Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla akiwasili katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo Aprili 19, 2024 kwa ajili ya ufunguzi wa Maonesho ya Biashara Miaka 60 ya Muungano. Anayempokea ni Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Khamis Hamza Khamis.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla akisikiliza maelezo kutoka kwa Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais Bi. Christina Mndeme kuhusu majukumu yanayotekelezwa na Ofisi hiyo alipotembelea banda la Ofisi ya Makamu wa Rais wakati wa ufunguzi wa Maonesho ya Biashara Miaka 60 ya Muungano katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo Aprili 19, 2024.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla akisikiliza maelezo kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi wa Muungano Ofisi ya Makamu wa Rais Bi. Hanifa Selengu wakati Makamu wa Pili wa Rais alipotembelea banda la Ofisi ya Makamu wa Rais wakati wa ufunguzi wa Maonesho ya Biashara Miaka 60 ya Muungano katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo Aprili 19, 2024.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla akisikiliza maelezo kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi wa Muungano Ofisi ya Makamu wa Rais Bi. Hanifa Selengu wakati Makamu wa Pili wa Rais alipotembelea banda la Ofisi ya Makamu wa Rais wakati wa ufunguzi wa Maonesho ya Biashara Miaka 60 ya Muungano katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo Aprili 19, 2024.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla akizungumza na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Khamis Hamza Khamis wakati akiondoka mara baada ya ufunguzi wa Maonesho ya Biashara Miaka 60 ya Muungano katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo Aprili 19, 2024. Kushoto ni Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Mhandisi Cyprian Luhemeja.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla akiwaaga wananchi mara baada ya kufungua Maonesho ya Biashara Miaka 60 ya Muungano katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo Aprili 19, 2024. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Ilala Edward Mpogolo aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam.
Wakiwa kwenye picha ya pamoja ni ujumbe kutoka Uganda, wakiwemo wabunge wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa, wa Bunge la Uganda. Katikati ni Mhe. Gilbert Olanya, wa Jimbo la Kilak Kusini, Mwenyekiti wa Kamati; na kushoto kwakwe ni Prof. Lughano Kusiluka, Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma, (aliyevaa Kaunda).

.......

Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa, ya Bunge la Uganda imeipongeza Serikali ya Tanzania kwa uwekezaji mkubwa iliyofanya katika ujenzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma, pamoja na kusifu Amani na Utulivu mkubwa uliopo, kwa kuzingatia idadi kubwa ya wanafunzi wanaosoma chuoni hapo.

Pongezi hizo zimetolewa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Gilbert Olanya, wa Jimbo la Kilak Kusini, Alhamisi tarehe 18 Aprili 2024, walipofanya ziara ya kutembelea maeneo mbalimbali ya chuo hicho pamoja na kufanya mazungumzo na Makamu Mkuu wa Chuo, Prof. Lughano Kusiluka, kwenye ofisi yake iliyopo jengo la Benjamin Mkapa, Dodoma.

Aidha, wamevutiwa na aina ya masomo yanayofundishwa katika Ndaki, Shule Kuu na Taasisi za Chuo, pamoja na namna chuo kinavyoendelea kuwekeza katika kuanzisha programu mpya za masomo zinazoakisi mabadiliko makubwa ya kisekta yanayozingatia utoaji mafunzo wenye kutatua changamoto kubwa za ajira, na matumizi ya teknolojia katika ufundishaji.

Akiukaribisha ujumbe huo, Makamu Mkuu wa Chuo, Prof. Kusiluka amelishukuru Bunge la Tanzania kwa kuona umuhimu wa kuwaleta wabunge hao kuja kujifunza UDOM, na kueleza ni kwa namna gani wabunge hao wana mchango mkubwa katika kuongeza hamasa ya ufundishaji wa lugha ya Kiswahili katika Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki, na kutunga Sera zenye kusaidia nchi hizo kuendana na mabadiliko makubwa ya kisanyansi na teknolojia katika Sekta ya Elimu.

Aidha, amewahamasisha waganda kuja kusoma Tanzania kutokana na uwepo wa mitaala mizuri na masomo yenye kukidhi mahitaji katika soko la Afrika Mashariki na Afrika kwa ujumla.

“Tunayo fursa ya wananchi wa Uganda na nchi nyinginezo za Afrika Mashariki kuja kusoma UDOM. Niwahakikishie tunayo mazingira mazuri na thabiti ya kujifunzia kwa wana Afrika Mashariki kuja kusoma Tanzania. Mazingira yetu, tamaduni na mahitaji yetu yanafanana, kwangu mimi hii ni fursa kwetu sote” alisisitiza

Wajumbe wengine wa Kamati hiyo waliofika kutembelea Chuo Kikuu cha Dodoma ni pamoja na Mhe. Betty Ethel Naluyima, Mhe. Dkt. Isingoma Patrick Mwesigwa, Mhe. Rwemulikya Ibanda Gerald, Mhe. Patrick Ocan na Mhe. Lillian Obiale Paparu.



Wajumbe wa Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa, wa Bunge la Uganda, wakiwa kwenye mazungumzo na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma, Prof. Lughano Kusiluka, ofisini kwake Dodoma.



