Jumuiya ya Umoja wa Wanawake wa Chama cha Mapinduzi (UWT) imepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya maafa iliyotokea tarehe 2/12/2023 Wilaya ya Hanang Mkoa wa Manyara kufuatia mvua kubwa iliyopelekea mafuriko na Mawe makubwa na Miti kutoka Mlima Hanang kuporomoka na kuingia mji wa Kateshi na kusababisha athari kwa kaya 1,150 na watu 5,600, na kusababisha  vifo vya watu zaidi ya 50 na majeruhi 80 ambao wamepelekwa hospital mbalimbali.

Natoa  pole kwa Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan,Rais Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,ndugu ,jamaa na marafiki walioguswa na misiba hiyo na nawaombe Marehemu wapumzike mahala pema Peponi na majeruhi wote wapone haraka,pia  natuma salam za pole kwa wananchi wote waliokumbwa na maafa hayo. 

UWT inapongeza Juhudi za Serikali kwa hatua mbalimbali za haraka zilizochukuliwa kutokana na maafa haya,ikiwemo msaada wa dharura  na uokoaji, kuwapatia makazi na kugharamia matibabu kwa waathirika.

Aidha sisi UWT tunaiunga Mkono Serikali kwenye jitihada hizo na leo tarehe 4/12/2023 jiji Dar Es Salaam imefanyika Kamati ya Utekelezaji ya Dharura ambayo imewaalika wajumbe wa Baraza Kuu waliopo Dar Es Saalam,wabunge wa Viti Maalum na baadhi ya viongozi na tumejipanga kwenda Hanang haraka kuwafariji wananchi wenzetu waliofikwa na maafa haya na kwenda kukabidhi vifaa mbalimbali ambavyo UWT kwa kushirikiana na wadau wetu tumefanikiwa kuvinunua ikiwemo; 

Magodoro-100 ,Mashuka -50,Mablangeti -50,Vikoa 500,Madila 520 na vifaa mbalimbali kama vinavyoonekana Kwa kutambua kuwa uhitaji ni mkubwa na kwakuwa waathirika wakubwa kwenye maafa haya ni Wanawake na Watoto UWT tumewaelekeza wabunge wanawake wa CCM waendelea kuchangia kwa UWT ili tuendelee kuongeza vifaa hivi na tunatoa wito wa Wanawake wote kuguswa na kilichotokea Hanang ili waungane na UWT na  tumuunge mkono  Rais wetu Dkt Samia kwa kuwasaidia wananchi wenzetu wa Hanang walikumbwa na maafa.

Pia nawakaribisha wadau mbalimbali wenye nguo na vifaa vingine ambavyo vinaweza kuwa sadaka yako kwa wananchi wenzetu wa hanang, tunawakaribisha sana mziwasilishe kwenye ofisi zetu za UWT Makao Makuu Dodoma,Ofisi ndogo Dar Es Salaam zilizopo ofisi za CCM Mkoa wa Dar Es salaam.












Na. Dennis Gondwe, HOMBOLO BWAWANI

Halmashauri ya Jiji la Dodoma imezindua zoezi la ubainishaji watoto wenye mahitaji maalum katika jamii ili waweze kupata haki yao ya elimu na matunzo kwa mujibu wa sheria.

Kauli hiyo ilitolewa na Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mwl. Issa Kambi alipokuwa akizindua zoezi la ubainishaji watoto wenye mahitaji maalum katika jamii uzinduzi uliofanyika katika Shule ya Msingi Hombolo Bwawani iliyopo Kata ya hombolo Bwawani jijini Dodoma.

Mwl. Kambi ambae ni Afisa Elimu Maalum katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma alisema “kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma ambae alipenda sana kuwa nasi hapa leo napenda kuzindua rasmi zoezi la ubainishaji watoto wenye mahitaji maalum kwa maana ya kwenda kuwatafuta mtaani na kuwaleta kwenye vituo vyetu kama hiki na vitengo vingine. Zoezi litafanyika katika mitaa nane ya Itega, Salama, Lugala, Mnyakongo, Mtube, Nala, Chigongwe na Mbalawala”.

Alisema kuwa lengo la zoezi hilo ni kuwabaini watoto hao mahali walipo na kuwasogeza kwenye huduma na kuwapatia afua stahiki ikiwa ni pamoja na elimu na matunzo. “Tunafahamu kwamba baadhi ya familia zinaamini watoto hawa hawawezi kufanya mambo, lakini tunapokwenda kufanya ubainishaji tunawatia moyo na kuwashawishi kuwaleta watoto hawa shule. Kuanzia ngazi za familia tunapeleka elimu na baadae tunawaleta kwenye vituo kama hivi na kama mlivyoona watoto hawa wanafuraha” alisema Mwl. Kambi.

