

Wasajili wa Chanjo na Wakurugenzi wanaosimamia uzalishaji wa chanjo za mifugo kutoka nchi 25 za ukanda wa Afrika wamekutana nchini Tanzania kujadili namna ya kuwa na mfumo wa pamoja wa kutokomeza ugonjwa wa sotoka ya mbuzi na kondoo. Mkutano huu umeanza tarehe 16 hadi 20 Juni 2025 katika Ukumbi wa King Jada Hotel uliopo jijini Dar es Salaam.
Akifunga mkutano huo tarehe 17 Juni 2025, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe, alisema kuwa mkutano huo umekuja kwa wakati muafaka kwani siku ya jana, tarehe 16 Juni 2025, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, alizindua rasmi kampeni ya chanjo za mifugo kitaifa, na ameidhinisha fedha kwa ajili ya kuchanja ng’ombe, mbuzi, kondoo na kuku, sambamba na kuwawekea utambuzi.
“Kikao hiki kina lengo la kuandaa mwongozo ambao utatumika na wazalishaji wa chanjo katika nchi hizo 25, hasa katika kupambana na sotoka ya mbuzi na kondoo. Pia wanakusudia kuanzisha mtandao wa mawasiliano baina yao kwa lengo la kuendelea kupata chanjo bora kwa mifugo ya Afrika.”
“Kitu kitakachotengenezwa Tanzania hakitapishana na kile kinachotoka Kenya, Zambia au nchi nyingine yoyote barani Afrika. Ndiyo maana wote wamekusanyika hapa kuridhia mfumo wa pamoja. Chanjo itakayouzwa Tanzania itauzwa sehemu yoyote Afrika bila vikwazo.” Alisema Prof. Shemdoe
Mkurugenzi wa AU-PANVAC, Dkt. Bodjo S. Charles, alisema kuwa mkutano huu unalenga kuweka viwango vya pamoja na mwongozo utakaosaidia kufanya ukaguzi na kuthibitisha ubora wa uzalishaji wa chanjo, jambo ambalo litahakikisha kuwa vifaa vyote vya uzalishaji vinazalisha chanjo bora. Baada ya hapo, kutakuwa na mtandao wa wadhibiti wa sekta hii ambao watakuwa wakibadilishana taarifa kati yao.
Naye Meneja wa Taasisi ya Chanjo Tanzania (TVLA), Dkt. Charles Ngassa, alisema kuwa mkutano huu umewakutanisha mamlaka zinazohusika na usajili wa chanjo pamoja na wakurugenzi wanaozalisha vya chanjo barani Afrika, kwa lengo la kupata mwongozo wa usajili wa chanjo ya sotoka ya mbuzi na kondoo.
“Chanjo hiyo ni muhimu sana kwa kutokomeza ugonjwa huo duniani ifikapo mwaka 2030. Kama bara, tunahitaji kuwa na mwongozo mmoja ili kupata chanjo bora kwa mifugo wetu.” Alisema DKt. Mayenga













Akizungumza katika maadhimisho hayo jijini Dodoma June 16,2025 Mkurugenzi mkuu wa EWURA, Dkt.James Andilile amesema EWURA itaendelea kujielekeza katika kuwahudumia wananchi kwa ufanisi na kuzingatia maadili ya utumishi wa umma, kwa kuhakikisha kuwa huduma zote za nishati na maji zinafikia walengwa kwa ubora unaostahili.
"Huduma kwa wananchi siyo fadhila, ni haki yao ya msingi,kama Taasisi ya Serikali, tunatambua wajibu wetu kwa Watanzania na ndiyo maana tunaendelea kujipanga kutoa huduma bora kwa kutumia mifumo ya kidijitali na kuimarisha usimamizi katika sekta tunazozihudumia," amesema .
