Na MWANDISHI WETU


WAWEKEZAJI kutoka China wamekutana na Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) na kujadiliana kuhusu uwekezaji hususan katika uzalishaji wa Nishati safi ya kupikia kwa lengo la kumuunga mkono Rais Samia Suluhu Hassan kuhamasisha matumizi ya nishati ya kupikia.

Wawekezaji hao waliongozwa na Shen Don kutoka Jimbo la Shangzhou ambapo wakiwa nchini wlikutana na wadau mbalimbali kutazama fursa za uwekezaji.

Kundi hilo la wawekezaji wameridhia kufanya uwekezaji wa zaidi ya dola za Marekani milioni 312 (zaidi ya sh. bilioni 800) katika maeneo ya nishati, afya, ujenzi, kilimo na vifaa vya uchakataji viwandani

Kutokana na hatua hiyo, UWT inaamini hiyo itakuwa fursa nzuri kwao kuwafikia na kuwawezesha wanawake kiuchumi.

Akizungumza na waandishi wa habari katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Lumumba jijini Das res Salaam, jana, Katibu Mkuu wa UWT, Jokate Mwegelo alisema wawekezaji hao ambao ujio wao umeratibiwa na Kampuni Canopus Energy Solution, wameonyesha utayari wa kushirikiana katika eneo la uzalishaji wa Nishati mbadala na maeneo mengine ya kimkakati.

“Chama Cha Mapinduzi kinachoongozwa na Mwenyekiti wetu Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kilizielekeza jumuiya zote Chama kutazama na kujiendeleza kupitia fursa mbalimbali, hii kwetu ni fursa tumejipanga kuzalisha nishati mbadala kupitia makaa yam awe.

“Wenzetu hawa wameonyesha utayari, tumefanya mazungumzo ya awali na wametualika kwenda China katika maeneo yao ya uzalishaji wa huduma na bidhaa mbalimbali kujionea namna walivyo tayari kutokana na maendeleo ya teknolojia,” alisema.

Alieleza kuwa UWT ina dhamana kubwa ya kuwaendeleza wanawake wa Tanzania kupitia fursa mbalimbali, hivyo imejipanga kuunga mkono juhudi za kumtua mama kuni kichwani kwa kutengeneza mkaa mbadala ambao ni salama kwa afya za binadamu.Kwa mujibu wa Jokate mbali na nishati mbadala, pia wanatazama uwezekano wa wa kushirikiana na wadau hao katika sekta ya madini lakini hilo litafanyika baada ya hatua mbalimbali kutekelezwa ili kuwa na ushirikiano wenye tija.

Jokate alisisitiza kwamba UWT imejipanga kutengeneza fursa ambazo zitawanufaisha wanawake katika sekta mbalimbali hususan uchumi ambao utawainua na kimaisha.

"Fursa yoyote tunayoitengeneza lengo letu ni kuona wanufaika wa kwanza wanakuwa wanawake wa Tanzania,” alisema.

Kwa upande wake Mhandisi Anna Nyangasi kutoka Kampuni ya Canopus Energy Solution, alisema ujio wa ujumbe huo ni fursa kwa uwekezaji katika sekta mbalimbali.

Anna alieleza kuwa wawekezaji hao waliongozwa na Shen Don kutoka Jimbo la Shangzhou ambapo ukiwa nchini ulikutana na wadau mbalimbali kabla ya jana kukamilisha ziara yao kwa kukutana na UWT ambapo wanaamini kuna kundi kubwa la wanawake ambalo linahitaji kuwa sehemu ya mabadiliko kutokana na uwekezaji unaoweza kufanywa na wawekezaji hao.

Kwa mujibu wa Anna, wawekezaji hao wameridhia kufanya uwekezaji wa zaidi ya dola za Marekani milioni 312 (zaidi ya sh. bilioni 800) katika maeneo ya nishati, afya, ujenzi, kilimo na vifaa vya uchakataji.

Pia, alisema ujumbe huo umeonesha nia kushirikiana na kutafuta wawekezaji katika maeneo takribani manane ambayo ni viwanda vya kuunganisha zana za kilimo (pawatila), kuzalisha vifaa vya trekta, majenereta, pampu za maji, vifaa tiba, viwanda vya bidhaa za umeme na ‘paneli’ za kuhifadhi baridi.

