Windhoek ni mji mkuu wa Jamhuri ya Namibia, upo katikati ya nchi hiyo katika miinuko ya Khomas, kiasi cha mita 1,700 kutoka usawa wa bahari. Idadi ya wakazi wake katika mwaka 2012 ilikuwa 322,500 na inazidi kuongezeka kutokana na uhamiaji wa wananchi kutoka kilka sehemu.
Jiji hili limejengwa miaka ya 1840 sehemu ambayo kuna mto wa maji moto baada ya mhamiaji kutoka Afrika ya Kusini aitwaye Kepteni Jonker Afrikaner kuhamia hapo na kujenga kanisa kubwa. Hata hivyo katika miongo kadhaa baadaye vita vya wenyewe kwa wenyewe vikapelekea kususwa kwa makazi hayo mapya hadi mwaka 1890 baada ya utawala wa Ujerumani chini ya Meja wa jeshi Curt von Francois kuamua kuujenga upya.
Jiji la Windhoek hujulikana na wenyeji kwa jina la Khoekhe (mto wa maji moto) na Otjiherero (mahali pa mvuke) kufuatia kuwepo kwa mto huo wa maji moto. Haijulikani ni wapi jina Windhoek lilikotokea ingawa wengi wanaamini kuwa linatokana na neno la Kiafrikaans Wind-Hoek (kona ya upepo). Wengine wanasema ni Kepteni Jonker Afrikaner aliyetoa jina la Windhoek kufuatia jina la milima ya Winterhoek iliyoko huko Tulbah, Afrika ya Kusini, walikotokea mababu zake.

Windhoek ni mojawapo ya majiji katika bara la Afrika yaliyojengwa kwa mpangillio mzuri na masafi kupindukia. Kwa picha zaidi BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...