katika kuonesha umahiri na ubunifu wa hali ya juu ulioipeleka jahazi modern taarab katika bahari kuu ya muziki huo nchini, mzee yusuf na kundi lake sasa wana madansa katika maonesho yao ambao linapopigwa sebene hufanya vitu si vya kawaida jukwaani. hii ilikuwa usiku wa kuamkia leo katika ukumbi wa bwawa la kuogelea wa city garden hotel gerezani (zamani railway club) dar
mzee yusuf akiongoza jahazi wakati wa shoo hiyo kali
mzee yusuf akiongoza jahazi wakati wa shoo hiyo kali
mbunge wa temeke mh. abbas mtemvu alishindwa kujizuia na kuja kumtuza mzee yusuf kwa vitu vyake vya uhakika.
Jahazi litazama kwakuwa ndombolo sasa
ReplyDeleteMh,hii mpya sasa sio kihivyo MZEE unahitaji ubunifu mpya sio huu,kaa chini utafakari wapi ulopojikwaa sio kama hivi
ReplyDeletehongera, kaka kumbe bado upo juu mpaka Mh, kakubali, Jahazi juu juu juu kabisa.
ReplyDeleteNakumbuka zamani nakaa hapo Gerezani nyumba namba 13 (Nyumbani kwa kina Matusi)Tulikuwa hatulali usiku ni makelele ya Bendi au harusi kwenye ukumbi wa Gerezani.Nafikiri uwepo utaratibu wa kutoa huo uchafuzi wa mazingira mpaka sasa tumeadhirika na makelele hayo toka utotoni mpaka sasa!!
ReplyDeleteBrave! lakini hilo koti halikuchomi na joto kweli kaka yangu?
ReplyDeleteTaarab na wanenguaji wapi na wapi??. Mzee Yusuph bibi yako ni Bi kidude nenda akakupe funzo la Taarab mana hii sio Taarab bali ni unashindana na twanga sasa,
ReplyDeletemkubwa Taarab ya sasa ni mabadiliko makubwa sana , taarabu ya zamani Gita si la umeme watu wanakunywa kahawa akuna bia, karibu kwenye maisha ya ki leo, hongera mzee yusuph.
ReplyDeleteHii siyo taarab.
ReplyDeleteWa Gerezani namba 13, Nyumbani kwa kina Matusi.
ReplyDeleteKwanini hukuwauliza wazazi wako kwamba nani kaanza kujenga hapo? hio club au nyumba namba 13?
Kama club ndio ya kwanza kujengwa basi waliyajua toka mwanzo matokeo yake
Hivi mzee unataka kutuhuzunisha sisi wapenzi wako wa sauti yako na taarabu zako,,haijakuwepo taarabu kunengua kama kina werason au twanga pepeta! ah,,labda nafuu uhamie huko tu.Sio ugeuze taarabu iwe ndombolo ya solo.
ReplyDeletemmh! Koti la ngozi bongo?
ReplyDeleteKama hataki nipe mie, nipe mie, nataka paja,haya-yaya-yaya-yaya-yaya-yaya-ya! kipapatio!
ReplyDeleteKhe! mzee yusuph jiachie mwaya,wanaokuponda hawajui taarabu.mabadiliko babu.linawahusu!scince na technolojia.wape vitu.
ReplyDelete