Kamati za Umoja wa Walimu na Wazazi (UWW) katika Shule za Msingi za Serikali nchini zimefanikiwa kudhibiti utoro, nidhamu na kutofanya vizuri kwa baadhi ya Wanafunzi katika shule hizo kwenye mitihani yao ya kumaliza Elimu ya Msingi. Lilian Lundo wa Idara ya Habari (MAELEZO) anaelezea.
Mwaka 2015 Serikali kupitia Mpango wa Kuinua Ubora wa Elimu Tanzania (Education Quality Improvement Programme –Tanzania (EQUIP-T), ilianzisha Kamati za Umoja wa Walimu na Wazazi (UWW) katika shule za msingi nchini kwa lengo la kujenga uhusiano mzuri kati ya Walimu na Wazazi ikiwa ni njia mojawapo ya kuinua ubora wa elimu.
Aidha, Kamati hizo zilipewa jukumu la kufuatilia maendeleo ya Kitaaluma kwa Wanafunzi, kubuni miradi mbalimbali kwa ajili ya maendeleo ya shule na kubuni klabu mbalimbali ambazo zitawashirikisha Wananfuzi katika kujadili masuala ya kijamii na hivyo kuwavutia Wanafunzi kupenda masomo.
Mpango huo ambao awamu ya kwanza ulianza katika mikoa ya Dodoma, Kigoma, Lindi, Mara, Simiyu, Shinyanga na Tabora, umeleta mafanikio makubwa kimaendeleo ya kitaaluma darasani, kuongezeka kwa nidhamu na kudhibiti utoro jambo ambalo pia limeongeza ufaulu katika mitihani yao ya Elimu ya Msingi.
Kwa mujibu wa wa Mwalimu Mkuu wa Shule ya msingi Uhelela iliyoko Wilaya ya Bahi mkoani Dodoma Bw. Dankan Kamwela, mpango huo umepata mafanikio makubwa katika shule yake ambapo imefanikiwa kupunguza utoro kutoka Wanafunzi 127 sawa na asilimia 30 kwa siku mwaka 2015 hadi Wanafunzi 12 sawa na silimia 8 kwa siku mwaka 2016.
Ameelezea kwamba, kwa kuitumia Kamati ya Umoja wa Walimu na Wazazi (UWW) wamekuwa wakifanya vikao mara kwa mara kwa kuwashirikisha Wazazi na Wanafunzi kujadili maendeleo ya Shule ikiwa ni pamoja na wajibu wa Walimu, Wazazi, na Wanafunzi kwa ujumla.
Amesema, kufuatia vikao hivyo ilibainika kuwa iko haja ya kuweka mikakati itakayosaidia kurekebisha kasoro zote zilizoonekana kuchangia kushuka kwa maendeleo ya kitaaluma, utoro na nidhamu ambavyo kwa pamoja vinasabisha kutofanya vizuri kwa Wananfunzi katika mitihani yao kwenye shule zilizo katika Kata hiyo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...