Mtaalam kutoka Kampuni Tanzu ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) ya GASCO inayojihusisha na usambazaji wa gesi, Mhandisi Mwanaidi Rashid (kulia) akielezea hatua iliyofikiwa ya ujenzi wa kituo Namba I cha gesi ambapo Kiwanda cha Saruji cha Dangote kitaunganishwa na huduma hiyo kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kwenye ziara hiyo.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo ( wa tatu kutoka kulia mbele) na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, Hawa Ghasia ( wa nne kutoka kulia mbele) wakiwa katika picha ya pamoja na kamati hiyo wakati wa ziara hiyo.
Mkurugenzi wa Kiwanda cha Uzalishaji wa Saruji cha Dangote, Hemendra Raithatha (kulia) akimpokea Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo (kushoto) aliyeambatana na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti mara baada ya kuwasili katika kiwanda hicho.
Mkurugenzi wa Kiwanda cha Uzalishaji wa Saruji cha Dangote, Hemendra Raithatha (kulia) akielezea mafanikio na changamoto za kiwanda hicho kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti (hawapo pichani). Wengine kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, Hawa Ghasia na Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Jaji Mstaafu Josephat Mackanja.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...