Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Jerry Slaa (kulia mbele) akizungumza kuwakaribisha Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, mara baada ya kuwasili katika Kituo cha Kutunza Data Kimtandao (Data Centre) katika ziara yao kutembelea kituo hicho.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania – TTCL, CPA Moremi Marwa (aliyesimama kulia) akizungumza kutoa taarifa fupi ya utendaji kwa Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, mara baada ya kuwasili katika Kituo hicho cha Kutunza Data Kimtandao (Data Centre) katika ziara yao.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania – TTCL, CPA Moremi Marwa (kulia aliyesimama) akizungumza kutoa taarifa fupi ya utendaji kwa Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, mara baada ya kuwasili katika Kituo hicho cha Kutunza Data Kimtandao (Data Centre) katika ziara yao.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, Mhe. Selemani Moshi Kakoso (Mb) akizungumza mara baada ya kamati yake kutembelea Kituo cha Kutunza Data Kimtandao (Data Centre) kilichopo jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, Mhe. Selemani Moshi Kakoso (Mb) akizungumza mara baada ya kamati yake kutembelea Kituo cha Kutunza Data Kimtandao (Data Centre) kilichopo jijini Dar es Salaam.

Picha ya pamoja na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, mara baada ya kamati kutembelea Kituo cha Kutunza Data Kimtandao (Data Centre) kilichopo jijini Dar es Salaam.

KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imefanya ziara katika Kituo cha Kutunza Data Kimtandao (Data Centre) kinachoendeshwa na Shirika la Mawasiliano Tanzania, (TTCL Corporation) na kuridhishwa na uwekezaji wa kisasa uliofanyika katika kituo hicho ambacho ni mhimili wa huduma za kidigitali nchini.

Akizungumza mara baada ya ziara kituoni hapo, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, Mhe. Selemani Moshi Kakoso (Mb) ameziomba Taasisi, Mashirika ya Umma na binafsi na Wizara mbalimbali kutumia Kituo cha Kutunza Data Kimtandao (Data Centre) ili kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuboresha huduma za kidijitali nchini.

Pamoja na hayo, Mwenyekiti huyo wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, ameishauri TTCL kufanya maboresho zaidi katika kitengo cha utafutaji masoko ili kuvutia ushawishi wa Mashirika ya Umma na hasa yale ya kibinafsi, Wizara mbalimbali na wateja wengine kujitokeza na kutumia Kituo hicho cha Data Centre.

Tumeona upo umuhimu mkubwa wa kuwepo kwa kituo hiki, lakini kunaitajika ushawishi wa masoko hasa wa sekta binafsi kujitokeza kwa wingi katika kutumia fursa hii ya huduma za Data Center. "...Mkurugenzi fanyeni jitihada za uwekezaji, ili muwe na kitengo kizuri cha masoko kiweze kujiuza hasa kwa sekta binafsi, muwe na ushawishi wa kutumia kitengo hiki cha masoko kwa ajili kuvuta wateja," alisema Mhe. Kakoso (Mb) akizungumza na wanahabari.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania – TTCL, CPA Moremi Marwa alisema kituo hicho kina umuhimu mkubwa kwa wateja wanaokitumia kwa sasa kwani licha ya uhifadhi taarifa lakini kinazipunguzia gharama za uendeshaji kwa taasisi na makampuni, hasa ya Kifedha, Bima na Mawasiliano.

Alisema alisema taasisi au makampuni yanayotumia kituo hicho yanakuwa na usalama mkubwa wa kuhifadhi taarifa zao, na pia hayana haja ya kuwa na vitengo vikubwa vya IT na vifaa vyake kwani shughuli kubwa hufanywa na wataalam wa kituo cha Data Center.

Alisema vaida zingine ambazo hupata mteja wa Data Centre ni pamoja na usalama wa taarifa na ulinzi kwani kituo kinatumia mifumo ya kisasa ya uhifadhi pamoja na kuwa na vyanzo vya uhakika wa umeme zaidi ya vitatu ambavyo uhakikisha taarifa zipo salama muda wote.

