Mkuu wa Wilaya ya Mtwara, Mhe. Abdallah Mwaipaya, aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, amesema hayo wakati wa hafla ya kuhitimisha mbio za Utumishi Marathoni 2025 zilizoandaliwa na Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania Kampasi ya Mtwara. 

Akiwasilisha salamu za Mkuu wa Mkoa, Mhe. Mwaipaya amesema, “Historia ya Chuo cha Utumishi wa Umma ni sehemu muhimu ya mafanikio ya utumishi wa umma nchini. Tangu kuanzishwa kwake mwaka 2000, chuo hiki kimekuwa mhimili muhimu wa kutoa elimu, mafunzo, na ujuzi unaowawezesha watumishi wa umma kutekeleza majukumu yao kwa weledi, uadilifu, na ufanisi.” 

Pia, Mhe. Mwaipaya amepongeza Chuo kwa maandalizi mazuri ya tukio hili na kusema kuwa mbio za marathoni si tu zinaboresha afya na mshikamano, bali pia zinaunda hisia za uzalendo na utu miongoni mwa washiriki. Ameongeza kuwa, “Marathon hii si tukio la michezo tu; ni kumbukumbu hai ya safari ndefu na mafanikio makubwa ambayo chuo chetu kimeipitia kwa kipindi cha miaka 25. Amessitiza kuwa, safari ya miaka ishirini na tano imejengwa juu ya misingi ya nidhamu, ubunifu, ushirikiano, na kujituma kwa manufaa ya taifa letu.”

Naye Makamu Mkuu wa Chuo -Taaluma, Tafiti na Shauri za Kitaalam, Dkt. Hamisi Amani, aliyemwakilisha Mkuu wa Chuo na kuwa Mtendaji Mkuu, amesema kuwa safari ya miaka 25 ya chuo tangu kuanzishwa kwake mwaka 2000 ni jambo la kujivunia. 

“Leo si tu tunakimbia kwa ajili ya afya na umoja, bali tunasherehekea mafanikio, historia, na mchango mkubwa wa chuo kwa taifa letu kwa takribani robo karne,” amesema Dkt. Amani. 

Ameongeza kuwa tangu kuanzishwa kwake, Chuo kimepata maendeo makubwa na mabadiliko chanya katika utoaji wa elimu, uboreshaji wa huduma, na katika kuimarisha uwezo wa watumishi wa umma nchini.

Dkt. Amani amesema kuwa, mafanikio yaliyopatikana nia ni pamoja na kupanuka kwa kampasi kutoka mbili hadi sita, kuongezeka kwa kozi na programu za muda mrefu, kuboreshwa kwa mafunzo ya muda mfupi kwa watumishi wa umma na matumizi yaa teknolojia katika kutoa mafunzo jambo liliwezesha chuo kuwafikia watumishi wa umma wengi kwa urahisi.

Akihitimisha hotoba yake, Dkt. Amani amesema kuwa, Utumishi Marathon 2025 ni sehemu ya maadhimisho yanayofanyika kwa kampasi zote za chuo cha utumishi wa umma Tanzania na kusema kuwa kilele cha maadhimisho haya kifanyika mapema mwakani.
Mkuu wa Wilaya ya Mtwara, Mhe. Abdallah Mwaipaya akiongea na washiriki wa Mbio za Marathon 2025 katika kuadhimisha Miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika  tarehe 13 Desemba  2025 katika Kampasi ya Mtwara
Makamu Mkuu wa Chuo – Taaluma, Tafiti za Kitaalamu, Dkt. Hamisi Amani akizungumza wakati wa Utumishi Maraton 2025
Mkuu wa Wilaya ya Mtwara, Mhe. Abdallah Mwaipaya, aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, akiwa na Makamu Mkuu wa Chuo – Taaluma, Tafiti za Kitaalamu, Dkt. Hamisi Amani, wakiwa tayari kuanzisha Utumishi Marathon 2025 katika viwanja vya Chuo cha Utumishi wa Umma, Kampasi ya Mtwara. Mbio hizi ni sehemu ya maadhimisho ya Miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania leo tarehe 13 Desemba 2025 Manispaa ya Mtwara.




Na Mwandishi Wetu

Chuo Kikuu cha Ardhi, Taasisi ya Ufundi ya Chongqing (CQVIE) kutoka nchini China, pamoja na Kampuni ya ujenzi ya Kichina nchini ya Group Six International Ltd, wamezindua Kampasi ya Chuo Kikuu cha Ardhi ili kuanzisha kituo cha Mafunzo ya Ustadi wa kitaalamu cha Kichina.

Uzinduzi huo umefanyika mwishoni mwa Novemba mwaka huu Jijini Dar es Salaam, katika Chuo Kikuu cha Ardhi ukiwa na malengo ya kukuza maendeleo ya vipaji na uboreshaji wa viwanda hapa nchini.

Mpango huu mkubwa wa ushirikiano unaongeza kasi mpya katika juhudi za kukuza na kuendeleza ujuzi kwa watanzania na unaashiria hatua muhimu mbele kwa nchi katika elimu ya uhandisi na ushirikiano wa kimataifa.

Sherehe hizo zilihudhuriwa na Prof. Evaristo Liwa, Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ardhi, Liu Ming, Makamu wa Rais wa CQVIE na Huang Zaisheng, Mwenyekiti wa Kampuni ya Group Six International Ltd., pamoja na wawakilishi kutoka pande zote tatu.

Kituo kipya kitazingatia mahitaji ya haraka ya ujuzi wa ujenzi, uhandisi, na viwanda vinavyochipukia vya Tanzania kwa kuunganisha mafundisho ya lugha ya Kichina na mafunzo ya ufundi yanayohusiana na uhandisi, kuwapa vijana uwezo ulioboreshwa katika ujuzi wa lugha na ufundi.

Akizunguza katika uzinduzi huo ulioambatana sambamba na kufanyika warsha Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ardhi Prof. Evaristo Liwa alisisitiza kwamba Warsha hiyo ya Luban imekuwa mfano wa ushirikiano wa Tanzania na China katika elimu ya ufundi, ikikuza idadi kubwa ya wafanyakazi wa kiufundi wanaozingatia mazoezi.

