• Tanzania, Rwanda na Uganda zakubaliana kusaini hati ya makubaliano ya ujenzi wa Kufua Umeme Nsongezi wa 39MW

Mkutano wa 17 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Nishati, Petroli na Madini la Jumuiya ya Afrika Mashariki umeipongeza Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kukamilisha maandalizi ya Kongamano na Maonesho ya 11 ya Petroli ya Jumuiya ya Afrika Mashariki yatakayofanyika tarehe 5 hadi 7 Machi 2025 jijini Dar es Salaam.

Pongezi hizo zimetolewa kwenye mkutano wa Baraza hilo uliofanyika katika Makao Makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) jijini Arusha.

Uenyeji wa Tanzania katika Kongamano hilo unatokana na Maamuzi ya Mkutano wa 16 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Nishati uliofanyika Februari 14, 2024 ambao uliamua Tanzania kuwa Mwenyeji wa Kongamano na maonesho hayo.

Kongamano na Maonesho hayo ni mkakati unaolenga kutangaza fursa zilizopo katika nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kuhusu rasilimali za mafuta na gesi asilia na kuielezea jiolojia ya ukanda wa Afrika Mashariki ili kuvutia uwekezaji, kuendelezaji wa miundombinu, udhibiti wa uharibifu wa mazingira, usimamizi wa taarifa za mafuta na gesi asilia.

Pia linalenga kutangaza maeneo mapya ya utafutaji na kutangaza maendeleo yaliyopatikana katika sekta ya nishati katika ukanda.

Malengo mengine ni kubadilishana uzoefu kuhusu sera, sheria, kanuni na utaalamu unaotumika kwenye sekta ya nishati, kuhamasisha uwekezaji, utafutaji, uzalishaji na uendelezaji wa mafuta na gesi asilia. Vilevile Kongamano hilo linatoa fursa ya kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo nchini na katika ukanda wa Afrika Mashariki.

Kongamano na maonesho hayo yanatoa fursa adhimu kwa Tanzania kutangaza fursa za uwekezaji katika sekta ya Nishati hususan katika sekta ndogo ya mafuta na gesi na hivyo kuongeza wigo wa kupata wawekezaji kwenye sekta hiyo.

Mbali na hayo, Mkutano 17 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Nishati, Petroli na Madini la EAC limepokea na kujadili taarifa ya utekelezaji wa miradi na programu mbalimbali katika sekta ya nishati, petroli na madini ikiwemo Mradi wa Kufua Umeme wa Nsongezi wenye Megawati 39 kwa kutumia maporomoko ya maji ya Mto Kagera utakaotelezwa kwa pamoja baina ya Tanzania, Rwanda na Uganda.

Ujumbe wa Tanzania katika Mkutano huo wa 17 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Nishati, Petroli na Madini uliongozwa na Waziri wa Madini Mhe. Antony Mavunde (Mb.), Naibu Waziri wa Nishati Mhe. Judith Kapinga (Mb.), Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi- Zanzibar Bw. Zahor Alharousy na Viongozi wengine waandamizi wa Serikali.








Mwanamuziki nyota wa Bongo Flava, Omary Ally Mwanga, anayefahamika kwa jina la kisanii Marioo, ametambulishwa rasmi kama Balozi wa Bahati Nasibu ya Taifa ya Tanzania. Ushirikiano huu wa kimkakati unaleta matumaini, burudani, na fursa zinazoweza kubadilisha maisha ya Watanzania.

Huku Bahati Nasibu ya Taifa ikikaribia kuzinduliwa rasmi, Kampuni ya ITHUBA, ambayeni mwendeshaji rasmi aliyepewa dhamana ya miaka nane, inaleta enzi mpya ya ushindi ambapo kuamini katika uwezekano wa kitu kunageuza ndoto kuwa uhalisia.

Katika kiini cha bahati nasibu hii ni kauli mbiu yenye nguvu: "Amini. Cheza. Ushinde."
Huu sio msemo wa kawaida—bali ni mwamko wa kuhamasisha Watanzania kuota ndoto kubwa, kuthubutu, na kuchukua hatua za kuyafikia mafanikio.

Akizungumzia jukumu lake jipya kama balozi wa Bahati Nasibu ya Taifa, Marioo hakuweza kuficha furaha yake:

"Nina furaha kubwa kutangaza kuwa mimi sasa ni balozi rasmi wa Bahati Nasibu ya Taifa! Huu ni wakati mkubwa—sio tu kwangu kama msanii, bali kwa kila Mtanzania anayethubutu kuota ndoto kubwa. Bahati Nasibu ipo hapa kufungua milango, kutengeneza washindi, na kuinua jamii—nami najivunia kuwa sehemu ya safari hii!"

Ushirikiano huu unamaanisha kwamba ushindi si ndoto tena—bali ni uhalisia unaosubiri kutokea!

