Viongozi wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali kuu na Afya (TUGHE) Tawi la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) wamepongezwa kwa kuandaa vyema mkutano mkuu wa mwaka jambo linalowapa fursa ya kujadili kwa mapana taarifa mbalimbali za kiutendaji ndani ya chama na hatimaye kuandaa mapendekezo yatakayoweza kuleta tija ndani ya TCAA.

Hayo yameelezwa leo Aprili 25, 2024 na Mkurugenzi wa Sheria wa TCAA Bi. Maria Makalla wakati wa kufungua mkutano mkuu wa mwaka wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali kuu na Afya (TUGHE) Tawi la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) uliofanyikia Mkoani Morogoro.

"Nimefarijika kuona kwamba ninyi kama viongozi wa chama cha wafanyakazi mnatambua wajibu wenu kama ulivyoainishwa katika sheria ya Mahusiano Kazini ya mwaka 2004 kifungu cha 62(4), na kwamba mnafanya jitihada zote kuhakikisha mnafuata taratibu za vikao halali,mnapopitisha mambo yenu. Nawapongeza pia kwa hili,"amesema Bi. Makalla

Kiongozi huyo amepongeza uongozi na wanachama wa TUGHE kwa kuandaa vyema mkutano huu wa mwaka jambo linalowapa fursa ya kujadili kwa mapana taarifa mbalimbali za kiutendaji ndani ya chama na hatimaye kuandaa mapendekezo yatakayoleta tija ndani ya taasisi.

Pia amesema TCAA imekuwa tulivu na hakuna migogoro kwa kipindi chote hiki hii yote ni matokeo ya uwepo wa daraja zuri la kuwakilisha wafanyakazi, jukwaa la kuwasemea, kutokana na kuwepo na misingi imara.

Mbali na hayo, Bi. Makalla aliwakumbusha kuwa wao ni daraja zuri la kuwakilisha wafanyakazi na jukwaa la kuwasemea, yote haya yametokana na kuwepo na misingi imara iliyotengenezwa na TCAA.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa TUGHE Tawi la TCAA Jackline Ngoda, amesema lengo la kufanya kikao hicho ni kuwakumbusha watumishi wajibu wao katika utendaji ikiwa na kauli mbiu isemayo Maslahi bora ni kiunganishi na kichocheo cha ufanisi mahala pa kazi kwani kupitia kauli mbiu hiyo inakuwa kama kipimo cha cha namna gani TCAA inaweza kuleta ufanisi katika kazi baada ya mambo ya maslahi kuwa mazuri.

Kwa upande wa Katibu wa TUGHE mkoa wa Dar es Salaam Bi. Sara Rwezaura ametoa wito kwa wanachama wa TUGHE tawi la TCAA kuwa wavumilivu pindi wanapowasilisha hoja zao na pia uvumilivu huo usiwakatishe tamaa waendelee kuwasilisha hoja zao na wasikae nazo.

Kwa upande wa Katibu wa Tughe tawi la TCAA Bw. Shukuru Mhina amesisitiza juu ya umuhimu wa mafunzo kwa viongozi wapya wa TUGHE TCAA na kuongeza kuwa kupitia mafunzo ndio viongozi wanajengwa.

Mkurugenzi wa Sheria  kutoka Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) Maria Makalla akizungumza wakati wa kufungua mkutano mkuu wa mwaka wa cha Chama cha Wafanyakazi wa Serikali kuu na Afya (TUGHE) Tawi la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) uliofanyika Mkoani Morogoro
Mwenyekiti wa TUGHE Tawi la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Bi. Jackline Ngoda akizungumza kuhusu namna wanavyoshirikiana na viongozi wa TCAA pamoja na kumkaribisha Mgeni rasmi.
Katibu wa TUGHE Mkoa wa Dar es Salaam Bi. Sara Rwezaula akitoa salamu za TUGHE Mkoa wa Dar es Salaam  wakati wa ufunguzi wa mkutano mkuu wa mwaka wa cha Chama cha Wafanyakazi wa Serikali kuu na Afya (TUGHE) Tawi la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) uliofanyika Mkoani Morogoro.
Katibu wa TUGHE Tawi la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA),Bw. Shukuru Mhina akifanywa utambulisho wa wajumbe wa mkutano mkuu wa mwaka wa TUGHE tawi la TCAA kwa Mgeni rasmi.
Baadhi ya Wanachama wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali Kuu na Afya (TUGHE) tawi la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) wakifuatilia mada wakati wa mkutano wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali Kuu na Afya (TUGHE) Tawi la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA).
Mgeni rasmi akiwa kwenye picha ya pamoja na Wanachama wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali Kuu na Afya (TUGHE) Tawi la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA).
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akikata utepe kuashiria Uzinduzi wa Jengo la Ofisi ya Taasisi ya Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) lililopo eneo la Njedengwa mkoani Dodoma. Tarehe 25 Aprili 2024.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akipokea zawadi kutoka kwa Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Nape Nnauye mara baada ya hafla ya Uzinduzi wa Jengo la Ofisi ya Taasisi ya Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) lililopo eneo la Njedengwa mkoani Dodoma. Tarehe 25 Aprili 2024.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akiwa na Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Nape Nnauye, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamule,Mtendaji Mkuu wa UCSAF Justina Mashiba na viongozi mbalimbali katika picha ya pamoja watumishi wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) mara baada ya kuzindua jengo la Taasisi hiyo lililopo eneo la Njedengwa mkoani Dodoma. Tarehe 25 Aprili 2024.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akihutubia wakati wa Uzinduzi wa Jengo la Ofisi ya Taasisi ya Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) lililopo eneo la Njedengwa mkoani Dodoma. Tarehe 25 Aprili 2024.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akiweka jiwe la msingi la Uzinduzi wa Jengo la Ofisi ya Taasisi ya Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) lililopo eneo la Njedengwa mkoani Dodoma. Tarehe 25 Aprili 2024.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akisikiliza maelezo kutoka kwa Msanifu Majengo Arch. Msuya Abdulkarim kuhusu Jengo la Ofisi ya Taasisi ya Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) wakati alipowasili kwaajili ya kuzindua jengo hilo lililopo eneo la Njedengwa mkoani Dodoma. Tarehe 25 Aprili 2024.

MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango ametoa maagizo kwa Taasisi ya Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) kuendelea kusimamia kwa karibu ujenzi wa minara ya mawasiliano na kuhakikisha vijiji ambavyo havina huduma za uhakika za mawasiliano ya simu vinapata mawasiliano.


Makamu wa Rais ametoa maagizo hayo wakati wa uzinduzi wa Jengo la Makao Makuu ya Ofisi ya Taasisi ya Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) lililopo eneo la Njedengwa mkoani Dodoma. Amesema ni muhimu kuhakikisha Wananchi wanapata mawasiliano ya uhakika wakati wote ili waweze kushiriki kikamilifu katika shughuli za kijamii na kiuchumi hususan katika kipindi hiki ambapo huduma nyingi zinawezeshwa na huduma za mawasiliano.


Aidha Makamu wa Rais ameitaka UCSAF kuendelea kutekeleza miradi ya kuongeza uwezo wa minara kutoka teknolojia ya 2G kwenda 3G na 4G. Amesema huduma nyingi za jamii hivi sasa zinawezeshwa kwa kutumia intaneti ni muhimu kuhakikisha kila mwananchi anapata huduma hiyo mijini na vijijini.