Mhandisi Anna alisema ujumbe huo wa watu 11 unahusisha wafanyabiashara, wawakilishi kutoka serikalini pamoja na ujumbe wa CCP, uliwasili nchini kwa mwaliko wa Canopus Energy Solution kwa kushirikiana na Kampuni ya Amec Group.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Jokate Mwegelo (kushoto) akisalimiana na ujumbe wa wafanyabiashara  kutoka China waliongozwa na Shen Don kutoka Jimbo la Shangzhou (wa pili kulia) baada ya kufika katika ofisi za Chama Cha Mapinduzi(CCM) zilizopo Lumumba jijini Dar es Salaam








Na. Vero Ignatus, Arusha

Katibu Mkuu mtendaji wa Smaujata amewataka Viongozi kusimamia vyema nafasi walizonazo sambamba na kuwa barua njema kwa kila anayewasoma

Ameyasema hayo katika kikao cha Viongozi wa Smaujata mkoa kilichofanyika Jijini Arusha, ambapo aliwataka kutambua kuwa Uongozi ni majukumu poa ni mgumu,kwani hawawezi kupendwa na kila mtu badala yake kila mmoja wao atambue nafasi yake, waitumikie jamii kwa moyo wa huruma,kwa kusimamia haki, pamoja na kuwa na kifua cha kubeba mambo.

Aidha aliwataka Viongozi hao wajitahidi kuwa waadilifu kwenye nafasi zao, watafute namna wanaweza kutengeneza utaratibu wa kufuatilia mambo pamoja na kutoa nafasi kwa wengine, zaidi kufahamu mipaka yao ya kiutendaji.

"Ninyi kama Mashujaa na Viongozi ni vyema kutambua kwa kupitia uzoefu wa namna moja ama nyingine mnaweza kuangalia namna gani njema ya kutatua changamoto"alisema Injinia Juliana

Akisoma ripoti ya utendaji wa kazi katika mkoa Kaimu Katibu wa Smaijata
Lussa Melembuki alisema kuwa hadi sasa wameweza kufikia jumla ya shule za msingi zaidi ya 246,shule za sekondari zaidi ya 118,Makanisa 42, wamefanya semina 12 pamoja na kushiriki zaidi ya matamasha 18 vyote hivyo ni kwaajili ya outta elimu kwa jamii dhidi ya Ukatili

Vile vile ameweza kuushukuru Uongozi wa seriali ngazi ya mkoa kwa kuwapatia ushirikiano mkubwa kwani wamekuwa sababu ya wao kufanikisha kutoa elimu katika jamii, ikiwemo kuwajuza madhara yatokanayo na Ukatili, na mahali sahihi pa Kutoa taarifa endapo wataona dalili ama jambo lolote lenye viashiria vya ukatili.

Aidha ifahamike kuwa Shujaa wa Maendeleo na Ustawi wa Jamii Tanzania ni kampeni mahususi ya Kitaifa kwaajili ya kupinga, kuibua na kutokomeza vitendo vyote vya ukatili katika Jamii zote nchini, kuelimisha Jamii kuondokana na fikra, Imani, Mila na desturi na tamaduni zinazokinzana na Maendeleo.

Baadhi ya malengo ya kampeni hiyo ni kutambua kutengeneza mtandao Jamii, sense uwezo wa kupaza Sauti kupinga nakupambanaa na kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na Watoto, kuelimisha na kurahisisha utambuzi na ufanyiaji kazi viashiria vyote vya ukatili kuanzia ngazi ya Familia.






Katibu Mkuu wa Shujaa wa Maendeleo na Ustawi wa Jamii (Smaujata)nchini Mhandisi Juliana Marko akizungumza na Viongozi wa Wilaya pamoja na wale wa mkoa alipotembelea Jijini hapo kwaajili ya shughuli za kikazi kushoto kwake ni Mwenyekiti wa mkoa wa Arusha Godfrey Zablon.


Katibu Mkuu Smaujata Taifa wa pili kutoka kushoto Juliana Marko akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Mkoa wa Arusha mapema Marchi 27,2024

Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTARADE) kwa kushirikiana na Wizara ya Mambo ya Nje na Wizara ya Viwanda na Biashara Imeratibu Semina ya Wafanyabiashara kuhusu fursa ya kuuza bidhaa katika soko la Uingereza kupitia Mpango wa Biashara wa Uingereza na Nchi zinazoendelea (UK-DCTS)

Semina hii ya inayofanyika katika ukumbi wa JNICC ulipo Jijin Dar es salaam. Inalenga kuwakutanisha wafanyabiashara wa Tanzania na nchini Uingereza ili kujenga uwezo wa taratibu na vigezo na hivyo kuwafungulia fursa za Masoko zinazopatikana nchini Uingereza.

