Tanzania imezindua rasmi Mfuko wa iDollar, ambao ni mfuko wa kwanza wa soko la pesa nchini unaotumia Dola za Kimarekani (USD).

Mfuko huu unawawezesha wawekezaji kusimamia ukwasi wa dola kwa njia salama na yenye ufanisi huku wakipata mapato ya ushindani.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam wakati wa hafla ya uzinduzi rasmi, Nicodemus Mkama, Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA), alisema hatua hii ni mafanikio makubwa katika ukuaji na kisasa cha masoko ya mitaji nchini.

“Kwa uzinduzi huu, Tanzania inaungana na nchi nne za Afrika—Kenya, Afrika Kusini, Mauritius na Ghana—ambazo tayari zina mifuko ya uwekezaji kwa dola inayodhibitiwa na mamlaka zao za masoko ya mitaji,” alisema.

Mkama alisema mfuko huo utawekeza kwenye aina mbalimbali za vyombo vya mapato ya kudumu vinavyotumia dola za kimarekani, ikiwa ni pamoja na hatifungani za kampuni, amana za muda maalum, na akaunti za simu.

Uwekezaji huu wa mseto unaanzisha darasa jipya la rasilimali katika soko la ndani, kupanua chaguzi za wawekezaji na kuvutia fedha za kigeni katika mifumo rasmi.

Alisisitiza kuwa mfuko huo unatoa fursa kwa Watanzania, hasa wale wenye akiba ya dola, kuwekeza ndani ya nchi badala ya kutafuta fursa hizo nje ya mipaka.

“Kwa uchumi wetu, mfuko huu ni nyenzo muhimu ya kuhamasisha fedha za kigeni, kuongeza utulivu wa kiuchumi, na kuimarisha uwezo wetu wa kukabiliana na mishtuko ya nje,” aliongeza.

Mfuko huo pia umetengenezwa ili kuwahudumia Watanzania waishio nje ya nchi (diaspora), kwa kuwawezesha kuwekeza mapato yao ya kigeni nyumbani kupitia mifumo salama na inayodhibitiwa.



“Diaspora mara nyingi hutuma fedha kwa dola za Marekani ambazo si kwa matumizi ya haraka. iDollar inawapa njia rahisi ya kutunza na kuwekeza fedha hizo ndani ya Tanzania,” alieleza.

“Leo si tu kusherehekea kuzinduliwa kwa bidhaa, bali pia ni hatua ya kuimarisha imani katika maendeleo ya sekta ya fedha ya Tanzania. Ni ushahidi wa nafasi muhimu ya mdhibiti, sekta binafsi na wawekezaji kufanya kazi kwa pamoja kuelekea lengo la pamoja la ukuaji jumuishi na dhabiti wa uchumi wetu,” aliongeza.



Kwa upande wake, Profesa Mohamed Warsame, Mkurugenzi wa iTrust Finance, alisema mfuko huo unawapa wawekezaji fursa ya kuwekeza kwenye mali zinazotumia dola huku wakilindwa dhidi ya kushuka kwa thamani ya sarafu ya ndani.

“Wawekezaji watapata mapato kwa Dola kupitia vyombo vya fedha vinavyotumia dola. Utoaji wa fedha ni rahisi—wawekezaji wanaweza kutoa fedha kwa dola au kuzibadilisha kuwa pesa za Kitanzania pale inapohitajika,” alisema.



Mfuko pia unatumia majukwaa ya kidijitali—ikiwemo programu za simu—ambazo hurahisisha usajili kwa wawekezaji wa ndani na wa diaspora kushiriki kwa urahisi na kufuatilia uwekezaji wao wakiwa popote.

Alexander Ngusaru, Mkurugenzi wa Hazina na Masoko ya Mitaji kutoka Benki ya CRDB Plc, alisema:

“Hii si bidhaa tu—ni lango la kuingia kwenye uwekezaji wa kimataifa na ni alama ya maendeleo ya kitaifa. CRDB inajivunia kuunga mkono mafanikio haya kwa uadilifu, ubunifu, na athari ya muda mrefu.”