Mkurugenzi kutoka ITHUBA Tanzania, Kelvin Koka, alisisitiza kuwa ushawishi wa Marioo unamfanya kuwa kiungo bora kati ya burudani na michezo ya kubahatisha.

"Marioo ni zaidi ya msanii—yeye ni alama ya kizazi kipya cha Watanzania wanaothubutu kuamini katika ndoto zao. Nguvu yake, uhalisia wake, na uhusiano wake wa karibu na mashabiki wake vinamfanya kuwa balozi sahihi wa Bahati Nasibu ya Taifa. Kupitia yeye, tutahamasisha Watanzania wengi zaidi kushiriki kwenye michezo ya bahati nasibu ambayo ni ya haki, ya kusisimua, na yenye uwezo wa kubadilisha maisha," alisema Koka.

Lakini Bahati Nasibu ya Taifa haihusiani tu na ushindi binafsi—ni chombo cha maendeleo kinachowekeza katika miradi ya michezo ili kuinua vipaji na kusaidia jamii.

"Tumejidhatiti katika uwazi, ubunifu, na michezo inayowajibika. Kila tiketi inayouzwa inachangia maendeleo ya taifa, kuhakikisha kuwa washindi si watu binafsi pekee bali ni Watanzania wote kwa ujumla," aliongeza Koka.

Ushirikiano wa Marioo unazinduliwa kwa kampeni kubwa za kitaifa, matukio ya kusisimua, na jackpots za kiwango cha juu ambazo zitawageuza mashabiki wake kuwa washindi.

"Mengi mazuri yanakuja! Kuna jackpots kubwa, matukio makubwa, na fursa kwa mashabiki wangu kushinda kama hawajawahi kushinda kabla. Hii ni mwanzo tu—Tanzania, jiandaeni!" Marioo alidokeza.

Muda wa kusubiri umekwisha. ITHUBA Tanzania iko tayari kuandika historia—ikibadilisha kila siku ya kawaida kuwa siku ya ushindi kwa kila Mtanzania!

Kwa kutumia hashtag rasmi #BahatiNasibuYaTaifa na #Inakuja, Bahati Nasibu ya Taifa inalenga kuongeza ushiriki wa kidijitali na kuwahamasisha Watanzania kote nchini kushiriki.




Rais wa Chama cha Walimu wa Tanzania (CWT) Mwalimu Leah Ulaya akizungumza kuhusiana na Kliniki ya Samia ya kutatua changamoto za Walimu,Mjini Tabora.

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Paul Chacha akizungumza wakati akifungua Kliniki ya Samia ya kutatua changamoto za Walimu iliyofanyika Ukumbi wa Isike Tabora.

Walimu wakiwa katika Kliniki ya kutatua changamoto yao iliyoratibiwa na CWT kwa kushirikiana na Serikali.

Ni Kliniki ya Samia ya kutatua changamoto za Walimu nchini.

Mkuu wa Mkoa wa Tabora asema Kliniki ni mafanikio ya Serikali kwa Walimu

Na Mwandishi Wetu Tabora

ZAIDI ya walimu 2000 wajitokeza kuhudumiwa Samia teachers clinik inayoratibiwa na CWT kwa kushirikiana na serikali kwa ajili ya kutatua changamoto za walimu nchini.

Ziara hiyo ya kutatua changamoto za walimu kwa Mkoa ndio Mkoa 15 Tangu kuanzishwa kwa Kliniki ambayo inaratibiwa na Chama cha Walimu Tanzania (CWT) kwa kushirikiana na Serikali katika kuwafikia Walimu kutoa changamoto za madai yao kwa ajili ya Serikali kufanyia kazi.

Akizungumza wakati akifungua Kliniki ya Walimu Mkoa Tabora Mkuu wa Mkuu wa Mkoa wa Tabora Paul Chacha amesema kuwa Kliniki ya Samia hiyo itatoa suluhu ya changamoto za Walimu ya madai ya walimu kulipwa.

Amesema kuwa Kliniki ya Walimu kuanzishwa kwake ni matokeo ya Serikali ya Awamu ya Sita ya Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan katika kwenda kutatua changamoto za Walimu kutokana na mchango wa walimu hao.

Amesema kuwa CWT ni Chama chenye nguvu na imara katika kusimamia masilahi ya Walimu na kutaka kuwa na umoja wao kushughulika katika kuendelea kuimarisha Chama.

Amesema kuwa vyama vingine zaidi ya CWT kwa viongozi hao kuendelea kuacha vyama hivyo na kuleta mawazo kujenga CWT kuendelea kuwa imara.

Mkuu wa Mkoa huyo amesema kuwa Walimu wa Mkoa wa wamejitoa sana katika kufundisha licha ya kuwa na madai na kufanya Mkoa kuendelea kufanya vizuri katika elimu.

Afisa Utumishi Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Judith Abdallah amesema wamejipanga katika kutatua changamoto za Walimu katika Kliniki ya Samia na kukutana na walimu na kuwasilisha madai yao.