Akiongelea umuhimu wa zoezi hilo, Mkazi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma Juliana Linus alisema kuwa zoezi hilo ni muhimu kwa sababu linakwenda kuwapatia haki ya msingi watoto wenye mahitaji maalum katika Jiji la Dodoma. “Ni kweli wapo baadhi ya wazazi ambao wamekuwa na tabia ya kuwaficha watoto wao wenye ulemavu jambo linalowanyika haki watoto hao kupata elimu, afya na malezi bora” alisema Linus.

Zoezi la uzinduzi wa ubainishaji watoto wenye mahitaji maalumu katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma lilihudhuriwa na Jumuiya ya Shule ya Msingi Hombolo Bwawani ambayo ni shule jumuishi, Diwani wa Kata ya Hombolo Bwawani, maafisa waandamizi kutoka Halmashauri ya Jiji la Dodoma na wawakilishi wa Jumuiya ya Shule ya Msingi Feza tawi la Dodoma na wawakilishi wa serikali ya mtaa.


 

NYOTA wa Muziki kutoka Nigeria, ambaye pia ni mtayarishaji, mpiga vyombo vya muziki Pheelz, leo ametoa EP ya ya Pheelz Good( Triibe Tape) yenye nyimbo 4 ambazo kwa sasa zinapatikana kupitia Warner Records.

EP inangoma kama JOY' aliyomshirikishwa gwiji wa Afrobeats Olamide, kwa mujibu wa Pheelz anasema ‘’Joy’ ni wimbo maalum kwangu kwa sababu mimi na Olamide tumekuza udugu wetu na tumekuwa marafiki kwa miaka mingi"

Pia EP hiyo ina ngoma nyingine kama 'JELO' ambayo ilitoka muda kidogo na amemshirikisha Young Jonn, na pia kuna remix of “JELO” akimshirikisha Lekyz na Henry X, na ngoma nyinginr ni “Riddim & Blues.”

Akizungumza leo Novemba 4, 2023 amesema "Triibe Tape ni kazi nzuri ya Kabila na baada ya hapa, nitasafiri kote ulimwenguni kuungana na mashabiki. Kwa hivyo, ni mradi wa sisi kushirikiana nao kwenye jukwaa., na kuburudika na mziki mzuri".

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Abdulrahman Kinana, amewahakikishia wananchi wilayani Hanang Mkoa wa Manyara hususan waliokumbwa na janga la mafuriko, kwamba maelekezo ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, yatatekelezwa kikamilifu na idara na taasisi zote kama walivyoagizwa chini ya usimamizi wa Waziri Mkuu

Kinana ameyasema hayo leo Desemba 4, 2023 alipowatembelea waathirika wa mafuriko hayo katika baadhi ya vijiji vya Wilaya ya Hanang.

Kinana amewatembelea na kuwafariji wananchi waliopoteza ndugu zao na waliojeruhiwa na kulazwa hopitalini kutokana na janga hilo ambapo amewapa pole na kuwaomba wawe na subira katika kipindi hiki kigumu wanachopitia.






 

Na Pamela Mollel,Arusha

Aliyewahi kuwa Mkuu wa Wilaya sehemu mbalimbali nchini na Mwenyekiti wa halmashauri ya Arumeru Mstaafu Thomas Loy Ole Sabaya amechaguliwa kuwa Mwenyekiti Mpya wa chama hicho Mkoa kwa kupata idadi kwa kupata kura 463 huku mpinzani wake wa karibu Daniel Palagyo akipata kura 374 kati ya kura 951 huku Moja ikiharibika.

Uchaguzi huo umekuja kufuatia kifo cha aliyekuwa Mwenyekiti wa chama hicho Mkoa wa Arusha Marehemu Zelothe Stephen aliyefariki octoba 26 Jijini Dar es salaam alipokuwa akipatiwa matibabu.

Akiongea mara baada ya kuchaguliwa Sabaya amesema amewashukuru sana wajumbe akisema CCM hii ndio domokrasia maana kijana wangu amenikimbiza na kuonyesha ukomavu hivyo nitashirikiana na Wanachama wote kuanzia ngazi ya kitongoji kuhakikisha Mradi wa uchaguzi Mkuu unafanikiwa.

Aidha Akabainisha kuwa Arusha tuna bahati kwa kuwa na wajumbe wa kamati kuu 4 na kama hatufanyi mambo yakaenda tutakuwa hatutendi haki kwa kuwa Mkoa huu ni kinara na hatuna sababu ya kulia Lia tujenge Umoja na kuondoa Makundi.