Prof. Liwa, alitangaza kwamba Chuo Kikuu cha ARDHI kitatenga ardhi maalum na vifaa vya kusaidia katika Kampasi yake Kuu ya Jijini Dar es Salaam ili kuendeleza Kituo cha Mafunzo ya Ustadi wa Kichina na Ufundi sambamba na kupanua zaidi wigo na kina kwa ajili ya kuimarisha ushirikiano wa pande zote tatu.

Naye Makamu Mkuu na Rais wa CQVIE Liu Ming alibainisha kuwa Warsha ya Luban imeanzisha jukwaa thabiti la kubadilishana elimu ya ufundi kati ya China na Tanzania

Liu Ming, alisema kuwa kuanzishwa kwa kituo hiki kipya cha mafunzo kutaendeleza zaidi uvumbuzi katika ukuzaji wa vipaji na kuunda fursa zaidi za maendeleo kwa vijana wa Tanzania.

Mwenyekiti Huang Zaisheng alithibitisha kwamba Group Six International Ltd itaendelea kuunga mkono uboreshaji wa Warsha ya Luban na ujenzi wa kituo kipya cha mafunzo, ikifanya kazi kwa karibu na vyuo vikuu vyote viwili ili kuharakisha utekelezaji wa Taasisi ya Teknolojia ya Uhandisi ya Tanzania na China.

Kufuatia sherehe hiyo, pande hizo tatu zilifanya tathmini ya ndani ikizingatia upangaji wa nafasi za kufundishia, ukuzaji wa mtaala, uimarishaji wa uwezo wa walimu, na uboreshaji wa vifaa, na kuweka msingi imara wa awamu inayofuata ya ushirikiano.

Kama mpango muhimu chini ya mfumo wa Belt and Road, kituo hicho kinatarajiwa kutoa mafunzo kwa vipaji vya hali ya juu zaidi vilivyo na ujuzi wa kisasa wa uhandisi, kutoa usaidizi mkubwa wa rasilimali watu kwa ajili ya mafunzo ya kisasa kwa upande wa viwanda vilivyopo Tanzania na kuchangia katika maendeleo ya kiuchumi na kijamii ya hali ya juu nchini.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan leo ameongoza familia, viongozi, wabunge na waombolezaji katika ibada ya kuaga mwili wa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Peramiho, Mhe. Jenista Joakim Mhagama, iliyofanyika katika Kanisa la Mwenyeheri Maria-Theresa Ledochowska, Parokia ya Kiwanja cha Ndege, Jimbo Kuu Katoliki Dodoma. 

Rais Dkt. Samia alieleza masikitiko makubwa ya Taifa kufuatia msiba huo, akimwelezea marehemu kuwa alikuwa kiongozi jasiri, mwaminifu na mlezi wa viongozi wengi ndani ya Bunge na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, aliyelitumikia Taifa kwa moyo wa kujitoa, nidhamu, uadilifu na hofu ya Mungu, akisimama imara kutetea haki, maendeleo na usawa wa wananchi. 

Aidha, alitambua mchango mkubwa wa Marehemu akihudumu kwa ufanisi katika nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya Serikali na Chama cha Mapinduzi, sambamba na uwezo wake wa kubeba majukumu mazito kwa weledi. 

Akigusia urithi wa uongozi aliouacha, Rais Dkt. Samia alisisitiza kuwa moyo wake wa kujali maslahi ya Taifa ndio nguzo kuu ya kumbukumbu ya Hayati Jenista Mhagama, na kutoa wito kwa wabunge na viongozi wote kuiga mfano wake wa maadili na uwajibikaji aliouonesha. 

Halikadhalika, Rais Dkt. Samia aliwataka viongozi kuuenzi mchango wa Marehemu kwa kuimarisha misingi ya uwajibikaji, mshikamano wa kitaifa na utumishi unaolenga maslahi mapana ya wananchi.

 Rais Dkt. Samia alitoa pole kwa familia, ndugu, wananchi wa Jimbo Peramiho, Bunge na Taifa kwa ujumla, na kumuomba Mwenyezi Mungu awape faraja, nguvu na amani, huku akiiombea roho ya Marehemu pumziko la amani ya milele.

Benki ya Stanbic Tanzania imetoa zawadi za msimu wa sikukuu kupitia kampeni inayoendelea ya Masta wa Miamala.

Akizungumza kwenye hafla hiyo iliyoambatana na semina kwa vijana kutoka taasisi mbalimbali, Mkuu wa kitengo cha Wateja Binafsi wa Benki ya Stanbic, Emmanuel Mahodanga alisema "Kampeni hii ya miezi mitatu inalenga kuongeza matumizi ya njia mbalimbali za malipo za benki ya Stanbic kuanzia kadi za Visa, ATM na mtandao smart App wenye zaidi ya mawakala 600, Internet banking na USSD *150*29#".

Aliongeza kusema huduma hii imebuniwa si tu kwa ajili ya kukuza matumizi ya kidigitali bali kuwahamasisha wateja wasiotumia akaunti zao ili kuwapatia nafasi kufurahia urahisi na usalama wa miamala isiyo na fedha taslimu.

Alihitisha kusema: “Tunaposherehekea miaka 30 nchini Tanzania, kampeni hii inaonyesha dhamira yetu ya kudumu ya kutembea na wateja wetu kwa kushiriki nao pamoja katika msimu huu wa sikukuu kwa kuwapatia zawadi mbalimbali zikiwemo simu, friji, microwave na pesa taslimu.” Washindi walitoka taasisi mbalimbali zikiwemo GSM, TBL, BLUE COAST, KPMG na PWC.


Mkuu wa kitengo cha Wateja Binafsi wa Benki ya Stanbic, Emmanuel Mahodanga akizungumza na vijana kutoka KPMG wakati wa semina ya promosheni ya Masta wa Miamala iliyofanyika jijini Dar es salaam ikiwa sehemu ya kuwaelemisha namna washindi wanavyopatikana kupitia promosheni hiyo.