Vilevile Makamu wa Rais ameiagiza UCSAF kujipanga kuongeza misaada ya vifaa vya TEHAMA hususan kwenye shule za umma ili kuongeza hamasa kwa wanafunzi kupenda masomo ya TEHAMA na kukuza matumizi ya intaneti nchini. Ametoa wito kwa sekta binafsi na sekta ya umma kushirikiana na UCSAF kuongeza idadi ya shule zinazopokea huduma hiyo na vifaa vya TEHAMA ili kuwezesha watoto kujifunza kwa urahisi.


Halikadhalika ametoa wito kwa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari kushirikiana na wadau ikiwemo sekta binafsi kuona uwezekano wa kuiongezea UCSAF uwezo, ikiwemo fedha na rasilimali nyingine ili kuiwezesha kufikisha huduma za mawasiliano katika maeneo yasiyo na huduma ya televisheni na redio za hapa nchini. Amesema ni vema UCSAF iangalie uwezekano wa kuwezesha matangazo ya televisheni na redio kuwafikia wananchi kwa njia ya mtandao.


Kwa upande wake Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Nape Nnauye amesema kupitia UCSAF asilimia 98 ya wananchi waliopo katika maeneo ya vijijini na maeneo ya mjini yasio na mvuto wa kibiashara wamenufaika na huduma za mawasiliano. Ameongeza kwamba wananchi wanaoishi maeneo ya vijijini wamepata fursa ya kushiriki katika mageuzi ya kidijiti nchini kwa kuwa sehemu ya watumiaji wa huduma za fedha kwa njia ya mtandao.


Aidha Waziri Nape amesema sekta ya mawasiliano imeendelea kukua kwa kasi hapa nchini ambapo kufikia mwaka 2024 jumla ya laini za simu milioni 72 zimesajiliwa kulinganisha na laini za simu milioni 51 mwaka 2020. Pia amesema zaidi ya minara 600 hapa nchini inatumia huduma ya 5G.


Amesema kwa sasa ni muhimu kufanya uwekezaji wa namna ya kutengeneza vifaa vinavyotumia mtandao ikiwemo simu janja hapa nchini ili uwekezaji unaofanywa na serikali katika kuboresha mawasiliano kuendelea kuwa na tija.


Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Dkt. Mngereza Mzee Miraji amesema kupitia UCSAF kwa kipindi kifupi jumla ya minara 47 imejengwa Zanzibar pamoja na ujenzi wa vituo 11 vya tehama Unguja na Pemba ambavyo imekua vikisaidia vijana kwa kiasi kikubwa.


Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) ni Taasisi ya Serikali ambayo ina jukumu la kuhakikisha mawasiliano yanafikishwa katika maeneo ya vijijini na mjini yasio na mvuto wa kibishara. Mfuko huo hushirikiana na watoa huduma za mawasiliano katika kujenga minara inayowezesha upatikanaji wa mawasiliano ya simu pamoja na uimarishaji wa matangazo ya redio na televisheni.


Uzinduzi wa Jengo hilo ni shamrashamra kuelekea Miaka 60 ya Muungano.

Imetolewa na

Ofisi ya Makamu wa Rais

25 Aprili 2024

Dodoma.
Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Tanga Victor Swella akizungumza na waandshi wa habari ambao hawapo pichani wakati akitoa taarifa ya utendaji kazi kwa kipindi cha Januari hadi Machi 2024 ambapo alisema kwamba moja ya kazi walioifanya ni ufuatiliaji wa ufanisi katika utekelezaji mkakati wa utoaji wa mikopo ya asilimia 10 kwa vijana,wanawake na watu wenye ulemavu.

Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Tanga Victor Swella akizungumza na waandshi wa habari ambao hawapo pichani wakati akitoa taarifa ya utendaji kazi kwa kipindi cha Januari hadi Machi 2024 ambapo alisema kwamba moja ya kazi walioifanya ni ufuatiliaji wa ufanisi katika utekelezaji mkakati wa utoaji wa mikopo ya asilimia 10 kwa vijana,wanawake na watu wenye ulemavu.

Na Oscar Assenga,TANGA.
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Takukuru Mkoani Tanga imefanikisha marejesho ya kiasi cha Sh. Milioni 439,279,300.00 kutoka kwa wanufaika wa mikopo asilimia 10 katika Halmashauri ya Jiji la Tanga.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Tanga Victor Swella wakati akitoa taarifa ya utendaji kazi kwaa kipindi cha Januari hadi Machi 2024 ambapo alisema kwamba moja ya kazi walioifanya ni ufuatiliaji wa ufanisi katika utekelezaji mkakati wa utoaji wa mikopo ya asilimia 10 kwa vijana,wanawake na watu wenye ulemavu.

Alisema kwamba miongoni mwa changamoto waliozozibaini katika ufuatiliaji huo ni kutokuzingatiwa kwa masharti ya urejeshaji mikopo hiyo kwa wakati kutoka kwa wanufaika ambapo kabla ufuatiliaji kufanyika kiasi cha Bilioni 2,152,229,900 zilikuwa hazijarejeshwa kutoka kwa wanufaika wa mikopo hiyo na muda wa marejesho ulikuwa umeshapita.

Aidha alisema baada ya kulibaini hilo taasisi hiyo iliwakutanisha wadau na kuweka mapendekezo ya kurejesha fedha hizo na hadi kufikia mwezi Februari 2024 Jumla ya Sh.Milioni 439,279,300.00 zilikuwa zimerejeshwa katika Halmashauri ya Jiji la Tanga na kufanya fedha ambazo hazijarejeshwa kuwa ni Bilioni 1,712,950,600.00 huku jitihada za ufuatiliaji zinaendelea.

Mkuu huyo wa Takukuru alisema pia katika kipindi hicho walifanikiwa kufanya ufuatiliaji wa utekelezaji wa miradi ya maendeleo 46 yenye thamani ya Bilioni 8,041,998,680.00 katika sekta za kipaumbele kama vile elimu,barabara ,maji na afya.

Alisema katika ufuatiliaji huo walibaini miradi 32 yenye thamani ya Bilioni 4,866,068,966.00 kuwa na mapungufu na ushauri ulitolewa wa kurekebisha mapungufu hayo kupitia vikao na wadau husika pamoja na kuanzisha uchunguzi wa miradi ambayo walibaini uwepo wa tuhuma za vitendo vya rushwa.

