Na Mwandishi wetu, Mihambwe

Afisa Tarafa Mihambwe Gavana Emmanuel Shilatu ametoa angalizo kwa Wajasiliamali wadogo kuhakikisha wale ambao hawana vitambulisho hivyo wanakuwa navyo kwani ndio mkombozi wao kibiashara.

Gavana Shilatu aliyasema hayo kijijini Mihambwe kilichopo kata ya Mihambwe, Tarafa ya Mihambwe wakati akiendelea na zoezi la utoaji wa vitambulisho vya Wajasiliamali kwa ambao wamelipia Tsh. Elfu ishirini.

*"Wajasiliamali wadogo changamkieni fursa hii adimu na adhimu ya kuwa na vitambulisho vitakavyowafanya msisumbuliwe na mkuze mitaji na maisha yenu. Fursa ya wanufaika imeongezeka, tuvichangamkie."* alisema Gavana Shilatu.

Zoezi la utoaji wa vitambulisho vya Wajasiliamali wadogo lilizinduliwa na Rais Magufuli kwa lengo la kuwasaidia Wajasiliamali wadogo wasisumbuliwe na wakuze mitaji yao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...