Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akibonyeza Kitufe kuashiria uzinduzi wa Mchakato wa ukusanyaji maoni kutoka kwa wananchi kuhusu Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050. Rais Samia alifanya uzinduzi huo wakati wa Maadhimisho ya miaka 62 ya Uhuru wa Tanzania Bara yaliyofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma tarehe 09 Desemba, 2023.



Viongozi, pamoja na wageni mbalimbali wakiwa kwenye Maadhimisho ya miaka 62 ya Uhuru wa Tanzania Bara pamoja na uzinduzi wa Mchakato wa ukusanyaji maoni kuhusu Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050. Maadhimisho hayo yamefanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma tarehe 9 Desemba, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) Bw. Gilead Teri wakati akielezea majukumu ya Kituo wakati wa Maadhimisho ya miaka 62 ya uhuru wa Tanzania Bara yaliyofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji Profesa Kitila Mkumbo, Waziri wa Fedha Mhe. Mwigulu Nchemba, Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera Bunge na Uratibu Mhe. Ummy Nderiananga, Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango Bw. Lawrence Mafuru pamoja na Wajumbe wengine wa Kamati ya Uongozi ya Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na viongozi pamoja na wageni mbalimbali kabla ya kuzindua Mchakato wa ukusanyaji maoni kutoka kwa wananchi kuhusu Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050. Rais Samia alifanya uzinduzi huo wakati wa Maadhimisho ya miaka 62 ya uhuru wa Tanzania Bara yaliyofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma.

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan ameainisha changamoto zinazopaswa kupewa kipaumbele ikiwemo kufungamanisha ukuaji wa uchumi na sekta za uzalishaji.


Rais Samia amesema hayo kwenye maadhimisho ya miaka 62 ya Uhuru wa Tanzania Bara sanjari na Mkutano wa kwanza wa uzinduzi wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete.


Aidha Rais Samia ametaka sekta mbalimbali za uzalishaji ziimarishwe zaidi ikiwemo kilimo ambayo inakua kwa asilimia 4 tu kwa sasa tofauti na inavyotakiwa.


Pia amesisitiza kuimarishwa kwa ushiriki wa sekta binafsi ndani na nje ya nchi ili kufanya wenyeji kuwa na utayari wa kupokea na kushirikiana na wageni wanaokuja kuwekeza na kufanya biashara nchini.


Rais Samia amesema dira hiyo mpya itatakiwa kuzingatia kigezo cha kuongeza pato la kila mwananchi kufikia dola za Kimarekani 3,000 kwa mwaka ambacho hakikufikiwa katika dira ya mwaka 2000-2025.


Amesema kushindwa huko kulisababishwa na ukuaji wa uchumi kutojielekeza kwenye sekta zinazogusa maisha ya watu wengi, hivyo umasikini vijijini haujapungua kwa kasi iliyotarajiwa.


Kuhusu suala la Maadili ya Taifa (ethos), Rais Samia amesema ni muhimu taifa kuwa na watu mahiri, makini na waadilifu ili kupata jamii inayochukia rushwa kila mahali, inayojituma na kufanya kazi bila kusukumwa na inayopinga na kulaani ukwepaji kodi.


Vile vile, Rais Samia ametoa wito kwa Watanzania wote ndani na nje ya nchi (Diaspora) kushiriki kutoa maoni katika kuandaa Dira ya Taifa ya Maendeleo kupitia njia za kisasa zitakazoainishwa na Tume ya Mipango.



Zuhura Yunus
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu


IKIWA zimebaki siku kadhaa kuelekea Fainali ya Shindano la Bingwa Kampuni ya StarTimes Media imetambulisha zawadi ya gari aina ya Toyota crown yenye thamani ya Sh milioni 20 itakayotoa kwa mshindi wa shindano la bingwa msimu wa pili katika fainali itakayofanyika wiki ijayo.

Shindano la bingwa msimu wa pili lilizinduliwa tangu Julai mwaka huu na kushirikisha washiriki 24 ambao ni maarufu mitandaoni waliokaa katika jumba moja maalum kuonesha uhalisia wa maisha yao na kuoneshwa kwenye televisheni ya Tv3.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Masoko na Maudhui wa StarTimes, David Malisa alisema mshindi wa jumla sio tu ataondoka na gari bali fedha taslimu ambazo itakuwa ni kama ‘surprise’ zitakazoenda kumsaidia kuendesha maisha yake.