“Miongoni mwa miradi tunayoichunguza katika Halmashauri ya wilaya ya Korogwe ni manunuzi ya Sh. Milioni 6,400,000 ya uwekaji milango kwenye mradi wa ujenzi wa nyumba za wakuu wa idara wenye thamani ya Milioni 245 lakini pia ujenzi wa madarasa mawili ,matundu 18 ya vyoo na mfumo wa uvunaji wa maji ya mvua wenye thamani ya Milioni 70,000,000 na uchunguzi unaofanyika ni wa ubadhirifu wa Sh.Milioni 30,000,000.00 kwenye ujenzi wa matundu hayo ya vyoo na mfumo wa uvunaji wa maji ya mvua.
Naibu Katibu Mkuu wa Usimamizi wa Uchumi, Wizara ya Fedha Bw. Elijah Mwamdumbya na Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Masuala ya Kodi Kimataifa wa Wizara ya Fedha ya Czech aliyeongoza ujumbe wa Czech Bw. Václav Zíka, wakisaini nyaraka za kukamilisha majadiliano, katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania jijini Dar es Salaam.
Naibu Katibu Mkuu wa Usimamizi wa Uchumi, Wizara ya Fedha Bw. Elijah Mwamdumbya na Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Masuala ya Kodi Kimataifa wa Wizara ya Fedha ya Czech aliyeongoza ujumbe wa Czech Bw. Václav Zíka, wakibadilishana nyaraka za kukamilisha majadiliano, katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania jijini Dar es Salaam.
Naibu Katibu Mkuu wa Usimamizi wa Uchumi, Wizara ya Fedha Bw. Elijah Mwamdumbya na Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Masuala ya Kodi Kimataifa wa Wizara ya Fedha ya Czech aliyeongoza ujumbe wa Czech Bw. Václav Zíka, wakionesha nyaraka za kukamilisha majadiliano, katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania jijini Dar es Salaam.
Naibu Katibu Mkuu wa Usimamizi wa Uchumi, Wizara ya Fedha Bw. Elijah Mwamdumbya na Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Masuala ya Kodi Kimataifa wa Wizara ya Fedha ya Czech aliyeongoza ujumbe wa Czech Bw. Václav Zíka, wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kukamilika kwa majadiliano ya kuondoa vikwazo vya kikodi katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania, jijini Dar es Salaam.
(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Fedha)

Na. Saidina Msangi, WF, Dar es Salaam
SERIKALI ya Tanzania na Serikali ya Jamhuri ya Czech zimekamilisha majadiliano ya Mkataba wa Kuondoa Utozaji Kodi Mara Mbili yatakayowezesha wawekezaji na wafanyabiashara watakaofanya shughuli zao kati ya nchi hizi mbili kutozwa kodi katika mapato yao katika nchi moja badala ya kila nchi kutoza kodi ya mapato.

Majadiliano hayo ambayo yamefanyika katika duru ya tatu yalikutanisha pande hizo mbili Tanzania ikiongozwa na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Bw. Elijah Mwandumbya na Serikali ya Czech ikiongozwa na Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Masuala ya Kodi Kimataifa wa Wizara ya Fedha ya Czech, Bw. Václav Zíka, katika ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), jijini Dar es Salaam.

Akizungumza katika kikao hicho Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Bw. Elijah Mwandumbya ambaye aliongoza ujumbe wa Tanzania katika majadiliano hayo, amesema kuwa hatua hiyo itavutia mzunguko wa biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na Czech na kufungua fursa mpya za kiuchumi.

‘‘Mkataba huo utakaposainiwa utawezesha wawekezaji na wafanyabiashara watakaofanya shughuli zao kati ya nchi hizi mbili kutozwa kodi katika mapato yao katika nchi moja badala ya kila nchi kutoza kodi mapato ya aina moja na kusababisha changamoto ya utozaji kodi mara mbili (Double Taxation)’’, alifafanua Bw. Mwandumbya.

Naye kiongozi wa ujumbe wa Czech, Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Masuala ya Kodi Kimataifa wa Wizara ya Fedha ya Czech Bw. Václav Zíka, alieleza kuwa Serikali ya Czech inatambua umuhimu wa Mkataba huo katika kuibua fursa za ajira, biashara na uwekezaji ambazo zitakuwa endelevu kutokana na kuweka mazingira ya kisera yanayotabirika.

Pamoja na hayo, amefafanua kuwa Mkataba huo utakaposainiwa unatarajiwa kuongeza ufanisi wa ukusanyaji wa mapato kwa nchi hizo mbili kupitia upatikanaji wa taarifa za kikodi na utatuzi wa migogoro ya kikodi.

Kufuatia kukamilika kwa majadiliano hayo, kwa sasa inasubiriwa kukamilika kwa taratibu za ndani za kisheria kwa kila nchi kuwezesha Mkataba huo kusainiwa na hatimaye kuridhiwa ili kuanza kutekelezwa.
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka wamiliki wa shule na madereva wa mabasi yanayotoa huduma za usafiri kwa wanafunzi wajiridhishe kuhusu njia wanazopita ili kuhakikisha kunakuwepo na usalama wa wanafunzi wanaowabeba katika vyombo vya usafiri.

“Wazazi, Walezi na Jamii ya Watanzania kwa ujumla tushiriki kikamilifu katika kuhakikisha usalama wa wanafunzi wanapokwenda na kurudi Shuleni wakati wote hususan katika kipindi cha mvua.”


Kadhalika amesema kwa kuwa Serikali imetoa maelekezo ya kufunga shule zilizoathiriwa na mafuriko, halmashauri na wamiliki wa shule zisizo za Serikali waweke utaratibu wa kufidia muda wa vipindi ili kukamilisha kalenda ya muhula kama ilivyopangwa.

Ametoa wito huo leo (Alhamisi, Aprili 25, 2024) wakati akitoa taarifa ya serikali kuhusu changamoto za hali ya hewa bungeni jijini Dodoma.

Pia, amezitaka Taasisi za Serikali ziendelee, kukabiliana na maafa kwa kushirikiana na wadau kutekeleza majukumu yaliyoanishwa katika Mpango wa Kujiandaa na Kukabiliana na Madhara ya El-Nino pamoja na mipango ya kisekta ili kuzuia na kupunguza athari zinazoweza kujitokeza.

“Kamati za Maafa za Wilaya na Mikoa ziendelee kuchukua hatua stahiki ikiwemo kutoa tahadhari kwa wananchi na kusaidia wananchi kwa wakati pindi maafa yanapojitokeza.”

Aidha, amewataka Wakuu wa mikoa na wilaya, maafisa tarafa, watendaji kata, mitaa na vijiji wasimamie ipasavyo usafi katika maeneo yao na kudhibiti utupaji taka ovyo unaosababisha kuziba kwa mitaro badala ya kusubiri usafi unaofanyika kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi.

“Kwa kuwa uharibifu wa mazingira umekuwa na athari kubwa kutokana na mabadiliko ya tabianchi, viongozi wa ngazi zote washirikiane na wananchi kudhibiti uharibifu wa mazingira katika maeneo yao.”

Mheshimiwa Majaliwa pia amelitaka Jeshi la Polisi kupitia Kikosi cha Usalama Barabarani liendelee kutoa tahadhari kwa madereva na watumiaji wengine wa barabara wakati wa mvua;

“Kamati za Maafa katika ngazi za Vijiji, Wilaya na Mikoa zisimamie kikamilifu ugawaji wa misaada inayotolewa kwa waathirika wa mafuriko na kuhakikisha kuwa misaada inawafikia walengwa”.

Kadhalika amewataka Viongozi wa Serikali kuanzia ngazi ya Vijiji wahamasishe na kuelimisha wananchi wanaoishi mabondeni kuhamia maeneo salama ili kuepusha maafa wakati wa mafuriko na kuhakikisha wanatenga maeneo salama yatakayotumika na wananchi watakaohamia kutoka mabondeni.

