Na Ripota Wetu, China
MAONESHO ya vivutio vya utalii (China Outboard Travel & Tourism Market – COTTM) kwa mwaka 2018 yameanza leo jijini Beijing China, na kuhusisha  mataifa zaidi ya 150. Tanzania imewakilishwa na Bodi ya Utalii kwa kushirikiana na  Kamisheni ya Utalii Zanzibar wakiambatana na baadhi ya kampuni ya kitalii hapa nchini.

Akizungumza kwa niaba ya  Bodi ya Utalii nchini, Irene  Mville ambaye pia ni Ofisa Utalii habari ameeleza lengo la maonesho hayo ni kutangaza utalii, ambapo Tanzania  inatumia  fursa hiyo kutangaza vivutio vinavyopatikana nchini.  Ameitaja China kama  soko jipya wanalopatikana watalii.

"Kwa kadri uchumi wa China unavyozidi kukua ndivyo idadi ya watalii kutoka China itazidi kuongezeka.  Mwaka 2016 Wachina milioni 120 walikwenda nje ya nchi kutalii na kutumia dola za Kimarekani Bilioni 1.2.

"Hivi sasa nyumbani Tanzania tunaendelea kupokea watalii kutoka China. Idadi ya watalii waliokwenda mwaka 2016 ni 37,000. Ukilinganisha na milioni 120 hiyo idadi ni ndogo sana,"amesema Irene

Aidha,amepongeza ushirikiano mkubwa na hatua kadhaa ambazo zimekuwa zikichukuliwa na ubalozi wa Tanzania nchini China ikiwa ni pamoja na uwepo wa maonesho na makongamano ya kitalii  na kutumia mitandao ya kijamii ya China  kutangaza vivutio vya utalii nchi yetu.
Afisa  Habari - Utalii (Bodi ya Utalii Tanzania) Bi.Irene F.Mville (Kushoto) akizungumza na baadhi ya Wateja waliojitokeza kwa nia ya Utayari wa Kupata taarifa juu ya Vivutio vya Utalii nchini  Tanzania kwenye maonyesho ya vivutio vya utalii yaliyofanyika jijini Beijing nchini China.
 Afisa Mipango kutoka Kamisheni ya Utalii Zanzibar Bw.Hassan Ameir Vuai (Katikati) akitoa huduma kwa moja ya wateja waliotembelea banda la Tanzania kwenye maonyesho ya vivutio vya utalii yaliyofanyika jijini Beijing nchini China.
 Afisa Masoko wa Bodi ya Utalii Tanzania Bw. Eugen S. Malley (kulia) akifafanua jambo mara baada ya kutembelewa na wadau wa Utalii katika banda la Tanzania kwenye maonyesho ya vivutio vya utalii yaliyofanyika jijini Beijing nchini China.
Mkurugenzi wa Hango Trade Company  ambaye pia ni Mtanzania anayesoma nchini China  Bi.Angelina Makoye akitafsiri lugha ya kingereza kwenda kichina wakati akielezea fursa za  Utalii  zilizopo nchini Tanzania kwenye maonyesho ya vivutio vya utalii yaliyofanyika jijini Beijing nchini China.
Umati mkubwa ukiwa umefurika katika banda la Tanzania kwenye maonyesho ya vivutio vya utalii yaliyofanyika jijini Beijing nchini China.
Moja ya Kampuni inayojishughulisha na Shughuli za Utalii hapa nchini, wakimhudumia mteja aliyetembelea Kampuni hiyo.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...