Na Angela Msimbira, NZEGA

NAIBU Waziri, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe. Zainab Katimba amesisitiza kuwa uchangiaji katika sekta ya elimu usitumike kumuadhibu mwanafunzi ambaye mzazi wake kashindwa kutoa mchango.

Mhe.Katimba ameyasema hayo leo Julai 26, 2024 akiwa katika ziara ya kukagua miundombinu ya sekta ya elimu katika mamlaka za serikali za mitaa.

Katimba amesema michango yenye kiwango kikubwa inaondoa dhana ya serikali ya elimu bila malipo, hivyo halmashauri zote zinatakiwa kufuata miongozo ya uchangishaji shuleni.

“Nimeona hapa mnautaratibu wa kuchangisha wanafunzi na mmesema mnawachangisha laki sita kwa mwaka, hiki ni kiwango kikubwa, na kimsingi kinaondoa tafsiri ya elimu bila malipo.”

“Huwezi ukamwambia mzazi au ukamwambia mtanzania kwamba elimu bila malipo, anamleta mtoto shule anakutana na mchango mikubwa na sio kila mzazi atakuwa na uwezo wa kutoa."

Kuhusu changamoto ya ukosefu wa kichomea taka na uzio, Mhe.Katimba aliielekeza halmashauri ya Mji Nzega kutumia mapato ya ndani kutatua changamoto hiyo.

Amesema dhamira ya Rais Samia Suluhu Hassan ni kuhakikisha watoto wote wa kitanzania wanapata haki ya kumaliza mzunguko wao wa elimumsingi tena bila malipo.

“Masharti ya michango hii ni kwamba wale wazazi watakaoshindwa kwasababu fulani kutoa michango hii watoto wao wasiadhibiwe kwa kuwambiwa watoto wao wasiingie shuleni. Mchango haimaanishi mtoto akose haki ya kwenda shule kwasababu amekosa mchango wakati amelipiwa ada na Mheshimiwa Dk Samia Suluhu Hassan.

Kuhusu changamoto ya uzio na kichomea taka, Katimba aliiagiza halmashauri ya Nzega kutenga fedha kupitia mapato ya ndani ili kutatua changamoto hiyo.

Naye Afisa Elimu Sekondari Halmashauri ya Mji wa Nzega, Lulu Nchiha alisema wazazi wanachangia chakula chenye thamani ya Sh laki sita.








Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Deogratius Ndejembi akizungumza na viongozi pamoja na watumishi wa wizara ya Ardhi mkoa wa Dar es Salaam tarehe 26 Julai 2024 jijini Dar es Salaam.

Na Munir Shemweta, WANMM

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Deogratius Ndejembi amewataka watumishi wa sekta ya ardhi nchini kuongeza uadilifu na kutenda haki katika utekelezaji wa majukumu yao sambamba na kuongeza kasi katika utendaji kazi.

Mhe. Ndejembi namesema, suala la ardhi ni gumu na linahitaji watumishi kuwa makini ambapo amesisitiza kuwa ni lazima watumishi wa sekta ya ardhi watende haki huku wakizingatia kuwa kuna sheria, kanuni na miongozo inayowaoongoza katika utendaji kazi.

Aidha, Mhe. Ndejembi amesema, yale yote mazuri yaliyofanywa na mtangulizi wake ikiwemo Klinik za Ardhi atayaendendeleza kwa lengo la kuleta ufanisi wa wizara.

‘’Sikuja kutengua torati, yote aliyoyaanzisha mtanguluzi wangu ikiwemo klinik za ardhi zitaendelea na vile vile anayehisi jambo lake limekwama ajitokeze na atahudumiwa’’ amesema Mhe. Ndejembi.

Mhe. Ndejembi ametoa kauli hiyo tarehe 26 Julai 2024 wakati akizungumza na viongozi pamoja na watumishi wa Wizara ya Ardhi mkoa wa Dar es Salaam mara baada ya kutoka kuapishwa kushika nafasi hiyo kutoka kwa mtangulizi wake Mhe. Jerry Silaa.

