FCOM). Katika uchaguzi huo Tanzania iliwakilishwa na Mkurugenzi wa Miundombinu na Huduma za Ufundi, TMA, , Dkt. Pascal Waniha.
Katika hafla ya Ugawaji wa Taulo hizo uliofanyika katika viwanja vya shule ya Sekondari Nyankumbu Tarehe 18 April, Mgeni Rasmi alikua ni Afisa Elimu Sekondari Cassian Luoga akimuwakilisha katibu Tawala Mkoa wa Geita. Hafla hiyo ilihudhuliwa na viongozi mbalimbali akiwemo Mkurugenzi wa Orica Tanzania, Asha Mambo, Kaimu Mkurugenzi Taasisi ya Victoria Foundation Steven T. Mruma, Mkurugenzi na Mzalishaji wa Taulo za Kike za Palesa Sherie De Wity kutoka Nchini Afrika kusini, Maafisa Elimu wa ngazi mbalimbali , Muwakilishi wa Dawati la Jinsia Kutoka Jeshi la Polisi Afande Christina Katana pamoja na Walimu na Wanafunzi kutoka shule sita za Wilaya Ya Geita Mji.
Taulo hizo za kike zitawanufaisha Jumla ya wasichana 2500 kutoka Shule 25 za mkoa wa Geita kutoka katika Wilaya zote Sita ambapo box moja la taulo za kike linaweza kutumiwa na Mwanafunzi kwa muda wa miaka mitano kwakua Taulo hizo zinaweza kufuliwa na kutumika tena (Re usable), Zilizotengenezwa na kampuni ya Palesa Pads kutoka nchini Africa ya Kusini.
Akizungumza katika hafla hiyo ya ugawaji Mgeni Rasmi Cassian Luoga aliwashukuru Orica Tanzania kwa kufadhili mradi wa Binti Ng'ara chini ya Taasisi ya Victoria Foundation na kuomba wadau wengine wajitokeze kwa wingi ili kusaidia kutatua kabisa tatizo la wasichana kukosa vipindi vya Darasani kutokana na kukosa taulo za kike hasa wakati wakiwa katika hedhi.
Nae Mkurugenzi Wa Orica Tanzania Asha Mambo aliahidi kuendelea kushirikiana na Serikali pamoja na Taasisi zisizo za serikali kukabaliana na changamoto mbalimbali zinazowakabili mabinti.
Akitoa shukrani kwa niaba ya Mkurugunzi wa Victoria, 'Vicky Kamata',Maneja wa Miradi wa Taasisi hiyo Ndugu Steven T. Mruma aliwashukuru Orica Tanzania kwa Ufadhili wa Mradi, na Uongozi wa Mkoa wa Geita kwa ushirikiano mkubwa walioutoa wakati wote wa utekelezaji wa Mradi huo.
Na Mwandishi wetu- Morogoro
Akiongea mjini Morogoro leo Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Bi. Lucy Kabyemera ambaye alimwakilisha Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Jerry Silaa alisema sintofahamu iliyopo haileti afya njema kwa maendeleo ya watumishi wa Wizara yake.
‘’Kwa mujibu wa mkataba ni kwamba vikao vinapaswa kufanyika mara mbili kwa mwaka kwa masikitiko makubwa Wizara yetu imeshindwa kufanya vikao hivyo kwa wakati kutokana na changamoto iliyojitokeza ambayo ni uwepo wa Vyama vya Wafanyakazi viwili ndani ya Wizara yetu’’.Aliongeza Lucy Kabyemera Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi.’’
Naibu Katibu Mkuu Kabyemera aliongeza kuwa hali ya kuwa na Chama zaidi ya kimoja ndani ya Wizara ilitokana na uamuzi wa Serikali wa kuwahamisha watumishi wa Sekta ya Ardhi kutoka Sekretarieti za Mikoa na Serikali za Mitaa na kuwaleta Wizara ya Ardhi Mwaka 2019.