Wakiwa kwenye picha ya pamoja ni ujumbe kutoka Uganda, wakiwemo wabunge wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa, wa Bunge la Uganda. Katikati ni Mhe. Gilbert Olanya, wa Jimbo la Kilak Kusini, Mwenyekiti wa Kamati; na kushoto kwakwe ni Prof. Lughano Kusiluka, Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma, (aliyevaa Kaunda).



Prof. Lughano Kusiluka akikamkabidhi zawadi ya ukumbusho Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa, Uganda, Mhe. Gilbert Olanya. Wabunge hao walifika kutembelea chuo na kujifunza mambo mbalimbali yanayohusu utoaji wa Elimu ya Juu nchiniTanzania.



Viongozi wa Chuo Kikuu cha Dodoma wakiagana na waheshimiwa wabunge wa Uganda, baada ya kuhitimisha ziara yao chuoni hapo.
*Ampongeza Rais Dkt. Samia kwa kutenga sh. trilioni 8.18 sekta ya nishati

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameendelea kutenga fedha za kutekeleza miradi ya nishati ambapo katika kipindi cha miaka mitatu zaidi ya shilingi trilioni 8.18 zilitolewa.

“Maono na maelekezo yake kuhusu usimamizi wa sekta hii yamekuwa na mchango mkubwa katika ufanisi wa shughuli za sekta, katika hili, ninampongeza sana Mheshimiwa Rais kwa kuweka kipaumbele kikubwa katika utekelezaji wa miradi ya nishati.”

“Katika kuhakikisha upatikanaji wa uhakika wa umeme nchini, tayari nchi yetu imeanza kutumia umeme wa bwawa la Julius Nyerere Hydropower Project (JNHPP). Huu ni ushindi na kielelezo tosha kwamba Mama yupo kazini.”

Ametoa pongezi hizo leo jioni (Ijumaa, Aprili 19, 2024) wakati akifunga Maonesho ya Wiki ya Nishati yaliyofanyika kwenye viwanja vya Bunge jijini Dodoma.

Waziri Mkuu amelipongeza Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) kwa kuweza kuzalisha umeme zaidi ya mahitaji yaliyopo sasa. “Leo tarehe 19 Aprili, 2024 uzalishaji wa umeme ni mkubwa. Shirika letu la TAMESCO limemudu kuzalisha umeme zaidi ya mahitaji tuliyonayo na bwawa la Julius Nyerere Hydropower Project limeanza kazi na tayari megawati 235 ziko kwenye mfumo.”

Ameitaka Wizara hiyo iweke mkakati wa kuhakikisha maonesho hayo yanakuwa endelevu ili Waheshimiwa Wabunge waweze kupata fursa ya kuwasilisha hoja zao mahsusi na kutatua kero za wananchi wanaowawakilisha.

Kutokana na kuongezeka kwa idadi ya washiriki wa maonesho hayo ikilinganishwa na miaka miwili iliyopita, Waziri Mkuu ameitaka Wizara hiyo ione uwezekano wa kuandaa maonesho kama hayo katika ngazi ya Mikoa na Halmashauri. “Wakurugenzi wa Kanda na Mameneja wa Mikoa na Wilaya mko hapa. Nendeni mkae na muangalie jinsi ya kutekeleza jambo hilo,” amesisitiza.

Ameitaka Wizara hiyo iweke mkakati wa kuhakikisha wananchi wote wanapata ufafanuzi wa masuala mbalimbali kuhusu fursa zinazopatikana kutokana na miradi inayotekelezwa na sekta ya nishati. “Pamoja na kuyaleta maonesho hapa Bungeni, kuna haja ya kupeleka maonesha kama haya kwenye maeneo ya katiati ya mji ili muweze kuwafikia wananchi wengi zaidi na kujibu hoja zao,” amesema.

Mapema, akimkaribisha Waziri Mkuu kuzungumza na wadau mbalimbali walioshiriki maonesho hayo, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko ameipongeza TANESCO kwa kuendelea kufanya kazi nzuri ya kuhakikisha wananchi wanapata nishati ya umeme.

Naye, Spika wa Bunge la Tanzania, Dkt. Tulia Ackson amesema sekta ya nishati ni kati ya sekta mtambuka kwa sababu inalisha sekta nyingine nyingi na ikitikisika, inatikisa na maeneo mengine pia.

Amesema pamoja na utoshelevu wa umeme kwenye gridi ya Taifa, ili kuwe na maendeleo bado nchi inahitaji umeme wa kutosha na hasa kwenye viwanda na siyo kuwasha taa za majumbani.

Ameitaka Serikali itafute njia ya kutumia vizuri maji yanayotoka kwenye bwa la JNHPP ili yaweze kuwanufaisha wananchi wanaoishi maeneo ya jirani na bwawa hilo. “Bwawa limejaa kwa hiyo Serikali ihakikishe maeneo ya jirani yanapata maji ya kutumia. Tuanzishe gridi ya maji kama ilivyo kwenye gridi ya umeme. Kule chini tutengeneze njia ya kutunza maji kwa ajili ya matumizi ya umwagiliaji na mifugo,” amesema.