Ameongeza kuwa katika kipindi cha wiki ya utumishi wa umma, EWURA imekuwa ikikutana moja kwa moja na wananchi ili kusikiliza changamoto, kutoa elimu kuhusu haki na wajibu wao, na kueleza namna taasisi hiyo inavyosimamia bei, ubora, na upatikanaji wa huduma za mafuta, umeme, gesi asilia, na maji safi na usafi wa mazingira.
Aidha, amesema EWURA inatambua kwamba huduma bora kwa umma ni chachu ya ustawi wa jamii na uchumi wa nchi, hivyo itaendelea kusimamia misingi ya utawala bora ikiwemo uwazi, uwajibikaji na kushirikisha wananchi katika maamuzi.
Katika hatua nyingine, Dkt.Andilile ametoa wito kwa jamii kuhakikisha wanatumia wiki ya utumishi kama jukwaa la kupata taarifa mbalimbali za EWURA na kueleza kuwa hali hiyo itaboresha mifumo ya utoaji huduma na kujifunza kutoka kwa wadau na wananchi.
Pamoja mambo mengine kiongozi huyo amesisitiza kuwa EWURA iko tayari kuwachukulia hatua kali wafanyabiashara wa vituo vya mafuta ya Taa, petroli au dizeli watakao fanya bishara kea kuchakachuo bidhaa hizo.
Pia wafanya bishara hao wametakiwa kuzingatia bei elekezi kwa kumuuzia mafuta mteja kadri ya mahitaji yake na si vinginevyo.
Wiki ya Utumishi wa Umma huadhimishwa kila mwaka kwa lengo la kuhamasisha uwajibikaji, maadili ya kazi, pamoja na kutoa nafasi kwa taasisi za umma kusikiliza na kutatua changamoto zinazowakabili wananchi katika upatikanaji wa huduma.




-Inahudumia kaya 2,463 katika vijiji 8.
Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Mhe. Balozi Meja Jenerali Mstaafu Jacob Kingu ameihakikishia ushirikiano kampuni ya kuzalisha na kusambaza umeme ya Matembwe Village Company Limited ya Mkoani Njombe ili kuiwezesha kuongeza upatikanaji wa umeme na kuwafikia wananchi wengi zaidi waishio maeneo hayo.
Amethibitisha hayo alipofanya ziara katika mradi wa kuzalisha na kusambaza umeme wa Matembwe uliopo katika Tarafa ya Lupembe Wilaya ya Njombe Mkoani Njombe Juni 17, 2025.
"Nimekagua mradi mzima kuanzia eneo la uzalishaji na nimetembelea baadhi ya wanufaika wa mradi ili kujionea uendeshaji wake, uwezo wake na namna ambavyo mradi huu unanufaisha wananchi katika kujiletea maendeleo," alifafanua Mhe. Balozi Kingu.
Alisema ameridhishwa na namna ambavyo mradi huo wa Matembwe unavyofanya kazi na alisisitiza kuwa ipo haja ya kuongeza uzalishaji hasa ikizingatiwa kuwa maji yapo yakutosha.
Aliuthibitishia uongozi wa mradi kuwa Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) itaendelea kutoa ushirikiano wa kuhakikisha uwezeshwaji unaendelea ili kuleta tija inayokusudiwa.
"Kazi iliyofanyika hapa ni kubwa na inaridhisha, ni wakati wenu sasa kujipanga vizuri kuongeza uwezo wa uzalishaji wa umeme katika mradi huu ili walau mtoke kwenye kiwango mnachozalisha sasa cha kilowati 550 muweze kuzalisha umeme mwingi zaidi ili kuinua shughuli za kiuchumi na kijamii kwa wananchi wa maeneo haya na nchi nzima kwa ujumla ," alielekeza Mhe. Balozi Kingu.
Aliwasisitiza kuendelea kutunza mazingira ili kuwezesha miradi hii kuwa endelevu sambamba na kuwajengea uwezo vijana wa vijiji vinavyonufaika na mradi kwenye usimamizi na uendeshaji wa mradi.
