Mkazi
wa Mvua, Kisaki mkoani Morogoo, Fredy Masawe (35) ameishinda Sh milioni
86.2 kwa kubashiri kwa usahihi mchezo maarufu kwa ‘Perfect 12’
unaondeshwa na kampuni ya mchezo wa kubahatisha ya M-Bet.
Masawe ambaye ni shabiki wa timu ya Manchester United ya Uingereza alifanikiwa kubashiri kwa usahihi mechi 12 kati ya 17 za mchezo na kufanikiwa kuwa mshindi pekee wa droo ya 20 ya mchezo.
Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Afisa Habari wa Kampuni ya M-Bet, David Malley alisema kuwa Masawe ni mshindi wa tatu kwa mwezi huu kupaza zawadi kiasi kikubwa cha fedha na serikali kupata ya jumla ya Sh milioni 15 kutoka kiasi hicho cha fedha ambacho ni asilimia 18 kwa mujibu wa sheria. “M-Bet ipo kwa ajili ya kuwanufaisha mashabiki wa soka hapa nchini, watashindi kibao wamefanikiwa kubadili maisha baada ya kujishindia fedha nyingi na sasa amekuwa mtu wa kipato kingine tofauti na alivyokuwa awali,” alisema Malley.
Alisema kuwa kiasi cha Sh 1,000 tu kimeweza kumnufaisha Masawe ambaye sasa ataweza kuendesha maisha yake tofauti na kuanzisha biashara mbalimbali. Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa fedha zake, Masawe alisema kuwa atazitumia fedha hizo kwa kupanua biashara yake ya kuuza mpunga.
“Sikuamini nilipoambiwa kuwa nimeshinda kiasi hiki cha fedha, kule kwetu Mvua, tumeweka eneo la kubashiri mchezo huu chini ya mwembe, nimebeki mara nyingi sana, na kupata fedha ndogo ndogo, sikukata tamaa kwa kukosa kushinda na leo nimekuwa mshindi, kwa fedha hizi pia nitamalizia nyumba yangu ya kuishi na kuwa ya kisasa, ” alisema Masawe.
Mke wa Masawe, Elizabeth Chifungo (26) alisema alikuwa anamzui mume wake kucheza mchezo huo kwa kuamini kuwa alikuwa anapoteza fedha. “Nilimzuia sana, akakataa na kuendelea kucheza, nimeamini kuwa michezo hii ya kubashiri ni ya ukweli, nawaomba watanzania kuendelea kubashiriki, kwa ushindi huu, nami nitaongeza mtaji wa biashara yangu,” alisema Elizabeth.
Afisa Habari wa Kampuni ya M-Bet, David Malley (kulia) akimkabidhi hundi mshindi wa mchezo wa Perfect 12, Fredy Masawe (katikati) ambaye amejishindia kitita cha sh milioni 86.2. anayeshuhudia ni baba wa Mshindi huyo, Geofrey Masawe.
Mshindi wa mchezo wa Perfect 12 Fredy Masawe (kushoto) akiwa na mkewe, Elizabeth Chifungo wakifurahia mara baada ya kukabdhiwa zawadi yake. Masawe alishinda kitita cha sh milioni 86.2
Masawe ambaye ni shabiki wa timu ya Manchester United ya Uingereza alifanikiwa kubashiri kwa usahihi mechi 12 kati ya 17 za mchezo na kufanikiwa kuwa mshindi pekee wa droo ya 20 ya mchezo.
Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Afisa Habari wa Kampuni ya M-Bet, David Malley alisema kuwa Masawe ni mshindi wa tatu kwa mwezi huu kupaza zawadi kiasi kikubwa cha fedha na serikali kupata ya jumla ya Sh milioni 15 kutoka kiasi hicho cha fedha ambacho ni asilimia 18 kwa mujibu wa sheria. “M-Bet ipo kwa ajili ya kuwanufaisha mashabiki wa soka hapa nchini, watashindi kibao wamefanikiwa kubadili maisha baada ya kujishindia fedha nyingi na sasa amekuwa mtu wa kipato kingine tofauti na alivyokuwa awali,” alisema Malley.
Alisema kuwa kiasi cha Sh 1,000 tu kimeweza kumnufaisha Masawe ambaye sasa ataweza kuendesha maisha yake tofauti na kuanzisha biashara mbalimbali. Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa fedha zake, Masawe alisema kuwa atazitumia fedha hizo kwa kupanua biashara yake ya kuuza mpunga.
“Sikuamini nilipoambiwa kuwa nimeshinda kiasi hiki cha fedha, kule kwetu Mvua, tumeweka eneo la kubashiri mchezo huu chini ya mwembe, nimebeki mara nyingi sana, na kupata fedha ndogo ndogo, sikukata tamaa kwa kukosa kushinda na leo nimekuwa mshindi, kwa fedha hizi pia nitamalizia nyumba yangu ya kuishi na kuwa ya kisasa, ” alisema Masawe.
Mke wa Masawe, Elizabeth Chifungo (26) alisema alikuwa anamzui mume wake kucheza mchezo huo kwa kuamini kuwa alikuwa anapoteza fedha. “Nilimzuia sana, akakataa na kuendelea kucheza, nimeamini kuwa michezo hii ya kubashiri ni ya ukweli, nawaomba watanzania kuendelea kubashiriki, kwa ushindi huu, nami nitaongeza mtaji wa biashara yangu,” alisema Elizabeth.
Afisa Habari wa Kampuni ya M-Bet, David Malley (kulia) akimkabidhi hundi mshindi wa mchezo wa Perfect 12, Fredy Masawe (katikati) ambaye amejishindia kitita cha sh milioni 86.2. anayeshuhudia ni baba wa Mshindi huyo, Geofrey Masawe.
Mshindi wa mchezo wa Perfect 12 Fredy Masawe (kushoto) akiwa na mkewe, Elizabeth Chifungo wakifurahia mara baada ya kukabdhiwa zawadi yake. Masawe alishinda kitita cha sh milioni 86.2
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...