Halmashauri ya jiji la Dar es salaam imefuta mikataba yote ya ujenzi ambayo imekuwa ikisuasua katika utekelezaji na kuisababishia halmashauri hasara kubwa 

akizungumza wakati wa kusaini mkataba mpya na mkandarasi anayejenga shule ya sekindari kipunguni mkurugenzi wa halmashauri ya jiji la Dar es Salaam Elihuruma Mabelya ametaja kuwa wameamua kufanya uamuzi huo kufuata maelekezo yaliyotolewa na Rais Dk Samia Suluhu Hassan wakati wa uzinduzi wa SGR.

Kwa upande wake mkuu wa  wilaya ya Ilala Mheshimiwa Edward Mpogolo amesema wao kama viongozi wanatekeleza agizo la Mhe.Rais Dkt Samia Suluhu Hassan alilolitoa wakati wa uzinduzi wa treni ya Mwendokasi(SGR) la kuwataka kukamilisha miradi inayowagusa wananchi moja kwa moja.

Mkuu huyo wa Wilaya ametoa kauli hiyo leo Januari 15,2025 wakati wa hafla fupi ya utiaji saini wa mkataba wa umaliziaji wa jengo la ghorofa la shule ya sekondari Kipunguni.

"Tunaposema Serikali imedhamiria kutimiza yale inayoahidi,mfano ni ukamilishwaji wa jengo la shule hii ambao ni utekelezaji wa agizo la Rais alilotoa kwamba tuhakikishe miradi inakamilika".Alisema Mkuu huyo wa Wilaya

Halmashauri ya Jiji la Dar es salaam imedhamiria kukamilisha miradi yote iliyokwama kutokana na sababu mbalimbali na ukamilishaji huu wa miradi una lengo la kutatua changamoto mbalimbali za wananchi ikiwemo huduma za afya,elimu nk.









 

Watanzania milioni 13.5 kusambaziwa umeme ifikapo 2030 kutoka milioni 5.2 ya sasa

Asema Mkutano wa Mission 300 umekuwa kivutio duniani; Taasisi za Kimataifa zaonesha nia ya kushiriki

Ataja sababu za mkutano wa M300 kufanyika Tanzania


Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe.Dkt.Doto Biteko amesema kuwa maandalizi ya Mkutano wa Nishati wa Wakuu wa Nchi za Afrika wenye lengo la kuharakisha upatikanaji umeme kwa Waafrika milioni 300 ifikapo 2030 (Mission 300) utakaofanyika tarehe 27 na 28 Januari jijini Dar es Salaam yamefikia asilimia 95.

Dkt.Biteko amesema hayo tarehe 15 Januari 2025 mara baada ya kukagua maandalizi ya Mkutano huo katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam akiwa ameambatana na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila.

Amesema Wakuu wa Nchi 54 kutoka Bara la Afrika  wanatarajiwa kushiriki  pamoja na  viongozi wengine ambao  ni Mawaziri wa Fedha na Nishati kutoka barani Afrika, Marais wa Benki ya Dunia (WB) na Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB), pamoja viongozi kutoka Jumuiya ya Ulaya na Jumuiya ya Umoja wa Afrika ambapo kazi zinazoendelea kwa sasa ni pamoja na kukamilisha ukarabati wa ukumbi wa JNICC.

“Kazi nyingine zinazoendelea ni pamoja na usajili na uthibitisho wa wageni ambao watakuja kwa ajili ya ushiriki na ukarabati wa maeneo mengine yatakayotumika kwenye mkutano huu, nichukue nafasi hii kuupongeza uongozi wa Mkoa wa Dar es Salaam kwa hatua iliyofikiwa na kuliweka jiji kwenye mandhari ya kuvutia.” Amesema Dkt.Biteko

Ameongeza kuwa, Mkutano wa M300  umekuwa kivutio ambacho kimewashawishi  Wakuu wa Taasisi nyingi za Kimataifa kuonesha nia ya kushiriki mkutano huo mkubwa katika Sekta ya Nishati.

Ameeleza kuwa, Tanzania kuwa mwenyeji wa mkutano huo kumetokana na Diplomasia nzuri ya Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ambayo imezidi kuimarisha uhusiano wa Tanzania kimataifa na kupelekea WB na AfDB kuichagua Tanzania kuwa mwenyeji wa Mkutano.

