

Na mwandishi wetu,Zanzibar.
TAKWIMU zinaonyesha kati ya watu elfu sita hadi elfu 12, wanahofiwa kuugua ugonjwa wa himofilia nchini huku idadi ya watu waliogundulika kuwa na ugonjwa huo hadi sasa wakiwa ni 451 pekee.
Hayo yalisemwa na Waziri wa Afya wa Zanzibar, Mhe. Nassor Ahmed Mazrui katika hafla ya maadhimisho ya Siku ya Himofilia Duniani iliyofanyika pamoja na uzinduzi wa Kliniki ya Himofilia, katika Hospitali ya Wilaya ya Ijitimai, Visiwani humo jana.
Hafla hiyo iliandaliwa na Chama cha Himofilia Tanzania (HST), kwa uwezeshaji kutoka Taasisi ya himofilia ya novo nordisk na Chama cha Himofilia Duniani kwa ushirikiano kutoka Serikali ya Tanzania na ya Zanzibar, wizara za afya kutoka pande zote mbili, Hospitali ya Taifa Muhimbili na wadau wengine.
Mheshimiwa waziri alisema takwimu za kidunia zinaonesha mtu mmoja kati ya 10 anapatikana na ugonjwa huo, hii ikimanisha kuwa Tanzania yenye watu takribani milioni 61 inaweza kuwa na wagonjwa elfu 6 hadi elfu 12, huku ikielezwa 97% ya watu wenye ugonjwa huu duniani kote hawajagundulika, ambapo kwa upande wa Tanzania waliogundulika mpaka sasa ni 451 tu.
“Kama tunavyofahamu himofilia ni ugonjwa wa damu kukosa uwezo wa kuganda unaosababishwa na ukosefu wa kiwango cha chembechembe za protini zinazotakiwa kugandisha damu hivyo kusababisha damu kuvuja kwa mda mrefu pindi mtu anavyopata jeraha hivyo kuhatarisha maisha yake.
“Maisha ya watu wenye matatizo haya yanahitaji uangalizi mkubwa na tahadhari kubwa ili kuzuia uvujaji wa damu, ulemavu na vifo hivyo kuwepo na hitaji la kubaini aina ya himofilia na kupata matibabu ya kuchomwa sindano yenye chembechembe za protini zinazokosekana mwilini ili kusaidia kuzalisha damu”, alisema Waziri Mazrui.
Alisema Mwaka 2020 Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ikishirikiana na Taasisi ya himofilia ya novo nordisk ilianzisha mradi wa kuongeza kasi ya upatikanaji wa huduma kwa watu wenye magonjwa ya damu lengo kuu ikiwa ni kuunga mkono serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya afya katika kupunguza madhara ya vifo vinavyotokana na magonjwa yasiyo ambukiza ikiwemo himofilia na selimundu.
Pamoja na hayo alisema, lengo kubwa la mradi huu ni kuwezesha upatikanaji wa vipimo vya wagonjwa wa damu, seli mundu, na himofilia katika hospitali za rufaa nchini sambamba na kuanzisha kliniki za magonjwa hayo, kuwezesha mafunzo na upatikanaji wataalamu wa afya waliobobea kwenye hospitali hizo pamoja na upatikanaji wa miundo mbinu sahihi, vipimo na dawa ili wagonjwa wahudumiwe mahali popote nchini bila kulazimika kufika Muhimbili.
“Katika maadhimisho haya leo nina furaha kubwa kuwaambia kuwa mradi huu katika kipindi cha uhai wake kuanzia kipindi cha kwanza hadi kipindi cha pili tayari umefanikisha kukamilisha ukarabati wa kliniki za himofilia katika hospitali 13 zikiwemo hospitali za Muhimbili, KCMC, mbeya na Bugando.
“Tunawashukuru pia wafadhili wetu kwa msaada wa dawa zenye thamani ya shs milioni 500, kwa kweli mmetusaidia sana na vifaa nyenye gharama kubwa, chini ya uongozi wa maraisi wetu, Samia Suluhu Hassan na Hussein Ali Mwinyi, tunaendelea kufanya kazi usiku na mchana kuhakikisha kila mtanzania anapata matibabu kwa usahihi na kwa wakati, hivyo juhudi zenu hizi zinatufanya twende sambamba na juhudi za viongozi wetu hawa”, aliongeza waziri huyo.
Akizungumzia zaidi kuhusu himofilia, Mwenyekiti wa Chama cha Himofilia Tanzania (HST), Dk. Stella Rwezaura alisema, asilimia 70 ya wagonjwa wa himofilia wanarithi na inabebwa katika kinasaba cha kike, kwani mwanamke ana ‘x’ mbili na mwanaume ana ‘xy’, hivyo endapo mwanamke ana ‘x’ yenye vinasaba vya himofilia, asilimia 50 ya watoto wake wa kiume watakuwa na tatizo hilo hivyo kufanya asilimia 99 ya wagonjwa wa himofilia kuwa wanaume.
“Tunaposherehea Siku ya Himofilia Duniani, sambamba na Kauli Mbiu ya Mwaka 2025 isemayo, ‘Wanawake na Wasichana pia wanakumbwa na tatizo la kuvuja damu, licha ya himofilia kuwapata zaidi wanaume, tuwaite wanawake waje kupima, waweze kutambulika mapema hivyo kupata matibabu sahihi.
“ Lengo la mradi huu ni kuwatambua wagonjwa wengi zaidi na kupata huduma kwani wapo wengi wenye tatizo hili na hii ilitokana na changamoto ya uhaba wa vifaa, mashine na vitendanishi vya kutambua ugonjwa huu, hivyo kwa msaada wa wafadhili, vyama vya wagonjwa pamoja na serikali yetu sikivu ya Tanzania, ikiongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan pamoja Rais wa Zanzibar, Dk. Hussein Mwinyi, wizara yake ya afya na wadau wengine, huduma hizi sasa zinafika karibu kwa wananchi kwa usahihi zaidi”, aliongeza Dk. Stella.