Alisema Tuanza Mradi wa kushinda uchaguzi tukienda katika uchaguzi na makundi hatutashinda tutafute kero za wananchi ili kushinda uchaguzi sitegemea Kuna mtu atakwamishi kama tumepatana na kuondoa Makundi

Nawaahidi kushirikiana na wenzangu wote na wananchi tusikwamishane tunataka kushika Dola tunatakiwa kutatua kero za wananchi ili tushike Dola naomba wote tujiandae kwa uchaguzi

"Sitegemei Kuna namna ya kukwamishana hivyo tuanze Mradi wa kushinda uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi Mkuu twendeni kukipigania chama chetu"

Akiongea wakati akitangaza Matokeo ya uchaguzi huo Msimamizi Mkuu wa uchaguzi huo Anthony Mtaka ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Njombe amesema Sabaya amepata kura 467 huku Dkt.Palangyo akipata kura 374 na Edna Kivuyo kura 10 na Solomon Kivuyo akipata kura 56

Amesema wajumbe 951 wamepiga kura ambapo idadi kamili ya wajumbe waliotakiwa kupiga kura ni 1001 ndipo akamtangaza rasmi Thomas Loy Sabaya kuwa Mwenyekiti wa chama hicho Mkoa wa Arusha.

Amesema kwamba uchaguzi huo uwe sehemu ya kuongeza mshikamano na wajumbe kutambua umuhimu wa uchaguzi na kanuni zake zitakazosaidia kupata kiongozi makini atakayewaongoza na kukisemea chama kuelekea uchaguzi Mkuu.

Mtaka amemtaka Mwenyekiti kushikamanisha Wanaarusha na kuhubiri upendo mshikamano utulivu na amani Arusha wape upendo Wanaarusha waheshimishe unapohubiri yatoke moyoni kujenga Arusha.

Kwa Upande wake Mwenyekiti wa Muda Namelock Sokoine kuwapongeza viongozi karibuni na poleni mwaka Jana tulifanywa uchaguzi tulimchagua Zelothe Stephen kuwa Mwenyekiti lakini Mungu kwa Shani yake amemchukuwa hivyo kamati kuu ilituletea wagombea wa nne nafasi hiyo.

Amesema Tunamshukuru Mwenyekiti wetu Samia na kamati kuu kwa kututeulia wajumbe hawa wataogombea nafasi hii tunaimani Mojawapo atakayechaguliwa hapa atatupitisha katika uchaguzi Mkuu na serikali za mitaa kwa kishindo.

Amesema Uchaguzi huo ukawe alama ya Umoja mshikamano wetu naomba kwa Kauli ya pamoja tunamuunga Mwenyekiti wetu Rais Samia Suluhu Hassan tuungane kwa pamoja tukionyesha Umoja wetu na mshikamano wetu katika uchaguzi huu..

Hata hivyo Katibu wa Mkoa wa CCM Arusha Mussa Matoroka akisoma akidi ya wajumbe wa Mkutano huo amesema Idadi ya wajumbe wa Mkutano huo Arusha Mjini 128 Arumeru 160 longido 115 Meru 161 Karatu 88 Ngorongoro 156 Meru 153 Monduli 124 Mkoa 19 ikiwa idadi kwa ujumla ya wapiga kura 951 kati ya wajumbe 1003.

Nao WASIMAMIZI wa uchaguzi waliombatana na Msimamizi Mkuu Shani Ngatite na Husein Mwaga walitoa angalizo la wajumbe kutoa idadi sahihi ili kutovuruga uchaguzi huo kwani hawatasita kuchukuwa hatua nawafuate kanuni taratibu za uchaguzi ndani ya chama.

Wagombea waliogombea katika Mkutano huo maalumu ni Loy Sabaya Daniel Palagyo,Edna Israel Kivuyo,Solomon Ole Sendeka Kivuyo

Wakati akiomba kura mgombea Edna Kivuyo amesema kuwa suala na makatibu wa CCM kata kulipwa fedha hilo nitaenda kusimamia kuhakikisha wanarudisha utaratibu wa zamani kwa Lengo la kurudisha nidhamu ndani ya chama.

Nae Mgombea Solomoni Kivuyo amesema ataunganisha chama na serikali sanjari na kuleta Umoja kwa kutumia uzoefu wake wa miaka zaidi ya 44 ndani ya serikali.

Awali Mgombea Daniel Palagyo amesema kwamba miaka 10 ya kuwepo ndani ya uongozi wa chama Sasa ameiva kuweza kuwa Mwenyekiti wa Mkoa katika kutatua changamoto za wafugaji wakulima wafanyabiashara wakubwa na wadogo wa Mkoa wa Arusha.

Wagombea wote baada ya kutagazwa Matokeo hayo wamepongeza uchaguzi huo na kuelezea umeenda kwa haki huku wakieleza kutoa ushirikiano kwa Mwenyekiti Huyo Kuendeleza umoja.




 

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akitoa heshima za mwisho Disemba 04, 2023 kwa miili ya watu waliofariki dunia katika maafa yaliyosababishwa na mafuriko yaliyotokea katika eneo la Katesh Mkoani Manyara.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akipita katika moja ya maeneo yaliyoathiriwa na mafuriko katika kijiji cha Gendabi, Katesh mkoani Manyara. Mheshimiwa Majaliwa yupo mkono humo kujionea hali ya athari iliyosababishwa na mafuriko.

