Na Khadija Kalili, Michuzi Tv
ASKARI wawili wa Jeshi la Zimamoto na uokoaji wamejeruhiwa wakiwa katika harakati za kuokoa marehemu waliokuwa wamenasia kwenye gari baada ya kuzuka moto ghafla na magari kuwaka moto .

Hayo yamesemwa leo Machi 28 na Kamanda wa Polisi Mkoa Mkoa wa Pwani (SACP) Pius Lutumo alipozungumza na Waandishiwa Habari.

RPC Lutumo amewataja askari waliojeruhiwa kuwa ni Koplo Elias Bwire na Koplo Hamisi Kungwi wote wamekimbizwa Hospitali ya Taifa Mloganzila kwa matibabu na hali zao zinzendelea vizuri.

" Machi 28 mwaka huu majira ya saa 10:15 alfajiri katika bonde la Ruvu Wilaya ya Kipolisi Mlandizi, Mkoa wa Pwani barabara ya Morogoro, Dar es Salaam gari namba T668 DTF aina ya Scania Kampuni ya Sauli ikiendeshwa na dereva Idd Aloyce (35),mkazi wa Mafinga ikitokea Dar es Salaam kwenda Mbeya liligonga ubavuni lori la mafuta ya Petroli lenye namba za usajiri RAF672N na tela lenye namban RL2594 aina ya Howo lililokuwa linatoka Dar es Salaam kwenda nchini Rwanda likiendeshwa na dereva Mushimana Musiyimana lililokuwa limesimama kupisha gari lililokuwa linakuja mbele yake".

Aidha basi hilo lilikuwa limeongozana na basi la Golden Deer Kampuni ya New Force lenye namba za usajiri RAF672N na likiendeshwa na dereva aitwaye Burton Jacob (33),.mkazi wa Mbeya ambapo nalo lililigonga kwa nyuma basi la Saul lililokuwa mbele yake na kusababisha vifo vya watu wawili ambao hawakufahamika majina yao na majeruhi watatu ambao ni Salimu Daud (50) mkazi wa Mbozi Mbeya, Farida Idrisa (26)mkazi wa Tabata Dar es Salaam na Kiambile Geofrey mkazi wa Uyole Mbeya.

RPC Lutumo chanzo cha ajali hiyo ni uzembe wa madereva wa mabasi yote mawili kushindwa kuchukua tahadhari kwa kuyapita magari mengine lakini pia kushindwa kutunza umbali kati ya gari moja na lingine huku yakiwa yamefatana.

"Pamoja na hayo uchunguzi wa awali unaonesha kuwa chanzo cha moto huo ni hitilafu ya injini ya basi la Saul iliyokua imekita chini baada ya kugonga gari lingine na kuripua petroli wakati wa uokoaji"amesema RPC Lutumo.

"Wito wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani unawataka madereva kutii sheria za Usalama Barabarani kwa mujibu wa taaluma zao na ifahamike kwamba madereva wanachukua dhamana kubwa ya maisha na mali za watu"

Mkuu wa mkoa wa Pwani Abubakari Kunenge amesema atayafungia mabasi yatakayoendelea kuvunja Sheria za Usalama Barabarani baada ya ajali iliyotokea alfajiri ya leo.

RC Kunenge amesema hayo wakati akizungumza na Waandishi wa Habari Ofisini kwake Kibaha Mkoani Pwani, amesema yeye ameamua kwa kushirikiana na wanaotoa lesseni, LATRA na Jeshi la Polisi kuwa wataweka mkakati wa kudhibiti ajali ndani ya Mkoa wa Pwani.

" Mtagundua kuwa Mkoa wa Pwani hii Barabara ni kubwa na mabasi yakitoka kule stendi kuu ya Dar es salaam Mbezi idadi ya mabasi ni mengi yakiwa yamekaguliwa lakini bado hapa pia tunakagua " amesema.















Kocha Mkuu wa Timu ya Tabora United Denis Laurence amesema kuwa katika kipindi cha siku saba tangu alipojiunga na timu anaridhishwa na viwango vya wachezaji kutokana na kujituma kwao kwenye mazoezi uwanjani.