Katika hatua nyingine Mheshimiwa Majaliwa amesema kutokana na maafa yaliyotokea nchini, Serikali kupitia Kamati za Usimamizi wa Maafa na wadau imechukua hatua mbalimbali kwa ajili ya kuzuia, kukabiliana na kurejesha hali.

“Hatua hizo zinajumuisha utoaji wa elimu kwa jamii ya kujikinga na kuchukua tahadhari, kukabiliana na maafa na kurejesha miundombinu iliyoharibika. Aidha, Serikali imetoa misaada ya kibinadamu ikiwemo chakula, vifaa vya ujenzi, vifaa vya malazi na vifaa vya usafi.”

Amesema, hatua mbalimbali zimeendelea kuchukuliwa na misaada kutoka Serikalini na wadau kama vile uokoaji, vyakula, mahema, madawa, marekebisho ya miundombinu ya utoaji huduma imeendelea kutolewa.

“Serikali imejipanga kikamilifu na inaendelea kuchukua hatua stahiki ili kuzuia na kupunguza makali ya majanga sambamba na kurejesha hali katika maeneo mbalimbali yaliyoathirika.”

Mheshimiwa Majaliwa amesema Serikali ya Awamu ya Sita imefanya uwekezaji mkubwa katika sekta ya hali ya hewa nchini ikiwemo kufunga miundombinu ya kisasa ya hali hewa, mafunzo kwa watumishi kwa kuzingatia vigezo vya kitaifa na kimataifa, na kuweka mifumo wezeshi ya usambazaji wa taarifa ya hali ya hewa pamoja na kuimarisha mifumo ya uhakiki wa ubora wa huduma.

Amesema uwekezaji wa miundombinu uliofanyika unajumuisha ununuzi wa Rada za Hali ya hewa ambapo Rada mbili zinakamilishwa kufungwa katika mikoa ya Kigoma na Mbeya. Vilevile, Rada nyingine mbili zinatarajiwa kufungwa Mikoa ya Dodoma na Kilimanjaro ifikapo mwishoni mwa mwaka 2024.

“Nitumie fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa uwekezaji mkubwa alioufanya katika sekta ya hali ya hewa na kuijengea uwezo nchi yetu na kuifanya kuwa kinara Afrika na nje ya Afrika katika masuala ya utabiri wa hali ya hewa.”
Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Frank Nyabundege na Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Tanzania Dinesh Balsingh wakibadilishana mkataba wa kuendeleza sekta ya kilimo na kuwa ya Kidijitali.
Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Frank Nyabundege na Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Tanzania Dinesh Balsingh wakisaini Mkataba wa kuendeleza sekta ya kilimo na kuwa ya Kidijitali.

AIRTEL TANZANIA imeingia makubalino na Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) kwa kusaini makubaliano (MoU) ya miaka mitatu ikiwa na lengo la kuinua na kuleta maendeleo katika sekta ya kilimo kwa njia ya mtandao yaani kidijitali.

Makubaliano ya ushirikiano huu kati ya Airtel Tanzania na TADB yanadhamira ya kufanikisha kupanua ushirikiano wa sekta ya kifedha kwa wadau mbalimbali ndani ya sekta kilimo, wakiwemo wakulima, wajasiriamali wadogo vijijini, hasa wanawake na vijana. Ushirikiano wa Airtel na TADB ni moja kati ya juhudi za Airtel Tanzania kuunga mkono serikali katika kuleta matokeo chanya katika maisha ya Watanzania.

Akizungumza wakati wa hafla ya kuweka saini makubaliano hayo Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Tanzania Dinesh Balsingh, alisema “Airtel kwa kushirikiana na TADB tunadhamira ya dhati ya kusaidia Watanzania kupitia ubunifu katika sekta ya mawasiliano. Hii ni kwakuwa tunaamini wakulima wanastahili kuwa miongoni mwa vikundi vinatakiwa kunufaika na ukuaji wa teknolojia nchini. Hivyo, Ushirikiano wetu na TADB unalenga katika kutatua changamoto zinazowakabili wakulima kwa kutumia bidhaa mbalimbali za kidijitali ambazo zitaibua masoko mapya kwa wakulima mijini na vijijini. Bidhaa hizo zitawezesha uzalishaji wa wakulima na kuongeza mapato yao”.

Balsingh alieleza kuwa ushirikiano wa Airtel na TADB unaungana moja kwa moja na maono ya Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan ya ukuaji wa sekta ya kilimo kwa asilimia 10 ifikapo mwaka 2030. (Chanzo World Economic Forum). " Na hii inaonesha jinsi kilimo kilivyo muhimu katika kuchangia ukuaji wa uchumi wa nchi kwa kuwa zaidi ya asilimia 70 ya watu wamejiajiri katika sekta ya Kilimo.".

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Frank Nyabundege alitoa shukrani zake kwa Airtel Tanzania akisema, ushirikiano wa Airtel na TADB utafungua milango ya fursa katika sekta ya kilimo. Ushirikiano huu utatoa fursa kwa wakulima kujipatia masuluhisho kwenye mahitaji na changamoto wanazokutana nazo katika shughuli zao za kila siku.

“Ubia wa Airtel na TADB unalenga kukuza ukuaji sekta ya kilimo. Ushirikiano huu ni mwanzo wa mabadiliko makubwa yatakayowagusa wakulima wote nchini Tanzania,” alisema Bw. Frank Nyabundege – Mkurugenzi Mkuu wa TADB.

Ushirikiano huu wa Airtel na TADB unakwenda sambamba pia na mikakati ya serikali ya kuunga mkono juhudi za wadau wa kilimo kwa kupambaa na changamoto mbalimbali ndani ya sekta ya kilimo kwa kuwawezesha wakulima kifedha kama ilivyotajwa na Rais wetu Dkt Samia Suluhu Hassan wakati wa mkutano wa wadau wa COP28 uliofanyika Disemba 4, 2023. Alisema, “tunatakiwa kubadilika na kufanya kilimo endelevu kwa kuunga mkono ubunifu mbalimbali unaoendana na hali ya sasa.”

Exim Bank, kupitia Mpango wake wa Kuwawezesha Kiuchumi Wanawake (WEP), imetoa mafunzo kuhusu masuala ya ujasiriamali, biashara, na uwezeshaji kwa wanawake wajasiriamali kama sehemu ya kuunga mkono ujumuishwaji wa watu wote, wakiwemo  wanawake, katika mipango mbalimbali ya maendeleo nchini Tanzania. 

Kupitia mpango wake wa ‘Exim Cares’, mwaka jana (2023) Exim Bank ilizindua Mpango wa Kuwakwamua Kiuchumi Wanawake ujulikanao ‘Women Empowerment Program (WEP)‘ wenye lengo la kuongeza ushirikishwaji na kuleta usawa kwa wanawake barani Afrika, hasa katika nchi ambazo zina matawi ya benki hiyo ikiwemo Tanzania, Comoros, Djibouti na Uganda. 

Akizungumza katika mahafali hayo, Mkuu wa Kitengo cha Masoko wa Exim Bank, Stanley Kafu, anasema, “Ukiwa mwaka wa pili mfululizo wa mpango wa Kuwakwamua Wanawake Kiuchumi (WEP), Exim Bank tunafuraha kubwa kuwa sehemu ya mafanikio haya na tunawapongeza washiriki wote kwa kuanza na kumaliza salama mafunzo haya kuhusu ujasiriamali, uwezeshaji, na biashara.”  