Sambamba na hayo Waziri huyo wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi ametaka kuimarishwa kwa mifumo ndani ya wizara ili migogoro ya ardhi isiendelee kujitokeza.

Mhe. Ndejembi ameapishwa na Rais Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan kuwa Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi akitokea Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Watu wenye ulemavu).

Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Geophrey Pinda akizungumza mara baada ya kuwasili kwa waziri wa wizara hiyo Mhe. Deogratoius Ndejembi kwenye ofisi za wizara Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi Mhandisi Anthony Sanga akizungumza mara baada ya kuwasili kwa waziri wa wizara hiyo Mhe. Deogratoius Ndejembi katika ofisi za wizara Dar es Salaam.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi Lucy Kabyemera, Mkurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Hamad Abdallah na Kamishna wa Ardhi nchini Nathaniel Nhonge wakimsikiliza Waziri wa Ardhi Mhe. Deogratius Ndejembi (hayupo pichani) alipowasili kwa mara ya kwanza katika ofisi za ardhi Dar es Salaam tarehe 26 Julai 2024.
Sehemu ya watumishi wa wizara ya Ardhi.
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Deogratius Ndejembi akizungumza na Naibu waziri wake Mhe. Geophrey Pinda (kushoto) pamoja na Katibu Mkuu Mhandisi Anthony Sanga (kulia) alipowasili ofisi za ardhi Dar es Salaam mara baada ya kutoka kuapishwa tarehe 26 Julai 2024 jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Deogratius Ndejembi akizungumza na Naibu waziri wake Mhe. Geophrey Pinda (kushoto), Katibu Mkuu Mhandisi Anthony Sanga (wa pili kulia) pamoja na Naibu Katibu Mkuu Lucy Kabyemera alipowasili ofisi za ardhi Dar es Salaam mara baada ya kutoka kuapishwa  tarehe 26 Julai 2024 jijini Dar es Salaam.
Na Mwamvua Mwinyi,Mkuranga
Julai 26

Mkuu wa mkoani Pwani, alhaj Abubakar Kunenge amejinasibu kuwa ongezeko la viwanda mkoani humo litaongeza uzalishaji wa bidhaa na malighafi hali itakayosaidia kupunguza uagizaji wa bidhaa hizo nje ya nchi.

Kutokana na mafanikio hayo, azielekeza Taasisi wezeshi kuondoa ukiritimba kwa wawekezaji badala yake watumie nafasi zao kuwaelekeza taratibu zinazotakiwa ili kufikia malengo waliyowekwa.

Kunenge alieleza hayo wakati alipotembelea kiwanda cha Vioo KEDA Tanzania ,kata ya Mbezi, Mkuranga mkoani Pwani, ambacho hadi kukamilika kitagharimu fedha ya kimarekani 309,000,000usd ikiwa ni sawa na fedha ya kitanzania sh.bilioni 803.4.

Mkuu huyo wa mkoa, alieleza , mkoa huo hadi sasa una viwanda 1,535 kati ya hivyo vikubwa ni viwanda 124.

Kunenge alisema, Serikali inaendelea kushirikiana na wawekezaji ili kuinua uchumi wa mkoa na Taifa kijumla.

Alifafanua, uwepo wa viwanda utasaidia ongezeko la ajira, kuongeza pato la Taifa sanjali na kukuza sekta ya viwanda nchini.

Vilevile alizisisitiza, wilaya kusimamia mipango mji kwa kutenga maeneo ya viwanda hatua itakayosaidia kuondoa migogoro ya ardhi kati ya wananchi na wawekezaji wa viwanda.

Awali akitoa taarifa ya mradi, Ofisa biashara Ruby Zhu alisema, ujenzi wa mradi ulianza march 2023, mradi upo awamu kwanza ambapo utakamilika baada ya miezi 18 na awamu ya pili itaanza mwaka 2027.

"Wiki mbili ijayo tutafanya majaribio ya mashine na kupata gesi, na mwezi wa tisa wataanza uzalishaji ambapo kila siku watazalisha tani 600 na kwa mwaka watakuwa na uwezo wa kuzalisha tani milioni 219." alisema Ruby.