"Vijana wanapaswa kutambua huu mradi ni wao; walianzisha babu zao na sasa wao wenyewe wananufaika," alisema.
Akizungumza hali ya uzalishaji na usambazaji umeme, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Matembwe, Johannes Kamonga alisema uhitaji wa umeme ni mkubwa hasa kipindi hiki ambacho viwanda vingi vinajengwa.
Aliipongeza REA kwa kuendelea kuuwezesha mradi huo na aliomba uwezeshaji uongezeke ili kuwezesha upanuzi wa mradi pamoja na kuunganisha wateja wengi zaidi
Alisema hapo awali mradi ulianza na kilowati 120 lakini kadri muda ulivyokwenda mahitaji yaliongezeka na hivyo walilazimika kutafuta uwezeshwaji ili kuongeza uzalishaji sambamba na kuongeza idadi ya wanufaika.
"Tunaishukuru REA kwani imekuwa bega kwa bega nasi, tulianza na vijiji viwili lakini kwa uwezeshwaji kutoka REA sasa tunahudumia vijiji nane," alisema Kamonga.
Akizungumzia uwezeshwaji wa mradi, Mkurugenzi wa Teknolojia za Nishati Jadidifu na Mbadala kutoka REA, Mhandisi Advera Mwijage alisema REA imechangia takriban shilingi bilioni moja kuuwezesha mradi kuunganisha wateja 357 sawa na 16.18%.
Alisema REA imewezesha kutekelezwa kwa miradi mbalimbali ya kuzalisha na kusambaza umeme vijijini katika maeneo mbalimbali ndani ya mikoa yote Tanzania Bara ili kuwezesha wananchi wengi kufikiwa na huduma bora ya Nishati, kupunguza uzalishaji wa hewa ya ukaa, kuongeza ajira nchini, kuongeza mapato serikalini na kuboresha maisha ya Watanzania waishio maeneo ya vijijini.
Aliongeza kuwa mradi unatumia teknolojia ya kusambaza umeme kwa kutumia nyaya zinazopita ardhini suala ambalo alisema huongeza usalama na kupunguza gharama za matengenezo.
"Kwa sasa REA ipo katika hatua ya kuongeza idadi ya kaya 95 kupitia mkataba wa ruzuku ya nyongeza ya fedha," alifafanua Mha. Mwijage.
Mhandisi Mwijage alifafanua kuwa REA imefadhili miradi ya uzalishaji na usambazaji nishati vijijini inayotekelezwa na taasisi mbalimbali za Serikali na Sekta Binafsi kwa kutoa ruzuku pamoja na kuwezesha mikopo ya masharti nafuu sambamba na kuwajengea uwezo waendelezaji wa miradi husika na miongoni mwa miradi iliyonufaika kwa Mkoa wa Njombe ni mradi huo wa Matembwe
Mradi wa kuzalisha na kusambaza umeme wa Matembwe unaendeshwa na kusimamiwa na Kampuni ya Matembwe Village Company Ltd iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Njombe kwa kushirikiana na Serikali za Vijiji vya Matembwe, Yembela na Ikondo.
Hayo yamebainishwa Juni 17, 2025 na Mkuu wa Kitengo cha Ushirikishwaji wa Wazawa na Uhusishwaji wa Wadau kutoka PURA, Bw. Charles Nyangi wakati wa Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea Jijini Dodoma.
“Sheria ya Petroli ya Mwaka 2015 imeipa PURA jukumu la kumshauri waziri mwenye dhamana ya masuala ya petroli katika maeneo mbalimbali ikiwemo kunadi vitalu vya utafutaji wa mafuta na gesi asilia”
"PURA imeendelea kutekeleza jukumu hili la msingi linalolenga kuvutia uwekezaji katika shughuli za utafutaji wa mafuta na gesi asilia nchini” alieleza Bw. Nyangi.