Washindi watatu, wa awamu hii ya kwanza mwaka huu, walipata zawadi za pesa taslimu zilitolewa kwa washindi watatu ambapo mshindi wa kwanza, Beatrice A. Msafiri, akizawadiwa kiasi cha TZS 8,000,000, mshindi wa pili, Catherine Assenga akipata TZS 5,000,000 na mshindi wa tatu, Rukia S. Mohamed akiondoka na TZS 3,000,000. Pia, wahitimu wote walipata fursa ya kuweza kupata mikopo bila riba kutoka Exim Bank ili waweze kujiendeleza kiuchumi. 

Exim Bank inaamini uwezeshaji wa wanawake na ujasiriamali unabaki kuwa sehemu muhimu ya mipango ya maendeleo nchini Tanzania na barani Afrika kijumla. Hii inadhihirishwa na ongezeko la idadi ya wanawake katika nafasi za uongozi katika sekta mbalimbali kama siasa, kijamii na kiuchumi. 

Akielezea kuhusu malengo ya mradi, Kafu alisema, “Mpango huu utakuwa ni endelevu kwa muda wa miaka mitano na tunatarajia kuwafikia wanawake zaidi ya 600,000 ifikapo mwaka 2028.” 

Kafu anasisitiza kuwa Mpango wa WEP ni sehemu ya mkakati mkubwa na wa kina unaolenga kutengeneza jukwaa la wanawake ili waweze kufanikiwa na kustawi katika maisha yao, hasa kwenye eneo la uchumi. 

Exim Bank imekuwa na itaendelea kuunga mkono juhudi za serikali katika kuleta maendeleo kwa Watanzania wote. Programu hii inawiana na Dira ya Maendeleo ya Tanzania 2025 na Dira ya Maendeleo ya Zanzibar 2050 na itakuwa chachu katika kuimarisha ustawi wa kijamii na kiuchumi kwa wanawake.

Mshindi wa tatu Rukia Said Mohamed (wa pili kulia), Zainab Nungu  Mkuu wa Kitengo cha Mikopo, Exim Bank (wa kwanza kushoto), na Faraja Nyalandu, Mkurugenzi Mtendaji wa Ndoto Hub (wa kwanza kulia) wakifurahi pamoja na Mkuu wa Kitengo cha Masoko wa Exim Bank, Stanley Kafu wakati wa mahafali ya mafunzo ya ujasiriamali, biashara na uwezeshaji kwa wanawake wajasiriamali chini ya mradi wa benki hiyo yajulikanayo kama WEP katika tukio lililofanyika tarehe 23 Aprili 2024 mjini Arusha

Mshindi wa pili Catherine Assenga (wa pili kulia), Zainab Nungu  Mkuu wa Kitengo cha Mikopo, Exim Bank (wa kwanza kushoto), na Faraja Nyalandu Mkurugenzi Mtendaji wa Ndoto Hub (kulia) wakifurahi pamoja na Mkuu wa Kitengo cha Masoko wa Exim Bank, Stanley Kafu wakati wa mahafali ya mafunzo ya ujasiriamali, biashara na uwezeshaji kwa wanawake wajasiriamali chini ya mradi wa benki hiyo yajulikanayo kama WEP katika tukio lililofanyika tarehe 23 Aprili 2024 mjini Arusha

 Stanley Kafu, Mkuu wa Kitengo cha Masoko wa Exim Bank, akizungumza wakati wa mahafali ya pili ya mpango endelevu wa kuwainua kiuchumi wanawake wajasiriamali ujulikanao kama WEP yaliyofanyika tarehe 23 Aprili, 2024, Mjini Arusha

Mshindi wa kwanza Beatrice Alban Msafiri (wa pili kulia), Zainab Nungu  Mkuu wa Kitengo cha Mikopo, Exim Bank (wa kwanza kushoto), na Faraja Nyalandu, Mkurugenzi Mtendaji wa Ndoto Hub (wa kwanza kulia) wakifurahi pamoja na Mkuu wa Kitengo cha Masoko wa Exim Bank, Stanley Kafu wakati wa mahafali ya mafunzo ya ujasiriamali, biashara na uwezeshaji kwa wanawake wajasiriamali chini ya mradi wa benki hiyo yajulikanayo kama WEP katika tukio lililofanyika tarehe 23 Aprili 2024 mjini Arusha

Washindi na baadhi ya washiriki wakiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Exim Bank wakati wa mahafali ya kumaliza mafunzo ya biashara, ujasiriamali, na uwezeshaji kwa wanawake wajasiriamali. Mafunzo hayo yalitolewa na Exim Bank chini ya mpango wake wa Kuwainua Kiuchumi Wanawake (WEP) na mahafali hayo yamefanyika tarehe 23 Aprili, 2024 mjini Arusha

Benki ya Stanbic Tanzania, ambayo ni kiungo muhimu katika sekta ya huduma za kibenki nchini Tanzania, na Ramani, kampuni namba moja kwenye teknolojia ya kifedha, wanafurahi kutangaza ushirikiano uliolenga kuleta mabadiliko kwenye sekta ya biashara, nakuendeleza upatikanaji wa huduma za kifedha nchini  kwa ufanisi zaidi. 

Ushirikiano huu wa kipekee unalenga kutumia teknolojia na msaada mkubwa wa kifedha, kuimarisha uwezo wa biashara za wasambazaji wa ndani na wajasiriamali.

Muunganiko huu unalenga kutumia miundombinu yakifedha ya kisasa ya Kampani ya Ramani, pamoja na rasilimali imara za kifedha za Benki ya Stanbic.

Pia, utasaidia zaidi ya wasambazaji 100 katika mwaka wake wa kwanza, ukiangazia mnyororo muhimu wa thamani katika sekta ya Bidhaa za Watumiaji (FMCG). 

Pamoja na majukwaa ya teknolojia ya hali ya juu na mikakati ya kifedha, ushirikiano huu utakabiliana na vipengele muhimu vya usimamizi wa biashara, ufuatiliaji wa mauzo, na miamala ya kidijitali ili kuongeza ufanisi wa uendeshaji kwa wasambazaji.

Fredrick Max, Mkuu wa Kitengo cha Biashara wa Benkiya Stanbic Tanzania, alisema, "Ushirikiano wetu na Ramani ni zaidi ya biashara; ni ushirikiano wa kimkakati ambao unaahidi kubadilisha jinsi biashara inavyofanywa nchini Tanzania. 

Kwa kuunganisha nguvu zetu na maono yetu, tunapanga kusaidia mahitaji ya kifedha ya wasambazaji wa ndani, na pia kuchangia kwa kiasiki kubwa katika ukuaji wa uchumi wa taifa letu."

Lengo kuu ni kutoa fedha kwa wasambazaji na wauzaji ili kuboresha usimamizi wa ugavi kwa wasambazaji na wafanyabiashara wa bidhaa kubwa. 

Hii itawezesha usimamizi bora wa manunuzi, udhibiti wahisa na ufuatiliaji wa mauzo ya kidijitali katika kuimarisha michakato ya biashara na miamala yakifedha.