Mfuko wa iDollar ni hatua kubwa ya maendeleo kwa sekta ya fedha ya Tanzania, ukilinganisha na mitazamo ya kimataifa ya uwekezaji, huku ukiwawezesha wawekezaji wa ndani na waishio nje ya nchi (diaspora) kushiriki kwa urahisi.












Dar es Salaam, Tanzania – Mwanaharakati maarufu wa kimataifa wa haki ya elimu, Mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel na Mjumbe Maalum wa Umoja wa Mataifa, Malala Yousafzai (pichani), anatarajiwa kuwasili nchini Tanzania wiki hii kwa ziara ya kikazi ya siku kadhaa kwa mwaliko wa Global Partnership for Education (GPE), ambayo Mwenyekiti wake ni Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete.


Hii itakuwa ni mara ya kwanza kwa Malala kutembelea Tanzania, ambapo atashiriki shughuli mbalimbali zinazolenga kuhamasisha haki ya elimu kwa watoto, hususan wasichana. Akiwa nchini, Malala atakutana na viongozi wa serikali, wadau wa sekta ya elimu, na kujionea namna elimu, sanaa na michezo vinavyotumika kama njia ya kukuza mwamko wa elimu katika jamii.


Akizungumza kuhusu ziara hiyo, Malala amesema:
“Hii ni mara yangu ya kwanza kufika nchini Tanzania. Nitasherehekea Siku ya Malala pamoja na jamii kwa kuonesha mshikamano na wasichana wa Tanzania, kupaza sauti zao na kujifunza kutoka kwenye mafanikio yao.”


Tarehe 12 Julai ambayo ni siku ya kuzaliwa kwa Malala, imekuwa ikiadhimishwa kimataifa kama Siku ya Malala Duniani tangu mwaka 2013, kufuatia hatua ya Umoja wa Mataifa kuenzi mchango wake mkubwa katika kupigania haki ya elimu kwa wasichana – harakati ambazo zilimfanya kushambuliwa kwa risasi na kundi la Taliban akiwa njiani kurejea nyumbani kutoka shule akiwa na umri wa miaka 15.


Katika ziara hii, Malala atakuwa pia anatekeleza majukumu yake kupitia Malala Fund, taasisi aliyoiunda pamoja na Shiza Shahid yenye lengo la kupigania upatikanaji wa elimu bora kwa wasichana kote duniani.


Kuhusu Malala Yousafzai

Malala alizaliwa tarehe 12 Julai 1997 huko Swat, Pakistan. Alianza harakati za kutetea elimu akiwa na umri wa miaka 11 kwa kuandika blogu kupitia BBC Urdu chini ya jina la “Gul Makai,” akielezea maisha ya wasichana chini ya utawala wa Taliban. Mwaka 2012, alijeruhiwa kwa kupigwa risasi kichwani na Taliban kutokana na harakati zake, tukio lililoibua mshikamano mkubwa wa kimataifa.


Alihamia Uingereza kwa matibabu, akaendelea na masomo na harakati zake za kimataifa, na kisha kuhitimu Shahada ya Falsafa, Siasa na Uchumi (PPE) katika Chuo Kikuu cha Oxford mwaka 2020. Ametunukiwa tuzo mbalimbali ikiwemo Sakharov Prize, uraia wa heshima wa Canada, na kutajwa mara kadhaa na jarida la TIME miongoni mwa watu 100 wenye ushawishi mkubwa duniani.


Kuhusu Global Partnership for Education (GPE)

GPE ni mfuko mkubwa zaidi wa kimataifa unaojikita kikamilifu katika kuimarisha sekta ya elimu katika nchi zenye kipato cha chini. Kwa zaidi ya miongo miwili, GPE imekuwa ikitoa rasilimali na usaidizi wa kimkakati kujenga mifumo imara ya elimu, kwa lengo la kuhakikisha watoto wengi zaidi – hususan wasichana – wanapata elimu wanayohitaji ili kustawi na kuchangia katika maendeleo ya dunia.