Kocha Laurence amesema kuwa ameshangwaza kuona wachezaji kwa kipindi kifupi tangu alipojiunga na Timu hiyo yenye Makazi yake Mkoani Tabora wanamuonesha ushirikiano wakutosha nakusikiliza kila anachowaelekeza kwenye uwanja wa mazoezi na kwamba hajapata changamoto yoyote hadi sasa.

Ameongeza kuwa ushirikiano ambao wachezaji wanampa unatoa  taswira njema kuelekea kwenye michezo tisa ya Ligi Kuu ya NBC Soka Tanzania Bara pamoja na michuano ya Kombe la Azam Sport Federation dhidi ya Singida Fountain Gate kufanya vizuri kwani ndio mkakati uliopo kwa sasa kama Timu.

“Nafurahi kuona wachezaji wananisikiliza vizuri, tunakwenda sawa ,tunazungumza Lugha moja , kwa huumuda mfupi ambao nimekuwa nao hapa kwangu ni maajabu, wanafuata ninachowaambia lakini pia wanafanyia kazi, hii kwangu ni kubwa sana kama kocha, muhimu nazidi kuwasisitiza kila mmoja ananafasi kwenye kikosi changu cha kwanza” amesema Kocha Laurence.

Ukiangalia kila mmoja anauwezo mkubwa, nahii ni kawaida kwa wachezaji wa  Afrika, muhimu ninachokifanya ni kuwaweka kwa pamoja wacheze kitimu ili tuweze kushinda, morali na hari zao zipo juu hivyo ninafurahia sana kuwepo na wachezaji wangu mazoezini na mazingira yote kwa ujumla.

Aidha katika hatua nyingine Kocha Laurence amesema kuwa hadi sasa tayari ameshapata kikosi chake cha kwanza lakini akasisitiza sio ndio kitadumu milele hapana kwani mfumo wake ni kuhitaji kila mmoja aweze kucheza kweye michezo hii iliyosalia kabla ya kumalizika kwa msimu wa 2023/2024.

Tabora United itakuwa ugenini siku ya Aprili Nne katika Uwanja wa CCM Kirumba Mwanza ikiwakabili Singida Fountain Gate kwenye mchezo wa ASFC na badae Aprili 14 katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC dhidi ya JKT Tanzania utakaopigwa katika Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi hapa Mjini Tabora.

Imetolewa leo Machi 28

Na Christina Mwagala

Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano

Tabora United


Na MWANDISHI WETU


WAWEKEZAJI kutoka China wamekutana na Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) na kujadiliana kuhusu uwekezaji hususan katika uzalishaji wa Nishati safi ya kupikia kwa lengo la kumuunga mkono Rais Samia Suluhu Hassan kuhamasisha matumizi ya nishati ya kupikia.

Wawekezaji hao waliongozwa na Shen Don kutoka Jimbo la Shangzhou ambapo wakiwa nchini wlikutana na wadau mbalimbali kutazama fursa za uwekezaji.

Kundi hilo la wawekezaji wameridhia kufanya uwekezaji wa zaidi ya dola za Marekani milioni 312 (zaidi ya sh. bilioni 800) katika maeneo ya nishati, afya, ujenzi, kilimo na vifaa vya uchakataji viwandani

Kutokana na hatua hiyo, UWT inaamini hiyo itakuwa fursa nzuri kwao kuwafikia na kuwawezesha wanawake kiuchumi.

Akizungumza na waandishi wa habari katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Lumumba jijini Das res Salaam, jana, Katibu Mkuu wa UWT, Jokate Mwegelo alisema wawekezaji hao ambao ujio wao umeratibiwa na Kampuni Canopus Energy Solution, wameonyesha utayari wa kushirikiana katika eneo la uzalishaji wa Nishati mbadala na maeneo mengine ya kimkakati.

“Chama Cha Mapinduzi kinachoongozwa na Mwenyekiti wetu Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kilizielekeza jumuiya zote Chama kutazama na kujiendeleza kupitia fursa mbalimbali, hii kwetu ni fursa tumejipanga kuzalisha nishati mbadala kupitia makaa yam awe.