Mkurugenzi Marwa alisema kwa sasa Kituo cha Kutunza Data Kimtandao (Data Centre) kinahudumia jumla ya taasisi 211 za Serikali zikiwa taasisi 123 huku za binafsi zikiwa 85, huku akiziomba taasisi, makampuni na watu binafsi kujitokeza kwa ajili ya kupata huduma katika kituo hicho.


Na Said Mwishehe,Ileje

VIJANA wenye sifa jitokezeni kugombea nafasi za ubunge na udiwani katika uchaguzi Mkuu mwaka huu unaotarajia kufanyika Oktoba mwaka huu.

Hayo yamesemwa na Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Tanzania Bara Stephen Wasira alipokuwa akizungumza na wanachama wa Chama hicho Wilaya ya Ileje mkoani Songwe.

Wasira amesema kwa vijana ambao wanajiona wana uwezo na sifa za kugombea udiwani au ubunge wajipange katika uchaguzi Mkuu ujao kwani hakuna mwenye haki miliki ya kushikilia nafasi hizo kwa miaka mitano, isipokuwa leseni zinapatikana kupitia kinyang'anyiro cha kushawishi wananchi na mwenye nguvu ya kushawishi wanapata ridhaa.

Makamu Mwenyekiti Wasira alitoa Maelezo hayo alipokuwa akiunga hoja iliyotolewa na Mwenyekiti wa Chama hicho mkoa wa Songwe Radiweli Mwapashi akiyetaka kuona vijana wapewe nafasi katika uchaguzi huo.

Wasira amesema ili kada apate nafasi ndani ya chama hicho lazima apambane na kukubalika kwa wananchi na kuongeza hata wabunge na madiwani waliopo hawakugombea peke yao.

Amesema katika uchaguzi Mkuu mwaka huu hakuna mtu kupita bila kupingwa kwahiyo hata watakao gombea lazima walijue hilo maana wamekubaliana kijana kama anataka kugombea muda ukifika ajitokeze na kama anataka kuwa msindikizaji shauri yake.

Wasira amesema katika kuelekea uchaguzi huo kwa nafasi ya udiwani na ubunge vitakuwa wazi isipokuwa nafasi ya urais pekee ambayo tayari Mkutano Mkuu Maalum uliofanyika Dodoma umeshapitisha jina la Rais Dk.Samia Suluhu Hassan kuwa mgombea Urais.

Amesisitiza mkutano mkuu maalum ulikubali nafasi ya Urais kugombewa na Rais Samia Suluhu Hassan kutokana na kazi nzuri aliyofanya ndani ya kipindi chake cha miaka minne ya uongozi wake.

“Tanzania inavijana wengi na kazi ya CCM ni kujenga viongozi bora kazi waliyoifanya tangu kupata uhuru hivyo wajitokeze wakanolewe ili wawe tayari kuwatumikia wananchi.”

Awali Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Songwe Radiweli Mwapashi amesema vijana wengi hasa katika mkoa huo wanaingiwa na uoga kukabiliana na madiwani na wabunge watakaotetea nafasi hizo katika uchaguzi ujao.

Hata hivyo amesema kuhamasisha vijana wachukue fomu isitafsiriwe kuwa anawabagua au kuwatenga waliopo madarakani, bali anatamani kuona wanatengeneza viongozi vijana ili Chama hicho kiendelee kupika viongozi kizazi hadi kizazi.







 


Na. Peter Haule, Nyanduga Mara, WF
 
Baadhi ya Wazee wa Kijiji cha Nyasoko na Nyanduga Kata ya Koryo, Wilayani Rorya Mkoani Mara m, wameeleza shauku yao ya kuona elimu ya fedha inawafikia zaidi vijana  ambao wanatafuta fedha kwa bidii lakini hawaendelei kiuchumi kutokana na kukosa elimu ya fedha.
 
