey Tengeneza wakati akizungumza kuhusiana mafanikio ya mamlaka hiyo.

Tengeneza amesema kuwa hadi kufikia kutoa Vitambulisho hivyo kulitokana na kuweka mipango mikakati na kuweza kufanikisha hilo.

Aidha amesema kuwa katika utoaji vitambulisho ulihusisha vitambulisho vya Uzawa asili na vitambulisho vya wageni waliopo nchini na kukidhi vigezo vya Ukazi.

Amesema katika kufanikisha hilo ni pamoja na Serikali ya Awamu ya Sita ya Dkt.Samia Suluhu Hassan kuweka jitihada katika kuhakikisha wananchi wanapata vitambulisho wakati awali walikuwa wakitumia namba.

Tengeneza amesema katika mipango mikakati ilikuwa ni kuimarisha ofisi katika Wilaya na Mikoa ambapo ndio kumefanya matokeo chanya bila kukutana na changamoto katika mchakato wa vitambulisho.

Hata hivyo katika 60 ya Muungano Mamlaka inaendelea na kusajili kwa mujibu wa sheria na kutambua vitambulisho vinahitajika katika utambuzi mbalimbali kwa wananchi katika upatikanaji wa huduma za kijamii na biashara.

Tengeneza amesema ametoa hofu ya wananchi kuwa kupata kitambulisho cha Taifa ni haki hivyo hakuhitaji kutumia gharama na kinachohitajika ni kukamilisha nyaraka zinazohitaji kutokana na muongozo wa fumu.
 

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA)Godfrey Tengeneza akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani kuhusiana na mafanikio katika miaka 60 ya Muungano kwa Mamlaka hiyo jijini Dar es Salaam.

Na Mwandishi W doetu

Serikali ya Tanzania imesema kuwa inatekeleza uhamaji wa hiari wa wananchi kutoka Ngorongoro ili kulinda haki za binadamu na uhifadhi.

Hayo ameyasema Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya UNESCO Tanzania kuwa
Prof. Hamis Malebo wakati akiwasilisha ujumbe Mkutano wa 23 wa Jukwaa la kudumu la Umoja wa Mataifa la Masuala ya Watu wa Asili (UNPFII) nchini Marekani ulichoanza Aprili 15 Aprili, 2024 na kuhitimishwa Aprili 26

Profesa Malebo, ameueleza mkutano huo kuwa, serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilifanya mapitio shirikishi ya hali ya maisha ya wananchi na uhifadhi katika Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (NCA) na kubaini umuhimu wa kuweka uwiano sawa wa uhifadhi wa maliasili na utamaduni, maendeleo ya jamii na maendeleo ya utalii.

Amesema kwa kutambua haki za binadamu, ambazo zimekuwa sauti ya wanaharakati na wahifadhi mbalimbali na kwa kuzingatia masharti ya Katiba yaTanzania na matakwa ya ulinzi na uhifadhi wa Mkataba wa Urithi wa Dunia wa 1972 na sheria za nchi, ni wazi kwamba, wananchi wanaoishi katika Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro wameathiriwa na migogoro ya binadamu na wanyamapori, magonjwa ya wanyamapori, kukosa haki ya kuwa na makazi ya kudumu, kudorora kwa maendeleo ya kijamii na kiuchumi, kukosa maji safi na salama, na umiliki wa ardhi.

Profesa Malebo amesema kwa mfano kuwa katika kipindi cha 2018 hadi 2023 watu 65 waliuawa na 205 walijeruhiwa na wanyama pori kama vile Simba, Chui, Fisi, Kiboko, Nyati na pamoja na Tembo.

Amesema Wananchi walio katika Hifadhi ya eneo la Ngorongoro wanaachwa nyuma katika Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs).

Prof. Malebo ameeleza kuwa, kwa kufuata misingi ya haki za binadamu, Serikali imefanya mashauriano na jamii ya wakazi wa Ngorongoro katika kipindi cha miaka 32 ili kwa pamoja kupata ufumbuzi wa kudumu wa changamoto za kijamii na kiuchumi zinazowakabili wananchi wake wanaoishi katika ardhi ya hifadhi.

