Mkurugenzi wa Ukodishaji Mitambo na Huduma za Vivuko Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Maselle (katikati) akitoa msisitizo wakati alipokua akizungumza na Mameneja na wakuu wa vituo kutoka wakala huo (hawapo pichani) kabla ya kuwatunuku vyeti baada ya kumaliza mafunzo ya Manunuzi na Usimamizi wa Mikataba yaliyomalizika mwishoni mwa wiki, Kulia ni Mhandisi Dkt Ramadhan Mlinga aliyeendesha mafunzo hayo na kushoto ni Mhandisi Aurelia Ngopa kutoka Temesa. Mafunzo hayo yalifanyika katika chuo cha Uhandisi na Teknolojia (COET) Chuo kikuu cha Dar es Salaam.
Baadhi ya Mameneja na wakuu wa vituo kutoka Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) wakimsikiliza Mhandisi Aurelia Ngopa alipokua akisoma risala kwa mgeni rasmi wakati wa sherehe ya kuwatunuku vyeti Mameneja hao baada ya kuhitimu mafunzo ya Manunuzi na Usimamizi wa Mikataba zilizofanyika mwishoni mwa wiki katika chuo cha Uhandisi na Teknolojia (COET) Chuo kikuu cha Dar es Salaam.
Baadhi ya Mameneja na wakuu wa vituo kutoka Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) wakimsikiliza mgeni rasmi Mhandisi Japhet Maselle alipokua akizungumza nao wakati wa sherehe ya kuwatunuku vyeti Mameneja hao baada ya kuhitimu mafunzo ya Manunuzi na Usimamizi wa Mikataba zilizofanyika mwishoni mwa wiki katika chuo cha Uhandisi na Teknolojia( COET) Chuo kikuu cha Dar es Salaam.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...