Naibu Katibu Mkuu wa Usimamizi wa Uchumi, Wizara ya Fedha Bw. Elijah Mwamdumbya na Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Masuala ya Kodi Kimataifa wa Wizara ya Fedha ya Czech aliyeongoza ujumbe wa Czech Bw. Václav ZÃka, wakionesha nyaraka za kukamilisha majadiliano, katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania jijini Dar es Salaam.
Exim Bank, kupitia Mpango wake wa Kuwawezesha Kiuchumi Wanawake (WEP), imetoa mafunzo kuhusu masuala ya ujasiriamali, biashara, na uwezeshaji kwa wanawake wajasiriamali kama sehemu ya kuunga mkono ujumuishwaji wa watu wote, wakiwemo wanawake, katika mipango mbalimbali ya maendeleo nchini Tanzania.
Kupitia mpango wake wa ‘Exim Cares’, mwaka jana (2023) Exim Bank ilizindua Mpango wa Kuwakwamua Kiuchumi Wanawake ujulikanao ‘Women Empowerment Program (WEP)‘ wenye lengo la kuongeza ushirikishwaji na kuleta usawa kwa wanawake barani Afrika, hasa katika nchi ambazo zina matawi ya benki hiyo ikiwemo Tanzania, Comoros, Djibouti na Uganda.
Akizungumza katika mahafali hayo, Mkuu wa Kitengo cha Masoko wa Exim Bank, Stanley Kafu, anasema, “Ukiwa mwaka wa pili mfululizo wa mpango wa Kuwakwamua Wanawake Kiuchumi (WEP), Exim Bank tunafuraha kubwa kuwa sehemu ya mafanikio haya na tunawapongeza washiriki wote kwa kuanza na kumaliza salama mafunzo haya kuhusu ujasiriamali, uwezeshaji, na biashara.”
Washindi watatu, wa awamu hii ya kwanza mwaka huu, walipata zawadi za pesa taslimu zilitolewa kwa washindi watatu ambapo mshindi wa kwanza, Beatrice A. Msafiri, akizawadiwa kiasi cha TZS 8,000,000, mshindi wa pili, Catherine Assenga akipata TZS 5,000,000 na mshindi wa tatu, Rukia S. Mohamed akiondoka na TZS 3,000,000. Pia, wahitimu wote walipata fursa ya kuweza kupata mikopo bila riba kutoka Exim Bank ili waweze kujiendeleza kiuchumi.
Exim Bank inaamini uwezeshaji wa wanawake na ujasiriamali unabaki kuwa sehemu muhimu ya mipango ya maendeleo nchini Tanzania na barani Afrika kijumla. Hii inadhihirishwa na ongezeko la idadi ya wanawake katika nafasi za uongozi katika sekta mbalimbali kama siasa, kijamii na kiuchumi.
Akielezea kuhusu malengo ya mradi, Kafu alisema, “Mpango huu utakuwa ni endelevu kwa muda wa miaka mitano na tunatarajia kuwafikia wanawake zaidi ya 600,000 ifikapo mwaka 2028.”
Kafu anasisitiza kuwa Mpango wa WEP ni sehemu ya mkakati mkubwa na wa kina unaolenga kutengeneza jukwaa la wanawake ili waweze kufanikiwa na kustawi katika maisha yao, hasa kwenye eneo la uchumi.
Exim Bank imekuwa na itaendelea kuunga mkono juhudi za serikali katika kuleta maendeleo kwa Watanzania wote. Programu hii inawiana na Dira ya Maendeleo ya Tanzania 2025 na Dira ya Maendeleo ya Zanzibar 2050 na itakuwa chachu katika kuimarisha ustawi wa kijamii na kiuchumi kwa wanawake.
Mshindi wa tatu Rukia Said Mohamed (wa pili kulia), Zainab Nungu Mkuu wa Kitengo cha Mikopo, Exim Bank (wa kwanza kushoto), na Faraja Nyalandu, Mkurugenzi Mtendaji wa Ndoto Hub (wa kwanza kulia) wakifurahi pamoja na Mkuu wa Kitengo cha Masoko wa Exim Bank, Stanley Kafu wakati wa mahafali ya mafunzo ya ujasiriamali, biashara na uwezeshaji kwa wanawake wajasiriamali chini ya mradi wa benki hiyo yajulikanayo kama WEP katika tukio lililofanyika tarehe 23 Aprili 2024 mjini Arusha
Na. Josephine Majura, WF, Dodoma
Serikali imesema kuwa inaandaa mfumo wa kielektroniki wa kutoa ankara ya pamoja kwa huduma zinazolandana ili kuondoa usumbufu kwa wananchi wanaostahili kulipa kodi ya jengo na kodi ya ardhi.
Hayo yameelezwa bungeni, jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb), alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Mheshimiwa Fakharia Shomar Khamis, aliyetaka kufahamu mpango wa Serikali wa kuziunganisha kodi ya jengo na kodi ya ardhi.
“Serikali kupitia Kamati ya Moberesho ya Mfumo wa Kodi inaendelea kufanya uchambuzi na tathmini ya mifumo ya kodi, ada na tozo za huduma kwa lengo la kuondoa urasimu na kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji nchini”, alisema Mhe. Chande.
Alisema tathmini hiyo inajumuisha mapendekezo ya maboresho ya mfumo wa usimamizi wa kodi ya jengo na kodi ya ardhi kama inavyopendekezwa na Mheshimiwa Khamis.
Aidha katika swali la nyongeza lililoulizwa na Mbunge wa Mwera Mhe. Zahor Mohamed Haji, alitaka kujua mpango wa Serikali wa utoaji elimu kwenye mifumo inayoanzishwa.
Mhe Chande alisema kuwa Serikali kupitia Taasisi zake imekuwa na utaratibu wa kutoa elimu siku hadi siku kwa wadau wake kulingana na uhitaji katika kipindi hicho.
Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb) akijibu swali bungeni jijini Dodoma la Mbunge wa Viti Maalum, Mheshimiwa Fakharia Shomar Khamis, aliyetaka kufahamu mpango wa Serikali wa kuziunganisha kodi ya jengo na kodi ya ardhi.