“Wenzetu hawa wameonyesha utayari, tumefanya mazungumzo ya awali na wametualika kwenda China katika maeneo yao ya uzalishaji wa huduma na bidhaa mbalimbali kujionea namna walivyo tayari kutokana na maendeleo ya teknolojia,” alisema.

Alieleza kuwa UWT ina dhamana kubwa ya kuwaendeleza wanawake wa Tanzania kupitia fursa mbalimbali, hivyo imejipanga kuunga mkono juhudi za kumtua mama kuni kichwani kwa kutengeneza mkaa mbadala ambao ni salama kwa afya za binadamu.Kwa mujibu wa Jokate mbali na nishati mbadala, pia wanatazama uwezekano wa wa kushirikiana na wadau hao katika sekta ya madini lakini hilo litafanyika baada ya hatua mbalimbali kutekelezwa ili kuwa na ushirikiano wenye tija.

Jokate alisisitiza kwamba UWT imejipanga kutengeneza fursa ambazo zitawanufaisha wanawake katika sekta mbalimbali hususan uchumi ambao utawainua na kimaisha.

"Fursa yoyote tunayoitengeneza lengo letu ni kuona wanufaika wa kwanza wanakuwa wanawake wa Tanzania,” alisema.

Kwa upande wake Mhandisi Anna Nyangasi kutoka Kampuni ya Canopus Energy Solution, alisema ujio wa ujumbe huo ni fursa kwa uwekezaji katika sekta mbalimbali.

Anna alieleza kuwa wawekezaji hao waliongozwa na Shen Don kutoka Jimbo la Shangzhou ambapo ukiwa nchini ulikutana na wadau mbalimbali kabla ya jana kukamilisha ziara yao kwa kukutana na UWT ambapo wanaamini kuna kundi kubwa la wanawake ambalo linahitaji kuwa sehemu ya mabadiliko kutokana na uwekezaji unaoweza kufanywa na wawekezaji hao.

Kwa mujibu wa Anna, wawekezaji hao wameridhia kufanya uwekezaji wa zaidi ya dola za Marekani milioni 312 (zaidi ya sh. bilioni 800) katika maeneo ya nishati, afya, ujenzi, kilimo na vifaa vya uchakataji.

Pia, alisema ujumbe huo umeonesha nia kushirikiana na kutafuta wawekezaji katika maeneo takribani manane ambayo ni viwanda vya kuunganisha zana za kilimo (pawatila), kuzalisha vifaa vya trekta, majenereta, pampu za maji, vifaa tiba, viwanda vya bidhaa za umeme na ‘paneli’ za kuhifadhi baridi.

Mhandisi Anna alisema ujumbe huo wa watu 11 unahusisha wafanyabiashara, wawakilishi kutoka serikalini pamoja na ujumbe wa CCP, uliwasili nchini kwa mwaliko wa Canopus Energy Solution kwa kushirikiana na Kampuni ya Amec Group.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Jokate Mwegelo (kushoto) akisalimiana na ujumbe wa wafanyabiashara  kutoka China waliongozwa na Shen Don kutoka Jimbo la Shangzhou (wa pili kulia) baada ya kufika katika ofisi za Chama Cha Mapinduzi(CCM) zilizopo Lumumba jijini Dar es Salaam








Na. Vero Ignatus, Arusha

Katibu Mkuu mtendaji wa Smaujata amewataka Viongozi kusimamia vyema nafasi walizonazo sambamba na kuwa barua njema kwa kila anayewasoma

Ameyasema hayo katika kikao cha Viongozi wa Smaujata mkoa kilichofanyika Jijini Arusha, ambapo aliwataka kutambua kuwa Uongozi ni majukumu poa ni mgumu,kwani hawawezi kupendwa na kila mtu badala yake kila mmoja wao atambue nafasi yake, waitumikie jamii kwa moyo wa huruma,kwa kusimamia haki, pamoja na kuwa na kifua cha kubeba mambo.

Aidha aliwataka Viongozi hao wajitahidi kuwa waadilifu kwenye nafasi zao, watafute namna wanaweza kutengeneza utaratibu wa kufuatilia mambo pamoja na kutoa nafasi kwa wengine, zaidi kufahamu mipaka yao ya kiutendaji.