Wakimwakilisha Mkurugenzi Mkuu TANTRADE Bi. Latifa M. Khamis, Meneja Uhusiano kwa Umma na Masoko Lucy Mbogoro pamoja na Afisa Biashara (Masoko ya Ndani na Nje ya Nchi) Bw. Deo Shayo wameshiriki Semina hii ambayo imefunguliwa rasmi na Mhe. Waziri wa Viwanda na Biashara Dr. Ashatu Kijaji.
 

Bi. Petronela Mlowe afisa ukaguzi na Mazingira anayefanya kazi uingereza na pia mtaalam elekezi wa Ukaguzi bidhaa
akitoa mada kuhusu namna bidhaa za vyakula vinavyoingizwa Uingereza vinakaguliwa.
Aidha, Bi. Mlowe ametoa hamasa kwa wafanyabiashara wa Tanzania kuuza uingereza na kukuza uchumi
6h





Tanzania imesainia Mkataba wa Ushirikiano na Nchi ya Hungary katika sekta ya maji ili kubadilishana uzoefu wa teknolojia katika sekta hiyo.

Akizungumza leo Machi 28,2024 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe Janury Makamba amesema kwa miaka mingi nchi hiyo inaongoza kwa teknolojia ya juu Duniani katika udhibiti wa maji ikiwemo maji taka,mafuriko na ya kunywa hivyo ushirikiano huo wa karibu utaleta tija kubwa kwa Taifa .

Sambamba na hayo amesema nchi hizi mbili zimekuwa zikifanya biashara hivyo kutafanyika makongamano ya kibiashara, ziara ili fursa zilizopo zifahamike na ushirikiano huo uendelee kudumu siku hadi siku.

"Tanzania ina vivutio vingi vya utalii na Hungary ni chanzo cha watalii kwani tumeshuhudia watalii wengi kutoka nchi hiyo wakija kutalii na miaka iliyopita walikuwa 5000 mwaka jana wakifikia 11000 hivyo kuna ongezeko kubwa kutoka nchi hiyo na kwa kuona hilo tumezungumza kwa kina na kujubaliana kuwa tutasaini usafiri wa anga watalii na wafanyabiashara watatoka moja kwa moja kutoka Hungary kuja Tanzani kwa ndege"Amesema Makamba

Sanjari na hayo amebainisha kuwa Vijana wa kitanzania wamekuwa wakinufaika kwa kupata ufadhili wa kwenda kusoma Hungari pia wamekubalina kunzisha mahusiano ya kituo cha Diplomasi cha kimataifa cha Dkt Salim Ahmed Salimna na chuo cha Diplomasia ambapo itasaidia wanadiplomasia kupata fursa ya kwenda Hungari kuongeza ujuzi.

Waziri Makamba amesema nchi ya Hungary wamedhamiria kuwekeza kwenye kiwanda cha kuwekeza ndege ndogo pale Morogoro na

Aidha nchi ya Hungary imekubali kujenga Ubalozi wao nchi Tanzania uliofungwa miaka ya 1990" hiyo ni moja ya kusaidia kuongeza mashirikiano makubwa baina ya nchi hizo mbili.

Naye Waziri wa Mambo ya nje na Biashara wa Hungary Mhe Peter Szijj'art'o amesema licha ya kufungwa kwa ubalozi lakini bado ushirikiano ikuwa unaendelea hivyo habari njema ni kuwa nchi yao mwaka huu Julay inatarajiwa kuchukua Urais wa Umoja wa Ulaya.




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokea Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka 2022/23 kutoka kwa Bw. Charles Kichere Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma leo tarehe 28 Machi, 2024.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokea Taarifa ya Utendaji Kazi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kwa mwaka 2022/2023 kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi hiyo Kamishna wa Polisi Salum Hamduni Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma leo tarehe 28 Machi, 2024. 


