September 15, 2020 Mgombea Ubunge Jimbo la Mbeya Mjini kwa tiketi ya CCM Dkt. Tulia Ackson akiwa kwenye kampeni katika kata ya igawilo iliyopo jijini humo ambao amewaeleza Wananchi baadhi ya mambo ambayo Serikali imeyabainisha katika Ilani yake endapo wataichagua katika uchaguzi mkuu wa October 28, 2020

“Ndugu zangu wa Mbeya siku zote nimekuwa nikiwaeleza kwamba CCM inahoja na wale wenzetu wanavihoja, tumejipanga kutatua changamoto mbalimbali hapa ikiwemo ujenzi wa miundombinu ya barabara ya njia nne, kumaliza tatizo la maji na umeme, ajira kwa vijana na wakinamama”

“Kuna watu wanasema kwamba eti muogopeni Tulia kama Corona, nimewaambia hao jamaa kwamba mwaka huu hatudanganyiki na ndio maana hata katika kipindi cha Corona yenyewe hao hao watu walikimbia Bungeni. Sasa waambieni hatuwezi kumuogopa Tulia kwasababu hata hiyo Corona yenyewe haipo…”-Dr. Tulia Ackson






 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...