Meneja wa Maendeleo ya Biashara kwa Wateja Binafsi wa Benki ya Stanbic, Alice Gamba (kulia) akimkabidhi zawadi microwave, Mike Kabero kutoka kampuni ya PWC mshindi wa promosheni ya Masta wa Miamala ikiwa ni sehemu ya kusherehekea msimu wa sikukuu. Jinsi ya kushiriki fanya miamala kwa kutuma pesa kwa uwapendao kwa kutumia huduma za malipo kwa mtandao wa stanbic utaweza kuingia kwenye droo ya kujishindia zawadi.


WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni amechaguliwa kuwa Makamu wa Rais wa Baraza la Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEA).

Hayo yamejiri katika mkutano wa saba wa Baraza hilo uliofanyika katika Makao Makuu ya Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEP), jijini Nairobi, Kenya Desemba 12, 2025.

Uchaguzi huo umefanyika kwa mujibu wa Kanuni ya 18 ya Kanuni za Utendaji za UNEP inayotaka Baraza kumchagua Rais, Makamu wa Rais pamoja na Mwandishi katika kikao cha mwisho cha mkutano wake.

Aidha, Mhandisi Masauni amependekezwa na Kundi la Nchi za Afrika, ambalo kwa kuzingatia kanuni za mzunguko na uwakilishi wa kijiografia, limepewa nafasi mbili za Makamu wa Rais katika Ofisi ya Baraza hilo.

Uchaguzi wake umeidhinishwa bila kupingwa, hatua inayodhihirisha imani na heshima kubwa ya jumuiya ya kimataifa kwa uongozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika masuala ya mazingira, mabadiliko ya tabianchi na maendeleo endelevu.

Kuchaguliwa kwa Waziri kushika wadhifa huo ni heshima kubwa kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na unaakisi dhamira, mchango na msimamo thabiti wa nchi katika kutekeleza sera, mikakati na ahadi za kikanda na kimataifa kuhusu ulinzi na uhifadhi wa mazingira.

Halikadhalika, katika uchaguzi huo Waziri wa Maji, Mazingira na Mabadiliko ya Tabianchi wa Jamaica Mhe.Matthew Samuda amechaguliwa kuwa Rais Baraza hilo baada ya kupendekezwa na Kundi la Nchi za Amerika ya Kusini na Karibiani.

Pia, Vilevile, Baraza limemchagua Balozi wa Masuala ya Mazingira na Mkuu wa Idara ya Masuala ya Kimataifa katika Shirika la Mazingira la Uswisi Mhe. Felix Wertli kuwa Mwandishi wa Baraza hilo. Mhe. Wertli amependekezwa na Kundi la Nchi za Ulaya Magharibi na Nyinginezo.

Na: Ofisi ya Waziri Mkuu - KAM
WAZIRI  wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, ameipongeza Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA) kwa mafanikio makubwa katika utatuzi wa migogoro ya kikazi, baada ya kusuluhisha migogoro 4,339 hadi kufikia Septemba 2025.

Waziri Sangu ametoa pongezi hizo Desemba 13, 2025, jijini Dodoma wakati wa mwendelezo wa ziara yake ya kutembelea taasisi zilizo chini ya Ofisi yake, ziara inayolenga kufahamu utekelezaji wa majukumu ya taasisi hizo, kuimarisha uhusiano wa kikazi, pamoja na kutoa maelekezo yatakayoongeza ufanisi, uwajibikaji na tija katika utoaji wa huduma kwa wananchi.

Akizungumza na Menejimenti ya CMA Mhe. Sangu ameitaka Tume kuendelea kukuza matumizi ya teknolojia katika utatuzi wa migogoro ya kikazi, hususan kuboresha na kuimarisha matumizi ya Mfumo wa e-Utatuzi.

Aidha, ameagiza kuwekwa kwa mazingira rafiki ya matumizi ya mfumo huo ili uweze kutumika kikamilifu kama nyenzo madhubuti ya kumaliza migogoro sehemu za kazi kwa haraka na kwa ufanisi.

Awali, Naibu Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Rahma Kisuo, ameisisitiza CMA kuendelea kujitangaza na kutoa elimu kwa umma kuhusu huduma zinazotolewa na Tume, sambamba na kuimarisha misingi ya usawa na haki mahala pa kazi.

Vile vile, amewahimiza watumishi wa Tume kuzingatia usuluhishi kama njia muhimu ya kutatua migogoro ya kikazi, akisisitiza kuwa mazungumzo huchangia utoaji wa haki kwa wakati na hupunguza migogoro kazini.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA), Bw. Usekelege Mpulla, amesema Tume itaendelea kuboresha utendaji wake kwa kuwekeza zaidi katika matumizi ya teknolojia ya kisasa ili kuongeza ufanisi na upatikanaji wa huduma za utatuzi wa migogoro ya kikazi kwa wananchi.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu (akiyesimama) akizungumza na Menejimenti ya Tume ya Usuluhishi na Uamuzi - CMA Disemba 13, 2025 Jijini Dodoma wakati wa mwendelezo wa ziara yake ya kutembelea taasisi zilizo chini ya Ofisi yake,
Na Munir Shemweta, WANMM MOROGORO


Mkuu wa mkoa wa Morogoro Bw. Adam Malima ameipongeza Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa kuweka kumbukumbu za ardhi vizuri jambo alilolieleza kuwa linasaidia katika utatuzi wa migogoro ya ardhi.

‘’Mhe Waziri kwa kweli nitoe pongezi kwa wizara yako kwa kuwa na kumbukumbu nzuri za wamiliki wa ardhi jambo hili limetusaidia kama mkoa wa morogoro kutatua migogoro ya ardhi pale inapojitokeza’’ amesema Bw. Malima

Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi moja ya vipaumbele vyake ni katika mwaka wa fedha 2025/2026 ni kuongeza kasi ya upangaji, upimaji, umilikishaji na usajili wa ardhi mijini, vijijini na katika maeneo ya kimkakati.