Dar es Salaam - Machi 27, 2024. Katika jitihada za kuongeza upatikanaji na matumizi ya simu janja ili kuziba pengo la kidijitali nchini, makampuni ya Vodacom Tanzania PLC na Benki ya CRDB wamezindua mpango wa kuwezesha Wateja wao kumiliki simujanja zenye ubora kwa gharama nafuu.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mpango huo wa kukopesha simu jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Philip Besiimire, alieleza kuwa kampuni hiyo ya simu inatekeleza mipango mbalimbali ya kupunguza gharama za vifaa vya mawasiliano ili kuwawezesha wateja wake kuhama kutoka kwenye matumizi ya mtandao wa 2G na kumiliki simu zenye uwezo wa 4G na kutumia fursa hiyo ili kunufaika na faida kemkem zinazopatikana kupitia mtandao huo.
"Tukiwa ni mdau na mshirika mkubwa wa sekta ya mawasiliano na teknolojia, Vodacom tunajivunia kuzindua mpango huu na Benki ya CRDB ambayo ni taasisi kubwa ya fedha nchini. Ushirikiano wetu unalenga kuwawezesha wateja kutoka pande zote mbili kupata aina mbalimbali za simujanja kwa bei nafuu na mpango wa malipo kwa awamu kwa kipindi fulani. Ili kujua kama amekidhi vigezo, mteja atatakiwa kupiga *150*00*44# nbaada ya hapo atafanya malipo ya awali na kupewa simujanja. Mkopo huu unaweza kulipwa kwa siku, kwa wiki au kwa mwezi kwa kipindi cha hadi miezi 12 kupitia M-Pesa," alifafanua bwana Besiimire.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela, alisema, “ushirikiano huu baina yetu na Vodacom ni fursa nzuri kwa Watanzania kupata huduma za kifedha na mawasiliano kwa gharama nafuu. Kwa hiyo kama wadau muhimu tunapaswa kuunga mkono juhudi za Serikali ili kuhakikisha wananchi wake wanafaidika na ukuaji na maendeleo katika sekta hizi.” 
Bwana Nsekela aliongeza kuwa, “Kwa mtandao wetu ulioenea nchi nzima, CRDB tumekuwa na mchango muhimu katika maendeleo ya Watanzania kwa kuwezesha upatikanaji wa huduma za kifedha. Hivyo basi, kwa kushirikiana na Vodacom, tutaweza kutoa mchango wetu ili kuongeza matumizi ya simujanja nchini.”


Licha ya juhudi za mamlaka nchini kusogeza huduma za mawasiliano, wananchi wengi bado wanatumia huduma za mtandao wa 2G. Hii inapunguza upatikanaji wa fursa zilizopo mtandaoni pamoja na kufurahia na kunufaika na intaneti yenye kasi zaidi kutoka Vodacom pamoja na bidhaa nyingine za kidijitali.

Matumizi ya simujanja na intaneti yana faida kwa jamii kama vile kukuza ukuaji wa kiuchumi kwa kuwezesha ujasiriamali wa kidijitali na kuchochea uvumbuzi, utafutaji masoko mitandaoni pamoja na kuongeza kipato kwa wananchi wanaoamua kujiajili kupitia dijitali.
Vodacom Tanzania imekuwa ikishirikiana na watengenezaji mbalimbali wa simu za mkononi na taasisi za kifedha ili kuwezesha Watanzania kumiliki simu kupitia mikopo nafuu na mipango rafiki ya malipo kwa mteja. 

Mwezi August 2020, Vodacom ilizindua programu ambayo inawaruhusu wateja wake kumiliki simujanja kupitia mkopo unaolipwa kwa awamu, huku kianzio kikiwa ni Shilingi 20,000 za Kitanzania kwa muda wa miezi 12. 