Amesema kuwa walimu wamejipanga kutoa huduma kwa idadi iliyofika huku akidai madai mengine ni maelekezo katika mifumo.

Rais wa rais wa Chama cha Walimu (CWT) Mwalimu Leah Ulaya amesema Kliniki ya Samia wameanzisha katika kuwa rahisi ya kuwafikia walimu wakiwa na madawati ya kutoa huduma katika Wizara tano zinazoshughulika na walimu.

Amesema kuwa Chama kimejipanga kushirikiana na serikali katika kufanya utatuzi wa madai ya walimu kukutana walimu kila Mkoa

Aidha amesema katika kipindi hiki watashughulika na walimu katika kuweka utulivu huku serikali ikifanya mchakato wa ulipaji wa madai yao.

Mjumbe wa Kamati ya Utendaji Taifa Mkoa wa Tabora wa CWT Mwalimu Ally Nohoye amesema kuwa Kliniki ya Samia kuwa endelevu katika utatuzi wa changamoto za walimu.

Ameshukuru kwa kibali cha kuzunguka nchi nzima ya kusikiliza changamoto za walimu na kwenda kufanyia kazi kwa timu inayosikiliza changamoto hizo.

Katibu wa CWT Mkoa wa Tabora Mwalimu Condrus Stephen amesema kuwa mwitikio ni mkubwa kwa Walimu Tabora waliofika katika Kliniki ya Samia.

Mwenyekiti wa CWT Mkoa wa Tabora Mwalimu Emmanuel Manziriri amesema Kliniki ya Samia ni mkombozi kwa walimu.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Rais wa Msumbiji Mhe. Daniel Francisco Chapo kabla ya kuanza kwa Mkutano wa Kawaida wa 38 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika (AU) uliofanyika kwenye ukumbi wa Nelson Mandela uliopo Makao Makuu ya Umoja huo Addis Ababa nchini Ethiopia tarehe 15 Februari, 2025.

 



NA DENIS MLOWE IRINGA

ZAIDI ya bilioni 18 zimetengwa kupitia mradi wa Uboreshaji Miji (TACTIC) kwa ajili ya ujenzi wa soko la kisasa katika kata ya Kihesa na ujenzi wa barabara ya Mkimbizi Mtwivila kwa kiwango cha Lami kupitia bajeti ya mwaka wa fedha 2025/2026.

Hayo yamezungumzwa na Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa Ibrahim ngwada wakati wa Kikao cha Baraza la madiwani kilichokaa hivi karibuni wakati wa Kupitisha Bajeti ya mwaka wa fedha 2025/2026 ya halmashauri hiyo.

Meya Ngwada alisema kuwa katika kuboresha mji wa Iringa watakamilisha miradi mbalimbali likiwemo soko la Kihesa ambalo litakuwa kubwa kuliko soko la kisasa la Mlandege.

Alisema kuwa soko lililopo sasa la Kihesa litabomolewa na kujengwa soko la kisasa ili kukidhi utoaji wa huduma bora kwa wananchi mkoani hapa.

Alisema kuwa hadi sasa halmashauri imeshatekeleza miradi mbalimbali 18 ikiwemo kituo cha afya Mkimbizi ambacho kimeshaanza kufanya kazi, Kituo cha Afya Mkwawa kinaendelea na kazi na uwekezaji shilingi bilioni 3.5 katika hospitali ya Flerimo.

Aliongeza kuwa wamekamilisha mradi mingine kama Wodi ya watoto, karakana ya madawa, wodi za baba na mama, kituo cha afya Isiikalilo, ujenzi kituo cha Afya kata ya Kitwiru.

"* Kwa upande wa Afya hakika mama Samia katupendelea sana kwani vituo na zahanati zimejengwa kusaidia wananchi tunashukuru sana rais wetu kwa kufanikisha yote hayo ndani ya muda mfupi" Alisema

Alisema kuwa elimu miradi mbalimbali imejengwa ikiwemo ujenzi wa mabwenj, shule bora ya kisasa ya eneo la Uyole, Nduli na Kitwiru.

Meya alisema kwa upande wa barabara zitajengwa kwa kiwango cha lami za km5.11 katika kata ya Mtwivila na Mkimbizi ambapo tangazo limeshatoka la ujenzi la kutafuta wakandarasi.

Aidha halmashauri ya Manispaa ya Iringa itajenga jengo la ghorofa moja kwa ajili ya ofisi ya mkandarasi, ujenzi wa daraja kata ya Kitwiru litakalounganisha na kata ya Isakalilo ikiwa ni moja ya ahadi ya rais Samia aliyotoa kwa wananchi mkoani hapa.

