KAMPUNI ya Tanzania(TBL) imedhamiria kuwasaidia wakulima nchini kwa kutambua uwezo wao wa kulisha watu, viwanda, na biashara katika ukanda huu kupitia mikataba ya wakulima iliyoimarishwa.

TBL walifanya hafla ya kushirikisha wadau jana ili kupitia, kuthibitisha na kuwasilisha mapendekezo kwa Serikali ya Tanzania ili kuwezesha mipango ya kimkataba na masoko yenye umuhimu kuwezesha fedha na uwekezaji kwa wakulima na miundombinu ya kilimo na ugavi, hususani nafaka na mazao mengine. ngano, alizeti, soya, nk).

Msukumo wa ushirikiano huo ni kwamba licha ya uwezekano wa Tanzania kuwa kapu la chakula la kikanda na kuwaunganisha wakulima na viwanda vya ndani na vya kikanda vya mazao kwa ajili ya uongezaji thamani na usindikaji, changamoto za uwezo ndani na kando ya mnyororo wa ugavi zinapunguza hili kutokea.

Changamoto hizi kwa kiasi kikubwa husababishwa na upatikanaji mdogo wa fedha na mitaji kwa wakulima, hasa kwa ajili ya uzalishaji wa kilimo, na kwa ajili ya uwekezaji wa miundombinu ya kilimo ili kuongeza tija na kupunguza hasara baada ya kuvuna.

Mpangilio unaopendekezwa wa kilimo cha mkataba unaohimizwa na ushirikiano hutoa kushughulikia mtaji na upatikanaji wa vikwazo vya kifedha na kuwaingiza wakulima zaidi na wasiochukua katika mipango ya kilimo cha mkataba, kuwezesha uwekezaji wa ugavi, na kuongeza nafaka na uzalishaji mwingine wa mazao.

Mnyororo wa thamani wa shayiri nchini Tanzania unatoa jaribio la kwanza la uboreshaji wa mpango wa kilimo cha kandarasi kama ilivyowezeshwa na ushirikiano huo.

Zao hilo linakabiliwa na ukuaji mkubwa wa mahitaji kutoka kwa TBL ambayo inapanua kiwanda chake cha kutengeneza kimea mkoani Kilimanjaro ambacho kitaongeza mahitaji hadi tani 32 kwa mwaka kutoka kwa usambazaji wa sasa wa tani 3.5 kwa mwaka (ukuaji wa karibu wa 10X).

Kwa sasa sekta hii inakabiliwa na changamoto mbalimbali, zikiwemo za uzalishaji mdogo na uwekezaji, ubora usio thabiti, uratibu hafifu baina ya wahusika, ushiriki mdogo wa wakulima, uhaba wa ardhi inayofaa, utafiti na miundombinu duni, mipangilio dhaifu ya mikataba na changamoto za uagizaji wa bidhaa nje ya nchi.

Mfumo wa kimkataba unaopendekezwa unatumika kama suluhu la sekta kama "chombo" muhimu cha kuwezesha sekta hiyo kukidhi mahitaji ya soko yanayoongezeka.

Ili kusaidia kutekeleza majaribio ya shayiri ya kimea, tukio hilo pia liliidhinisha mkakati kwa watendaji wa sekta ya shayiri ili kukidhi mahitaji ya soko la 10X kwa kutumia mfumo uliopendekezwa wa kimkataba.

Majukumu, majukumu na hatua zinazohusiana zinazokubalika zitafafanua "mkataba wa shayiri" au mpango wa utekelezaji kwa wadau wa sekta ambao utatumika kama msingi wa maendeleo zaidi na uboreshaji kupitia ushirikiano unaoendelea.

Tukio hilo ni nyongeza ya warsha ya siku nne ya kubuni iliyowakutanisha wataalam na watendaji ili kuandaa mfumo wa kuboresha kilimo cha mkataba na mkakati wa kukidhi mahitaji ya shayiri.

Timu ya kubuni suluhisho ilijumuisha wawakilishi kutoka wizara za serikali, mashirika, mamlaka za udhibiti, taasisi za fedha na vyama. Huu ni ushirikiano wa kwanza wa namna hii kuimarisha mifumo ya kilimo cha mkataba nchini Tanzania na unatoa thamani na athari kwa washirika na wadau:

Michelle Kilpin ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Bia Tanzania, alisema, “Haja ya TBL kutafuta shayiri ndani ya nchi inaendana na maendeleo ya soko nchini Tanzania ambayo yatawezesha kuongeza uzalishaji wa tani 3,500 za shayiri hadi kufikia karibu tani 20,000 za shayiri kutoka kwa wakulima wengi iwezekanavyo.

