NA EMMANUEL MBATILO, MICHUZI TV

SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) limetoa elimu ya viwango vya ubora kwa Wajasiriamali wadogo waliojitikeza katika Maonesho ya Kibiashara ya Miaka 60 ya Muungano katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam.

Akizungumza wakati wa maadhimisho hayo leo Aprili 25,2024, Afisa Masoko (TBS), Bw. Mussa Luhombero amesema wametoa elimu kwa Wajasiriamali hao jinsi ya kuzalisha bidhaa bora pamoja na ujuzi ambao utawawezesha kupata alama ya ubora ambayo itawafungulia wigo wa soko la ndani na la Kimataifa.

“Alama ya ubora kutoka TBS itawasaidia Wajasiriamali kuaminika sokoni na kukubalika katika masoko ya ndani na ya Kimataifa ambapo itawapatia mafanikio yenye tija kwao na Taifa kwa ujumla”. Amesema

Amesema wameshiriki katika maadhimisho hayo kwa lengo la kutoa huduma kwa wananchi hasa katika makundi mbalimbali ambayo ni wazalishaji,waagizaji,watumiaji wa bidhaa pamoja na wajasiriamali.

Aidha ametoa wito kwa waingizaji wa vipodozi nchini,kuingiza vipodozi ambavyo vimesajiliwa ambapo amesema kuwa kupitia tovuti yao kuna orodha ya vipodozi hivyo ambavyo haviruhusiwi kuingia nchini.

"Lakini pia wanaotumia vipozi wanaweza kututembelea ili tuweze kuwapa matumizi sahihi ya vipodozi na kwa wale wenye maduka ya chakula na vipodozi ambapo pia tunatoa elimu jinsi gani ya kusajiri maduka yao ya chakula au vipodozi". Amesema Bw. Luhombero

Sambamba na hayo Bw.Luhombero ametoa hamasa kwa wananchi wote kutumia bidhaa yenye alama ya ubora ya (TBS) ambapo itasaidia kuepukana na matumizi ya bidhaa zisizo na ubora ambazo zinaweza kuhatarisha afya kwa watumiaji.

Kwa Upande wake, Mfanyabiashara wa Vipodozi, Bw.Hamza Kamba ambaye ni muagizaji wa bidhaa kutoka nje ya nchi ameeleza kuwa yeye kama mdau ametembelea banda la TBS na amejifunza bidhaa ambazo ni bora na zisizobora.

TBS ili kuhakikisha inalinda usalama wa wananchi imetoa namba yake kupiga bure ili kuripoti bidhaa ambazo ziko sokoni zenye kutiliwa shaka kuhusiana na kuthibitishwa na Shirika la viwango ambayo ni 0800 110 827.



Mkuu wa Wilaya ya Ilemela, Hassan Masala,kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Said Mtanda, akizungumza na viongozi wa serikali wakiwemo wa vyama vya siasa wakiongozwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM),leo katika uzinduzi wa kampeni ya Elimu kwa Umma kuhusu utekelezaji wa Mradi wa Ujenzi wa Minara 758 ya Mawasiliano nchini.

NA BALTAZAR MASHAKA, MWANZA
SERIKALI mkoani Mwanza kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF), imezindua kampeni ya elimu kwa umma kuhusu utekelezaji wa miradi ya mawasiliano inayolenga kufikisha huduma hiyo kwa wananchi waishio maeneo yaliyo mbali vijijini yasiyo na mvuto wa kibiashara kwa watoa huduma.

Pia,imewataka wadau wanaotekeleza mradi wa ujenzi wa minara ya mawasiliano vijijini washirikiane na UCSAF kuhakikisha minara hiyo inakamilika kwa wakati wananchi wafikiwe na huduma hiyo.

Akizindua kampeni hiyo,leo Mkuu wa Wilaya ya Ilemela,Hassan Masala kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Said Mtanda,amesema lengo ni kuelimisha wananchi wengi wa Kanda ya Ziwa,hatua zilizofikiwa na serikali katika utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa minara ya mawasiliano vijijini na maeneo machache ya mijini.

Pia, kampeni hiyo inalenga kuweka msukumo wa kufikisha huduma za mawasiliano kwa wananchi waishio vijijini,hivyo wadau na UCSAF wakishirikiana kukamilisha mradi wa ujenzi wa minara 758,huduma za mawasiliano ya simu (Sauti na intenet/data),zitapatikana za uhakika maeneo yote.

Masala amesema huduma za mawasiliano ya simu zinagusa maisha ya watu,ni nyenzo muhimu katika kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi kwa mtu mmoja moja na taifa kwa ujumla,hivyo viongozi walioshikiri uzinduzi huo wawe mabalozi wazuri wa kuisemea serikali vizuri kwa wananchi utokana na elimu waliyoipata.

“Tunazindua kampeni hii kuhakikisha jamii ya Watanzania maeneo mbalimbali wanapata taarifa muhimu za utekelezaji wa ujenzi wa minara ya mawasiliano,licha ya kuzinduliwa Mwanza,itaendelea mikoa yote ya Kanda ya Ziwa (Shinyanga,Mara,Simiyu,Geita na Kagera),iliyofaidika na mradi huu na mengine ya mawasiliano, ”amesema.

Masala amesema serikali kupitia UCSAF iliingia makataba na makampuni (watoa huduma ya mawasiliano ya simu) kufikisha mawasiliano katika kata 713 kwa kujenga minara 758, inayopaswa kukamilika 2024/25.

“UCSAF imewaita viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Serikali mnaowakilisha Watanzania mpate elimu hii nanyi mkaisambaze,mkaisemee vizuri serikali kuhusu utekelezaji wa mradi huu, wananchi wafahamu Rais Dk.Samia Suluhu Hassan anavyotekeleza masuala ya mawasiliano bila ubaguzi kwa Mtanzania yeyote,”amesema .

MKuu huyo wa Wilaya ya Ilemela amesema Ibara ya 61 ya Ilani ya CCM inaelekeza katika kipindi cha miaka mitano,sekta ya mawasiliano itajikita kuimarisha ubora wa mawasiliano nchini na kuhakikisha wigo unaongezeka na kuwafikia wananchi wote,katika kutekeleza hilo, Rais Dk.Samia alishudia utiaji saini mikataba ya ujenzi wa minara 758 ya mawasiliano.

