Na Dac Popos, Globu ya Jamii.
Solomon Rondon ameiwezesha Venezuela kutinga hatua ya robo fainali, baada ya kuifungia timu yake bao pekee dhidi ya Uruguay kwenye mchezo wa kundi C. Rondon alifunga bao hilo kunako dakika ya 36 ya mchezo akiuwahi mpira ulimbabatiza mlinda lango wa UruguayFernando Muslera na kugonga mwamba kufuatia shuti kali lililopigwa na kiungo Alejadro Guerra.
Mshambulizi Edison Carvan alikosa nafasi nyingi za kufunga ikiwemo moja aliyobaki yeye na kipa Jose Contreras wa Venezuela.
Katika mechi ya pili Mexico iliichapa Jamaica kwa mabao 2-0 na kutinga hatua ya robo fainali. Ikicheza kwenye uwanja wa Pasadena Rose Bowl na kushuhudiwa na watazamaji wapatao 63, 263, iliwachukuwa Mexico dakika 18 kujipatia bao lililowekwa kimiani na Chicharito kwa kichwa akiunganisha krosi ya Jemenez.
Hilo likawa bao lake la 45 kwa timu yake ya taifa.Kunako dakika ya 65 mchezaji Donaldson wa Jamaica aliangushwa ndani ya sanduku la penati lakini kwa mshangao wa watazamaji wengi mwamuzi alipeta na kuwafanya Jamaica kulalamika sana. Dakika ya 81 Oribe Peratta aliipatia Mexico bao la pili na kufanya matokeo yasomeke 2-0 mpaka mwisho wa mchezo.
Kitim tim cha leo ni
CHILE vs BOLIVIA
PANAMA vs ARGENTINA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...