Na Said Mwishehe,Michuzi TV

WAZIRI wa Maendeleleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Zanzibar Pembe Riziki Juma amewahimiza wadau wa maendeleo kuendelea kushirikiana na Serikali kuendeleza jitihada za kuwaendeleza wanawake na kuimarisha usawa wa kijinsia nchini na Afrika kwa ujumla.

Ameyasema hayo jijini Dar es Salaam alipokuwa akifungua Kongamano la Uongozi wa Wanawake lililoandaliwa na Taasisi ya Uongozi chini ya ufadhili wa Serikali ya Tanzania, Finland, Umoja wa Ulaya (EU) na Umoja wa Mataifa (UN).

"Kumwezesha kiongozi mwanamke kunafungua fursa mbalimbali zinazoweza kumsaidia kufanya maamuzi jumuishi na yenye kuliletea Taifa maendeleo pamoja na kuleta mabadiliko katika nyanya mbalimbali.Tukimjenga mwanamke tunampa nafasi nzuri ya kuleta mabadiliko katika nyanya zote za maendeleo.

"Na hasa katika kushughulikia masuala muhimu ya kuondoa umaskini, kuimarisha elimu hasa kukuza ujuzi na vipaji unaohitajika katika soko la sasa na baadae, kuimarisha huduma za afya na kuongeza fursa za kiuchumi kwa jinsia zote,” amesema Waziri Juma.

Ameongeza Serikali inatambua uzingatiaji wa masuala ya jinsia una mchango mkubwa katika kukuza ustawi wa wananchi na maendeleo ya taifa na kwa kutambua hilo msisitizo umewekwa katika kukuza usawa wa kijinsia katika kufanya maamuzi katika ngazi zote.

Waziri Juma amesema ushiriki wa wanawake katika ngazi mbalimbali za maamuzi na uongozi ni moja ya vipaumbele vya Serikali katika kuhakikisha usawa kati ya wanaume na wanawake.

Amesema kwamba takwimu zinaonesha wanawake katika nafasi za uongozi wakiwemo mawaziri, naibu mawaziri, makatibu wakuu, naibu makatibu wakuu na wakurugenzi katika taasisi mbalimbali za umma ni asilimia 28.6 ya viongozi wote.

“Hiki ni kiashiria chanya kuelekea kufikia asilimia 30 ya uwakilishi wa wanawake katika uongozi, ambayo ni hatua muhimu kuelekea kufikia lengo Na. 5 la Usawa wa Kijinsia (SDG 5) kufikia asilimia 50 ifikapo 2030,” alisema Juma

Pamoja na jitihada za Serikali, bado kumekuwa na changamoto za namna ya kutekeleza ujumuishwaji wa jinsia katika usimamizi wa rasilimaliwatu hali inayosababisha kukosekana kwa uwiano sawa kati ya wanawake na wanaume katika baadhi ya maeneo nchini.

Awali Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uongozi, Kadari Singo amesema kuwa kongamano hilo ni sehemu ya programu yao ya Uongozi wa Wanawake (WLP) inayolenga kusaidia wanawake kusonga mbele katika majukumu ya uongozi.

"Kupitia kongamano hili limewaleta pamoja viongozi wakuu wa kiafrika na wanaoibukia kutoka Zambia, Ethiopia, Kenga, Uganda, Afrika Kusini, Botswana, Msumbiji na Cameroon ili kubadilishana mawazo na kupeana mbinu bora ili kukuza ushirikishwaji wa wanawake katika majukumu ya uongozi."

Ameongeza tafiti zilizofanywa na Taasisi ya Uongozi inaonesha wanawake wapo wengi katika nafasi za chini za utendaji na katika nafasi za juu za maamuzi wanapungua hivyo wameona waongeze jitihada za kuwaweka zaidi katika programu hiyo.




Serikali imesaini mkataba wa ujenzi wa Daraja la Jangwani lenye urefu wa mita 390 na barabara za maungio zenye urefu wa mita 700 katika barabara ya Fire - Ubungo kwa gharama ya Shilingi Bilioni 97.1 ambapo kazi ya ujenzi itatekelezwa kwa miezi 24.

Mkataba huo umesainiwa leo Oktoba 22, 2024 Mkoani Dar es Salaam kati ya Wakala ya Barabara (TANROADS) na Mkandarasi wa Kampuni ya China Communications Construction Company Limited na kushuhudiwa na Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa na viongozi wengine.