 Ametaja sababu nyingine ya Tanzania kuchaguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano huo muhimu ni mafanikio yaliyofikiwa katika sekta ya Nishati huku akitoa mfano wa mafanikio katika usambazaji wa nishati vijijini.

Amesema vijiji vyote nchini 12,318 vimesambaziwa umeme na Vitongoji 34,000 kati  ya 64,274  vilivyopo nchini,  tayari    vimesambaziwa umeme.

Ametaja baadhi ya faida za mkutano huo kuwa ni pamoja na kuongezeka idadi ya  Watanzania watakaounganishwa na umeme ifikapo mwaka 2030 hadi kufikia milioni 13.5 kutoka milioni 5.2 ya sasa.

Ameongeza kuwa, katika mkutano huo nchi zitasaini mikakati ya kuharakisha kusambaza umeme kwa wananchi ambayo itaeleza kwa kina hatua gani zitachukuliwa chini ya mwavuli wa WB na AfDB. 

Ameongeza kuwa, faida nyingine zitakazotokana na mkutano wa M300 ni kuongezeka kwa fursa za uwekezaji, kuimarisha biashara na kuongeza heshima ya nchi katika Duru za kimataifa na Tanzania kuwa Taifa linalopigiwa mfano kwenye nyanja mbalimbali.

Dkt. Biteko ametoa wito kwa Watanzania kuupokea kwa mikono miwili mkutano huo ambao kwa kiasi kikubwa unazidi kumheshimisha Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan na Watanzania kwa ujumla. 

Aidha, ametoa wito kwa wananchi kuendelea na hali ya amani na utulivu kuelekea katika mkutano huo wa kihistoria kutoka nchi ipige hatua kwenye Sekta ya Nishati kwani ni Mkutano Mkubwa wa kwanza kufanyika.

Vilevile ametoa wito kwa Waandishi wa Habari kuutangaza Mkutano huo kwa Watanzania ili waufahamu kwa kina na kufahamu fursa zilizopo.







Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila amesema maandalizi ya kupokea ugeni huo yako katika hatua za mwisho.

Amesema ili kufanikisha mkutano huo, baadhi ya mitaa itafungwa ili kuwezesha  maonesho na utalii wa ndani ikiwa ni pamoja na utalii wa tiba.



USIKU wa leo ni usiku wa mapene kwani itapigwa michezo ya kutosha katika ligi tofauti tofauti kuanzia Uingereza, Italia, na Ujerumani ambapo zitakupa fursa ya kunyakua mkwanja wako.

Pale ligi kuu ya Uingereza itapigwa michezo kadhaa, ligi kuu ya Ujerumani halikadhalika itapigwa michezo kadhaa, bila kusahau ligi kuu ya Italia ambayo nayo itashuhudia mchezo mkali ambao utachezwa pale San Siro.

Ligi kuu ya Uingereza leo itapigwa michezo kadhaa lakini mchezo ambao utatupiwa macho zaidi ni mchezo kati ya klabu ya Arsenal dhidi ya Tottenham Hotspurs ambao utapigwa pale kwenye dimba la Emirates mchezo huu unatarajiwa kua mkali kwelikweli kwani ni mchezo huo ni mchezo wa wapinzani wa jadi.

Michezo mingine ambyo itachezwa leo katika ligi kuu ya Uingereza itazikutanisha timu kama Everton Vs Aston Villa, Newcastle Vs Woves, bila kusahau klabu ya Leicester City wataikaribisha klabu ya Crystal Palace pale King Power.

Ligi kuu ya Ujerumani leo itashuhudia michezo kadhaa ikiwemo mchezo wa vinara wa ligi hiyo klabu ya Bayern Munich ambao wataikaribisha klabu ya Hoffenheim, michezo mingine ni kati ya Vfb Stuttgart Vs Rb Leipzig, Union Berlin Vs Augsburg, na Werder Vs Fc Heidenheim.

Kule nchini Italia ligi kuu ya Serie A kutakua na mchezo mkali pale katika dimba la San Siro ambapo klabu ya Inter Milan mabingwa watetezi watamenyana na klabu ya Bologna, Mchezo muhimu kwa vijana wa Inzaghi katika kuhakikisha wanarejesha nafasi yao ya kukaa kileleni mwa msimamo.

Michezo yote ambayo itachezwa leo imewekwa kwenye tovuti ya Meridianbet ambapo imepewa Odds bomba ambapo unaweza kujishindia maokoto ya kutosha kama utaweka mkeka wako leo bashiri sasa kupitia https://meridianbet.co.tz/sw/nyumbani ujinyakulie kititaaa.