Hayo yameelezwa na Wazee wa Vijiji hivyo akiwemo Mzee Cleophas Otieno Obelo, Ray Abich na Mchungaji Thomas Msoke, wakati Timu ya Wataalamu wa elimu ya Fedha kutoka Wizara ya Fedha, ikiongozwa na Bw. Salim Khalfan Kimaro ilipofika katika kata hiyo, kutoa elimu ya fedha.
 
Walisema kuwa vijana hawana elimu ya fedha na wanapoteza mali nyingi wanazotafuta kwa jasho kwa kukosa maarifa na kushauri elimu inayotolewa sasa ifike vijiji vyote ili vijana waweze kujinasua kwenye changamoto ya maisha.
 
Wazee hao waliipongeza Serikali kwa kutoa elimu ya fedha kwa kuwa wamepata maarifa ambayo hawakuyatarajia, hivyo wangependa vijana wengi washiriki katika mafunzo hayo kwa kuwa wana nafasi ya kufanya mambo makubwa kwa maisha yao ya baadae.
 
Akizungumza kuhusu elimu aliyoipata, Mzee Cleophas Otieno Obelo, alisema kuwa licha ya umri wake kuwa mkubwa anakwenda kuweka mambo sawa na ana uhakika wa kuongeza kipato kwa kuwa yeye ni mjasiriamali wa muda mrefu kuanzia mwaka 1981 lakini mikopo isiyofaa na ukosefu wa elimu ya namna bora ya kuwekeza vilikuwa changamoto katika shughuli zake.
 
“Elimu imetupatia mwanga mkubwa, kwa muda uliobaki tunaweza kuwekeza kwa maisha ya uzeeni wakati huu ambao nguvu zinaelekea kuisha na kushindwa kushiriki katika kutafuta kipato ukilinganisha na vijana”, alisema Mzee Obelo.
 
Alisema kabla ya elimu hiyo wamekuwa wakishuhudia watu wengi wakidhurumiwa hususani wanaokopa katika taasisi zisizosajiliwa rasmi, hivyo elimu hiyo imetoa mwelekeo wa eneo zuri la kukopa ili kuepukana na mikopo isiyo na faida.
 
Aidha, aliwashauri wananchi wanaokopa katika maeneo yasiyo rasmi kuacha kukopa katika maeneo hayo kwa kuwa madhara yake ni makubwa.
 
Kw upande wa wakina mama wa eneo hilo akiwemo Bi. Judithi Zephania na Matha Joseph, walisema kuwa, wao ndio waathirika wakubwa wa mikopo umiza kutokana na kutozwa riba kubwa, jambo linalosababisha kushindwa kuirejesha na kuwa chanzo cha migogoro ya familia, ila kwa sasa wanaweza kuwatumia maafisa maendeleo kupata mwongozo wa namna bora ya kukopa kwa kuwa wamepata elimu.
 
Kwa upande wake Kiongozi wa Timu ya Wataalamu wa Elimu ya Fedha kutoka Wizara ya Fedha, Bw. Salim Khalfan Kimaro, alisema kuwa miongoni mwa chanzo kikubwa cha mikopo yenye riba kubwa ni tabia ya watu kutojiwekea akiba, hivyo wanapopata uhitaji wa ghafla wanajikuta wanakopa bila kuwa na uelewa na kusababisha changamoto.
 
Alisema kuwa elimu itaendelea kutolewa kwa kuwa ni program endelevu, lengo ni kuhakikisha wananchi wanapata elimu na kumudu vema shughuli zao za kujipatia kipato.
 