Pia,alishuhudia utiaji saini wa kuboresha na kuongeza nguvu minara 304 kutoka teknolojia ya 2G ya sauti pekee kwenda teknolojia ya intaneti/data ya 3G,4G na zaidi,hivyo kujengwa kwa minara hiyo vijijini ni utekelezaji wa ilani hiyo ya uchaguzi 2020-2025.
Naye Mratibu wa UCSAF Kanda ya Ziwa,Benard Buremo amesema baada ya makubaliano ya ujenzi wa minara hiyo kati ya wadau hao na serikali,watoa huduma walipewa miezi 24 ya kuikamilisha,kabla ya uchaguzi mkuu 2025 na kufafanua idadi ya minara hiyo 758 kwa kila kampuni ambapo Airtel inajenga 169,TTCL 104,Vodacom 190,Tigo 261 na Halotel 34.
Awali Ofisa Uhusiano wa UCSAF,Celina Mwakabwale amesema katika kuongeza ushindani katika soko la mawasiliano lilijitokeza ombwe lililosababishwa na nguvu za ushindani kujikita kupeleka mawasiliano maeneo yenye mvuto wa kibiashara na kuyaacha maeneo ya vijijini na ya mijini yasio na mvuto huo.

Amesema makampuni ya simu ni wabia wa serikali katika kutekeleza mradi huo unaogharimu sh.bilioni 126,ushirikiano huo umekuwa imara katika kufikisha huduma za mawasiliano hadi vijijini.


“Changamoto ya wananchi hawaufahamu Mfuko wa UCSAF,ulioanzishwa na Serikali kwa Sheria ya Bunge Namba 11 ya mwaka 2006 sura ya 422,kuwezesha na kufikisha huduma za mawasiliano kwa wananchi waishio maeneo machache mijini na mengine ya mbali vijijini yasio na mvuto wa kibiashara kwa watoa huduma wakihofia hasara,”ameeleza Mwakabwale.
Kwa mujibu wa Ofisa Uhusiano huyo serikali kupitia UCSAF imeingia mikataba na watoa huduma ya mawasiliano kufikisha huduma hiyo katika kata 1,974 zenye vijiji 5,111 kwa kujenga minara 2,158,ikikamilika wananchi 23,978,848 watapata huduma ya mawasiliano ya simu kwa uhakika.sssss
Ofisa Uhusiano wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF),Celina Mwakabwale,leo akizungumza na wadau (hawapo pichani) waliodhuria uzinduzi wa kampeni ya Elimu kwa Umma kuhusu utekelezaji wa Mradi wa Ujenzi wa Minara 758 ya Mawasiliano nchini.
Wakuu wa Wilaya za Misungwi na Sengerema,Johari Samizi (kushoto) na Senyi Ngaga (katikati), wakiwa katika uzinduzi wa kampeni hiyo ya elimu kwa umma leo.Walioketi nyuma ni makatibu tawala wa wilaya mbalimbali za Mkoa wa Mwanza.
Maofisa Tarafa na Watendaji Kata mbalimbali mkoani Mwanza,wakiwemo viongozi wa vyama vya siasa,leo wakifuatilia uzinduzi wa kampeni ya Elimu kwa Umma kuhusu utekelezaji wa Mradi wa Ujenzi wa Minara 758 ya Mawasiliano nchini.
Picha zote na Baltazar Mashaka

Na Mwandishi Wetu
SERIKALI ya Tanzania imesema kuwa inatekeleza uhamaji wa hiari wa wananchi kutoka Ngorongoro ili kulinda haki za binadamu na uhifadhi.

Hayo ameyasema Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya UNESCO Tanzania kuwa Prof. Hamis Malebo wakati akiwasilisha ujumbe Mkutano wa 23 wa Jukwaa la kudumu la Umoja wa Mataifa la Masuala ya Watu wa Asili (UNPFII) nchini Marekani ulichoanza Aprili 15 Aprili, 2024 na kuhitimishwa Aprili 26

Profesa Malebo, ameueleza mkutano huo kuwa, serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilifanya mapitio shirikishi ya hali ya maisha ya wananchi na uhifadhi katika Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (NCA) na kubaini umuhimu wa kuweka uwiano sawa wa uhifadhi wa maliasili na utamaduni, maendeleo ya jamii na maendeleo ya utalii.

Amesema kwa kutambua haki za binadamu, ambazo zimekuwa sauti ya wanaharakati na wahifadhi mbalimbali na kwa kuzingatia masharti ya Katiba yaTanzania na matakwa ya ulinzi na uhifadhi wa Mkataba wa Urithi wa Dunia wa 1972 na sheria za nchi, ni wazi kwamba, wananchi wanaoishi katika Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro wameathiriwa na migogoro ya binadamu na wanyamapori, magonjwa ya wanyamapori, kukosa haki ya kuwa na makazi ya kudumu, kudorora kwa maendeleo ya kijamii na kiuchumi, kukosa maji safi na salama, na umiliki wa ardhi.

Profesa Malebo amesema kwa mfano kuwa katika kipindi cha 2018 hadi 2023 watu 65 waliuawa na 205 walijeruhiwa na wanyama pori kama vile Simba, Chui, Fisi, Kiboko, Nyati na pamoja na Tembo.

Amesema Wananchi walio katika Hifadhi ya eneo la Ngorongoro wanaachwa nyuma katika Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs).

Prof. Malebo ameeleza kuwa, kwa kufuata misingi ya haki za binadamu, Serikali imefanya mashauriano na jamii ya wakazi wa Ngorongoro katika kipindi cha miaka 32 ili kwa pamoja kupata ufumbuzi wa kudumu wa changamoto za kijamii na kiuchumi zinazowakabili wananchi wake wanaoishi katika ardhi ya hifadhi.

Hata hivyo amesema Mikutano ya uhamasishaji imefanyika kuanzia ngazi ya chini hadi ngazi ya tawala za Wilaya na Mikoa juu Wakazi wanaoishi katika walioko katika Mamlaka ya Ngorongoro mbalo ni eneo lililohifadhiwa walipewa elimu kuhusu sheria zinazosimamia utendakazi wa NCA ambazo haziruhusu wala kutoa kibali chochote cha kisheria kwa ajili ya shughuli za kijamii na kiuchumi wala kutoa haki ya umiliki wa ardhi katika eneo hilo la hifadhi ambalo pia ni eneo la Urithi wa Dunia.

Aidha wakazi hao walifahamishwa kuhusu manufaa yanayohusiana na kuhama kwao kwa hiari Kwenda katika maeneo yaliyo nje ya hifadhi nchini Tanzania.