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewasili wilaya ya Hanang mkoani Manyara na kukutana viongozi wa mkoa huo na wa Serikali na kupokea taarifa ya hali halisi ya tukio la maafa lililotokea jana na kusababisha vifo na majeruhi.

Waziri Mkuu alitoa pole kwa viongozi na wananchi wa Hanang kwenye kikao kilichofanyika leo (Jumatatu, Desemba 4, 2023) kwenye ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Hanang na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Mawaziri, Naibu Mawaziri, Makatibu Wakuu, vyombo vua ulinzi na usalama na Watendaji wa taasisi za Serikali.

Waziri Mkuu amesema tukio la jana linafanana na tukio jingine lililowahi kutokea mwaka 1990 katika eneo la Ndanda ambako mlima uliporomoka na kusomba nyumba na barabara, hali ambayo ilisababisha vifo na majeruhi.

Amezishukuru Kamati za Maafa za Wilaya na Mkoa ambazo zilianza kuchukua hatua za uokoaji tangu jana, lakini pia mawaziri na watendaji wao ambao walikuja kutoa msaada kwa kuungana na viongozi wa mkoa wa Manyara.

Amesema matibabu yanaendelea kutolewa kwa majeruhi ambapo timu ya madaktari bingwa kutoka Dodoma, Singida na Arusha imeungana na kuanza kutoa huduma za upasuaji kwa wagonjwa watatu waliovunjika mifupa.


Amesema majeneza yameagizwa kutoka Babati na Singida ili ndugu waliotambuliwa waweze kuhifadhiwa kwenye nyumba zao za milele.


Hivi sasa, Waziri Mkuu na baadhi ya mawaziri wamekwenda kukagua eneo la Mlima Hanang kwa kutumia helikopta. Eneo hilo ndiko maporomoko ya udongo yalianzia. Baadaye atashiriki kuaga miili ya marehemu na ndipo taarifa rasmi itatolewa.
Mwakilishi wa Taasisi ya Tanzania China Friendship Jijini Dar es Salaam wanaofanya kazi na Ubalozi wa China nchini Husna Abdurhaman Sharif kushoto akimkabidhi Mbunge wa Jimbo la Muheza (CCM) ambaye pia ni Naibu Waziri wa Wizara ya Utamaduni,Sanaa na Michezo Hamisi Mwijuma alimaarufu MWANA FA sehemu ya Msaada wa vitanda 24 katika Hospitali ya wilaya ya Muheza vyenye thamani ya Milioni 16.1 katikati ni Mbunge wa Jimbo la Muheza (CCM) Hamisi Mwijuma alimaarufu Mwana FA kwa ajili ya Hospitali ya wilaya ya Muheza Samia

Mwakilishi wa Taasisi ya Tanzania China Friendship Jijini Dar es Salaam wanaofanya kazi na Ubalozi wa China nchini Husna Abdurhaman Sharif kushoto akimkabidhi Mwenyekiti wa Halmashauri Msaada wa vitanda 24 katika Hospitali ya wilaya ya Muheza vyenye thamani ya Milioni 16.1 katikati ni Mbunge wa Jimbo la Muheza (CCM) Hamisi Mwijuma alimaarufu Mwana FA kwa ajili ya Hospitali ya wilaya ya Muheza Samia
Mwakilishi wa Taasisi ya Tanzania China Friendship Jijini Dar es Salaam wanaofanya kazi na Ubalozi wa China nchini Husna Abdurhaman Sharif kushoto akimkabidhi Mwenyekiti wa Halmashauri Msaada wa vitanda 24 katika Hospitali ya wilaya ya Muheza vyenye thamani ya Milioni 16.1 katikati ni Mbunge wa Jimbo la Muheza (CCM) Hamisi Mwijuma alimaarufu Mwana FA kwa ajili ya Hospitali ya wilaya ya Muheza Samia


Na Oscar Assenga, MUHEZA

TAASISI ya Tanzania China Friendship wameshukuru Rais Dkt Samia Suluhu kwa kufanya kazi kubwa kukuza uhusiano huo mkubwa uliopo kati ya China na Tanzania

Hayo yamesemwa leo na Mwakilishi wa Taasisi hiyo iliyopo Jijini Dar es Salaam wanaofanya kazi na Ubalozi wa China nchini Husna Abdurhaman Sharif wakati wa halfa ya kukabidhi msaada wa vitanda 24 katika Hospitali ya wilaya ya Muheza vyenye thamani ya Milioni 16.1.

Msaada huo ni kuunga mkono juhudi za Mbunge wa Jimbo la Muheza Hamisi Mwinjuma “Mwana FA ambaye amekuwa akipambana usiku na mchana kuhakikisha anawapa maendeleo wakazi wa Jimbo hilo.