Zoezi la kutoa elimu ya fedha linaendelea kwa rika zote katia vijiji na Kata za Wilaya zilizopo Mkoani Mara ikiwa ni pamoja na Wilaya za Rorya, Musoma, Bunda, Butiama
Afisa Masoko Mwandamizi wa Kampuni ya Uwekezaji wa UTT AMIS, Bw. Rahim Mwanga, akieleza maeneo ya uwekezaji ikiwa ni pamoja na Hati Fungani za Serikali na Hisa, kwa wakazi wa Nyanduga Mkoani Mara, ikiwa ni sehemu ya utoaji wa elimu ya fedha, Mkoani Mara.
 
Mzee Ray Abich na Cleophas Otieno Obelo (kulia), wakipata elimu ya fedha, Mkoani Mara, zoezi linalofanywa na Timu ya Wataalamul kutoka Wizara ya Fedha, Mkoani Mara
Wakazi wa Nyanduga na Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Nyanduga, wakipata elimu ya fedha katika zoezi la kutoa elimu ya fedha mkoani Mara linalofanywa na Timu ya Wataalamu wa Elimu hiyo kutoka Wizara ya Fedha, Mkoani Mara
Wanafunzi wa Kidato cha Tano wa Shule ya Sekondari Nyaduga, Adam Muda na Livingston Samwel, wakisoma kipeperushi kuhusiana na elimu ya Fedha, katika zoezi la kutoa elimu ya fedha mkoani Mara linalofanywa na Timu ya Wataalamu wa Elimu hiyo kutoka Wizara ya Fedha, Nyanduga Mkoani Mara.
 
Meneja wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa NSSF Wilaya ya Tarime na Rorya, Bw. Felix Uiso, akiwaeleza wakazi wa Nyanduga Mkoani Mara kuhusu umuhimu wa kujiunga katika Mfuko huo kwa maisha ya baadae, wakati zoezi la kutoa elimu ya fedha mkoani Mara linalofanywa na Timu ya Wataalamu wa Elimu hiyo kutoka Wizara ya Fedha, Nyanduga Mkoani Mara.
Kiongozi wa Timu ya Wataalamu wa Elimu ya Fedha kutoka Wizara ya Fedha, Bw. Salim Khalfan Kimaro (kushoto) akiagana na Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Katuru Wilayani Rorya Mkoani Mara baada ya zoezi la kutoa elimu ya fedha kwa wanafunzi wa Shule hiyo, zoezi linalofanywa na Wataalamu wa Elimu ya Fedha kutoka Wizara ya Fedha.
 
Mchumi wa Idara ya Uendelezaji wa Sekta ya Fedha, Bw. Renatus Lukas, akitoa elimu ya fedha kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari Katuru Wilayani Rorya Mkoani Mara wakati wa zoezi la kutoa elimu ya fedha mkoani Mara, linalofanywa na Wataalamu wa Elimu ya Fedha kutoka Wizara ya Fedha.Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Katuru Wilayani Rorya Mkoani Mara, wakipata elimu ya fedha katika zoezi la kutoa elimu ya fedha Mkoani Mara, linalofanywa na Wataalamu wa Elimu ya Fedha kutoka Wizara ya Fedha.
 

Na Mwandishi, Michuzi Tv

BANK OF AFRICA Tanzania imeeleza dhamira yake ya kuendelea kuwekeza katika huduma bora kwa wateja wake ili kuchochea maendeleo ya kifedha na ukuaji wa uchumi nchini.

Akizungumza kwenye hafla ya futari iliyoandaliwa na benki hiyo jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki, Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Wasia Issa Mushi, alisema benki hiyo inapanua huduma zake kwa kuleta bidhaa mpya kama kadi za VISA na kadi za mkopo (credit cards).

"Tunataka kuwarahisishia wateja wetu upatikanaji wa huduma za kifedha kwa kuimarisha huduma zetu na kuja na bidhaa zinazokidhi mahitaji yao," alisema Mushi.