Ruby alieleza, wanatarajia kuwa na ajira zaidi 1,600, walianza uwekezaji mkoani Pwani kwa kuwekeza kiwanda cha marumaru Chalinze, Kiwanda cha taulo za watoto,sabuni KEDS Kibaha Mjini na Kiwanda cha Vioo Mkuranga.



Na Mwamvua Mwinyi,Mkuranga
Julai 26

Mkuu wa mkoani Pwani, alhaj Abubakar Kunenge amejinasibu kuwa ongezeko la viwanda mkoani humo litaongeza uzalishaji wa bidhaa na malighafi hali itakayosaidia kupunguza uagizaji wa bidhaa hizo nje ya nchi.

Kutokana na mafanikio hayo, azielekeza Taasisi wezeshi kuondoa ukiritimba kwa wawekezaji badala yake watumie nafasi zao kuwaelekeza taratibu zinazotakiwa ili kufikia malengo waliyowekwa.

Kunenge alieleza hayo wakati alipotembelea kiwanda cha Vioo KEDA Tanzania ,kata ya Mbezi, Mkuranga mkoani Pwani, ambacho hadi kukamilika kitagharimu fedha ya kimarekani 309,000,000usd ikiwa ni sawa na fedha ya kitanzania sh.bilioni 803.4.

Mkuu huyo wa mkoa, alieleza , mkoa huo hadi sasa una viwanda 1,535 kati ya hivyo vikubwa ni viwanda 124.

Kunenge alisema, Serikali inaendelea kushirikiana na wawekezaji ili kuinua uchumi wa mkoa na Taifa kijumla.

Alifafanua, uwepo wa viwanda utasaidia ongezeko la ajira, kuongeza pato la Taifa sanjali na kukuza sekta ya viwanda nchini.

Vilevile alizisisitiza, wilaya kusimamia mipango mji kwa kutenga maeneo ya viwanda hatua itakayosaidia kuondoa migogoro ya ardhi kati ya wananchi na wawekezaji wa viwanda.

Awali akitoa taarifa ya mradi, Ofisa biashara Ruby Zhu alisema, ujenzi wa mradi ulianza march 2023, mradi upo awamu kwanza ambapo utakamilika baada ya miezi 18 na awamu ya pili itaanza mwaka 2027.

"Wiki mbili ijayo tutafanya majaribio ya mashine na kupata gesi, na mwezi wa tisa wataanza uzalishaji ambapo kila siku watazalisha tani 600 na kwa mwaka watakuwa na uwezo wa kuzalisha tani milioni 219." alisema Ruby.

Ruby alieleza, wanatarajia kuwa na ajira zaidi 1,600, walianza uwekezaji mkoani Pwani kwa kuwekeza kiwanda cha marumaru Chalinze, Kiwanda cha taulo za watoto,sabuni KEDS Kibaha Mjini na Kiwanda cha Vioo Mkuranga.




RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na kuwasalimia Waumini wa Dini ya Kiislam, baada ya kumalizika kwa Ibada ya Sala ya Ijumaa iliyofanyika katika Masjid Taqwaa Meli Nne Mwanakwerekwe Wilaya ya Magharibi “B” Unguja leo 26-7-2024.(Picha na Ikulu)

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na Viongozi wa Dini alipowasili katika viwanja vya Masjid Taqwaa Mwanakwerekwe Meli Nne Wilaya ya Magharibi “B” Unguja, kuhudhuria Ibada ya Sala ya Ijumaa iliyofanyika katika Masjid hiyo leo 26-7-2024.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na Wananchi baada ya kumalizika kwa Ibada ya Sala ya Ijumaa, iliyofanyika katika Masjid Taqwaa Meli Nne Mwanakwerekwe Wilaya ya Magharibi “B” Unguja leo 26-7-2024.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa katika picha ya pamoja na Watoto, baada ya kumalizika kwa Ibada ya Sala ya Ijumaa, iliyofanyika katika Masjid Taqwaa Meli Nne Mwanakwerekwe Wilaya ya Magharibi “B” Unguja leo 26-7-2024.(Picha na Ikulu)

-Zege yapigwa chapuo, magogo kuzuiwa

SERIKALI kupitia Wizara ya Madini, Tume ya Madini imepata mwarobaini wa kupunguza majanga kwenye migodi kwa kuwaelimisha wachimbaji wadogo kutumia zege kwenye kingo za miamba badala ya magogo.