Naye, Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Mhandisi Felchesmi Mramba amesema ushiriki wa mwaka huu umevunja rekodi kwani watu zaidi ya 480 walitembelea maonesho hayo ambapo 267 walikuwa ni Waheshimiwa Wabunge.

Ameyataja maeneo ambayo washiriki walikuwa wakiulizia zaidi ni umeme, nishati ya jua, nishati jadidifu, nishati safi ya kupikia, mafuta na gesi.

Amesema ili kujenga uelewa mpana kwa wananchi, wanapanga kuandaa kongamano maalum juu ya gesi asilia ambalo linatarjiwa kufanyika Mei, mwaka huu.




-Asisitiza uadilifu na uwajibikaji kwa mali za umma

-Apongeza Serikali Njombe mrejesho kwa wananchi, chama kwa usimamizi

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk Emmanuel John Nchimbi, amesema kazi kubwa iliyofanywa na Serikali, chini ya uongozi wa Rais Dk Samia Suluhu Hassan, ndani ya miaka mitatu, ni nyezo inayobeba ukweli wa kutosha kusambaratisha uongo unaoenezwa na baadhi ya wapinzani wa kisiasa kupitia mikusanyiko yao.

Amewataka wana-CCM wote kuendelea kujiamini na kutembea kifua mbele wanapozisema, kuzitangaza na kuikumbusha jamii kuhusu kazi za maendeleo na ustawi wa jamii, zinazofanywa na Serikali za CCM ili wananchi waendelee kuuona ukweli, wakitofautisha na uongo unaoenezwa kwa propaganda nyepesi za kisiasa.

Balozi Nchimbi amesema hayo leo, Aprili 19, 2024, alipokuwa akiwahutubia maelfu ya wanaCCM wa Mkoa wa Njombe, kupitia Mkutano Maalum wa Mkoa, uliofanyika mjini Njombe.

“Mambo yaliyofanywa na Serikali ndani ya hii miaka mitatu, unaweza kuona kama ni miujiza. Kazi kubwa sana inafanyika. Ni wajibu wetu kuitumia nyenzo yenye ukweli kupambana,” amesema.

Kupitia mkutano huo, ambao Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Antony Mtaka aliwasilisha taarifa ya mrejesho wa utekelezaji wa Ilani ya CCM ya 2020 - 2025, iliyohusisha miradi mbalimbali ya maendeleo na ustawi wa wananchi, Balozi Nchimbi pia amerudia kusisitiza kwa watendaji wa Chama na Serikali ulazima na umuhimu wa kuwa waadilifu wakati wote kwenye masuala yanayohusu rasilimali za umma, kwa kupiga vita rushwa na ubadhirifu.






Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk Emmanuel John Nchimbi, akiwa kwenye Kikao cha Kamati ya Siasa ya Halmashauri Kuu ya Mkoa wa Njombe, kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya CCM Mkoa wa Njombe, Njombe Mjini, kabla ya kuelekea kwenye Mkutano Mkuu Maalum wa Mkoa wa Njombe, leo asubuhi, Aprili 19, 2024.

Dk Nchimbi, akiambatana na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC), Oganaizesheni, Ndugu Issa Haji Usi Gavu na Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Ndugu Amos Gabriel Makala, yuko mkoani Njombe kwa ziara ya siku mbili, ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake katika mikoa 6 ya Katavi, Rukwa, Songwe, Mbeya, Njombe na Ruvuma.








Waziri wa Maji Mhe.Jumaa Aweso (MB) amefika Wilaya ya Monduli kunusuru Bwawa la Nanja ambalo ni Tegemeo la Vijiji 30 katika chanzo Maji pekee baada ya kumeguka kingo kutokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha.

Amesisitiza kwamba pamoja na ugumu wa kukarabati bwawa hilo wakati likiwa na maji maamuzi magumu yafanyike wataalamu wa Wizara ya Maji watumie utaalamu wao kulifanikisha hiko kwani hakuna namna nyingine.

Akizungumza na mamia wa wananchi wa Kata za Lepruko, Sepeko, na Makuyuni Waziri wa maji maelekezo kwa Wataalamu wa Wizara kama ifuatavyo kwanza kutumia taaluma zao kuhakikisha Bwawa hilo linakarabatiwa kwa dharula haraka kuanzia kesho tarehe 19.04.2024 kudhibiti maji kuebdelea kupotea pili kufanya usanifu wa kina nyakati za kiangazi kusudi bwawa hilo liweze kukarabatiwa kwa uhakika zaidi.

Katika hatua nyingine Mbunge wa Jimbo la Monduli Mh Fred Lowassa amesema Bwawa hilo ndio tegemeo la wana Monduli kwenye matumizi ya maji kwa Binadamu, mifugo na wanyamapori hivyo anaiomba Serikali ione namna ya kukarabati bwawa hilo kwa dharura.

Aidha, Wakizungumza katika nyakati tofauti madiwani wa kata zinazoguswa na bwawa hilo wameishukuru serikali inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan kuwafikia kwa haraka na kutafuta suluhu ya utatuzi ya changamoto hii.