Akizungumza baada ya kushuhudia utiaji saini huo, Waziri Bashungwa ameeleza kuwa ujenzi wa daraja hilo utaondoa kero kwa wananchi na adha ya usafiri kutokana na eneo hilo kujaa maji mara kwa mara na kusababisha barabara kufungwa na kutopitika mvua zinaponyesha.

Bashungwa amemuelekeza Mkandarasi huyo kukamilisha maandalizi na kupeleka vifaa na mitambo ndani ya miezi mitatu katika eneo la Jangwani ili kazi iweze kuanza na kuhakikisha anajenga haraka kwa mujibu wa usanifu na mkataba kama ilivyopangwa.

Aidha, Bashungwa ameeleza kuwa ujenzi wa daraja hilo utaenda sambamba na ujenzi wa kingo za Mto Msimbazi ambao utatekelezwa na Ofisi ya Rais - TAMISEMI ikiwa ni katika programu ya uendelezaji wa Bonde la Msimbazi.

Bashungwa amebainisha kuwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa shilingi Bilioni 125 kwa ajili ya kurejesha miundombinu katika Mkoa wa Dar es Salaam iliyoathiriwa na mvua za El-Nino ikiwa ni pamoja na ujenzi wa daraja la Kigogo, daraja la Mpiji chini, daraja la Mtongani, daraja la Mkwajuni, daraja la Mzinga, daraja la Nguva na box kalavati la Mikadi, daraja la JKT – Ununio, daraja la Kisarawe, Amani, Gomvu, Geti jeusi, mifereji ya maji Kigamboni – Kibada na maeneo mengine.

Akitoa taarifa ya mradi, Mtendaji Mkuu wa TANROADS, Mhandisi Mohamed Besta ameeleza kuwa mkandarasi aliyeshinda zabuni ya ujenzi ni kampuni ya China Communications Construction Company Limited na kusimamiwa na kampuni ya Leporogo Specialist Engineers ya Afrika Kusini ikishirikiana na Afrisa Consulting Ltd ya Tanzania na Dong Myeong Engineering Consultants & Architecture Co. Ltd ya Korea Kusini.

Naye, Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mbunge wa Jimbo la Ilala, Mussa Hassan Zungu ameeleza kuwa utekelezaji wa ujenzi wa daraja la Jangwani ni matokeo ya 4R za Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Albert Chalamila amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuweka historia ya kuanza kutekeleza ujenzi wa daraja la Jangwani.

Mradi wa Ujenzi wa Daraja la Jangwani ni moja ya mikakati ya Serikali ya kuharakisha maendeleo ya kiuchumi na kijamii Mkoani Dar es Salaam kwa kuboresha barabara ili kuongeza ufanisi katika sekta ya Usafiri.











Na Seif Mangwangi, Arusha

KIONGOZI Mkuu wa jamii ya Kimaasai nchini, Laigwanan Issack Ole Kisongo amesema wanaendelea na mazungumzo na Serikali kwa lengo la kuangalia uwezekano wa zoezi la uhamishwaji wa wafugaji katika Tarafa ya Ngorongoro kusitishwa.

Akijibu swali kutoka kwa washiriki wa mdahalo kuhusu nafasi ya Mila katika kutoka Haki ya vijana na wanawake kumiliki Ardhi katika kongamano la nne la Kimataifa linalohusu vijana na utawala wa Ardhi ( CIGOFA4 ), linaloendelea Jijini Arusha, Ole Kisongo amesema changamoto iliyopo nchini ni kwamba aridhi yote iko chini ya Rais hivyo anaweza kuamua matumizi ya ardhi hiyo wakati wowote.

Aidha amesema jamii hiyo imeamua kuwashirikisha Wanawake kwenye umiliki wa ardhi kwa kuwa vijana wengi katika jamii hiyo wamekuwa wakiuza ardhi pindi wanaporithishwa.

Amesema jamii hiyo imepitisha Sheria kuruhusu Wanawake kutambulika kwenye umiliki wa Ardhi jambo ambalo halikuwahi kufanyika hapo awali.

" Siku hizi vijana wetu hawaaminiki, ukimmilikisha ardhi ataiuza na kutelekeza familia, tumepitisha Sheria ili kukomesha tabia hii ili ikitokea Kijana anataka kuuza ardhi lazima Mke wake aridhie kwanza lasivyo hatoweza kuiuza,"amesema.