Akifafanua juu ya mkakati wa kuhama kwa hiari.
Prof. Malebo alibainisha kuwa, kwa kuongozwa na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mikataba ya Umoja wa Mataifa, Tamko la Kimataifa la Haki za Binadamu, Mikataba ya Kimataifa ya Haki za Binadamu, maazimio ya vyombo vingine muhimu vya haki za binadamu na Azimio la Vienna, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaunga mkono uhamaji wa hiari wa wananchi kutoka hifadhi ya eneo la Ngorongoro.

Serikali pia inawezesha zoezi hilo na inabeba gharama za uhamaji, fidia na inatoa mkono wa shukrani kwa wananchi wanaohama kwa hiari Kwenda nje ya eneo la hifadhi.

Profesa Malebo amesema Serikali inahakikisha wanajamii wanaoishi katika ardhi iliyohifadhiwa wanasaidiwa kuhama na kwenda kuishi katika maeneo ambayo wataendelea na kutekeleza tamaduni zao kwa uhuru tofauti na ambako kwa sasa wanaishi kwa kukabiliwa na changamoto zinazotishia maisha, utamaduni na kuchochea umaskini.

Prof. Malebo pia aliueleza mkutano huo kuwa, Serikali ya Tanzania imepanga kwa umakini uhamaji wa hiari wa wananchi kutoka katika Hifadhi ya Ngorongoro ambayo ni hatarishi kutokana na ugumu wa maisha na migogoro na wanyamapori jambo ambalo linatoa fursa kubwa za kupunguza maafa na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi kwa wakazi na eneo hilo la Urithi wa Dunia.

Amesema Serikali iliainisha maeneo nje ya hifadhi ambapo wakazi wa Ngorongoro wataweza kuhamia kwa hiari na kuendelea na shughuli zao za kujitafutia riziki kwa amani kama ilivyoainishwa kwenye Katiba ikiwa ni pamoja na kumiliki ardhi na kufanya shughuli za kijamii na kiuchumi.

Wajumbe wengine wa Tanzania wanaohudhuria mkutano huo ni pamoja na Bi. Zuleikha Tambwe, Afisa Mwandamizi wa Mambo ya Nje katika Ubalozi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Bi. Hindu Zarooq Juma, Afisa Mwandamizi wa Mambo ya Nje katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Pellage Kauzeni, Afisa Mhifadhi Mkuu wa Wanyamapori katika Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Agnes Gidna, Kaimu Meneja wa Urithi wa Dunia katika Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro, Bw. Edward Kutandikila, Mwanasheria wa Serikali na Bw. Erick J. Kajiru, Afisa Mwandamizi Mkuu katika Tume ya Taifa ya UNESCO ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

 

AIRTEL TANZANIA imeibuka kinara wa kutoa huduma bora za mtandao kufuatia ripoti ya Takwimu ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) inayoishia Machi 2024 ya kila robo ya mwaka iliyochapishwa Aprili 23, 2024.

Taarifa hii ya matokeo ya kuwa kinara kwenye utoaji wa huduma za mtandao ni uthibisho wa dhamira na mikakati Madhubuti ya Airtel iliojiwekea katika kupanua huduma ili kuiweka Tanzania kwenye ulimwengu wa kidigitali. Airtel inavunja rekodi ya kuwa mtandao unaongoza kwa kuwa na simu nyingi zilizopigwa kwa robo hiyo ya mwaka kwa uwiano wa asilimia 38 (simu za Airtel kwenda Airtel) na asilimia 30 (kwa simu zilizopigwa kwenda mitandao mingine). Hii ni kwa mujibu wa ripoti ya takwimu za mawasiliano zilizochapishwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania kwa robo ya tatu ya mwaka wa fedha 2023/2024.

Vilevile, ripoti hiyo inabainisha kuwa simu nyingi zaidi zilizopigwa ndani ya mtandao Airtel Kwenda Airtel zilichangia 53% ikilinganishwa na simu za nje ya mtandao 47%. Hii inadhirisha kwamba wateja wa Airtel wanaridhishwa zaidi na kupiga simu za ndani ya mtandao wa Airtel kutokana na kuwa na huduma zinazokidhi mahitaji ya wateja.

Akizungumzia matokeo hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Tanzania, Bw. Dinesh Balsingh, alisema, “Ubunifu tulionao Airtel kwenye huduma unatufanya kuwa mtandao pendwa, gharama zetu ni nafuu na shindani, hii inawavutia wateja kuendelea kufurahia kuwa ndani ya mtao wetu. Airtel tutaendelea kutoa huduma na masuluhisho mbalimbali ili kuufanya mtandao wetu kuwa nyenzo muhimu katika kuwezesha shughuli za biashara ndani na nje ya nchi.”

Uchambuzi zaidi wa ripoti hiyo unaonyesha kuwa simu zilizopigwa na watumiaji takribani dakika 35 bilioni zilikuwa kwenye viwango bora zaidi ndani ya robo ya mwisho ya Machi 2024, ikilinganishwa na dakika 39 bilioni katika robo iliyoishia Desemba 2023. Pia imeonesha kukua kwa bilioni 4 zaidi ndani ya robo ya mwaka huo ukilinganisha na kipindi kilichopita. Kumekuwa na ongezeko la simu zinazopigwa kwa kipindi chote ndani ya mtandao.

Ripoti hiyo pia inaweka wazi uboreshaji mkubwa uliofanywa kwenye Ubora wa Huduma za mtandao wa Airtel, Airtel ikishika nafasi ya kwanza kwa asilimia 97, ikifuatiwa na Halotel kwa asilimia 94 na Tigo kwa asilimia 94.8, hivyo Airtel ikiongoza kwenye tasnia ya mawasiliano.

Bw. Dinesh alisisitiza kuwa “Airtel Tanzania tutaendelea na uboreshaji wa miundombinu ya mtandao, tutatoa huduma za kibunifu zaidi ili kukidhi mahitaji ya watanzania na wateja wetu kupitia mawasiliano. Tuna nia ya kuendelea kuiunganisha Tanzania kidigtali katika kila jambo linalohitaji huduma za mtandao.

Aidha, Airtel kwa kutajwa kuwa katika nafasi nzuri katika ripoti ya takwimu ya TCRA, Airtel inaendela kijidhihirisha kuwa lango la mawasiliano katika ukanda wa Afrika Mashariki.Pia Airtel imeweza kukamilisha mradi wa ujenzi wa Mkongo wa mawasiliano unaopita baharini wa Airtel 2Africa mwaka jana nakuzinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan. Airtel imejidhatiti kuendelea kutoa suluhu za mawasiliano ya simu, huduma za fedha kwa njia ya mtandao pamoja na huduma za Intaneti.