GPE huleta pamoja serikali, wafadhili, mashirika ya kimataifa, asasi za kiraia, vyama vya walimu, vijana na sekta binafsi katika juhudi za pamoja za kuleta mageuzi ya elimu.

Mkemia Mkuu wa Serikali Dkt.Fidelice Mafumiko akizungumza na Wahariri na Waandishi wa Habari kuhusiana na Mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Sita ya Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan.




 Baadhi ya Matukio wakati wa Mkutano wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali na Wahariri.


*Yakusanya mapato ya zaidi ya Bilioni 36

Na Mwandishi Wetu
MAMLAKA ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali (GSLA) imesema kuwa kwa mwaka 2023 hadi 2025 wamekusanya zaidi ya Bilioni 36 ambapi makusanyo hayo inatokana Serikali ya awamu ya Sita ya Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kuwekeza kwenye maabara ya Taasisi hiyo.

Akizungumza na waandishi wa Wahariri na Waandishi wa Habari katika vikao vinavyiratibiwa na Ofisi ya Msajili wa Hazina ,Mkemia Mkuu wa Serikali Dkt.Fidelice Mafumiko amesema makusanyo hayo yanatokana na uelewa wa wadau kuhusiana na kupata huduma katika ofisi hiyo.

Amesema katika mapato waliyoyapata wamefikia lengo la asilimia 92 waliojipangia katika kipindi hicho.

Dkt.Mafumiko amesema ongezeko hili ni kutokana na ushirikiano na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan,yamejikita Mwaka Fedha 2021/2022 hadi kufikia sampuli 188,362 kwa mwaka wa Fedha 2023/2024, sawa na ongezeko laasilimia 21. Katika kipindi cha mwaka wa Fedha huu.

Dkt.Mafumiko amesema Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali ni mojawapo ya taasisi za Serikali Majukumu ya msingi ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali yamebainishwa usalama na ubora wake ,uchunguzi wa sampuli/vielelezo vyenyemaslahi ya Kitaifa kwa ajili ya Kulinda Afya, Mazingirana usalama wa nchi.

Amesema Mamlaka ilianzishwa chini ya Sheria ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Sheria

katika mazingira zikiwemo sampuli za uchafuzi wa hewa, maji, na afya za wananchi,Usimamizi na Udhibiti wa Kemikali za Viwandani na Majumbani uchunguzi zitolewazo na Mamlaka.

Amesema Sura Na. 182. Sheria hiyo inatoa nguvu ya kisheria kwa Mamlaka kufanya ukaguzi na kusajili

unaoweza kusababisha kemikali hizo kutumika kutengeneza dawa za kulevya au kutumika katika Huduma za uchunguzi wa Kimaabara, Utoaji wa Ushahidi wa Kitaalam, na Usimamizi ,Ongezeko la sampuli zinazochunguzwa na Mkemia Mkuu wa Serikali linatokana na taasisi za serikali za udhibiti kama vile Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Madawa wa 2024/2025, kuanzia mwezi Julai hadi Mei 2025,sampuli 175,561zilifanyiwa Kisayansi wa kimaabara kwa sampuli/vielelezo umeongezeka kutoka sampuli 155,817 kama silaha za maangamizi.

Hata hivyo amesema madhumuni yaliyokusudiwa ikiwa ni pamoja na kuzuia uchepushaji wa baadhi ya kemikali wadau wote wanaojishughulisha na shughuli za kemikali zikiwemo kemikali hatarishi ,Udhibiti wa Kemikali za Viwandani na Majumbani, ujenzi wa miundombinu wezeshi ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan.

Mafanikio ya Mamlaka kwa kipindi cha miaka minne cha awamu ya sita chini ya Uongozi wa

Usimamizi na Udhibiti wa kemikali chini ya Sheria ya Kemikali za Viwandani na Majumbani, Afya ya binadamu na mazingira.

Lengo la kusajili na kukagua ni kuhakikisha kuwa, kemikali hizo zinatumika kwa kuzingatia usalama kwa afya za watu na mazingira na pia kwa ofisi na maabara, uimarishaji wa matumizi ya TEHAMA katika utoaji na mafunzo kwa wadau.