Bw. Malima amesema hayo tarehe 12 Desemba 2025 ofisini kwake alipokutana na Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo aliyekuwa mkoani humo kwa ajili ya kuhudhuria mahafali ya 44 ya Chuo cha Ardhi Morogoro (ARIMO).

Amesema, migogoro ya ardhi katika mkoa wake wa Morogoro imepungua kwa kiasi kikubwa kutokana na juhudi kubwa za wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kupitia ofisi ya Kamishna wa Ardhi Msaidizi mkoa ambapo imefanya kazi kubwa ya kufikia wananchi kupitia Kliniki ya Ardhi.

Kwa upande wake Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo alimueleza mkuu wa mkoa wa Morogoro kuwa, wizara yake kwa sasa inafanya juhudi kubwa kuhakikisha migogoro ya ardhi iliyopo inatatuliwa na hakuna migogoro mipya inayozalishwa kwenye maeneo mbalimbali nchini.

‘’Nikuhakikishe RC sisi ndani ya wizara tumejiwekea mikakati ya kuhakikisha migogoro iliyopo tunaimaliza lakini pia hakuna migogoro mipya inayozalishwa’’ amesema Mhe. Dkt Akwilapo.

Aidha, Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi amezihimiza taasisi za umma kuhakikisha zinalinda maeneo yao ili kuepuka uvamizi alioueleza kuwa ndiyo unaochangia kwa kikubwa migogoro ya ardhi katika maeneo ya umma.

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo (kushoto) akimsikiliza kwa makini Mkuu wa mkoa wa Morogoro Bw. Adam Malima alipomtembelea ofisini kwake jana.

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo (kushoto) akizungumza na Mkuu wa mkoa wa Morogoro Bw. Adam Malima alipomtembelea ofisini kwake jana.

Mkuu wa mkoa wa Morogoro Bw. Adam Malima akizungumza wakati Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo (Kushoto) alipomtembelea ofisini kwake. Kulia ni Katibu Tawala wa mkoa wa Morogoro Dkt Mussa Ali Mussa. (PICHA ZOTE NA WIZARA YA ARDHI)



Na Khadija Kalili, Kibaha
MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakari Kunenge amewaelekeza Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Wilaya zote za Mkoa wa Pwani kuacha tabia ya urasimu wa kufanya maamuzi yenye tija kwani yamekua Haya wawekezaji pia ni kero kwa wananchi.

RC Kunenge amesema hayo alipozungumza na viongozi hao katika kikao kazi cha tathmini ya utekelezaji wa ahadi za kuelekea siku 100 za Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan .

Kikao hicho kimefanyika tarehe 11 Desemba 2025 kwenye Ukumbi wa Mikutano Mkoani hapa.

"Kila kiongozi ana wajibu wa kuhakikisha kwamba urasimu unaondoka ndani ya Mkoa wetu ili tuweze kuleta maendeleo naagiza nendeni mkasimamie ndinyi ndiyo

Watendaji acheni urasimu wa kukwamisha mambo mbalimbali ndani ya Mkoa ".

"Bajeti ya nchi ni 1.9 ni misaada na inakwenda kupungua kutokana na changamoto tuliyoipitia hivyo tujipange kuziba pengo hili aidha kwa kuongeza kukopa ama kuzalisha , tufanye kazi kitaalam tusipoteze muda na rasilimali za Mkoa asilimia 20% ya utendaji wetu unapimwa na asilimia 80% ya matokeo yetu,kafanyeni maamuzi kwa wakati" amesema Kunenge.

Akizungumza kuhusu kujipanga uwasilishaji wa utekelezaji wa ahadi za siku 100 za Mhe. Rais Samia kwamba wameangalia katika maeneo ya Mkoa na namna watakavyotekeleza ili utakapofika wakati wa kuwasilisha wakawasilishe vyema katika ngazi ya maeneo yanayohusu Mkoa wa Pwani na kusisitiza kutoa taarifa zilizo sahihi.

"Tunafahamu kuwa Rais Dkt. Samia atatekeleza ahadi zake alizozitoa ndani ya siku 100,jambo kubwa ni kuhakikisha na sisi tunatekeleza ya kwetu katika ngazi ya Mkoa, japo kuna mambo ya kisera,kitaifa ,

Mkoa, Wilaya na Halmashauri bila kujipanga na kujua yapi ya kufanya tathmini kutekeleza mikakati ili muda utakapofika tuwasilishe kwa weledi wa hali ya juu"

Wakati huohuo Baraka Mwambange ambaye ni Meneja wa Wakala wa Barabara Mkoa wa Pwani (TANROAD) amepewa tuzo ya kutambua mchango wake katika utendaji wa kazi zake amabapi amehakikisha na kusimamia barabara za Mkoa wa Pwani zinapitika katika kipindi chote.

"Barabara na madaraja sawa na mishipa ya damu kwa binadamu ,hii ni mara ya kwanza kutoa tuzo na itamjengea ari ya kuchapa kazi zaidi muhusika" amesema Kunenge.

"Tutaendelea na utaratibu wa kutambua kazi za watumishi wa umma ambao wataonekana kufanya kazi zao kwa weledi na tunatakiwa kutambua kila mtumishiin anapofanya jambo jema huwa tunawaandikia barua na kupelekwa wakuu wake wa Idara pia barua hiyo huwekwa kwenye faili lake ikiwa linaambatana na taarifa zake za kumbukumbu katika kazi" amesema RC Kunenge.

RC Kunenge amesema kuwa mbali ya tuzo hiyo pia wamemuandikia barua ya pongezi na nakala imekwenda kwa viongozi wake.

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Asha-Rose Migiro, akiwa pamoja na viongozi mbalimbali wa CCM, amejumuika na waombolezaji wengine kushiriki ibada ya kumuaga aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Peramiho, marehemu Jenista Joakimu Mhagama, inayofanyika katika Kanisa Katoliki Kiwanja cha Ndege, jijini Dodoma. 