"Hata hivyo, kuegemea kutoka kiasi cha sasa hadi kiasi kinacholengwa kutahitaji mabadiliko katika mipangilio ya uuzaji ili kuwezesha uwekezaji katika ubora na uwezo wa mnyororo wa ugavi, kwa kutumia zana za kidijitali kuongeza ufanisi na uwazi, upatikanaji wa fedha kwa wakulima na wengine katika msururu wa ugavi, na ushirikishwaji na uendelevu.”

*Ni katika kutoa vitambulisho Kwa idadi kubwa ya wananchi

Na Chalila Kibuda,Michuzi TV

Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) imesema kuwa katika miaka 60 Muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar mamlaka imepata mafanikio ya kutoa Vitambulisho Kwa idadi kubwa.

Hayo ameyasema Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano Godfrey Tengeneza wakati akizungumza kuhusiana mafanikio ya mamlaka hiyo.

Tengeneza amesema kuwa hadi kufikia kutoa Vitambulisho hivyo kulitokana na kuweka mipango mikakati na kuweza kufanikisha hilo.

Aidha amesema kuwa katika utoaji vitambulisho ulihusisha vitambulisho vya Uzawa asili na vitambulisho vya wageni waliopo nchini na kukidhi vigezo vya Ukazi.

Amesema katika kufanikisha hilo ni pamoja na Serikali ya Awamu ya Sita ya Dkt.Samia Suluhu Hassan kuweka jitihada katika kuhakikisha wananchi wanapata vitambulisho wakati awali walikuwa wakitumia namba.

Tengeneza amesema katika mipango mikakati ilikuwa ni kuimarisha ofisi katika Wilaya na Mikoa ambapo ndio kumefanya matokeo chanya bila kukutana na changamoto katika mchakato wa vitambulisho.

Hata hivyo katika 60 ya Muungano Mamlaka inaendelea na kusajili kwa mujibu wa sheria na kutambua vitambulisho vinahitajika katika utambuzi mbalimbali kwa wananchi katika upatikanaji wa huduma za kijamii na biashara.

Tengeneza amesema ametoa hofu ya wananchi kuwa kupata kitambulisho cha Taifa ni haki hivyo hakuhitaji kutumia gharama na kinachohitajika ni kukamilisha nyaraka zinazohitaji kutokana na muongozo wa fumu.
 

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA)Godfrey Tengeneza akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani kuhusiana na mafanikio katika miaka 60 ya Muungano kwa Mamlaka hiyo jijini Dar es Salaam.

Na Mwandishi W doetu

Serikali ya Tanzania imesema kuwa inatekeleza uhamaji wa hiari wa wananchi kutoka Ngorongoro ili kulinda haki za binadamu na uhifadhi.

Hayo ameyasema Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya UNESCO Tanzania kuwa
Prof. Hamis Malebo wakati akiwasilisha ujumbe Mkutano wa 23 wa Jukwaa la kudumu la Umoja wa Mataifa la Masuala ya Watu wa Asili (UNPFII) nchini Marekani ulichoanza Aprili 15 Aprili, 2024 na kuhitimishwa Aprili 26

Profesa Malebo, ameueleza mkutano huo kuwa, serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilifanya mapitio shirikishi ya hali ya maisha ya wananchi na uhifadhi katika Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (NCA) na kubaini umuhimu wa kuweka uwiano sawa wa uhifadhi wa maliasili na utamaduni, maendeleo ya jamii na maendeleo ya utalii.

Amesema kwa kutambua haki za binadamu, ambazo zimekuwa sauti ya wanaharakati na wahifadhi mbalimbali na kwa kuzingatia masharti ya Katiba yaTanzania na matakwa ya ulinzi na uhifadhi wa Mkataba wa Urithi wa Dunia wa 1972 na sheria za nchi, ni wazi kwamba, wananchi wanaoishi katika Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro wameathiriwa na migogoro ya binadamu na wanyamapori, magonjwa ya wanyamapori, kukosa haki ya kuwa na makazi ya kudumu, kudorora kwa maendeleo ya kijamii na kiuchumi, kukosa maji safi na salama, na umiliki wa ardhi.

Profesa Malebo amesema kwa mfano kuwa katika kipindi cha 2018 hadi 2023 watu 65 waliuawa na 205 walijeruhiwa na wanyama pori kama vile Simba, Chui, Fisi, Kiboko, Nyati na pamoja na Tembo.