Bwana Nsekela alimalizia kwamba anaamini kuwa taasisi hizo mbili zina huduma mbalimbali za kibunifu ambazo zitawanufaisha na kuboresha maisha ya wateja wao. Pia alitoa wito kwa Watanzania wanaotumia simu za kawaida na wanataka zenye ubora zaidi kufika katika maduka ya Vodacom na kupata simujanja kwa bei nafuu ili kuendana na kasi ya ukuaji wa uchumi wa kidijitali duniani.
Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), akiongoza mkutano wa Benki ya Dunia wa Jukwaa la Tatu la Kanda ya Afrika Kundi la Kwanza kwa nchi za Kipato cha Kati lililolenga kujadili namna mashirika ya fedha ya kimataifa yanavyoweza kuongeza fedha kuzisaidia nchi za kipato cha kati kufikia maendeleo endelevu ya kiuchumi na kijamii. Mkutao huo umefanyika kwa njia ya Mtandao, kutokea Jengo la Hazina (Treasury Square), jijini Dodoma.
Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), akitoa wito kwa taasisi za fedha za kimataifa kuongeza fedha kwaajili ya kuzisaidia nchi za kipato cha kati wakati akifungua mkutano wa Benki ya Dunia wa Jukwaa la Tatu la Kanda ya Afrika Kundi la Kwanza kwa nchi za Kipato cha Kati lililolenga kujadili namna mashirika hayo ya fedha yanavyoweza kuongeza fedha kwa nchi hizo. Mkutano huo umefanyika kwa njia ya Mtandao kutokea Jengo la Hazina (Treasury Square), jijini Dodoma.
Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia Kanda ya Mashariki na Kusini mwa Afrika, Bi. Victoria Kwaka, akitoa mada wakati wa mkutano wa Benki ya Dunia wa Jukwaa la Tatu la Kanda ya Afrika Kundi la Kwanza kwa nchi za Kipato cha Kati, ambapo Waziri wa Fedha Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) aliongoza mkutano huo uliofanyika kwa njia ya mtandao, kutokea Jengo la Hazina (Treasury Square), jijini Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizaraya Fedha, Bi Amina Khamis Shaaban na Afisa Mwandamizi wa Idara ya Fedha za Nje wa Wizara hiyo, Bw. John Kuchaka, wakifuatilia uwasilishwaji wa taarifa wakati wa mkutano wa Benki ya Dunia wa Jukwaa la Tatu la Kanda ya Afrika Kundi la Kwanza kwa nchi za Kipato cha Kati, ambapo Waziri wa Fedha Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) alikuwa Mwenyekiti wa mkutano huo uliofanyika kwa njia ya mtandao, kutokea Jengo la Hazina (Treasury Square), jijini Dodoma.
(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Fedha)


Na. Peter Haule, WF, Dodoma
WAZIRI wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), ameongoza mkutano wa Benki ya Dunia wa Jukwaa la Tatu la Kanda ya Afrika Kundi la Kwanza kwa nchi za Kipato cha Kati uliolenga kujadili namna mashirika ya fedha ya kimataifa yanavyoweza kuongeza fedha kwa ajili ya kuzisaidia nchi za kipato cha kati ili ziweze kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo katika nchi zao itakayochochea ukuaji wa uchumi na maendeleo ya jamii.

Akifungua mkutano huo uliofanyika kwa njia ya mtandao jijini Dodoma, Mwenyekiti wa Mkutano huo, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba alisema kuwa Dunia inakabiliwa na migogoro mingi na changamoto za maendeleo ya kiuchumi ambazo zinasababisha kutofikiwa kikamilifu kwa malengo ya maendeleo endelevu (SDGs).

Alisema kuwa kupungua kwa nafasi ya kifedha katika kushughulikia migogoro hiyo kunadhoofisha uwezo wa Serikali za nchi hizo kufadhili programu za kijamii, kuharakisha ufufuaji wa Uchumi na pia kuongeza madeni katika nchi hizo.

“Mizozo inayoendelea nchini Urusi na Ukraine, Mashariki ya Kati na baadhi ya nchi nyingine za Afrika imechochea kupanda kwa bei ya vyakula na kuwasukuma mamilioni ya watu kwenye uhaba wa chakula”, alisema Dkt. Nchemba.

Aidha Dkt. Nchemba aliishukuru Benki ya Dunia kwa mchango wake wa kuzijengea uwezo taasisi katika kuyafikia maendeleo endelevu lakini pia kufufua uchumi kutokana na changamoto mbalimbali zinazotokea Duniani.

Vilevile alisema kuwa kukabiliana na changamoto zinazoikumba dunia sio kazi rahisi kwa nchi moja, hivyo ameomba kuwa na nguvu ya pamoja katika Kanda na Bara la Afrika katika kutafuta utatuzi wa changamoto hizo.

Dkt. Nchemba ameishukuru Benki ya Dunia kwa kummwamini kuongoza kikao hicho kikubwa lakini pia amewashukuru viongozi mbalimbali waliotoa mada ambazo zimewafunbua macho kwa kuona fursa zilizopo katika kukuza una kuwezesha biashara na pia kuwa na majadiliano mazuri wakati wa mikutano ijayo ya majira ya kipupwe ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) itakayofanyika mwezi Aprili, 2024 jijini Washington D.C nchini Marekani.

Kwa upande wake Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia anayesimamia Kanda ya Mashariki na Kusini mwa Afrika, Bi. Victoria Kwaka, alisema kuwa katika kipindi cha miaka mitano ilitoa misaada na mikopo nafuu yenye thamani ya zaidi ya dola bilioni tatu kwa nchi za Kanda ya Mashariki na Kusini mwa Afrika.