Na Oscar Assenga,TANGA

WAZIRI wa Ardhi,Nyumba na Mendeleo ya Makazi Jerry Silaa anatarajiwa kuongoza Kliniki ya Ardhi kwa mkoa wa Tanga itakayofanyika kuanzia Aprili 22 mpaka 28 mwaka huu ikifanyika kwenye maeneo mawili Kijiji cha Miaka 21 Chumbageni Tanga na Korogwe.

Akizungumza na waandishi wa habari leo,Kamishna Msaidizi wa Ardhi mkoa wa Tanga Tumaini Gwakisa alisema zoezi hilo litafanyika kwenye maeneo mawili ambapo litaanzia Ofisi ya Kamishna wa Ardhi Msaidizi wa Mkoa wa Tanga eneo la Kijiji cha miaka 21 Chumbageni kuanzia Aprili 22 mpaka 25 mwaka huu.

Alisema baada ya kumaliza kwa Tanga wataelekea wilayani Korogwe ambapo litafanyika kuanzia Aprili 26 mpaka 28 mwaka hu na uendeshwaji wa program hiyo utasimaiwa na itaongozwa na Waziri wa Ardhi Jerry Silaa akiwa na wataalamu wa Wizara hiyo.

“Nichukue nafasi hii kwaalika wananchi wote wa mkoa wa Tanga kuhudhuria na kupata huduma mbalimbali za sekta ya ardhi katika maeneo ambayo kliniki hiyo itafanyika kwani kutakuwa na utatuzi wa migogoro ya ardhi ambapo Waziri atasikiliza kero mbalimbali za Migogoro hiyo”Alisema

Alisema pia kutakuwa na utolewaji wa elimu kuhusu usimamizi wa ardhi pamoja na uwepo wa kituo jumuishi kitakachotoa huduma ya kupokea maoni mbalimbali na utoaji hati miliki ,ukadiriaji wa kodi ya ardhi na ulipaji wa kodi ya ardhi.

Gwakisa aliwataka wananchi wa mkoa wa Tanga kuhudhuria na kushiriki ambapo Waziri atakuwepo na wataalamu kutoka Wizarani


KILA kukicha Meridianbet inasambaza tabasamu na upendo kwa wateja wake wanaocheza michezo ya kasino ya mtandaoni au kubashiri mubashara, odds kubwa na bonasi za kasino ni sehemu ya zawadi za kila siku. Jisajili sasa uwe wa kwanza kupata tabasamu kila kukicha.

Kama wewe ni mdau wa kucheza kasino ya mtandaoni pale Meridianbet bila shaka neno Expanse sio geni kichwani mwako! Sasa mchongo uko hivi, kila unapocheza michezo ya kasino au sloti zilizotengenezwa na Expanse Studio unakuwa na nafasi ya kupata mgao wa mpaka Tsh 1,250,000/=

Shindano la Expanse na Meridianbet Kasino ya Mtandaoni.

Promosheni hii imeanza 18.04. 2024 ambapo bonasi za kasino zitagawiwa kwa washindi watakaokuwa wanatangazwa kila siku, baada ya kucheza moja kati ya michezo ya kasino ya mtandaoni iliyopo Meridianbet kutoka Expanse studio.

Promosheni ni halali kwa wachezaji waliosajiliwa kwenye APP na tovuti ya meridianbet.co.tz

Promosheni itafanyika katika mtindo wa mashindano kwa wachezaji kwenye sloti zinazotolewa na Expanse Studio. Michezo ya kasino ya mtandaoni itakayotumika wakati wa promosheni ni:
Battle of Egypt
Forest Rock
Fortune Farm
Lucky's Betting Shop
Maya's Treasure
Piggy Party
Spinning Buddha
Sticky 777
The Book of Eskimo
Veni Vidi Vici
Wild Corrida
Zombie Apocalypse
Battle for the Throne
Bounty Hunters
Capital City Derby
Casino Heist
Fairy in Wonderland
Odd One Out
Planet Power
Shaolin Crew

Wachezaji watashindana kwa mfumo wa pointi ambapo kila dau la jumla ya TZS 2,500 litatoa pointi 2. Dau la chini kwa kila mzunguko kwa promosheni hii ni TZS 400.

Kulingana na msimamo wa mwisho, wachezaji 40 watazawadiwa pesa taslimu na mizunguko ya bure kucheza kwenye kasino ya mtandaoni kama ifuatavyo:

Nafasi ya 1 – TSH 1,250,000
Nafasi ya 2 - TSH 750,000
Nafasi ya 3 – TSH 250,000
Nafasi ya 4 na 5 - TSH 125,000
Nafasi ya 6 mpaka 10 – Mizunguko 300 ya bure kwenye sloti ya PIA
Nafasi ya 11 mpaka 20 - Mizunguko 200 ya bure kwenye sloti ya PIA
Nafasi ya 21. mpaka 30 - Mizunguko 100 ya bure kwenye sloti ya PIA
Nafasi ya 31. mpaka 40 - Mizunguko 50 ya bure kwenye sloti ya PIA

Ushindi utakaotokana na Mizunguko ya bure utahitaji kuzungushwa mara 60x (kwa mfano, ukishinda TZS 10,000 kwenye Mizunguko ya bure, utahitaji kucheza TZS 600,000 kwenye mchezo uleule ili kuhamisha ushindi wako kwenye akaunti ya pesa halisi).