Aliongeza kuwa Manispaa itajenga barabara ya mawe kama mfano kutoka shule ya Kiingereza ya Mapinduzi hadi eneo la Sunset Hotel ikiwa ni kuongeza uboreshaji wa barabara hizo ambapo eneo hilo limetengwa kwa ajili ya ujenzi wa mahotel mbalimbali na kutaka wananchi kujitokeza kununua viwanja.

Katika bajeti hiyo maeneo mengine yatakayofaidika ni barabara ya Kondoa Wihanzi hadi Mwembetogwa na Kijificheni, barabara ya kuelekea ofisi ya mkuu wa wilaya ambapo zitajengwa kwa kiwango cha lami.

"Jumla ya Mitaa 11 kunufaika na barabara za lami na vumbi na mawe, manispaa itaongeza taa za barabarani 10 ikiwemo eneo la Makanyagio na kuelekea ikulu ndogo eneo la Gangilonga." Alisema

Kwa upande wake Kaimu Meneja wa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini TARULA Mkoa wa Iringa Carol Lunyili alisema kupitia mradi wa kimkakati wa Uboreshaji miji (TACTIC) utaboresha miundombinu hasa ya barabara zilizopo katika kata za Mkimbizi Mtwivila na Kihesa kutokana na changamoto zilizopo.

Naye Diwani wa Kata ya Mtwivila Addo Gwegime amewashukuru TARULA wanazofanya na kuwaomba kuzifanyia kazi baadhi ya barabara zilizopo katika kata hiyo kwa kuwa zimekuwa zikiingizwa kwenye bajeti lakini hakuna utekelezaji.





 

Watanzania kutoka maeneo mbalimbali ya nchi wamejitokeza kwa wingi kutembelea Hifadhi ya Taifa ya Milima Udzungwa kusherehekea Sikukuu ya Wapendanao, Februari 14. Tukio hilo ni sehemu ya kuhamasisha utalii wa ndani na kuunga mkono juhudi za Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika kukuza sekta ya utalii kupitia kampeni mbalimbali.

Akizungumza kwa niaba ya Kamanda wa Kanda ya Mashariki wakati wa hafla maalum ya kuwapokea wageni hao, Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi Kanda ya Mashariki TANAPA, Fredrick Malisa, aliwapongeza Watanzania kwa mwitikio wao mkubwa wa kutembelea vivutio vya utalii nchini, akisema kuwa hatua hiyo ni ya kizalendo na inachangia kukuza uchumi wa taifa kupitia sekta ya utalii.

"Ni jambo la kufurahisha kuona Watanzania wakizidi kutambua thamani ya rasilimali za Nchi yao kwa kujitokeza kwa wingi kutembelea vivutio vya utalii. Hii inaonesha uzalendo na mchango wao katika kukuza sekta hii muhimu," alisema Malisa.

Kwa upande wake, Afisa Muhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Milima Udzungwa, Consepta Siima, akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Hifadhi hiyo, Theodora Bathio, alisema mwitikio huo ni ishara ya ongezeko la uelewa kuhusu umuhimu wa utalii wa ndani na faida zake kwa jamii na Taifa kwa ujumla.

"Tunafarijika kuona Watanzania wakishiriki kwa wingi katika utalii wa ndani, hasa katika siku muhimu kama hii ya Wapendanao. Hii ni ishara kwamba juhudi za serikali na wadau wa utalii za kuhamasisha wananchi kutembelea vivutio vyetu zinaendelea kuzaa matunda," alisema Siima.

Naye, Afisa Uhifadhi wa Hifadhi ya Taifa ya Milima Udzungwa, Ahmed Nassor, alieleza kuwa ujio wa wageni wengi katika Hifadhi hiyo unadhihirisha jinsi vivutio vya ndani vinavyothaminiwa na Wananchi.

"Hifadhi ya Milima Udzungwa ina hazina kubwa ya vivutio vya kipekee kama vile maporomoko ya maji ya Sanje, misitu ya mvua yenye viumbe wa kipekee, na njia za kupanda milima zinazotoa mandhari nzuri kwa wapenda mazingira. Tumejipanga kuhakikisha wageni wetu wanapata huduma bora na uzoefu wa kipekee," alisema Nassor.

Kwa upande wa wageni waliotembelea Hifadhi hiyo, Elia Wandwi, mmoja wa watalii wa ndani, alieleza kufurahishwa na uzoefu wake wa kwanza wa kulala kwenye mahema ndani ya Hifadhi, huku akifurahia mazingira ya asili na huduma zilizotolewa.

"Maandalizi na mapokezi yamekuwa mazuri sana. Tumefurahia mandhari ya kuvutia, burudani, na hata vyakula vya asili vinavyoakisi utamaduni wa eneo hili. Ni uzoefu wa kipekee ambao nitaukumbuka kwa muda mrefu," alisema Wandwi.