Amesema Wananchi walio katika Hifadhi ya eneo la Ngorongoro wanaachwa nyuma katika Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs).

Prof. Malebo ameeleza kuwa, kwa kufuata misingi ya haki za binadamu, Serikali imefanya mashauriano na jamii ya wakazi wa Ngorongoro katika kipindi cha miaka 32 ili kwa pamoja kupata ufumbuzi wa kudumu wa changamoto za kijamii na kiuchumi zinazowakabili wananchi wake wanaoishi katika ardhi ya hifadhi.

Hata hivyo amesema Mikutano ya uhamasishaji imefanyika kuanzia ngazi ya chini hadi ngazi ya tawala za Wilaya na Mikoa juu Wakazi wanaoishi katika walioko katika Mamlaka ya Ngorongoro mbalo ni eneo lililohifadhiwa walipewa elimu kuhusu sheria zinazosimamia utendakazi wa NCA ambazo haziruhusu wala kutoa kibali chochote cha kisheria kwa ajili ya shughuli za kijamii na kiuchumi wala kutoa haki ya umiliki wa ardhi katika eneo hilo la hifadhi ambalo pia ni eneo la Urithi wa Dunia.

Aidha wakazi hao walifahamishwa kuhusu manufaa yanayohusiana na kuhama kwao kwa hiari Kwenda katika maeneo yaliyo nje ya hifadhi nchini Tanzania.
Akifafanua juu ya mkakati wa kuhama kwa hiari.

Prof. Malebo alibainisha kuwa, kwa kuongozwa na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mikataba ya Umoja wa Mataifa, Tamko la Kimataifa la Haki za Binadamu, Mikataba ya Kimataifa ya Haki za Binadamu, maazimio ya vyombo vingine muhimu vya haki za binadamu na Azimio la Vienna, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaunga mkono uhamaji wa hiari wa wananchi kutoka hifadhi ya eneo la Ngorongoro.

Serikali pia inawezesha zoezi hilo na inabeba gharama za uhamaji, fidia na inatoa mkono wa shukrani kwa wananchi wanaohama kwa hiari Kwenda nje ya eneo la hifadhi.

Profesa Malebo amesema Serikali inahakikisha wanajamii wanaoishi katika ardhi iliyohifadhiwa wanasaidiwa kuhama na kwenda kuishi katika maeneo ambayo wataendelea na kutekeleza tamaduni zao kwa uhuru tofauti na ambako kwa sasa wanaishi kwa kukabiliwa na changamoto zinazotishia maisha, utamaduni na kuchochea umaskini.

Prof. Malebo pia aliueleza mkutano huo kuwa, Serikali ya Tanzania imepanga kwa umakini uhamaji wa hiari wa wananchi kutoka katika Hifadhi ya Ngorongoro ambayo ni hatarishi kutokana na ugumu wa maisha na migogoro na wanyamapori jambo ambalo linatoa fursa kubwa za kupunguza maafa na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi kwa wakazi na eneo hilo la Urithi wa Dunia.

Amesema Serikali iliainisha maeneo nje ya hifadhi ambapo wakazi wa Ngorongoro wataweza kuhamia kwa hiari na kuendelea na shughuli zao za kujitafutia riziki kwa amani kama ilivyoainishwa kwenye Katiba ikiwa ni pamoja na kumiliki ardhi na kufanya shughuli za kijamii na kiuchumi.

Wajumbe wengine wa Tanzania wanaohudhuria mkutano huo ni pamoja na Bi. Zuleikha Tambwe, Afisa Mwandamizi wa Mambo ya Nje katika Ubalozi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Bi. Hindu Zarooq Juma, Afisa Mwandamizi wa Mambo ya Nje katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Pellage Kauzeni, Afisa Mhifadhi Mkuu wa Wanyamapori katika Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Agnes Gidna, Kaimu Meneja wa Urithi wa Dunia katika Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro, Bw. Edward Kutandikila, Mwanasheria wa Serikali na Bw. Erick J. Kajiru, Afisa Mwandamizi Mkuu katika Tume ya Taifa ya UNESCO ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
NA EMMANUEL MBATILO,MICHUZI TV

WADAU mbalimbali wa masuala ya Jinsia na Maendeleo wamekutana katika Semina za Jinsia na Maendeleo (GDSS) na kuichambua bajeti ya Ofisi ya Rais (Mipango na uwekeshaji) na kubaini kuwa haijazingatia masuala ya jinsia.