“Tunawashukuru Watanzania wanaoendelea kufuatilia vipindi vyetu, msimu huu wa sikukuu tunawaambia Lipa Tukubusti, lipia vifurushi tofauti upate nyongeza na kushuhudia fainali hii kuona bingwa ni nani msimu huu.

Pia, amesema shindano hilo limekuwa ni daraja la kufunguka kwa fursa nyingi kwani wapo watakaopata ubalozi wa bidhaa kutoka katika makampuni mbalimbali ya biashara.

Kwa upande wake, Meneja Mradi wa shindano hilo, Ombeni Phiri amesema washiriki wamebaki 12 walioingia fainali hivyo, wataendelea kuchuana hadi wiki ijayo mshindi mmoja ataondoka na gari hilo Pia, kutakuwa na zawadi kwa mshindi wa pili na tatu.

Aidha ameongeza kuwa washiriki hao wakiwa ndani ya jumba hilo walijifunza vitu vingi ikiwemo fursa za kutumia mitandao ya kijamii kujiinua kiuchumi na kukuza majina yao.
Kaimu Mkuu wa Idara ya Ujenzi nguvu za pamoja na harakati, kutoka TGNP, Florah Ndaba akizungumza jijini Dar es Salaam leo Desemba 9, 2023 na Wanaassi za Kiraia kutoka mikoa tofauti tofauti hapa nchini juu ya mfumo ambao Mashrika yasiyo ya kiserikali kuweka taarifa zao na kazi zao wanazozifanya katik jamii juu ya kutetea haki za Wanawake, wasichan na watu waliopembezoni ili jamii ione.






Baadhi ya wadau wakiwa katika mafunzo ya jinsi ya kuweka taarifa za Aasi zao za kiraia katika mfumo.

KATIKA Kutekeleza Mradi wa Pamoja Tapo sauti ya Mwanamke na Uongozi Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) watoa elimu kwa vitendo juu ya Mfumo wa taarifa za Asasi za kiraia.

Kaimu Mkuu wa Idara ya Ujenzi nguvu za pamoja na harakati, kutoka TGNP, Florah Ndaba jijini Dar es Salaam leo Desemba 9, 2023 amesema kuwa mafunzo hayo yatawawezesha wamiliki au wafanyakazi wa mashirika yasiyo ya kiserikali kuweka taarifa zao pamoja na kazi mbalimbali wanazozifanya ili kuleta maendeleo katika utetezi wa kazi za mwanamke, msichana na watu waliopembezoni.

Amesema kuwa kupitia Mradi huo unafanywa na Mashirika Mawili ambayo ni Women Fund Tanzania na TGNP ambao unafanywa katika Mikoa 10 ambayo ni Dar es Salaam, Mbeya, Lindi, Mtwara, Dodoma, Kilimanjaro, Shinyanga, Kigoma na Mara.

Lengo kuu la Mradi huo ni kuhakikisha wanawake na wasichana na watu walio pembezo wanafaidika na wanafurahia haki za binadamu na haki zao.

Frolah amesema wakati wanaanza mradi huo kulikuwa na maeneo yenye changamoto kwa nchi ambayo waliyaibua, maeneo hayo ni ushirikiano wa pamoja baina ya watetezi wa haki za wasichana na Wanawake ambao wanapelekea kufanya mabadiliko ambayo yanapekekea wanawake na wasichana na watu waliopembozoni kufurahia haki zao.

"Tunajua ili watu wafurahie haki kunawafadhili wengi ambao wanatakiwa washirikishwe ikiwemo Asasi za kiraia zinazofanya kazi ya kutetea haki za wanawake lakini pia tuligundua kuwa na changamoto ya taarifa za jinsi ya Asasi za kiraia zinafanya kazi."

Kwa hiyo mfumo huo ulitengenezwa kwaajili ya kusaidia Asasi za kiraia hasa zisizo na uwezo mkubwa wa kujiendesha, ingawawanafanys kazi katika ngazi ya jamii.