Iain Usiri, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampani ya Ramani, alisema, "Tunafurahi kushirikiana na Benki ya Stanbic Tanzania. Ushirikiano huu utarahisisha na kuimarisha usimamizi wa wasifu wa mikopo na kukuza huduma za kifedha.  Tunable mabadiliko chanya katika kuendesha biashara, na kuboresha upatikanaji wa huduma za kifedha."


Mafanikio ya ushirikiano huu yatapimwa nauandikishwaji wa wafanyabiashara 100 katika mwaka wakwanza, na mipango ya kukuza ufikiaji kwa kiasikikubwa, ili kufikia biashara zaidi nchini Tanzania.

Takwimu za mitandao ya kijamii, ukuaji wa kifedha, naviwango vya kuandikisha wateja, zitatumika kamaviashiria muhimu vya mafanikio na ufanisi wamuunganiko huu.

Ushirikiano kati ya Benki ya Stanbic Tanzania na Ramani, unatengeneza kiwango kipya cha ushirikiano katika sekta ya kifedha na teknolojia, huku ukionyeshamatumaini makubwa katika kuboresha jinsi biasharainavyofanywa na kusaidiwa kifedha nchini Tanzania.

Kupitia hatua hii, mashirika yote mawili yanathibitishatena azma yao ya kuchochea ukuaji wa kiuchumi, nakuboresha upatikanaji wa huduma za kifedha kwaWatanzania wote.


Na. Josephine Majura, WF, Dodoma

Serikali imesema kuwa inaandaa mfumo wa kielektroniki wa kutoa ankara ya pamoja kwa huduma zinazolandana ili kuondoa usumbufu kwa wananchi wanaostahili kulipa kodi ya jengo na kodi ya ardhi.

Hayo yameelezwa bungeni, jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb), alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum,  Mheshimiwa Fakharia Shomar Khamis, aliyetaka kufahamu mpango wa Serikali wa kuziunganisha kodi ya jengo na kodi ya ardhi.

“Serikali kupitia Kamati ya Moberesho ya Mfumo wa Kodi inaendelea kufanya uchambuzi na tathmini ya mifumo ya kodi, ada na tozo za huduma kwa lengo la kuondoa urasimu na kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji nchini”, alisema Mhe. Chande.

Alisema tathmini hiyo inajumuisha mapendekezo ya maboresho ya mfumo wa usimamizi wa kodi ya jengo na kodi ya ardhi kama inavyopendekezwa na Mheshimiwa Khamis. 

Aidha katika swali la nyongeza lililoulizwa na Mbunge wa Mwera Mhe. Zahor Mohamed Haji, alitaka kujua mpango wa Serikali wa utoaji elimu kwenye mifumo inayoanzishwa. 

Mhe Chande alisema kuwa Serikali kupitia Taasisi zake imekuwa na utaratibu wa kutoa elimu siku hadi siku kwa wadau wake kulingana na uhitaji katika kipindi hicho.

Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb) akijibu swali bungeni jijini Dodoma la Mbunge wa Viti Maalum, Mheshimiwa Fakharia Shomar Khamis, aliyetaka kufahamu mpango wa Serikali wa kuziunganisha kodi ya jengo na kodi ya ardhi.



SERIKALI kupitia Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) imesema kuwa ina lengo la kuboresha maisha ya wananchi wa tarafa hiyo kwa kuwaelimisha na kuwahamisha wananchi waliojiandikisha kuhama kwa hiyari kwenda Kijiji cha Msomera Handeni Mkoani Tanga na maeneo mengine nchini.

Akizungumza na wananchi wa tarafa ya Ngorongoro kwa nyakati tofauti katika zoezi la uelimishaji, uhamaishaji na uandikishaji kaimu meneja wa Uhusiano kwa Umma wa mamlaka hiyo Hamis Dambaya amesema zoezi la kuwaelimisha wananchi hao litaendelea ili kuhakikisha kila mkazi wa tarafa ya Ngorongoro anahama kwa hiyari.

Amewaeleza wananchi hao kwamba serikali haina nia mbaya kwa kuwashawishi kuhama kutoka ndani ya hifadhi kwani inatambua kuwa iwapo wananchi hao watakubali kuhama wataweza kuboresha maisha yao katika maeneo mbalimbali watakayoamua kuelekea sambamba na kulinda usalama wao kutokana na uwepo wa matukio ya wanyama wakali ndani ya hifadhi.

“Mnaishi katika mazingira magumu hasa kutokana na kukosa uhuru wa kuingia na kutoka ndani ya hifadhi, kuhofia Wanyama wakali ambao wamekuwa hatari kwa mifugo na baadhi ya wananchi, serikali imefanya uamuzi sahihi wa kuwahamasisha ili kuwa na Maisha bora na huru nje ya hifadhi,”alisema bwana Dambaya.

Bwana Dambaya amesisitiza kuwa serikali imejipanga vizuri katika kuhakikisha kila mwananchi anayekubali kuhama kwa hiyari kutoka ndani ya hifadhi anapata stahiki zake zote za kisheria ikiwemo kitita cha shilingi milioni kumi wanaohamia msomera na shilingi Milioni kumi na tano wanaohamia maeneo mengine ambapo fedha hizi zinatolewa kama motisha na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan.

Amewataka wananchi hao kuachana na propaganda za baadhi ya wanasiasa na wanaharakati wasiowatakia mema kwa kuwashawishi kuendelea kubaki ndani ya hifadhi huku wao na familia zao wakiishi katika miji mbalimbali nchini na kufanya shughuli zao katika mazingira magumu.

“Msihadaike na watu wenye nia ovu wanaowashawishi mbaki ndani ya hifadhi, hameni kwa hiyari kuelekea katika Kijiji cha Msomera na maeneo mengine ambayo huduma za kijamii zimeboreshwa kwa mustakabali wenu na vizazi vyenu”,alisema bwana Dambaya.

Katika ziara hiyo ya tarafa ya Ngorongoro timu ya uhamasishaji imeweza kutembelea kaya mbalimbali katika Kijiji cha Naiyobi, Kapenjiro na endulen ambapo wananchi kadhaa walielimishwa na kukubali kuhama kwa hiyari na kuamua kujiandikisha.
Na Nihifadhi Issa Zanzibar.
SHERIA ya Ofisi ya Mufti wa Zanzibar ya mwaka 2021 kwenye kipengele cha ufafanuzi imefafanua Ulamaa kuwa ni “ Mwanachuoni wa Kiislamu mwenye elimu ya kutosha ya fani mbalimbali ya dini ya kiislam na lugha ya kiarab”. Hapana hakuna sehemu iiyowekwa jinsia maana wanawake na wanaume wenye uwezo wa kielimu wapewe nafasi. Ila suala hili kwa baadhi ya dini ni jambo lisilopewa kipaombele.

Sheikh Khamis Shabaan Khamis ni Iman wa Msikiti pia ni Kiongozi wa dini anayepinga suala la wanaume kuona na kuzungumza kuwa wanawake hawana haki ya kuwa kwenye sehemu za maamuzi, amesema suala la kuharamisha na kuhalilisha suala lolote la kidini ni jambo ambalo linatakiwa litokane na Quran na Mafundisho ya Mtume Muhammad (S.W.A).”Kumzuia mwanamke asishiriki katika utowaji wa Fatwa au maamuzi, kumharimisha wanamke asishiriki katika harakati za kijamii au kutokuwa kadhi au kiongozi basi lazima awe na Ushahidi.” Sheikh Khamis amesema maana yake ni kwamba hakuna pingamizi ya wanamke kuwa kiongozi au kuwepo kwa masuala ya kusema hili halifai.