Na Mwandishi Wetu

SERIKALI ya Marekani kupitia Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID) na Kituo cha Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa cha Marekani (CDC) wameungana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuadhimisha Siku ya Malaria Duniani na kutangaza kampeni ya usambazaji wa vyandarua vilivyowekwa dawa kwa Zanzibar yote.

Kwa mujibu wa Utafiti wa Viashiria vya Malaria Tanzania wa mwaka 2022, Zanzibar bado ina kiwango cha malaria chini ya asilimia moja kwa zaidi ya muongo mmoja.

Hiyo ni kutokana na mchango mkubwa kutoka serikali ya Marekani kupitia Mpango wa Rais wa Marekani wa mapambano dhidi ya malaria na ushirikiano na serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na kwamba hivi karibuni idadi hii iliongozeka.

Akizungumza kuhusu Mpango huo Waziri wa Afya Zanzibar Dk.Nassor Ahmed Mazuri amesema pamoja na kupungua kwa namba ya wagonjwa wa malaria Zanzibar, amegundua hivi karibuni kuna baadhi ya wilaya zimeshuhudia ongezeko la wagonjwa wa malaria.

" Hili halikubaliki Zanzibar, naomba hatua zote zichukuliwe kudhibiti ugonjwa ya malaria kwa kushirikisha sekta zote zinazohusika” amesema Dk Mazrui.

Mwaka huu Maadhimisho ya Siku ya Malaria Duniani yalishuhudia uzinduzi wa wa kampeni ya usambazaji wa vyandarua vilivyotiwa dawa iliyopewa jina la’ Usingizi Bul Bul.’

Kampeni hiyo inayoongozwa na Mpango wa Rais wa Marekani wa kupambana na Malaria (PMI), itasambaza vyandarua 782,000 katika Shehia 314 Unguja na Pemba.

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar pia ilizindua Baraza la Kutokomeza Malaria, ambalo litaimarisha utokomezaji wa malaria kwa kuonesha umuhimu wa kuongeza rasimili zaidi.

“Marekani ina heshima kubwa kuungana na serikali ya Zanzibar katika kuanzisha kampeni ya usambazaji wa vyandarua vilivyotiwa dawa Zanzibar na kuhakikisha vinatumika ipasavyo.

" Kwa pamoja, tuna elimisha jamii kutoka kuelewa tu mpaka kutumia kwa vitendo,” amesema Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la USAID Craig Hart wakati wa hafla hiyo.

“Naipongeza serikali ya Zanzibar kwa kuzindua pia Baraza la Kutokomeza Malaria, litakaloimarisha programu za kupambana na malaria kwa kuongeza rasilimali zaidi kusaidia afua za malaria, kwa kushirikiana na sekta binafsi."

Kampeni hiyo ya usambazaji wa vyandarua vyenye dawa inawakilisha mbinu bunifu na ya kina ya kutokomeza malaria. Itatumia mfumo wa kielektroniki kufuatilia maoteo ya vyandarua, usajili wa kaya zitakazopata vyandarua, na ugawaji wa vyandarua hivi.

Itatumia jumbe fupi kufahamisha kaya siku ya kupokea vyandurua na kusambaza jumbe kuhusu matumizi sahihi ya vyandarua na utunzaji wa vyandarua. Mfumo huu umewezeshwa na kufadhiliwa na serikali ya Marekani kupitia PMI.

Ukitekelezwa na USAID na CDC, PMI ilianza kushirikiana na Tanzania mwaka 2006 na imewekeza zaidi ya dola milioni 747 nchini. Marekani bado ina dhamira ya dhati ya kuendelea kushirikiana na serikali na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, asasi za kiraia na watu wa Tanzania katika mapambano yanayoendelea ya kutokomeza malaria na kuboresha afya na ustawi wa wananchi wake.



 

Mkurugenzi Mkazi wa USAID Dk Crag Hart akizungumza wakati wa uzinduzi wa mpango huo uliozinduliwa leo

Na Mwandishi Wetu

Wakati kesho Tanzania ikisherehekea miaka 60 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) na Mamlaka ya Ununuzi na Uondoaji wa Mali za Umma Zanzibar (ZPPDA) zimesaini rasimu ya mkataba wa maelewano (MOU) kufanya kazi pamoja na kuimarisha muungano.

Makubaliano hayo yamesainiwa leo jijini Dodoma mbele ya wenyeviti wa bodi zote mbili za wakurugenzi na wajumbe wa bodi ya wakurugenzi, wawakilishi wa wafanyakazi na makamu Mwenyekiti ZPPDA, wajumbe wa bodi wa pande zote mbili, Mkurugenzi Mkuu PPRA, Eliakim Maswi na Mkurugenzi Mtendaji ZPPDA, Othman Juma Othman na menejimenti ya Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA).

Akizungumza baada ya kusaini MOU hiyo, Mkurugenzi Mkuu Mamlakaya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA), Eliakim Maswi, amesema wamekubaliana kushirikiana katika kujenga uzoefu kwa watendaji na kukuza maarifa ya kiutendaji kwa kubadilishana utaalamu katika kutekeleza mbinu za kimkakati na taaluma ya ununuzi.

Vilevile, kushirikiana katika kuzitambua sheria na miongozo ili kuleta tija na uwajibikaji ndani ya taasissi hizo, kuelimishana taarifa na ujuzi muhimu unaohusu ununuzi wa umma na uendeshaji mali za umma, kuhabarishana, kubadilishana uzoefu na kuhusishana katika fursa za kushiriki katika majukwaa na mikutano inayohusu ununuzi wa umma.

“Tumeamua kushirikiana kwa sababu wote tuko katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kazi tunazofanya zinafanana tumeamua kushirikiana na kubadilishana uzoefu katika utendaji kazi wetu hiyo ilikuwa ni mwaka 2022 na mwaka jana 2023 bodi yetu ya PPRA ilienda Zanzibara na kufanya kikao,” amesema Maswi na kuongeza;

“Baada ya kikao kile viongozi wetu wa pande zote mbili walitoa maelekezo kwamba tukutane na tuandae makubaliano ambayo yatatuwezesha kushirikiana na kuwezesha pande zote mbili kufanya kazi.

Wanasheria kutoka pende zote mbili wamefanya kazi kwa kushirikiana na wametuleta mapendekezo ambayo wameona yanafaa na mimi na mwenzangu tumekubaliana kwamba haya yanafaa,”

Ameongeza kwamba wamekubaliana kupeana msaada unaohitajika kupitia rasilimali walizonazo, kuimarisha, kuwajengea uwezo watendaji wa pande zote mbili na kuwaweka pamoja.