Amesema kwa mujibu wa Mila za Kimaasai kijana anapoingia jando anakabidhiwa ardhi na Mali zote za familia na Baba katika familia hiyo anakuwa kama mwangalizi pekee.

Aidha amesema migogoro mingi ambayo imekuwa ikitokea katika maeneo ya wafugaji imekuwa ikisababishwa na utetezi wa Ardhi kwaajili ya shughuli za uchumi.

Wakichangia mada katika kongamano hilo, washiriki wamesema kuna umuhimu mkubwa kwa vijana na wanawake kumilikishwa ardhi kwa kuwa wao ndio nguvukazi katika jamii.

Wamesema hata hivyo pamoja na madai ya vijana wengi kukimbilia mijini na kuacha ardhi Vijijini Bado elimu kuhusu rasilimali ardhi inatakiwa kutolewa kwa vijana kabla ya kukabidhiwa.

Mkurugenzi wa shirika la Jumuiko la Maliasili nchini (TNRF), Faustin Zakaria amesema suala la umiliki wa ardhi kwa vijana linatakiwa kuanza katika ngazi ya jamii kwa kutambua umuhimu wa ardhi, utambulisho. na mgawanyo wa rasilimali hiyo na fursa zinazopatikana kwa vijana.

Aidha ametoa wito kwa Serikali kuwashirikisha vijana katika uundaji wa sera itakayokuwa ikitambua umiliki wa ardhi kwa vijana.

Kongamano hilo lililoanza Jana Jijini hapa, linalofanyika pia kwa njia ya mtandao linashirikisha washiriki zaidi ya 500 kutoka nchi mbalimbali za Kiafrika wengi wao wakiwa ni vijana pamoja na taasisi zinazofanya programu za utetezi wa haki za ardhi.


Na Farida Ramadhani na Joseph Mahumi, WF – Mbeya

Viongozi wa kimila (Machifu), jijini Mbeya, wameiomba Serikali kuweka program ya elimu ya fedha kuwa endelevu ili kuwawezesha wananchi wengi zaidi kupata uelewa na kutatua changamoto mbalimbali za masuala ya kifedha.

Wametoa wito huo walipotembelea Maadhimisho ya Nne ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa kwa mwaka 2024 yanayoendelea katika Viwanja vya Ruanda-Nzovwe Jijini Mbeya, yaliyobeba kauli mbiu ya “Elimu ya Fedha, Msingi wa Maendeleo ya Kiuchumi”.

Akizungumza kwa niaba ya Machifu hai, Chifu Lyoto, alisema elimu ya fedha ni muhimu kwa kuwa inatoa mwongozo wa namna bora ya kutumia fedha, umuhimu wa uwekaji akiba, mikopo pamoja na namna bora ya kujikwamua kiuchumi.

“Tunaishukuru Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuleta Maadhimisho haya Mbeya, tunaiomba iendelee kutuletea hii elimu hasa katika maeneo ya vijijini kwa kuwa masuala ya fedha ni muhimu katika maisha yetu”, alisema Chifu Lyoto.

Alisema katika Maadhimisho hayo wamejifunza mengi kuhusu masuala ya fedha na watatumia elimu hiyo kuwaelimisha wengine ambao hawajapata nafasi ya kufika katika viwanja hivyo.

Aidha, aliwakaribisha wananchi wote wa jiji la Mbeya na viunga vyake kutembelea Maadhimisho hayo ili kupata elimu muhimu kwa maendeleo yao na maendeleo ya Taifa kwa ujumla.

Maadhimisho ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa ni utekelezaji wa Mpango Mkuu wa Maendeleo ya Sekta ya Fedha wa Mwaka 2020/21 – 2029/30 ambao pamoja na mambo mengine elimu kwa umma ni moja ya maeneo ya kipaumbele katika utekelezaji wa Mpango huo.