Dkt.Mafumiko amesema katika uuimarisha Huduma za Uchunguzi wa Kimaabara uchunguzi sawa na asilimia 92 ya lengo la kuchunguza sampuli 191,420.

Amesema ufanisi katika utoaji wa huduma za Uchunguzi wa kimaabara kuongezekakwa uelewa wa wananchi na wadau wa Mamlakana ubora wa huduma za Katika kipindi cha miaka minne cha Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt.Samia Sukuhu Hassan Mkemia Mkuu Dkt.Mafumiko amesema kuwa katika kufanya kazi wanashiriakina na Mamlaka ya Kupambana na Kudhiti Dawa za Kulenya (DCEA),Jeshi la Polisi na Mamlaka ya Mapato (TRA), wadau wa afya.

Amesema wanafanya utambuzi wa miili ya Wahanga iliyoharibika vibaya kutokana na majanga ,Utambuzi wa sumu kabla ya kifo kutokea kwa kubainisha Uchunguzi wa kisayansi wa kimaabara umekuwa na mchango mkubwa katika kusaidia utambuzi wa jinsi tawala, Kufanya uchunguzi wa kisayansi wa kimaabara sumu ili kupata tiba sahihi na kwa wakati, sumu iliyosababisha kifo kwa waathirika,Kusafishwa figo,kufanya uchunguzi wa sampuli za maji tiba

kuchangia katika mnyororo wa Haki Jinai na hivyo kuwezesha utoaji wa haki stahiki Usimamizi wa Mazingira(NEMC)na wadau wengine wanaotumia huduma za Mamlaka.

Amesema wagonjwa wanaodhaniwa kuvuta, kunywa au kula chakula chenye jamii na mazingira inalindwa kwa wagonjwa wenye changamoto ya jinsi, utambuzi wa sumu baada ya kifo kutokea kwa kubanisha katika vyombo vya maamuzi kwa mhusika na kwa wakati wa Kupandikizwa figo kwa kufanya uchunguzi wa kimaabara kubainisha Mchango wa utoaji wa matokeo ya Uchunguzi wa Sampuli kwa wakati dawa asili),mazingira, usalama mahala pa kazi kwa lengo la kuhakikisha afya yanayotumika kwa wagonjwa wanaohitaji kusafisha figo,kutoa ushauri stahiki kwa Madaktari Bingwakwa lengo la kutoa matibabu mbalimbali ikiwemo ajali za majini, magari, kuangukiwa na majengo, moto, ndege.

Hata hivyo amesema Uwekezaji katika mitambo na vifaa vya kisasa vya uchunguzi kimaabara imefanikiwa kuendelea ya Kisheria na mifumo ya Ubora katika ngazi ya kitaifa na kimataifa viwango vya kitaifa na Kimataifa. Kukubalika huko kwa matokeo ya uchunguzi ya Chakula.

Amesema mwaka 2024/2025 GSLA imeongeza mitambo mikubwa 16 na midogo 274 katika Utoaji wa Huduma za Kimaabara katika Viwango vya Kimataifa
 utoa huduma za Uchunguzi wa Kimaabara na matokeo yake kukubalika na umeongezeka kwa shughuli za Mamlaka uliyohuishwa kwa mara nne mfululizo na mfumo wa IthibatiKatika kipindi cha miaka mine cha Serikali ya awamu ya sitapekee, Mamlaka imefanikiwa Katika kipindi cha Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Rais wa Jamhuri ya ssilimia 23.6, kutoka Shilingi Bilioni 13.6kwa mwaka wa fedha 2017/2018 na Mamlaka kutekeleza mifumo miwili ya ubora na umahiri ya kimataifa, 2021/2022 hadi kufikia thamani ya jumla ya Bilioni 17.8 kwa mwaka wa Fedha.

Mamlaka imepata ithibati katika Umahiri wa uchunguzi wa kimaabara (ISO 17025:2027) kwenye maabara zake sita ambazo ni Maabara ya Vinasaba vya Binadamu, Mikrobiologia, ambayo ni Ithibati ya Mifumo ya Usimamizi wa Ubora(ISO 9001:2015) ya uendeshaji wa
ya kisasa kwa ajili ya kuendelea kuboresha huduma za uchunguzi.