Naye mmoja wa wagonjwa wa Himofilia ambaye pia anauguza watoto wawili wenye ugonjwa huo, Regina Shirima alisema anakabiliwa na changamoto kubwa ya hali duni ya kiuchumi baada ya kutumia muda wake mwingi katika kuhudumia watoto hivyo kutokuwa na muda kabisa wa kujishughulisha na kazi za kujitafutia kipato.
“changamoto nyingine ni kwa watoto wenyewe hawapati muda wa kusoma, kucheza na wenzao ama kuwa na furaha kwani muda mwingi wanakuwa wagonjwa, lakini ni ukweli kuwa wanawake ndio wanabeba vinasaba vya himofilia, lawama nyingi zinakuja kwetu kwa kuzaa watoto wenye changamoto hii, hivyo unajikuta familia imekuacha”. Akiongeza kuwa kuna wakati kulikuwa na changamoo ya upatikanaji wa dawa ukizingatia kuwa mgonjwa wa himofilia akikosa dawa tu anaweza uhai wake unakuwa hatarini.
“Natoa wito kwa jamii kuwa gonjwa hili la himofilia lipo na mama sio anayesababisha mtoto kuzaliwa na ugonjwa huu, kwani huwezi kupata mtoto bila ya baba”, aliongeza Bi. Regina kwa mshangao.
Awali akizungumza katika hafla hiyo, Mwenyekiti wa Bodi ya Chama cha Himofilia Tanzania (HST), Dk. Lawrence Museru alisema HST imekuwa sauti ya wenye ugonjwa wa himofilia katika kuangalia changamoto wanazopitia katika kutafuta tiba, moja ya changaoto ni utambuzi wa ugonjwa huu katika jamii.
“Wagojwa wamekuja kutambulika baada ya kupoteza maisha ama kupata ulemavu wa kudumu kwasababu ugonjwa huo haukutambulika hivyo tunaokoa sauti yao kuona jamii na watoa huduma za afya wanatambua ugonjwa huo na wagonjwa wanapata tiba sahihi.
“Tiba sahihi ni ghali sana na serikali haiwezi peke yake, hivyo lazima uwepo ushirikiano kutoka kwa sisi chama ambacho kina wataalamu na wadau wengine ili kuusemea ugonjwa huu, na tunaimani uwepo wako mheshimiwa waziri unafanya ugonjwa huu usemeke katika vyombo vya maaumuzi”, alisema Prof. Museru.
Akimkaribisha Mheshimiwa Waziri, Mkurugenzi wa Tiba na Elimu ya Afya Zanzibar, Dk. Marijani Msafiri alisema katika kipindi cha miaka minne, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar chini ya uongozi wa Dr. Hussein Ali Mwinyi imefanya mapinduzi makubwa katika kuboresha huduma za afya, ikiwa ni pamoja na ujenzi wa hospitali 10 za wilaya na hospitali moja kubwa ya kisasa ya mkoa ya Lumumba.
“Ndani ya hospitali hizi sasa tumeimarisha miundombinu na huduma, serikali yetu ya awamu na nane pia imeamua kufanya kazi na sekta binafsi ili kutoa huduma bora kwa wagonjwa wote ikiwa ni pamoja na wagonjwa wa himofilia, zikiwemo huduma za maabara, utoaji wa dawa na uendeshaji wa hospitali”, alisema Dk. Msafiri.


Waziri wa Afya wa Zanzibar, Mhe. Nassor Ahmed Mazrui (katikati), akiagana na Mwenyekiti wa Chama cha Himofilia Tanzania (HST), Dk. Stella Rwezaura, mara baada ya maadhimisho ya Siku ya Himofilia Duniani iliyofanyika pamoja na uzinduzi wa Kliniki ya Himofilia, katika Hospitali ya Wilaya ya Ijitimai, Visiwani Zanzibar jana. Mstari wa chini ni baadhi ya watoto wanaougua ugonjwa wa himofilia.

Mwenyekiti wa Bodi ya Chama cha Himofilia Tanzania (HST), Prof. Lawrence Museru (katikati), akiongoza maandamano kuadhimisha Siku ya Himofilia Duniani, Visiwani Zanzibar jana. Maadhimisho hayo yalifanyika pamoja na uzinduzi wa kliniki ya Himofilia katika Hospitali ya Wilaya ya Ijitimai, visiwani humo.


Mkazi wa Zanzibar, Baba mwenye watoto wawili wanaougua himofilia, Suleiman Ali Seif, akishiriki matembezi akiwa na watoto wake wenye ugonjwa huo, Murshin Ali (kulia), na Sahir Ali, wakati wa maadhimisho ya Siku ya Himofilia Duniani, mjini Zanzibar jana. Maadhimisho hayo yaliyofanyika pamoja na uzinduzi wa Kliniki ya Himofilia, yaliandaliwa na Chama cha Himofilia Tanzania (HST), kwa uwezeshaji kutoka Taasisi ya himofilia ya novo nordisk na Chama cha Himofilia Duniani. Himofilia ni ugonjwa wa damu kukosa uwezo wa kuganda unaosababishwa na ukosefu wa kiwango cha chembechembe za protini zinazotakiwa kugandisha damu hivyo kusababisha damu kuvuja kwa mda mrefu pindi mtu anavyopata jeraha hivyo kuhatarisha maisha yake.

Waziri wa Afya wa Zanzibar, Mhe. Nassor Ahmed Mazrui (kushoto), akisalimiana na Mwenykiti wa Bodi ya Chama cha Himofilia Tanzania, Prof. Lawrence Museru, wakati akipokea maandamano, yaliyokuwa sehemu ya shamrashamra za maadhinisho ya Siku ya Homifilia Duniani, sambamba na uzinduzi wa Kliniki ya Himofilia, katika Hospitali ya Wilaya ya Ijitimai, mjini Zanzibar, jana.