Endelea kufurahia kubashiri na Meridianbet mabingwa wa michezo ya kubashiri ambao wanatoa ODDS BOMBA kuliko mahala pengine, Lakini pia machaguzi mengi zaidi ya 1000 Bashiri sasa michezo itakayopigwa wikiendi hii uweze kupiga mkwanja.

KUPITIA Meridianbet utakutana na mchezo wa kasino ya mtandaoni unaoelezea kisa cha Farao aliyelaaniwa kwa matendo yake, unachopaswa kufanya ni kuwa mkali kwa kucheza vizuri ni njia sahihi kukupa ushindi mkubwa. Jisajili Meridianbet ufurahie mchezo huu.

The Cursed King ni mchezo wa kasino ya mtandaoni yenye nguzo tano zna mistari 19 ya malipo. Ili kupata ushindi, unahitaji kuunganisha alama tatu au zaidi kwenye mstari wa malipo, kupitia mchezo huu utapata bonasi za kasino na mizunguko mingi ya bure.

Mchanganyiko wote wa kushinda huzingatiwa tu kutoka kushoto kwenda kulia, ukiwaza na safu ya kwanza kushoto.

Kwenye mstari mmoja wa kulipa, unaweza kupata ushindi mmoja tu. Ikiwa una mchanganyiko wa kushinda zaidi kwenye mstari mmoja wa malipo, utapata ushindi wa thamani kubwa zaidi.

Kwenye mchezo huu wa kasino ya mtandaoni upande wa sehemu ya Bet, kuna mishale ya juu na chini ambayo unaweza kutumia kuweka thamani ya dau kwa kila mzunguko.

Pia kuna chaguo la Autoplay unaweza kuamilisha wakati wowote unapotaka. Kupitia chaguo hili, unaweza kuweka hadi mizunguko 1,000.

Mchezo huu unafaa kwa aina zote za wachezaji kwani una kasi tatu za mizunguko. Ikiwa unapenda mchezo wa haraka, au za haraka sana. Kuwa moja ya washindi kwenye mcheo huu kwa kucheza kasino ya mtandaoni kwa dau kubwa uwezalo.

Alama za Ushindi Ndani ya The Cursed King

Linapokuja suala la alama katika mchezo huu, alama za kadi za kawaida, kama vile 10, J, Q, K na A, huleta ushindi mdogo zaidi. Miongoni mwao, A ni yenye thamani zaidi.

Zifuatazo ni alama ya kijani na nge ambazo huleta ushindi wa wastani kuliko alama za kadi.

Nzi wa buluu atakuletea ushindi wa wastani zaidi. Ikiwa utaunganisha alama tano za nzi hizi kwenye mchanganyiko wa kushinda, utashinda mara sita zaidi ya dau lako.

Chupa ya zambarau huleta ushindi wa wastani zaidi, na ikiwa utaunganisha alama tano za chupa hizi kwenye mchanganyiko wa ushindi, utashinda mara nane zaidi ya dau lako.

Ndege mwekundu ni alama yenye thamani zaidi katika mchezo. Ikiwa utaunganisha alama tano za ndege hizi kwenye mchanganyiko wa kushinda, utashinda mara kumi zaidi ya dau lako.

Bonasi maalum

Mchezo huu wa kasino ya mtandaoni una aina mbili za majoka. Majoka ya kawaida yanawakilishwa na alama ya Wild. Yanachukua nafasi ya alama zote, isipokuwa Scatter, na husaidia kukamilisha mchanganyiko wa ushindi.

Yanaonekana kwenye nguzo zote na huleta malipo tu na nakala tano kwenye mstari wa kulipa. Wakati huo, utashinda mara kumi zaidi ya dau lako.

Aina nyingine ya majoka inawakilishwa na Farao. Wakati inapatikana hata kwenye mchanganyiko wa kushinda mmoja, inapanuka kwenye nguzo nzima.

Nguzo ya majoka inaonekana na miale ya nasibu yenye thamani ambayo inaweza kuwa: x2, x3, x4, x5, x10, x15, x20, x25, x50 na x100. Ikiwa kuna majoka mengi ya nguzo sawa katika mstari wa kushinda, mizani yao itasimamishwa.

Scatter inawakilishwa na alama ya bonasi ya kasino na inaonekana kwenye nguzo zote. Tatu, nne au tano ya alama hizi zinaleta mizunguko mitatu, minne au mitano ya bure.