Alisema kuwa mwaka wa fedha uliopita Benki ya Dunia kupitia Mfuko wa IDA ilitoa dola bilioni 2.4 na kwamba kiwango cha misaada na mikopo hiyo imeendelea kuongezeka na miongoni mwa nchi zilizonufaika na mpango huo ni Tanzania, Kenya na Eswatini.

Aidha, Bi. Kwakwa amevitaja vipaumbele vya Benki hiyo kuwa ni pamoja na kuhakikisha nchi zitapata umeme wa uhakika, kuwa na maendeleo ya kidigitali, upatikanaji wa ajira, mapinduzi ya kiuchumi, kujenga uwezo kwa rasilimali watu na masuala ya elimu.

Baadhi ya Viongozi walioshiriki mkutano huo ni pamoja na Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia anayesimamia Kanda ya Mashariki na Kusini mwa Afrika, Bi. Victoria Kwakwa, Makamu wa Rais wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IFC) Kanda ya Afrika, Bw. Sergio Pimenta, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Dunia, Bi. Anshula Kant, Mawaziri wa fedha na Mipango (Magavana) na wajumbe wengine.
Katika kuhadhimisha mwezi wa kumsheherekea Mwanamke na kukaribisha sikuukuu za Pasaka, Halotel Tanzania yatoa msaada kwa wanawake chini ya Taasisi ya ‘Jukwaa la wanawake na wasichana wenye ulemavu Mtwara’ kusaidia changamoto mbalimbali wanazozipata wanawkae hao.

Halotel ikiwa ni kampuni ya mawasiliano Tanzania, ikitoa huduma mbalimbali za mawasiliano na ikiendelea kukidhi mahitaji ya wateja wao. Kwa kuzingatia usalama na uaminifu Halotel inaendelea kutoa huduma bora na kuleta mabadiliko chanya katika sekta ya mawasiliano na jamii kiujumla.

Akiongea katika tukio hilo Mkurugenzi wa Halotel tawi la Mtwara Bwana Emmanuel Monyo “Halotel inaendelea kusimama imara katika kufanikisha malengo yake ya kukuza usawa na ujumuishaji katika pande zote za jamii.

 Lakini kwa kuwasaidia wanawake hawa Mtwara Halotel inaonyesha dhamira yake ya kuleta mabadiliko katika jamii na kuunda ulimwengu weye uwezekano na fursa kwa wote”.

Afisa uhusiano na mawasiliano wa Halotel, Roxana Kadio ambae aliwasilisha msaada huo alisema Halotel inaedelea kujenga ujumuishaji ambao kila mtu bila kujali uwezo wao anaweza kushiriki kikamilifu katika jamii, aliendelea kusema kuwa Halotel iliamua kuwaunga mkono wanawake wa Mtwara baada ya kujifunza kuwa wanapitia changamoto za chakula na vifaa vya nyumbani na kama kampuni inayokua nia yetu kutoa mkono wa msaada kwa jamii ya kitanzania.

“Mahitaji yaliyotolewa na Halotel ni pamoja na Chakula kama Mchele, Sukari na Mafuta ya kupikia lakini pia kutoa msaada wa magodoro na vifaa vingine vya nyumbani. Vyote hivi ni katika kuwahudumia wanawake hawa na kuwaonesha kuwa hawako peke yao katika changamoto wanazozipita” Roxana alisema.

 Aliendelea kusema kuwa msaada huu pia unalenga katika kuwatoa upweke wanawake hawa katika mahitaji yao. Na kwamba Halotel haitoishia kusaidia tu wanawake na wako kwenye mpango wa kukuza uhitaji wa jamii kiujumla.

Halotel itaendelea kutoa ushirikiano kwa majukwaa ambayo yanajikita katika kuwainua wanawake. Lakini pia Halotel itaendelea kutia chachu ya maendeleo kwa wateja wake na jamii kiujumla.



Halotel wakikabidhi msaada wa Vifaa vya nyumbani na Chakula katika taasisi ya Jukwaa la Wanawake walemavu Mtwara. Kushoto akiwa Mkurugenzi wa Tawi la Halotel Mtwara Bw. Emmanuel Monyo, Kati ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Jukwaa la Wanawake walemavu Mtwara Bi. Fatuma Mohamed Mkondomoka, Kulia Afisa uhusiano na Mawasiliano makao makuu Halotel Bi. Roxana Kadio.






