NA MWAMVUA MWINYI, CHALINZE.
NAIBU Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari (ICT) - Mhandisi. Andrea Mathew Kundo amemwagiza Mkuu wa Kanda wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Kanda ya Mashariki kushughulikia haraka maombi ya Halmashauri ya Chalinze ya kuimarisha MIundombinu ya mawasiliano.
Hatua hiyo ni pamoja na kupatiwa kibali cha Masafa ya radio (radio frequency) na Televisheni ambayo yalikwama kwa muda. Aidha mbunge wa jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete ameeleza ,Halmashauri ya Chalinze,imepokea vifaa kwa ajili ya kupimia Ardhi.
Vifaa hivyo vinasaidia kurahisisha Upimaji ambapo vitawezesha kwa siku kupimwa kwa viwanja hadi 200 toka utaratibu wa kawaida wa viwanja 5.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...