Dkt Mzuri Issa ni Mkurugenzi wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Zanzibar – TAMWA-Z amekuwa akizungumzia suala la usawa na ushirikishwaji wa wanawake kwenye vyombo vya maamuzi anasema .”Kikatiba wanawake wanahaki ya kuwa kwenye sehemu za maamuzi, ni ukweli usioficha kuwa wanawake wanakuwa huru kuzungumza na wanawake wenzao kuliko wanaume hususan kwenye matatizo kama hayo ambayo yanayowakumba zaidi wanawake “Dkt Mzuri anaendelea kusema kuwa kukosekana kwa wanawake kwenye sehemu za maamuzi inaweza kuwa wanawake hawaridhiki na maamuzi yanayotolewa “Ikiwa wanawake wanakosekana kwenye vyombo vya maamuzi ambavyo vinawajibika kwenye masuala haki basi hapo hakuna utekelezaji wa haki,wala usawa na inawavunja moyo sawa wanawake waliosomo kwenye kada hizo wakikosa nafasi za kushirikishwa au kupatiwa nafasi naweza kusema hawatendewi haki” Amemalizia Dkt Mzuri Issa.

Amina Salum Khalfan ni Mwanarakati wa Kiislam anapingana na mawazo ya viongozi wa dini wasioamini nafasi ya mwanamke kwenye masuala ya kijamii na upatikanaji wa haki. “Nikiletewa kesi nawaambia nendani ofisi ya Kadhi au ya Mufti wanawake wanakataa kwa sasa huwezi kuzungumza faragha zako za ndani zinamhusu mwanaume mbele ya wananaume wenzao ni aibu na sio jambo linakubalika kidini “Anaendelea kusema “Kuna madhara makubwa ikiwa wanawake hawatapata nafasi kwenye sehemu hizo maana dini haijasema hivyo, wanaona uzito kwenye suala hili maana waliowengi wameshikilia dini na kukosa maarifa ya hio dini lakini zaidi ni mitazamo yao” Amemalizia kusema Amina.

Mwaka 2019 kupitia Baraza la Wakilishi kulizuka mjadala mkubwa juu ya suala la wanawake kupatiwa nafasi kwenye sehemu za maamuzi huku baadhi ya wawakilishi wakipinga suala hilo kwa kunasabisha dini kukataza baadhi ya masuala ya wanawake kuwa hawafai kuwa kwenye baraza la Maulama .Novemba 27, 2019 kupitia kikao cha kwanza,Mkutano wa 16 wakati wa kuwasilisha Mswada wa Marekebisho ya Kuanzishwa Afisi ya Mufti Nam.9 ya Mwaka 2001 ambao kupitia kikao hicho wajumbe wa Baraza la Wakilishi walijadili kuhusu nafasi ya kuwepo wa maulamaa wanawake.

Akichangia muswada huo Rashid Makame Shamsi ambaye alikuwa Mwakilishi wa Jimbo la Magomeni alihoji juu ya kuwepo kwa wajumbe 16 wanaume katika baraza la Maulama “Sasa Wajumbe waliotajwa katika Baraza hilo ukipiga mahesabu ni wajumbe 16, sasa ndani ya Wajumbe 16 ni Masheikh, Shekhe mmoja mmoja kutoka kila wilaya na wilaya tuna 10. Sasa ukitizama sitarajii kwamba ndani ya hao Masheikh watakuwemo Masheikh wanawake sitarajii. Kwa sababu ulamaa ni mtu mwenye elimu ya juu katika uwanja wa dini kwa mujibu wa kamusi zote za kiswahili na watu wenye upeo wa dini ya kiislamu wanawake hivi sasa wako wengi sana na kazi kubwa sio kutoa fatwa ni kumshauri Mufti wa Zanzibar.Mimi sifikirii kabisa na nimefanya utafiti kwa Masheikh maulamaa na wasomi wa dini ya kiislam suala hili halina madhara kuwaingiza wanazuoni wanawake katika Baraza la Maulamaa la Zanzibar” Alimalizia Rashid Makame Shamsi – Mwakilishi wa Jimbo la Magomeni- Zanzibar.

Kupitia Hansad za Baraza la Wakilishi Zanzibar aliyekuwa Waziri wa Katiba na Sheria Khamis Juma Mwalimu akijibu hoja na wajumbe waliochgia mjadala huo aliunga mkono hoja ya kufanyika kwa marekebisho ya baadhi ya vifungu hivyo na wanawake wapate nafasi ya kuingia kwenye Baraza ma Ulamaa kupitia Afisi ya Mufti Mkuu wa Zanzibar “hili la uanzishwaji wa Baraza la Ulamaa, sisi binafsi ushauri huu ulitolewa awali kuona uwezekano pengine na akina mama waweze kuwemo katika Baraza hili.Lakini vile vile, tuangalie uwezekano kwamba kina mama wanaweza kwamba hapa wasiorodheshwe kwamba wawepo katika hii sheria na mimi naungana nao moja kwa moja kwamba ziwepo pengine nafasi mbili za kina mama za wanawake katika Baraza hili.” Alimalizia kuchangia hoja hio.

Jamila Mahmoud ni Mkurugenzi wa Chama Cha Wanasheria Wanawake Zanzibar – ZAFELA amesema suala la kuwepo kwa msisitizo wa kuchaguliwa na kupatiwa nafasi kwa Maulama wanawake halipo kisheria hivyo hio ni miongoni kwa sababu kubwa ya wanaotoa nafasi cha kuchagu kuona hili jambo sio lazima na halina umuhimu “ Kwa mfano Sheria ya Mahakama ya Kadhi yam waka 2003 Kifungu cha 10(4) “Sheri ya Ofisi ya Mufti wa Zanzibar yam waka 2021 kwenye kipengele cha ufafanuzi imefafanua Ulamaa kuwa ni “ Mwanachuoni wa Kiislamu mwenye elimu ya kutosha ya fani mbalimbali ya dini ya kiislam na lugha ya kiarab”. Hapana hakuna sehemu iiyowekwa jinsia maana wanawake na wanaume wenye uwezo wa kielimu wapewe nafasi.

Jamila ameongeza kuwa changamoto kubwa iliyopo kwenye suala la wanawake Maulama kutokuwepo kwenye ngazi za maamuzi ni kwa sababu wanaopata nafasi za kuwateuwa hao maulama bado wanaamini kwenye mifumo dume”. Amemalizia Jamila.

Ofisi ya Mufti Mkuu kutokuwateua wanawake kwenye baraza la Maulamana Sheikh Khalid Ali Mfaume ni Katibu Mtendaji Ofisi ya Mufti Mkuu Zanzibar amesema wao hawana jukumu la kuwapatia wanawake nafasi ila Serikali ndio inajukumu hilo na pia serikali inazingatia vigezo maalum vya kupewa ajira. “Wanawake wanamchango wao kwenye jamii ila bado suala la wanawake kuwa kwenye baraza la ulama ani suala ambalo linahitajika kufanyiwa kazi” Alimalizia Sheikh Khalid.