Akizungumza leo Julai 26, 2024 katika mafunzo ya kuwajengea uwezo watumishi wa Tume ya Madini kutoka Idara ya Ukaguzi wa Migodi na Mazingira yaliyofanyika jijini Dodoma, kwa niaba ya Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Meneja wa Mazingira Mhandisi Ephraim Mushi amesema njia mbadala ya zege kwa wachimbaji wadogo itasaidia kuondoa tatizo la ajali migodini kwa watu kupoteza maisha na wengine kuwa walemavu.

“Wachimbaji wadogo wanatumia magogo maarufu kama matimba kwa kuweka kingo kwenye miamba, sasa njia hii imeonekana sio salama kwa uchimbaji mdogo kwa maana yanakaa baada ya muda yanaoza, yanaanguka na kusababisha ajali kwenye migodi,”amesema Mhandisi Mushi na kuongeza,

“Lakini pia imeonekana wachimbaji wadogo wanatumia sana haya magogo ambayo kimsingi yanaleta uhabiribifu wa mazingira, Wizara ya Madini kupitia Tume ya Madini tumeona kuna haja ya kuja na njia mbadala ili kupunguza au kuondoa kabisa ajali migodini.

“Idara ya Ukaguzi wa Migodi na Mazingira, elimu hii tutaenda kuitoa kwa wachimbaji wadogo, namna ya kukinga na zege ili miamba inapoanguka isije kuleta madhara kwa wachimbaji, wakiweza kwenda na huu mfumo uzalishaji utaongezeka na utakuwa na tija na vifo vya wachimbaji vitapungua na mapato ya serikali yataongezeka,”amesisitiza Mushi.

Naye Mjiolojia Mwandamizi Fabian Mshai akitoa shukrani kwa wakufunzi kwa niaba ya washiriki amesema mafunzo waliyoyapata yamejenga uwezo zaidi, ari na nguvu mpya kwa wakaguzi wa migodi na mazingira katika kutekeleza majukumu yao.

Amesema kuwa ili uchimbaji wa madini uwe endelevu lazima kuwe na usalama, kusiwe na ajali na utunzaji wa mazingira kwa manufaa ya kizazi cha sasa na cha baadaye na ina umuhimu katika kukuza sekta ya madini nchini.

“Elimu hii tutaishusha chini kwa wachimbaji wadogo sambamba na kukagua hali ya usalama mara kwa mara ili kuwasaidia wachimbaji kuepuka ajali wakati wa utekelezaji wa shughuli zao.

Mafunzo hayo yalianza rasmi Jumatatu Julai 22 hadi leo Julai 26, 2024 ambapo mawasilisho mbali mbali yaliwasilishwa na wakufunzi Mhandisi Gervas Wiliam kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Mhandisi Selemani Msangi kutoka Kampuni ya HETAMIS, Mhandisi Japhet Mmary kutoka Shanta Mining Co. Ltd, Fikiri Juma kutoka Bulyanhulu Gold Mine na Fey Kidee kutoka Kidee Mining (T) Ltd.






Na. Mwandishi Jeshi Dar es Salaam.

Fainali ya wiki ya nenda kwa Usalama kupigwa Julai 27,2024 katika viwanja vya chuo cha Taaluma ya Polisi DPA ambapo itawakutanisha timu kutoka jimbo la Kibamba na timu kutoka Jimbo la Segerea.

Akitoa taarifa ya fainali hiyo leo Julai 26,2024 mratibu wa Mashindano hayo Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Muhidini Mpinga amesema mtanange huo utapigwa kesho kuanzia muda wa saa tisa alasiri katika Viwanja vya chuo cha Taaluma ya Polisi Dar es Salaam.

