Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kulia) akiwa na watendaji kutoka Shirika la Maendeleo la Ufaransa (AFD), Mwakilishi wa Shirika hilo nchini, Emmanuel Baudran (katikati) na kushoto ni Dennis Munuve kutoka Shirika hilo.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo ( wa kwanza kulia) akiwa katika kikao na watendaji kutoka Shirika la Maendeleo la Ufaransa (AFD), Wizara ya Nishati na Madini na Taasisi zake.

Na Teresia Mhagama,

Shirika la Maendeleo la Ufaransa (AFD) limesema kuwa limeshatoa jumla ya Euro milioni 321 kuanzia mwaka 2009 mpaka sasa ambazo ni sawa na wastani wa Euro milioni 50 kwa mwaka kwa ajili ya shughuli za maendeleo nchini na kwamba mpango wake ni kuongeza kiwango hicho ifikapo mwakani.

Hayo yamesemwa na Mwakilishi wa Shirika hilo nchini Tanzania, Emmanuel Baudran wakati alipofika Wizara ya Nishati na Madini ili kuzungumza masuala mbalimbali na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo pamoja na Watendaji kutoka Wizara ya Nishati na Madini na Taasisi zake.

Baudran alieleza kuwa fedha hizo ambazo zimetolewa kupitia mkopo wenye masharti nafuu zimeelekezwa katika Sekta za Maji, Nishati na Miundombinu ya usafirishaji.

BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...