Akizungumza leo Aprili 24,2024 jijini Dar es salaam, wakati wa semina ambazo hufanyika kila Jumatano katika Ofisi za TGNP Mtandao, Mhadhiri Chuo Kikuu Mzumbe Lihoya Chamwali amesema uwekezaji ambao umekuwa unafanyika kwa wanawake haukuzingatiwa hasa kufufua viwanda ambavyo wanawake wamekuwa wakishiriki.

Aidha ameishauri serikali kutoa elimu kwa wananchi kuhusu maswala ya uwekezaji kwani elimu hiyo imekuwa haijulikani kwa watu wengi hasa wanawake.

"Tunaishauri serikali iweke mifumo rafiki na elimu itolewe ili kila mwanamke ambae anaweza kuwekeza aweze kuingia kwenye mfumo na ndio maana tunasisitiza elimu itolewe kwani mifumo mingi ya uwekezaji inafanyika kielektroniki kitu ambacho wanawake wanawake wamekuwa wanaachwa kwa sababu wengi hawana ujuzi wa elimu hiyo". Amesema Chamwali.

Amesema bajeti ya mwaka huu imekuwa ndogo tofauti ya mwaka jana kwani mwaka 2023 bajeti ilikuwa bilioni30 lakini mwaka huu bilioni 17.

Amesema kufuatia na upungufu huo wa bajeti katika kupitia malengo wameona malengo mengi ya mwaka huu ni muendelezo wa malengo yaliyofanyika mwaka jana ikiwemo kupitia uundaji wa sera ya dira ya maendeleo 2050.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa kituo cha maarifa kata ya Majohe Tabu Ally ametoa rai kwa serikali kuwaangali wanawake waliopembezoni ili waweze kujikwamua kiuchumi kwa kuwapa elimu bora ya uwekezaji.

Amesema changamoto kubwa inayowakabili wanawake waliopembezoni ni miundombinu ya barabara kwani wanazalisha lakini wanashindwa kufika sokoni kutokana na uharibifu mkubwa wa barabara hivyo inawalazimu kutumia ghalama kubwa ili kufika sokoni jambo ambalo linawarudisha nyuma kimaendeleo.

"Kila kitu ili kiende ni lazima barabara zipitike na hiyo ndio changamoto ambayo sisi tunalia nayo lakini hata tukiwezeshwa mitaji bado tutashindwa kutokana na hii moundombinu",Amesema Tabu

Naye,Mdau wa maswala ya jinsia kutoka Kigamboni Ayub Sharif amesema serikali inapaswa kutoa kipaumbele kwenye maeneo ambayo nguvu kazi kubwa inatumika ili kuongeza motisha ya ufanyaji kazi.

"Mimi naishauri serikali kuangali maeneo ambayo nguvukazi kubwa inatumia ndio uwezeshaji uanzie kwani tumeona katika sekta ya madini wanawake ndio wachenjuaji wakubwa lakini madini yakipatikana anaenufaika mwingine hii sio sawa serikali inapaswa kuangali swala hili kabla ya kuwekeza kwenye mitambo waweke mazingira mazuri kwa hizi nguvu kazi". Amesema.










SHINDANO la Mtindo wa Maisha (Life style) Kwa Vijana wenye ushawishi Mitandaoni ( BINGWA ) Msimu wa tatu umezundiliwa rasmi Vijana Mikoani wapewa nafasi .

Akizungumza na Wanahabari Leo Aprili 24,024 Ukumbi wa Serena Hoteli Jijini Dar es Salaam wakati wa kuzindua Shindano hilo kwa Msimu wa tatu Meneja wa Shindano hilo Ombeni Phiri amesema Shindano hilo limewapa fursa Vijana wengi mitandaoni kubadilisha maisha kutokana na fursa mbalimbali ambazo wamekuwa wakizipata na hivyo kulazimika Shindano hilo kuendelea kuwepo ambapo msimu huo wa tatu umekuwa wa kitofauti zaidi.

"Misimu miwili imekuwa yenye Mafanikio makubwa zaidi na Vijana wengi wa mitandao kuonesha Maisha yao halisi wanapokuwa kwenye mjengo huo hivyo kwa Msimu huu watatu Umepewa nguvu na Kampuni ya Kubashiri ya Parimatch ili kumsukuma Mshindi huyo kufanya vitu vikubwa zaidi Pape Shindano linapomalizika

Msimu Mpya wa tatu wa show ya Bingwa itatembelea Mikoa mitano kwa ajili ya kutafuta Vijana wengine ambapo maoni mengi yamekuwa yakiwafikia Vijana wakihitaji kushiriki Shindano hilo.