Taarifa kuhusu malipo ya juu kwa kila Kundi la Mizunguko ya bure, washindi watapokea taarifa ambayo itatumwa kwao si zaidi ya saa 13:00 AM tarehe 03.05.2024.
KAMPUNI bingwa kabisa ya michezo ya kubashiri kampuni ya Meridianbet imeing’arisha kata ya Makongo jijini Dar-es-salaam baada ya kufika kwenye eneo hilo na kutoa vifaa vya usafi.

Mara kwa mara mabingwa hao wa michezo ya kubashiri wamekua wakihakikisha wanarudisha fadhila kwenye jamii yao ambayo imewazunguka, Leo imekua ni zamu ya eneo la Makongo jijini Dar-es-salaam ambao ndio wamekua wanufaika.

Meridianbet wamegawa matoroli, Mafagio, pamoja na Reflectors kwajili ya kuhakikisha wanaimarisha usafi katika eneo hilo la Makongo kata ya Mlalakua, Hili limekua zoezi endelevu kua kwa kampuni hiyo katika kuhakikisha wanaiunga mkono serikali katika juhudi za kuweka mazingira safi.

Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano na Masoko kutoka Meridianbet Bi Nancy Ingram ndio aliyeongeza zoezi hilo zima la ugawaji wa vifaa hivo”Kwanza kabisa nishukuru kwa mapokezi yenu mazuri mliyotupatia, Lakini jambo muhimu zaidi ni kuja hapa kugawa vifaa hivi vya usafi kwajili ya kuhakikisha usafi unaimarishwa mara dufu na hii tunaungana na serikali yetu pendwa ambayo inapambana kuhakikisha mazingira yapo safi”

Suka mkeka wako kwenye michezo mikali itakayopigwa leo kwenye michuano ya Uefa Europa League na Uefa Conference League. Machaguo zaidi za 1000 yapo huku lakini vile vile Turbo Cash pia ipo. Unasubiri nini sasa? Ingia meridianbet na ubashiri sasa.`

Wakati huohuo wakazi wa eneo hilo wameonekana kufurahishwa na jambo ambalo limefanywa na uongozi wa Meridianbet, Huku moja ya viongozi wa eneo hilo akitoa shukrani zake za dhati kwa mabingwa hao wa kubashiri na kutoa wito wa makampuni mengine kuiga mfano wa Meridianbet.



Na; Mwandishi Wetu – Dar es Salaam

Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Patrobas Katambi amesema Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuyapa kipaumbele masuala ya maendeleo ya vijana nchini.

Aidha, Mhe. Katambi amesema vijana ni nguvu kazi ya taifa, hivyo kuwezesha kundi hilo kunatoa fursa kubwa ya kuongeza kasi ya ukuaji wa uchumi na kuwafanya vijana kuwa chachu kwa maendeleo ya nchi.

Ameyasema hayo wakati wa hafla ya uzinduzi wa Programu ya Mpango wa Ulinzi wa Vijana Awamu ya Pili “Safeguard Young People (SYP)” iliyofanyika jijini Dar es Salaam.

Vile vile, Naibu Waziri Katambi amesema serikali imeboresha mwongozo wa utoaji mikopo kupitia mfuko wa maendeleo ya vijana ambapo kwa sasa mfuko huo unatoa mikopo kwa kijana mmoja mmoja, ambapo maboresho hayo yatawawezesha vijana walio katika sekta isiyo rasmi na wahitimu wa vyuo kujiajiri kwa kuanzisha miradi ya uzalishaji mali.

Kwa upande wengine, Mhe. Katambi amesema programu ya Safeguard Young People ni fursa kwa vijana kujikwamua na changamoto za kijamii na kiuchumi, hivyo amehamasisha ushirikiano katika utekelezaji wa programu hiyo ili kufikia malengo na kuleta mabadiliko chanya kwa vijana.

Naye, Balozi wa Switzerland Nchini Tanzania, Mhe. Didier Chassot amesema ni wakati wa kutambua mchango wa vijana katika kukuza maendeleo ya taifa. Aidha, ameongeza kuwa serikali ya Uswisi itaendelea kushirikiana na Tanzania katika kutekeleza programu hiyo ya SYP kwa lengo la kuwaondolea vijana changamoto za kiafya, kiuchumi, kisaikolojia na kijamii.

Akizungumza mmoja wa wanufaika amesema programu hiyo imewasaidia vijana kujitambu, kijithamini na kuwa na uthubutu katika kufanya maamuzi sahihi.