Upande wa Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Kijinsia Tanzania (TGNP),Lilian Liundi akizungumza wakati wa kufungua Kilinge salama kwa Wanawake, Wasichana na Viongozi kilichofanyika leo Machi 28, 2024 katika Ukumbi wa Mtandao huo Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Kijinsia Tanzania (TGNP),Lilian Liundi akizungumza wakati wa kufungua Kilinge salama kwa Wanawake, Wasichana na Viongozi kilichofanyika leo Machi 28, 2024 katika Ukumbi wa Mtandao huo Jijini Dar es Salaam.
Diwani wa wilaya ya Mtwara, Farida Abdallah akizungumza wakati akitoa Kestoria yake ya kuwania nafasi ya uongozi katika Kilinge salama kwa Wanawake, Wasichana na Viongozi kilichofanyika leo Machi 28, 2024 katika Ukumbi wa Mtandao huo Jijini Dar es Salaam.
Diwani wa wilaya ya Mtwara, Farida Abdallah akizungumza wakati akitoa Kestoria yake ya kuwania nafasi ya uongozi katika Kilinge salama kwa Wanawake, Wasichana na Viongozi kilichofanyika leo Machi 28, 2024 katika Ukumbi wa Mtandao huo Jijini Dar es Salaam.

Diwani wa wilaya ya Mtwara, Farida Abdallah akizungumza wakati akitoa Kestoria yake ya kuwania nafasi ya uongozi katika Kilinge salama kwa Wanawake, Wasichana na Viongozi kilichofanyika leo Machi 28, 2024 katika Ukumbi wa Mtandao huo Jijini Dar es Salaam.
Diwani wa wilaya ya Mtwara, Farida Abdallah akizungumza wakati akitoa Kestoria yake ya kuwania nafasi ya uongozi katika Kilinge salama kwa Wanawake, Wasichana na Viongozi kilichofanyika leo Machi 28, 2024 katika Ukumbi wa Mtandao huo Jijini Dar es Salaam.
Wanawake na Wasichana ambao ni washiriki kutoka Dar es Salaam, Pwani na Mtwara wakimsikiliza Diwani wa wilaya ya Mtwara, Farida Abdallah wakati akitoa Kestoria yake ya kuwania nafasi ya uongozi katika Kilinge salama kwa Wanawake, Wasichana na Viongozi kilichofanyika leo Machi 28, 2024 katika Ukumbi wa Mtandao huo Jijini Dar es Salaam.

KILINGE Salama (Safe Space) kilichoandaliwa na Mtandao wa Kijinsia Tanzania (TGNP) Chamwibua Diwani, Farida Abdallah ambaye ni Diwani wa wilaya ya Mtwara ambapo ameeleza changamoto mbalimbali wanazokumbana nazo wanawake viongozi ikiwemwo kukatishwa tamaa ili wasiweze kugombea nafasi mbalimbali za uongozi.

Akizungumza leo Machi 28, 2024 wakati wa kilinge salama kilichofanyika katika ukumbi wa TGNP jijini Dar es Salaam, Diwani huyo ambaye aliishia kidato cha pili na kupata ujauzito huku akimpote Mama yake mzazi amewaasa wanawake kutokukata tamaa pale yanapojitokeza maneno ya kukatisha tamaa pale yanapojitokeza wakati wa harakati za kutafuta nafasi za uongozi.

“Wakati nawania nafasi ya uongozi watu walikuja kunikatisha tamaa ili ni sigombee….. hata kwenda kumshawishi Mme wangu ili anikatishe tamaa lakini hawakufanikiwa….” Amesema Farida.

Kwa Upande wa Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP Lilian Liundi akizungumza wakati wa kufungua Kilinge salama ambapo ni mazingira ambayo ni rasmi au yasiyo rasmi ambayo wanawake na wasichana wanapata nafasi ya kujadili kwa uhuru masuala yao, amesema kuwa Katika mwezi Machi wa wanawake, TGNP imekuwa ikiandaa vilinge hivyo ili kuhamasisha wanawake kuingia katika nafasi za uongozi. 

“Mategemeo yangu ni kwamba mwisho wa siku ya leo tutaungana kwa pamoja kuendelea kusimamia Agenda ya mwanamke na uongozi katika mkoa wetu wa Dar es Salaam.” 

Pia Mkurugenzi Mtendaji Lilian ameweka bayana takwimu za Wenyeviti wa vijiji kuwa ni asilimia 2.1, Wenyeviti vitongoji ni asilimia 6.7 na Wenyeviti mitaa ni asilimia 12.6. 

