
Dar es Salaam, Mei 16, 2025 – Kampuni ya Serengeti Breweries Limited (SBL), kwa kushirikiana na Chuo cha Taifa cha Utalii (NCT), wamefanya mahafali ya kwanza ya programu ya mafunzo ya ukarimu kwa vijana chini ya mpango wa SBL wa "Learning for Life", wenye lengo la kuwajengea vijana wa Kitanzania ujuzi wa vitendo katika sekta ya ukarimu na utalii.
Mahafali haya, yaliyofanyika katika kampasi ya NCT jijini Dar es Salaam, yalikutanisha wanafunzi 109 waliohitimu, wadau wa sekta ya ukarimu, pamoja na viongozi wa serikali. Mgeni rasmi wa hafla hiyo alikuwa Mhe. Edward Mpogolo, Mkuu wa Wilaya ya Ilala, huku Mgeni Maalum akiwa ni Mhe. Dkt. Pindi Hazara Chana (Mb), Waziri wa Maliasili na Utalii.
Mpango huu ulioanza Septemba mwaka jana ni sehemu ya mkakati mpana wa SBL wa Society 2030: Spirit of Progress, ukilenga kuwawezesha vijana kupitia mafunzo ya vitendo, masomo darasani na mafunzo kwa vitendo kazini ili wawe tayari kuajiriwa kwenye soko la ajira linalokua la utalii na ukarimu.
Akizungumza katika hafla hiyo, Mhe. Dkt. Pindi Chana alisisitiza umuhimu wa ushirikiano katika kufanikisha malengo ya maendeleo ya taifa kupitia utalii shirikishi:
“Utalii siyo tu kusafiri – ni injini ya ukuaji wa uchumi jumuishi, ajira kwa vijana na kubadilishana tamaduni. Tanzania inalenga kufikia watalii milioni 5 kwa mwaka, na programu kama hizi zinahakikisha tunajenga rasilimali watu sahihi kufanikisha lengo hilo.”
Alibainisha kuwa serikali imeanzisha vifurushi vipya vya vivutio vya utalii, vikiwemo utalii wa chakula, ili kutangaza utajiri wa vyakula vya asili vya Tanzania:
“Watalii wa leo wanatafuta uzoefu wa kweli. Sasa tunawaletea vyakula vya asili vya Kitanzania – ‘vyakula vya asili’ – kama sehemu ya vivutio vya utalii. Kutoka kwenye chakula safi, kisicho na kemikali moja kwa moja kutoka shambani, hadi vyakula vya kipekee vya mikoa mbalimbali, utalii wa chakula utawawezesha watalii kujifunza utamaduni wetu huku pia tukikuza uchumi wa jamii zetu,” alisema Waziri.
Aidha, Dkt. Chana alisisitiza kuwa utalii ni lazima uwe endelevu, shirikishi, na wenye manufaa kwa jamii, huku akipongeza ushirikiano kati ya SBL na NCT:
“Ushirikiano huu ni mfano wa ubunifu tunaouhitaji – ambapo vijana wanapewa ujuzi siyo tu wa ajira, bali wa kujenga taaluma endelevu zinazoweka mbele maadili, utamaduni na huduma bora kwa watalii wetu.”
Mhe. Edward Mpogolo, Mkuu wa Wilaya ya Ilala, naye aliipongeza programu hiyo kwa kuchangia katika jitihada za serikali kukuza sekta ya utalii “Sekta ya utalii na ukarimu nchini Tanzania ina fursa kubwa ya kuzalisha ajira na kuchochea maendeleo ya taifa. Programu kama hii siyo tu kwamba inawapatia vijana wetu ujuzi, bali pia inasaidia kutekeleza dira ya serikali ya kugeuza utalii kuwa nguzo ya maendeleo jumuishi na endelevu. Nawapongeza SBL na NCT kwa dhamira yao ya kuwawezesha vijana wa Kitanzania kwa vitendo.”
Programu hii iliwafundisha wanafunzi ujuzi katika mawasiliano, uongozi, uwasilishaji binafsi, usimamizi wa muda, upangaji wa bajeti na huduma kwa wateja. Kupitia Diageo Bar Academy, walipata pia mafunzo maalum ya uendeshaji wa baa, huduma kwa wateja, na sanaa ya mchanganyiko wa vinywaji (mixology). Ili kuhakikisha uendelevu, SBL ilianzisha pia programu ya kuwajengea uwezo wakufunzi wa NCT (Training of Trainers – ToT), ili waweze kufundisha programu hiyo kwa kujitegemea kwa awamu zijazo.
Dkt. Obinna Anyalebechi, Mkurugenzi Mtendaji wa SBL, alisema:
“Mahafali haya siyo tu kusherehekea mafanikio ya kitaaluma – bali ni wakati wa mabadiliko. Tunajivunia sana wanafunzi hawa na tunashukuru kwa ushirikiano wa NCT. Kupitia ‘Learning for Life’, tunafungua milango ya ajira na kuwawezesha vijana kufanikisha ndoto zao katika sekta ya utalii na ukarimu inayokua kwa kasi hapa Tanzania.”
Dkt. Florian Mtey, Mkuu wa NCT, alisifu mpango huo:“Programu hii imefungua milango kwa wanafunzi wetu. Inawapeleka nje ya darasa na kuwapa uzoefu halisi wa kazi, kuwajengea kujiamini na kuwafanya kuwa tayari kwa soko la ajira la leo. Tunajivunia ushirikiano huu na tunatazamia kuupanua zaidi.”