Waziri wa Afya wa Zanzibar, Mhe. Nassor Ahmed Mazrui (katikati), akiwa na wawakilishi kutoka Chama cha Himofilia Tanzania (HST), Taasisi ya himofilia ya novo nordisk, Wizara za afya kutoka Tanzania na Zanzibar, Hospitali ya Taifa Muhimbili, Chama cha Himofilia Duniani na wadau wengine katika hafla ya maadhimisho ya Siku ya Himofilia Duniani iliyofanyika pamoja na uzinduzi wa Kliniki ya Himofilia, katika Hospitali ya Wilaya ya Ijitimai, Visiwani Zanzibar jana.
Na: Calvin Gwabara
Vijana kama nguvu kazi ya
maendeleo ya Jumuiya ya Afrika Mashariki wametakiwa kujifunza, kuipenda na kuisambaza
lugha ya Kiswahili ili kuifanya jumuiya hiyo kuwa imara na kudumisha umoja kwa
nchi zote.
Wito huo umetolewa na Mhadhiri mwandamizi
na Mkuu wa Idara ya Taaluma za lugha kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo
SUA Dkt. Onesmo Nyinondi wakiti akitoa wasilisho lake kwenye kongamano la
kwanza la kimataifa la Kiswahili lililofanyika kwenye uwanja wa taifa wa
sherehe za uhuru Kololo Kampala nchini Uganda.
“Vijana ukisikiliza wimbo wetu wa Jumuiya ya
afrika mashariki unazungumzia umoja wetu ndio nguzo yetu lakini ili tuweze
kufikia lengo hilo ni lazima tuwe na lugha moja inayotuunganisha wanajumuiya yote
ya afrika mashariki ili mtu anapotoka eneo moja kwenda kwingine kufanya
biashara au kutafuta maisha aweze kuelewana kwa lugha moja na sisi lugha yetu
ni Kiswahili” alifafanua Dkt. Nyinondi.
Aliongeza “ Umoja tunaouimba
unatoka wapi kama mtu akitoka Guru kwenda Mbarara haelewani lugha na watu wa
pale na akitoka Mbarara kwenda DRC kongo au Kenya hawezi kuwasiliana? Swala la
Kiswahili linahitaji msukumo wa kipekee ili kifahamike na kutumiwa na watu wote
ndani ya jumuiya yetu”.
Akitolea mfano maneno kwenye kitabu
cha mwanzo 11 msatari ule wasita kuhusu waliotaka kujenga mnara wa babeli na
baada ya Mungu kuona watu wale kwa umoja wao wanaweza kweli kufika mbinguni
aliwabadilishia lugha na hivyo kuwafanya washindwe kuelewana na hatimae ujenzi
wa mnara wa babeli ukakwama.
Dkt. Onesmo amesema umoja na maendeleo
ya Jumiya ya Afrika ya Mashariki yanawahitaji vijana ambao wanaongea lugha moja ya Kiswahili vizuri katika
shughuli mbalimbali ili kuondoa kikwazo cha lugha kwenye masuala ya
mashirikiano baina yao.
Aidha amependekeza kuwepo na
vitabu vidogovidogo ambavyo vinaeleza kwa Kiswahili mambo mbalimbali ya
makabila yaliyo ndani ya jumuia hiyo ili kila mmoja aweze kuelewa pamoja na
vitabu vyene istilahi zake kwenye shughuli mbalimbali za maendeleo.
Pia amependekeza kuwe na wiki ya
Kiswahili ili kuongeza uelewa kwa jamii kwenye jumuiya yote na kuona kuwa
pamoja na mipaka ya afrika mashariki lakini Kiswahili kiwe kiunganishi kikubwa
cha watu ndani ya jumuiya nzima.
Mhadhiri huyo kutoka SUA amesema mapinduzi
ya jambo lolote huanza na mtu mmoja na kisha kikundi na baadae jamii nzima
hivyo kila mmoja aanze kufikiria umuhimu wa lugha ya Kiswahili kwa maendeleo ya
watu maana penye nia pana njia.
Akitoa wasilisho lake
liliohudhuriwa na Balozi wa Tanzania nchini Uganda na Balozi wa Uganda nchini
Tanzania sambamba wawasilishaji wengine akiwemo Prof. PLO Lumbumba, Prof
A. Mtembei, Prof Wala na maguru wengine wa Kiswahili duniani na
kushirikisha watu wengine mbalimbali zaidi ya 8000 wakiwemo Wanasiasa, Maafisa
wa serikali, mabalozi, wasimamizi kutoka vyuoni, walimu, wanafunzi
Kongamano hilo lilihusisha washiriki kutoka nchi za Uganda, Tanzania, Kenya, Somalia, South Sudan, DRC, Rwanda, Burundi, Ghana, Nigeria and Canada.
Vijana kama nguvu kazi ya
maendeleo ya Jumuiya ya Afrika Mashariki wametakiwa kujifunza, kuipenda na kuisambaza
lugha ya Kiswahili ili kuifanya jumuiya hiyo kuwa imara na kudumisha umoja kwa
nchi zote.
Wito huo umetolewa na Mhadhiri mwandamizi na Mkuu wa Idara ya Taaluma za lugha kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA Dkt. Onesmo Nyinondi wakiti akitoa wasilisho lake kwenye kongamano la kwanza la kimataifa la Kiswahili lililofanyika kwenye uwanja wa taifa wa sherehe za uhuru Kololo Kampala nchini Uganda.
“Vijana ukisikiliza wimbo wetu wa Jumuiya ya
afrika mashariki unazungumzia umoja wetu ndio nguzo yetu lakini ili tuweze
kufikia lengo hilo ni lazima tuwe na lugha moja inayotuunganisha wanajumuiya yote
ya afrika mashariki ili mtu anapotoka eneo moja kwenda kwingine kufanya
biashara au kutafuta maisha aweze kuelewana kwa lugha moja na sisi lugha yetu
ni Kiswahili” alifafanua Dkt. Nyinondi.
