Na Mwandishi Wetu
WAFANYAKAZI 20 wa hoteli ya Lark iliyopo ndani ya jengo la Noble Centre Dar es Salaam, linalomolokiwa na CRJE wamezuiwa kuingia ndani ya hoteli hiyo kutokana na kile kinachoelezwa kuwa ni mgogoro wa kimkataba baina ya mwekezaji wa hoteli hiyo na wamiliki wa jengo.

Hatua hiyo imezua taharuki na vilio miongoni mwa wafanyakazi hao,huku wakilalamika kunyimwa haki zao bila taarifa rasmi kutoka kwa muajiri wao.

Mfanyakazi na kiongozi wa wafanyakazi wa hoteli hiyo, Irene Mushi amesema walifika kazini kama kawaida asubuhi wakiwa katika sare zao za kazi, lakini walishangazwa na hatua ya kuzuiwa kuingia ndani na walinzi wa jengo.

“Sisi tunatofautiana kuingia kazini wapo wa mchana na wengine usiku, lakini jana tulianza kuona dalili mbaya za milango ya baadhi ya sehemu kama vile vyumba vya wafanyakazi na vile vya kubadilishia nguo vimefungwa kwa kufuli. Mwezetu aliyeingia usiku alizuiwa kuingia jana jioni bila sababu. Tulipojaribu kuwasiliana na uongozi wa juu, hatukupata majibu ya kueleweka,” amesema Irene.

Irene na wenzake wanadai hatua hiyo ya kuzuia wafanyakazi si ya kisheria na inaleta picha ya dhuluma kwa Watanzania ndani ya nchi yao.

“Muajiri wetu hajatuambia tusije kazini. Hawa wanaotufungia milango siyo waajiri wetu. Kama wana mgogoro, waumizane wao bila kutuingiza. Tunachohitaji ni Serikali itusikie. Hatuna mahali pengine pa kwenda, kazi ndiyo maisha yetu, tunawatoto na familia zetu,” amesema Irene

Wakili wa hoteli hiyo, Method Kagoma amefika eneo la tukio na kueleza kuwa hatua ya CRJE kuifungia hoteli hiyo ni kinyume cha sheria, kwani hakuna utaratibu wowote wa kisheria uliokuwa umefuatwa, licha ya madai kwamba mkataba wa upangaji umeisha.

“Jumamosi mmiliki wa jengo aliandika barua kwa mmiliki wa hoteli kumtaka aondoke ndani ya siku tatu, bila kufuata mkataba wala taratibu za kisheria. Jana wafanyakazi walizuiwa, leo wamefungiwa milango vifaa viko ndani, hakuna taarifa rasmi kutoka kwa CRJE wala agizo la Mahakama,” amesema Wakili Kagoma.

Kagoma amsema tayari wamefungua kesi katika Mahakama Kuu Divisheni ya Biashara wakilalamikia kuvunjwa kwa makubaliano ya kibiashara kinyume cha utaratibu.
“Kwa sasa tumefungua kesi rasmi na tunaendelea kufuatilia hatua za mbele. Tanzania ni nchi ya sheria, na kama CRJE walikuwa na madai yao, walipaswa kwenda Mahakamani au kuomba msaada wa Serikali, si kujichukulia sheria mikononi,” amesema.

Kwa mujibu wa Kagoma, shughuli za hoteli hiyo zilianza kuyumba mwishoni mwa mwezi Aprili baada ya CRJE kukata umeme kwenye jengo, hali iliyosababisha kupungua kwa wateja.

“Wateja hawakuweza kukaa ghorofani kwa sababu ya kukosa umeme. Hii ni hasara kwa mmiliki na wafanyakazi. Wengine bado wana mikataba mipya, lakini hawajui hatma yao,” amesema.

Wafanyakazi wanatoa wito kwa Serikali kuingilia kati mgogoro huo kwa kuwa unawadhulumu watumishi wasiohusika moja kwa moja katika mvutano wa kibiashara.

“Tunaomba Serikali ituangalie kwa jicho la huruma. Hatujafukuzwa kazi na bosi wetu, lakini hatuwezi kufanya kazi,” alisema Ester Besta.