Alisema kwa sababu ndani ya mwaka mmoja tayari amekutana na Rais wa China mara mbili na amekuwa kipenzi cha wachina wengi barani Afrika hivyo wanampongeza Rais samia kwa kazi kubwa ya kuwapa maendeleo nchini.

“Hii ni hatua kubwa sana hivyo tuna kila sababu ya kumpongeza Rais Dkt Samia Suluhu kwa kazi kubwa anayoifanya kuhakikisha anawapa maendeleo watanzania “Alisema

Msaada huo ulitolewa kufuatia ombi la Mbunge huyo wa Muheza ambaye pia ni Naibu Waziri wa Michezo Utamaduni na Sanaa hivyo nao wakaona wamuunge mkono hasa katika kusaidia sekta ya afya kwenye Hospitali ya wilaya kwa wakina mama na watoto.

“Kwani wakina mama duniana kote wana changamoto na tumeona tutoe msaada wa vitanda kwa wakina mama wajifungue salama na vitenda kazi vyengine na hii ni kiufuatia ombi la Mbunge wenu na hasa na urafiki wa kihistoria kati ya Tanzania na China nchi hizi ni marafiki wakubwa”Alisema Husna

Alisema taasisi yao ya Tanzania China Friendship wamekuwa wakitoa misaada nchi nzima katika Sekta ya Afya,Elimu na Teknolojia kuenzi urafiki huo mkubwa

Alisema kwamba wakina mama kwa ujumla wao kama taasisi wapo tayari kushirikiana na majimbo mbalimbali ambayo yatapeleka maombi ya ufadhili hata kwa fursa ya kwenda kusoma nje ya nchi na safari ya maendeleo ni ndefu lakini watafika na leo wanatoa vitanda vya aina tatu.

Awali Mbunge wa Jimbo la Muheza Hamisi Mwinjuma alimaarufu Mwana FA-aliishukuru Taasisi hiyo kwa kuamua kuwasaidia wananchi ikiwemo kusikia kusikia kilio chao ambacho walikiwasilisha kwao.

Alisema kwamba siku zote wanasema wanazungumzia hospitali hiyo na wana juhudi za kuwa na Hospitali ya wilaya ya Muheza huku akieleza ina historia kubwa akiwamo Rais Samia.

Alisema kwa sasa wana juhudi za kuhakikisha wanakuwa na Hospitali ya wilaya ya Muheza wakati wanakwenda kwenye uchaguzi 2025 wanataka wawe na kitu tofauti na kile ambazo walikikuta mwaka 2020.

Alisema na namna bora ya kuwa kiongozi wakati wanakwenda kwenye uchaguzi wawe wamefanya mabadiliko makubwa katika maendeleo tofauti na walivyoomba mara ya kwanza.

Aidha alisema wao kama viongozi kazi yao ni kutafuta suluhu hya matatizo ya wananchi ikiwemo yatakayojitokeza mapya wakati wanapokwenda kuomba tena ridhaa ya wananchi kwa mara nyengine.

“Matatizo yaje lakini yawe …Hospitali ni fursa ya kuonyesha kuna kitu tunafanya ndio maana tunahaingaika na ndugu zetu hawa wa Tanzania China Friendship wamesikia kilio chetu na kutusaidia”Alisema Mbunge Mwana FA.

Katika hatua nyengine Mbunge hiyo alimshukuru Rais Dkt Samia Suluhu kwa kuwapatia fedha kiasi cha Bilioni 3.7 kwa ajili ya Hospitali hiyo na bado wanaendelea kumuomba na wanajua kwa moyo wake wataendelea kupata zaidi.

“Ukija miaka miwili ijayo tutakuwa na Hospitali ya wilaya ya Samia Suluhu iliyokamilika,tunakushukuru na tunaendelea kukuomba mtusaidie kutushika mkono na DMO ataweza kuorodhesha mahitaji ili mtakapoweza mtusaidie”Alisema

Naye kwa upande wake,Katibu wa CCM wilaya ya Muheza alisema wanamshukuru Mbunge wao kwa sababu bado anahangaikia kuhakikisha wananchi wanapata maendeleo.

“Nikupongeze Mbunge wetu ambaye amekuwa ukifanya kazi kubwa kuhakikisha wana Muheza wanapata maendeleo makubwa sana na sisi Muheza tunaupendeleo wa kuletewa maendeleo kwa sababu ya juhudi zako mbunge hivyo nikuombe uweke nguvu kubwa sana kuhakikisha majengo yaliyopo kwenye eneo hilo la Hospitali yanamalizika”Alisema
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Said Mussa Shaib akizungumza wakati wa kufungua Semina ya siku tatu ya Ngazi ya Juu kuhusu Afrika tunayoitaka inayojadili fursa na changamoto mbalimbali zinazolikabili bara la Afrika katika masuala ya maendeleo inayofanyika jijini Dar es Salaam.
Mwakilishi Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Tanzania Mhe. Milisick Milovan (kulia) akifuatilia ufunguzi wa Semina ya siku tatu ya Ngazi ya Juu kuhusu Afrika tunayoitaka inayojadili fursa na changamoto mbalimbali zinazolikabili bara la Afrika katika masuala ya maendeleo inayofanyika jijini Dar es Salaam.



