

Akizungumza na waandishi wahabari leo Mei20,2025 katika mafunzo yaliyotolewa jijini Dar es salaam, Kaimu Msajili Bodi ya maziwa Tanzania Deorinidei Mng’ong’o amesema maziwa yaliyosindikwa ni salama kwa matumizi ya binadamu, yanadumu kwa muda mrefu na yana viwango bora vya usafi na virutubisho, hivyo kuwa chaguo bora kwa jamii zote, mijini na vijijini.
“Tunapoelekea kilele cha Wiki ya Maziwa, tunawakumbusha wananchi kuwa kuchagua maziwa yaliyosindikwa si tu ni njia ya kulinda afya zao, bali pia ni kuunga mkono juhudi za wakulima na viwanda vya maziwa nchini,” alisema Kaimu Msajili wa Bodi hiyo.
Maadhimisho ya Wiki ya Maziwa huadhimishwa kila mwaka kwa lengo la kuelimisha umma kuhusu umuhimu wa maziwa katika lishe, kuhamasisha matumizi yake, na kutoa fursa kwa wadau wa sekta hiyo kuonesha mafanikio na changamoto zinazowakabili.
Maadhimisho ya mwaka huu yanatarajiwa kufanyika mkoani Morogoro kuanzia mei 27 hadi juni mosi mwaka huu.
Bodi ya Maziwa imeandaa shughuli mbalimbali zitakazofanyika kuelekea na wakati wa kilele cha wiki hiyo, zikiwemo maonesho ya bidhaa za maziwa, midahalo ya kitaaluma, na kampeni za uelimishaji mashuleni na katika jamii kwa ujumla.






Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Namibia Mhe. Netumbo Nandi-Ndaitwah mara baada ya kuwasili Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 20 Mei, 2025.
Zoezi hilo ni katika kuelekea Maadhimisho ya Miaka 50 ya TET yanayotarajia kufanyika Juni mwaka huu, limefanyika katika Makao Makuu ya TET, jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa TET, Dkt. Aneth Komba ameishukuru Agha Khan Foundation kwa hatua hiyo kwani wanatekeleza kwa vitendo utunzaji wa mazingira na kulinda mabadiliko ya tabianchi.
"TET katika kusheherekea Miaka 50 inaendeleza utunzaji wa mazingira kwa vitendo kwani hata katika maboresho ya mitaala ya kielimu tumezingatia utunzaji mazingira.
"Maboresho ya mitaala ya mwaka 2023 yameweka somo la jiografia kuwa ni somo la lazima na katika somo hilo tumewezesha wanafunzi kuhimili na kutunza mazingira," amesema.
Kwa upande wake Mkuu wa Programu wa Agha Khan Foundation Tanzania, Bi. Carolyn Mlewa amesema wamepanda miti hiyo zaidi ya 200 yenye aina 25 tofauti ikiwemo ya kivuli, matunda, dawa, na miti pori kama ishara ya kulinda mazingira.
"Hii ni katika kuendeleza ushirikiano wetu na TET katika uhimilivu wa tabianchi, ni mabadiliko ya tabia na namna ya kulinda hali hiyo, hivyo kupanda miti hiyo ambayo itakuwa na umuhimu mkubwa katika kulinda mazingira," amesema Bi. Mlewa.
Naye Msimamizi wa Mradi wa Mazingira wa taasisi hiyo, Japhet Wangwe amesema amesema upandaji msitu huo mdogo ni moja ya hatua ya kuboresha mazingira lakini pia kuhifadhi viumbe vya asili na vya Kiikolojia.
GEITA MJINI: KATIBU wa Halmashauri Kuu (NEC), Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Amos Makalla amesema serikali imeazimia kuwainua wachimbaji wadogo wa madini lengo ni kuhakikisha uchumi wa wachimbaji wote unakuwa kwa pamoja.
Makalla ameeleza hayo leo Mei 20 wakati akizungimza na wananchi wa Geita Mjini mkoani Geita, ikiwa ni muendelezo wa ziara yake ya siku saba katika mikoa mitano ya Kanda ya Ziwa ambayo ni Kagera, Geita, Mwanza Simiyu na Shinyanga.
Akifafanua hilo Makalla amesema azma ya serikali ikiongozwa na Rais Samia ni kuwajali wachimbaji wadogo wa madini na ndo maana rais wao na wachimbaji wameendekea kumuunga mkono na jitihada zake kwa sababu ameingia kwenye rekodi ya kuwajali wachimbaji wadogo.
Ameeleza hilo akisisitiza kuwa wachimbaji wakubwa waliopo alianza kama wachimbaji wadogo, hivyo wachimbaji hao wakipewa fursa wataweza kukua na kuajiri watu na kuongeza mapato na azma ya serikali ya CCM ni kuwajali wachimbaji wote kuhakikisha uchumi unakuwa kwa pamoja.
Makalla amewasisitiza wananchi kuwapuuza watu wanaowahadaa wananchi kwa kusema kuwa wachimbaji wadogo wamesahaulika, kwani kuwepo na madini katika eneo hilo kunaonyesha kuna mtu muadilifu anayesimamia rasilimali hizo.
Wakala wa Vipimo Tanzania wamepokea na kusimika mtambo mpya wa kisasa wenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 400, kwa ajili ya kuhakikisha dira za maji. Mtambo huo una uwezo wa kupima hadi dira 1,000 kwa siku, hatua inayolenga kuongeza ufanisi na usahihi katika uhakiki wa mita za maji nchini.
Kupitia maadhimisho ya Siku ya Vipimo Duniani, Wakala wa
Vipimo wameendesha zoezi la kutoa elimu kwa wananchi pamoja na madereva wa
malori katika kituo chao kilichopo Misugusugu, Kibaha mkoani Pwani. Elimu hiyo
ililenga kuwaeleza wananchi umuhimu wa uhakiki wa dira za maji pamoja na faida
zake katika matumizi ya kila siku ya maji majumbani na kwenye taasisi
mbalimbali.
Akizungumza katika zoezi hilo, Mkurugenzi wa Huduma Saidizi
wa Wakala wa Vipimo, Bw. Karim Mkorehe, alitoa shukrani kwa Mheshimiwa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuwapatia mtambo
huo mpya wenye uwezo mkubwa wa kuhakiki dira za maji.
Kwa upande wake, Kaimu Meneja wa Wakala wa Vipimo katika
Kituo cha Misugusugu, Bw. Gaudence Gaspary, alisema kuwa elimu hiyo imetolewa
kwa makundi mbalimbali ya wananchi, wakiwemo madereva wanaopata huduma katika
kituo hicho. Alifafanua kuwa dira ya maji inapaswa kuhakikiwa angalau mara moja
kwa mwaka ili kuhakikisha usahihi wa gharama za matumizi ya maji.
Aidha, baadhi ya wananchi waliopatiwa elimu hiyo walieleza kufurahishwa na mafunzo hayo huku wakikiri kuwa wengi wao hawakuwa na uelewa juu ya uwepo wa huduma za uhakiki wa mita za maji.

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, akiwa kwenye kituo cha uandikishaji wapiga kura kilichopo katika Ofisi ya Mtendaji wa Kata ya Kilimani, Mtaa wa Kilimani, jijini Dodoma, kwa ajili ya kuboresha taarifa zake kwenye Daftari la Kudumu la Mpiga Kura, leo tarehe 20 Mei, 2025.