Jitihada za kumtafuta mmiliki wa jengo hilo hazikuzaa matunda kutokana na simu yake kutopokelewa.
Na Khadija Kalili, Michuzi TV
MKURUGENZI wa Rasilimali Watu na Mafunzo ya Wizara ya Afya Dkt. Saitore Laizer aliyekuwa mgeni rasmi katika hafla ya kufunga mafunzo ya wahitimu kutoka Chuo Kikuu Cha MUHAS amesema amefurahishwa na tasnia hiyo kuoata mafunzo kwani katika hali ya hali ya kawaida matabibu na wataalamu wa afya hawafundishwi uongozi.

Ikumbukwe kuwa Chuo Kikuu cha Afya kilichotangulia katika sekta ya afya tunatambua mchango mkubwa wa kuzalisha watalamu wengi , MUHAS kwa wingi wake wamezalisha matabibu, famasia, wauguzi stashahada na astashahada ubingwa na bingwa bobezi, na kama taifa tumejiwekea malengo ya kupunguza kwa kiwango kikubwa cha wagonjwa wa Tanzania kwenda kutibiwa nje ya nchi.

Katika uuguzi na taaluma magonjwa mengi ambayo wagonjwa wengi walikua wakienda kutibiwa nje ya nchi hivi sasa wanatibiwa nchini kutokana na Chuo kikuu cha sayansi shirikishi Muhimbili MUHAS kuzalisha wataalamu wa afya wa magonjwa hayo hivyo tumeokoa kiasi kikubwa cha fedha za kigeni.

"ikiwamo dola , unapopunguza idadi ya watanzania kwenda kutibiwa nje unapunguza matumizi ya dola, unapoongeza huduma za bingwa bobezi pia huvutia utalii wa kiafya, ndani ya Afrika Mashiki na nje ya Afrika wagonjwa wengi wanakuja kutibiwa kama MOI, KJCI tunapata wagonjwa wengi kutoka nje ya nchi hivyo tunaingiza fedha za kigeni" amesema.

Wataalamu wa nchi yetu wanatumika kwenda nje ya nchi kwenda kuwajengea uwezo madakri wa nchi za jirani, ikikwamo visiwa vya jirani wanakwenda kupeleke huduma kwa majirani sababu magonjwa hayana mipaka, tunaongeza urafiki na masuala ya kujenda diplomasia na nchi za jirani.

Magonjwa yaliyokua yanaongoza kupeleka wagonjwa nje ya nchi hasa ni moyo, mishipa ya damu, mishipa ya fahamu pamoja na ubongo yameengoza kuvutia wagonjwa kutoka nje ya nchi kuja kutibiwa hapa nchini.

Wahitimu wa mafunzo ya uongozi kutoka Chuo Kikuu Cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS ), wamehitimu mafunzo hayo huku wakitoa wito kwa taasisi mbalimbali kupeleka wataalamu wao ili kupata elimu hiyo.

Akizungumza kuhusu mafunzo hayo Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili MUHAS Prof. Appolinary Kamuhabwa amsema kuwa katika mafunzo hayo ya siku tatu wamefundishwa katika maeneo mbalimbali ya uongozi ambayo yatakwenda kutusaidia katika utendaji wetu wa kazi.
KUELEKEA Kilele cha maadhimisho ya Wiki ya Maziwa mwaka huu, Bodi ya Maziwa nchini imeendelea kutoa wito kwa wananchi kuongeza unywaji wa maziwa, hasa yale yaliyosindikwa, ili kuboresha afya, lishe bora na kuunga mkono sekta ya maziwa nchini.

Akizungumza na waandishi wahabari leo Mei20,2025 katika mafunzo yaliyotolewa jijini Dar es salaam, Kaimu Msajili Bodi ya maziwa Tanzania Deorinidei Mng’ong’o amesema maziwa yaliyosindikwa ni salama kwa matumizi ya binadamu, yanadumu kwa muda mrefu na yana viwango bora vya usafi na virutubisho, hivyo kuwa chaguo bora kwa jamii zote, mijini na vijijini.