"Msimu wa tatu umefanya Maboresho mbalimbali ikiwemo ongezeko la Mikoa mitano ya washiriki ikiwemo Arusha, Dodoma,Mwanza, Mbeya pamoja na kitovu chenyewe Dar es Salaam.

Pia ameeleza kuwa usahili kila Mkoa utachukua washiriki 10 kila Mkoa na kufatia mchujo katika App ya Startimes (Startimes On) ambapo washiriki 08 watatoka Dar hivyo kukamilisha Jumla ya watakaoingia ndani ya nyumba washiriki 24 huku zawadi ya Mshindi kugharimu zaidi ya Milioni 35 za Kitanzania.

Kwa Upande wake Meneja Masoko wa Kampuni ya Startimes David Malisa amesema Msimu wa tatu utaendelea kuwapa fursa vijana zaidi na Atakaeibuka Mshindi Kampuni ya Startimes itaweza kumpa Ubalozi.

Aidha amewapongeza Kampuni ya Parimatch kuona haja ya kuwapa Moyo Vijana hao wenye ushawishi Mitandaoni kukuza vipaji vyao.

Pia amewataka wateja kulipia vifurushi cha Uhuru elfu 23000 ili kuweza kuona shindano hilo kupitia Tv3 ndani ya King'amuzi cha Startimes.

Nae Meneja Masoko wa Parimatch Levis Paul ameeleza sababu ya Kampuni hiyo kuishika mkono Shindano hilo la " Bingwa".

"Sababu ya Parimatch kuungana na Msimu wa tatu wa Shindano la bingwa ni kutokana na shindano hilo Kuhusisha Vijana na Kauli mbiu ikibeba Jumba la Washindi ambapo Kampuni yetu inalenga zaidi kutafuta Washindi walipo kwa kupitia ubashiri."

Paul ameeleza wao kama Parimatch wanatambua kuwa Washiriki wanahitaji kukaa siku 70 ambapo kila kitu kinahitaji uwezeshwaji kuanzia Malazi na vitu mbalimbali hivyo Tv3 na Startimes peke wanahitaji nguvu ya ziada ya kuendesha Shindano hilo hivyo sisi tumeona tuongeze nguvu hiyo kwa msimu huu wa tatu."

Pia amefafanua zaidi kuwa Wana amini kuwa chapa ya Kampuni hiyo ipo sehemu na sahihi hivyo kudhamini shindano hilo itaongeza na kujiweka kwenye nafasi nyingine nzuri zaidi ya kujitangaza kama Kampuni.
Meneja programu wa shindano la Bingwa Ombeni Phiri akieleza namna Shindano hilo litakavyoshirikisha Mikoa mitano ambayo ni Arusha,Mbeya,Mwanza,Dodoma pamoja na Dar es Salaam
 

Meneja Masoko wa Kampuni ya Startimes David Malisa akizungumza na Wanahabari Leo Aprili 24,2024  Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam  wakati wa Uzinduzi wa Msimu wa tatu wa Shindano la Bingwa ambapo amewataka wateja wa Kisimbuzi cha Startimes kulipia kifurushi ili kuendelea kuona shindano hilo kupitia Tv3
 

Meneja Masoko wa Kampuni ya Parimatch  Levis Paul akizungumza machache mara baada ya Kuzinduliwa kwa Msimu wa tatu wa Shindano la Bingwa ambapo msimu huo Kampuni hiyo ikiwa wadhamini wakuu wa shindano

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda leo amekutana na kufanya mazungumzo na Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa anayeshughulikia Operesheni za Ulinzi wa Amani ( UN Under Secretary General for Peace Operations) Bw. Jean Pierre Lacroix ofisini kwa Mkuu wa Majeshi, Upanga, Jijini Dar es salaam.

Katika mazungumzo yao, Bw. Jean Pierre Lacroix amelipongeza JWTZ na kusema Umoja wa Mataifa unaridhishwa na weledi na utendaji kazi wa JWTZ katika operesheni za ulinzi wa amani sehemu mbalimbali duniani na ameahidi Umoja wa Mataifa kushirikiana na Tanzania ili kuhakikisha amani inadumishwa duniani.

Naye Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Jacob John Mkunda ameushukuru Umoja wa Mataifa kwa kuendelea kuliamini JWTZ na kuwahakikishia kuwa JWTZ liko imara na litaendelea kutekeleza majukumu ya ulinzi wa amani duniani wakati wowote litakapohitajika


Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amewatembelea Mabalozi wa Tanzania wanaoshiriki warsha ya siku 4 ambayo imekamilika mjini Kibaha leo Aprili 24, 2024 kwa kufikia makubaliano mbalimbali ambayo yanalenga kuipaisha diplomasia ya Tanzania duniani.