Amesema Asasi hizo zilikuwa hazina uwezo wa kuonesha ushahidi wa kazi wanasozifanya kutokana na kutokuwa na uelewa wa kufungua tovuti na mitandao ya kijamii. Ila kwa sasa Teknolojia imeenea tunaona inawezekana ndio maana tumekuja na programu ya pamoja kwaajili ya kuweka taarifa za kila Shirika.

Akizungumzia kuhusiana na mashirika ambayo yamejisajili TGNP na yameshaingia katika mfumo hio, Frolah amesema kuwa mashirika 100 ya mfano yameshaingiza taarifa zao katika mfumo huo ingawa Mtandao huo umesajili Asasi za kiraia 260.

Amesema kazi kubwa ya Programu hiyo nikuonesha kazi za Asasi za Kiraia lakini kuonesha nguvu iliyopo katika maeneo tofautitofauti kwa sababu itakuwa Programu moja inayoonesha Asasi za Kiraia kuona zinaonesha mambo makubwa wanayofanya.

Pia ni amesema kuwa Asasi za Kiraia zinazoweka taarifa zake katika mfumo huo zitakuwa zinatoa ushahidi wa kazi ambazo wanazinafanya katika maeneo yao.

"Pia ni njia mojawapo ya fundruising tool pale wanapotaka kufanya kazi zao na zionekane kupitia mfumo huo." Ameeleza Florah

Amesema kubuni mfumo huo ilikuwa ni kuwasaidia mashirika kuonesha kazi zao lakini kuyasaidia mashirika kuwapa uelewa juu ya umhimu wa kukusanya taarifa, kwa sababu walikuwa hawana uelewa wakukusanya taarifa ambazo zinatakiwa kusambazwa kwa jamii ili jamii ione.

NA DENIS MLOWE, NKASI

HALMASHAURI ya Wilaya Nkasi Mkoani Rukwa Katika kipindi cha mwaka 2022/2023 imepokea zaidi ya shilingi bilioni 13.02 kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo katika wilaya hiyo ikiwemo ya elimu, afya iliyotolewa na serikali ya awamu ya sita chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan.


Akizungumza na wanahabari , Mkuu wa Wilaya ya Nkasi, Peter Lijualikali alisema kuwa fedha hizo zimetolewa na Mama Samia Suluhu Hassan ikiwa ni kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo katika wilaya hiyo ambayo yote iko katika kiwango cha asilimia 96 na mingine kukamilka wananchi kuona matunda yake.


Alisema kuwa fedha hizo zimetumika kwenye miradi mbalimbali ikiwemo ya elimu afya, kilimo na mifugo na miradi mingine ya maendeleo ambayo imejengwa katika maeneo ambayo awali yalikuwa hayana kabisa ikiwemo shule za msingi pembezoni mwa wilaya ya Nkasi na nchi jirani.

Lijualikali alisema kuwa Shilingi bilioni 1,535,600,000 zimepokelewa na kufanya kazi ya ujenzi wa shule mpya tatu za msingi za Isaba, Mtakuja na Ntalamila ambapo ujenzi umehusisha vyumba 8 vya madarasa, jengo la utawala, vyumba 2 vya madarasa kwa ajili ya wanafunzi wa awali pamoja na ujenzi wa vyoo vya walimu na wanafunzi na kuongeza kuwa fedha hizo zimetumika kujenga vyumba 15 vya madarasa katika shule za msingi za Mtapenda.


Aliongeza kuwa kati Shilingi milioni 200,000,000 zilitumika kwa ajili ya ukamilishaji wa nyumba 8 za walimu katika shule za msingi za Sentamapufi, Mjimwema, Nkata, Lyantwiya, Itanga, Mkiringa, Lwesusi na Lusembwa.Shilingi 180,000,000 zilipokelewa kwa kufanya kazi ya ukarabati wa vyumba 9 vya madarasa katika shule za msingi za Mkwamba, Itete, Kate, Kala, Utinta na Chalantai,Tundu,Mkombe, Kirando na Lupata.