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa CCM, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan anawaongoza waombolezaji katika shughuli hiyo ya kumuaga marehemu Jenista Mhagama, kanisani hapo.





 

KAMA wewe ni mbashiri kwelikweli basi umewahi kutamani kuwa mahali ambapo burudani, ushindi, na msisimko vinakutana kwa wakati mmoja. Meridianbet sasa inakuletea kilele kipya cha michezo ya kasino mtandaoni kwa kuungana na Ruby Play, mtoa huduma maarufu wa kimataifa. Hapa, kila raundi siyo burudani tu, ni fursa ya kuunda hadithi yako ya ushindi na kujaribu bahati yako kila hatua.

Ruby Play imeweka kiwango kipya cha ubunifu. Michezo yake inakuja ikiwa imeundwa kwa umakini mkubwa, ukiwa na vipengele maalum vya kushinda vinavyoongeza msisimko na fursa ya ushindi mkubwa. Kila mzunguko, kila bonasi, inakuletea msisimko wa kweli. Hakika, hii sio burudani ya kawaida, bali ni safari ya hisia na fursa ya pesa.

Meridianbet haikuachi nyuma, kuna michezo mbalimbali ya kasino mtandaoni pamoja na mechi za kimataifa za kubashiri zenye odds bomba zinazokuongezea nafasi ya kuongeza kipato chako kila siku. Kujiunga ni rahisi! Tembelea meridianbet.co.tz au piga *149*10#.

Kwa wapenzi wa Meridianbet na jamii nzima ya wacheza kasino mtandaoni, ladha ni kubwa na ya kusisimua. Michezo kama Dragon Ladies, Immortal Empress, Lady Phoenix, Vegas Hotties, Medusa Money, Book of Richies na mingine mingi inakuletea mchanganyiko wa hadithi, rangi, sauti, na picha zinazofanya kila mzunguko uwe tukio lisilosahaulika. Kila mchezo ni kama tiketi ya kupata furaha na ushindi.

Sasa ni wakati wako wa kuingia kwenye dunia hii ya burudani isiyo na mipaka. Jisajili kwenye Meridianbet, chagua michezo ya Ruby Play, na uanze safari ambapo kila mzunguko ni mwendelezo wa ushindi na furaha. Usikose nafasi ya kuunda historia yako ya bahati na ushindi.

JE, unajua kuwa siku ya leo unaweza ukapiga mkwanja wa uhakika na Meridianbet?. Mechi kibao kuendelea huku nafasi ya wewe kuondoka na mzigo wa kutosha ikiwa wazi kabisa. Usisubiri kuhadithiwa, ingia na ubeti hapa.

Ligi kuu pendwa ya Uingereza, EPL itazidi kuwaka moto ambapo Chelsea atamenyana dhidi ya Everton mechi ambayo itapigwa katika dimba la Stamford Bridge. Mara ya mwisho kukutana hawa wawili The Blues waliondoka na ushindi mwembamba kabisa. Leo hii nani kuondoka mbabe?. Bashiri hapa.

Mtanange mwingine ni huu wa Liverpool vs Brighton ambapo tofauti ya pointi kati yao ni moja pekee. Msimu uliopita timu hizi ziligawana pointi kila mechi ambapo mechi ya kwanza vijana wa Slot walishinda kwao huku mechi ya pili vijana wa Fabian walishinda. Je leo hii nani kuondoka na alama 3?. Jisajili hapa.

Vijana wa Mikel Arteta, Arsenal watakuwa Emirates kukipiga dhidi ya Wolves ambao msimu huu umekuwa mzito sana kwao mpaka sasa wamekusanya pointi 2 kwenye mechi 13 walizocheza. The Gunners wanahitaji taji la ligi kuu msimu huu hivyo ushindi huu ni muhimu sana kwao. Bashiri hapa.

Piga mpunga wa maana na michezo ya Kasino ya mtandaoni kama vile Keno, Aviator, Poker, Roulette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Tengeneza pesa pia mechi hizi za ligi kuu ya Hispania, yaani LALIGA ambapo Atletico Madrid ataumana dhidi ya Valencia ambao wapo nafasi ya 15 kwenye msimamo. Vijana wa Diego Simeone wao wapo 4 wakiwa nyuma pointi 6 kwa kinara wa ligi. ODDS KUBWA zipo hapa. Suka jamvi hapa.

Nao Mallorca wataumana dhidi ya Elche ambao wanatofautiana pointi 3 huku mwenyeji yeye akiwa nafasi ya 16 na mgeni wake akiwa nafasi ya 11. Meridianbet wanasema kuwa mechi hii ina machaguo zaidi ya 1000. Ingia na ubashiri mechi hii sasa.

FC Barcelona wao watakuwa nyumbani kumenyana dhidi ya CA Osasuna ambao mpaka sasa wana pointi 12 kwenye mechi 14 ambazo wamecheza hadi sasa. Mara ya mwisho kukutana Barca alishinda, lakini mechi ya nyuma yake walipoteza. Je leo hii nani kushinda?. Tandika jamvi hapa.

BUNDESLIGA kule Ujerumani nayo kitawaka Frankfurt atakipiga dhidi ya Augsburg ambapo mara ya mwisho kukutana hakuna ambaye alikuwa mbabe kati yao hadi sasa. Tofauti kati yao ni pointi 11 na leo hii kila mtu anataka kuonesha ubabe kwa mwenzake. Je nani kushinda leo?. Bashiri hapa.

Nao ST. Pauli atamenyana dhidi ya FC Heidenheim ambao mpaka sasa wana pointi 8 wakati wenyeji wao wakiwa na pointi 7 hadi sasa kwenye mechi 12 ambazo wamecheza. Meridianbet wameweka machaguo zaidi ya 1000 kwenye mechi hii. Unangoja nini sasa, ingia na ubeti hapa.

Pia beti mechi za ligi kuu ya Italia, yaani SERIE A ambapo Torino atakipiga dhidi ya Cremonese ambao wapo nafasi ya 11 huku wenyeji wao wakiwa nafasi ya 13. Kwenye ligi mara ya mwisho kukutana walitoa sare, hivyo leo hii nani anaondoka na ushindi?. Meridianbet wameipa mechi hii machaguo zaidi ya 1000. Suka jamvi hapa.