Utalii wa ndani umeendelea kushamiri Nchini Tanzania kutokana na juhudi za Serikali na wadau mbalimbali wa sekta hiyo. Kampeni kama Royal Tour zimechochea hamasa kubwa kwa Wananchi kujivunia na kutembelea vivutio vyao vya asili, hali inayochangia si tu maendeleo ya sekta ya utalii, bali pia uchumi wa Taifa kwa ujumla.










 








Benki ya Tanzania Commercial Bank (TCB)imewazawadia washindi wawili safari ya kwenda Zanzibar na malazi waliofanya miamala mingi katika msimu wa wapendanao kupitia kampeni iliyoendeshwa na benki hiyo ijulikanayo kwa jina la Mahaba Kisiwani.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Adam Mihayo, Mkurugenzi wa Biashara za Wateja Wadogo na Kati, Lilian Mtali amesema TCB imefanikiwa kukuza uelewa na matumizi ya bidhaa zake za kidijitali kwa kuwazawadia wateja hao waliofanya miamala mingi katika msimu wa wapendanao.

Amesema kampeni ya Mahaba Kisiwani inadhihirisha malengo ya kimkakati ya TCB kutumia teknolojia kukuza matumizi ya njia za kidijitali katika kufanya malipo.

Mtali amesema mbali na kuwakabidhi zawadi hizo washindi hao pia TCB inaadhimisha hatua muhimu ya miaka 100 ya huduma na ubora wa benki tangu kuanzishwa kwake.

Amewapongeza wafanyakazi wa benki hiyo kwa juhudi na mchango wao katika mafanikio ya benki hiyo. “Mafanikio ya benki yetu katika kipindi cha miaka 100 iliyopita ni matokeo ya juhudi na bidii za kila mmoja wetu.

“Tunadhamiria kuendelea kuboresha mazingira ya kazi ambayo kila mmoja anathaminiwa, anaungwa mkono na kuwezeshwa tunapoendelea kutoa huduma bora kwa wateja wetu,”amesema

Amesema TCB inaendelea kuahidi kuwekeza katika uvumbuzi wa kidijitali na kuongeza ubora kwa wafanyakazi wake ili kuhakikisha mustakabali wenye mafanikio kwa wateja pamoja na wafanyakazi wake

'HomeHabariTCB yawazawadia washindi wa kampeni ‘Mahaba Kisiwani.'

 

Na Mwandishi Wetu

SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar, imesema Bodi ya Mikopo ya Tanzania (HESLB) imeonyesha dhamira ya kweli kuwahudumia wanafunzi kwa kutoa mikopo kwa usawa bila ubaguzi wala upendeleo.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali, Lela Muhamed Mussa kupitia hotuba yake iliyosomwa na Katibu Mkuu Wizara hiyo, Khamis Abdalla Said alipomwakilisha katika kilele cha maadhimisho ya maonyesho ya elimu ya juu kisiwani Zanzibar.

“Tumeshuhuduia maendeleo makubwa kuwahudumia wananchi, hii hii ni kutekeleza dhamira ya serikali na mikopo hii inatolewa kwa usawa bila ubaguzi,” amesema

Amesema serikalii kupitia bodi hiyo imepunguza mzigo kwa wazazi na walezi kuhakikisha watanzania wanapata eimu ya juu na utekelezaji wake umekuwa wa haki sawa bila ubaguzi.

Akizungumzia kuhusu maonyesho hayo yamekuwa na tija kwa wadau wa elimu kwani changamoto zao zimesikilizwa na kupatiwa ufumbuzi.

Amesema hatua ya sasa kuwapo maofisa wa bodi katika vyuo vya Zanzibar, kumewasaidia wanafunzi hao kutatua changamoto na kupata miongozo mbalimbali.

Mkurugenzi Mtendaji Bodi ya Mikopo (HESLB) Dk Bill Kiwia amesema katika safari ya bodi ya mikopo, mpaka sasa imeshatoa mikopo ya Sh8.2 trilioni kwa wanafunzi 830,000.

Amesema kuna bidhaa mbalimbali zinazotolewa na bodi hiyo ikiwamo mikopo kwa shahada na stashahada na ruzuku ya Samia Scholarship kwa wanafunzi waliofanya vizuri katika masomo yao.

“Tunayo kila sababu katika kipindi hiki cha miaka 20, kuadhimisha na kusherehekea kwasabu ni safari ndefu tumepiga, amesema 

Amesema kwa mwaka huu 2024/25 wanadhani watakaribia wanafunzi milioni moja kwasababu wanasomesha wanafunzi 247,000 na Sh787 bilioni zimetolewa kuwalipa wanafunzi hao.

