Yassir Simba, Michuzi TV

Uzi mpya wa Yanga waja na baraka zake kwa Mkapa huku Yanga wakimchakaza Mbeya City kwa bao 1-0.

Ligi kuu Tanzania bara VPL imeendelea tena leo Septemba 13,2020 huku Yanga wakitaka na uzi mpya Yani jezi mpya kwa ushindi wa bao 1-0 dhidi ya wanakoma kumwanya Mbeya City, bao la dakika ya 86 likifungwa na beki kisiki wa Yanga Lamine Moro akiunganisha mpira wa Kona uliopigwa na Carlinhos na kuipatia Yanga bao la kuongoza na la ushindi katika mchezo huo.

Mchezo huo uliotawaliwa na ufundi na mbinu kwa asilimia kubwa huku Yanga wakiingia katika mchezo huo na mabadiliko katika kikosi chao wakianza na Lamine Moro,Haruna Niyonzima,Mukoko Tonombe pamoja na Tuisila Kisinda ambao walikuwa chachu ya mabadiliko katika kikosi hicho huku Saprong pamoja Yacouba  wakifanya majaribio kadhaa ambayo mlinda mlango wa Mbeya City Haroun Mandanda akifanya kazi kubwa kuzuia mashambulizi ya Yanga.

Mabadiliko yaliyofanywa na Yanga kumtoa Feisal Salum na nafasi yake kuchukuliwa na Carlinhos ambaye alifanya kazi kubwa katika mchezo huo huku akitoa pasi ya goli ambalo limewapa Yanga alama tatu muhimu katika mchezo huo.

Baada ya ushindi huo Yanga wanashika nafasi ya sita katika msimamo wa ligi wakiwa na alama 4 magoli 2 katika michezo miwili waliocheza huku Mbeya City wao wakiburuza mkia katika nafasi ya mwisho nafasi ya 18 katika msimamo wa ligi.








 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...