Lazio watakua ugenini kumenyana dhidi ya Parma FC ambao wapo nafasi ya 17 wakiwa na pointi 11 pekee hadi sasa. Mgeni yeye hadi sasa amekusanya pointi 18 na wanashika nafasi ya 8 kwenye msimamo wa ligi. ODDS KUBWA zipo kwenye mechi hii hadi sasa. Jisajili hapa.

Na mechi ya mwisho kabisa itakuwa ya Atalanta vs Cagliari ambao tofauti ya pointi kati yao hadi sasa ni 5 pekee. Ni suluhu ambayo ilipatikana kwenye mtanange wa mwisho kukutana. Je leo hii nani kushinda?. Beti hapa.

Na Avila Kakingo, Michuzi Tv
SERIKALI imeeleza dhamira yake ya kusogeza huduma karibu na wananchi na kuongeza uwazi katika ajira za umma kupitia matumizi ya teknolojia ya kidijitali, hatua inayolenga kupunguza urasimu na gharama kwa waombaji wa ajira na wapokeaji wa huduma za Serikali.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete, amesema Serikali imeanza tathmini ya rasilimali watu katika taasisi za umma ili kuhakikisha mahitaji halisi ya watumishi yanazingatiwa kwa haki na weledi.

Amesema tathmini hiyo itawezesha Serikali kujenga mfumo wa ajira unaozingatia ushindani, uwajibikaji na ufanisi, sambamba na kutekeleza ahadi ya kuongeza ajira kwa Watanzania, hususan katika sekta za afya na elimu.

Kwa mujibu wa Waziri Ridhiwani, mchakato mpya wa ajira utaanza Desemba 13, 2025, ambapo kwa mara ya kwanza usaili utafanyika katika mikoa yote nchini kwa kutumia mfumo wa mtandaoni wa online aptitude test, hatua itakayopunguza gharama na usumbufu kwa waombaji.

Katika kuimarisha mawasiliano kati ya Serikali na wananchi, Waziri huyo amezindua rasmi mfumo wa Mrejesho unaopatikana kwa kupiga 15400#, utakaomwezesha mwananchi kutoa maoni, malalamiko au pongezi moja kwa moja kwa viongozi na taasisi za umma bila vikwazo.

Aidha, amesema kuanzishwa kwa Daftari la Huduma za Serikali (GSD) kutawawezesha wananchi kupata taarifa sahihi za huduma, gharama na taratibu bila kulazimika kufika ofisini, hivyo kuongeza uwazi na kuokoa muda.

Akizungumzia masuala ya maadili, Ridhiwani amesema Serikali ipo katika hatua za kurekebisha sheria za maadili ya viongozi na watumishi wa umma ili kuimarisha uwajibikaji na uadilifu katika ngazi zote.

Amesisitiza kuwa licha ya changamoto za awali za mifumo mipya, Serikali imelenga kufikisha zaidi ya asilimia 80 ya huduma zote za umma kwenye mifumo ya kidijitali ifikapo mwaka 2050, kama sehemu ya mkakati wa kujenga Serikali inayowajibika na inayomlenga mwananchi.

MOROGORO

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo amewaasa wahitimu wa Chuo cha Ardhi Morogoro (ARIMO) kujiepusha na matendo maovu na elimu na maarifa waliyopata yawe tunu na faida kwa Taifa.

Mhe. Dkt Akwilapo ametoa wito huo tarehe 12 Desemba 2025 wakati wa mahafali ya 44 ya Chuo cha Ardhi Morogoro (ARIMO) yaliyofanyika mkoani Morogoro ambapo jumla ya wahitimu 450 wa fani za Jiomatikia (Upimaji Ardhi), Upangaji Miji na Vijiji na Mifumo ya Taarifa za Kijiografia (GIS) walitunukiwa Astashada na Stashahada katika fani hizo.

Mhe. Dkt Akwilapo amewataka wahitimu hao kukumbuka kuwa utii, nidhamu na tabia njema ni silaha itakayowafanya wapendwe mahali popote.

‘’Tukiwa hapa Morogoro tunakumbuka maneno yaliyoimbwa na mwanamuziki wa hapa hayati Mbaraka Mwinshehe na bendi yake ya Okestra Volcano; alisema “Heshima Kijana tanguliza kwanza mbele, ujeuri mbaya; uzuri si hoja tabia njema ni silaha utapendwa popote” mwisho wa kunukuu, alisema Mhe. Dkt Akwilapo.

Amewataka vijana kutodanganyika na maneno ya eti kuna watu wanaitwa Gen Z ambapo alieleza kuwa, hizo ni propaganda za kujenga hofu na kufifisha juhudi za nchi maskini kujitafutia maendeleo.

“Msidanganywe kuwa eti nyie ni kizazi cha vijana wasio na nidhamu, wapenda fujo, wasiosikiliza wazee wao, viongozi wao, chenye kujiamulia mambo yao bila kufuata sheria, taratibu, miongozo na tamaduni zetu; na mambo mengine ya hovyo’’ amesisitiza Mhe. Dkt Akwilapo.

Kwa mujibu wa Waziri huyo wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, inasikitisha na kushangaza kuona vijana wa Kitanzania wanasikiliza maelekezo ya watu ambao hawaishi Tanzania na wala hawajawahi kuwaona na kupuuza  maelekezo ya Viongozi wao na hata wazazi wao ambao wamewalea mpaka hapo walipoifikia.

Amesema, kuhitimu masomo kunatakiwa kuendane na uzalendo waliojengewa wa kuipenda Tanzania na kusisitiza kuwa waithamini nchi yao.

Mhe. Dkt Akwilapo amewataka kutumia utaalamu walioupata kwa weledi, uadilifu na kufuata sheria, kanuni, taratibu na miongozo na kuepuka vitendo vinavyoenda kuhatarisha amani.