Umrat Suleiman mwenyekiti wa bodi ya mikopo Zanzibar  amesema zaidi ya wanafunzi 18570 wamenufaika na mkopo huo, wametoa Sh118 bilioni kuwakopesha na wamekusanya Sh24.10 bilioni 

Mmoja wa wanufaika kupitia Tasaf, Salha Bakari Said kutoka Chuo Kikuu cha Abdurahman Al Sumait ameshukuru kupatiwa mikopo wanafunzi na Tasaf kwani imekuwa link kati yao na bodi kupatiwa mikopo

Ameomba Serikali kuendeleza mpango huo kwani sio tu watasaidia wanafunzi pekee hata jamii kwa ujumla

“Tumeambiwa kuwa mwezi wa tisa mpango huu unafika mwisho, tunaomba uendelee umesaidia wengi,” amesema 

 Aisha Ali Mtumwa anayesoma kozi ya sayansi ya Elimu Sumait, ameishukuru Tasaf na bodi kwa kuwapatia mikopo huku akiomba waongezewe fedha kwa ajili ya kuwasaidia kumudu gharama zao.

“Sisi nyumbani tupo wengi lakini mimi mmoja pekee ndio nimefaidika kwahiyo bado wapo wengine wanahitaji kupata msaada kama huu,” amesema Aisha

Mwanafunzi mwingine, anayenufaika na Tasaf akisoma kozi ya sanaa katika elimu, Miraji Alfan Musa amesema iwapo mpango huo ukisitishwa utaleta changamoto kubwa kwa jamii kwani mpango huo umewanufaisha wengi. 

Amesema mzazi wake amepewa fedha za kujikimu na Tasaf “lakini ameanzisha biashara ya kufuga kuku, pamoja na mimi kupewa mkopo lakini kile anachokipata mzazi wangu kwenye biashara yake ananisaidia katika matumizi mengine ya kujikimu.”

Amesema serikali izidi kuziangalia kaya masikini ziendelee kunufaika na iwapo mpango ukisitishwa itaumia jamii nyingi kwa silimia kubwa imekuja kuwanyanyua wenye hali ya chini, kwasasa Tanzania sio masikinia sana kwasbabu ya Tasaf.

Kwa upande  Mratibu wa Tasaf Unguja, Makame Ali Haji amesema kupitia bodi ya mikopo kuanzia mwaka 2020 hadi sasa zaidi ya wanafunzi 100 kutoka kaya masikini wamefanikiwa kuingia elimu ya juu na kupata mikopo.

Amesema wanafunzi 60 wanafanya mitihani wamepatiwa mikopo kutoka bodi ya mikopo na kwa kushirikiana na bodi ya mikopo waongeze ili wapate asilimia 100 kwa wale ambao hawajapata.

Amesema katika fomu ya maombi ya mkopo bodi imeweka kipengele maalumu kumfanya mtoto atambulike ikiwa anatoka kaya masikini ambapo mwanafunzi anaingiza namba ya mpango wa kaya masikini.

“Tunashukuru sana bodi ya mikopo lakini tunaomba wandelee kutengeneza wigo ili wanafunzi wengi wapate elimu na kupata mikopo ili tupate rasilimali nzuri baadaye,” amesema






 

 

Na. Eva Ngowi, WF, KILIMANJARO

Serikali kupitia Wizara ya Fedha imewashauri wazazi na walezi kuwafundisha Watoto kuwa na utamaduni wa kujiwekea akiba ili kuwasaidia katika Maisha yao ya baadae.

Ushauri huo umetolewa na Mkurugenzi Msaidizi kutoka Wizara ya Fedha, Idara ya Uendelezaji wa Sekta ya Fedha, Bi. Dionensia Mjema, wakati wa semina zinazoendelea katika miji na vijiji mkoani Kilimanjaro, ikiwemo Shule za Sekondari, Mangi Mariale iliyopo Kata ya Mwika Kusini  na Mwika Sekondari iliyopo Kata ya Mwika Kaskazini Wilaya ya Moshi Vijijini.

Bi. Mjema alisema kuwa kuwafundisha Watoto kuweka akiba kutawajengea mfumo madhubuti wa kujenga uhakika wa masuala ya kifedha.

“Watoto wengi wamekiri kwamba walikuwa hawafahamu kwamba wanapopewa pesa wanatakiwa watumie kiasi na kiasi kingine waweke kama akiba ili siku wazazi wao wanapokosa pesa za kuwapa waweze kuzitumia.” Alisema Bi. Mjema.

Bi. Mjema alisema kuwa kwa sasa kuna Taasisi mbalimbali kama vile Benki, Mifuko ya Uwekezaji wa Pamoja inayoendeshwa na UTT AMIS zinatoa elimu kwa Watoto kuhusu namna ya kuweka akiba, hivyo ni muhimu kwa wazazi na walezi kutumia fursa hizo kwa ajili ya Watoto wao.

Awali, akifundisha wanafunzi katika Shule ya Sekondari Mwika, Bi. Mjema aliwataka wanafunzi hao wawe na tabia ama utamaduni wa kupanga bajeti ili wapate akiba ya kuweka, kutoka katika fedha wanazopewa na wazazi kwa ajili ya matumizi yao ya kawaida na kununua vitu ili waweke  akiba kiasi fulani cha fedha kinachobaki.