Bw. Nyangi aliongeza kuwa kupitia uwekezaji huo, shughuli za utafutaji wa mafuta na gesi asilia zitaongezeka hivyo kupelekea ugunduzi wa mafuta au ugunduzi zaidi wa gesi asilia hivyo kuwezesha nchi kuwa na gesi asilia ya kutosha kwa matumizi mbalimbali.
Akizungumzia uzalishaji wa gesi asilia, Bw. Nyangi alieleza kuwa PURA imeendelea kusimamia na kudhibiti shughuli za uzalishaji wa gesi asilia kutoka katika kitalu cha Mnazi Bay kilichopo Mkoani Mtwara na Songo Songo kilichopo Mkoani Lindi.
Kupita udhibiti, PURA imewezesha kuchukuliwa kwa hatua mbalimbali zinazolenga kuhakikisha uzalishaji endelevu wa gesi asilia.
Miongoni mwa hatua hizo ni pamoja na kuwataka waendeshaji wa vitalu hivyo kufanya ukarabati wa visima kwa wakati, kuchimba visima vipya vya uzalishaji na kufanya ukaguzi wa mara kwa mara wa miundombinu ya uzalishaji wa gesi asilia.
Katika suala la uchimbaji wa visima, Bw. Nyangi alibainisha kuwa kupitia ushauri wa PURA, Kampuni ya Maurel et Prom Tanzania ambaye ni Mwendeshaji wa Kitalu cha Mnazi Bay ipo katika maandalizi ya kuchoronga visima vitatu.
Visima hivyo vitaongeza uzalishaji wa gesi asilia kwa zaidi ya futi za ujazo milioni 30 kwa siku.
PURA pia imeendelea kusimamia kuhusu maandalizi ya uchorongaji wa visima vya gesi asilia katika Eneo la Ugunduzi la Ntorya Mkoani Mtwara mbapo futi za ujazo milioni 60 hadi 140 za gesi asilia zitazalishwa kwa siku.


Na John Mapepele - OR TAMISEMI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt, Samia Suluhu Hassan leo amezindua Hospitali ya Wilaya ya Itilima iliyogharimu shilingi bilioni 4.7 iliyojumuisha ujenzi wa miundombinu na ununuzi wa vifaatiba huku wananchi wakimpongeza.
Mhe. Rais amezindua Hospitali hiyo leo akiwa kwenye siku ya tatu ya ziara yake ya kikazi katika mkoa wa Simiyu ambapo tangu aanze ziara hiyo amekagua na kuzindua miradi mbalimbali ya maendeleo iliyogharimu mabilioni ya fedha huku akifanya mikutano na wananchi.

Akizungumza mara baada ya kuzindua hospitali hiyo, amefafanua kuwa dhamira ya Serikali yake ni kusogeza huduma bora kwa wananchi.
" Nimeridhishwa na miundombinu ya hospitali hii ilivyo ya kisasa na fedha iliyotumika, kimsingi hospitali hii ina kila kitu ambacho kinatakiwa kuwepo kwenye hospitali". Ameongeza Mhe. Rais huku akishangiliwa na wananchi waliofurika kumlaki

Amewaahidi wananchi kuwa Serikali yake itaendelea kuwaletea maendeleo wananchi wake na kuwa kuwaboreshea maisha.
Akimkaribisha Mhe. Rais Samia ili aongee na maelfu ya wananchi katika mkutano wa kuhitimisha ziara kwa siku ya leo Waziri wa Ardhi, nyumba na maendeleo ya Makazi Mhe. Deogratius Ndejembi kwaniaba ya Waziri wa Nchi, TAMISEMI, Mhe Mohamed Mchengerwa amesema TAMISEMI kupitia Idara ya afya ilipewa shilingi trilioni 1.34 kwa ajili ya ujenzi wa hospitali za wilaya na zahanati nchini nzima kwenye Halmashauri zote 184 zikihusisha pia ununuzi wa Vifaa tiba.