Aliongeza “ Umoja tunaouimba
unatoka wapi kama mtu akitoka Guru kwenda Mbarara haelewani lugha na watu wa
pale na akitoka Mbarara kwenda DRC kongo au Kenya hawezi kuwasiliana? Swala la
Kiswahili linahitaji msukumo wa kipekee ili kifahamike na kutumiwa na watu wote
ndani ya jumuiya yetu”.
Akitolea mfano maneno kwenye kitabu
cha mwanzo 11 msatari ule wasita kuhusu waliotaka kujenga mnara wa babeli na
baada ya Mungu kuona watu wale kwa umoja wao wanaweza kweli kufika mbinguni
aliwabadilishia lugha na hivyo kuwafanya washindwe kuelewana na hatimae ujenzi
wa mnara wa babeli ukakwama.
Dkt. Onesmo amesema umoja na maendeleo
ya Jumiya ya Afrika ya Mashariki yanawahitaji vijana ambao wanaongea lugha moja ya Kiswahili vizuri katika
shughuli mbalimbali ili kuondoa kikwazo cha lugha kwenye masuala ya
mashirikiano baina yao.
Aidha amependekeza kuwepo na
vitabu vidogovidogo ambavyo vinaeleza kwa Kiswahili mambo mbalimbali ya
makabila yaliyo ndani ya jumuia hiyo ili kila mmoja aweze kuelewa pamoja na
vitabu vyene istilahi zake kwenye shughuli mbalimbali za maendeleo.
Pia amependekeza kuwe na wiki ya
Kiswahili ili kuongeza uelewa kwa jamii kwenye jumuiya yote na kuona kuwa
pamoja na mipaka ya afrika mashariki lakini Kiswahili kiwe kiunganishi kikubwa
cha watu ndani ya jumuiya nzima.
Mhadhiri huyo kutoka SUA amesema mapinduzi
ya jambo lolote huanza na mtu mmoja na kisha kikundi na baadae jamii nzima
hivyo kila mmoja aanze kufikiria umuhimu wa lugha ya Kiswahili kwa maendeleo ya
watu maana penye nia pana njia.
Akitoa wasilisho lake
liliohudhuriwa na Balozi wa Tanzania nchini Uganda na Balozi wa Uganda nchini
Tanzania sambamba wawasilishaji wengine akiwemo Prof. PLO Lumbumba, Prof
A. Mtembei, Prof Wala na nguli wengine wa Kiswahili duniani na
kushirikisha watu wengine mbalimbali zaidi ya 8000 wakiwemo Wanasiasa, Maafisa
wa serikali, mabalozi, wasimamizi kutoka vyuoni, walimu, wanafunzi
Kongamano hilo lilihusisha washiriki kutoka nchi za Uganda, Tanzania, Kenya, Somalia, South Sudan, DRC, Rwanda, Burundi, Ghana, Nigeria and Canada.
Akizungumza Mwenyekiti wa Kamati hiyo, ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Madaba Mkoani Ruvuma Dkt. Joseph Kizito Mhagama, ametoa pongezi hizo Jijini Dodoma kwa niaba ya Kamati yake wakati wa ziara ya kikazi ya Kamati hiyo iliyolenga kutembelea na kujifunza utendaji kazi wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma.
Dkt. Mhagama ametolea mfano maoni ambayo Kamati yake iliyatoa kuhusu usaili kufanyika katika ngazi za mikoa badala ya kuwalazimu waombaji kazi wote kufika Dodoma kumeleta matokeo chanya kwa waombaji kazi hao.
Vilevile, Dkt. Mhagama amezungumzia matumizi ya mfumo wa Ajira Portal kwa waombaji kazi kuondokana na dhana tofauti ya upendeleo wa kupata ajira katika Utumishi wa Umma.
“Mfumo wa Ajira Portal umeondoa dhana ya kuwepo kwa upendeleo kwa waombaji kazi, ninaamini wengi wamepata ajira serikalini pasipo kupitia kwa mtu yeyote,” amesema Mhe. Dkt. Mhagama.
Kwa upande wake, Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Deus Sangu, ameishukuru Kamati hiyo kwa kutoa maoni na ushauri mara zote ambao kwa kiasi kikubwa umesaidia kutekeleza majukumu ya Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma kikamilifu.
Aidha, Naibu Waziri Sangu amewaomba Wajumbe wa Kamati hiyo kuendelea kuwa Mabalozi wazuri wa Sekretarieti ya Ajira Katika Utumishi wa Umma ili kuwahakikishia wananchi kuhusu uwazi wa namna ajira katika Utumishi wa Umma zinavyopatikana kwa kuzingatia Sheria, Kanuni na Taratibu zilizowekwa na Sekretarieti hiyo wakati wa kuomba kazi.
Akielezea mafanikio baada ya kutumia mfumo wa Ajira Portal, Kaimu Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma, Mhandisi Samweli Tanguye amesema, kupitia mifumo wameweza kuajiri Rasilimaliwatu yenye uwezo wa kufanya kazi na kutoa matokeo chanya pamoja na kuondoa hoja za kuajiri kwa dhana ya upendeleo.
MIAKA minne ya serikali ya awamu ya sita madarakani Mfuko wa Maendeleo ya Jamii(TASAF),kupitia Mpango wa kunusuru kaya maskini umefanikiwa kuhitimisha kaya za walengwa takribani 400,000 nchi nzima baada ya kuhudumiwa kwa takribani miaka 10.
Hilo limefanikiwa kutokana na utekelezaji wa afua mbalimbali ambapo zimeboresha maisha,kuongeza rasilimali na zinaweza kuendelea kuendesha maisha yao bila ya ruzuku ya TASAF.
Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora George Simbachawene amesema hayo April 17,2025,Jijini Dodoma wakati akieleza mafanikio ya serikali ya awamu ya sita kwa waandishi wa habari.
Amesema kupitia mpango wa miradi ya kutoa ajira za muda kwa walengwa hadi kufikia Disemba 2024,jumla ya miradi 27,863 ya kutoa ajira za muda kwa walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini imetekelezwa ambapo jumla ya Kaya za Walengwa 662,000 zimelipwa jumla ya shilingi bilioni 213.8.
"Licha ya kuongeza kipato, walengwa pia wameweza kupata ujuzi wa utekelezaji wa miradi hiyo unaoweza kutumika katika shughuli za kukuza uchumi wa kaya na kuongeza kipato,miradi hii imenufaisha sekta za kilimo, barabara, misitu, maji na mazingira,"amesema.
Pia kupitia miradi ya kuendeleza na kuboresha Miundombinu ya Huduma za Jamii jumla ya miradi 137 ya uendelezaji miundombinu yenye thamani ya shilingi bilioni 12.67 ilitekelezwa katika Mamlaka za maeneo ya utekelezaji 29.
Kati ya hiyo miradi hiyo 6 imekamilika na 72 ilikuwa katika hatua mbalimbali za utekelezaji. ambapo miradi ya aina hiyo imetatua changamoto za jamii zinazotokana na upungufu au kutokuwepo kabisa kwa miundombinu ya kutosha ya kutolea huduma za jamii katika sekta za Elimu, Afya na Maji.
"Hadi kufikia Desemba, 2024, jumla ya miradi ya jamii 1,518 yenye thamani ya shilingi bilioni 81.8 imetekelezwa ambapo miradi 659 imekamilika na inatumika kutoa huduma na miradi 859 ipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji kupitia miradi ya Kupunguza Umaskini Tanzania-Awamu ya Nne(TPRP IV),"amesema Waziri Simbachawene.
Aidha, amesema TASAF kwa kushirikiana na Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu(HESLB) imewezesha waombaji wa mikopo ya elimu ya juu kutoka kaya za walengwa kutambulika, kupatiwa mikopo ya elimu kwa asilimia 100 ambapo hadi kufikia Novemba 2024 jumla ya wanafunzi 8,274 wamenufaika na mikopo hii.
MBUNIFU na Mkurugenzi wa Kampuni ya Nunu get software Development Company Jeremiah Malamka ameipongeza serikali kupitia Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH),Kwa kufanikisha kuwawezesha wabunifu kupata mikopo nafuu.
Malamka ambaye ni mnufaika wa mikopo hiyo,amesema hatua hiyo imefuta dhana ya muda mrefu ya “Poor Government Support” na ukosefu wa fedha, ambayo kwa miaka mingi ilikuwa ikitajwa kwenye vitabu vya taaluma.
“Tumeisoma ‘Poor Government Support’ kwenye vitabu miaka mingi, lakini sasa tumeishuhudia historia ikiandikwa,"amesema Malamka.
Amesema Serikali imeonyesha kwa vitendo kuwa ipo tayari kusimama na wabunifu wake hivyo nao wataendelea kupambana ilinkuhakikisha wanatumia fursa zinazotolewa na serikali.
Aidha, Malamka ameishukuru COSTECH kwa hatua ya kuwatambua wabunifu wa Kitanzania na kuwapa hadhi inayostahili, akisema hatua hiyo si tu imewapa heshima, bali pia imewapa nguvu mpya ya kuamini kuwa wanathaminiwa na taifa lao.
“Kwa miaka mingi wabunifu tulikuwa kama watu walioachwa nyuma. Leo COSTECH imetufanya tuhisi kuwa sehemu ya mfumo rasmi wa maendeleo. Tunawashukuru sana kwa kututambua,” amesema.
Mpango huu wa ushirikiano kati ya COSTECH na CRDB unalenga kutoa mikopo nafuu ya jumla ya Shilingi Bilioni 4.6, ambapo kati ya hizo, Serikali kupitia COSTECH imetoa dhamana ya Bilioni 2.3.
Hii ni hatua ya utekelezaji wa moja kwa moja wa maelekezo ya Rais Samia Suluhu Hassan ya kuwawezesha vijana na kukuza uchumi wa viwanda kupitia ubunifu wa ndani.
Mbali na hayo, aliwahimiza wadau wengine kutoka sekta binafsi, mashirika ya maendeleo, na serikali za mitaa kujitokeza na kuunga mkono juhudi hizi ili kuhakikisha kuwa kila wazo la ubunifu linapewa nafasi ya kukua na kuwa chanzo cha ajira, mapato, na heshima ya kitaifa.






TAARIFA RASMI KUTOKA CHAMA CHA NLD
APRILI 18, 2025,
MABADILIKO YA NEMBO NA BENDERA YA CHAMA, NI HATUA YA KIHISTORIA KWA NLD.
Chama cha National League for Democracy (NLD) kinapenda kuwataarifu wanachama, wafuasi na wananchi kwa ujumla kuwa, kufuatia Mkutano Mkuu Maalum uliofanyika tarehe 10 Aprili 2025, wajumbe wa mkutano huo kwa kauli moja waliridhia mapendekezo ya kubadilisha bendera na nembo ya chama.
Mabadiliko haya ni ya heshima na kihistoria, yakilenga kusawiri kwa undani zaidi maono, dira, na mwelekeo mpya wa chama chetu kuelekea kujenga taifa lenye demokrasia imara, usawa wa kijamii, Uzalendo Haki na Maendeleo.

Kupitia uongozi imara wa Mwenyekiti wa Taifa Mhe. Khamis Mfaume na Katibu Mkuu Doyo Hassan Doyo, Sekretarieti ya chama imekamilisha maboresho ya nembo na bendera mpya, ambazo sasa zinakwenda kutambulika rasmi kitaifa na kimataifa kama utambulisho wa chama.