Na WILLIUM PAUL, SAME.

KUFUATIA taarifa za ujauzito kwa wanafunzi wanne wa shule tofauti za msingi na sekondari katika kata za Kalemawe na Bendera, Mkuu wa Wilaya ya Same, Kasilda Mgeni, ameagiza Jeshi la Polisi kuhakikisha wahusika wa matukio hayo wanakamatwa mara moja na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.

Kasilda ametoa maagizo hayo jana wakati wa ziara yake ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi, pamoja na kuhamasisha wazazi kuwapeleka watoto shule na kuwahimiza umuhimu wa kuwasaidia na kuwapeleka shule watoto wanaoanza chekechea, darasa la kwanza, na waliofaulu kujiunga na kidato cha kwanza ili kufanikisha ndoto zao.

Akiongea kwa uchungu, Kasilda amesisitiza kuwa vitendo vya kuwapa mimba wanafunzi vinaharibu ndoto za watoto wa kike na juhudi za serikali ya awamu ya sita, ambayo imejikita kuboresha mazingira ya elimu kwa wanafunzi wote, hasa wa kike.

"Mazingira rafiki ya elimu yanayoboreshwa na serikali yetu ya awamu ya sita yanahitaji msaada wa jamii vitendo kama hivi havikubaliki, vinaharibu maisha ya watoto wetu na kukiuka maadili yetu wahusika wote watawajibishwa kwa mujibu wa sheria," amesema kwa msisitizo.

Kasilda pia amewataka wazazi, walezi, na jamii kwa ujumla kuhakikisha watoto wanalelewa kwa maadili mema na kulindwa dhidi ya vitendo vya ukatili vinavyoweza kuathiri maendeleo yao ya kielimu na maisha yao kwa ujumla.

Ameagiza pia kukamatwa kwa wazazi wanaowaficha wanaume waliowapa mimba wanafunzi, akiwataja wazazi hao kuwa washiriki wa uhalifu kwa kuficha wabakaji.

"Hata wazazi walioshirikiana na wanaume waliowapa mimba wanafunzi kwa kupokea kitu kidogo nao hawatapona nimeagiza nao watafutwe na washitakiwe kwa kosa la kuficha wabakaji," ameongeza Kasilda.

Wananchi walioshiriki mkutano huo walionesha kuridhishwa na hatua za haraka zilizochukuliwa na Kasilda, huku wakiahidi kushirikiana na serikali kwa kutoa taarifa za wahusika wa ukatili dhidi ya wanafunzi.

Kwa upande wao, baadhi ya walimu wakuu wa shule hizo wameeleza kuwa changamoto kubwa ni ushirikiano mdogo kutoka kwa wazazi wa wahanga, ambao mara nyingi huficha ukweli na kuweka vikwazo katika upatikanaji wa ushahidi wa kisheria.

Walitoa wito kwa wazazi kutoa ushirikiano ili kuhakikisha hatua stahiki zinachukuliwa dhidi ya wahusika wa vitendo hivyo.







 

Baadhi ya Wajumbe wa Tume ya Rais ya Maboresho ya Kodi wamewasili Mkoani Kagera  Januari 15, 2025  kwa lengo la Kusikiliza na kupokea Kero na Changamoto zinazohusiana na masuala ya Kodi na Tozo mbalimbali.

Wajumbe hao wakiongozwa na Balozi Mwanaidi Maajar wamewasili Mkoani Kagera na Kukutana na Mwenyeji wao Mkuu wa Mkoa wa Kagera Bi. Fatma Mwassa, ambaye pamoja na mambo mengine ametoa ushauri na maoni yake juu ya masuala ya Kodi na njia za kuzitafutia ufumbuzi baadhi ya changamoto.

Pamoja na hayo Wajumbe hao wamepata fursa ya kukutana na sehemu ya Viongozi wa Jumuiya za Wafanyabiashara pamoja na wawakilishi wa wafanyabiashara, ambao nao wamekuwa na mazungumzo nao katika cha awali kabla ya Kikao kingine ambacho watakutana na Wafanyabiashara na wadau wa Kodi.







 



NA WILLIUM PAUL, MWANGA.

MKUU wa wilaya ya Mwanga mkoani Kilimanjaro, Mwanahamisi Munkunda amewataka wawekezaji kwenda kuwekeza katika wilaya hiyo kwani tatizo la maji ambalo lilikuwa kero kwao limeshapatiwa ufumbuzi wa kudumu.