“Tunapoelekea kilele cha Wiki ya Maziwa, tunawakumbusha wananchi kuwa kuchagua maziwa yaliyosindikwa si tu ni njia ya kulinda afya zao, bali pia ni kuunga mkono juhudi za wakulima na viwanda vya maziwa nchini,” alisema Kaimu Msajili wa Bodi hiyo.

Maadhimisho ya Wiki ya Maziwa huadhimishwa kila mwaka kwa lengo la kuelimisha umma kuhusu umuhimu wa maziwa katika lishe, kuhamasisha matumizi yake, na kutoa fursa kwa wadau wa sekta hiyo kuonesha mafanikio na changamoto zinazowakabili.

Maadhimisho ya mwaka huu yanatarajiwa kufanyika mkoani Morogoro kuanzia mei 27 hadi juni mosi mwaka huu.

Bodi ya Maziwa imeandaa shughuli mbalimbali zitakazofanyika kuelekea na wakati wa kilele cha wiki hiyo, zikiwemo maonesho ya bidhaa za maziwa, midahalo ya kitaaluma, na kampeni za uelimishaji mashuleni na katika jamii kwa ujumla.









KWA mara nyingine tena, Meridianbet imeonesha kuwa iko pamoja na jamii – si kwa maneno tu, bali kwa vitendo. Leo hii, timu ya Meridianbet imefika katika maeneo ya Makumbusho na Mwananyamala, kwa lengo la kuwagusa wale ambao kwa namna moja au nyingine wanapitia changamoto za maisha.

Katika moyo wa upendo na mshikamano wa kijamii, Meridianbet imewafikia familia zenye uhitaji na wajane, ikiwa ni sehemu ya dhamira yao ya dhati ya kurudisha kwa jamii – utamaduni ambao kampuni hii imeendelea kuuenzi kila siku.

Kwa tabasamu na machozi ya furaha, wakazi wa maeneo hayo walipokea msaada wa vyakula na bidhaa muhimu za nyumbani ikiwemo:Mchele, Sukari, Mafuta ya kupikia, Sabuni, Unga wa sembe na ngano.

Ni msaada uliokuja kwa wakati muafaka, hasa kwa familia ambazo zimekuwa zikiendelea kupambana na hali ngumu ya kiuchumi. Kila kifurushi kilichotolewa kilikuwa ni zaidi ya msaada, kilikuwa ni ishara ya matumaini, upendo na mshikamano.

"Jamii ndiyo msingi wa kila mafanikio tunayoyapata. Leo tumefika hapa sio kwa sababu tuna mengi, bali kwa sababu tuna moyo wa kugawana na wale wanaohitaji zaidi," alisema mmoja wa wawakilishi wa Meridianbet aliyeongozana na timu katika tukio hilo.

Kwa miaka kadhaa sasa, Meridianbet imeendelea kuonesha kuwa kamari si tu burudani, bali pia ni chombo cha kuleta mabadiliko chanya katika maisha ya watu. Kupitia miradi mbalimbali ya Uwajibikaji kwa Jamii (CSR), Meridianbet imeweza kufanikisha misaada kwenye sekta za elimu, afya, michezo na sasa chakula kwa familia zenye uhitaji.

Kwa hakika, leo Makumbusho na Mwananyamala wameandika historia mpya ya upendo – historia ambayo itaendelea kuishi mioyoni mwa walioguswa.

Meridianbet – Daima na Jamii.

NB: Jisajili na Meridianbet na cheza michezo ya kasino ya mtandaoni upate ushindi kirahisi, Pia ongeza maokoto yako kwa kubashiri michezo mbalimbali yenye ODDS KUBWA. PIGA *149*10# AU tembelea tovuti yao meridianbet.co.tz

Farida Mangube, Morogoro

Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Mussa Kilakala, ametoa wito kwa wananchi na taasisi zote kuhakikisha wanazingatia ubora wa vipimo katika shughuli zao za kila siku, akisisitiza kuwa vipimo visivyo sahihi vinaweza kuathiri afya, usalama, haki katika biashara, na maendeleo ya taifa kwa ujumla.