Bi. Lucy Kabyemera aliongeza kuwa uamuzi huu ulipelekea Wizara kuwa na makundi mawili ya wanachama wa vyama vya wafanyakazi wanaotokana na Chama cha Wafanyakazi wa Serikali Kuu na Afya (TUGHE), ambacho kina wanachama 295 na Chama cha Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa (TALGWU) chenye wanachama 792.
Aidha kutokana na uwepo wa vyama hivyo, Wizara ilikusudia kuunda baraza jumuishi la wafanyakazi ili kuwa na wawakilishi wa vyama hivyo viwili. Hata hivyo, Baraza hili limelazimika kufanyika kwa kibali cha nyongeza kwakuwa bado vyama hivyo havijafikia maridhiano ya kuwa na Baraza shirikishi.
‘’Nawasihi vyama kurejea katika meza ya majadiliano na kuchochea utendaji kazi wa Wizara ya Ardhi kwakuwa vyama vyote ni sehemu muhimu ya Wizara hii. Aidha, nimuombe Msajili wa Vyama vya Wafanyakazi pamoja na Kamishna wa Kazi kusaidia katika kumaliza sintofahamu ya uhalali wa Vyama hivi ndani ya Wizara ya Ardhi, kwakuwa ninaamini vyama vyote vina lengo sawa la kusimamia haki na ustawi wa Wafanyakazi.’’Alinukuliwa akisema Bi. Lucy Kabyemera Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi.
Aidha Naibu Katibu Mkuu huyo kwa niaba ya Waziri Silaa amewakumbusha wajumbe wa Baraza hilo kuhusu vipaumbele vyake tangu alipoingia katika Wizara yake aikibainisha kuwa moja ya vipaumbele ni utatuzi wa migogoro ya ardhi ambapo nilitoa siku 100 kwa kila mtendaji kutatua mgogoro kwenye ngazi yake ya utendaji.
Aidha, Waziri alitoa maelekezo kuhusu usimamizi wa maeneo ya wazi na maeneo ya huduma ikiwemo kuhimiza matumizi sahihi ya ardhi na ubadilishaji holela wa matumizi ya ardhi mfano ujenzi wa vituo vya mafuta, kukamilishwa zoezi la urasimishaji na kuboresha utendaji wa Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya
Mengineyo ni maendeleo ya makazi na upimaji ardhi na utendaji kazi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) na kuwataka wote wanaoguswa na vipaumbele hivi kufanya kazi kwa bidii ili nitakapofanya tathmini ya kila eneo, asiwepo atakayeathirika.
Baraza hili linakutana kujadili kwa kina Makadirio ya Mipango na Matumizi kwa mwaka 2024/2025 na kuweka mipango ambayo inatekelezeka itakayosaidia kuleta maendeleo na kutatua changamoto zinazowakabili watumishi.
Akipokea Magari hayo April 18, 2024 Wilayani Rufiji, Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amempongeza Amiri Jeshi Mkuu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mkuu wa Majeshi kwa magari hayo.
Ameeleza kuwa wamepata misaada ya vyakula lakini kulikuwa na changamoto ya usafiri na Barabara katika kufikia walengwa.
Amesema magari hayo yatasaidia kufika kirahisi maeneo hayo yenye changamoto.
Vilevile Kunenge amepongeza Jeshi kwa kuendelea kulinda mipaka ya nchi na Amani kuendelea kuhudumia Jamii.
Kadhalika Kunenge,amekabidhi magari hayo kwa Wakuu wa Wilaya za Kibiti na Rufiji.
.......
Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa, ya Bunge la Uganda imeipongeza Serikali ya Tanzania kwa uwekezaji mkubwa iliyofanya katika ujenzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma, pamoja na kusifu Amani na Utulivu mkubwa uliopo, kwa kuzingatia idadi kubwa ya wanafunzi wanaosoma chuoni hapo.
Pongezi hizo zimetolewa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Gilbert Olanya, wa Jimbo la Kilak Kusini, Alhamisi tarehe 18 Aprili 2024, walipofanya ziara ya kutembelea maeneo mbalimbali ya chuo hicho pamoja na kufanya mazungumzo na Makamu Mkuu wa Chuo, Prof. Lughano Kusiluka, kwenye ofisi yake iliyopo jengo la Benjamin Mkapa, Dodoma.