Alitoa kauli hiyo jana alipofanya kikao na Wadau wa maji na menejimenti ya Mamlaka ya Maji Same Mwanga (Samwasa) mara baada ya kutembelea na kujionea mradi wa maji Mwanga - Same - Korogwe ambao awamu ya kwanza imeshakamilika na maji yanatoka katika wilaya ya Mwanga na Same.

Alisema kuwa, awali wawekezaji walikuwa wakishindwa kuwekeza katika wilaya hiyo kutokana na tatizo la maji lakini kwa sasa kupitia serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeweza kukamilisha mradi huo.

"Tunatambua wawekezaji wengi walikuwa wakikataa kuja kuwekeza katika wilaya yetu kutokana na tatizo la maji tulilokuwa nalo lakini serikali imeonyesha kwa vitendo kuondoa changamoto zinazowakabili wananchi wake ambapo kwa sasa tunapata maji masaa 24" Alisema Mwanahamisi.

Alisema kuwa, mradi huo umeliliwa na wananchi kwa muda mrefu lakini Dkt. Samia amekuja kuumaliza na kutatua kiu ya Wanamwanga ambapo kwa sasa wanayo maji ya kutosha.

Mkuu huyo alidai kuwa, lengo la mradi huo ni kuifungua wilaya ya Mwanga kiuchumi na kimaendeleo na kuwataka kuwa walinzi wa mradi huo ili uweze kudumu muda mrefu.

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa wilaya amewataka Watumishi wa Mamlaka ya maji Samwasa kubadilisha utendaji kazi na kuachana kufanya kazi kwa mazoea ili lengo la serikali na kuwahudumia wananchi wake liweze kutimia.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Mamlaka ya maji Samwasa, Mhandisi Rashid Mwinjuma alisema kuwa, uhitaji wa maji kwa wilaya ya Mwanga na Same ni lita za ujazo milioni 8 kwa siku huku mradi huo ukiweza kuzalisha lita za ujazo milioni 55.5 kwa siku hivyo maji yapo ya kutosha.

Mhandisi Mwinjuma alisema kuwa, kwa sasa Mamlaka hiyo inazidai taasisi za serikali na watu binafsi milioni 149.23 kwa Mwanga na milioni 132.22 kwa Same ambapo amehimiza wananchi kuendelea kulipa Ankara zao pamoja na madeni.

Alisema kuwa, kwa sasa Mamlaka hiyo inakabiliwa na changamoto ya uchelewaji wa vifaa kama mabomba kea ajili ya maunganisho ya maji kwenye mtandao wa mradi, uhaba wa fedha inayopelekea kutomudu gharama za ujenzi wa miradi na uendeshaji.

"T inakabiliwa na changamoto ya baadhi ya wateja kutolipa Ankara zao kwa wakati ambapo kwa sasa tunadai zaidi ya milioni 281 lakini pia upotevu wa maji mkubwa kutokana na uchakavu wa miundombinu" Alisema Mhandisi Mwinjuma.






Farida Mangube, Morogoro

 Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro limemkamata dereva Daniel Benaya Mwiluli, mwenye umri wa miaka 39, mkazi wa Makambako, mkoa wa Njombe, kwa tuhuma za uzembe uliosababisha ajali ya gari lililokuwa limebeba mafuta aina ya diesel.

Dereva huyo alikamatwa Januari 15, 2025, katika eneo la Mzambarauni, kata ya Mafisa, wilaya ya Morogoro, baada ya gari lenye namba za usajili T257 EAU/T620 ABG aina ya HOWO kupinduka kutokana na uzembe wa dereva hiyo ambapo hakuna taarifa za vifo vilivyoripotiwa

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro ameendelea kuwakumbusha madereva wa magari ya masafa marefu kuchukua muda wa kupumzika kabla ya safari ili kuzuia ajali zinazosababishwa na uchovu, ulevi, msongo wa mawazo, au usingizi.

Katika tukio hilo, Mrakibu Msaidizi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji wa Mkoa wa Morogoro, Daniel Ibrahim Mnyara, pia alitoa wito kwa wananchi kuepuka kufika kwenye maeneo ya ajali za mafuta kwa lengo la kuchota mafuta. Alisema vitendo hivyo ni hatarishi kwa maisha yao, mali zao, na vinaweza kuchukuliwa kama wizi.