Aidha alisema kuwa fedha nyingine zaidi ya sh.milioni 180 zilitumika katika ujenzi wa ukamirishaji wa maabara sita katika shule sita za Korongwe Beach, Mashete, Sintali, Ninde, Wampembe na Kirando Itete na Shilingi 40,000,000 kwa ajili ya ukamilishaji wa mabweni 2 katika shule mbili za sekondari za Nkasi na Kate ,Shilingi 50,000,000 zimepokelewa na kufanya kazi ya ukamilishaji wa bwalo moja katika shule ya sekondari Nkasi


“Sekta ya elimu tushukuru kwamba Mama samia kaitendea haki katika wilaya yetu ya Nkasi na kuwataka wazazi wawapeleke Watoto wao shule kwani hatapenda kusikia kuna michango ya ada wala madawati kwani kila kitu kipo sawa kwenye shule zetu na zimejengwa shule za kisasa kutokana na fedha za mama samia zilizoletwa kwenye kipindi hiki” alisema

Akizungumzia sekta ya afya alisema kuwa miradi mingi imetekelezwa na serikali chini ya Mama Samia Suluhu Hassan ambapo fedha mbalimbali zimepokelewa na katika wilaya hiyo ikiwemo kiasi cha Shilingi 800,000,000 zimepokelewa na kutumika kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba katika hospitali ya Wilaya ,Shilingi 200,000,000 zimepokelewa na kufanya kazi ya ukamilishaji wa zahanati katika vijiji vinne.


Aliongeza kuwa Shilingi 659,093,063 fedha za Mfuko wa pamoja wa Afya (HSBF) zimepokelewa Na kufanya kazi ya ufuatiliaji, ununuzi wa dawa, mafunzo pamoja na ukarabati Mdogo wa vituo vya kutolea huduma za afya, shilingi 456,140,548 zimepokelewa na kufanya kazi ya ujenzi wa vyoo bora katika Zahanati za 9 za Utinta, Miombo, Kizumbi, Musilihofu, Mlambo, Mpasa, Kate, Swaila na Lyele na Shilingl 300,132,000 zimepokelewa kwa ajili ya Mitihani kwa wanafunzi wa kidato cha pili na nne.


“Kwa kweli tunamshukuru sana Mh. Rais Mama Samia Suluhu Hassan kwa kuweza kutimiza ahadi mbalimbali kwa wananchi wa Nkasi katika sekta ya afya wananchi wanajivunia sana kuwa kiongozi anayewajali kwani sekta ya afya imepokea fedha nyingi zaidi na wanahabari nitawaomba mje kutembelea kujionea wenyewe mambo yaliyofanyika katika wilaya hii.” Alisema LijualikaliS


Lijualikali alisema kuwa kwa kipindi hichi Shilingl 315,523,910 fedha ambazo zlipokelewa za ujenzi wa miundombinu katika vituo vya kutolewa huduma za afya ambavyo ni Kasu, Kate, Nkundi (Kantawa) Londokazi, Korongwe, Mwai, Nkomolo, Kabwe, Mashete na Hospitali ya Wilaya.

“{Kuna fedha nyingi zimeendelea kutolewa na serikali ya Mama Samia kwa ajili ya wananchi wa wilaya hii hivyo napenda kutoa shukrani za dhati kwa Serikali ya awamu ya sita ikiongozwa na Mhe. Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dr. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha nyingi za utekelezaji wa miradi ya Maendeleo. Aidha fedha hizi zimesaidia uboreshaji wa utoaji wa huduma za elimu na afya katika vituo vya kutolea huduma pamoja na huduma zingine.Tunaomba Mungu azidi kumlinda siku zote za Maisha yake “ alisema.


 





 Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani, Mhe. Hassan Iddi Mwamweta amewasilisha Hati za Utambulisho kwa Rais wa Ujerumani Mhe. Frank -Walter Steinmeier, Rais wa Ujerumani. Katika mazungumzo yao viongozi hao wameahidi kuendeleza ushirikiano mzuri uliopo kati ya Ujerumani na Tanzania.





East African Community Headquarters, Arusha, Tanzania, 9th December, 2023: In a groundbreaking development for regional trade, the East African Community (EAC) Secretariat today unveiled a new mobile application (App) dedicated to the elimination of Non-Tariff Barriers (NTBs) – the EAC NTBs App.

This innovative App is set to revolutionise the region’s trading landscape by streamlining the reporting, monitoring, and resolution of impediments traders face as they conduct business across borders.

The development of the EAC NTBs APP was funded by the Netherlands through TradeMark Africa (TMA).