DC Kilakala alitoa kauli hiyo Mei 20, kwenye Maadhimisho ya Siku ya Vipimo Duniani yaliyofanyika kitaifa mkoani Morogoro, ambapo amsema vipimo sahihi ni msingi wa maendeleo ya kiuchumi, kijamii na kisayansi. 

“Tunapoadhimisha Siku ya Vipimo Duniani, ni wajibu wetu kuhakikisha vipimo vinavyotumika katika shughuli zetu za kila siku vinakidhi viwango vya kimataifa.”

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Dkt. Ashura Katunzi, amesema kuwa uhakiki wa usahihi wa vipimo katika sekta kama viwanda, afya, ujenzi, na usafiri wa anga ni hatua muhimu ya kuhakikisha bidhaa na huduma zinazotolewa zina ubora unaostahili na zinawalinda watumiaji.

“Vipimo vikihakikiwa kwa usahihi wake vitaleta manufaa makubwa kwa jamii,” alisema Dkt. Katunzi. 

“Vitawezesha utoaji wa huduma bora na bidhaa zenye ubora katika sekta kama afya, mawasiliano, chakula, na nyingine nyingi.”

Aidha, amesema Tanzania, kupitia maabara ya TBS, imekuwa nchi ya kwanza katika Ukanda wa Afrika Mashariki kupata ithibati ya kimataifa katika vipimo vya torque, barometa na unyevu — hatua inayoiwezesha kutoa huduma za ulinganifu wa vipimo kwa kiwango cha kimataifa.

Katika maadhimisho hayo TBS imewakutanisha wadau kutoka sekta mbalimbali za umma na binafsi ambapo Kaulimbiu ya mwaka huu ni “Vipimo kwa Nyakati Zote na kwa Watu Wote”, ikisisitiza umuhimu wa vipimo sahihi katika kuchangia maendeleo endelevu na ustawi wa jamii katika nyanja zote za maisha.





 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Namibia Mhe. Netumbo Nandi-Ndaitwah mara baada ya kuwasili Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 20 Mei, 2025.







Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimkaribisha mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Namibia Mhe. Netumbo Nandi-Ndaitwah mara baada ya kuwasili Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 20 Mei, 2025.

Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) kwa kushirikiana na Agha Khan Foundation, Tanzania leo tarehe 20/05/2025 wamepanda miti zaidi ya 200 katika zoezi la kulinda mazingira kwa kuanzisha msitu bustani.

Zoezi hilo ni katika kuelekea Maadhimisho ya Miaka 50 ya TET yanayotarajia kufanyika Juni mwaka huu, limefanyika katika Makao Makuu ya TET, jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mkuu wa TET, Dkt. Aneth Komba ameishukuru Agha Khan Foundation kwa hatua hiyo kwani wanatekeleza kwa vitendo utunzaji wa mazingira na kulinda mabadiliko ya tabianchi.

"TET katika kusheherekea Miaka 50 inaendeleza utunzaji wa mazingira kwa vitendo kwani hata katika maboresho ya mitaala ya kielimu tumezingatia utunzaji mazingira.

"Maboresho ya mitaala ya mwaka 2023 yameweka somo la jiografia kuwa ni somo la lazima na katika somo hilo tumewezesha wanafunzi kuhimili na kutunza mazingira," amesema.

Kwa upande wake Mkuu wa Programu wa Agha Khan Foundation Tanzania, Bi. Carolyn Mlewa amesema wamepanda miti hiyo zaidi ya 200 yenye aina 25 tofauti ikiwemo ya kivuli, matunda, dawa, na miti pori kama ishara ya kulinda mazingira.

"Hii ni katika kuendeleza ushirikiano wetu na TET katika uhimilivu wa tabianchi, ni mabadiliko ya tabia na namna ya kulinda hali hiyo, hivyo kupanda miti hiyo ambayo itakuwa na umuhimu mkubwa katika kulinda mazingira," amesema Bi. Mlewa.