Aidha Mpinga amebainisha kuwa katika fainaili hiyo elimu ya Usalama Barabarani itatolewa kabla na baada ya Mashindano hayo ambayo yamebeba kauli mbiu isemayo endesha salama Ufike Salama.

Ameongeza kuwa kutokana na umahiri na umaarufu wa Mashindano hayo yaliyojichukulia sifa kubwa katika kuibua vipaji na kufikisha ujumbe kwa Jamii katika matumizi sahihi ya Barabara kutakuwepo burudani kutoka kwa wasanii wa hapa nchini.

Vile vile ametumia fursa hiyo kuwashukuru kampuni ya uuzaji wa pikipiki ya King Lion ambao wanauza pikipiki za mataili mawili na matatu.

Sambamba na hilo amewakaribisha wananchi katika viwanja vya Chuo Cha Taaluma ya Polisi Dar es Salaam ili kushuhudia mtanange huo wa kutaka nashoka ambao unawakutanisha vijana wa kabumbu kutoka Kipamba na Segerea.

KAMISHNA Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Yusuph Mwenda amekutana na kuzungumza na wafanyabiashara mkoani Dodoma. 

Akizungumza na wafanyabiashara hao Julai 24 mwaka huu, Kamishna Mwenda ameahidi kufanya kazi kwa ukaribu na wafanyabiashara hao pamoja na kutatua changamoto zao za kikodi kwa wakati ili kuleta ari ya ulipaji kodi wa hiari.

Wafanyabiashara hao wamemshukuru na kumpongeza Kamishna Mkuu huyo kwa kutenga muda wake na kuwasikiliza na kujenga ari ya kulipa kodi kwa hiari.





 

Raisa Said, Tanga

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) imetakiwa kuandaa mkakati shirikishi na asasi za kiraia na mashirika yasiyo ya kiserikali mkoani Tanga ili kupambana na rushwa wakati wa uchaguzi ujao.

Wito huu wa kuchukua hatua ulitolewa wakati wa semina ya siku moja iliyoandaliwa na TAKUKURU Julai 26 na kuhudhuriwa na viongozi kutoka AZAKi, NGOs, na wakala wa serikali.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Huduma ya Kujitolea kwa Jamii Tanzania (CVS), Simon Mashairi akifafanua hisia za washiriki wa mkutano huo ambapo alisisitiza umuhimu wa mkakati wa shirikishi wa kuongeza uelewa wa rushwa na kubainisha kuwa rushwa inazidi kukita mizizi katika jamii.

“Watu wana uelewa duni wa rushwa na athari zake katika haki yao ya kuchagua viongozi bora, jambo ambalo linapochangiwa na umaskini, huwafanya wawe rahisi kuhongwa,” alisema Mashairi ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa VCS.

Mashauri aligundua changamoto kubwa: ukosefu wa fedha kwa ajili ya kampeni zinazofaa za uhamasishaji." Ni lazima pia tufikirie kutumia teknolojia ya kisasa ya kidijitali, kama vile kuunda programu maalum au kutangaza ujumbe kupitia mitandao," alipendekeza mwanasiasa huyo.

Pia alihimiza ufuatiliaji na tathmini ya kina ya juhudi za kupambana na rushwa wakati wa uchaguzi ili kuepuka kurudia makosa na kuimarisha mikakati.

Bibi Mwaimu wa Msaada wa Kisheria kwa Wanawake na Watoto (WOLEA) alisisitiza kwamba, wakati kampeni za uhamasishaji zikifanyika kila mzunguko wa uchaguzi, hakuna tathmini iliyofanywa ya jinsi rushwa inavyoathiri mchakato wa uchaguzi.

Victor Swila, Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Tanga, alikubaliana na umuhimu wa kushirikiana kwa karibu na AZAKi na Mashirika Yasiyo ya Kiserikali, huku akibainisha kuwa mashirika hayo yanafanya kazi moja kwa moja na wananchi. "TAKUKURU haiwezi kumfikia kila mtu nchini Tanzania; kwa hiyo, tunahitaji kushirikisha AZAKi," alisema, akiahidi kuongezeka kwa ushirikiano na mashirika hayo.