Aidha aliongeza kuwa Rais Samia ameongeza bajeti ya ujenzi wa barabara za mijini na vijijini katika Halmashauri ya Wilaya ya Itilima kutoka Shilingi Milioni 800 mwaka 2021 hadi kufikia Bilioni 2.5, suala ambalo limewezesha barabara zote za wilaya hiyo kupitika kwa msimu wote wa mwaka.
Anna Masanja, Mkazi wa Itilima amesema kuwa Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia imefanya maboresho makubwa kwenye kila sekta katika kipindi kifupi cha uongozi wake.
"Kwa kusema ukweli Mama Samia ametuheshimisha wananchi kwa kufanya makubwa kwenye elimu, miundombinu, afya, umeme hata maji" ameongeza Buliga Amos Mkazi wa Meatu.
▪️Aelekeza mabadiliko ya Kanuni ili kuruhusu uhaulishwaji teknolojia kwa Kampuni za Kigeni
▪️Ataka Watanzania kuchangamkia Trilioni 5.3 za usambazaji bidhaa na utoaji huduma
▪️Rais Samia apongezwa kwa uongozi wa maono
▪️Watanzania 19,371 wanufaika na ajira rasmi
▪️Kamati ya Bunge yaipongeza Wizara kwa ukuaji wa sekta
Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde ameitaka Tume ya Madini kuwapa kipaumbele watanzania kwenye usambazaji wa huduma na bidhaa kwenye migodi ya madini ili kujipatia kipato, kuongeza mzunguko wa fedha nchini hivyo Sekta ya Madini kuendelea kuwa na mchango mkubwa kwenye Pato la Taifa.
Mhe. Waziri Mavunde ameyasema hayo mapema leo Juni 17, 2025 jijini Mwanza kwenye ufunguzi wa Jukwaa la Nne la Utekelezaji wa Ushirikishwaji wa Watanzania katika Sekta ya Madini linalokutanisha wadau mbalimbali ikiwa ni pamoja na Wizara ya Madini na Taasisi zake, Taasisi za Serikali, Taasisi Binafsi, Taasisi za Fedha, Kampuni za Uchimbaji wa Madini na Watoa Huduma kwenye Migodi ya Madini.
Amesema kuwa katika kuboresha mazingira ya uwekezaji nchini na kuhakikisha watanzania wananufaika na rasilimali madini, Serikali imeendelea kusimamia ipasavyo Sheria ya Madini, Sura 123 Kifungu Na. 102 na Kanuni za Ushirikishwaji wa Watanzania za Mwaka 2018 ili kuweka usimamizi thabiti katika utekelezaji wa masuala ya Ushirikishwaji wa Watanzania katika Sekta ya Madini nchini.
Amesisitiza kuwa lengo la uwepo wa Kanuni za Ushirikishwaji wa Watanzania katika Sekta ya Madini ni kuhakikisha watanzania wanashiriki ipasavyo kupitia usambazaji wa bidhaa na huduma kwenye migodi ya madini badala ya kampuni kuagiza bidhaa kutoka nje ya nchi.
Aidha Mhe. Mavunde ameitaka Tume ya Madini kufanya mabadiliko ya Kanuni ili kuruhusu uhaulishwaji teknolojia kwa Kampuni za Kigeni ambapo itatoa fursa kwa kampuni za kitanzania kushirikiana na kampuni za kigeni kwenye utoaji wa huduma migodini na kujifunza teknolojia mpya kutoka kampuni za kigeni.
Katika hatua nyingine, Mhe. Mavunde amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa maono yake makubwa ya kuendeleza Sekta ya Madini hali iliyopelekea mabadiliko makubwa ambapo mpaka sasa mafanikio makubwa yamepatikana.