Hata hivyo amesema Mikutano ya uhamasishaji imefanyika kuanzia ngazi ya chini hadi ngazi ya tawala za Wilaya na Mikoa juu Wakazi wanaoishi katika walioko katika Mamlaka ya Ngorongoro mbalo ni eneo lililohifadhiwa walipewa elimu kuhusu sheria zinazosimamia utendakazi wa NCA ambazo haziruhusu wala kutoa kibali chochote cha kisheria kwa ajili ya shughuli za kijamii na kiuchumi wala kutoa haki ya umiliki wa ardhi katika eneo hilo la hifadhi ambalo pia ni eneo la Urithi wa Dunia.

Aidha wakazi hao walifahamishwa kuhusu manufaa yanayohusiana na kuhama kwao kwa hiari Kwenda katika maeneo yaliyo nje ya hifadhi nchini Tanzania.
Akifafanua juu ya mkakati wa kuhama kwa hiari.

Prof. Malebo alibainisha kuwa, kwa kuongozwa na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mikataba ya Umoja wa Mataifa, Tamko la Kimataifa la Haki za Binadamu, Mikataba ya Kimataifa ya Haki za Binadamu, maazimio ya vyombo vingine muhimu vya haki za binadamu na Azimio la Vienna, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaunga mkono uhamaji wa hiari wa wananchi kutoka hifadhi ya eneo la Ngorongoro.

Serikali pia inawezesha zoezi hilo na inabeba gharama za uhamaji, fidia na inatoa mkono wa shukrani kwa wananchi wanaohama kwa hiari Kwenda nje ya eneo la hifadhi.

Profesa Malebo amesema Serikali inahakikisha wanajamii wanaoishi katika ardhi iliyohifadhiwa wanasaidiwa kuhama na kwenda kuishi katika maeneo ambayo wataendelea na kutekeleza tamaduni zao kwa uhuru tofauti na ambako kwa sasa wanaishi kwa kukabiliwa na changamoto zinazotishia maisha, utamaduni na kuchochea umaskini.

Prof. Malebo pia aliueleza mkutano huo kuwa, Serikali ya Tanzania imepanga kwa umakini uhamaji wa hiari wa wananchi kutoka katika Hifadhi ya Ngorongoro ambayo ni hatarishi kutokana na ugumu wa maisha na migogoro na wanyamapori jambo ambalo linatoa fursa kubwa za kupunguza maafa na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi kwa wakazi na eneo hilo la Urithi wa Dunia.

Amesema Serikali iliainisha maeneo nje ya hifadhi ambapo wakazi wa Ngorongoro wataweza kuhamia kwa hiari na kuendelea na shughuli zao za kujitafutia riziki kwa amani kama ilivyoainishwa kwenye Katiba ikiwa ni pamoja na kumiliki ardhi na kufanya shughuli za kijamii na kiuchumi.

Wajumbe wengine wa Tanzania wanaohudhuria mkutano huo ni pamoja na Bi. Zuleikha Tambwe, Afisa Mwandamizi wa Mambo ya Nje katika Ubalozi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Bi. Hindu Zarooq Juma, Afisa Mwandamizi wa Mambo ya Nje katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Pellage Kauzeni, Afisa Mhifadhi Mkuu wa Wanyamapori katika Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Agnes Gidna, Kaimu Meneja wa Urithi wa Dunia katika Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro, Bw. Edward Kutandikila, Mwanasheria wa Serikali na Bw. Erick J. Kajiru, Afisa Mwandamizi Mkuu katika Tume ya Taifa ya UNESCO ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
NA EMMANUEL MBATILO,MICHUZI TV

WADAU mbalimbali wa masuala ya Jinsia na Maendeleo wamekutana katika Semina za Jinsia na Maendeleo (GDSS) na kuichambua bajeti ya Ofisi ya Rais (Mipango na uwekeshaji) na kubaini kuwa haijazingatia masuala ya jinsia.

Akizungumza leo Aprili 24,2024 jijini Dar es salaam, wakati wa semina ambazo hufanyika kila Jumatano katika Ofisi za TGNP Mtandao, Mhadhiri Chuo Kikuu Mzumbe Lihoya Chamwali amesema uwekezaji ambao umekuwa unafanyika kwa wanawake haukuzingatiwa hasa kufufua viwanda ambavyo wanawake wamekuwa wakishiriki.