Dkt. Nchimbi aliwapongeza Mabalozi hao kwa kazi nzuri wanayoifanya ya kuitangaza nchi na kuchangia kwa kiasi kikubwa ongezeko la biashara, uwekezaji na utalii nchini.

Warsha hiyo ambayo ililazimika kumalizika usiku kila siku ilifanyika chini ya uenyekiti wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe January Makamba (Mb) ilijadili mikakati ya kuboresha utekelezaji wa Sera ya Mambo ya Nje na namna ya kutafuta ufumbuzi wa kudumu wa changamoto ambazo zimekuwa kikwazo kufikia ufanisi wa shughuli za Wizara hiyo.

Katika siku zao 4, Mabalozi pamoja na mambo mengine, walipitia mikakati ya Utekelezaji wa Diplomasia ya Uchumi, uendelezaji wa majengo ya ofisi na makazi ya Balozi, Diplomasia ya Umma na Diplomasia ya kidigitali na viashiria vya kupima utendaji (Key Performance Indicators- KPIs).

Mabalozi walieleza kuwa kukamilika kwa nyaraka hizo ambazo hazikuwahi kuwepo Wizarani kabla ni chachu katika mwelekeo mpya wa Utekelezaji wa Diplomasia ya Uchumi.

Mabalozi walisisitiza umuhimu wa kumaliza changamoto za kimawasiliano baina yao na wadau ambazo zimekuwa kikwazo za kukamilika kwa wakati kwa fursa na miradi ambayo imekuwa ikiletwa nchini. Changamoto nyingine kubwa ambayo Mabalozi wamesisitiza itafutiwe ufumbuzi ni uwezo mdogo wa nchi yetu wa kuzalisha bidhaa za kukidhi soko katika maeneo yao ya uwakilishi.

Waheshimiwa Mabalozi walisema kuna soko kubwa la nyama, maparachichi, korosho, mchele na bidhaa nyingine lakini hakuna bidhaa za kutosha nchini za kulisha soko hilo.

Mabalozi katika warsha hiyo walipata fursa ya kusikiliza nasaha za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa njia ya mtandao ambaye aliwataka kuwa jicho la Tanzania katika maeneo yao ya uwakilishi ili nchi isipitwe na mabadiliko yanayotokea duniani.

Aidha, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses Kusiluka alifika katika warsha hiyo na kuwambia Mabalozi kuwa wapo katika Wizara iliyokusanya watu wenye taaluma, ujuzi, uzoefu na historia ya kutoka sekta tofauti mchini. Aliwasihi washirikiane kutumia fursa hiyo kuharakisha mabadiliko ndani ya Wizara ya Mambo ya Nje na kutatua changamoto zinazowakabili.

Taasisi kadhaa pia zilialikwa na kuwasilisha mada kuhusu shughuli za ofisi zao ambazo ni Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) na Benki ya Azania.

Warsha hiyo pia wakati wa ufunguzi, walikaribishwa Mabalozi wastaafu ambao walipata fursa ya kubadilishana uzoefu na Mabalozi wa sasa kwa lengo moja tu la kujengeana uwezo wa kukuza na kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia baina ya Tanzania na mataifa mengine, mashirika ya Kikanda na Kimataifa.

Waziri Makamba ambaye ana muda wa takribani miezi 7 tokea ahamishiwe Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki amesema Wizara inaweza kufanya zaidi kuliko inavyofanya hivi sasa. Hivyo, warsha hiyo iliandaliwa ili kupigana msasa wa kufikia nchi ya ahadi.







Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimkabidhi Mama Salma Kikwete Nishani ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambayo aliipokea kwa niaba ya Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Serikali ya Awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kwenye hafla iliyofanyika katika Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 24 Aprili, 2024. Nishani ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere hutunukiwa kwa Wakuu wa Nchi Wastaafu (hai au marehemu) wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania walioingia madarakani kwa njia ya kikatiba na wameendelea kuonesha Maadili mema yenye nidhamu, heshima na mfano wa kuigwa.
 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimkabidhi Mama Janeth Magufuli Nishani ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambayo aliipokea kwa niaba ya Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Serikali ya Awamu ya Tano Hayati Dkt. John Pombe Magufuli kwenye hafla iliyofanyika katika Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 24 Aprili, 2024. Nishani ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere hutunukiwa kwa Wakuu wa Nchi Wastaafu (hai au marehemu) wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania walioingia madarakani kwa njia ya kikatiba na wameendelea kuonesha Maadili mema yenye nidhamu, heshima na mfano wa kuigwa.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimtunuku na kumvalisha Nishani ya Mwenge wa Uhuru Daraja la Pili Makamu wa Kwanza wa Rais na Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Samwel Malecela kwenye hafla iliyofanyika katika Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 24 Aprili, 2024.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimtunuku na kumvalisha Nishani ya Mwenge wa Uhuru Daraja la Pili Makamu wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mohamed Gharib Bilal kwenye hafla iliyofanyika katika Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 24 Aprili, 2024.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimtunuku na kumvalisha Nishani ya Mwenge wa Uhuru Daraja la Pili Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Serikali ya Awamu ya Tatu Mhe. Frederick Tluway Sumaye kwenye hafla iliyofanyika katika Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 24 Aprili, 2024.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizindua Kitabu cha Miaka 60 ya Historia ya Ofisi ya Makamu wa Rais kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 24 Aprili, 2024.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Wageni pamoja na viongozi mbalimbali kabla ya kuzindua Kitabu cha Miaka 60 ya Historia ya Ofisi ya Makamu wa Rais pamoja na Kitabu cha Safari za Picha ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa miaka 60 kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 24 Aprili, 2024.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizindua Kitabu cha Safari za Picha ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa miaka 60 kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 24 Aprili, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akionesha vitabu vya Miaka 60 ya Historia ya Ofisi ya Makamu wa Rais pamoja na Kitabu cha Safari za Picha ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa miaka 60 mara baada ya uzinduzi kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 24 Aprili, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza jambo na Rais wa Zanzibar Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi wakati wa hafla ya uzinduzi wa Kitabu cha Miaka 60 ya Historia ya Ofisi ya Makamu wa Rais pamoja na Kitabu cha Safari za Picha ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa miaka 60 kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 24 Aprili, 2024.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwapa vitabu vya Miaka 60 ya Historia ya Ofisi ya Makamu wa Rais pamoja na Kitabu cha Safari za Picha ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa miaka 60, Mama Hasna Kawawa mjane wa Waziri Mkuu Mstaafu Hayati Rashid Mfaume Kawawa (kulia) na Mama Fatuma Jumbe Mjane wa Rais wa Pili wa Zanzibar Hayati Aboud Jumbe Mwinyi kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 24 Aprili, 2024.

Mmoja wa Waandishi wa Kitabu cha Safari za Picha ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Balozi wa Tanzania nchini Italia Mhe. Mahamoud Thabit Kombo akizungumza kabla ya uzinduzi wa Kitabu hicho kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 24 Aprili, 2024.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimpa Rais Mstaafu wa Zanzibar Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein vitabu vya Miaka 60 ya Historia ya Ofisi ya Makamu wa Rais pamoja na Kitabu cha Safari za Picha ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa miaka 60 kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 24 Aprili, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa ameshika Kitabu cha Safari za Picha ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa miaka 60 mara baada ya kukizindua kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 24 Aprili, 2024.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amemvalisha nishani ya Kumbukumbu ya miaka 60 ya Muungano Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Mzee Ramadhani Nyamka leo Aprili 24, 2024 Ikulu chamwino Jijini Dodoma

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo amewaongoza viongozi na wananchi wa Mkoa wa Dodoma katika mapokezi ya viongozi wa dini waliosafiri kwa treni ya mwendokasi wakitokea Dar es Salaam leo Aprili 21, 2024.

Viongozi hao wanatarajia kushiriki ibada maalumu ya kuliombea Taifa itakayofanyika katika Uwanja wa Jamhuri Aprili 22, 2024 na kuongozwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango.

Akizungumza mara baada ya treni hiyo kuwasili, Dkt. Jafo amesema hiyo ni fahari kubwa kwa nchi yetu kupata usafiri huo ambao pamoja ya kwamba unatumia muda mfupi kusafiri lakini pia umewaunganisha Watanzania wote kwani kuna wengine wametoka Pemba na Unguja.

Amesema wakati Taifa linaelekea kuadhimisha miaka 60 ya Muungano hayo ni mafanikio makubwa katika sekta ya usafiri kwani kupitia Muungano wananchi wa Tanzania Bara na Zanzibar wanajenga uchumi kwa mafanikio makubwa ya nchi.