Jeshi la Polisi limeahidi kuendelea kusimamia sheria na kuchukua hatua stahiki dhidi ya madereva wazembe kwa lengo la kudhibiti ajali barabarani.





 



Na Mwandishi Maalum,Ruvuma

WANANCHI wa kijiji cha Liweta Halmashauri ya wilaya Songea mkoani Ruvuma,wameishukuru Wakala wa barabara za vijijini na mijini(TARURA)kwa kuwajengea daraja la kudumu katika mto Liweta linalounganisha kijiji hicho na Masuku na maeneo yao ya kilimo.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti walisema,awali walikuwa wakipata shida kubwa kupitia katika eneo hilo hasa wakati wa masika wanapotaka kwenda mashambani na vijiji vya jirani kutokana na kukosekana kwa kivuko hali iliyochangia kuwarudisha nyuma kiuchumi.

Micheal William alisema,kabla ya daraja hilo walitumia siku tatu hadi nne kusubiri maji yapungue ndipo waendelee na safari kwenda kitongoji cha Litapatile na kijiji cha Masuku,lakini sasa hakuna tena changamoto hiyo baada ya kujengewa daraja la kudumu.

Hata hivyo,ameiomba Serikali kuendelea kuwasaidia kwa kuboresha barabara hiyo hadi maeneo ya Litapatile ambako kuna uzalishaji mkubwa wa mazao ya chakula na biashara ili wakulima waweze kuwa na uhakika wa kusafiri mazao yao.

“Wapo ndugu zetu waliofariki Dunia kwa kusombwa na maji walipokuwa wakijaribu kuvuka kipindi cha mvua kutokana na kukosekana kwa daraja,lakini sasa baada ya kujengwa kwa daraja hili ni furaha na neema kubwa kwetu”alisema.

Aidha alisema,awali hali ilikuwa mbaya zaidi kwa watoto wanaoishi mashambani kwani mto huo unapojaa maji walikaa muda mrefu kusubiri hadi maji yapungue ili waweze kwenda shule hivyo kukosa baadhi ya vipindi vya masomo.

Mkazi mwingine wa kijiji cha Masuku Malaika Komba alisema,miaka ya nyuma walikuwa kwenye mateso makubwa kupita katika eneo hilo kutokana na kujaa maji mengi na pindi walipotaka kwenda upande mwingine walitumia muda mrefu.

“tunaishukuru sana Serikali kwa kutuangalia kwa jicho la huruma na kutujengea daraja katika eneo hilo,hapa tumepoteza mazao yetu kwa kusombwa na maji pindi tulipotaka kuvuka kwenda kijijini kutafuta masoko”alisema Komba.

Kaimu meneja wa Tarura wilaya ya Songea Godfrey Mngale alisema,Serikali imetumia Sh.milioni 449 kujenga daraja na kufanya upanuzi wa barabara hiyo ili kurahisisha shughuli za usafiri na usafirishaji wa mazao kutoka shambani kwenda sokoni.

Alisema kuwa,daraja hilo ni muhimu katika kurahisisha mawasiliano na itarahisisha kufungua maendeleo ya wananchi wa kijiji cha Liweta,Masuku na Halmashauri ya wilaya Songea ambao walikuwa na uhitaji mkubwa wa daraja la kudumu.

Mngale,ametoa wito kwa wananchi kulilinda miundombinu ya daraja kwa kutojihusisha na vitendo vya kuchimba mchanga chini ya daraja,kuiba alama za barabarani na kuacha kupitisha mifugo juu ya daraja kwani Serikali imetumia gharama kubwa kujenga daraja na barabara.

Kwa upande wake meneja wa TARURA mkoa wa Ruvuma Silvester Chinengo alisema,daraja la Liweta ni moja ya miradi ya kuondoa vikwazo vya usafirishaji katika mkoa wa Ruvuma na daraja lina upana wa mita 20 na njia nne za kupitisha maji.

Chinengo alisema,daraja la Liweta linaunganisha kijiji cha Liweta na Masuku na kabla ya kujengwa wananchi walikuwa wanapata adha kubwa kupita kwenye maji na msimu wa kilimo walishindwa kwenda upande wa pili kwa ajili ya kuendelea na shughuli zao za uzalishaji.

“kwa hiyo Serikali kupitia mradi wa kuondoa vikwazo vya usafirishaji unaofadhiliwa na Benki ya Dunia ndiyo uliofanikisha ujenzi wa daraja hili na kwa sasa wananchi wanafurahia huduma inayotolewa na Serikali yao ya awamu ya sita”alisema Chinengo.