“Mpaka sasa mafanikio makubwa yamepatikana hasa kwa wachimbaji wadogo ambapo wameanza kukopesheka kutoka kwenye Taasisi za Fedha, ushiriki wa watanzania kwenye shughuli za uchimbaji, uchenjuaji, biashara ya madini na utoaji wa bidhaa na huduma kwenye migodi ya madini umeongezeka na mchango wa wachimbaji wadogo kwenye makusanyo ya maduhuli umeendelea kuimarika,” amesisitiza Mhe. Mavunde.
Akielezea mafanikio ya utekelezaji wa kanuni za ushirikishwaji wa watanzania katika Sekta ya Madini, Waziri Mavunde amesema katika kipindi cha mwaka 2023/2024 jumla ya ajira rasmi 19,874 zilizalishwa katika migodi ya madini ambapo ajira 19,371 sawa na asilimia 97 zilitolewa kwa Watanzania na ajira 503 sawa na asilimia 3 zilitolewa kwa wageni.
![]() |
Aidha, amewataka watanzania kuchangamkia fursa za uwekezaji katika Sekta ya Madini hasa kwenye usambazaji wa bidhaa na huduma kwenye migodi ya madini kama vile usambazaji wa vifaa, vyakula na huduma na kuzitaka Taasisi za Kifedha kuendelea kuwakopesha mitaji.
Amesema kuwa kampuni za madini zinatumia kiasi cha shilingi Trilioni 5.3 kila mwaka kwa ajili ya manunuzi ya bidhaa na huduma zinazotumika migodini na kuwataka watanzania kuchangamkia fursa hizo.
Naye Mkuu wa Wilaya Ilemela, Mhe. Hassan Masala akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda amempongeza Waziri Mavunde kwa usimamizi mzuri wa Sekta ya Madini hali iliyopelekea mafanikio makubwa ikiwa ni pamoja na ongezeko la wawekezaji nchini.
Ametumia fursa hiyo kuwakaribisha wawekezaji kuwekeza katika mkoa wa Mwanza hasa katika eneo la uchimbaji wa madini na utoaji wa huduma mbalimbali kwenye migodi ya madini.
Naye Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Msafiri Mbibo amesisitiza kuwa Wizara ya Madini itaendelea kufungamanisha Sekta ya Madini na sekta nyingine muhimu za kiuchumi ili kuongeza ushiriki wa watanzania kwenye shughuli za madini nchini.
Wakati huohuo akizungumza kwa niaba ya Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Dkt David Mathayo, Mbunge wa Ilemela, Dkt. Angeline Mabula amepongeza kazi kubwa inayofanywa na Waziri Mavunde hali iliyochangia kwa kiasi kikubwa ukuaji wa mchango wa Sekta ya Madini kwenye Pato la Taifa.
“Kupitia uongozi wa Mhe. Mavunde tumeshuhudia mapinduzi makubwa kwenye Sekta ya Madini ambapo Tanzania imepiga hatua kubwa ya kihistoria kwa kufikia mchango wa asilimia 10.1 katika Pato la Taifa kwa Mwaka 2024, ikiwa ni Mwaka mmoja (1) kabla ya lengo la asilimia 10 lililowekwa kwenye Sera ya Madini ya Mwaka 2009 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026),” amesisitiza Dkt. Mabula
Naye Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Dkt. Janet Lekashingo amesema kuwa Tume imeanza kukusanya takwimu za bidhaa zinazoingizwa nchini ili kushauri Serikali kuhusu uanzishwaji wa viwanda vinavyotoa bidhaa husika na kuongeza mzunguko wa fedha nchini huku wananchi wakijipatia ajira.
Katika hatua nyingine, Kamishna wa Tume ya Madini ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ushirikishwaji wa Watanzania katika Sekta ya Madini, Dkt. Theresia Numbi ameeleza mikakati iliyowekwa na Tume ya Madini ya kuongeza ushiriki wa watanzania katika Sekta ya Madini kuwa ni pamoja na mikutano, majukwaa na vyombo vya habari.