Mwenyekiti wa Jukwaa la Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Mkoa wa Tanga, Goodluck Malilo, alieleza kuwa AZAKi na Mashirika Yasiyo ya Kiserikali ni lazima kutambua wajibu wao katika jamii. Malilo aliyataka mashirika hayo kuchangamkia fursa hiyo kwa ushirikiano wa karibu na TAKUKURU.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Balozi Dk.Batilda Buriani, alifungua semina hiyo kwa kuzitaka Asasi za kiraia kuisaidia TAKUKURU kuongeza uelewa wa masuala ya rushwa ili watu waweze kufanya maamuzi sahihi.

Pia alionya AZAKi na AZISE dhidi ya kutekeleza programu zinazokiuka maadili na sheria za kitaifa za Tanzania. "Ukikubali pesa za wafadhili na ukubaliane na chochote wanachotaka kwa sababu tu unahitaji ufadhili," alionya, akitoa mfano wa mashirika yanayoshinikizwa kuunga mkono mila kama vile mahusiano ya jinsia moja.







Madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, wamemchagua Michael Urio (Diwani wa Kata ya Kunduchi ), kuwa Naibu Meya Mteule wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni.

Michael Urio ameshinda uchaguzi wa kiti cha unaibu Meya kwa kura 16 kati ya 26 za wabunge na madiwani wa kinondoni kwenye uchaguzi uliofanyika LEO.

Uchaguzi huo umefanyika ikiwa ni baada ya kumalizika kwa kipindi cha mwaka mmoja cha uongozi wa Naibu Meya aliyekuwa madarakani ambaye ni Joseph Rwegasira.

Uchaguzi huo wa ndani ya chama cha mapinduzi ulihusisha wagombea wawili ambao ni Joseph Rwegasira aliyekuwa akitetea kiti chake na Michaeli Urio (Diwani wa Kunduchi)

Akizungumza baada ya uchaguzi huo, Urio alisema , “Ninawashukuru sana waheshimiwa madiwani kwa kuonyesha imani kubwa kwangu, naomba niwahakikishie kwa kushirikiana na Mstahiki meya tutahakikisha tunafanyakazi kwa pamoja ili kuwaletea maendeleo wananchi wetu ndani ya Manispaa yetu ya kinondoni.”


Uchaguzi huo ulisimamiwa na Meya wa Kinondoni Mnyonge Songoro, ambae alikuwa mwenyekiti wa uchaguzi songoro.

Akizungumza kwa niaba ya chama cha mapinduzi Mwendez wa CCM wilaya ya Kinondoni Lilian Lwebangila alisema chama cha mapinduzi ni wako,mavu katika chaguzi na aliwaasa Naibu Meya aliyemaliza muda na huyu alieshinda kushirikiana katika kuijenga Kinondoni


Makundi hayakosi ndani ya chaguzi lakini baada ya kumalizika kwa uchaguzi sisi woote ni wamoja alimaliza na kumponeza Urio kwa kuteuliwa kuwa Naibu Meya Kinondoni.


 

MKUU wa Mkoa wa Dodoma Bi Rosemary Senyamule amethibitisha kukamilika kwa maadalizi ya msimu wa tano mbio za NBC Dodoma Marathon huku akionyesha kuridhishwa na ubora wa mbio hizo sambamba na mchango wake katika kuchochea kasi ya Uchumi wa mkoa huo kupitia sekta za biashara, michezo na utalii.

Mbio zinatarajiwa kufanyika Julai 28 mwaka huu kwenye Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma zikiwa na lengo la kukusanya fedha ili kusaidia mapambano dhidi ya saratani ya shingo ya kizazi na kutoa ufadhili wa elimu kwa wakunga ili kuboresha afya ya mama na mtoto. Waziri Mkuu Kassim Majaliwa anatarajiwa kuongoza washiriki zaidi ya 8,000 waliothibitisha kushiriki mbio hizo.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma leo RC Senyamule pamoja na kuipongeza benki hiyo kwa maandalizi hayo mazuri alisema ujio wa mbio hizo mkoani humo kwa miaka mitano sasa umekuwa ukiambatana na fursa mbalimbali ikiwemo ongezeko la mzuguko wa fedha unaotokana na ongezeko la mahitaji ya chakula, vinywaji,mavazi na malazi kutona na idadi kubwa ya watu wanaotoka mikoa mbalimbali ili kushiriki mbio hizo jijini humo.