The EAC NTBs App, seamlessly blending SMS, email, and phone reporting methods, offers economic operators a one-stop solution for effectively reporting Non-Tariff Barriers to trade. By streamlining the NTB reporting process, the App will aid traders and producers in tackling obstacles that impede their trade efficiency and competitiveness. Additionally, it ensures transparency and quick resolution of issues by engaging technical and policy-level mechanisms, such as National Focal Points, the National Monitoring Committees (NMCs) and the Regional Monitoring Committee (RMC).

Speaking during the launch of the App, EAC Deputy Secretary General in charge of Customs, Trade and Monetary Affairs, Ms. Annette Ssemuwemba said the EAC NTBs App marks a pivotal moment in creating a smooth trading environment across the EAC region.

“We are dedicated to eradicating the barriers that impede economic growth, and integration. This innovative solution serves as a powerful tool to empower traders, producers and economic operators offering them with a unified platform to promptly address and resolve NTBs,” she added.

The Deputy Secretary General further noted that the removal of NTBs holds paramount significance in fostering a more efficient and equitable trade environment. Noting that these barriers, often in the form of procedural complexities, or administrative hurdles, hinder the smooth flow of goods and services across borders.

“Empowering the private sector to report NTBs encountered and enabling them to track the progress of the NTB through the App is key to enhancing the business environment in the region, it is our hope that this will be the turning point in effectively identifying and swiftly resolving NTBs in the region,” Ms. Ssemuwemba.

“At TradeMark Africa, we believe in fostering a vibrant and conducive trade environment that propels economic growth and regional integration. This revolutionary app is a testament to our commitment to providing strategic solutions in digital trade,” emphasised Director, Trade Policy, and Trade Facilitation, Benedict Musengele.

NTBs pose a major problem for traders and producers, as they can reduce profits and limit market access. NTBs include issues that can hinder trading effectively such as discriminatory requirements for special licenses and permits, excessive paperwork, complicated customs procedures, and bureaucratic delays at borders.

A recent EAC Regional Meeting Committee (RMC) report (2023) estimated the direct costs of NTB’s at USD16,703,970 and total trade impact at USD94,918,000 decreasing trade by an average of 58%.

However, since 2017, EAC has resolved 89.5% of the reported NTBs (EAC Time Bound Programme report, 2023). In addition, there has been a relatively steady decrease in reported NTBs. In recent years, from 2021 to 2023, the number of reported NTBs complaints has remained stable, ranging between 8 and 11 cases annually with a significant improvement in the resolution of NTBs reported to an average of 88.3 days.

Between June 2022 and June 2023, a total of 16 NTBs complaints were reported within EAC. Out of these, 9 NTBs have been resolved while 7 complaints remained in progress. A significant number of NTB complaints were addressed (56.25%) and resolved within the given timeframe. However, a notable portion of complaints, specifically (43.75%) were still in progress by end of June 2023.

The EAC NTBs App allows the users to report the complaints in one of the three (3) EAC official languages; English, Swahili and French and can be downloaded from the Apple Store, Google’s Play Store, and other Android devices.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimsikiliza Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango Bw. Lawrence Mafuru kuhusu kazi mbalimbali ambazo zinafanyika katika Tume hiyo wakati wa Maadhimisho ya miaka 62 ya Uhuru wa Tanzania Bara tarehe 9 Desemba, 2023. Maadhimisho hayo pamoja na uzinduzi wa Mchakato wa ukusanyaji maoni kuhusu Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, yamefanyika kwenye ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimsikiliza Msajili wa Hazina Bw. Nehemia Mchechu mara baada ya kuwasili katika Banda la Maonesho la Hazina wakati wa Maadhimisho ya miaka 62 ya Uhuru wa Tanzania Bara tarehe 9 Desemba, 2023.