Aidha ameishauri serikali kutoa elimu kwa wananchi kuhusu maswala ya uwekezaji kwani elimu hiyo imekuwa haijulikani kwa watu wengi hasa wanawake.

"Tunaishauri serikali iweke mifumo rafiki na elimu itolewe ili kila mwanamke ambae anaweza kuwekeza aweze kuingia kwenye mfumo na ndio maana tunasisitiza elimu itolewe kwani mifumo mingi ya uwekezaji inafanyika kielektroniki kitu ambacho wanawake wanawake wamekuwa wanaachwa kwa sababu wengi hawana ujuzi wa elimu hiyo". Amesema Chamwali.

Amesema bajeti ya mwaka huu imekuwa ndogo tofauti ya mwaka jana kwani mwaka 2023 bajeti ilikuwa bilioni30 lakini mwaka huu bilioni 17.

Amesema kufuatia na upungufu huo wa bajeti katika kupitia malengo wameona malengo mengi ya mwaka huu ni muendelezo wa malengo yaliyofanyika mwaka jana ikiwemo kupitia uundaji wa sera ya dira ya maendeleo 2050.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa kituo cha maarifa kata ya Majohe Tabu Ally ametoa rai kwa serikali kuwaangali wanawake waliopembezoni ili waweze kujikwamua kiuchumi kwa kuwapa elimu bora ya uwekezaji.

Amesema changamoto kubwa inayowakabili wanawake waliopembezoni ni miundombinu ya barabara kwani wanazalisha lakini wanashindwa kufika sokoni kutokana na uharibifu mkubwa wa barabara hivyo inawalazimu kutumia ghalama kubwa ili kufika sokoni jambo ambalo linawarudisha nyuma kimaendeleo.

"Kila kitu ili kiende ni lazima barabara zipitike na hiyo ndio changamoto ambayo sisi tunalia nayo lakini hata tukiwezeshwa mitaji bado tutashindwa kutokana na hii moundombinu",Amesema Tabu

Naye,Mdau wa maswala ya jinsia kutoka Kigamboni Ayub Sharif amesema serikali inapaswa kutoa kipaumbele kwenye maeneo ambayo nguvu kazi kubwa inatumika ili kuongeza motisha ya ufanyaji kazi.

"Mimi naishauri serikali kuangali maeneo ambayo nguvukazi kubwa inatumia ndio uwezeshaji uanzie kwani tumeona katika sekta ya madini wanawake ndio wachenjuaji wakubwa lakini madini yakipatikana anaenufaika mwingine hii sio sawa serikali inapaswa kuangali swala hili kabla ya kuwekeza kwenye mitambo waweke mazingira mazuri kwa hizi nguvu kazi". Amesema.










SHINDANO la Mtindo wa Maisha (Life style) Kwa Vijana wenye ushawishi Mitandaoni ( BINGWA ) Msimu wa tatu umezundiliwa rasmi Vijana Mikoani wapewa nafasi .

Akizungumza na Wanahabari Leo Aprili 24,024 Ukumbi wa Serena Hoteli Jijini Dar es Salaam wakati wa kuzindua Shindano hilo kwa Msimu wa tatu Meneja wa Shindano hilo Ombeni Phiri amesema Shindano hilo limewapa fursa Vijana wengi mitandaoni kubadilisha maisha kutokana na fursa mbalimbali ambazo wamekuwa wakizipata na hivyo kulazimika Shindano hilo kuendelea kuwepo ambapo msimu huo wa tatu umekuwa wa kitofauti zaidi.

"Misimu miwili imekuwa yenye Mafanikio makubwa zaidi na Vijana wengi wa mitandao kuonesha Maisha yao halisi wanapokuwa kwenye mjengo huo hivyo kwa Msimu huu watatu Umepewa nguvu na Kampuni ya Kubashiri ya Parimatch ili kumsukuma Mshindi huyo kufanya vitu vikubwa zaidi Pape Shindano linapomalizika

Msimu Mpya wa tatu wa show ya Bingwa itatembelea Mikoa mitano kwa ajili ya kutafuta Vijana wengine ambapo maoni mengi yamekuwa yakiwafikia Vijana wakihitaji kushiriki Shindano hilo.