“Baada ya mkataba huu mimi nikitaka mtu kutoka Zanzibar mwenzangu atamruhusu pia akitaka nitamruhusu maana tunataka kubadilisha uzoefu, kutengeneza ushirikiano maalum katika shughuli za ufuatiliaji, ukaguzi na uchunguzi unaojumuisha uchunguzi wa uzingatiaji wa sheria na thamani ya fedha,” amesema Maswi

“Pia tutashauriana kuhusu nyenzo za kisasa za utendaji wa majukumu ikiwemo vifaa vya kielektroniki na vingine vya kazi ya uchunguzi na ufuatiliaji. Tutakuwa na shughuli za pamoja ambazo tunazifanya ikiwemo kikao cha pamoja cha bodiya Wakurugenzi, kila upande utakuwa na wajibu wa kuzingatia, kufuata na kutekeleza ratiba hiii,”

“Ni wajibu wa pamoja kuandaa dira sisi PPRA na ZPPDA na ripoti itolewe ili kubuni mikakati ya kuleta tija katika nch yetu. Tumekubaliana kufanya mafunzo ya muda mfupi ya mara kwa mara kwa watendaji wetu wa mamlaka kwenda kwa kila mamlaka kujifunza yanayohusu shughuli za usimamizi wa mali za umma na uondoaji wa mali,” amesema

Ameeleza kuwa kupitia makubaliano hayo wanaweza kufanya vikao vya pamoja vya dharura kama kuna changamoto imejitokeza ili kuimarisha Muungano, pia watakuwa wanawasiliana kupeana msaada unaohitajika kwa wakati muafaka kwa ajili ya kupeana mbinu za kutatua changamoto.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji Mamlaka ya Ununuzi na uondoaji wa Mali za Umma Zanzibar (ZPPDA), Othman Juma Othman amesema “tunafanya kazi kwa pamoja kwa maslahi ya Watanzania leo tumesaini MOU tunaishukuru idara ya Mwanasheria Mkuu Zanzibar imetoa maoni yake na leo hii yametuwezesha kufika hapa.

Naye, Makamu Mwenyekiti Bodi ya Wakurugenzi Mamlaka ya Ununuzi na uondoaji wa Mali za Umma (ZPPDA), Ahmed Makame Haji, amesema makubaliano hayo yameishasainiwa lakini hayatakamilika na hayatakuwa na umuhimu kama hakutakuwa na utekelezaji na suala hilo kubaki katika makaratasi.

“Kama ambavyo tumekubaliana kuna umuhimu mkubwa wa kuhakikisha makubaliano hayo yanatekelezwa na kujiwekea utaratibu wa kuangalia kama makubaliano hayo yanatekelezwa. Tutakuwa na suala la ufuatiliaji na kuangalia kila mwaka tumefikia wapi katika utekelezaji wa makubalaino haya na pale ambapo tutabaini kasoro tutazitatua na kuhakikisha tunafikia hayo makubaliano,” amesema Haji

Naye,Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi PPRA, Dkt. Leonada Mwagike, amesema “tumeishasaini mkataba kilichobaki ni utekelezaji kwa wakati ili kuhakikisha thamani halisi ya fedha inapatikana katika ununuzi wa umma na kuhakikisha tunafanya tathimini ya utekelezaji wa makubaliano haya mara kwa mara ili kuhakikisha mkataba huu unatekelezeka."
Mkurugenzi Mkuu Mamlakaya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA), Eliakim Maswi na Mkurugenzi Mtendaji Mamlaka ya Ununuzi na uondoaji wa Mali za Umma Zanzibar (ZPPDA), Othman Juma Othman wakisaini hati za makubaliano ya ushirikiano wa kiutendajiji  kati ya Tanzania Bara na Zanzibar katika hafla iliyofanyika Dodoma.

Na Mwandishi Wetu

Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET), Kanda ya Magharibi, limewapatia elimu wanafunzi 5,000 katika shule za sekondari 20 za Manispaa ya Tabora kuhusu kazi za Baraza, taratibu na miongozo mbalimbali ya kujiunga na vyuo vya Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi nchini.

Akizungumza na baadhi ya wanafunzi, Meneja wa NACTVET Kanda ya Magharibi, Bi. Faraja Makafu amesema, kampeni hiyo imelenga kuondoa changamoto wanazopata wanafunzi wakati wa kuomba kujiunga na vyuo mbalimbali vya elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi mara baada ya kuhitimu masomo yao ikiwemo changamoto ya kudahiliwa katika vyuo na programu zisizo na ithibati ya Baraza.

“Uzoefu wetu na maoni toka kwa wadau wetu mbali mbali umetufanya tuanzishe kampeni ya Kanda kwa kanda ili kuwasaidia wanafunzi kufanya maamuzi na machaguo sahihi wakati wa kuomba vyuo. Wanafunzi wanapaswa kuomba udahili kwa usahihi na kwa kuzingatia taratibu na miongozo iliyowekwa ili waweze kutimiza ndoto zao”, alitamatisha Bi. Faraja.

Aidha, Meneja huyo wa Kanda amewataka wanafunzi hao kusoma kwa makini kitabu cha mwongozo wa udahili ambacho kinapatikana katika tovuti ya Baraza (www.nactvet.go.tz) kwani kina maelezo ya kina ya hatua kwa hatua hadi kukamilisha udahili wa wanafunzi katika vyuo vya Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi.

Kwa upande wao, wanafunzi hao kwa nyakati tofauti wameshukuru hatua ya NACTVET kuanzisha zoezi la kuwapatia wanafunzi Elimu hiyo muhimu kwao na kuahidi kuwa mabalozi wazuri kwa wengine kwa kuwaeleza umuhimu wa kuzingatia taratibu na miongozo pindi watakapoamua kujiunga na vyuo mbalimbali.

Kampeni ya uelimishaji wanafunzi wa shule za sekondari za Kanda ya Magharibi, mkoani Tabora imeanza tarehe 22 Aprili, 2024 na itafikia tamati mnamo tarehe 1 Mei, 2024, ambapo miongoni mwa shule zilizokwishatembelewa ni pamoja na Shule ya Sekondari ya Wavulana Milambo, Shule ya Sekondari ya Wasichana Tabora, Shule ya Sekondari Themi Hill, Shule ya Sekondari ya wavulana Tabora, Shule ya Sekondari Ipuli, Shule ya Sekondari Cheyo, Shule ya Sekondari Isevya na Shule ya Sekondari Mihayo.