Balozi wa Comoro nchini Tanzania Mhe. Dkt. Ahamada El- Badaoui akipiga makofi kushangilia kitu wakati wa ufunguzi wa Semina ya siku tatu ya Ngazi ya Juu kuhusu Afrika tunayoitaka inayojadili fursa na changamoto mbalimbali zinazolikabili bara la Afrika katika masuala ya maendeleo inayofanyika jijini Dar es Salaam.





Balozi na Mwakilishi wa Tanzania nchini Ethiopia na katika Umoja wa Afrika Addiss Ababa, Mhe. Innocent Shio akishiriki ufunguzi wa Semina ya siku tatu ya Ngazi ya Juu kuhusu Afrika tunayoitaka inayojadili fursa na changamoto mbalimbali zinazolikabili bara la Afrika katika masuala ya maendeleo inayofanyika jijini Dar es Salaam



Washiriki wa Tanzania katika Semina ya siku tatu ya Ngazi ya Juu kuhusu Afrika tunayoitaka inayojadili fursa na changamoto mbalimbali zinazolikabili bara la Afrika katika masuala ya maendeleo inayofanyika jijini Dar es Salaam wakifuatilia ufunguzi wa Semina hiyo.

Washiriki wa Semina ya siku tatu ya Ngazi ya Juu kuhusu Afrika tunayoitaka inayojadili fursa na changamoto mbalimbali zinazolikabili bara la Afrika katika masuala ya maendeleo inayofanyika jijini Dar es Salaam katika picha ya pamoja baada ya ufunguzi wa Semina hiyo.






















Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Said Mussa Shaib amefungua Semina ya Ngazi ya Juu kuhusu Afrika tunayoitaka inayojadili fursa na changamoto mbalimbali zinazolikabili bara la Afrika katika masuala ya maendeleo.

Akifungua semina hiyo Balozi Said amesema Tanzania imejidhatiti kutekeleza Ajenda 2063 na Ajenda 2030 kwakuwa imeziweka katika mipango ya maendeleo ya kitaifa na kufanya ajenda hizo kutekelezwa kwa vitendo kupitia mipango ya maendeleo.


“Bara la Afrika bado linakabiliwa na changamoto mbalimbali zikiwemo umasikini, ukosefu wa maendeleo, ajira, amani na usalama, kutokuwa na sauti moja katika majukwaa ya kimataifa, nchi za Afrika lazima ziendelee kupambana ili kuhakikisha Afrika inayotakiwa inafikiwa” alisema Balozi Said Mussa Shaib.


Amesema Tanzania imepiga hatua katika kutekeleza malengo ya Ajenda ya Umoja wa Afrika ya mwaka 2063 na Malengo ya Maendeleo Endelevu ya Umoja wa Mataifa ya mwaka 2030 na hivyo kuendelea kuimarika kwa kiwango cha ukuaji ambacho alisema kuwa kinatarajiwa kuendelea kukua kwa zaidi ya asilimia 5 kwa mwaka 2024 na kuendelea.


Amesema Kiwango hicho cha ukuaji kimechochewa na utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati ya miundombinu na uwekezaji inayotekelezwa na Serikali katika sekta mbalimbali. Ametaja miradi hiyo kuwa ni pamoja na ujenzi wa Reli ya Kisasa ya SGR, Barabara, Bwawa la kuzalisha Umeme la Mwalimu Nyerere pamoja na urekebishaji wa miundombinu ya bandari na viwanja vya ndege nchini.


Amesema Tanzania imeendelea kuwekeza kwa kiasi kikubwa katika kilimo ili kuongeza uzalishaji wa chakula na kutokomeza njaa nchini na kuongeza kuwa hatua kadhaa zimechukuliwa kuimarisha upatikanaji na usawa katika Elimu na Mafunzo ya Ufundi na Ufundi (TVET) na elimu ya juu.


Amesema Tanzania pia imefanikiwa kupunguza viwango vya vifo vya mama na watoto wachanga na watoto walio chini ya umri wa miaka mitano huku ikiendelea kufurahia amani na utulivu kwa kuboresha demokrasia, utawala bora, haki za binadamu na kuzingatia utawala wa sheria.


“Mbali na mafanikio niliyoyaeleza, bado nchi wanachama zinakabiliwa na changamoto mbalimbali katika kutekeleza Ajenda ya Umoja wa Afrika ya mwaka 2063 na Ajenda ya Umoja wa Mataifa ya mwaka 2030 na hivyo taarifa za tathmini katika nchi mbalimbali zinaonyesha utendaji wa jumla uko katika kiwango cha wastani” alisema Balozi Mussa.