"Msimu wa tatu umefanya Maboresho mbalimbali ikiwemo ongezeko la Mikoa mitano ya washiriki ikiwemo Arusha, Dodoma,Mwanza, Mbeya pamoja na kitovu chenyewe Dar es Salaam.

Pia ameeleza kuwa usahili kila Mkoa utachukua washiriki 10 kila Mkoa na kufatia mchujo katika App ya Startimes (Startimes On) ambapo washiriki 08 watatoka Dar hivyo kukamilisha Jumla ya watakaoingia ndani ya nyumba washiriki 24 huku zawadi ya Mshindi kugharimu zaidi ya Milioni 35 za Kitanzania.

Kwa Upande wake Meneja Masoko wa Kampuni ya Startimes David Malisa amesema Msimu wa tatu utaendelea kuwapa fursa vijana zaidi na Atakaeibuka Mshindi Kampuni ya Startimes itaweza kumpa Ubalozi.

Aidha amewapongeza Kampuni ya Parimatch kuona haja ya kuwapa Moyo Vijana hao wenye ushawishi Mitandaoni kukuza vipaji vyao.

Pia amewataka wateja kulipia vifurushi cha Uhuru elfu 23000 ili kuweza kuona shindano hilo kupitia Tv3 ndani ya King'amuzi cha Startimes.

Nae Meneja Masoko wa Parimatch Levis Paul ameeleza sababu ya Kampuni hiyo kuishika mkono Shindano hilo la " Bingwa".

"Sababu ya Parimatch kuungana na Msimu wa tatu wa Shindano la bingwa ni kutokana na shindano hilo Kuhusisha Vijana na Kauli mbiu ikibeba Jumba la Washindi ambapo Kampuni yetu inalenga zaidi kutafuta Washindi walipo kwa kupitia ubashiri."

Paul ameeleza wao kama Parimatch wanatambua kuwa Washiriki wanahitaji kukaa siku 70 ambapo kila kitu kinahitaji uwezeshwaji kuanzia Malazi na vitu mbalimbali hivyo Tv3 na Startimes peke wanahitaji nguvu ya ziada ya kuendesha Shindano hilo hivyo sisi tumeona tuongeze nguvu hiyo kwa msimu huu wa tatu."

Pia amefafanua zaidi kuwa Wana amini kuwa chapa ya Kampuni hiyo ipo sehemu na sahihi hivyo kudhamini shindano hilo itaongeza na kujiweka kwenye nafasi nyingine nzuri zaidi ya kujitangaza kama Kampuni.
Meneja programu wa shindano la Bingwa Ombeni Phiri akieleza namna Shindano hilo litakavyoshirikisha Mikoa mitano ambayo ni Arusha,Mbeya,Mwanza,Dodoma pamoja na Dar es Salaam
 

Meneja Masoko wa Kampuni ya Startimes David Malisa akizungumza na Wanahabari Leo Aprili 24,2024  Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam  wakati wa Uzinduzi wa Msimu wa tatu wa Shindano la Bingwa ambapo amewataka wateja wa Kisimbuzi cha Startimes kulipia kifurushi ili kuendelea kuona shindano hilo kupitia Tv3
 

Meneja Masoko wa Kampuni ya Parimatch  Levis Paul akizungumza machache mara baada ya Kuzinduliwa kwa Msimu wa tatu wa Shindano la Bingwa ambapo msimu huo Kampuni hiyo ikiwa wadhamini wakuu wa shindano

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda leo amekutana na kufanya mazungumzo na Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa anayeshughulikia Operesheni za Ulinzi wa Amani ( UN Under Secretary General for Peace Operations) Bw. Jean Pierre Lacroix ofisini kwa Mkuu wa Majeshi, Upanga, Jijini Dar es salaam.

Katika mazungumzo yao, Bw. Jean Pierre Lacroix amelipongeza JWTZ na kusema Umoja wa Mataifa unaridhishwa na weledi na utendaji kazi wa JWTZ katika operesheni za ulinzi wa amani sehemu mbalimbali duniani na ameahidi Umoja wa Mataifa kushirikiana na Tanzania ili kuhakikisha amani inadumishwa duniani.