"Ninyi kama Mashujaa na Viongozi ni vyema kutambua kwa kupitia uzoefu wa namna moja ama nyingine mnaweza kuangalia namna gani njema ya kutatua changamoto"alisema Injinia Juliana

Akisoma ripoti ya utendaji wa kazi katika mkoa Kaimu Katibu wa Smaijata
Lussa Melembuki alisema kuwa hadi sasa wameweza kufikia jumla ya shule za msingi zaidi ya 246,shule za sekondari zaidi ya 118,Makanisa 42, wamefanya semina 12 pamoja na kushiriki zaidi ya matamasha 18 vyote hivyo ni kwaajili ya outta elimu kwa jamii dhidi ya Ukatili

Vile vile ameweza kuushukuru Uongozi wa seriali ngazi ya mkoa kwa kuwapatia ushirikiano mkubwa kwani wamekuwa sababu ya wao kufanikisha kutoa elimu katika jamii, ikiwemo kuwajuza madhara yatokanayo na Ukatili, na mahali sahihi pa Kutoa taarifa endapo wataona dalili ama jambo lolote lenye viashiria vya ukatili.

Aidha ifahamike kuwa Shujaa wa Maendeleo na Ustawi wa Jamii Tanzania ni kampeni mahususi ya Kitaifa kwaajili ya kupinga, kuibua na kutokomeza vitendo vyote vya ukatili katika Jamii zote nchini, kuelimisha Jamii kuondokana na fikra, Imani, Mila na desturi na tamaduni zinazokinzana na Maendeleo.

Baadhi ya malengo ya kampeni hiyo ni kutambua kutengeneza mtandao Jamii, sense uwezo wa kupaza Sauti kupinga nakupambanaa na kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na Watoto, kuelimisha na kurahisisha utambuzi na ufanyiaji kazi viashiria vyote vya ukatili kuanzia ngazi ya Familia.






Katibu Mkuu wa Shujaa wa Maendeleo na Ustawi wa Jamii (Smaujata)nchini Mhandisi Juliana Marko akizungumza na Viongozi wa Wilaya pamoja na wale wa mkoa alipotembelea Jijini hapo kwaajili ya shughuli za kikazi kushoto kwake ni Mwenyekiti wa mkoa wa Arusha Godfrey Zablon.


Katibu Mkuu Smaujata Taifa wa pili kutoka kushoto Juliana Marko akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Mkoa wa Arusha mapema Marchi 27,2024


Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji  Dkt.Taus Kida akizungumza katika mkutano wa masuala ya uwekezaji kati ya Tanzania na China uliofanyika  jijini Dar es Salaam.
Na Mwandishi Wetu
KATIBU Mkuu wa Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji, Dkt. Tausi Kida, amesema kuwa juhudi kubwa zinazofanywa na serikali ya awamu ya sita ya kuhamasisha uwekezaji imefanikisha ongezeko la usajili wa miradi kutoka China kauli ambayo ameitoa wakati wa kongamano la uwekezaji kati ya China na Tanzania, Jijini Dar es Salaam.

Akizungumza katika kongamano hilo, Dkt. Kida ameipongeza China kwa mafanikio yake katika uwekezaji katika miaka ya hivi karibuni. Ameeleza kuwa China ni kuwa miongoni mwa nchi zinazoongoza katika kuleta Uwekezaji wa Kigeni (FDI) nchini Tanzania. Kwa mfano, katika kipindi cha Januari 2021 hadi Desemba 2023, Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) kimesajili miradi 256 yenye thamani ya zaidi ya bilioni 2.4 za dola za Kimarekani, katika sekta mbalimbali kama vile viwanda, ujenzi, kilimo, usafirishaji, na huduma.