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan katika Maadhimisho ya Miaka 62 ya Uhuru wa Tanzania Bara pamoja na Mchakato wa ukusanyaji maoni kuhusu Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla, Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Bara Abdulrahman Kinana pamoja na Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango Bw. Lawrence Mafuru wakati wa Maadhimisho ya miaka 62 ya Uhuru wa Tanzania Bara tarehe 9 Desemba, 2023 pamoja na Mkutano wa Kwanza wa Kitaifa wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla, Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango Bw. Lawrence Mafuru pamoja na baadhi ya Watumishi wa Tume hiyo na Wajumbe wa Bodi wakati wa Maadhimisho ya miaka 62 ya Uhuru wa Tanzania Bara pamoja na Mkutano wa Kwanza wa Kitaifa wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, uliofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma tarehe 9 Desemba, 2023.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji Profesa Kitila Mkumbo, Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango Bw. Lawrence Mafuru pamoja Makamishna wa Tume ya Mipango wakati wa Maadhimisho ya miaka 62 ya Uhuru wa Tanzania Bara pamoja na Mkutano wa Kwanza wa Kitaifa wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, katika ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma tarehe 9 Desemba, 2023.










Viongozi mbalimbali wakiwa kwenye Maadhimisho ya miaka 62 ya Uhuru wa Tanzania Bara pamoja na uzinduzi wa Mchakato wa ukusanyaji maoni kuhusu Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050. Maadhimisho hayo yamefanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma tarehe 9 Desemba, 2023.







Shirika la mazingira na maendeleo EMEDO limeutambulisha mradi wa kuzuia watu kuzama maji katika Ziwa Victoria kwa wadau mbalimbali wa uvuvi mkoani Mwanza.


Afisa Mradi huo, Arthur Mgema amesema lengo ni kuzuia vifo vitokanavyo watu kuzama maji katika Ziwa Victoria hasa wavuvi, watoto na wanawake wachakataji wa mazao ya samaki/ dagaa ambao wako kwenye hatari zaidi.

Akifungua kikao cha kuutambulisha mradi huo, Katibu Tawala Mkoa Mwanza, Elikana Balandya amesema matukio ya watu kuzama maji yanazuilika endapo kila mmoja atatimiza wajibu wake.

Amesema kwa Mkoa Mwanza Serikali inatekelezeka mpango wa BBT (Building Better Tomorrow) katika sekta ya ufugaji na uvuvi hivyo mradi wa kuzuia kuzama maji katika Ziwa Victoria utasaidia kutoa elimu ili kuzuia vifo zitokanavyo na kuzama maji.

Mradi wa kuzuia kuzama maji katika Ziwa Victoria unatekelezwa na shirika la EMEDO katika mikoa ya Mwanza, Mara na Kagera katika kipindi cha miaka mitatu hadi mwaka 2025 kwa ufadhili wa taasisi ya RLNI- Life Boats ya nchini Uingereza.
Na George Binagi- GB Pazzo, BMG

Afisa Mradi wa kuzuia kuzama maji Ziwa Victoria, Arthur Mgema (kulia) akimkabidhi Katibu Tawala Mkoa Mwanza, Elikana Balandya (kushoto) ripoti ya utafiti uliofanywa na shirika la EMEDO mwaka 2021 kuhusu sababu za wavuvi kuzama maji pamoja na rasimu ya uvuvi salama iliyoandaliwa katika mwalo wa Busekera mkoani Mara.

Katibu Tawala Mkoa Mwanza, Elikana Balandya akifungua kikao cha kuutambulisha mradi wa kuzuia kuzama maji katika Ziwa Victoria kilichowakutanisha wadau jijini Mwanza.

Afisa Mradi wa kuzuia kuzama maji Ziwa Victoria, Arthur Mgema akieleza kuhusu mradi huo ambao umelenga kutoa elimu kwa jamii ya wavuvi ili kuchukua tahadhari za kuzuia kuzama maji.

Kaimu Afisa Maendeleo Mkoa Mwanza, Rehema Mkinze akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao cha kuutambulisha mradi wa kuzuia kuzama maji Ziwa Victoria.

Wadau mbalimbali mkoani Mwanza wakifuatilia kikao cha kuutambulisha mradi wa kuzuia kuzama maji katika Ziwa Victoria.

Kwa mujibu wa shirika la afya duniani (WHO) watu 236,000 hupoteza maisha kwa kuzama maji. Hata hivyo bado kuna changamoto ya upatikanaji wa takwimu za watu wanaofariki kwa kuzama maji katika mataifa mbalimbali duniani, Tanzania ikiwemo hivyo pamoja na mambo mengine, pia mradi wa kuzuia kuzama maji Ziwa Victoria utasaidia upatikanaji wa takwimu hizo.
SOMA PIA>>> HABARI ZAIDI HAPA

Top News