Naye Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Jacob John Mkunda ameushukuru Umoja wa Mataifa kwa kuendelea kuliamini JWTZ na kuwahakikishia kuwa JWTZ liko imara na litaendelea kutekeleza majukumu ya ulinzi wa amani duniani wakati wowote litakapohitajika


Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amewatembelea Mabalozi wa Tanzania wanaoshiriki warsha ya siku 4 ambayo imekamilika mjini Kibaha leo Aprili 24, 2024 kwa kufikia makubaliano mbalimbali ambayo yanalenga kuipaisha diplomasia ya Tanzania duniani.

Dkt. Nchimbi aliwapongeza Mabalozi hao kwa kazi nzuri wanayoifanya ya kuitangaza nchi na kuchangia kwa kiasi kikubwa ongezeko la biashara, uwekezaji na utalii nchini.

Warsha hiyo ambayo ililazimika kumalizika usiku kila siku ilifanyika chini ya uenyekiti wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe January Makamba (Mb) ilijadili mikakati ya kuboresha utekelezaji wa Sera ya Mambo ya Nje na namna ya kutafuta ufumbuzi wa kudumu wa changamoto ambazo zimekuwa kikwazo kufikia ufanisi wa shughuli za Wizara hiyo.

Katika siku zao 4, Mabalozi pamoja na mambo mengine, walipitia mikakati ya Utekelezaji wa Diplomasia ya Uchumi, uendelezaji wa majengo ya ofisi na makazi ya Balozi, Diplomasia ya Umma na Diplomasia ya kidigitali na viashiria vya kupima utendaji (Key Performance Indicators- KPIs).

Mabalozi walieleza kuwa kukamilika kwa nyaraka hizo ambazo hazikuwahi kuwepo Wizarani kabla ni chachu katika mwelekeo mpya wa Utekelezaji wa Diplomasia ya Uchumi.

Mabalozi walisisitiza umuhimu wa kumaliza changamoto za kimawasiliano baina yao na wadau ambazo zimekuwa kikwazo za kukamilika kwa wakati kwa fursa na miradi ambayo imekuwa ikiletwa nchini. Changamoto nyingine kubwa ambayo Mabalozi wamesisitiza itafutiwe ufumbuzi ni uwezo mdogo wa nchi yetu wa kuzalisha bidhaa za kukidhi soko katika maeneo yao ya uwakilishi.

Waheshimiwa Mabalozi walisema kuna soko kubwa la nyama, maparachichi, korosho, mchele na bidhaa nyingine lakini hakuna bidhaa za kutosha nchini za kulisha soko hilo.

Mabalozi katika warsha hiyo walipata fursa ya kusikiliza nasaha za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa njia ya mtandao ambaye aliwataka kuwa jicho la Tanzania katika maeneo yao ya uwakilishi ili nchi isipitwe na mabadiliko yanayotokea duniani.

Aidha, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses Kusiluka alifika katika warsha hiyo na kuwambia Mabalozi kuwa wapo katika Wizara iliyokusanya watu wenye taaluma, ujuzi, uzoefu na historia ya kutoka sekta tofauti mchini. Aliwasihi washirikiane kutumia fursa hiyo kuharakisha mabadiliko ndani ya Wizara ya Mambo ya Nje na kutatua changamoto zinazowakabili.

Taasisi kadhaa pia zilialikwa na kuwasilisha mada kuhusu shughuli za ofisi zao ambazo ni Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) na Benki ya Azania.

Warsha hiyo pia wakati wa ufunguzi, walikaribishwa Mabalozi wastaafu ambao walipata fursa ya kubadilishana uzoefu na Mabalozi wa sasa kwa lengo moja tu la kujengeana uwezo wa kukuza na kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia baina ya Tanzania na mataifa mengine, mashirika ya Kikanda na Kimataifa.

Waziri Makamba ambaye ana muda wa takribani miezi 7 tokea ahamishiwe Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki amesema Wizara inaweza kufanya zaidi kuliko inavyofanya hivi sasa. Hivyo, warsha hiyo iliandaliwa ili kupigana msasa wa kufikia nchi ya ahadi.






Top News