Aidha, wamevutiwa na aina ya masomo yanayofundishwa katika Ndaki, Shule Kuu na Taasisi za Chuo, pamoja na namna chuo kinavyoendelea kuwekeza katika kuanzisha programu mpya za masomo zinazoakisi mabadiliko makubwa ya kisekta yanayozingatia utoaji mafunzo wenye kutatua changamoto kubwa za ajira, na matumizi ya teknolojia katika ufundishaji.
Akiukaribisha ujumbe huo, Makamu Mkuu wa Chuo, Prof. Kusiluka amelishukuru Bunge la Tanzania kwa kuona umuhimu wa kuwaleta wabunge hao kuja kujifunza UDOM, na kueleza ni kwa namna gani wabunge hao wana mchango mkubwa katika kuongeza hamasa ya ufundishaji wa lugha ya Kiswahili katika Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki, na kutunga Sera zenye kusaidia nchi hizo kuendana na mabadiliko makubwa ya kisanyansi na teknolojia katika Sekta ya Elimu.
Aidha, amewahamasisha waganda kuja kusoma Tanzania kutokana na uwepo wa mitaala mizuri na masomo yenye kukidhi mahitaji katika soko la Afrika Mashariki na Afrika kwa ujumla.
“Tunayo fursa ya wananchi wa Uganda na nchi nyinginezo za Afrika Mashariki kuja kusoma UDOM. Niwahakikishie tunayo mazingira mazuri na thabiti ya kujifunzia kwa wana Afrika Mashariki kuja kusoma Tanzania. Mazingira yetu, tamaduni na mahitaji yetu yanafanana, kwangu mimi hii ni fursa kwetu sote” alisisitiza
Wajumbe wengine wa Kamati hiyo waliofika kutembelea Chuo Kikuu cha Dodoma ni pamoja na Mhe. Betty Ethel Naluyima, Mhe. Dkt. Isingoma Patrick Mwesigwa, Mhe. Rwemulikya Ibanda Gerald, Mhe. Patrick Ocan na Mhe. Lillian Obiale Paparu.
Wajumbe wa Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa, wa Bunge la Uganda, wakiwa kwenye mazungumzo na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma, Prof. Lughano Kusiluka, ofisini kwake Dodoma.
Wakiwa kwenye picha ya pamoja ni ujumbe kutoka Uganda, wakiwemo wabunge wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa, wa Bunge la Uganda. Katikati ni Mhe. Gilbert Olanya, wa Jimbo la Kilak Kusini, Mwenyekiti wa Kamati; na kushoto kwakwe ni Prof. Lughano Kusiluka, Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma, (aliyevaa Kaunda).
Prof. Lughano Kusiluka akikamkabidhi zawadi ya ukumbusho Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa, Uganda, Mhe. Gilbert Olanya. Wabunge hao walifika kutembelea chuo na kujifunza mambo mbalimbali yanayohusu utoaji wa Elimu ya Juu nchiniTanzania.
Viongozi wa Chuo Kikuu cha Dodoma wakiagana na waheshimiwa wabunge wa Uganda, baada ya kuhitimisha ziara yao chuoni hapo.
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameendelea kutenga fedha za kutekeleza miradi ya nishati ambapo katika kipindi cha miaka mitatu zaidi ya shilingi trilioni 8.18 zilitolewa.
“Maono na maelekezo yake kuhusu usimamizi wa sekta hii yamekuwa na mchango mkubwa katika ufanisi wa shughuli za sekta, katika hili, ninampongeza sana Mheshimiwa Rais kwa kuweka kipaumbele kikubwa katika utekelezaji wa miradi ya nishati.”
“Katika kuhakikisha upatikanaji wa uhakika wa umeme nchini, tayari nchi yetu imeanza kutumia umeme wa bwawa la Julius Nyerere Hydropower Project (JNHPP). Huu ni ushindi na kielelezo tosha kwamba Mama yupo kazini.”