Chinengo,ameishukuru Serikali kwa kutoa fedha zilizotumika kujenga daraja hilo ambalo limewezesha kuondoa kikwazo cha usafirishaji kilichowatesa wananchi wa maeneo hayo kwa muda mrefu.
muonekano wa daraja la Liweta-Masuku Halamshauri ya wilaya Songea linalojengwa na wakala wa barabara za vijijini na mijini Tarura ambapo ujenzi wake umekamilika kwa zaidi ya asilimia 98.
Meneja wa TARURA Mkoa wa Ruvuma Mhandisi Silvester Chinengo kushoto na kaimu meneja wa TARURA Wilaya ya Songea Godfrey Mngale wakikagua ujenzi wa daraja la Liweta-Masuku jana.







Kaimu meneja wa TARURA wilaya ya Songea Mhandisi Godfrey Mngale wa pili kulia na baadhi ya Waandishi wa habari wakikagua ujenzi wa daraja la Liweta-Masuku katika Halmashauri ya wilaya Songea mkoani Ruvuma.






 

Na Mwandishi Wetu.

Dar es Salaam. Kampuni inayojulikana kwa ubunifu katika sekta ya michezo ya kubahatisha, M-Bet Tanzania, imezindua muonekano mpya wa tovuti yake kwa lengo la kuboresha huduma kwa wateja. 

Tovuti hiyo, inayopatikana kupitia www.m-bet.co.tz, inawawezesha wateja kubashiri aina mbalimbali za michezo na kufanya miamala ya kuweka na kutoa fedha kwa urahisi zaidi. Kupitia tovuti hiyo pia unaweza kucheza Aviator na defender bila ya kwenda Casino.

Meneja Masoko wa M-Bet Tanzania, Levis Paul, amesema  kuwa uboreshaji huo ni hatua ya kuthamini wateja na kuwapa huduma bora zaidi ambapo ili kujiunga unajisajili kwenye tovuti hiyo www. m-bet.co.tz na kufuata maelelezo ambapo kwa wateja wa zamani, wanatakiwa kujiunga na kuingiza neno siri (password) upya.

"Mbali na kuwa na odds kubwa, tumeamua kuboresha tovuti yetu ili kuwarahisishia wateja wetu. Sasa wanaweza kucheza michezo kama aviator na defender bila kutembelea casino, kupitia simu ya mkononi, laptop, au kompyuta ya nyumbani," alisema Levis.

Kwa mujibu wa Levis, M-Bet imekuwa mstari wa mbele katika sekta ya michezo ya kubashiri nchini kwa zaidi ya muongo mmoja. "Tumekuwa sehemu ya ukuaji wa sekta hii, na mchango wa wateja wetu ni muhimu sana. Tunataka kuhakikisha wanapata thamani ya fedha zao na huduma zenye viwango vya juu," aliongeza.

Tovuti hiyo mpya inatoa nafasi kwa wateja kuweka mkeka, kushiriki au kubashiri katika michezo mbalimbali, na kuchukua ushindi wao papo hapo. Levis alibainisha kuwa maboresho haya ni sehemu ya mkakati wa muda mrefu wa kampuni hiyo kuhakikisha kuwa kila mteja anapata huduma bora zaidi.

Alisema kuwa katika kipindi cha zaidi ya miaka 10, M-Bet imejijengea sifa kama waanzilishi wa michezo ya sports betting nchini Tanzania. "Tunajivunia kuwa sehemu ya mafanikio ya sekta hii, na tunawahakikishia wateja wetu kwamba tutaendelea kuboresha huduma zetu ili kukidhi mahitaji yao," alisema Levis.

Alifafanua kuwa wa maboresho haya, M-Bet Tanzania inadhihirisha dhamira yake ya kuwawezesha wateja kushiriki michezo ya kubahatisha kwa njia salama, rahisi, na ya haraka. Tovuti hii ni hatua kubwa katika kuwapa wateja huduma zinazolingana na mahitaji yao ya kila siku.
Meneja Masoko wa M-Bet Tanzania, Levis Paul akizungumza wakati wa utambulisho mpya wa tovuti ya kampuni hiyo ambayo imeboreshwa na kuwa ya kisasa na kuwawezesha watejawao kubashiri



 
Na Mwandishi Wetu,Geita 

MPANGO wa kunusu kaya maskini nchini (TASAF) umetumia zaidi ya Shilingi bilioni 59 kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo pamoja na fedha kwa ajili ya walengwa wa mpango huo kwa kipindi cha Julai 2020 hadi Januari 2025 Mkoani Geita.
Fedha hizo zimetumika kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya elimu,afya,ujenzi wa barabara,utunzaji wa mazingira na ujenzi wa malambo lengo likiwa ni kuwasogezea wananchi huduma karibu na kuwasaidia kujikwamua kiuchumi.