*MWENYEKITI Lee Man-hee -Jukumu langu ni kushuhudia matukio ya Ufunuo kama nilivyoyasikia na kuyaona."

*Ushuhuda juu ya ukweli uliotimizwa wa Ufunuo' ulielezea kimantiki na kwa utaratibu.

MWENYEKITI wa kanisa la Shincheonji, Lee Man-hee amesema ikiwa mtu anatamani mbingu na uzima wa milele, ni lazima waende hadi mwisho wa dunia ikiwa ni lazima ili kujua kama ni ukweli unaotimizwa kulingana na Biblia.

Hayo amesema Wakati wa Semina ya bibilia iliyofanyika Barani Asia katika nchi ya Uphilipino Aprili 20, 2024. mkutano huo ulikuwa na lengo la kuwajulisha wakristo wote kuhusu ukweli uliotimizwa kwenye kitabu cha Ufunuo.

Mwenyekiti Lee alisisitiza, "Imani sio kutafuta pesa," na "Sio wakati wa kuwa na imani na mawazo ya zamani. Mtu lazima athibitishe. Baada ya kuthibitisha, lazima aamue kuamini au la."

"Ni kazi ya mtu huyu kufikisha kile kilichoonekana na kusikika kutoka kwa matukio ya Ufunuo sura ya 1 hadi 22. Nilichokiona na kusikia, kile nilichogusa na kile kilichopo katika hali halisi, ndicho nilichokuja hapa kushiriki nanyi. Sasa sio wakati wa kusema chochote na kukubaliana tu na 'Amina'. Lazima uelewe nyakati za ukweli. Ni wakati ambao ahadi zimetimizwa."

Katika ukumbi wa mihadhara ya ndani huko Ufilipino, makofi yalijaza nafasi, ambayo ilionekana kukaa maelfu kwa mtazamo wa kwanza. Sauti yenye nguvu na hotuba ya ujasiri inayotokana na kimo kidogo, ambayo ilionekana kuwa haiwezekani kwa mtu zaidi ya miaka tisini, ilifanya maneno rahisi hata mtoto anaweza kuelewa. Katika muda mfupi, hali ilizidi kuwa kali. Mtu ambaye alifanya hivyo kutokea hakuwa mwingine isipokuwa Shincheonji Kanisa la Yesu, Hekalu la Hema ya Ushuhuda, Mwenyekiti Lee Man-hee.

Siku hiyo, Mwenyekiti Lee alizindua Semina za Biblia za Shincheonji za 2024 za Bara la Asia (I)' kwa kutembelea Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Ufilipino. Mfululizo wa hotuba utaendelea mwaka mzima huko Ulaya, Afrika, Amerika, Oceania, na kuhitimisha tena Asia (II). Kanisa la Shincheonji la Yesu liliandaa Semina hiyo ya Neno kutokana na majibu mengi na maombi ya dhati kutoka kwa wachungaji na waumini wengi ulimwenguni kote kufuatia 'Semina ya Neno la Ufunuo Shincheonji '.

Akiwa na ukumbi wa mihadhara ambao una viti 4,000 vilivyojaa watu, Mwenyekiti Lee alichukua hatua na kwanza akajitambulisha na kile kilichomfanya aamini. Ilitoa hisia sawa na jinsi waandishi wa kibiblia walivyoanza kuelezea ukoo wao na nyakati kabla ya maudhui kuu

Mwenyekiti Lee alisema kwa nguvu, "Sasa si wakati wa kusema chochote na kukubaliana tu na 'Amina,'" na "Lazima uelewe nyakati ya ukweli. Ni zama ambazo ahadi zimetimizwa." Alisisitiza, "Ufunuo unatia ndani mnyama mwenye vichwa saba na pembe kumi, na pia nyota saba. Ni juu ya kuelewa kile ambacho kuonekana kwa kweli kunawakilisha," na akasisitiza kwamba "wakati Mungu anaandika kuibuka kwa watu kama hao, ni ili leo utimizo utimie. kuona, kusikia, na kuamini."

Akirejelea Ufunuo 22:18-19, Mwenyekiti Lee alisisitiza mara kwa mara kwamba mtu hawezi kuingia mbinguni ikiwa wataongeza au kuondoa kutoka kwa Kitabu cha Ufunuo. Kwa kufanya hivyo, aliamsha hisia ya uharaka katika imani kwa kusema, "Mtu lazima ajue kila kitu bila kupunguza. Ni vigumu kutosha kufanya mazoezi hata wakati wa kujua kila kitu; bila ujuzi, mtu angeweza kupoteza matumaini."

Pia alikazia kwa mara nyingine tena kwamba ni lazima mtu afahamu kikamili Ufunuo na kutiwa muhuri kana kwamba anapigwa muhuri. Mwenyekiti Lee aliuliza, "Kwa nini unafikiri imeandikwa katika Ufunuo 22:18-19 kwamba mtu hataingia katika ufalme wa mbinguni na atalaaniwa ikiwa ataongeza au kupunguza kutoka humo?" Akajibu, "Ni kwa sababu maneno haya yanatimia kana kwamba yanapigwa muhuri."

Mwenyekiti Lee alisisitiza umuhimu wa kuandika maneno katika moyo wa mtu, kuwa 'Biblia inayotembea' na 'neno lililo hai.' Alitaja kwamba wale wanaofanya hivyo wanakuwa wale waliotiwa muhuri wanaotajwa katika Ufunuo 7, ambao wameokolewa. Mwenyekiti Lee alitangaza, "Hakuna wokovu unaotajwa isipokuwa wale waliotiwa muhuri 144,000 na kundi kubwa la watu waliovaa mavazi meupe; mtu ye yote ambaye hajatiwa muhuri anakuwa kama udongo, asiye na uhusiano wowote nalo. Ni wale tu waliotiwa muhuri wanaweza kuingia ufalme wa mbinguni." Pia alisema kwa uthabiti, "Wale ambao wametiwa muhuri wanaweza kuishi mbinguni, kuwa na uzima wa milele, na kuwa sehemu ya familia ya Mungu, lakini wale ambao hawana basi hawana uhusiano na Mungu."

Kwa wenyeji, Mwenyekiti Lee mara kwa mara aliwasilisha salamu kama vile "Nina uhusiano wa kina na Ufilipino," "Ufilipino ilikuwa mahali pa kwanza nilipokuja kutoa ushahidi baada ya kupokea neno," na "Ninaipenda sana Ufilipino.

Kwa kweli, Ufilipino imedumisha uhusiano na Mwenyekiti Lee kwa zaidi ya muongo mmoja. Mbali na shughuli zake za kidini, akiwa mwakilishi wa shirika lisilo la kiserikali la kimataifa la HWPL (Heavenly Culture, World Peace, Restoration of Light), alitembelea Ufilipino na kupatanisha makubaliano ya kwanza ya amani ya kiraia huko Mindanao, ambayo yamekuwa katika migogoro kwa muda mrefu. miaka 40. Kufuatia hili, amani ilianzishwa katika kanda, na habari hii ilipata tahadhari ya kimataifa.


Top News