NACTVET ilianzishwa kwa Sheria ya Bunge, Sura ya 129 na Marekebisho Madogo Na.4 ya mwaka 2021, kwa lengo la kurekebu Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi nchini. Fasiri ya Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi ina nasibishama “Elimu na Mafunzo yanayotolewa kwa wanachuo kwa misingi ya ujuzi na umahiri (CBET), ili kuwajengea uwezo wahitimu kutekeleza majukumu yao yanayohitaji kiwango cha juu cha ujuzi, maarifa, uelewa na weledi kuwawezesha kutimiza wajibu wao kwa ufanisi na tija katika maeneo ya taaluma walizosomea”.

NACTVET ina jumla ya kanda nane zilizoanzishwa kwa lengo la kusogeza huduma karibu na wadau. Kanda hizo ni ni pamoja na Kanda ya Mashariki Dar es salaam, Kanda ya Kati Dodoma, Kanda ya Magharibi Tabora, Kanda ya Ziwa Mwanza, Kanda ya Kusini Mtwara, Kanda ya Kaskazini Arusha, Kanda ya Kati Dodoma pamoja na Ofisi ya Zanzibar.
 

Meneja wa NACTVET Kanda ya Magharibi Tabora Bi. Faraja Makafu akitoa Elimu kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari Mihayo
 

Afisa Uthibiti wa NACTVET Kanda ya Magharibi Tabora, Bw. Mohamed Kaunasa akizungumza na Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Wavulana  Milambo.
 

 Meneja wa NACTVET Kanda ya Magharibi Tabora, Bi. Faraja Makafu akitoa zawadi kwa  mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Kamazima.


 

Picha za matukio mbalimbali katika utoaji elimu wa NACTVET.

Na Mwandishi wetu, Rombo
MKUU wa wilaya ya Rombo mkoani Kilimanjaro, Raymond Mwangala amewataka wakazi wa eneo hilo kuwekeza kwenye elimu kwani mataifa mengi yameendelea kutokana na kuwekeza katika elimu.


Mwangala akizungumza kwenye kikao cha tathmini ya elimu ya sekondari na kugawa zawadi kwa wanafunzi waliofaulu vyema kidato cha nne, shule zilizofaulisha na walimu wao amesema Rombo mpya ya maendeleo imezaliwa hivyo jamii iwekeze kwenye elimu.


Amesema hivi sasa wilaya ya Rombo imezaliwa upya ikilenga kutazamwa kwa mtazamo chanja tofauti na awali ilivyozungumzwai na ndiyo sababu eneo la kwanza la Mamsera itawekwa taa za barabarani hadi Mkuu.


"Tunaiona Rombo mpya ya maendeleo, tuna maprofesa wengi nchi nzima wametokea Rombo, kuna madokta, mapadri hata marehemu Gadna G Habash kumbe kwao ni Tarakea na aliyekuwa mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali (CAG) Ludovick Utouh ametokea Rombo," amesema.


Amesema amelenga kushirikiana na jamii ya Rombo kuwekeza kwenye elimu ili maendeleo yapatikane kwani nchi nyingi zilizoendelea zimewekeza katika elimu.


"Matajiri wengi wa Dar es salaam, Dodoma, Arusha na kwingine wametokea Rombo, tunataka Rombo mpya ya maendeleo, watu waje Rombo kuona utalii wa mtori na ndizi na watu wenye maendeleo," amesema.


Ofisa elimu sekondari wa halmashauri ya wilaya ya Rombo, Silvanus Tairo amesema kikao hicho kitakuwa chachu ya kuongeza ufaulu mzuri kwa wanafunzi kwani wamejipangia mikakati ya kuboresha elimu na kupambana na changamoto zilizopo.


Tairo amewapongeza walimu waliofanikisha wanafunzi 1,700 kupata daraja la kwanza hadi daraja la tatu ambao ndiyo wenye sifa za kuendelea na elimu ya juu na vyuo mbalimbali.


"Lengo ni kufanya tafakuri ya elimu na kuweka mikakati ambayo itatusaidia kufanya vzuri zaidi kwenye mitihani ijayo na pia kuwapa motisha wanafunzi, walimu na shule husika kufanya vyema zaidi," amesema Tairo.


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof Adolf Mkenda ambaye pia ni mbunge wa Rombo, akizungumza kwa njia ya simu, amewapongeza walimu kwa namna wanavyojitahidi kunyanyua kiwango cha elimu kwa kuwafundisha wanafunzi.


"Nawaahidi kuwa tutaendelea kushirikiana pamoja walimu wangu ili sekta hii muhimu iweze kuwanufaisha watoto wetu ambao watakuwa na manufaa kwa Taifa," amesema Prof Mkenda.


Kaimu mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Rombo, Christina Marwa ameipongeza idara ya elimu sekondari kwa ubunifu huo wa kufanya tathimini na kutoa zawadi kwa ufaulu.


"Tumeona jambo hili ni jema mno hivyo mwakani mjipange upya na kulifanya kwani litakuwa na matokeo chanya kutokana na hamasa hii iliyofanyika kwa walimu na wanafunzi," amesema Marwa.


Mmoja kati ya wanafunzi walipatiwa zawadi kwa ufaulu mzuri Deus Mdee wa shule ya sekondari Kelamfua amesema motisha walizopata zitaongeza ari kwa wanafunzi kusoma zaidi na walimu kufundisha kwa moyo wote.


"Nashukuru kwa zawadi ya madaftari kwani lengo langu ni kuwa daktari na sasa nasubiria kupangiwa shule ili niende na masomo ya kidato cha tano," amesema.



Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni(kulia) na Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Rasilimaliwatu wa wizara hiyo, Miriam Mmbaga(wapili kushoto) wakisikiliza ufafanuzi wa programu maalumu ya kudhibiti uhalifu wa Kimtandao kutoka kwa Meneja Mauzo wa Kampuni ya SOLAR,Timul Solovev wakati wa Maonesho ya Teknolojia ya Kudhibiti Uhalifu huo yanayoendelea katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa EXPOFORUM ambapo Maafisa wa Daraja la Juu kutoka serikalini wanaohusika na mambo ya Usalama kutoka takribani nchi 20 Duniani wamekutana nchini Urusi.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.