Dkt. Kida amewahimiza Watanzania kutumia fursa zilizopo katika kushirikiana na wageni ili kunufaika na kupata ujuzi, huku wakiendelea kukua kiuchumi. Amesisitiza kuwa Ofisi yake iko tayari kutoa ushirikiano ili kuhakikisha sekta ya uwekezaji inaendelea kufanya vizuri na kuleta maendeleo kwa manufaa ya kila Mtanzania. Hii ni sehemu ya malengo ya serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Mkutano huo uliofungwa na Makamu wa Rais Mhe. Dkt. Phillip Mpango, ulihudhuriwa na washiriki zaidi ya 300 ikiwemo kampuni za kibiashara 60 kutoka China na nyingine 240 kutoka Tanzania, lengo likiwa ni kujadili masuala ya biashara na uwekezaji.

"Kongamano hili la Jukwaa la Uwekezaji kati ya Tanzania na China limekuja katika muda ambao nchi hizi mbili zinaadhimisha miaka 60 ya uhusiano wa kidiplomasia na ushirikiano wa kiuchumi, na katika kipindi hiki chote kimeimairisha mahusiano yao kiuchumi ikiwa ni pamoja na kuanzisha Mpango wa Belt and Road Initiatives (BRI), huu ni mpango mkubwa wa kidunia unaohusu uboreshaji wa miundombinu ambao uliasisiwa na serikali ya China mwaka 2013 na utatekelezwa katika nchi zaidi ya 150 ikiwemo Tanzania"amesema Dkt. Tausi Kida, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji.
Makamu wa Rais Dkt.Philip Mpango akifatilia mada wakati wa Kongamano kati ya Tanzania na China lililofanyika jijini Dar es Salaam.
Baadhi washiriki wa kongamano la Uwekezaji  kati ya Tanzania na China lililofanyika jijini Dar es Salaam.

Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTARADE) kwa kushirikiana na Wizara ya Mambo ya Nje na Wizara ya Viwanda na Biashara Imeratibu Semina ya Wafanyabiashara kuhusu fursa ya kuuza bidhaa katika soko la Uingereza kupitia Mpango wa Biashara wa Uingereza na Nchi zinazoendelea (UK-DCTS)

Semina hii ya inayofanyika katika ukumbi wa JNICC ulipo Jijin Dar es salaam. Inalenga kuwakutanisha wafanyabiashara wa Tanzania na nchini Uingereza ili kujenga uwezo wa taratibu na vigezo na hivyo kuwafungulia fursa za Masoko zinazopatikana nchini Uingereza.

Wakimwakilisha Mkurugenzi Mkuu TANTRADE Bi. Latifa M. Khamis, Meneja Uhusiano kwa Umma na Masoko Lucy Mbogoro pamoja na Afisa Biashara (Masoko ya Ndani na Nje ya Nchi) Bw. Deo Shayo wameshiriki Semina hii ambayo imefunguliwa rasmi na Mhe. Waziri wa Viwanda na Biashara Dr. Ashatu Kijaji.
 

Bi. Petronela Mlowe afisa ukaguzi na Mazingira anayefanya kazi uingereza na pia mtaalam elekezi wa Ukaguzi bidhaa
akitoa mada kuhusu namna bidhaa za vyakula vinavyoingizwa Uingereza vinakaguliwa.
Aidha, Bi. Mlowe ametoa hamasa kwa wafanyabiashara wa Tanzania kuuza uingereza na kukuza uchumi
6h





Tanzania imesainia Mkataba wa Ushirikiano na Nchi ya Hungary katika sekta ya maji ili kubadilishana uzoefu wa teknolojia katika sekta hiyo.

Akizungumza leo Machi 28,2024 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe Janury Makamba amesema kwa miaka mingi nchi hiyo inaongoza kwa teknolojia ya juu Duniani katika udhibiti wa maji ikiwemo maji taka,mafuriko na ya kunywa hivyo ushirikiano huo wa karibu utaleta tija kubwa kwa Taifa .

Sambamba na hayo amesema nchi hizi mbili zimekuwa zikifanya biashara hivyo kutafanyika makongamano ya kibiashara, ziara ili fursa zilizopo zifahamike na ushirikiano huo uendelee kudumu siku hadi siku.