Aliongeza kuwa benki hiyo inatilia mkazo uhusiano wa karibu na wateja wake wa viwango vyote—wakubwa, wa kati, na wadogo—ili kuhakikisha ustawi wa sekta ya kifedha na uchumi kwa ujumla.

Kwa sasa, BANK OF AFRICA Tanzania ina zaidi ya mawakala 200 nchini na inalenga kuongeza idadi hiyo hadi kufikia mawakala 500 mwishoni mwa mwaka huu. "Tunapanua mtandao wa huduma zetu ili kuhakikisha wateja wanapata huduma kwa urahisi zaidi, hususan wafanyabiashara," aliongeza Mushi.

Mgeni rasmi wa hafla hiyo, Katibu wa Baraza la Ulamaa nchini, Shekhe Hassan Chizenge, aliipongeza benki hiyo kwa hatua yake ya kuandaa futari ya pamoja na wateja wake, akisema ni njia nzuri ya kuimarisha mahusiano.

"Ni jambo la heri kuona taasisi ya kifedha kama BANK OF AFRICA ikiweka mkazo katika kujenga mahusiano ya karibu na wateja wake kupitia hafla kama hii," alisema Shekhe Chizenge.

Naye Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Biashara wa benki hiyo, Hamza Cherkaoui, alisema benki hiyo itaendelea kuwekeza katika mifumo ya kidigitali na uvumbuzi wa kiteknolojia ili kuimarisha huduma zake.

BANK OF AFRICA Tanzania ilianza shughuli zake nchini mwaka 2007 baada ya kununua Benki ya Eurafrican, ambayo ilianzishwa Tanzania mwaka 1995. Benki hii ni sehemu ya BANK OF AFRICA GROUP, mtandao wa benki unaofanya kazi katika nchi 18 barani Afrika na pia kuwa na uwakilishi katika nchi kama Ufaransa, Hispania, Uingereza, na China.

Tangu mwaka 2010, benki hiyo imekuwa sehemu ya BMCE Bank ya Morocco, ambayo ni moja ya benki kubwa zaidi barani Afrika, ikiwa na matawi katika zaidi ya nchi 31.

Kwa sasa, BANK OF AFRICA Tanzania ina mtandao wa matawi 18, yakiwemo 9 Dar es Salaam na mengine mikoani kama Arusha, Mwanza, na Zanzibar, ikiwa na lengo la kufikisha huduma bora kwa wateja wake kote nchini.

Katibu wa Baraza la Ulamaa wa Bakwata , Sheikh Hassan Chizenga akizungumza wakati wa futari iliyoandaliwa na Bank of Africa kwa ajili ya wateja wa benki hiyo iliyofanyika mwishoni mwa wiki hii jijini Dar es Salaam
Naibu Mkurugenzi Mtendaji (Biashara) wa Bank of Africa, Hamza Cherkaoui akitoa neno la shukrani kwa wageni waalikwa na wateja kwenye futari iliyoandaliwa benki hiyo hivi
Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Bank of Africa, Wasia Issa Mush akizungumza na wateja wa benki hiyo katika futari iliyoandaliwa na benki kwa ajili ya wateja  hivi karibuni jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wateja wakishiriki futari iliyoandaliwa na Benki hiyo kwa wateja wake mwishoni.

 Serikali ya Tanzania, kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA), imewekeza katika ujenzi wa Bandari Kavu ya Kwala, mradi wa kimkakati unaolenga kuongeza ufanisi wa Bandari ya Dar es Salaam na kuifanya kuwa kitovu bora cha biashara kwa nchi jirani.


Akizungumza na waandishi wa habari leo, Machi 16, 2025, Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, wakati wa ziara yake ya kikazi katika eneo la Bandari Kavu ya Kwala amesema bandari hiyo iliyopo Vigwaza, Kibaha, mkoani Pwani, ni suluhisho la muda mrefu kwa changamoto ya msongamano wa mizigo bandarini.