“Kukamilika kwa maadalizi ya mbio hizo tena katika viwango vya kimataifa kunatoa taswira sahihi ya hadhi ya mbio hizo na jiji la Dodoma kama makao makuu ya nchi. Nitoe wito kwa wananchi wa jiji la Dodoma hususani wafanyabiashara kuchangamkia fursa mbalimbali zitokanazo na ongezeko hili la watu ambao nje ya washiriki hao 8,000 waliothibitisha kushiriki pia wapo wengine zaidi walioambatana nao.’’ Alisema.

Aidha, Bi Senyamule aliowamba washiriki wa mbio hizo kutumia fursa hiyo pia kutembelea vivutio mbalimbali vya utalii vilivyomo mkoani humo ukiwemo utalii wa majengo ya serikali kama vile Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ikulu, Mji wa serikali sambamba na utalii wa utamaduni ikiwemo ngoma za asili za wenyeji wa mkoa huo ambao ni kabila la Wagogo huku pia wakipata wasaa wa kujionea kilimo cha zao la zabibu ambalo kwa Afrika Mashariki linalimwa mkoa huo pekee.

“Zaidi nitoe wito kwa wananchi wajitokeze kwa wingi kandokando ya Barabara ili kushangilia na kuwapa nguvu washiriki wa mbio hizo watakaotumia baadhi ya barabara hapa mjini. Kwa wale ambao hawatakuwa na ulazima wa kutumia magari yao ni vema wasiingie nayo barabarani ili kupunguza msongamano wa vyombo hivyo barabarani ili kuepuka ajali na usumbufu kwa washiriki wa mbio hizi,’’ aliongeza.

Awali akizungumza kwenye mkutano huo, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Mahusiano ya Umma wa Benki ya NBC, ambayo ndio inaratibu mbio hizo Bw Godwin Semunyu alisema maandalizi yote yamekamilika na tayari washiriki mbalimbali wa mbio zinazohusisha umbali wa km 5, km 10, km 21 na km 42 wanaendelea kuingia jijini humo ili kushiriki mbio hizo.

“Ili kuongeza mchango wa mbio hizi kiuchumi na burudani zaidi tumebuni matukio kadhaa likwemo tamasha la kuonja mvinyo yaani ‘Wine Testing Festival’ litakalofanyika Julai 27 hapa Dodoma na zaidi tumeandaa matukio mengine ya burudani za vichekesho na tafrija mbalimbali lengo likiwa ni kuongeza burudani wa washiriki wa mbio hizi hususani wageni huku pia tukilenga kuchochea mzunguko wa fedha ili kuwanufaisha zaidi wenyeji wa jiji hili,’’ alisema Semunyu huku akiwashukuru wadau mbalimbali wakiwemo wadhamini wa mbio hizo kufanikisha matukio hayo.