"Tanzania ina vivutio vingi vya utalii na Hungary ni chanzo cha watalii kwani tumeshuhudia watalii wengi kutoka nchi hiyo wakija kutalii na miaka iliyopita walikuwa 5000 mwaka jana wakifikia 11000 hivyo kuna ongezeko kubwa kutoka nchi hiyo na kwa kuona hilo tumezungumza kwa kina na kujubaliana kuwa tutasaini usafiri wa anga watalii na wafanyabiashara watatoka moja kwa moja kutoka Hungary kuja Tanzani kwa ndege"Amesema Makamba

Sanjari na hayo amebainisha kuwa Vijana wa kitanzania wamekuwa wakinufaika kwa kupata ufadhili wa kwenda kusoma Hungari pia wamekubalina kunzisha mahusiano ya kituo cha Diplomasi cha kimataifa cha Dkt Salim Ahmed Salimna na chuo cha Diplomasia ambapo itasaidia wanadiplomasia kupata fursa ya kwenda Hungari kuongeza ujuzi.

Waziri Makamba amesema nchi ya Hungary wamedhamiria kuwekeza kwenye kiwanda cha kuwekeza ndege ndogo pale Morogoro na

Aidha nchi ya Hungary imekubali kujenga Ubalozi wao nchi Tanzania uliofungwa miaka ya 1990" hiyo ni moja ya kusaidia kuongeza mashirikiano makubwa baina ya nchi hizo mbili.

Naye Waziri wa Mambo ya nje na Biashara wa Hungary Mhe Peter Szijj'art'o amesema licha ya kufungwa kwa ubalozi lakini bado ushirikiano ikuwa unaendelea hivyo habari njema ni kuwa nchi yao mwaka huu Julay inatarajiwa kuchukua Urais wa Umoja wa Ulaya.




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokea Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka 2022/23 kutoka kwa Bw. Charles Kichere Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma leo tarehe 28 Machi, 2024.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokea Taarifa ya Utendaji Kazi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kwa mwaka 2022/2023 kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi hiyo Kamishna wa Polisi Salum Hamduni Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma leo tarehe 28 Machi, 2024. 


Dar es Salaam - Machi 27, 2024. Katika jitihada za kuongeza upatikanaji na matumizi ya simu janja ili kuziba pengo la kidijitali nchini, makampuni ya Vodacom Tanzania PLC na Benki ya CRDB wamezindua mpango wa kuwezesha Wateja wao kumiliki simujanja zenye ubora kwa gharama nafuu.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mpango huo wa kukopesha simu jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Philip Besiimire, alieleza kuwa kampuni hiyo ya simu inatekeleza mipango mbalimbali ya kupunguza gharama za vifaa vya mawasiliano ili kuwawezesha wateja wake kuhama kutoka kwenye matumizi ya mtandao wa 2G na kumiliki simu zenye uwezo wa 4G na kutumia fursa hiyo ili kunufaika na faida kemkem zinazopatikana kupitia mtandao huo.
"Tukiwa ni mdau na mshirika mkubwa wa sekta ya mawasiliano na teknolojia, Vodacom tunajivunia kuzindua mpango huu na Benki ya CRDB ambayo ni taasisi kubwa ya fedha nchini. Ushirikiano wetu unalenga kuwawezesha wateja kutoka pande zote mbili kupata aina mbalimbali za simujanja kwa bei nafuu na mpango wa malipo kwa awamu kwa kipindi fulani. Ili kujua kama amekidhi vigezo, mteja atatakiwa kupiga *150*00*44# nbaada ya hapo atafanya malipo ya awali na kupewa simujanja. Mkopo huu unaweza kulipwa kwa siku, kwa wiki au kwa mwezi kwa kipindi cha hadi miezi 12 kupitia M-Pesa," alifafanua bwana Besiimire.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela, alisema, “ushirikiano huu baina yetu na Vodacom ni fursa nzuri kwa Watanzania kupata huduma za kifedha na mawasiliano kwa gharama nafuu. Kwa hiyo kama wadau muhimu tunapaswa kuunga mkono juhudi za Serikali ili kuhakikisha wananchi wake wanafaidika na ukuaji na maendeleo katika sekta hizi.” 
Bwana Nsekela aliongeza kuwa, “Kwa mtandao wetu ulioenea nchi nzima, CRDB tumekuwa na mchango muhimu katika maendeleo ya Watanzania kwa kuwezesha upatikanaji wa huduma za kifedha. Hivyo basi, kwa kushirikiana na Vodacom, tutaweza kutoa mchango wetu ili kuongeza matumizi ya simujanja nchini.”