Ameeleza kuwa moja ya faida kubwa ya Bandari Kavu ya Kwala ni kupunguza muda wa kushughulikia mizigo katika Bandari ya Dar es Salaam kwa kuhifadhi makontena na shehena kubwa za bidhaa na kuongeza ufanisi wa bandari kuu utaongezeka, hivyo wateja watahudumiwa kwa haraka zaidi. 


“Hii itapunguza gharama za ucheleweshaji wa mizigo na kuimarisha mazingira ya biashara na uwekezaji nchini.”



Msigwa amesema bandari hiyo inatarajiwa kuhudumia makasha 823 kwa siku, yakiwemo yanayokwenda nchi jirani. Hii inamaanisha kuwa kwa mwaka itahudumia hadi makasha 300,395, sawa na asilimia 30 ya makasha yote yanayopitia Bandari ya Dar es Salaam.



Aidha, amesema Serikali imewekeza katika miundombinu muhimu ili kuhakikisha ufanisi wa bandari hiyo, ikiwemo ujenzi wa reli ya mchepuko inayounganisha Kwala na Shirika la Reli Tanzania (TRC), barabara za zege, na mtandao wa umeme wa uhakika.




“Kupitia reli, mizigo kutoka Bandari ya Dar es Salaam itaweza kusafirishwa moja kwa moja hadi Kwala, hatua itakayopunguza idadi ya malori barabarani, msongamano na ajali,” amesema Msigwa.



Mbali na hayo, Msigwa ameeleza kuwa awamu ya kwanza ya ujenzi wa miundombinu ndani ya eneo la mradi imekamilika kwa asilimia 80. 




“Shughuli hizo zinahusisha na Mtandao wa barabara za zege zinazoweza kubeba malori ya mizigo, Jengo la kituo cha kupambana na moto, Jengo la utawala litakalohifadhi ofisi za mashirika ya serikali na watoa huduma za kitaalamu, Mfumo wa maji ya mvua, Mtandao wa umeme na maji safi, Hifadhi za viwanda zenye jumla ya mita za mraba 26,000 na Lango kuu na malazi ya wafanyakazi.”



Kadhalika Msigwa amesema bandari hiyo itakapokamilika, itakuwa na viwanda vikubwa na vya kati 200 pamoja na viwanda vidogo 300 vinavyohusika na Usindikaji wa vyakula, Utengenezaji wa vifaa, Viwanda vya dawa, Vifaa vya ujenzi, Usindikaji wa viatu na nguo, pamoja na Viwanda vya kemikali.



Mbali na faida za kiuchumi, Bandari Kavu ya Kwala inaleta ajira nyingi kwa Watanzania ambapo inatarajiwa kutoa ajira za moja kwa moja 100,000 na ajira zisizo za moja kwa moja 500,000 huku Mradi huo  ukijengwa kwa awamu tano.


Hadi sasa, viwanda vitatu tayari vimeanza uzalishaji, vingine vitatu vipo katika hatua za mwisho za kufunga mitambo, na viwanda vinne vinatarajiwa kuanza ufungaji wa mitambo ifikapo mwisho wa Aprili 2025.



Na Mwandishi Wetu

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimepiga marufuku akina mama wajawazito wanaokwenda kujifungua hospitalini kutozwa fedha kwani huduma ya kujifungua ni bure na maelekezo tayari yalishatolewa.

Akizungumza mbele ya wananchi wa Mlowo katika Wilaya ya Mbozi mkoani Songwe akiwa katika ziara yake ya kikazi Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho Stephen Wasira amesema sera ya CCM inaeleza wazi huduma ya kujifungua pamoja na watoto wenye umri kuanzia mwaka 0-5 hawatatozwa fedha ,hivyo ni marufuku kuwatoza fedha.