Programu ya Mpango wa Ulinzi wa Vijana “Safeguard Young People (SYP)” inalenga kuboresha huduma za afya, elimu ya afya kwa vijana, kuongeza ushirikishwaji wa vijana katika ngazi za maamuzi na pia kuwaunganisha vijana na fursa za kujipatia ujuzi na kipato.
Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Patrobas Katambi akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa wa Programu ya Mpango wa Ulinzi wa Vijana Awamu ya Pili “Safeguard Young People (SYP II)” iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya washiriki wakifuatilia hotuba ya Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Patrobas Katambi (hayupo pichani) wakati wa hafla ya uzinduzi wa wa Programu ya Mpango wa Ulinzi wa Vijana Awamu ya Pili “Safeguard Young People (SYP II)” iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Balozi wa Switzerland Nchini Tanzania, Mhe. Didier Chassot akieleza jambo wakati wa hafla ya uzinduzi wa wa Programu ya Mpango wa Ulinzi wa Vijana Awamu ya Pili “Safeguard Young People (SYP II)” iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Mwakilishi Mkazi wa UNFPA Tanzania, Mark Shreiner akieleza jambo kuhusu utekelezaji wa Programu ya Mpango wa Ulinzi wa Vijana Awamu ya Pili “Safeguard Young People (SYP)” wakati wa hafla ya uzinduzi wa programu hiyo jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Patrobas Katambi (kulia) akizindua rasmi Programu ya Mpango wa Ulinzi wa Vijana Awamu ya Pili “Safeguard Young People (SYP II)”. Wa pili kutoka kulia ni Mkurugenzi wa Maendeleo ya Vijana Zanzibar, Bw. sahib Mohamed na Balozi wa Switzerland Nchini Tanzania, Mhe. Didier Chassot (wa pili kutoka kushoto).
Mmoja wa Kijana aliyeshiriki tukio la uzinduzi wa Programu ya Mpango wa Ulinzi wa Vijana Awamu ya Pili “Safeguard Young People (SYP II), Getrude Clement akitoa neno la shukrani wakati wa hafla hiyo.

Wasanii wa muziki wa kizazikipya Ben Pol, Phina na Tommy Flavor wakitoa burudani wakati wa hafla hiyo ya uzinduzi wa Programu ya Mpango wa Ulinzi wa Vijana Awamu ya Pili “Safeguard Young People (SYP II), iliyofanyika jijini Dar es Salaam.


Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Patrobas Katambi (kushoto) akiteta jambo na Mwakilishi Mkazi wa UNFPA Tanzania, Mark Shreiner (kulia). Katikati ni Balozi wa Switzerland Nchini Tanzania, Mhe. Didier Chassot.

PICHA NA OFISI YA WAZIRI MKUU

(KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU)
IKIWA wikendi inaanza leo hii hapo baadae ligi mbalimbali zinatarajiwa kupigwa kuanzia kule Ujerumani mpaka Italia huku meridianbet wakikupa nafasi kubwa za kupiga maokoto ukisuka jamvi lako na kubashiri nao. Ingia sasa meridianbet ushinde pesa.

LALIGA leo itapigwa mechi moja majira ya saa 4:00 usiku ambapo Athletic Bilbao atakuwa mwenyeji wa Granada. Bilbao yupo nafasi ya 5 kwenye msimamo wa ligi na mgeni wake yupo nafasi ya 19 mkiani kabisa. Mara ya mwisho kukutana walitoshana nguvu. Je leo hii nani ataondoka na ushindi? Mechi hii imepewa ODDS 1.22 kwa mwenyeji na 12.74 kwa mgeni. Suka jamvi hapa.

Kumbuka kucheza michezo ya Kasino ya Mtandaoni ambayo inatolewa ndani ya meridianbet kama vile Poker, Roullette, Aviator, Rockertman, Keno, Sloti na mingine kibao. Ingia mchezoni na ucheze sasa.

Ligi nyingine ambayo itaendelea Ijumaa ya Leo ni SERIE A ambapo saa 1:30 kutakuw ana mtanange mzito kabisa kati ya Genoa dhidi ya Lazio ambaye yupo nafasi ya 7 kwenye msimamo wa ligi huku mwenyeji akiwa nafasi ya 12. Tofauti ya pointi kati yao ni 10 pekee ambapo mechi ya mwisho kukutana kwenye ligi, Genoa lishinda. Mechi hii imepewa ODDS 2.99 kwa 2.50. Wewe leo hii unamdhamini nani kukupa pesa? Jisajili sasa.

Juventus chini ya Allegri baada ya kulazimishwa sare mechi iliyopita, leo hii atakuwa ugenini kupepetana dhidi ya Cagliari Calcio katika Unipol Domus huku Meridianbet wakimpa nafasi kubwa ya kushinda Juve kwa ODDS 1.76 kwa 4.90. Ikumbukwe kuwa mwenyeji hayupo nafasi nzuri kwenye msimamo wa ligi baada ya mechi iliyopita kutoa sare. Je leo hii anaweza pata pointi 3 akiwa nyumbani?. Tengeneza mkeka wako hapa.