Licha ya juhudi za mamlaka nchini kusogeza huduma za mawasiliano, wananchi wengi bado wanatumia huduma za mtandao wa 2G. Hii inapunguza upatikanaji wa fursa zilizopo mtandaoni pamoja na kufurahia na kunufaika na intaneti yenye kasi zaidi kutoka Vodacom pamoja na bidhaa nyingine za kidijitali.

Matumizi ya simujanja na intaneti yana faida kwa jamii kama vile kukuza ukuaji wa kiuchumi kwa kuwezesha ujasiriamali wa kidijitali na kuchochea uvumbuzi, utafutaji masoko mitandaoni pamoja na kuongeza kipato kwa wananchi wanaoamua kujiajili kupitia dijitali.
Vodacom Tanzania imekuwa ikishirikiana na watengenezaji mbalimbali wa simu za mkononi na taasisi za kifedha ili kuwezesha Watanzania kumiliki simu kupitia mikopo nafuu na mipango rafiki ya malipo kwa mteja. 

Mwezi August 2020, Vodacom ilizindua programu ambayo inawaruhusu wateja wake kumiliki simujanja kupitia mkopo unaolipwa kwa awamu, huku kianzio kikiwa ni Shilingi 20,000 za Kitanzania kwa muda wa miezi 12. 

Bwana Nsekela alimalizia kwamba anaamini kuwa taasisi hizo mbili zina huduma mbalimbali za kibunifu ambazo zitawanufaisha na kuboresha maisha ya wateja wao. Pia alitoa wito kwa Watanzania wanaotumia simu za kawaida na wanataka zenye ubora zaidi kufika katika maduka ya Vodacom na kupata simujanja kwa bei nafuu ili kuendana na kasi ya ukuaji wa uchumi wa kidijitali duniani.
Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), akiongoza mkutano wa Benki ya Dunia wa Jukwaa la Tatu la Kanda ya Afrika Kundi la Kwanza kwa nchi za Kipato cha Kati lililolenga kujadili namna mashirika ya fedha ya kimataifa yanavyoweza kuongeza fedha kuzisaidia nchi za kipato cha kati kufikia maendeleo endelevu ya kiuchumi na kijamii. Mkutao huo umefanyika kwa njia ya Mtandao, kutokea Jengo la Hazina (Treasury Square), jijini Dodoma.
Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), akitoa wito kwa taasisi za fedha za kimataifa kuongeza fedha kwaajili ya kuzisaidia nchi za kipato cha kati wakati akifungua mkutano wa Benki ya Dunia wa Jukwaa la Tatu la Kanda ya Afrika Kundi la Kwanza kwa nchi za Kipato cha Kati lililolenga kujadili namna mashirika hayo ya fedha yanavyoweza kuongeza fedha kwa nchi hizo. Mkutano huo umefanyika kwa njia ya Mtandao kutokea Jengo la Hazina (Treasury Square), jijini Dodoma.
Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia Kanda ya Mashariki na Kusini mwa Afrika, Bi. Victoria Kwaka, akitoa mada wakati wa mkutano wa Benki ya Dunia wa Jukwaa la Tatu la Kanda ya Afrika Kundi la Kwanza kwa nchi za Kipato cha Kati, ambapo Waziri wa Fedha Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) aliongoza mkutano huo uliofanyika kwa njia ya mtandao, kutokea Jengo la Hazina (Treasury Square), jijini Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizaraya Fedha, Bi Amina Khamis Shaaban na Afisa Mwandamizi wa Idara ya Fedha za Nje wa Wizara hiyo, Bw. John Kuchaka, wakifuatilia uwasilishwaji wa taarifa wakati wa mkutano wa Benki ya Dunia wa Jukwaa la Tatu la Kanda ya Afrika Kundi la Kwanza kwa nchi za Kipato cha Kati, ambapo Waziri wa Fedha Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) alikuwa Mwenyekiti wa mkutano huo uliofanyika kwa njia ya mtandao, kutokea Jengo la Hazina (Treasury Square), jijini Dodoma.
(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Fedha)


Na. Peter Haule, WF, Dodoma
WAZIRI wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), ameongoza mkutano wa Benki ya Dunia wa Jukwaa la Tatu la Kanda ya Afrika Kundi la Kwanza kwa nchi za Kipato cha Kati uliolenga kujadili namna mashirika ya fedha ya kimataifa yanavyoweza kuongeza fedha kwa ajili ya kuzisaidia nchi za kipato cha kati ili ziweze kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo katika nchi zao itakayochochea ukuaji wa uchumi na maendeleo ya jamii.