Ametoa pongezi hizo leo jioni (Ijumaa, Aprili 19, 2024) wakati akifunga Maonesho ya Wiki ya Nishati yaliyofanyika kwenye viwanja vya Bunge jijini Dodoma.
Waziri Mkuu amelipongeza Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) kwa kuweza kuzalisha umeme zaidi ya mahitaji yaliyopo sasa. “Leo tarehe 19 Aprili, 2024 uzalishaji wa umeme ni mkubwa. Shirika letu la TAMESCO limemudu kuzalisha umeme zaidi ya mahitaji tuliyonayo na bwawa la Julius Nyerere Hydropower Project limeanza kazi na tayari megawati 235 ziko kwenye mfumo.”
Ameitaka Wizara hiyo iweke mkakati wa kuhakikisha maonesho hayo yanakuwa endelevu ili Waheshimiwa Wabunge waweze kupata fursa ya kuwasilisha hoja zao mahsusi na kutatua kero za wananchi wanaowawakilisha.
Kutokana na kuongezeka kwa idadi ya washiriki wa maonesho hayo ikilinganishwa na miaka miwili iliyopita, Waziri Mkuu ameitaka Wizara hiyo ione uwezekano wa kuandaa maonesho kama hayo katika ngazi ya Mikoa na Halmashauri. “Wakurugenzi wa Kanda na Mameneja wa Mikoa na Wilaya mko hapa. Nendeni mkae na muangalie jinsi ya kutekeleza jambo hilo,” amesisitiza.
Ameitaka Wizara hiyo iweke mkakati wa kuhakikisha wananchi wote wanapata ufafanuzi wa masuala mbalimbali kuhusu fursa zinazopatikana kutokana na miradi inayotekelezwa na sekta ya nishati. “Pamoja na kuyaleta maonesho hapa Bungeni, kuna haja ya kupeleka maonesha kama haya kwenye maeneo ya katiati ya mji ili muweze kuwafikia wananchi wengi zaidi na kujibu hoja zao,” amesema.
Mapema, akimkaribisha Waziri Mkuu kuzungumza na wadau mbalimbali walioshiriki maonesho hayo, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko ameipongeza TANESCO kwa kuendelea kufanya kazi nzuri ya kuhakikisha wananchi wanapata nishati ya umeme.
Naye, Spika wa Bunge la Tanzania, Dkt. Tulia Ackson amesema sekta ya nishati ni kati ya sekta mtambuka kwa sababu inalisha sekta nyingine nyingi na ikitikisika, inatikisa na maeneo mengine pia.
Amesema pamoja na utoshelevu wa umeme kwenye gridi ya Taifa, ili kuwe na maendeleo bado nchi inahitaji umeme wa kutosha na hasa kwenye viwanda na siyo kuwasha taa za majumbani.
Ameitaka Serikali itafute njia ya kutumia vizuri maji yanayotoka kwenye bwa la JNHPP ili yaweze kuwanufaisha wananchi wanaoishi maeneo ya jirani na bwawa hilo. “Bwawa limejaa kwa hiyo Serikali ihakikishe maeneo ya jirani yanapata maji ya kutumia. Tuanzishe gridi ya maji kama ilivyo kwenye gridi ya umeme. Kule chini tutengeneze njia ya kutunza maji kwa ajili ya matumizi ya umwagiliaji na mifugo,” amesema.
Naye, Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Mhandisi Felchesmi Mramba amesema ushiriki wa mwaka huu umevunja rekodi kwani watu zaidi ya 480 walitembelea maonesho hayo ambapo 267 walikuwa ni Waheshimiwa Wabunge.
Ameyataja maeneo ambayo washiriki walikuwa wakiulizia zaidi ni umeme, nishati ya jua, nishati jadidifu, nishati safi ya kupikia, mafuta na gesi.
Amesema ili kujenga uelewa mpana kwa wananchi, wanapanga kuandaa kongamano maalum juu ya gesi asilia ambalo linatarjiwa kufanyika Mei, mwaka huu.