Mamlaka imeweza kudhibiti uingizaji na usafirishaji wa kemikali hatarishi na zile
usalama wa nchi kwa kutoa vibali vya kuingiza na kusafirisha kemikali hizo. Katika kipindi Mamlaka hufanya ukaguzi wa mara kwa mara kwenye maghala yanayohifadhi kemikali na asilimia 119 ya lengo la kukagua maghala 7,160, Kemikali zinazoingizwa nchini ni zile ambazo zinaruhusiwa kisheria kuingia nchini, zinazodhibitiwa chini ya mikataba ya kimataifa ili kulinda afya ya binadamu, mazingira na Serikali ya awamu ya sita kumekuwa na ukuaji wa biashara kwa wadau wanaojihusisha.

Mamlaka imeendelea kufanya maboresho ya kuharakisha mchakato wa usajili wa Utoaji wa Vibali vya Kuingiza au Kusafirisha Kemikali 2,125Mwaka 2021 hadi Wadau3835kufikia Juni, 2025sawa na ongezeko la asilimia 81

cha miaka minne (4)cha Serikali ya awamu ya sita (6), kumekuwa na ongezeko la vibali Katika kuhakikisha kuwa kemikali zinatumika kwa usalama na kwa kufuata taratibu zote kampuni zinazojihusisha na biashara ya kemikali. Katika kipindi cha miaka minne ya Mamlaka imefanya ukaguzi wa maghala 8,521ya kuhifadhia kemikali, Uingizaji wa kemikali kutoka vibali 40,270 kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 hadi maghala na maeneo ambapo kemikali zinatumika,ukaguzi wa maeneo ya mipaka ambapo na biashara ya kemikali, ambapo wadau waliosajiliwa wameongezeka kutoka Wadau.

Sheria ya Usimamizi na Udhibiti wa Kemikali za Viwandani na Majumbani, Sheria Na. 3 Vibali 67,200 kufikia kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025 sawa na ongezeko la asilimia mazuri ya biashara na uwekezaji yaliyowekwa na Serikali ya awamu ya sita, Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali imefanikiwa kujenga maabara ya uchunguzi wa Vinasaba tatu (3) zinafanya kazi baada ya ununuzi na usimikaji wa mitambo ya uchunguzi.

Biashara ya kemikali kumekuwa na ongezeko kubwa la wadau wanaotimiza matakwa ya kutumia jengo lake Makao Makuu ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, mikoa ya Dar es Salaam, Pwani, Mtwara, Lindi ,Ruvuma.

Aidha, Mamlaka imekamilisha kupitia mpango wa elimu kwa umma unaotekelezwa na Mamlaka kwa wadau wa
Mutukula,Holili na Namanga juhudi hizo zinalenga kuweka mazingira mazuri ya kufanyia kazi Katika kipindi cha miaka minne, Mamlaka imefanikiwa utoaji matokeo ya uchunguzi kwa wakati ikiwemo nunuzi wa Mitambo Katika kipindi cha miaka Serikali ya Sita, Mamlaka umechangia kwenye Mfuko Mkuu wa Serikali, jumla ya Shilingi 3,999,375,100.00kupitia katika kipindi cha miaka minne (2021–2025). 

Mamlaka imepata Hati Safi mfululizo (2021/2022 hadi 2024/2025) za ukaguzi wa Hesabu.



Na Avila Kakingo, Michuzi Tv
SERIKALI ya Tanzania imeendelea kuchukua hatua thabiti za kuboresha upatikanaji wa nishati ya uhakika kwa ajili ya kuharakisha maendeleo ya viwanda na kuchochea ukuaji wa uchumi, kupitia mradi mkubwa wa usafirishaji wa umeme kutoka Chalinze hadi Kituo cha Kinyerezi III wenye urefu wa kilomita 135 na uwezo wa kusafirisha hadi megawati 1,000.