RANGI YA BENDERA MPYA YA NLD NA MAANA YAKE.
Njano, Inaashiria maliasili, misitu na madini.
Nyeusi, Ni alama ya utu wetu, asili yetu na uafrika wetu.
Bluu, Inawakilisha rasilimali za maji, bahari, mito na maziwa (Blue Economy).
Nyekundu, Inawakilisha harakati za mapambano ya demokrasia katika nchi yetu.
NEMBO MPYA YA NLD.
Mkono mmoja wa ushindi (Victoria), unaashiria matumaini, nguvu na mafanikio.
Nyota tatu, zinawakilisha dira isiyo na kikomo ya chama chetu.
Kwa niaba ya uongozi wa chama, tunawapongeza sana wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa kwa uamuzi huu wa busara na kizalendo. Mabadiliko haya yanadhihirisha kukua kwa chama na dhamira ya chama kusimamia misingi ya demokrasia, utawala bora na mshikamano wa kitaifa.
#NLD #MageuziYaKihistoria #DemokrasiaKwaVitendo #BenderaMpyaNLD #NemboMpyaNLD
NLD: Ukombozi wa Umma.
NLD: Mtetezi wa Umma.
NLD: Moto Moto Motooo!
Imetolewa na: Idara ya Habari na Mawasiliano
Chama cha NLD
Tandika, Temeke Jijini Dar es salaam, Tanzania
Tarehe: 18 Aprili 2025
Hayo yamezungumzwa na Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Wizara ya Ujenzi Mrisho Mrisho, wakati akifunga kikao cha ndani chaWafanyakazi wa Bodi ya Mfuko wa Barabara kilichofanyika kwa siku tatu mkoani Morogoro kwa ajili ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji katika utumishi wa umma .
Mrisho amesema miongozo hiyo inatoa viwango vya uandishi wa nyaraka kama vile uandishi wa barua za Serikali na una dhumuni la kuweka muundo wa pamoja katika mawasiliano ya kiserikali.
Katika hatua nyingine, Mkurugenzi huyo ametoa wito kwa watumishi wa Bodi hiyo kuboresha mahusiano na mawasiliano ndani ya Bodi ili kuongeza tija na ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao.
Aidha Kaimu Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Mfuko wa Barabara Mhandisi Rashid Kalimbaga, ameeleza kuwa jumla ya watumishi 32 wameshiriki katika kikao hicho na kupata mafunzo yenye lengo la kuwajengea uwezo na kuwaongezea ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku na kwamba watumishi hao pia wameapa na kutia saini viapo vya utunzaji siri za Serikali.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Idara ya Mipango na Mapato kutoka Bodi ya Mfuko wa Barabara Godlove Stephen amesema watahakikisha wanayatekeleza vyema waliyojifunza hasa katika uandishi wa taarifa mbali mbali za Bodi kwa kuzingatia miongozo iliyopo pamoja na kuimarisha ushirikiano baina ya watumishi.
Naye, Afia Ndyamukama Mtumishi kutoka Bodi ya Mfuko wa Barabara ameiomba Bodi kutoa mafunzo kama hayo kwa watumishi mara kwa mara ili kuwajengea uwezo na kuwaongezea ufanisi zaidi katika utendaji kazi wao wa kila siku.
SERIKALI inatarajia kuanza kutoa ripoti ya kila mwaka ya Mradi wa Jenga iliobora (BBT),ili kuonyesha kilichofanyika kwa wanawake na vijana kwa mwaka mzima katika maeneo mbalimbali kupitia mradi huo.
Aidha amesema Waziri Mkuu Kassim Majaliwa,ataizindua rasmi ripoti hiyo Aprili 27 jijini Dodoma itahusisha mambo mbalimbali kwenye sekta ya kilimo kwa upande wa serikali na sekta binafsi.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Kilimo Hussein Bashe katika mkutano wa wadau wanaotekeleza miradi ya kuwezesha vijana na wanawake katika sekta ya kilimo -mazao uliofanyika jana jijini Dodoma.
Bashe amesema wanafanya hivyo ili kuonyesha maendeleo yaliyofanyika na wizara ya kilimo kwenye sekta ya kilimo kwa mwaka mzima kupitia vijana wa BBT na sekta nyingine zinazohusu kilimo,lakini pia na wanawake ambao wamewezeshwa kwenye kilimo.
Amesema uzinduzi wa ripoti hiyo utaenda sambamba na maandalizi ya uzinduzi wa benki ya ushirika.ambayo utazinduliwa rasmi Aprili 28 kwa ajili ya kuanza kuwanufaisha wakulima na wafanya biashara katika maeneo mbakimbali hapa nchini.
"Tumepanga kutoa ripoti kila mwaka ya mradi wa BBT,tunaizindua rasmi Aprili 27,mkakati huo utaendelea kila mwaka ili kuijulisha jamii nini serikali inafanya kitu gani katika mradi wa BBT,"alisema Bashe.
Amesema ripoti ambayo itazinduliwa na kuanza kutolewa kila mwaka,itawasaidia jamii kujua nini kinaendelea katika mradi wa BBT ambao unahusisha vijana na wanawake kwa ajili ta kujiinua kiuchumi kupitia kilimo wanachofanya.
Aidha amesema pia mradi huo una manufaa makubwa sana kwa wananchi hususani vijana na wanawake,wengi wao sasa hivi wananufaika na kilimo cha umwagiliaji na wengine cha matunda pamoja na mazao ya chakula.
Bashe pia aliwapongeza wadau wa sekta ya kilimo wanaotekeleza miradi ya kuwezesha vijana na wanawake katika sekta ya kilimo kutokana na kuunga mkono juhudi za serikali kwenye sekta ya kilimo hapa nchini.
Amesema serikali itaendelea kushirikiana na sekta binafsi katika ukuzaji wa kilimo hususani kwenye kilimo cha umwagiliaji ambapo wanaendelea kuboresha miundombinu ya umwagiliaji katika skimu za umwagiliaji ili kuhakikisha wakulima wanapiga hatua.