Vilevile bila kukosa utamu wa BUNDESLIGA leo hii kuna mechi ya kusisimua vilivyo ambapo Eintracht Frankfurt atamkaribisha nyumbani kwake Augsburg huku timu hizo zikiwa zinafuatan kwenye msimamo wa ligi yaani wa 6 kwa wa 7. Wamepishana pointi 3 tuu. Mara ya mwisho kukutana, Augsburg alishinda. Je Frankfurt atalipa kisasi kwa kushinda. Bashiri mechi hii ambayo ina machaguo zaidi ya 1000, ndani ya Meridianbet.

Tukimalizia na ligi kuu ya Ufaransa leo hii, LIGUE 1 napo ni mechi moja Ijumaa ya leo OGC Nice atakipiga dhidi ya FC Lorient saa 4:00 usiku huku wakitoshana nguvu mechi ya mwisho kukutana. Meridianbet wamempendelea Nice kushinda kwa ODDS 1.50 kwa 6.07. Ikumbukwe kuwa mwenyeji yupo nafasi ya 5 kwa 16. Beti sasa.

NA EMMANUEL MBATILO, MICHUZI TV

KAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation wamekabidhi mitungi ya gesi ya kupikia ya Oryx 50 kwa wauguzi katika Hospitali ya Rufaa ya Mwananyamala jijini Dar es Salaam kati ya mitungi  1000  inayotarajiwa kukabidhiwa kwa wauguzi na madaktari katika mikoa 10 nchini .

Akizungumza wakati wakisaini makubaliano ya ushirikiano yaliyofanyika katika hospitali ya rufaa ya Mwananyama, Mkurugenzi wa Kampuni ya gesi ya oryx Araman Benoite amesema makubaliano walioingia baina ys kampuni hiyo na taasisi ya Doris Mollel ni kusaidia kuongeza matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa watanzania.

Aidha amesema katika kampeni hiyo ya kuwezesha watanzania kuingia katika matumizi ya nishati safi ya kupikia, mpaka sasa tayari wameshatoa mitungi kwa wananchi zaidi ya elfu 32 ili kusaidia lengo la kufikia asilimia 80 ya watumiaji wa nishati safi.

Amesema matumizi ya nishati safi ya kupikia inasaidia kuondoa hatari za kiafya kwa watumiaji wa kuni na mkaa kama nishati ya kupikia lakini pia hatari za kimazingira na ustawi wa jamii.

"Takribani watu 33,000 wanapoteza maisha nchini Tanzania kwa maradhi yanayotokana na kuvuta moshi unaotokana na mkaa au kuni hiyo ndio sababu ya Oryx gas kuja na suluhisho la kuwahamasisha wananchi kutumia gesi kwa matumizi ya kupikia", amesema Benoite

Ameeleza kuwa matumizi ya gesi yanaepusha wamama na watoto kuumika kubeba kuni hivyo kuepuka kujeuriwa na wanyama wakali wakiwa katika harakati za kutafuta kuni pia kuimarisha maisha ya wanawake na kuwalinda dhidi ya vitendo vya udhalilishaji.

“Kuanzia mwezi wa saba mwaka 2021 tumekuwa mstari wa mbele kuunga mkono utekelezaji wa mkakati wa serikali uliopewa nguvu na Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania , Dk. Samia Suluhu Hassan kwa lengo kwamba ifikapo mwaka 2033 asilimia 80 ya Watanzania wawe wanatumia nishati safi ya kupikia”, ameeleza.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Taasisi ya Doris Mollel , Doris Mollel amesema katika makubaliano waliosaini na oryxy watawafikia waguzi elfu moja ambapo watawapa mitungi na majiko ya gesi kama mabalozi kwa kina mama waweze kutumia nishati safi ya kupikia ikiwa ni programu ya miaka miwili.

Amesema mitungi hiyo itakwenda kwa wauguzi walioko maeneo magumu ambapo watakuwa wanawatembelea kwenye vituo vya afya na zahanati ili kuweza kuwafikia wafanyakazi ambao ni wauguzi wanaofanya kazi kubwa ya kuokoa maisha hususani ya mama na mtoto.

Wakati huo huo Mganga Mfawidhi Hospitali ya Rufaa ya Mwananyamala  Dk.Zavery Benela ameeleza kwamba hospitali hiyo  inakabiliwa na ongezeko la wagonjwa wa mifumo ya hewa.

Amefafanua kati ya wagonjwa wa nje 500 wanaofika kuonwa na madaktari bingwa asilimia 30 ya wagonjwa hao ni wa matatizo ya mfumo wa hali ya hewa unaosababishwa na hali ya hewa pamoja na mazingira ya kuandaa chakula kutokna na kuni na mkaa.

Aidha Dokta Benela amesema magonjwa ya mfumo wa hali wa hewa  yamekuwa changamoto hasa kwa watu wazima na watoto.