Vile vile amewataka kuendelea kujifunza kwani elimu ni bahari, haina mwisho na kuwataka wanaobaki chuoni kuongeza bidii katika masomo, nidhamu na kutunza amani na umoja kwani kesho yao inajengwa na maamuzi ya leo.

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Morogoro, Bw. Musa Ramadhani Kilakala akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Bw. Adam Malima amesema, migogoro ya ardhi imepungua mkoani humo hasa pale wizara ya ardhi ilipoanzisha Kliniki za Ardhi ambazo amezieleza zimesaidia kwa kiasi kikubwa kuwafikia wananchi katika maeneo yao.

Akitoa taarifa kwa Mgeni Rasmi, Mkuu wa Chuo cha Ardhi Morogoro (ARIMO) Charles Saguda amesema chuo hicho kina Mpango Kabambe wa Miaka 20 (2023-2043) unaolenga kuboresha mazingira ya kujifunza na kujifunzia na utendaji wa chuo katika kuwaandaa wataalamu wa sekta ya ardhi.

“Mpango kabambe huu unalenga kuongeza udahili wa wana chuo kutoka 660 hadi 5000, kuongeza watumishi kutoka 58 hadi 310 kuongeza program za mafunzo ya wanafunzi kutoka 2 hadi 7 pamoja na kujenga kampasi mpya katika eneo Mlima Kola mkoani Morogoro’’. Amesema Bw. Saguda







 

Kamishna wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Yusuph Mwenda, akizungumza na  wafanyabiashara pamoja na washauri wa walipakodi  jijini Dar es Salaam.


KAMISHNA wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Yusuph Mwenda, ametoa wito kwa wafanyabiashara pamoja na washauri wa walipakodi kuimarisha maadili, uaminifu na weledi katika utoaji wa huduma zao, ili kujenga mazingira salama, shindani na yenye utii wa kodi kwa manufaa ya uchumi wa taifa.

Hayo ameyasema leo Desemba 12, 2025 wakati akizungumza katika kikao maalum na wataalamu hao, Kamishna Mwenda aliwakumbusha kuwa nafasi yao katika mfumo wa kodi ni nyeti na ina athari kubwa kwa ustawi wa biashara nchini.

Amesema kuwa licha ya mafanikio makubwa yaliyopatikana katika kurahisisha biashara na kuongeza utii wa hiari, bado kunahitajika kutumia utaalamu wao kwa njia inayolinda uadilifu kuliko kusaidia ukwepaji kodi au kutoa taarifa za kupotosha.

Amesisitiza kuwa vitendo hivyo vinaharibu sifa ya sekta, vinapunguza mapato ya serikali, na kuvuruga uwanja sawa wa ushindani kwa wafanyabiashara wanaofuata sheria.

Kamishna Mwenda amesema baadhi ya changamoto zinazojitokeza katika ukusanyaji wa kodi zimekuwa zikichangiwa na washauri wachache wanaowasilisha taarifa zisizo sahihi kwa niaba ya wateja wao au wanaoshiriki moja kwa moja katika vitendo vya smuggling. Ameeleza kuwa tabia kama hizo haziwezi kufanyika bila ushirikiano kati ya baadhi ya maafisa wasio waadilifu na wataalamu wa kodi wenye maslahi binafsi, hali ambayo imekuwa ikihatarisha uaminifu katika mfumo wa kodi.

Aidha, ametoa rai kwa washauri wa kodi kujitambua kama watu wanaotekeleza wajibu wa umma (public officials) kwa kuwa wanahusika moja kwa moja katika kuhakikisha taarifa zote muhimu za walipakodi zinawasilishwa kwa ukweli na kwa wakati. Amesema hatua hiyo itasaidia si tu kuongeza mapato ya serikali, bali pia kuimarisha mazingira ya biashara na kuondoa malalamiko ya viwango vikubwa vya kodi vinavyotokana na utii mdogo wa baadhi ya walipakodi.

Kwa upande wa wafanyabiashara, Kamishna Mwenda amewasihi kuepuka kutafuta njia za mkato kupitia washauri wasiokuwa waaminifu, kwa kuwa kufanya hivyo kunawaweka katika hatari ya kisheria, kunaharibu taswira ya biashara zao na kunachangia ushindani usio sawa katika sekta.

Amesema biashara inayofuata sheria ina nafasi nzuri ya kukua, kupata huduma bora kutoka TRA na kuongeza uaminifu wa masoko ya ndani na nje.

Aidha, katika kuelekea msimu wa mwisho wa mwaka ambapo biashara na uingizaji mizigo huongezeka, Kamishna Mwenda amewataka washauri wa kodi na wafanyabiashara kuendelea kushirikiana kwa karibu na TRA kwa kuwasilisha taarifa sahihi za bidhaa, kuepuka hofu zisizo na msingi na kufanya maamuzi kwa uadilifu.

Amesema ushirikiano huu utasaidia kuondoa misuguano, kujenga uaminifu na kuhakikisha shughuli za Desemba hazitetereki.

Kamishna Mwenda amewahimiza wadau hao kutoa maoni ya kuboresha mahusiano kati yao na TRA, huku akiweka msisitizo kuwa maadili na weledi ndiyo msingi wa kuongeza wigo wa walipakodi bila kuongeza viwango vya kodi.

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imekutana na washauri wa kodi na wafanyabiashara kwa lengo la kuhamasisha utii wa kodi, kuboresha mawasiliano, na kujadili changamoto zinazowakabili walipakodi kuelekea mwisho wa mwaka wa fedha unaoishia Desemba 31, 2025. Kikao hicho, kilichoongozwa na Kamishna Mkuu wa TRA, kililenga kuhakikisha walipakodi wanawasilisha marejesho yao kwa usahihi na kwa wakati ili kuimarisha ukusanyaji wa mapato ya nchi na uendelevu wa biashara.

Mfanyabiashara, Melkzedek Festo, amesema kikao hicho kimetoa mwelekeo mpana kuhusu wajibu wa walipakodi katika kipindi hiki cha mwisho wa mwaka, hususan kwa biashara zinazotumia kalenda ya Januari hadi Desemba.