Naye msajili wa vyama vya Ushirika Nyagilo alisema makubaliano waliosaini kwa ajili ya kuendelea kusaidia vijana kwenye sekta ya kilimo yatasaidia kuzidi kupanua wigo wa kilimo kwa upande wa rika hilo.
Nyagilo amesema ushirika huo wa pamoja ni moja ya mkakati wa kuwainua vijana na wanawake kujikita kwenye kilimo ili kuhakikisha wanajiinua kiuchumi wao na familia zao lakini pia watachangia pato la taifa.





MIAKA minne ya serikali ya awamu ya sita madarakani Mfuko wa Maendeleo ya Jamii(TASAF),kupitia Mpango wa kunusuru kaya maskini umefanikiwa kuhitimisha kaya za walengwa takribani 400,000 nchi nzima baada ya kuhudumiwa kwa takribani miaka 10.
Hilo limefanikiwa kutokana na utekelezaji wa afua mbalimbali ambapo zimeboresha maisha,kuongeza rasilimali na zinaweza kuendelea kuendesha maisha yao bila ya ruzuku ya TASAF.
Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora George Simbachawene amesema hayo April 17,2025,Jijini Dodoma wakati akieleza mafanikio ya serikali ya awamu ya sita kwa waandishi wa habari.
Amesema kupitia mpango wa miradi ya kutoa ajira za muda kwa walengwa hadi kufikia Disemba 2024,jumla ya miradi 27,863 ya kutoa ajira za muda kwa walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini imetekelezwa ambapo jumla ya Kaya za Walengwa 662,000 zimelipwa jumla ya shilingi bilioni 213.8.
"Licha ya kuongeza kipato, walengwa pia wameweza kupata ujuzi wa utekelezaji wa miradi hiyo unaoweza kutumika katika shughuli za kukuza uchumi wa kaya na kuongeza kipato,miradi hii imenufaisha sekta za kilimo, barabara, misitu, maji na mazingira,"amesema.
Pia kupitia miradi ya kuendeleza na kuboresha Miundombinu ya Huduma za Jamii jumla ya miradi 137 ya uendelezaji miundombinu yenye thamani ya shilingi bilioni 12.67 ilitekelezwa katika Mamlaka za maeneo ya utekelezaji 29.
Kati ya hiyo miradi hiyo 6 imekamilika na 72 ilikuwa katika hatua mbalimbali za utekelezaji. ambapo miradi ya aina hiyo imetatua changamoto za jamii zinazotokana na upungufu au kutokuwepo kabisa kwa miundombinu ya kutosha ya kutolea huduma za jamii katika sekta za Elimu, Afya na Maji.
"Hadi kufikia Desemba, 2024, jumla ya miradi ya jamii 1,518 yenye thamani ya shilingi bilioni 81.8 imetekelezwa ambapo miradi 659 imekamilika na inatumika kutoa huduma na miradi 859 ipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji kupitia miradi ya Kupunguza Umaskini Tanzania-Awamu ya Nne(TPRP IV),"amesema Waziri Simbachawene.
Aidha, amesema TASAF kwa kushirikiana na Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu(HESLB) imewezesha waombaji wa mikopo ya elimu ya juu kutoka kaya za walengwa kutambulika, kupatiwa mikopo ya elimu kwa asilimia 100 ambapo hadi kufikia Novemba 2024 jumla ya wanafunzi 8,274 wamenufaika na mikopo hii.





Maoni ya Kidhahania Pekee kutoka kwa Wanachama wa Zamani Yalitumiwa Kuhukumu Kanisa Zima… “Mistari Miwili Pekee Iliyotolewa kwa Majibu ya Dhati ya Kanisa” “Uandishi wa Habari wa Haki uhitajika ili Kulinda Uhuru wa Kidini na Kuwalinda Waamini”
Mnamo Aprili 9, Kanisa la Shincheonji la Yesu nchini Ufaransa lilitoa tamko rasmi likilisema gazeti la kila siku la Ufaransa Le Parisien kwa makala yake iliyochapishwa Aprili 7, likidai kuwa ripoti hiyo ililihusisha kanisa kwa njia iliyopotoshwa na kusema kwamba “heshima ya kanisa na waumini wake imeharibiwa vibaya.”
Kanisa hilo lilieleza kuwa makala hiyo ilisisitiza mno madai ya upande mmoja kutoka kwa wanachama wa zamani huku ikipuuza kwa kiasi kikubwa hali halisi ya jumuiya ya imani, hivyo kuwasilisha mtazamo wa upendeleo. Pia walieleza kuwa licha ya kutoa majibu ya dhati wakati wa mahojiano, msimamo wao uliwakilishwa kwa mistari miwili pekee kwenye makala hiyo.
Tamko hilo lilihimiza haja ya kuanzisha maadili ya haki ya uandishi wa habari na viwango sahihi vya kuripoti ili kulinda uhuru wa kidini na haki za waumini.
Makala hiyo yenye utata, iliyopewa kichwa “Walitutendea Kama Wanyama,” ililitaja Kanisa la Shincheonji la Yesu kama mojawapo ya “makundi ya kiinjili yenye matatizo” nchini Ufaransa, kwa mujibu wa ushuhuda wa mtu aliyekuwa mwanachama wa zamani. Makala hiyo ilijumuisha madai kuhusu kambi za mafunzo, kutengwa na mahusiano ya kibinafsi, na madai ya fedha. Hata hivyo, kanisa lilibainisha kuwa msimamo wao uliwasilishwa kwa sentensi mbili tu.