Akizungumza wakati wa ziara ya wajumbe wa kamati ya uongozi Tasaf makao makuu waliofika mkoani Geita kwa ajili ya kukagua miradi inayotekelezwa kwa fedha za Tasaf,Katibu Tawala Mkoa wa Geita Mohamed Gombati amesema uwepo wa mpango umewezesha watoto wa walengwa wanaosoma shule za msingi na sekondari kumudu kupata mahitaji ya shule na kuendelea na masomo.

Amesema mpango huo umesaidia kuongeza mahudhurio ya kliniki kwa watoto chini ya miaka mitano na wazazi kupata mafunzo na malezi ya watoto,huku baadhi ya walengwa wakifanikiwa kuanzisha biashara ndogondogo kwa ajili ya kupata kipato na kuimarisha uchumi wa kaya.

“Walengwa wengi wamemudu kupata mahitaji ya msingi katika kaya na kuweza kumudu kupata milo miwili tofauti na awalai hali zao zilivyokuwa kabla ya mpango”amesema

Katika ziara hiyo ya siku moja Wajumbe hao wa kamati ya Uongozi Tasaf makao makuu wametembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa kituo cha afya Nyabilezi kilichopo Wilayani Chato kilichojengewa kwa gharama ya Shilingi bilioni 1.4 ambazo ni fedha za Tasaf.

Akizungumza katika kituo hicho Mganga mfawidhi wa kituo Sylivester Bundalah amesema kupitiaTasaf miradi kumi ya miundombinu imetekelezwa kwenye kituo hicho.

Miradi hiyo ni pamoja na Ujenzi waa jengo la wagonjwa wa nje,Jengo la maabara ,jengo la upasuaji na lile la wazazi,nyumba ya kuhifadhia maiti,kichomea taka ngumu,nyumba za watumishi,jengo la kufulia,ujenzi wa vyoo,uzio pamoja na njia ya kupita wagonjw ana watumishi.

Amesema kukamilika kwa kituo hicho kumewaondolea wananchi zaiid ya 12,000 adha ya kutembea umbali mrefu kufuata huduma za afya kwenye hospitali ya Wilaya iliyoko umali w akm 18.

Amesema pamoja na kuwaondolea wananchi adha ya kutembea umbali mrefu bado wanalazimika kufuata huduma mbali pale wanapohitaji matibabu makubw akutokana na vifaa vilivyopo kituoni kushindwa kufanya kazi kutokana na kituo kukosa umeme wa njia tatu.

Wakizungumza mara baada ya kutembelea kituo hicho wajumbe wa kamati ya uongozi Dk Ruth Lugwisha na Dk Naftali Ng’ondi w ameutaka uongozi wa halmashauri kwa kushirikiana na uongozi w a kituo kuona namna ya kufunga umeme mkubwa kwenye kituo hicho ili vifaa hivyo viweze kutumika.

“Vitu vya umeme visipotumika vinaharibika Halmashauri angalieni uwezekano wa kupata fedha hata kutoka kwenye mapato ya ndani kwa ajili ya kufunga umeme mkubwa kwenye kituo hiki ili lengo la Serikali la kutoa vifaa tiba kwa ajili ya wagonjwa liwe na tija”amesema N’gondi

“Hivi ni vitu vya gaharama halmashauri na uongozi wa hospitali kaeni chini muone njia ya kuleta umeme mkubwa hapa ,mfano kuna Wafanyabiashara ,kuna watu wakubwa hapa kuna viwanda washirikisheni naimani hawatakataa ili vifaa hivi viweze kutoa huduma”amesema Dk Lugwisha.

Katika hatua nyingine Wajumbe hao wa kamati ya uongozi ya Tasaf  wameshauri walengwa wa Tasaf waelimishwe ili watambue kuwa Umaskini sio sifa nzuri hivyo wanapaswa kutumia kidogo wanachopokea kwa malengo ili baada ya muda watoke kwenye lindi la umaskini na kujitegemea.










Top News