Dkt. Jafo ameongeza kuwa kwa vile Serikali imefanya uwekezaji mkubwa wa reli ya kisasa imeona ni jambo la heri viongozi wa dini wawe wa kwanza kupanda chombo hicho wakati wanakwenda kuliombea Taifa.

Amesema Tanzania ni Taifa la mfano duniani ambalo wananchi wake kutoka Bara na Zanzibar wameungana na kujenga uhusiano wa damu ambao umedumu kwa kipindi kirefu.

“Ndugu zangu najua mmetoka mbali tunawakaribisha sana Dodoma, lakini naomba niwaambie viongozi wa dini Serikali inayoongozwa na Rais Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan inawapenda sana na kesho tutakuwa na maombi ya kuliombea Taifa letu kwa tunu ya Muungano tuliyonayo,” amesema.

Akielezea namna maadhimisho hayo yatakavyoadhimishwa, Dkt. Jafo amesema kuwa Serikali imeamua kufanya maombi maalumu tarehe 22 na tarehe 24 kutakuwa na tuzo maalumu kwa waasisi wa Muungano, tarehe 25 kutakuwa shamrashamra za Muungano jijini Dar es Salaam na kufuatiwa na kielele cha maadhimisho hayo Aprili 26, 2024.

Miongoni mwa waliosafiri na treni hiyo kutoka jijini Dar es Salaam ni Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Mhandisi Cyprian Luhemeja pamoja na watendaji kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais.

Viongozi walioshiriki katika mapokezi hayo ni Naibu Katibu Mkuu (Muungano) Ofisi ya Makamu wa Rais Bw. Abdallah Hassan Mitawi, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamule na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Jabir Shekimweri. 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo akimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamule wakati wakisubiri treni ya majaribio iliyobeba viongozi wa dini waliosafiri kwa treni ya mwendokasi wakitokea Dar es Salaam leo Aprili 21, 2024. Katikati ni Naibu Katibu Mkuu (Muungano) Ofisi ya Makamu wa Rais Bw. Abdallah Hassan Mitawi.
 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo akiongoza viongozi na wananchi wa mkoa wa Dodoma katika mapokezi ya treni ya mwendokasi ya majaribio iliyobeba viongozi wa dini waliosafiri kwa treni ya mwendokasi wakitokea Dar es Salaam leo Aprili 21, 2024
 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo akisalimiana na viongozi wa dini wakati wakiwasili mkoani wakitokea Dar es Salaam kwa treni ya kisasa ya mwendokasi ikitokea Dar es Salaam leo Aprili 21, 2024.
 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo akizungumza na viongozi pamoja na wananchi wakati wa mapokezi ya treni ya mwendokasi iliyobeba viongoza wa dini waliowasili mkoani Dodoma wakitokea Dar es Salaam leo Aprili 21, 2024.
 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo akiwa katika picha ya pamoja na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Dodoma SACP Theopista Mallya mara baada ya mapokezi ya treni ya mwendokasi iliyobeba viongoza wa dini waliowasili mkoani Dodoma wakitokea Dar es Salaam leo Aprili 21, 2024.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo na Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Mhandisi Cyprian Luhemeja wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamule mara baada ya mapokezi ya treni ya mwendokasi iliyobeba viongozi wa dini waliosafiri wakitokea Dar es Salaam leo Aprili 21, 2024 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo akitoa maelezo kuhusu kitabu cha Miaka 60 ya Historia ya Ofisi ya Makamu wa Rais kabla ya kuzinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma Aprili 24, 2024.
 

Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Mhandisi Cyprian Luhemeja akitoa utambulisho mfupi wakati wa hafla ya uzinduzi wa Kitabu cha Miaka 60 ya Historia ya Ofisi ya Makamu wa Rais pamoja na Kitabu cha Safari za Picha ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliyoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma Aprili 24, 2024.
 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo akiwa na mawaziri mbalimbali hafla ya uzinduzi wa Kitabu cha Miaka 60 ya Historia ya Ofisi ya Makamu wa Rais pamoja na Kitabu cha Safari za Picha ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliyoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma Aprili 24, 2024.
 

Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Mhandisi Cyprian Luhemeja (kulia) akiwa na Naibu Katibu Mkuu (Muungano) Bw. Abdallah Hassan Mitawi na Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Bi. Christina Mndeme wakiwa katika hafla ya uzinduzi wa Kitabu cha Miaka 60 ya Historia ya Ofisi ya Makamu wa Rais pamoja na Kitabu cha Safari za Picha ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliyoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma Aprili 24, 2024.


Top News