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Mashaka Biteko, amesema hayo leo Julai 10, 2025 jijini Dar es Salaam alipokuwa akikagua miradi mbalimbali ya uzalishaji wa umeme kwa kutumia gesi asilia katika vituo vya Kinyerezi I, I Extension na Kinyerezi II.

Katika ziara hiyo, Dkt. Biteko ameeleza kuwa ujenzi wa njia hiyo mpya ya umeme ni sehemu ya mpango wa Serikali kuhakikisha nishati ya uhakika inafika katika maeneo ya viwanda, hususan katika mikoa ya pwani na magharibi, ambayo awali ilikuwa inakabiliwa na changamoto ya upatikanaji wa umeme wa kutosha.

 “Maeneo kama Mkuranga yana viwanda vingi yanayohitaji umeme wa kutosha. Hali hii inatufanya tuongeze uwezo wa vituo vya kuzalisha, mfano Kinyerezi III kutoka megawati 600 hadi 1,000 ili kukidhi mahitaji yanayoendelea kuongezeka,” amesema Dkt. Biteko.

Akizungumzia maendeleo ya upatikanaji wa umeme nchini, Dkt. Biteko amesema mafanikio yaliyopatikana hadi sasa yanatokana na uwekezaji mkubwa unaofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

“Mhe. Rais Samia amewekeza kwa kiwango kikubwa katika sekta ya nishati. Kwa mwaka huu wa fedha, tumetenga Shilingi trilioni 2.3 kwa ajili ya kuendeleza miradi ya umeme na kuimarisha miundombinu ya usambazaji,” amesema Dkt. Biteko.

Aidha, Dkt. Biteko amesisitiza kuwa sekta ya nishati ni uti wa mgongo wa uchumi wa taifa, na ndio msingi wa maendeleo ya viwanda, biashara, elimu, na huduma za afya.

Amepongeza Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kwa maboresho makubwa ya huduma zake kwa wananchi, ikiwemo kuondoa gharama za simu kwa wateja wanaotaka msaada wa haraka na kuimarisha usikivu na ufuatiliaji wa changamoto za wateja.

Kwa mujibu wa taarifa ya hali ya uchumi ya mwaka 2024, sekta ya nishati imekuwa kwa asilimia 14, ikishika nafasi ya pili nyuma ya sekta ya Sanaa, Utamaduni, Michezo na Habari ambayo imekua kwa asilimia 17.

Dkt. Biteko amehitimisha kwa kutoa wito kwa wananchi kushiriki katika ulinzi wa miundombinu ya umeme na kulipa gharama za matumizi kwa wakati, ili kuendeleza juhudi za Serikali katika kujenga taifa lenye nishati ya uhakika kwa wote.

Kwa Upande wa Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Endward Mpogolo amesema kuwa ziara hiyo ni ya muhimu sana kwa kuwa inatoa mwanga wa wazi kuhusu hali ya uzalishaji wa nishati nchini, hasa wakati huu ambapo mahitaji ya umeme yanaongezeka kufuatia ukuaji wa viwanda, hasa katika Wilaya ya Kigamboni.

"Ni hatua muhimu katika kuhakikisha huduma ya umeme inaimarishwa ili kuendana na kasi ya maendeleo," amesema Mpogolo.

Aidha, Mkuu huyo wa Wilaya alitumia fursa hiyo kupeleka salamu za shukrani kwa Mheshimiwa Rais kwa kushughulikia kwa vitendo changamoto ya maji jijini Dar es Salaam.

"Tupelekee salamu kwa Mheshimiwa Rais kwa kuleta zaidi ya Shilingi bilioni 37 ambazo zimewezesha ujenzi wa tanki kubwa la maji lililopo Bangulo, Wilaya ya Ilala. Tenki hilo litakuwa sehemu muhimu ya kusaidia upatikanaji wa maji kwa wakazi wa jiji na pia litachangia katika upatikanaji wa umeme," ameongeza.

Vilevile, ameeleza shukrani kwa Serikali kwa kuendelea kupeleka fedha za maendeleo katika wilaya mbalimbali za Dar es Salaam, jambo ambalo limechochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi na kuchangia ustawi wa nchi kwa ujumla.

Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Edward Mpogolo akizungumza wakati wa ziara ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Dotto Biteko.
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Mashaka Biteko (wa tatu kulia) akikagua maendeleo ya miradi ya kuzalisha umeme kwa gesi asilia katika vituo vya Kinyerezi I, Kinyerezi I Extension na Kinyerezi II leo, Julai 10, 2025, jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO Lazaro Twange akisalimiana na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Mashaka Biteko wakati akiwasili katika miradi ya kuzalisha umeme leo, Julai 10, 2025, jijini Dar es Salaam.
Mitambo ya miradi ya kuzalisha umeme kwa gesi asilia katika vituo vya Kinyerezi I, Kinyerezi I Extension na Kinyerezi II.
 
Matuki mbalimbali.
-Ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuongeza ushiriki wa Watanzania katika Sekta ya Madini

Dar es Salaam, Julai 10, 2025

Tume ya Madini imejipanga kwa dhati kuhakikisha Watanzania wanapewa kipaumbele katika usambazaji wa bidhaa na huduma katika migodi ya madini ili kuwajengea uwezo wa kiuchumi, kuongeza mzunguko wa fedha ndani ya nchi na kuchochea ukuaji wa Pato la Taifa kupitia Sekta ya Madini.

Akizungumza katika Maonesho ya 49 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu J.K. Nyerere, Meneja wa Mahusiano kwa Umma na Mawasiliano wa Tume hiyo, Bw. Greyson Mwase amesema Serikali kupitia Tume ya Madini inaendelea kusimamia kwa karibu utekelezaji wa Sheria ya Madini, Sura ya 123 Kifungu cha 102 pamoja na Kanuni za Ushirikishwaji wa Watanzania za mwaka 2018.

“Lengo kuu la kanuni hizi ni kuhakikisha kuwa Watanzania wanashiriki kikamilifu katika uchumi wa madini kupitia utoaji wa bidhaa na huduma migodini badala ya kuziacha kampuni kuagiza bidhaa hizo kutoka nje ya nchi,” amefafanua Mwase.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Tume ya Madini, katika mwaka wa fedha 2023/2024, migodi ya madini nchini ilizalisha ajira rasmi 19,874 ambapo kati ya hizo, ajira 19,371 sawa na asilimia 97 zilitolewa kwa Watanzania, huku wageni wakipewa ajira 503 tu sawa na asilimia 3.

Bw. Mwase ameongeza kuwa kampuni za madini nchini hutumia wastani wa shilingi trilioni 5.3 kila mwaka kwa ajili ya ununuzi wa bidhaa na huduma mbalimbali zinazotumika migodini, na hivyo kuwataka Watanzania kuchangamkia fursa hizo kwa kuanzisha au kuimarisha biashara zinazohusiana na sekta hiyo.

Aidha, ameshauri taasisi za kifedha nchini kuongeza wigo wa utoaji mikopo na mitaji kwa Watanzania wenye nia ya kuwekeza katika sekta ya madini, hasa katika maeneo ya usambazaji wa vifaa, huduma za vyakula, usafiri, usafi na nyinginezo zinazohitajika katika migodi.

Tume ya Madini inaendelea kuelimisha umma kuhusu fursa hizi kupitia maonesho mbalimbali, ikiwa ni pamoja na maonesho ya Sabasaba, kwa lengo la kuhakikisha Watanzania wengi zaidi wananufaika na rasilimali za taifa lao.




Waziri wa Mambo ya Nje wa Cyprus. Dkt. Constantinos Kombos amekamilisha ziara yake ya kikazi ya siku tatu nchini na kuagwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Said Shaib Mussa kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar Es Salaam Julai 10, 2025.

Wakati wa ziara yake nchini, Dkt. Constantinos Kombos alikutana na viongozi mbalimbali akiwemo mwenyeji wake, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo ambapo kwa pamoja walisaini Hati ya Makubaliano Kuhusu Mashauriano ya Kisiasa kati ya Tanzania na Cyprus ambayo yanatarajiwa kukuza na kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia na kiuchumi baina ya mataifa hayo mawili.














Top News