Na Mwandishi Wetu,URUSI

SERIKALI imedhamiria kushirikiana na nchi ya Urusi katika kudhibiti uhalifu nchini ikiwemo uhalifu wa mtandao ambao umeanza kushamiri katika maeneo mbalimbali nchini huku ikiweka wazi dhamira ya kujengewa uwezo kwa askari wa vyombo vya ulinzi na usalama kwa kushirikiana na nchi zilizoendelea kiteknolojia katika kudhibiti uhalifu huo unaotajwa kuvuka mipaka.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni wakati wa Mkutano wa Kimataifa wa Maafisa wa Daraja la Juu kutoka serikalini wanaohusika na mambo ya Usalama unaoendelea nchini Urusi ambao ulifunguliwa na Rais wa Shirikisho la Urusi na kuongozwa na Katibu wa Baraza la Usalama la Shirikisho la Urusi, Nikolai Patrushev.

‘Katika kudhibiti masuala ya uhalifu wa kimtandao matumizi ya teknolojia hayaepukiki ndio maana serikali imeona kuna haja ya kuimarisha vyombo vyetu vya ulinzi na usalama katika Nyanja mbalimbali ikiwemo ujuzi kwa askari wetu sasa kupitia mkutano huu tunaenda kujenga mahusiano kati ya Jeshi la Polisi la Tanzania na Jeshi la Polisi la Urusi ili tuweze kudhibiti uhalifu wa kimtandao ambao umekua ukisababisha madhara mbalimbali katika jamii ikiwemo ya kiusalama,kiuchumi na hata maadili’. Alisema Waziri Masauni

Akizungumza wakati wa Mkutano huo Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Rasilimaliwatu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Miriam Mmbaga alisema muelekeo wa wizara katika kuendana na kasi ya ukuaji wa teknolojia ina mkakati maalumu wa kuwajengea uwezo askari waliopo katika Vyombo vya Ulinzi hasa katika masuala ya teknolojia huku akiweka wazi juu ya suala la ajira pia kuweka kipaumbele kwa watu waliosomea masuala ya teknolojia ya Habari.

Mkutano huo wa Kimataifa wa Maafisa wa Daraja la Juu kutoka serikalini wanaohusika na mambo ya Usalama umehudhuriwa na nchi takribani 20 huku msisitizo zaidi ukiwekwa katika kupambana na uhalifu wa kutumia teknolojia ambao umekua ni tishio katika mataifa mbalimbali.
Katibu wa Baraza la Usalama la Shirikisho la Urusi, Nikolai Patrushev (wa kumi na tano kulia), akiwa katika picha ya pamoja na Maafisa wa Daraja la Juu kutoka serikalini wanaohusika na mambo ya Usalama kutoka takribani ya nchi 20 Duniani waliokutana nchini Urusi katika Jiji la St.Petersburg kujadili changamoto ya uhalifu wa kimtandao na jinsi ya kupambana nao.Tanzania pia inashiriki mkutano huo ikiwakilishwa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mhandisi Hamad Masauni.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni(wapili kushoto) akionyeshwa jinsi ndege isiyo na rubani inavyoweza kupambana na uhalifu na Afisa kutoka Kampuni ya DOMINA,Alexeen Alexander wakati wa Maonesho ya Teknolojia ya Kudhibiti Uhalifu huo yanayoendelea katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa EXPOFORUM ambapo Maafisa wa Daraja la Juu kutoka serikalini wanaohusika na mambo ya Usalama kutoka takribani nchi 20 Duniani wamekutana nchini UrusiPicha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
aziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni na Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Rasilimaliwatu wa wizara hiyio, Miriam Mmbaga(katikati) wakisikiliza maelezo ya kudhibiti uhalifu wa kimtandao kutoka kwa Meneja Masoko wa Kampuni ya Kupambana na Uhalifu wa Kimtandao(CyberED),Gadzhi Akhmedov wakati wa Maonesho ya Teknolojia ya Kudhibiti Uhalifu huo yanayoendelea katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa EXPOFORUM ambapo Maafisa wa Daraja la Juu kutoka serikalini wanaohusika na mambo ya Usalama kutoka takribani nchi 20 Duniani wamekutana nchini Urusi.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (watatu kulia) na Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Rasilimaliwatu wa wizara hiyo, Miriam Mmbaga(kulia) wakionyeshwa jinsi Mfumo wa Kudhibiti Uhalifu wa Kimtandao unavyofanya kazi na Mtaalumu wa Teknolojia ya Habari kutoka Kampuni ya KOMIB,Egor Bogomolov wakati wa Maonesho ya Teknolojia ya Kudhibiti Uhalifu huo yanayoendelea katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa EXPOFORUM ambapo Maafisa wa Daraja la Juu kutoka serikalini wanaohusika na mambo ya Usalama kutoka takribani nchi 20 Duniani wamekutana nchini Urusi.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi  ameipongeza Jumuiya  ya  Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) kwa kazi kubwa waliyoifanya kuwaletea maendeleo wanawake na kukiimarisha Chama Cha Mapinduzi (CCM) pamoja na kuandaa mdahalo wa wanawake na Muungano.

 Pia, ameupongeza umoja huo kwa kuendelea kuwa kinara katika kubuni na kutengeneza mambo mbalimbali yenye lengo la kuimarisha CCM, kikiunganisha na wananchi na kuimarisha umoja na mshikamano na wananchi.

Dkt. Mwinyi amesema hayo jijini Dar es Salaam leo Aprili 25, 2024 alipofungua mdahalo wa kitaifa wa Wanawake na Muungano uliondaliwa na Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) na kufanyika katika ukumbi wa Mlimani City.

Mdahalo huo uliohudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo wake za viongozi  wakuu wastaafu, mawaziri, naibu mawaziri, wabunge, wawakilishi, wananchi na wanachama wa jumuiya hiyo na wa CCM.

Kwa upande wake mwenyekiti wa UWT Taifa Ndg. Mary Pius Chatanda amesema wanafanya mdahalo wa kuelekea miaka 60 ya Muungano na kujadili nafasi ya mwanamke katika kipindi cha nyuma,sasa na kijacho

Kwa upande wake, Makamu Mwenyekiti wa UWT, Ndg.Zainab Shomari amesema muungano huo uliletwa na nchi mbili za Tanganyika na Zanzibar zikiwa huru, haukuwa wa kuchanganya mchanga tu, bali wa kidamu  kwa kuwa Zanzibar kuna watu wa makabila mbalimbali.