“Kamishna Mkuu amesisitiza umuhimu wa walipakodi kupitia faida halisi ya mwaka, kuhesabu kodi sahihi, na kuwasilisha returns pamoja na kulipa kabla ya tarehe 31 Desemba 2025,” amesema Festo.

Ameongeza kuwa walipakodi wanapaswa kurekodi kikamilifu mauzo yao kwa kutumia risiti za EFD, na kuhakikisha wanalipa kodi kwa wakati ili kuepuka riba na adhabu zinazoweza kujitokeza kutokana na ulipaji wa kuchelewa.

“Ukaribu kati ya walipakodi na TRA utasaidia kuongeza uelewa wa sheria za kodi na kuimarisha uwezo wa sekta kukusanya kodi kwa ufanisi,” ameongeza.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama cha Washauri wa Kodi Tanzania, CPA Victoria Alex, amesema mkutano huo ni hatua muhimu katika kuimarisha mahusiano kati ya washauri wa kodi na TRA, hususan katika kipindi hiki ambacho walipakodi wanajiandaa kukamilisha majukumu yao ya mwisho wa mwaka.

“Mawasiliano ni muhimu sana. Mkutano huu umetupa fursa ya kushirikiana kwa karibu na TRA ili kuhamasisha ulipaji kodi kwa hiari, ambayo ndiyo msingi wa kuimarisha uchumi,” amesema.

CPA Victoria amesema kupitia mkutano huo, washauri wa kodi wamepata ufafanuzi wa changamoto mbalimbali pamoja na nafasi ya kuwasilisha maoni yao moja kwa moja kwa Kamishna Mkuu.

“Jambo hili linasaidia serikali na TRA kuwa kwenye nafasi nzuri ya kutatua changamoto za walipakodi. Lengo ni kuwa kwenye daraja moja katika kuwaelimisha na kuwahimiza walipakodi kutekeleza wajibu wao,” amesema.

Aidha, amesema washauri wa kodi wataendelea kushirikiana na TRA katika kipindi hiki cha mwisho wa mwaka ili kuhakikisha walipakodi wanalipa kodi kwa wakati na kwa hiari, kwa manufaa ya maendeleo ya taifa.

“Tumejipanga kutoa ushirikiano wa karibu ili kuhakikisha hakuna mlipaji anayekosa kutimiza wajibu wake kabla ya kuingia mwaka 2026,” amesema CPA Victoria




Baadhi ya Matukio mbalimbali wakati Kamishna Mkuu wa TRA akizungumza na wafanyabiashara pamoja na washauri wa walipakodi.

 

Meneja Mkuu wa Shirika la Masoko ya Kariakoo, CPA. Ashiraf Abdulkarim,akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya uchambuzi na uandaaji wa mpango Mkakati mpya wa miaka mitano 2026-2031 wa Shirika la Masoko ya Kariakoo.

....

Shirika la Masoko ya Kariakoo limeanza rasmi maandalizi ya Mpango Mkakati mpya wa miaka mitano 2026-2031, hatua inayolenga kulifanya soko hilo la kimataifa kutoa huduma bora, kwa wakati na kuzingatia mabadiliko ya teknolojia yanayojitokeza duniani.

Mpango huo unakuja baada ya baada ya mpango wa 2021-2025 kumaliza muda wake wa utekelezaji kwa mafanikio makubwa.

Akizungumza wakati wa ufunguzi mafunzo ya uchambuzi na uandaaji wa mpango huo, Meneja Mkuu wa Shirika la Masoko ya Kariakoo, CPA. Ashiraf Abdulkarim , amesema maandalizi ya mpango huo umeshirikisha wadau ikiwemo Ofisi Waziri Mkuu TAMISEMI, Wafanyabiashara wa Kariakoo, Wapangaji na wadau wengine ili kuwa na mpango mkakati bora, uliochukua mawazo ya wengi na unaojibu matamanio ya kila mmoja na hivyo kuwa rahisi katika utekelezaji wake.

CPA Abdulkarim ameongeza kuwa katika kuandaa mpango huo, Shirika litazingatia nyaraka mbalimbali ikiwemo Dira ya Maendeleo ya Taifa 2025-2050, hotuba ya Rais wakati akifungua Bunge la 13, Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Taifa, Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2025-2030 pamoja na Sheria na miongozo mbalimbali iliyoanzisha Shirika la Kariakoo.

“Mafunzo haya yatafanyika kwa siku tano na yatakuwa endelevu. Lengo ni kuwa na mpango mkakati bora, unaotekelezeka na unaoweza kupimika kila mwaka kwa kipindi cha miaka mitano ambao utalifanya soko la kariakoo kuwa kinara na linalotoa huduma anuai na sio mazao pekee" amebainisha CPA Abdulkarim.

Amesema mpango huo ukikamilika utalibadilisha soko la Kariakoo kuwa kituo cha kisasa cha biashara, chenye mifumo ya kisasa ya uendeshaji na utoaji huduma.

CPA. Abdulkarim amesema kuwa Kariakoo mpya itakuwa na miundombinu ya kisasa kuanzia maeneo ya maegesho ya magari, mifumo ya kuzima moto, maeneo ya dharura, hewa ya kutosha na mifumo ya kiteknolojia ya uendeshaji. Tunataka kuwahudumia Watanzania katika mazingira bora na ya kisasa.

Kwa upande wake, Meneja wa Mipango na Biashara wa Shirika la Kariakoo, Bi. Mwinga Luhoyo amesema maandalizi ya mpango huo yanahusisha tathmini ya mpango uliopita wa 2021–2025 ili kubaini mafanikio, changamoto na maeneo yanayohitaji maboresho.

Meneja huyo ameongeza kuwa lengo ni kuhakikisha mpango huo unaendana na mikakati ya kitaifa na huku ukilenga kuongeza tija, kuimarisha biashara, na kukuza mchango wa Kariakoo katika uchumi wa taifa.


Top News