Maadhimisho hayo yanalenga kuelimisha wananchi kuhusu matumizi ya huduma rasmi za fedha pamoja na kuongeza mchango wa Sekta ya Fedha kwenye ukuaji wa Uchumi.
Kamishna Msaidizi wa Idara ya Uendelezaji wa Sekta ya Fedha, Wizara ya Fedha, Bi. Janeth Hiza (Kulia), akiwakaribisha Machifu wa Jiji la Mbeya walipotembelea Banda la Wizara ya Fedha, katika Maadhimisho ya Nne ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa, yenye kaulimbiu “Elimu ya Fedha, Msingi wa Maendeleo ya Kiuchumi”, yanayoendelea katika Viwanja vya Ruanda-Nzovwe, Jijini Mbeya, ambayo yamezikutanisha Taasisi Ndogo za Fedha, Benki, Mifuko ya Hifadhi ya Jamii pamoja na wajasiriamali kutoka jijini Mbeya na mikoa jirani.
Kamishna Msaidizi wa Idara ya Uendelezaji wa Sekta ya Fedha, Wizara ya Fedha, Bi. Janeth Hiza (Kulia), akitoa maelezo kuhusu Maadimisho ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa kwa Machifu wa Jiji la Mbeya, walipotembelea Banda la Wizara ya Fedha, wakati wa Maadhimisho ya Nne ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa, yenye kaulimbiu “Elimu ya Fedha, Msingi wa Maendeleo ya Kiuchumi”, yanayoendelea katika Viwanja vya Ruanda-Nzovwe, Jijini Mbeya, ambayo yamezikutanisha Taasisi Ndogo za Fedha, Benki, Mifuko ya Hifadhi ya Jamii pamoja na wajasiriamali kutoka jijini Mbeya na mikoa jirani.
Afisa Usimamizi wa Fedha Mkuu wa Wizara ya Fedha, Bi. Grace Muiyanza, akitoa elimu ya Fedha kwa Machifu na wawakilishi wa vikundi vya kijamii jijini Mbeya, kuhusu utunzaji wa fedha binafsi, umuhimu wa kuweka akiba pamoja na kupanga bajeti walipotembelea Maadhimisho ya Nne ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa, yenye kaulimbiu “Elimu ya Fedha, Msingi wa Maendeleo ya Kiuchumi”, yanayoendelea katika Viwanja vya Ruanda-Nzovwe, Jijini Mbeya, ambayo yamezikutanisha Taasisi Ndogo za Fedha, Benki, Mifuko ya Hifadhi ya Jamii pamoja na wajasiriamali kutoka jijini Mbeya na mikoa jirani.
Machifu wa jiji la Mbeya wakiongozwa na Chifu Lyoto wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kutembelea mabanda mbalimbali katika Maadhimisho ya Nne ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa, yenye kaulimbiu “Elimu ya Fedha, Msingi wa Maendeleo ya Kiuchumi”, yanayoendela katika Viwanja vya Ruanda-Nzovwe, Jijini Mbeya, ambayo yamezikutanisha Taasisi Ndogo za Fedha, Benki, Mifuko ya Hifadhi ya Jamii pamoja na wajasiriamali kutoka jijini Mbeya na mikoa jirani.
Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Mbeya, Bw. Emmanuel Kayuni (kushoto), akimsikiliza kwa makini Afisa Tehama Mwandamizi, Wizara ya Fedha, Bi. Zaina Mwanga, kuhusu Mfumo wa Ukusanyaji wa Maduhuli ya Serikali (GePG), alipotembelea Banda la Wizara ya Fedha, katika Maadhimisho ya Nne ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa, yenye kaulimbiu “Elimu ya Fedha, Msingi wa Maendeleo ya Kiuchumi”, yanayoendelea katika Viwanja vya Ruanda-Nzovwe, Jijini Mbeya, ambayo yamezikutanisha Taasisi Ndogo za Fedha, Benki, Mifuko ya Hifadhi ya Jamii pamoja na wajasiriamali kutoka jijini Mbeya na mikoa jirani.
Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa, Bw. Emmanuel Kayuni (kushoto), akimsikiliza Mhasibu Mkuu, Wizara ya Fedha, Bi. Kurthum Juma, kusuhu masuala ya madeni, alipotembelea Banda la Wizara ya Fedha, katika Maadhimisho ya Nne ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa, yenye kaulimbiu “Elimu ya Fedha, Msingi wa Maendeleo ya Kiuchumi”, yanayoendelea katika Viwanja vya Ruanda-Nzovwe, Jijini Mbeya, ambayo yamezikutanisha Taasisi Ndogo za Fedha, Benki, Mifuko ya Hifadhi ya Jamii pamoja na wajasiriamali kutoka jijini Mbeya na mikoa jirani.
Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF, Bw. Abdul-razaq Badru, akiagana na Mchumi Mkuu kutoka Idara ya Uendelezaji wa Sekta ya Fedha, Wizara ya Fedha, Bw. Mudith Cheyo baada ya kutembelea Banda la Wizara ya Fedha, katika Maadhimisho ya Nne ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa, yenye kaulimbiu “Elimu ya Fedha, Msingi wa Maendeleo ya Kiuchumi”, yanayoendelea katika Viwanja vya Ruanda-Nzovwe, jijini Mbeya, ambayo yamezikutanisha Taasisi Ndogo za Fedha, Benki, Mifuko ya Hifadhi ya Jamii pamoja na wajasiriamali kutoka jijini Mbeya na mikoa jirani.
Mtunza Kumbukumbu kutoka Kitengo cha Pensheni, Idara ya Mhasibu Mkuu wa Serikali, Wizara ya Fedha, Bi. Stella Mtally, akimkabidhi kipeperushi kinachoelezea aina ya mafao yanayotolewa na Wizara ya Fedha, mmoja wa wananchi wa jiji la Mbeya, waliotembelea Banda la Wizara ya Fedha, katika Maadhimisho ya Nne ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa, yenye kaulimbiu “Elimu ya Fedha, Msingi wa Maendeleo ya Kiuchumi”, yanayoendelea katika Viwanja vya Ruanda-Nzovwe, jijini Mbeya, ambayo yamezikutanisha Taasisi Ndogo za Fedha, Benki, Mifuko ya Hifadhi ya Jamii pamoja na wajasiriamali kutoka jijini Mbeya na mikoa jirani.
Afisa Maendeleo ya Jamii Mbeya, Bw. Marco Fihavango, akitoa elimu kuhusu mikopo inayotolewa na Halmashauri kwa wanafunzi wa Chuo cha Uhasibu Tanzania (TIA) tawi la Mbeya, walipohudhuria madarasa yanayoendelea katika Maadhimisho ya Nne ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa, yenye kaulimbiu “Elimu ya Fedha, Msingi wa Maendeleo ya Kiuchumi”, yanayoendelea katika Viwanja vya Ruanda-Nzovwe, jijini Mbeya, ambayo yamezikutanisha Taasisi Ndogo za Fedha, Benki, Mifuko ya Hifadhi ya Jamii pamoja na wajasiriamali kutoka jijini Mbeya na mikoa jirani.