Akiwa katika eneo hilo Wasira alipokea kero za wananchi hao wakidai wanawake wajawazito wanapokwenda kujifungua wanatakiwa kulipa fedha Sh.300,000 ili kupata huduma ya kujifungua hali iliyomshangaza na kutoa maelekezo ya kupiga marufuku huduma ya kujifungua kutozwa fedha.

“Sera ya CCM iko wazi kabisa kuwa hairuhusiwi mama mjamzito anapokwenda kujifungua kulipa fedha ili apate huduma,hivyo wale ambao wanapisha sera hii waache mara moja na hii ni kwa maeneo yote ambayo wanaendelea kupindisha utaratibu uliopo kwa kuchukua fedha.

“Watoto ni baraka na wala sio dhambi,kwanini mama anapokwenda kujifungua atoe fedha,nitoe maelekezo kwa wenyeviti wa Chama Wilaya na Mkoa kufuatilia haya yanayosemwa kama ni kweli, tuchukue hatua na nisisitize huduma ya kujifungua ni bure.”

Wasira amesisitiza suala la kina mama kujifungua bila malipo mi sera ya CCM na hiyo haina mjadala wala haina tarehe ya kuanza maana tarehe ya kuanza ilishapita nyuma.

"Kuna mambo mawili, kwanza tunataka kinamama wote wajifungue bila masharti yoyote la pili tunataka watoto wadogo kuanzia mwaka sulfuric hadi miaka mitano wapate huduma bure, kwa hiyo wale ambao wanatoza hela...kujifungua sio adhabu kama ingekuwa adhabu sote tusingezaliwa.

"Kwa sababu jambo hili ni la CCM tunaagiza uongozi wa mkoa wa Songwe na kila mahali kuhakikisha watoto na akinamama wanaokwenda kujifungua wanapewa heshima wannayostahili na hawaliposhwi fedha," amesema.




 



Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI imefanya ziara ya kikazi katika mgodi wa Dhahabu wa Barrick Bulyanhulu na kupongeza jitihada zinazofanywa na mgodi kujali afya za wafanyakazi wake na jamii nzima ya vijiji vinavyozunguka mgodi huo.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Hassan Mtenga akiongea baada ya kuhitimisha ziara hiyo amesema Kamati imeridhishwa kwa jinsi mgodi unavyotekeleza programu za afya za ndani na nje hususani katika kupambana na UKIMWI, Malaria, Kifua Kikuu na magonjwa mengineyo yanayoweza kusababishwa na shughuli za uzalishaji mgodini.


"Katika wasilisho lenu tumeona ni jinsi gani kampuni ya Barrick iko mstari wa mbele kulinda afya za wafanyakazi wake na jamii nzima ya maeneo yanayozunguka mgodi na kwa jinsi inavyofanikisha miradi ya Afya kupitia fedha za Uwajibikaji kwa Jamii (CSR) pia tumefurahi kusikia asilimia kubwa vya wafanyakazi katika migodi ya Barrick hapa nchini ni watanzania",amesema Mtenga.


Kwa niaba ya Kamati, Mtenga ametoa pendekezo kwa Mgodi wa Barrick kuangalia uwezekano wa kuchangia Mfuko wa Taifa wa UKIMWI, pendekezo ambalo uongozi wa Mgodi umesema utalifanyia kazi kwa kushirikiana na Serikali ya Mkoa na Wilaya kupitia Kamati za Maendeleo ya jamii.


Kwa upande wake Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa, amesema uendeshwaji wa migodi ya Barrick ambayo ina ubia na Serikali kupitia kampuni ya Twiga Minerals ni wa weledi mkubwa na viwango vya kimataifa, uwazi ,unazingatia sheria za nchi na ni kielelezo cha uwekezaji wa kupigiwa mfano katika sekta ya Madini nchini.


Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Anamringi Macha, amepongeza Mgodi wa Barrick Bulyanhulu kwa kuhakikisha wakati wote unafanya kazi kwa ushirikiano mkubwa na Serikali sambamba na kufanikisha miradi mikubwa ya maendeleo katika mkoa hususani katika sekta za elimu, afya, maji na ujenzi wa miundo mbinu ya barabara.