 

 

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa na Mkewe Mama Mariam Mwinyi wakiwasilimia Viongozi wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT)  walipowasili katika ukumbi wa mkutano wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kulifungua Kongamano la Wanawake na Muungano lililofanyika leo 25-4-2024.(Picha na Ikulu)
WASHIRIKI wa Kongamano la Wanawake na Muungano kuadhimisha Miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lililofanyika leo 25-4-2024 katika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam, wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akihutubia na kulifungua Kongamano hilo.(Picha na Ikulu)
MKE wa Rais wa Zanzibar Mama Mariam Mwinyi akiwa na Wake wa Viongozi wakifuatilia hutuba ya ufunguzi wa Kongamano la Wanawake na Muungano kuadhimisha Miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wakati Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akifungua Kongamano hilo lililofanyika leo 25-4-2024 katika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam.(Picha na Ikulu)
WASHIRIKI wa Kongamano na Wanawake na Muungano kuadhimisha Miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakishingilia wakati Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akihutubia na kulifungua Kongamano hilo lililofanyika katika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam leo 25-4-2024.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi, akimkabidhi Zawadi Maalum ya Picha iliyotolewa na Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) kwa Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan, akipokewa kwa niaba Mhe.Wanu Hafidh Ameir, wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Kitaifa la Wanawake na Muungano lililofanyika katika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam leo 25-4-2024.(Picha na Ikulu)   
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi,akimkabidhi Zawadi Maalum ya Picha iliyotolewa na Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Mjane wa Rais wa Kwanza wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Hayati Sheikh Abeid Amani Karume Mama Fatma Karume,wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Kitaifa la Wanawake na Muungano lililofanyika katika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam leo 25-4-2024.(Picha na Ikulu)  
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi, akimkabidhiwa Zawadi Maalum ya Picha iliyotolewa na Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) kwa mchango wake, akikabidhiwa na Mwenyekiti wa UWT Taifa Mary Chatanda, wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Kitaifa la Wanawake na Muungano  kuadhimisha Miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lililofanyika katika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam leo 25-4-2024.(Picha na Ikulu)   
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akihutubia na kulifungua Kongamano la Kitaifa la Wanawake na Muungano kuadhimisha Miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,i lililofanyika katika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam leo 25-4-2024.(Picha na Ikulu)
VIONGOZI Wastaafu wa UWT wakifuatilia hutuba ya ufunguzi wa Kongamano la Kitaifa la Wanawake na Muungano lililofanyika leo 25-4-2024 na kufunguliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi, lililofanyika katika ukumbi wa Mlomani City Jijini Dar es Salaam leo 25-4-2024.(Picha na Ikulu)
Na Khadija Kalili ,Michuzi Tv
MKUU wa Mkoa wa Pwani Alhaji Abubakari Kunenge leo amepokea hundi yenye thamani ya Mil.20 kutoka Wakala wa Misitu Tanzania (TFS) ikiwa ni katika muendelezo wa kuchangia watu wa Kibiti na Rufiji ambao wamepata changamoto ya mafuriko yaliyotokana na mvua zinazoendelea nchini kote.

Imeelezwa na Afisa Uhusiano wa TFS Johary Kachwamba kuwa msaada huo umetolewa na Kamishna wa Uhifadhi TFS ikiwa na lengo la kuwapa pole wakazi hao.

Afisa Uhusiano Kachambwa ndiye aliyemkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Pwani Kunenge hundi hiyo ambapo makabidhiano yamefanyika katika viwaja vya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Pwani.

"Wakaazi wa Kibiti na Rufiji ni wenzetu kwani tunazo hifadhi za misitu zaidi ya kumi zenye Hekta 32,000 hivyo ni wajibu wetu kuwapa pole" amesema Kachwamba.

"Tunatoa pole kwa RC Kunenge

Akizungumza mara baada ya kupokea hundi hiyo RC Kunenge ametoa shukrani zake za Mkoa kwa TFS dhati kwa hundi hiyo pia kwa kuwapa eneo ambalo watahamishiwa watu ambao wamepata chagamoto ya nyumba zao kukumbwa na mafuriko katika maeneo ya Kibiti na Rufiji.

"Pia namshkuru Mhe. Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa misaada ya hali na mali aliyowapatia wananchi wa maneo yaliyokumbwa na changamoto ya mafuriko ndani ya Mkoa wa Pwani ,Tunawashukuru TFS kwani fedha hizi zitasaidia kutatua changamoto zilizowakumba wenzetu wa KibitinaRufiji.
Mkuu wa Mkoa wa Pwani Alhaji Abubakari Kunenge akizungumza  na Waandishi wa Habari  Ofisini kwake leo Aprili  25, 2024 hawapo pichani.

Na Khadija Kalili, Michuzi Tv
MKUU wa Mkoa wa Pwani Alhaji Abubakari Kunenge ametoa ratiba ya kuukimbiza Mwenye wa Uhuru ambao utaingia Mkoa wa Pwani Aprili 29 ukitokea Mkoa wa Morogoro.

Akizungumza katika mkutano na Waandishi wa Habari uliofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano leo Aprili 25 amesema kuwa Mwenge huo wa Uhuru utakimbizwa kwa siku saba.

RC Kunenge amesema kuwa baada ya kuupokea Mwenge wa Uhuru utaanza kukimbizwa Aprili 29 ndani ya Halmashauri ya Chalinze na Aprili 30 utakimbizwa Halmashauri ya Bagamoyo huku Mei mosi utaikimbiza Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha na Mei mbili utakimbizwa Halmashauri ya Mji Kibaha Mei tatu utakimbizwa Kisarawe, Mei 4 Mkuranga, Mei tano Mwenge wa Uhuru utakimbizwa Rufiji na Mei 6 utakimbizwa Kibiti huku Mei 7 utakimbizwa Mafia na Mei nane utakabidhiwa Mkoa wa Dar es Salaam.

"Mkoa wa Pwani haturudi nyuma tutakuwa na mipango mizuri zaidi awali ya yote tumegundua changamoto ambazo zimetukabili za mvua hivyo kuna baadhi ya miradi ambayo imebidi tuighairi kutokanaa na mvua.

"Kimkoa tumejipanga vizuri na tunatarajia utakimbizwa katika Wilaya zetu zote tisa pia napenda kuchukua fursa hii kiwaomba wananchi wote wajitokeze kukimbiza Mwenge na kukahikisha tunafanikisha mbio za mwaka huu za mwaka 2024, huku tukitarajia kufumisha upendo,amani utu na heshima.

Amesema pindi mwenge ukikimbizwa Mkoa ni pwani utakua nakauli mbiu za Kuzuia na kuoambana a rushwa ni jukumu lako na langu tutimize wajibu,jamii iunge jitihada za kutokomeza uonjwa wa UKIMWI, Epuka dawa za kukevya zingatia utu boresha tiba na kinga na mwisho Lishe siyo kujaza tumbo zingatia unachokula,

Ziro Malaria inaanza na mimi chukua hatua kuotokomeza.

Top News