Kwa upande wa Wabunge wa kuchaguliwa, wanawake ni 25 ya Wabunge 264 ambayo ni sawa na asilimia 9.5 tu ya Wabunge wote, idadi ya Wabunge wanawake wa Viti Maalumu ni 113 ambayo ni sawa na asilimia 29 ya Wabunge wote.  Jumla ya Wabunge Wanawake ni 142 sawa na asilimia 37 ya idadi ya Wabunge wote ambao ni 393 ambapo ili kufikia 50 kwa 50 ya uongozi wa Wanawake Viongozi lazima ifikiwe kwa kutoa elimu kwa wanawake na wasichana waweze kuwania nafasi mbalimbali za uongozi.

Lilia pia ameeleza kuwa malengo ya Kilinge salama kwa Wasichana na Wanawake ni kukaa pamoja na viongozi wanawake wanaochipukia na viongozi wanawake wenye uzoefu, kuandika na kusambazi kestoria za safari za uongozi za wanawake viongozi mahiri ili kuonesha michango waliyonayo katika maendeleo ya nchi.

Pia kutoa hamasa kwa viongozi wanawake wanaochipukia au wanawake wanaotamani kuwa viongozi. 

Kilinge Salama kwa Wanawake na Wasichana pamoja na viongozi leo ni kutoka mkoa wa Dar es Salaam, halmashauri za Ilala, Kinondoni na Temeke, Mtwara, Lindi na Pwani.

 

Na: Mwandishi Wetu – KILIMANJARO

 Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Patrobas Katambi ameeleza hadi sasa maandalizi ya uzinduzi wa mbio za mwenge wa uhuru yamefikia zaidi ya asilimia 90 huku akihimiza Mkoa wa Kilimanjaro kuhakikisha unahamasisha wananchi kushiriki kwa wingi katika tukio hilo la kihistoria.

 

Amesema hayo wakati akikagua maandalizi ya uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru katika uwanja wa michezo wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU), Mkoani Kilimanjaro.

 

Aidha, Naibu Waziri Katambi amesema kuwa Mbio hizo za Mwenge wa Uhuru kwa mwaka huu 2024 zinaadhimisha miaka 60 tangu kuanzishwa rasmi mwaka 1964 zikienda sanjari na Miaka 60 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na Miaka 60 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.

 

Vile vile, Mhe. Katambi ameupongeza mkoa huo kwa utayari na maandalizi mazuri ya tukio hilo la kitaifa na kuongeza kuwa mwenge huo ni alama ya umoja, hivyo utakimbizwa katika halmashuri 195 kwa lengo la kuunganisha wananchi sambamba na kukagua viwango vya utekelezaji wa miradi ya serikali katika kuwahudumia wananchi.

 

Naye Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Zanzibar, Fatma Rajab amesema kuwa Ofisi ya Waziri Mkuu pamoja na Wizara hiyo wamekua wakishirikiana kwa karibu na ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo wa Kilimanjaro katika kuhakikisha maandalizi yanakamilika ndani ya muda uliopangwa.

 

Kwa upande wake, Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Kilimanjaro, Mhandisi Jackson Masaka amesema kuwa viongozi wa mkoa wamekua na utaratibu wa kukutana na makundi mbalimbali ya wananchi ikiwemo Bodaboda, Wazee, Wafanyabiashara, Wanawake kwa lengo la kuwahamasisha kujitokeza kwa wingi katika uzinduzi huo.

 

Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa kwa mwaka 2024 zinaogozwa na kauli mbiu isemayo “Tunza Mazingira na Shiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa Ujenzi wa Taifa Endelevu”.


Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Patrobas Katambi akizungumza na viongozi wa Mkoa wa Kilimanjaro na Kamati ya Mkoa wakati akikagua maandalizi ya uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa kwa Mwaka 2024 zitakazofanyika katika Uwanja wa michezo wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU), Mkoani Kilimanjaro.

Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Patrobas Katambi akikagua baadhi ya maeneo alipotembelea Uwanja wa michezo wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU), ambapo uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa kwa Mwaka 2024 zitakazofanyika Mkoani Kilimanjaro.Vijana wa Halaiki wakiwa katika mazoezi kwenye uwanja wa shule ya msingi Mwereni, uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa kwa Mwaka 2024 zitakazofanyika katika Uwanja wa michezo wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU), Mkoani Kilimanjaro.
Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Patrobas Katambi (katikati) akifuatilia vijana wa halaiki wakati akikagua maandalizi ya uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa kwa Mwaka 2024 zitakazofanyika katika Uwanja wa michezo wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU), Mkoani Kilimanjaro. Wa tatu kutoka kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Zanzibar, Fatma Rajab.


 


Top News