Awali akitoa taarifa kwa Kamati hiyo, Meneja Mkuu wa Mgodi wa Barrick Bulyanhulu, Victor Lule amesema kuwa mgodi umekuwa mstari wa mbele kuendesha programu za kudhibiti maambukizi ya UKIMWI na Malaria kwa wafanyakazi wake pia umeimarisha zahanati ya mgodi kuhakikisha inatoa huduma bora na za kisasa wakati wote.


Lule ameongeza kuwa mbali na kuimarisha huduma za ndani ya Mgodi pia mgodi umekuwa mstari wa mbele kuboresha kituo cha afya cha Bugarama na kupeleka kampeni ya kupambana na Malaria ijulikanayo kama Zero Malaria kwenye vijiji vinavyozunguka Mgodi kwa kupuliza dawa za kuua mazalia ya mbu na kuwagawia wananchi vyandarua vyenye dawa.


Naibu Mkurugenzi Mkuu wa TACAIDS, Dkt. Catherine Joachim ametoa ushauri kwa Mgodi kuendesha programu za tohara kwa wanaume na dawa za kuzuia maambukizi mapya ndani na nje ya mgodi na kuongeza kuwa licha ya kuwepo madawa ya kufubaza virusi vya UKIMWI bado kuna maambukizi mapya yanaendelea kujitokeza na sehemu mojawapo hatarishi kupata ugomjwa huo ni maeneo ya migodini.

Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI wakitembelea Zahanati ya mgodi wa Dhahabu wa Barrick Bulyanhulu

Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI wakitembelea Zahanati ya mgodi wa Dhahabu wa Barrick Bulyanhulu

Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI wakitembelea Zahanati ya mgodi wa Dhahabu wa Barrick Bulyanhulu

Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI wakitembelea Zahanati ya mgodi wa Dhahabu wa Barrick Bulyanhulu

Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI wakitembelea Zahanati ya mgodi wa Dhahabu wa Barrick Bulyanhulu

Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Afya, UKIMWI Mhe. Hassan Mtenga akizungumza wakati ziara ya kikazi ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI katika mgodi wa Dhahabu wa Barrick Bulyanhulu

Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Afya, UKIMWI Mhe. Hassan Mtenga akizungumza wakati ziara ya kikazi ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI katika mgodi wa Dhahabu wa Barrick Bulyanhulu

Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Afya, UKIMWI Mhe. Hassan Mtenga akizungumza wakati ziara ya kikazi ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI katika mgodi wa Dhahabu wa Barrick Bulyanhulu


Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa akizungumza wakati ziara ya kikazi ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI katika mgodi wa Dhahabu wa Barrick Bulyanhulu
Meneja Mkuu wa Mgodi wa Barrick Bulyanhulu, Victor Lule akizungumza wakati ziara ya kikazi ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI katika mgodi wa Dhahabu wa Barrick Bulyanhulu

Mkuu wa Mahusiano ya Jamii na Mazingira Mgodi wa Barrick Bulyanhulu, Agapit Paul akizungumza wakati ziara ya kikazi ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI katika mgodi wa Dhahabu wa Barrick Bulyanhulu

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Anamringi Macha akizungumza wakati ziara ya kikazi ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI katika mgodi wa Dhahabu wa Barrick Bulyanhulu

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Anamringi Macha akizungumza wakati ziara ya kikazi ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI katika mgodi wa Dhahabu wa Barrick Bulyanhulu

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Anamringi Macha akizungumza wakati ziara ya kikazi ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI katika mgodi wa Dhahabu wa Barrick Bulyanhulu

Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mhe. Mboni Mhita akizungumza wakati ziara ya kikazi ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI katika mgodi wa Dhahabu wa Barrick Bulyanhulu





Top News