Vilevile Bi. Mjema alisema kuwa kuweka akiba ni njia za kuondokana na madeni yanayotokana na matumizi ya kila siku pamoja na gharama nyingine za maisha.Mkurugenzi Msaidizi kutoka Wizara ya Fedha, Idara ya Uendelezaji wa Sekta ya Fedha, Bi. Dionensia Mjema, akitoa Elimu ya Fedha kwa Wanafunzi walioshiriki semina ya Elimu ya Fedha kuhusu Umuhimu wa kuweka Akiba iliyofanyika katika Sekondari ya Mwika, Kata ya Mwika Kaskazini Wilaya ya Moshi Vijijini Mkoa wa Kilimanjaro.Wanafunzi wa Sekondari ya Mwika wakisikiliza Elimu ya umuhimu wa kuweka Akiba kutoka kwa Mkurugenzi Msaidizi wa Wizara ya Fedha, Idara ya Uendelezaji wa Sekta ya Fedha Bi. Dionensia Mjema (hayumo pichani) iliyofanyika katika Sekondari ya Mwika, Kata ya Mwika Kaskazini Wilaya ya Moshi Vijijini Mkoa wa KilimanjaroAfisa Mkuu Mwandamizi Idara ya Uendelezaji wa Sekta ya Fedha kutoka Wizara ya Fedha, Bw. Salimu Kimaro, akitoa elimu ya fedha kuhusu Akiba na Bajeti kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Mwika iliyoko Kata ya Mwika Kaskazini Wilaya ya Moshi Vijijini Mkoa wa Kilimanjaro.Afisa Mkuu Mwandamizi Idara ya Uendelezaji wa Sekta ya Fedha kutoka Wizara ya Fedha, Bw. Salimu Kimaro, akitoa elimu ya fedha kuhusu Akiba na Bajeti kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Mangi Mariale iliyoko Kata ya Mwika Kusini Wilaya ya Moshi Vijijini Mkoa wa Kilimanjaro.
Afisa Maendeleo ya Jamii Mwandamizi Mkuu kutoka Divisheni ya Maendeleo ya Jamii, Halmashauri ya Wilaya ya Moshi akiwapongeza wanafunzi waliojibu maswali vizuri baada ya kupata Elimu kutoka kwa Wataalamu wa Wizara ya Fedha katika Shule ya Sekondari ya Mareale iliyopo Kata ya Mwika Kusini Wilaya ya Moshi Vijijini Mkoa wa Kilimanjaro.
Picha ya Pamoja ya Walimu na Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Mareale mara baada ya kumaliza semina ya Elimu ya Fedha iliyofanyika katika shule hiyo iliyopo Kata ya Mwika Kusini Wilaya ya Moshi Vijijini Mkoa wa Kilimanjaro.
(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF, Kilimanjaro) 


Na. Eva Ngowi, WF, KILIMANJARO

Serikali imetoa rai kwa Wananchi kuwekeza fedha zao sehemu sahihi na salama badala ya kuwekeza fedha mahali ambapo pana vihatarishi.

Rai hiyo imetolewa katika Semina ya Elimu ya Fedha iliyotolewa katika Kata za Pasua na Majengo, Wilaya ya Moshi Manispaa Mkoa wa Kilimanjaro.  

Akiongea katika semina na Wajasiriamali wadogo, Vyama vya Waendesha Boda Boda/Bajaji na Vikundi vya Vikoba, Mchambuzi Fedha Mwandamizi kutoka Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA), CPA Gladness Mollel alisema kuwa ni vyema wananchi wakawekeza kwenye Masoko ya Mitaji ikiwemo uwekezaji katika Hisa za kampuni zilizoorodheshwa katika Soko la Hisa, Hati Fungani za Serikali na za Kampuni na katika Mifuko ya Uwekezaji wa pamoja. 

“Kuna faida nyingi za kuwekeza katika Hisa ikiwemo kupata gawio, ongezeko la thamani linalotokana na kupanda kwa thamani ya hisa” Alisema CPA Mollel

Alifafanua kuwa Hati Fungani za Serikali hutolewa kwa Umma na Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kwa niaba ya Serikali kupitia Soko la Awali ili kuiwezesha Serikali kupata fedha za kugharamia miradi ya maendeleo na kwamba CMSA huidhinisha utoaji wa hatifungani za kampuni ili kuziwezesha kupata mitaji na kutekeleza majukumu yake yaliyopangwa.

“Baada ya mauzo ya awali, Hati Fungani huorodheshwa kwenye Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE) ambapo huuzwa na kununuliwa na wawekezaji mbalimbali kulingana na nguvu ya Soko. 

Uwekezaji katika Hati Fungani unamsaidia mwekezaji kupata riba ya kila mwaka waliyokubaliana awali hadi pale Hati Fungani hiyo itakapokomaa. Vilevile, Mwekezaji anaweza kutumia hatifungani kama dhamana ya mkopo na huweza kukopeshwa na Benki za Biashara.” Alifafanua CPA Mollel.

