Mkurugenzi wa Kampuni ya ubashiri wa Matokeo ya mechi mbalimbali Gal's sport betting nchini akizungumza na waandishi wahabari jijini Dar es salaam wakati wa kukabidhi hundi ya fedha kwa mshindi aliepatikana kwenye ubashiri wake.
Mkurugenzi wa Kampuni ya ubashiri wa Matokeo ya mechi Gal's sport betting nchini Hakan Aric akimkabidhi hundi ya fedha shillingi 100,000,000 Mshindi aliebatikana kwenye ubashiri wake Juma yusuph Kadoga mkazi wa chamazi jijini Dar es salaam
Na. Khadija seif, Michuzi TV
MUUZA matunda Juma Kadoga awashauri vijana kutokata tamaa na kuwa imani juu ya matokeo chanya wakati wa kufanya ubashiri wa michezo.
Juma ambae ni kijana mwenye miaka 30 mkazi wa chamazi jijini Dar es salaam mwenye asili ya Tanga anaeishi na mke pamoja na watoto wanne.
Aidha ,Juma ameeleza kuwa Hali ya maisha kiuchumi si nzuri sana kutokana na mahitaji mengi ya kifamilia yakiongezeka siku hadi siku.
"Watoto wanne wanahitaji chakula,mavazi pamoja na kwenda shule ambapo pia fedha kwa kiasi kikubwa hutumika ili kukidhi mahitaji yao na ya nyumbani kwa ujumla,"
Pia ameshukuru Kampuni ya ubashiri wa matokeo ya mechi mbalimbali Gal sport betting kwa kubadilisha maisha yake kwa kumpatia fedha za kitanzania 100,000,000.
"Nina furaha kubwa kuwa mshindi wa kiwango cha fedha Kama hiko na fedha nilizozipata nitazitumia kuwasaidia wazazi wangu walioko Tanga ili nipate baraka zao Kwanza kabla ya kuanza kutafakari ni kwa namna gani nitazitumia fedha zangu za ushindi,"
Hata hivyo Juma anafafanua kuwa maisha yalimpelekea kupoteza ndoto yake ya kujishughulisha na uuzaji wa vifaa vya umeme Jambo ambalo kwa sasa ataweza kulifanikisha kupitia fedha alizozipata
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kampuni hiyo ya ubashiri wa matokeo Hakan Aric amesema mshindi huyo amejishindia kitita cha shillingi Milioni mia moja za kitanzania.
''Viwango vyetu vya ubashiri ni ya Hali ya juu nchi nzima,hata hivyo tutaongeza bidhaa zaidi kwenye wasifu ili kuongeza burudani Jambo litakalo panua wigo wa ushindi kwa wateja wetu".
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...