Ametaja baadhi ya sababu zinazochangia utekelezaji wa ajenda hizo kuwa wa kiwango cha wastani kuwa ni pamoja na utawala dhaifu, mifumo mibovu ya usimamizi na uratibu kati ya wahusika wa maendeleo wa ndani na nje katika ngazi ya nchi, pamoja na rasilimali zisizotosha.


Ameishukuru Ofisi ya Umoja wa Mataifa Tanzania kwa kuendelea kushirikiana na Tanzania katika kuhakikisha utekelezaji wa Malengo ya Milenia yanaendelea kufanyiwa kazi na kuahidi kuwa Tanzania itaendelea kufanya kazi kwa karibu na Ofisi hiyo ili kufikia malengo hayo kwa ukamilifu.

Semina hiyo imeandaliwa na Kamisheni ya Umoja wa Afrika kwa kushirikiana na Kamisheni ya Umoja wa Mataifa ya Uchumi Barani Afrika (UNECA) inajadili utekelezaji wa Agenda 2063 na Agenda 2030 katika ngazi ya Nchi na Mpango wa utekelezaji wa Miaka 10 wa Ajenda 2063 ambao utatoa ramani ya mabadiliko ya Bara la Afrika ndani ya muongo mmoja kama ulivyopitishwa na Mawaziri wa Umoja wa Afrika mwezi Oktoba 2023

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Bi. Jenifa Omolo, akipokea Tuzo kutoka kwa Mhasibu Mkuu Fungu 50 Wizara ya Fedha CPA Nuru Abdallahmed, baada ya Wizara kuwa mshindi wa kwanza na kufanikiwa kupata Tuzo ya Waandaji bora wa hesabu kwa mwaka wa Fedha ulioishia 30 Juni 2022 katika kundi la Wizara na Idara za Serikali zinazojitegemea. Tuzo hizo zimetolewa na Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi Tanzania (NBAA), jijini Dar es salaam.


Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Bi. Jenifa Omolo, akionesha tuzo ambayo Wizara imepata baada ya kuwa mshindi wa kwanza na kufanikiwa kupata Tuzo ya Waandaji bora wa hesabu kwa mwaka wa Fedha ulioishia 30 Juni 2022 katika kundi la Wizara na Idara za Serikali zinazojitegemea. Tuzo hizo zimetolewa na Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi Tanzania (NBAA), jijini Dar es salaa

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Bi. Jenifa Omolo, akiwa katika picha ya Pamoja na na Timu ya uandaaji wa Hesabu za mwisho (Final Account), baada ya Wizara kuwa mshindi wa kwanza na kufanikiwa kupata Tuzo ya Waandaji bora wa hesabu kwa mwaka wa Fedha ulioishia 30 Juni 2022 katika kundi la Wizara na Idara za Serikali zinazojitegemea. Tuzo hizo zimetolewa na Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi Tanzania (NBAA), jijini Dar es salaam.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Bi. Jenifa Omolo, na Timu ya uandaaji wa Hesabu za mwisho (Final Account), wakifurahia tuzo baada ya Wizara kuwa mshindi wa kwanza na kufanikiwa kupata Tuzo ya Waandaji bora wa hesabu kwa mwaka wa Fedha ulioishia 30 Juni 2022 katika kundi la Wizara na Idara za Serikali zinazojitegemea. Tuzo hizo zimetolewa na Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi Tanzania (NBAA), jijini Dar es salaam.

(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF, Dodoma)

WAAJIRI Wakumbushwa kuweka Mazingira wezeshi na Jumuishi kwa watu wenye ulemavu ili kuwepo kwa usawa na usalama mahala pa kazi na kuwavutia wawekezaji.

Akizungumza jijini Dar es Salaam Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Prof. Joyce Ndalichako wakati wa kugawa tuzo ya kutambua mwajiri bora wa mwaka 2023, amesema Serikali inatambua mchango mkubwa unaofanywa na Chama cha Waajiri (ATE) Katika kupigania maslahi ya waajiri wote nchini na kutengeneza mazingira wezeshi na Jumuishi kwa waajiri.

Ndalichako ameongeza kuwa Waziri Mkuu anawapongeza wadau mbalimbali ikiwemo TUCTA kwa kufanya kazi pamoja ili kuongeza tija kwenye serikali yetu. Kipekee nampongeza mshauri elekezi aliyekamilisha mchakato wote wa kuwapata washindani waliopata tuzo siku ya leo.

"Nawapongeza sana Washiriki wote na kama wahenga walisema asiyekubali kushindwa sio mshindani, na mchakato ulionesha Ushindani wa hali ya Juu na ninawapongeza sana ATE kwa kuratibisha mchakato huu." Amesema Ndalichako

Aidha amesisitiza kuwa tuzo hizo zitawasukuma zaidi hata wale ambao hawaja pokea tuzo ili kipindi kijacho waweze kushiriki kushindania na hata wale ambao wameibuka washindi waendelea kufanya kazi kwa bidii ili kuonesha walistahili kupokea tuzo hizo.