Msemaji wa kanisa alisema, “Tulituma majibu ya kina ya maandishi kwa dhati , yenye maelfu ya herufi, tukijibu maswali 12 ambayo mwandishi wa habari alitutumia kabla. Hata hivyo, sentensi mbili pekee kutoka kwa majibu yetu ndizo zilizojumuishwa kwenye makala hiyo.” Msemaji huyo alikosoa hali hiyo akisema, “Hiyo ni chini ya 1% ya majibu yetu yote, na hivyo kuzuia uwezo wa wasomaji kupata mtazamo ulio sawa.”
Aliongeza kusema, “Ikizingatiwa kuwa makala ilichapishwa saa nne tu baada ya kutuma majibu yetu, inaonekana kuwa ripoti hiyo ilikuwa imeandikwa tayari kwa mtazamo uliokusudiwa tangu awali.”
Waliongeza, “Iwapo majibu ya maandishi hayakutosha, mwandishi angeweza kutembelea kanisa yeye mwenyewe ili kujionea hali halisi ya jumuiya ya imani na kusikiliza moja kwa moja kutoka kwa waumini wa sasa. Kanisa letu lipo wazi kila wakati na tayari kwa mawasiliano ya wazi na vyombo vya habari.”
Ili kuonyesha hali halisi ya waumini wake, kanisa pia lilitoa ushuhuda kutoka kwa waumini waliopo. Teresa (29), ambaye amehudhuria kanisa hilo mjini Paris kwa miaka sita, alisema, “Imani ni jambo la hiari. Kupitia kanisa hili, nimeweza kumwelewa Mungu kwa kina na kujifunza jinsi ya kuwa nuru duniani kama mtu wa Mungu.”
Mwanachama mwingine, Axel (30), alisema, “Kabla ya kuja Kanisa la Shincheonji, nilikuwa natafuta maana ya maisha yangu. Kupitia imani yangu hapa, nimeelewa kile ambacho Mungu anataka kweli, na kufanya kazi ya Mungu hunipa furaha kubwa. Hata nikiwa katika kazi ya utume, nimeweza kusafiri, jambo ninalolipenda, na nilikutana na mke wangu kanisani. Naishi maisha yenye utimilifu wa kweli.”
Kuhusu kichwa cha makala hiyo, “Walitutendea Kama Wanyama,” kanisa lilijibu, “Kauli hiyo iliwashtua na kuwatatiza sana waumini wetu. Hakuna mtu aliyewahi kutendewa hivyo, wala hakuna anayehisi hivyo. Kichwa hicho kilitumiwa kwa makusudi ili kuchochea hamasa kwa umma.”
Kanisa liliongeza, “Kwa hakika, haturuhusu vitisho au unyanyapaa wowote dhidi ya wanaoamua kuondoka kanisani. Kuna utamaduni wa kuheshimu chaguo binafsi, hata baada ya mtu kuamua kuondoka.”
Kuhusu dai kuwa mwanamke ‘aliachana na mchumba wake kwa ombi la kanisa,’ kanisa lilikana vikali hilo, likisema, “Hili si kweli. Mwanaume husika pia alikuwa muumini wa kanisa kwa wakati huo na alionekana kuwa na nia ya ndoa.
Baada ya kutembelea vituo hivyo katika ofisi za Chama Kikuu cha Ushirika Mirambo na ofisi za Chama Kikuu cha Ushirika wa Wakulima wa Tumbaku Kanda ya Magharibi (WETCU), Bw. Laurent amesema kuwa, zoezi hilo limefikia hatua nzuri itakayowezesha kuanza kwa taratibu za malipo kwa wakulima wa Tumbaku nchini.
Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Bw. Laurent ameeleza kuwa, lengo la uhakiki ni kuhakikisha wakulima wote waliozalisha Tumbaku katika msimu wa mwaka 2023/2024 wanalipwa na fedha hizo zinamfikia mkulima anayestahili moja kwa moja kupitia akaunti yake.
Ameeleza kuwa, zoezi hili linafanyika kwa ushirikiano kati ya Wizara ya Kilimo, TFRA, TCDC na vyama vikuu vya ushirika vilivyo chini ya shirikisho la TCJE.
Akizungumza na Mkurugenzi Laurent, Ndg. Innocent Nsena Katibu Tawala wa Wilaya ya Urambo alieleza kuwa, suala la ruzuku limekuwa kilio cha muda mrefu kutoka kwa wakulima na kwamba utekelezaji wa mpango huu utapunguza gharama za uzalishaji kwa mkulima.
“Ninamshukuru Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuridhia ombi la kutoa ruzuku kwa wakulima wa tumbaku, kwa kuwa zao hili awali halikuwa miongoni mwa mazao yanayopata ruzuku” alisema Ndg. Nsena.
Kwa upande mwingine, akitoa taarifa ya utekelezaji wa zoezi la uhakiki katika ofisi za Chama Kikuu cha Ushirika WETCU, kiongozi wa timu hiyo, Ndg. Byaga Nzohumpa, alieleza kuwa, zoezi hilo limekamilika kwa asilimia 100 baada ya kuhakiki taarifa za vyama vya msingi 248 walivyokabidhiwa.
Naye Ndg. Godwin Mwalongo, kiongozi wa timu ya uhakiki katika ofisi za Chama Kikuu cha Ushirika Mirambo, amesema kuwa, kazi ya uhakiki imefikia hatua nzuri na inatarajiwa kukamilika kwa wakati.
Kwa upande wake, Kaimu Meneja wa TCJE, Ndg. Seleman Abasi Maona, alieleza kuwa, miongoni mwa changamoto kubwa zilizokabili zoezi hilo ni uandaaji hafifu wa takwimu za wakulima wa tumbaku kwa msimu wa kilimo wa 2023/2024, hasa kutokana na taarifa zisizo sahihi kutoka kwa wakulima.
Alisisitiza kuwa kama kungekuwepo mfumo madhubuti wa ukusanyaji taarifa kuanzia ngazi ya chini, changamoto hizo zingeweza kuepukwa na kuahidi kuboresha kwa ajili ya manufaa ya baadaye kwa wakulima





