Hafla ya Iftar iliyoandaliwa na Kampuni hiyo ikiongozwa na Mkurugenzi Mkuu wake Fatma Abdallah imefanyika jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa wadau mbalimbali wakiwemo wakuu wa taasisi za umma na binafsi pamoja na wateja wa kutoka maeneo mbalimbali nchini.
Mgeni rasmi katika Iftar hiyo alikuwa Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam Alhad Walid aliyewakilishwa na Sheikh wa Wilaya ya Temeke ...
Akizungumza wakati wa Iftar hiyo, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni hiyo Dk Selemani Majige ametumia nafasi hiyo kueleza kuwa ni vema kila Mtanzania kwa nafasi yake kuendelea kuliombea Taifa sambamba na kumuunga mkono Rais Dk.Samia Suluhu Hassan.
"Tunafahamu kwa sasa tunaendelea na Mfungo wa Ramadhan pamoja na Kwaresima hivyo wakati tukiendelea na Mfungo ni vema tukaliombea Taifa letu lakini wakati huo huo kudumisha Umoja,amani na mshikamano,"amesema Dk Majige.
Amesisitiza kuendelea kudumisha amani katika nchini Kunafanya uchumi Wetu kuendelea kuimarika na biashara zetu ziendelee vizuri."Kulinda amani ni jambo kubwa kwani kama hakuna amani basi hata biashara haziwezi kufanyika vizuri.
"Hivyo kupitia mwezi mtukufu wa Ramadhan ni vema kuendelea kumuomba Mungu na kuendelea kumuombea Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ili aendelee kutuongoza na kudumisha amani katika taifa letu."
Pia amewaomba Watanzania kuendelea kutumia mafuta ya Puma Energy Tanzania pamoja na bidhaa zake zote huku akifafanua mafuta ya Kampuni hiyo yana ubora na viwango vya hali ya juu.
"Tunawaomba muendelee kutumia mafuta ya Puma ili tuongeze faida na tukiongeza faida Serikali inapata gawio na inapotoa gawio zinapatikana fedha ambazo zinakwenda kuhudumia jamii katika maeneo mbalimbali,"
Kwa upande wake Sheikh wa Wilaya ya Temeke Sheikh Zailai Hassan Mkoyogole aliyemwakilishwa Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam Walid Alhad Omar aliyekuwa mgeni rasmi, amesema kipindi hiki cha Mwezi mtukufu wa Ramadhan jambo kubwa ni kuzidisha wema kwa maana wanadamu ni wakosaji mbele za Mwenyezi Mungu.
"Binadamu anamkosea Mwenyezi Mungu kwa vitu vingi hivyo sasa ameleta Mwezi mtukufu wa Ramadhan ili kutubu kwa yale yote ambayo ameyafanya.Hivyo kinachotakiwa katika mwezi huu ni kufanya yale yaliyomema na kurejea kwake,"
Pia amesema Mwenye Mungu anapenda kuombwa ,hivyo ametoa mwito kwa watu wote kurejea kwa Muumba kuomba msamaha.
Awali Mkurugenzi Mkuu wa Puma Energy Tanzania Fatma Abdallah amewashukuru wadau waliojitokeza katika futari hiyo huku akitumia nafasi hiyo kuwaomba Watanzania kuwaunga mkono kwa kununua bidhaa za mafuta ya Kampuni hiyo.
Aidha amesema wao kama Puma Energy Tanzania wataendelea kuunga mkono juhudi za Serikali hasa katika kutekeleza matumizi ya nishati safi ili kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi kwa lengo la kuendelea kutunza mazingira .
"Puma Energy Tanzania tunatambua mwelekeo wa Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan na hasa kwenye suala la nishati safi hivyo tutaendelea kuaidia kwa lengo la kuhakikisha mazingira yanalindwa na matumizi ya nishati safi kwa watanzania yanakuwa kipaumbele."
Wakati huo huo Mkurugenzi Mkuu UDA- RT Waziri Kindamba aliyeshiriki futari hiyo amewapongeza kwa kuandaa futari hiyo ni kuwaalika wateja wao ambao wanatumia vilainishi na mafuta.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni ya Mafuta ya Puma Tanzania Dk . Selemani Majige akisalimiana na Mkurugenzi wa UDA-RT Waziri Kindamba pamoja na wageni wengine waalikwa waliohudhuria futari iliyoandaliwa na Kampuni hiyo jijini Dar es Salaam.
Na Mwandishi wetu- Dodoma
Serikali kupitia Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu inaendelea kuratibu utekelezaji wa Mpango wa Taifa wa Dharura wa Kuzuia na Kukabiliana na Madhara ya El Nino kuanzia Septemba 2023 hadi Juni 2024.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Idara ya Menejimenti ya Maafa-Ofisi ya Waziri Mkuu (SBU) Brigedia Hosea Ndagala katika Kikao Kazi cha kujadili utekelezaji wa Mpango wa Taifa wa Dharura wa Kuzuia na Kukabiliana na Madhara ya El Nino Septemba 2023 hadi Juni 2024 ambapo alisema kutokea kwa maafa husababisha madhara ambayo huathiri utendaji kazi, kuzorotesha maendeleo na ukuaji wa kiuchumi kwa wananchi na kupotea kwa mafanikio yaliyopatikana kwa muda mrefu na hivyo, kuzorotesha hatua za maendeleo.