Aidha, CPA Mollel alisema kuwa Uwekezaji wa Mifuko ya Uwekezaji wa Pamoja unahusisha kununua vipande kutoka kwa Meneja wa Mfuko ambapo mwekezaji ataweza kupata faida pale ambapo bei ya kipande inapoongezeka.

“Nawashauri wananchi kuwekeza kwenye Masoko ya Mitaji na Dhamana kwani ni salama kwa sababu hakuna athari.” Alisema CPA Mollel.

Kwa upande wake, Afisa Mwandamizi Masoko na Mawasiliano, kutoka Kampuni ya Uwekezaji ya UTT AMIS, Bw. Rahim Mwanga alisema kuwekeza kwenye Taasisi zilizosajiliwa kwa Mujibu wa Sheria inawezesha mwananchi kuwa na uhakika wa usalama wa mitaji yao, kupata faida shindani na kuwa na uhakika wa ukwasi endapo watahitaji tena kupata fedha zao.

”Tumepata fursa ya kukutana na wajasiriamali hapa Pasua na Majengo, na kuwapa elimu ya fedha kuhusu masuala mbalimbali ikiwemo kuwekeza kwenye Mifuko ya Uwekezaji wa Pamoja inayoendeshwa na UTT AMIS. Mifuko ya Uwekezaji wa Pamoja inawawezesha wananchi wengi zaidi kuendeleza utamaduni wa kuweka akiba na kuwekeza kwa urahisi kwenye Masoko ya Fedha na Mitaji kama sehemu mbadala ya uwekezaji. 

“UTT AMIS tunaendelea kusisitiza kuwa pamoja na mambo mengine, kuwekeza katika Mifuko sahihi ni uwekezaji ambao utawasaidia mbali na shughuli zao za biashara wanakuwa na uhakika wa kupata kipato nje ya biashara ile wanayoifanya moja kwa moja” Alisema Bw. Mwanga

Aidha, Bw. Mwanga alifafanua kuwa kupitia Mifuko ya Umoja, Wekeza Maisha, Watoto , Kujikimu, Ukwasi na Hati Fungani wananchi wanaweza kuanza kuwekeza kwa kiasi cha chini cha shilingi 10,000 hadi 100,000 kutegemeana na aina Mifuko.

Akitoa Elimu kwa Wananchi Bw. Rahim Mwanga aliongeza kuwa, Wawekezaji wanapata faida nzuri na shindani kati ya asimilia 12 hadi 15 kwa mwaka kulingana na hali ya soko. Pia urahisi wa kuwekeza na kutoa pesa. Wawekezaji wanaweza kujiunga kwa kupiga msimbo *150*82# na kuwekeza kwa kupitia mitandao yote ya simu na benki zote nchini.Diwani wa Kata ya Majengo Mhe. Humphrey Nelson Mosha akisoma vipeperushi ya Elimu ya Fedha alivyopewa wakati wa Semina ya Elimu ya Fedha kuhusu uwekezaji iliyofanyika katika Kata ya Majengo Wilaya ya Moshi Manispaa Mkoa wa Kilimanjaro.Mchambuzi Fedha Mwandamizi kutoka Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA), CPA Gladness Mollel akitoa elimu ya fedha juu ya Uwekezaji katika Hati Fungani wakati wa semina ya  Elimu ya Fedha iliyofanyika katika Kata ya Majengo Wilaya ya Moshi Manispaa Mkoa wa Kilimanjaro.

Afisa Mwandamizi Masoko na Mawasiliano, kutoka Kampuni ya Uwekezaji ya UTT AMIS, Bw. Rahim Mwanga, akitoa elimu ya fedha kuhusu Uwekezaji unaopatikana UTT AMIS wakati wa semina ya  Elimu ya Fedha iliyofanyika katika Kata ya Majengo Wilaya ya Moshi Manispaa Mkoa wa Kilimanjaro.Afisa Mkuu Mwanadamizi kutoka Wizara ya Fedha, Idara ya Uendelezaji wa Sekta ya Fedha, Bw. Salim Kimaro, akitoa Elimu ya Fedha kwa Wajasiriamali Wadogo, waendesha BodaBoda na Vikundi vya Vikoba katika Kata ya Pasua Wilaya ya Moshi Manispaa Mkoani Kilimanjaro.
Afisa Usimamizi Fedha Mwandamizi kutoka Wizara ya Fedha, Idara ya Uendelezaji wa Sekta ya Fedha Bw. Jackson Mshumba, akitoa Elimu ya Fedha kwa Wajasiriamali Wadogo, waendesha BodaBoda na Vikundi vya Vikoba katika Kata ya Pasua, Wilaya ya Moshi Manispaa Mkoani Kilimanjaro.


Top News