Mkurugenzi wa Taasisi ya Doris Mollel , Doris Mollel akisaini hati ya makubaliano ya ushirikiano na Kampuni ya Oryx Gas kuwezesha nishati safi ya kupikia kwa wauguzi na madaktari 1000 kutoka mikoa 10  nchini watakabidhi mitungi ya kupikia ya Oryx Gas lengo likiwa kuliwezesha kundi hilo la sekta ya afya kuondokana na matumizi ya kuni na mkaa. Hafla hiyo imefanyika leo Aprili 19, 2024.
Mkurugenzi wa Kampuni ya gesi ya oryx Araman Benoite akizungumza wakati wa hafla ya utiaji saini na Taasisi ya Doris Mollel kushirikiana kuwezesha nishati safi ya kupikia kwa wauguzi na madaktari 1000 kutoka mikoa 10 nchini watakabidhi mitungi ya kupikia ya Oryx Gas lengo likiwa kuliwezesha kundi hilo la sekta ya afya kuondokana na matumizi ya kuni na mkaa. Hafla hiyo imefanyika leo Aprili 19, 2024.
Mkurugenzi wa Taasisi ya Doris Mollel , Doris Mollel akizungumza katika hafla ya utiaji saini ya makubalinao na Kampuni ya Oryx Gas kushirikiana kuwezesha nishati safi ya kupikia kwa wauguzi na madaktari 1000 kutoka mikoa 10  nchini watakabidhi mitungi ya kupikia ya Oryx Gas lengo likiwa kuliwezesha kundi hilo la sekta ya afya kuondokana na matumizi ya kuni na mkaa. Hafla hiyo imefanyika leo Aprili 19, 2024.

Mkurugenzi wa Taasisi ya Doris Mollel , Doris Mollel (katikati) akizungumza katika hafla ya utiaji saini ya makubalinao na Kampuni ya Oryx Gas kushirikiana kuwezesha nishati safi ya kupikia kwa wauguzi na madaktari 1000 kutoka mikoa 10  nchini watakabidhi mitungi ya kupikia ya Oryx Gas lengo likiwa kuliwezesha kundi hilo la sekta ya afya kuondokana na matumizi ya kuni na mkaa. Hafla hiyo imefanyika leo Aprili 19, 2024.
Mganga Mfawidhi Hospitali ya Rufaa ya Mwananyamala mkoani Dar es Salaam  Dk.Zavery Benela akizungumza wakati wa hafla ya utiaji saini na Taasisi ya Doris Mollel kushirikiana kuwezesha nishati safi ya kupikia kwa wauguzi na madaktari 1000 kutoka mikoa 10 nchini watakabidhi mitungi ya kupikia ya Oryx Gas lengo likiwa kuliwezesha kundi hilo la sekta ya afya kuondokana na matumizi ya kuni na mkaa. Hafla hiyo imefanyika leo Aprili 19, 2024.
Mkurugenzi wa Kampuni ya gesi ya oryx Araman Benoite na Mkurugenzi wa Taasisi ya Doris Mollel , Doris Mollel wakionesha mkataba waliosaini  kwaajili ya kuwezesha nishati safi ya kupikia kwa wauguzi na madaktari 1000 kutoka mikoa 10  nchini watakabidhi mitungi ya kupikia ya Oryx Gas lengo likiwa kuliwezesha kundi hilo la sekta ya afya kuondokana na matumizi ya kuni na mkaa. Hafla hiyo imefanyika leo Aprili 19, 2024.
Mkurugenzi wa Kampuni ya gesi ya oryx Araman Benoite na Mkurugenzi wa Taasisi ya Doris Mollel , Doris Mollel wakimkabidhi mtungi wa kupikia wa gesi ya Oryx mmoja wa wauguzi katika hospitali ya rufaa ya Mwananyamala Jijini Dar es Salaam wakati wa hafla ya utiaji saini makubalino kati ya kampuni ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation kuwezesha nishati safi ya kupikia kwa wauguzi na madaktari 1000 kutoka mikoa 10  nchini watakabidhi mitungi ya kupikia ya Oryx Gas lengo likiwa kuliwezesha kundi hilo la sekta ya afya kuondokana na matumizi ya kuni na mkaa. Hafla hiyo imefanyika leo Aprili 19, 2024.
Mkurugenzi wa Kampuni ya gesi ya oryx Araman Benoite  akitoa elimu ya matumizi sahihi ya mtungi wa kupikia wa gesi ya Oryx kwa wauguzi wa hospitali ya rufaa ya Mwananyamala katika hafla ya utiaji saini kati ya kampuni ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation kuwezesha nishati safi ya kupikia kwa wauguzi na madaktari 1000 kutoka mikoa 10  nchini watakabidhi mitungi ya kupikia ya Oryx Gas lengo likiwa kuliwezesha kundi hilo la sekta ya afya kuondokana na matumizi ya kuni na mkaa. Hafla hiyo imefanyika leo Aprili 19, 2024.


Baadhi ya wauguzi wa hospitali ya rufaa ya Mwananyamala wakifuatilia hafla ya utiaji saini kati ya kampuni ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation kuwezesha nishati safi ya kupikia kwa wauguzi na madaktari 1000 kutoka mikoa 10  nchini watakabidhi mitungi ya kupikia ya Oryx Gas lengo likiwa kuliwezesha kundi hilo la sekta ya afya kuondokana na matumizi ya kuni na mkaa. Hafla hiyo imefanyika leo Aprili 19, 2024.

(PICHA ZOTE NA EMMANUEL MBATILO)


Top News