Naye Msimamizi wa Mradi wa Mazingira wa taasisi hiyo, Japhet Wangwe amesema amesema upandaji msitu huo mdogo ni moja ya hatua ya kuboresha mazingira lakini pia kuhifadhi viumbe vya asili na vya Kiikolojia.




GEITA MJINI: KATIBU wa Halmashauri Kuu (NEC), Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Amos Makalla amesema serikali imeazimia kuwainua wachimbaji wadogo wa madini lengo ni kuhakikisha uchumi wa wachimbaji wote unakuwa kwa pamoja.

Makalla ameeleza hayo  leo Mei 20 wakati akizungimza na wananchi wa Geita Mjini mkoani Geita, ikiwa ni muendelezo wa ziara yake ya siku saba katika mikoa mitano ya Kanda ya Ziwa ambayo ni Kagera, Geita, Mwanza Simiyu na Shinyanga.

Akifafanua hilo Makalla amesema azma ya serikali ikiongozwa na Rais Samia ni kuwajali wachimbaji wadogo wa madini na ndo maana rais wao na wachimbaji wameendekea kumuunga mkono na jitihada zake kwa sababu ameingia kwenye rekodi ya kuwajali wachimbaji wadogo.

Ameeleza hilo akisisitiza kuwa wachimbaji wakubwa waliopo alianza kama wachimbaji wadogo, hivyo wachimbaji hao wakipewa fursa wataweza kukua na kuajiri watu na kuongeza mapato na azma ya serikali ya CCM ni kuwajali wachimbaji wote kuhakikisha uchumi unakuwa kwa pamoja.

Makalla amewasisitiza wananchi kuwapuuza watu wanaowahadaa wananchi kwa kusema kuwa wachimbaji wadogo wamesahaulika, kwani kuwepo na madini katika eneo hilo kunaonyesha kuna mtu muadilifu anayesimamia rasilimali hizo.








Wakala wa Vipimo Tanzania wamepokea na kusimika mtambo mpya wa kisasa wenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 400, kwa ajili ya kuhakikisha dira za maji. Mtambo huo una uwezo wa kupima hadi dira 1,000 kwa siku, hatua inayolenga kuongeza ufanisi na usahihi katika uhakiki wa mita za maji nchini.

 

Kupitia maadhimisho ya Siku ya Vipimo Duniani, Wakala wa Vipimo wameendesha zoezi la kutoa elimu kwa wananchi pamoja na madereva wa malori katika kituo chao kilichopo Misugusugu, Kibaha mkoani Pwani. Elimu hiyo ililenga kuwaeleza wananchi umuhimu wa uhakiki wa dira za maji pamoja na faida zake katika matumizi ya kila siku ya maji majumbani na kwenye taasisi mbalimbali.

 

Akizungumza katika zoezi hilo, Mkurugenzi wa Huduma Saidizi wa Wakala wa Vipimo, Bw. Karim Mkorehe, alitoa shukrani kwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuwapatia mtambo huo mpya wenye uwezo mkubwa wa kuhakiki dira za maji.

 

Kwa upande wake, Kaimu Meneja wa Wakala wa Vipimo katika Kituo cha Misugusugu, Bw. Gaudence Gaspary, alisema kuwa elimu hiyo imetolewa kwa makundi mbalimbali ya wananchi, wakiwemo madereva wanaopata huduma katika kituo hicho. Alifafanua kuwa dira ya maji inapaswa kuhakikiwa angalau mara moja kwa mwaka ili kuhakikisha usahihi wa gharama za matumizi ya maji.

 

Aidha, baadhi ya wananchi waliopatiwa elimu hiyo walieleza kufurahishwa na mafunzo hayo huku wakikiri kuwa wengi wao hawakuwa na uelewa juu ya uwepo wa huduma za uhakiki wa mita za maji.







Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, akiwa kwenye kituo cha uandikishaji wapiga kura kilichopo katika Ofisi ya Mtendaji wa Kata ya Kilimani, Mtaa wa Kilimani, jijini Dodoma, kwa ajili ya kuboresha taarifa zake kwenye Daftari la Kudumu la Mpiga Kura, leo tarehe 20 Mei, 2025.





Top News