Mahafali haya ni ushuhuda wa mafanikio yanayopatikana kupitia ushirikiano wa kimkakati kati ya sekta ya umma na binafsi, na ni sehemu ya dhamira ya SBL katika kuendeleza jamii kupitia programu jumuishi na endelevu. Programu ya Learning for Life itaendelea kufikia vijana zaidi na kuimarisha msingi wa sekta ya ukarimu kote nchini.
Na John Mapepele
Kwa mara ya kwanza katika historia ya maadhimisho ya Siku ya Misitu Duniani ya mwaka huu hapa nchini yanayofanyika katika viwanja vya Saba Saba Mjini Njombe Wizara ya Maliasili na Utalii imeandaa maonesho maalum ya mnyororo wa thamani wa sekta ya misitu pamoja na Wanyamapori.
Kwa vipindi tofauti wakikagua maandalizi ya siku ya Misitu Duniani kwenye maonesho Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe Pindi chana na Katibu Mkuu Dkt. Hassan Abbasi wamefafanua kuwa Serikali imeamua kuwaleta Wanyamapori katika maonesho hayo ili kutoa hamasa kwa wananchi kupenda utalii wa ndani.
" Tanzania imebarikiwa kuwa na eneo kubwa la misitu takribani asilimia 50 ambalo ni makazi ya Wanyamapori, hivyo tumeamua kuwaleta wanyama wananchi waweze kupenda kutembelea hivyo kuliingizia taifa letu fedha." Amepongeza Mhe. waziri
Naye Dkt. Abbasi amewaarika wananchi kutembelea maonesho ya Wanyamapori hao na kwamba Serikali imetoa fursa ya wanyama hao kuendelea kuwepo katika viwanja hivyo katika siku za mwisho wa juma hata baada ya kilele hapo kesho ili wananchi wengi wapate fursa ya kuwaona.
Mgeni rasmi hapo kesho ni Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kauli mbiu ya kitaifa ya mwaka huu ni ongeza thamani ya mazao ya misitu kwa uendelevu wa raslimali kwa kizazi hiki na kijacho.
Turaco Collection yashiriki Maonyesho Makubwa ya Utalii yanayofahamika kama ITB -Berlin yaliyofanyika nchini Ujerumani tarehe 4-6 March 2025.
Mkurugenzi wa Mauzo wa Turaco Collection Tanzania, Florenso Kirambata akiziwakilisha hotel zao katika maonesho hayo ya ITB- Berlin anasema kwamba, maonesho hayo ni eneo jema kabisa la kujitangaza kubadilishana uzoefu hasa katika dunia ambayo walaji (watumiaji wa huduma) wamekuwa wakibadilika kutokana na mazingira yanayotokea duniani.
Turaco Collection kwa upande wa Dar es Salaam wana Element By Westin Marriott na Delta By Marriott na kwa upande wa utalii wa kaskazini pamoja na bidhaa mbalimbali za utalii pia wana; Turaco Ngorongoro Valley Lodge Tribute portfolio under Marriott International na Turaco Manyara View Lodge Tribute portfolio under Marriott International na kwa Zanzibar wana Turaco Nungwi Beach Reasort Tribute portfolio under Marriott International na Turaco Spice Tree Stone Town Tribute portfolio under Marriott International na Beyt Aly Salaam-By Turaco.
Viongozi na Wataalamu wa Mfumo wa Anwani za Makazi kutoka Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari (WHMTH), Wizara ya Maliasili na Utalii (WMU) na Wahifadhi na Viongozi wa Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania-TANAPA, wakiwa kwenye kikao cha majumuisho ya zoezi la ukusanyaji wa taarifa za Anwani za Makazi lililofanyika awamu ya kwanza katika Hifadhi za Arusha, Ziwa Manyara na Tarangire tarehe 10 Septemba, 2024 mkoani Arusha.
Viongozi na Wataalamu wa Mfumo wa Anwani za Makazi kutoka Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari (WHMTH), Wizara ya Maliasili na Utalii (WMU) na Wahifadhi na Viongozi wa Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania-TANAPA, wakifuatilia wasilisho kwenye kikao cha majumuisho ya zoezi la ukusanyaji wa taarifa za Anwani za Makazi lililofanyika awamu ya kwanza katika Hifadhi za Arusha, Ziwa Manyara na Tarangire tarehe 10 Septemba, 2024 mkoani Arusha.
Viongozi na Wataalamu wa Mfumo wa Anwani za Makazi kutoka Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari (WHMTH), Wizara ya Maliasili na Utalii (WMU) na Wahifadhi na Viongozi wa Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania-TANAPA, wakifuatilia wasilisho kwenye kikao cha majumuisho ya zoezi la ukusanyaji wa taarifa za Anwani za Makazi lililofanyika awamu ya kwanza katika Hifadhi za Arusha, Ziwa Manyara na Tarangire tarehe 10 Septemba, 2024 mkoani Arusha.

.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)



.jpeg)



.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)



















.jpeg)

.jpeg)