Akifungua mkutano huo uliofanyika kwa njia ya mtandao jijini Dodoma, Mwenyekiti wa Mkutano huo, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba alisema kuwa Dunia inakabiliwa na migogoro mingi na changamoto za maendeleo ya kiuchumi ambazo zinasababisha kutofikiwa kikamilifu kwa malengo ya maendeleo endelevu (SDGs).

Alisema kuwa kupungua kwa nafasi ya kifedha katika kushughulikia migogoro hiyo kunadhoofisha uwezo wa Serikali za nchi hizo kufadhili programu za kijamii, kuharakisha ufufuaji wa Uchumi na pia kuongeza madeni katika nchi hizo.

“Mizozo inayoendelea nchini Urusi na Ukraine, Mashariki ya Kati na baadhi ya nchi nyingine za Afrika imechochea kupanda kwa bei ya vyakula na kuwasukuma mamilioni ya watu kwenye uhaba wa chakula”, alisema Dkt. Nchemba.

Aidha Dkt. Nchemba aliishukuru Benki ya Dunia kwa mchango wake wa kuzijengea uwezo taasisi katika kuyafikia maendeleo endelevu lakini pia kufufua uchumi kutokana na changamoto mbalimbali zinazotokea Duniani.

Vilevile alisema kuwa kukabiliana na changamoto zinazoikumba dunia sio kazi rahisi kwa nchi moja, hivyo ameomba kuwa na nguvu ya pamoja katika Kanda na Bara la Afrika katika kutafuta utatuzi wa changamoto hizo.

Dkt. Nchemba ameishukuru Benki ya Dunia kwa kummwamini kuongoza kikao hicho kikubwa lakini pia amewashukuru viongozi mbalimbali waliotoa mada ambazo zimewafunbua macho kwa kuona fursa zilizopo katika kukuza una kuwezesha biashara na pia kuwa na majadiliano mazuri wakati wa mikutano ijayo ya majira ya kipupwe ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) itakayofanyika mwezi Aprili, 2024 jijini Washington D.C nchini Marekani.

Kwa upande wake Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia anayesimamia Kanda ya Mashariki na Kusini mwa Afrika, Bi. Victoria Kwaka, alisema kuwa katika kipindi cha miaka mitano ilitoa misaada na mikopo nafuu yenye thamani ya zaidi ya dola bilioni tatu kwa nchi za Kanda ya Mashariki na Kusini mwa Afrika.

Alisema kuwa mwaka wa fedha uliopita Benki ya Dunia kupitia Mfuko wa IDA ilitoa dola bilioni 2.4 na kwamba kiwango cha misaada na mikopo hiyo imeendelea kuongezeka na miongoni mwa nchi zilizonufaika na mpango huo ni Tanzania, Kenya na Eswatini.

Aidha, Bi. Kwakwa amevitaja vipaumbele vya Benki hiyo kuwa ni pamoja na kuhakikisha nchi zitapata umeme wa uhakika, kuwa na maendeleo ya kidigitali, upatikanaji wa ajira, mapinduzi ya kiuchumi, kujenga uwezo kwa rasilimali watu na masuala ya elimu.

Baadhi ya Viongozi walioshiriki mkutano huo ni pamoja na Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia anayesimamia Kanda ya Mashariki na Kusini mwa Afrika, Bi. Victoria Kwakwa, Makamu wa Rais wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IFC) Kanda ya Afrika, Bw. Sergio Pimenta, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Dunia, Bi. Anshula Kant, Mawaziri wa fedha na Mipango (Magavana) na wajumbe wengine.

Top News