Akuizungumza kwa niaba ya wadau hao, Mkuu wa Kanda ya Kati wa Kampuni ya Mawasiliano ya Vodacom Tanzania Bw Joseph Sayi alisema kampuni hiyo ikiwa kama mdau mkuu wa mawasiliano kwenye mbio hizo imejipanga kutoa huduma ya mawasiliano ya internet bure kwa washiriki wote wa mbio hizo.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Bi Rosemary Senyamule  (wa pili kulia) akipokea sweta maalum la mbio za NBC Dodoma Marathon kutoka kwa Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Mahusiano ya Umma wa Benki ya NBC, Godwin Semunyu (wa pili kushoto) na Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya mbio hizo Bi Tasiana Massimba (Kulia) ikiwa ni ishara ya kumkaribisha rasmi mkuu wa mkoa huyo kwenye mbio hizo zinazotarajiwa kufanyika Julai 28 mwaka huu kwenye Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma. Mbio hizo zinalenga kukusanya fedha ili kusaidia mapambano dhidi ya saratani ya shingo ya kizazi na  kutoa ufadhili wa elimu kwa wakunga  ili kuboresha afya ya mama na mtoto makabiziano hayo yamefanyika  makao makuu ya benki hiyo jijini Dodoma leo. Kushoto ni Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma Bi Joyce Fisoo.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Bi Rosemary Senyamule  (kulia) akitapata maelezo kuhusu alama mbalimbali ziliwekwa kwenye sweta maalum la mbio za NBC Dodoma Marathon kutoka kwa Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Mahusiano ya Umma wa Benki ya NBC, Godwin Semunyu (wa pili kushoto) baada ya kukabidhiwa sweta hilo ikiwa ni ishara ya kumkaribisha rasmi mkuu wa mkoa huyo kwenye mbio hizo zinazotarajiwa kufanyika Julai 28 mwaka huu kwenye Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma. Mbio hizo zinalenga kukusanya fedha ili kusaidia mapambano dhidi ya saratani ya shingo ya kizazi na  kutoa ufadhili wa elimu kwa wakunga  ili kuboresha afya ya mama na mtoto makabiziano hayo yamefanyika  makao makuu ya benki hiyo jijini Dodoma leo. Kushoto ni Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma Bi Joyce Fisoo.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Bi Rosemary Senyamule  (katikati) akiwaonesha waandishi wa habari (hawapo pichani) moja ya fulana maalum  za mbio za NBC Dodoma Marathon mwaka 2024 mara baada ya kukabidhiwa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Mahusiano ya Umma wa Benki ya NBC, Godwin Semunyu (kushoto) na Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya mbio hizo Bi Tasiana Massimba (Kulia) ikiwa ni ishara ya kumkaribisha rasmi mkuu wa mkoa huyo kwenye mbio hizo zinazotarajiwa kufanyika Julai 28 mwaka huu kwenye Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma. Mbio hizo zinalenga kukusanya fedha ili kusaidia mapambano dhidi ya saratani ya shingo ya kizazi na  kutoa ufadhili wa elimu kwa wakunga  ili kuboresha afya ya mama na mtoto makabiziano hayo yamefanyika  makao makuu ya benki hiyo jijini Dodoma leo.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma leo RC Senyamule (pichani) pamoja na kuipongeza benki ya NBC  kwa maandalizi hayo mazuri alisema ujio wa mbio hizo mkoani humo kwa miaka mitano sasa umekuwa ukiambatana na fursa mbalimbali ikiwemo ongezeko la mzunguko wa fedha unaotokana na ongezeko la mahitaji ya chakula, vinywaji,mavazi na malazi kutona na idadi kubwa ya watu wanaotoka mikoa mbalimbali ili kushiriki mbio hizo jijini humo.

Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya mbio za NBC Dodoma Marathon Bi Tasiana Massimba (Pichani) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kukamilika kwa mbio hizo zinazotarajiwa kufanyika Julai 28, mwaka huu jijini Dodoma.

Awali akizungumza kwenye mkutano huo, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Mahusiano ya Umma wa Benki ya NBC, ambayo ndio inaratibu mbio hizo Bw Godwin Semunyu (pichani) alisema maandalizi yote yamekamilika na tayari washiriki mbalimbali wa mbio zinazohusisha umbali wa km 5, km 10,km  21 na km 42 wanaendelea kuingia jijini humo ili kushiriki mbio hizo.

Akizungumza kwenye mkutano huo Mkuu wa Kanda ya Kati wa Kampuni ya Mawasiliano ya Vodacom Tanzania Bw Joseph Sayi (pichani) alisema kampuni hiyo ikiwa kama mdau mkuu wa mawasiliano kwenye mbio hizo imejipanga kutoa huduma ya mawasiliano ya internet bure kwa washiriki wote wa mbio hizo.

Baadhi ya wajumbe wa kamati ya maandalizi ya mbio za NBC Dodoma Marathon wakifutilia mkutano huo.



 


Top News