"Nawapongeza Sana ndugu waajiri kwa kufanya kazi na Serikali ili kuhakikisha sehemu zote za kazi ziko salama na kuhakikisha Usalama mahali pa kazi halina budi kutiliwa mkazo na kupewa kipaumbele kwanza."

Moja ya vipengele vilivyozingatiwa ni vile vinayotambua mahitaji ya watu wanaoishi na Ulemavu mahali pa kazi. Hivyo waajiri wote wanapaswa kuwajumuisha katika waajiriwa 20 basi 3% wawe watu wanaoishi na Ulemavu.

Kwa Uapnde wa Mkurugenzi wa Chama cha Waajiri (ATE) Suzanne Ndomba amesema tuzo ya Mwajiri Bora kwa Mwaka huu ina na vipengele 14 ambavyo vimejikita katika maeneo mbalimbali ambayo yamelenga kuongeza chachu kwa waajiri ili kuongeza tija na ushindani.

"Naomba pia nitumie fursa hii kuipongeza Serikali kwa kuendelea kuboresha mazingira ya kufanya biashara nchini ni ombi letu kwamba juhudi hizi ziendelee kwa kuendelea kuboresha mazingira ya kufanya biashara nchini."

Aidha ameiomba Serikali kupitia Sheria zao ili ziandane na wakati, kuendelea kupunguza tozo mbalimbali ambazo zinaongeza gharama ya kufanya biashara ili kuendelea kuwavutia wawekezaji wengi kutoka ndani na nje ya nchi kwa ustawi wa uchumi wa nchi yetu.

"ATE kama sehemu ya Wajumbe wa Baraza la Ushauri la Taifa kwa Watu Wenye Ulemavu nchini, tumeendelea pia kutambua umuhimu wa kujenga mazingira yanayojali mchango wa watu wote hususani wenye ulemavu."

Pia ndomba ameeleza kuwa tuzo hizo, zimeendelea kutambua mwajiri anayezingatia umuhimu wa kuwa na mazingira wezeshi kwa Wenye Ulemavu ili kuhamasisha waajiri kuweka mazingira yenye staha na rafiki yanayowawezesha watu wenye ulemavu kufanya kazi na kuchangia katika maendeleo ya nchi yetu.

Aidha Kampuni mbalimbali zimeibuka ikiwemo Mshindi katika Kipengele cha Usawa wa Kijinsia na usawa katika Maeneo ya kazi imeibuka mshindi Benki ya NMB,wakati Mshindi wa kipengele cha Makampuni yanayokabiliana na majanga yanayotokea imeibukq ushindi kampuni ya Barrick gold mine, Mshindi wa Kipengele cha Mabadiliko ya tabia ya nchi imeibuka WWF, Mshindi katika Kipengele uwajibikaji katika Mwenendo biashara na utendaji unaokidhi imeibuka na ushindi Benki ya CRDB, Mshindi wa Kipengele cha Maudhui ya Ndani imeibuka ushindi benki ya Stanbic.
Picha ya tuzo za vipengele mbalimbali zilizoshindaniwa kwa Makampuni zilizoandaliwa na Chama cha Waajiri nchini (ATE) zilizofanyika leo Disemba 04,2023 Mlimani City Jijini Dar es Salaam
Waziri wa Nchi,Ofisi ya Waziri Mkuu, Vijana,Ajira na Wenye Ulemavu, Prof. Joyce Ndalichako akizungumza wakati wa Kugawa tuzo ya kutambua mwajiri bora wa mwaka 2023 tuzo zilizoandaliwa na Chama cha Waajiri  (ATE) Mlimani City Jijini Dar es Salaam akisisitiza zaidi Waajiri kueka mazingira wezeshi na Jumuishi kwa watu wenye Ulemavu nchini
Mkurugenzi wa Chama cha Waajiri (ATE) Suzanne Ndomba akiongea machache wakati akikaribisha wadau mbalimbali waliohudhuria hafla ya ugawaji tuzo za mwajiri bora wa mwaka 2023 zilizofanyika Leo Disemba 04,2023 Mlimani City Jijini Dar es Salaam
Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Theopista Mallya akiwa na Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi SACP Mkisi, ambaye aliwahi kuwa Mkuu wa Shule ya Polisi Moshi (CCP) ambaye kwa sasa amestaafu utumishi kwa mujibu wa sheria.

Kamanda Mallya alifika nyumbani kwa Mstaafu huyo Kata ya Igamba wilayani Mbozi kwa lengo la kumjulia hali ikiwa pamoja na kujadili mambo mbalimbali ikiwemo usalama.





Top News