Alisema Maafa hayo yamekuwa yakisabibisha madhara mbalimbali ikiwemo vifo, ulemavu wa kudumu, upotevu na uharibifu wa mali na miundombinu, na ongezeko la tegemezi kutokana na Watoto kupoteza wazazi.
“Nchi yetu imekuwa ikishuhudia matukio ya majanga ambayo yamekuwa yakisababisha maafa na kuathiri mfumo wa kawaida wa maisha ya jamii. Maafa haya yamekuwa yakisabibisha madhara mbalimbali ikiwemo vifo, ulemavu wa kudumu, upotevu na uharibifu wa mali na miundombinu,”Alisema Brigedia huyo.
Aidha Brigedia Ndagala alizitaka kila sekta kuwasilisha tathmini ya utekelezaji wa Mpango wa Taifa wa Dharura wa Kuzuia na Kukabiliana na Madhara ya El Nino ambao una lengo la kuhakikisha serikali na wadau wanachukua hatua stahiki kuzuia au kupunguza madhara na kujiandaa kukabili na kurejesha hali kutokana na maafa yanayosababishwa na El Nino ili kuokoa maisha na mali.
“Hatua hii ni muhimu ili kuweka mikakati ya pamoja kwa ajili ya maandalizi ya msimu wa mvua za Masika. Ni imani yangu kuwa kikao kazi hiki kitatoka na mikakati madhubuti itakayosaidia kuendelea kuongeza ufanisi katika kukabiliana na maafa,” Alieleza.
Mkurugenzi Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Brigedi Hosea Ndagala akizungumza wakati akifungua Kikao Kazi Cha Kujadili Utekelezaji Wa Mpango Wa Taifa Wa Dharura wa Kuzuia na Kukabiliana na madhara ya mvua za El Nino kikao kilichofanyika Jijini Dodoma.
Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Luteni Kanali Selestine Masalamado akichangia wakati wa wasilisho la Madhara yaliyotokana na mvua za El-Nino katika kikao kazi kilichofanyika Jijini Dodoma.
Mkurugenzi wa Udhibiti na Usimamizi wa Ubora wa huduma za hali ya hewa kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) Bw. Geofrid Chikojo akitoa wasilisho kuhusu taarifa ya muelekeo wa mvua za msimu wa masika kwa mwezi Machi hadi Mei 2024 katika kikao kazi kilichofanyika Jijini Dodoma.
Katibu Tawala Msaidizi Mipango na Uratibu Mkoa wa Morogoro Ndug. Anza-Amen Ndossa akichangia mada wakati wa wasilisho lililohusu madhara yaliyotokana na mvua za El-Nino katika kikao kazi kilichofanyika Jijini Dodoma .
Picha ya pamoja ya washiriki wa kikao kazi cha Kujadili Utekelezaji Wa Mpango Wa Taifa Wa Dharura wa Kuzuia na Kukabiliana na madhara ya mvua za El Nino katika kikao kazi kilichofanyika Jijini Dodoma.
Mkuu wa Wilaya ya Ludewa Victoria Mwanziva akiambatana na Mkurugenzi wa Halamashauri, viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) pamoja na wananchi wilayani humo wamefanya Dua/Kisomo Maalum cha kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ili azidi kupata kheri, hekmana baraka.
Akizungumza mara baada ya kufanyika kisomo hicho katika msikiti wa Wilaya ya Ludewa mkuu huyo wa wilaya amesema Rais Dkt. Samia amekuwa ni kiongozi anaye liongoza vyema Taifa la Tanzania hivyo anapopata baraka taifa zima linapata baraka pia kupitia yeye.
"Rais wetu amekuwa ni kiongozi bora na mwenye hekma, hivyo hatuna budi kumwombea kwa Mungu ili aweze kuendeleza ubora alio nao na kile ambacho Mungu amekiweka ndani yake".
Naye Mkurugenzi wa halmashauri ya Wilaya hiyo Sunday Deogratius amempongeza mkuu huyo wa Wilaya kwa kuandaa kisomo hicho kilicho ambatana na futari na kuongeza kuwa Rais Dkt. Samia amefanya maendeleo makubwa katika halmashauri mbalimbali ikiwemo halmashauri ya Wilaya ya Ludewa ambayo imepiga hatua kwenye maendeleo ya elimu, afya, miundombinu ya barabara na sekta nyinginezo.
Aidha kwa upande wake shekhe wa Wilaya hiyo Haruna Rahim amemshukuru mkuu wa wilaya kwa kuwaunganisha katika kufanya kisomo hicho pamoja na kupata futari kwani kwa kufanya hivyo kunaongeza Swawabu kutoka kwa mwenyezi Mungu na hasa katika kipindi hiki cha mfungo wa Ramadhan.
Kisomo hicho cha kumwombea Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kiliambatana na Iftari iliyo andaliwa na mkuu huyo wa Wilaya Victoria Mwanziva katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya hiyo ambapo waumini wote wa kiislamu na wageni waalikwa walijuika pamoja kupata ftari hiyo.
Sanjari na kisomo hicho na futari lakini pia mkuu huyo wa Wilaya alimkabidhi Shekhe Haruna zawadi ya pikipiki aina ya King lion 150 yenye thamani ya shilingi 2,600,000 milion ili iweze kumsaidia katika mizunguko yake mbalimbali huku mbunge wa jimbo la Ludewa akitoa hundi ya shilingi 1,000,000 kwaajili ya ujenzi wa msikiti.