(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF, Mbeya)

 

 

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na wageni wake Balozi wa Egypt Nchini Tanzania Mhe.Sharif A.Ismail na (kulia kwake) Balozi wa Malawi Nchini Tanzania Mhe.Andrew Kumwenda,baada ya kumaliza mazungumzo yao yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar leo 20-10-2024.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na kuagana na Balozi wa Morocco Nchini Tanzania Mhe.Zakaria El Goumiri,baada ya kumaliza mazungumzo na Ujumbe wa Umoja wa Mabalozi mbalimbali wa Nchi za Bara la Afrika, yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar leo 20-10-2024.(Picha na Ikulu)

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na Ujumbe wa Umoja wa Mabalozi mbalimbali wa Nchi za Bara la Afrika,ukiongozwa na Mwenyekiti wake Balozi wa Comoro Nchini Tanzania Dkt.Ahamada El Badaoui Mohammed (kulia kwa Rais) mazungumzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar leo 20-10-2024.(Picha na Ikulu)

 

Na Mwandishi wetu  Oktoba 22,2024

Mwenyekiti wa Kamati ya Utawala na Fedha ya Bodi ya Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST), CPA Constantine Mashoko ameitaka Menejimenti ya taasisi hiyo kukamilisha mchakato wa upatikanaji wa Ithibati wa Vyungu vinavyo tutumika kuyeyushia sampuli za madini ya dhahabu.

CPA Mashoko ameyasema hayo leo Oktoba 22, 2024 kwenye kikao cha Kamati wakati akipokea Ripoti ya Utawala na Fedha kilichofanyika katika ukumbi wa Prof. Abdulkarim Mruma uliyopo Jijini Dodoma.

Aidha, CPA Mashoko amebariki pendekezo la Menejimenti la kuiomba Serikali kutumia Sheria ya Local Content ili kuwataka wadau kutumia Vyungu vya kuyeyushia sampuli za Dhahabu kutoka ndani ya Nchi kwa asilimia kadhaa ya mahitaji yao.

Aidha, imeelezwa kuwa,  kutokana na umuhimu wa usalama wa sampuli katika kutoa majibu sahihi, wadau wengi walioko sokoni, wanahitaji Vyungu imara na vyenye ubora uliodhibitishwa na Taasisi za udhibiti Ubora zinazoaminika Kimataifa ambapo, vyungu vinavyotengenezwa na GST vina ubora wa hali ya juu na vipo katika hatua za mwisho za kupata Ithibati hiyo.

Pamoja na mambo mengine, Taarifa mbalimbali za utekelezaji kwa kipindi kinachoanzia Julai hadi Septemba, 2025 zimewasilishwa katika Kamati hiyo ambapo Meneja wa Fedha kutoka GST amewasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Sehemu ya Fedha na Uhasibu, Meneja wa Utawala na Rasilimaliwatu Jacqueline Kalua amewasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Sehemu ya Usimamizi na Maendeleo ya Rasilimalwatu na Utawala;

Pia, Mkuu wa Kitengo cha Ununuzi na Ugavi Datus Matuma amewasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Kitengo cha Ununuzi na Ugavi na Meneja wa Mipango na Masoko Priscus Benard amewasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Sehemu ya Mipango na Masoko.

Vikao vya Kamati vya GST ni maandalizi ya vikao vya Bodi vinavyofanyika mara nne kwa Mwaka ambapo ni kila baada ya kila Robo ya Mwaka wa Fedha ambapo kwa taasisi ya GST kuna jumla ya Kamati tatu ikiwemo Kamati ya Jiosayansi, Kamati ya Ukaguzi na Kamati ya Fedha na Utawala.





 

TAMASHA la 43 la Kimataifa la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) linatarajiwa kufanyika kwa siku nne ambapo litafunguliwa na Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Dk. Damas Ndumbaro Oktoba 23, 2024 katika Viwanja vya TaSUBa.

Tamasha hilo litahusisha shughuli mbalimbali za kisanii, kiuchumi na kijamii. Lengo kuu likiwa kuvutia wadau na watazamaji kutoka ndani na nje ya nchi.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Oktoba 22, 2024 Bagamoyo, mkoani Pwani Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma, amesema tamasha hilo limekuwa na mafanikio makubwa kuhakikisha wanaendeleza sanaa.

Amesema anatarajia wasanii wote watakaoshiriki watatoa burudani ya aina yake na kukata kiu ya mashabiki wao.

“Tamasha limeshakuwa na mafanikio makubwa kwa wasanii na sanaa yetu kwa ujumla, tunatarajia mwaka huu kutakuwa na burudani tofauti kutoka mataifa mbalimbali ambao pia wamekuwa wakishiriki,” amesema

Kwa upande wake Mkuu wa Taasisi ya TaSUBa, Dkt. Herbert Makoye amesema tamasha la msimu huu linatarajiwa kuhusisha vikundi mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi vikiwemo vya ngoma za asili, muziki wa asili na wa kisasa, maigizo, sarakasi, ushairi, vichekesho na mazingaombwe.

Amesema kuwa pia katika tamasha la hilo mwaka huu kutakuwa na wafanyabiashara watakaokuwa na bidhaa mbalimbali za asili.

“Tamasha la mwaka huu litakuwa la aina yake kwani maandalizi yote yalishakamilika na kwamba tunatarajia litahusisha wasanii kutoka ndani nan je ya nchi.

“Pia wageni wote watapata fursa ya kutembelea maeneo mbalimbali ya vivutio na utalii yakiwemo Mji Mkongwe, Kaole Ruins, Caravan Serai na Boma la Wajerumani,” amesema.

Ameongeza kuwa katika tamasha hilo kutakuwa na mada mbalimbali zitakazojadiliwa zikilenga kuwainua wasanii na kuwajengea uwezo.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Shaibu Ndemanga amesema kuwa wamejipanga vyema kuhakikisha wanaimarisha usalama zaidi na kila atakeyeshiriki tamasha hilo ataondoka salama.

“Niwatoe wasiwasi wadau wa sanaa na utamaduni kwamba tumejipanga vyema kuhakikisha usalama unaimarishwa na kila atakayehudhuria ataondoka salama,” amesema.


Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma akizungumza na waandishi wa habari leo Oktoba 22, 2024 Bagamoyo mkoani Pwani wakati akitoa taarifa kuhusu ujio wa Tamasha la 43 la Kimataifa la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) ambalo litafanyika Oktoba 23-26, 2024 katika viwanja vya TaSUBa.

 

Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma akizungumza na waandishi wa habari leo Oktoba 22, 2024 Bagamoyo mkoani Pwani wakati akitoa taarifa kuhusu ujio wa Tamasha la 43 la Kimataifa la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) ambalo litafanyika Oktoba 23-26, 2024 katika viwanja vya TaSUBa.


Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma akizungumza na waandishi wa habari leo Oktoba 22, 2024 Bagamoyo mkoani Pwani wakati akitoa taarifa kuhusu ujio wa Tamasha la 43 la Kimataifa la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) ambalo litafanyika Oktoba 23-26, 2024 katika viwanja vya TaSUBa.

Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Shaibu Ndemanga akizungumza na waandishi wa habari leo Oktoba 22, 2024 Bagamoyo mkoani Pwani wakati wakitoa taarifa kuhusu ujio wa Tamasha la 43 la Kimataifa la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) ambalo litafanyika Oktoba 23-26, 2024 katika viwanja vya TaSUBa.

Mkuu wa Taasisi ya TaSUBa, Dkt. Herbert Makoye akizungumza na waandishi wa habari leo Oktoba 22, 2024 Bagamoyo mkoani Pwani wakati wakitoa taarifa kuhusu ujio wa Tamasha la 43 la Kimataifa la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) ambalo litafanyika Oktoba 23-26, 2024 katika viwanja vya TaSUBa.

Mkuu wa Taasisi ya TaSUBa, Dkt. Herbert Makoye akizungumza na waandishi wa habari leo Oktoba 22, 2024 Bagamoyo mkoani Pwani wakati wakitoa taarifa kuhusu ujio wa Tamasha la 43 la Kimataifa la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) ambalo litafanyika Oktoba 23-26, 2024 katika viwanja vya TaSUBa.


Mkuu wa Taasisi ya TaSUBa, Dkt. Herbert Makoye akimuonesha baadhi ya picha ambazo zimechorwa na wanafunzi wa taasisi hiyo Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma mara baada ya kutembelea TaSUBa kukagua maandalizi ya Tamasha la 43 la Kimataifa la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) ambalo litafanyika Oktoba 23-26, 2024 katika viwanja vya TaSUBa.

Mkuu wa Taasisi ya TaSUBa, Dkt. Herbert Makoye akimuonesha baadhi ya picha ambazo zimechorwa na wanafunzi wa taasisi hiyo Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma mara baada ya kutembelea TaSUBa kukagua maandalizi ya Tamasha la 43 la Kimataifa la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) ambalo litafanyika Oktoba 23-26, 2024 katika viwanja vya TaSUBa.

Mkuu wa Taasisi ya TaSUBa, Dkt. Herbert Makoye akimuonesha baadhi ya picha ambazo zimechorwa na wanafunzi wa taasisi hiyo Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma mara baada ya kutembelea TaSUBa kukagua maandalizi ya Tamasha la 43 la Kimataifa la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) ambalo litafanyika Oktoba 23-26, 2024 katika viwanja vya TaSUBa.


Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma akimsikiliza Mkuu wa Taasisi ya TaSUBa, Dkt. Herbert Makoye wakati alipokuwa anaelezea namna walivyofanya maandalizi ya Tamasha la 43 la Kimataifa la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) ambalo litafanyika Oktoba 23-26, 2024 katika viwanja vya TaSUBa.


Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma akimsikiliza Mkuu wa Taasisi ya TaSUBa, Dkt. Herbert Makoye wakati alipokuwa anaelezea namna walivyofanya maandalizi ya Tamasha la 43 la Kimataifa la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) ambalo litafanyika Oktoba 23-26, 2024 katika viwanja vya TaSUBa.


Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma akiongozana na Mkuu wa Taasisi ya TaSUBa, Dkt. Herbert Makoye pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Shaibu Ndemanga wakati alipokuwa anatembelea na kukagua maandalizi ya Tamasha la 43 la Kimataifa la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) ambalo litafanyika Oktoba 23-26, 2024 katika viwanja vya TaSUBa.

(PICHA ZOTE NA EMMANUEL MBATILO)


Top News