Mkutano wa 30 wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi (COP30) unaotarajiwa kuanza Novemba 10-21,2025 kwenye jiji la Belém do Pará, nchini Brazil,umebeba fursa mpya ya Tanzania kusukuma agenda za mapambano dhidi ya uchafuzi wa bahari unaosababishwa na taka za plastiki hasa katika fukwe zilizopo kwenye mwambao wa Kigamboni, jijini Dar es Salaam.

Takwimu kutoka katika vyanzo mbalimbali likiwemo Baraza la Taifa la Uhifadhi wa Mazingira (NEMC) vinabainisha kuwa jiji la Dar es Salaam, linazalisha wastani wa tani 4100 hadi 5,600 za taka ngumu kwa siku na ndilo linalochangia kiasi kikubwa cha taka hizo zinazoingia baharini.

Kutokana na umuhimu wa COP30 ambalo ni jukwaa rasmi la kimataifa kwa ajili ya kujadili na kuamua malengo ya kukataa uzalishaji wa hewa ukaa, kutafuta ufadhili wa fedha za kukabiliana na madhara ya mabadiliko tabianchi na kufikia makubaliano ya kimataifa yanayoathiri sera za kitaifa za utekelezaji wake kama vile mkataba wa Kyoto na Paris, Tanzania inayo nafasi ya kutafuta fedha za kukabiliana na changamoto ya taka ngumu zinazoingia baharini.

Ikumbukwe kuwa matokeo ya makubaliano hayo yanayofikiwa kwenye mikutano ya COP, yaliyoanza rasmi mwaka 1995 nchini Ujerumani yanagusa maisha ya kila siku ya mwananchi kupitia sera zinazoamuliwa na serikali kama vile miongozo ya nishati safi ya kupikia, ukarabati wa mazingira, mipango ya ujenzi wa miundombinu inayostahimili mabadiliko tabianchi na msaada kwa wakulima na wavuvi walioathika.

Mkutano wa mwaka huu ni mwendelezo wa mikutano hiyo inayofanyika kila mwaka tangu mwaka 1995 na msingi wake ni Mkutano wa Mazingira wa Dunia uliofanyika Brazili mwaka 1992 ambao uliridhia kuanzishwa kwa COP ambayo ni kifupi cha ‘Conference of the Parties’ unaohusisha wanachama wa UNFCCC-‘United Nation Framework Convention on Climate Change’, ambao ni mkataba wa kimataifa wa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi uliopewa jukumu la kuwa chombo cha utekelezaji na usimamizi wa mkataba huo.

CoP30 ni moja ya majukwaa muhimu zaidi duniani kwa majadiliano ya sera, mikakati na hatua za pamoja za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi. Kwa Tanzania, hii ni fursa adhimu ya kutafuta fedha zitakazosaidia kuwaongezea uelewa wa wananchi kuhusu nafasi ya nchi katika utekelezaji wa mikataba ya kimataifa, na kuhamasisha ushiriki wa jamii katika kulinda mazingira ya bahari na kukabiliana na athari mabadiliko tabianchi.

Tanzania ni miongoni mwa nchi zinazoathiriwa zaidi na mabadiliko ya tabianchi licha ya kuchangia kidogo katika utoaji wa gesi joto (greenhouse gases). Hali hii imekuwa ikijitokeza kupitia mabadiliko ya mifumo ya mvua na ukame wa mara kwa mara, kupungua kwa upatikanaji wa samaki, uzalishaji wa chakula, kuongezeka kwa mafuriko, uharibifu wa miundombinu na magonjwa yanayosababishwa na mabadiliko tabianchi.

Katika kipindi hiki cha kuelekea kwenye mkutano huo wananchi hasa wakazi wa pwani ya Kigamboni, jijini Dar es Salaam wanalo jukumu la kuhifadhi mazingira, kutambua sera na mikakati ya taifa kama vile Mkakati wa Kitaifa wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (NCCS), Mpango wa Taifa wa kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi na kushiriki kikamilifu katika hatua za kijamii, kiuchumi na kiteknolojia zinazolenga kupunguza athari za tabianchi.

Umuhimu wa mkutano wa COP30 unafungua milango kwa serikali na wadau wa mazingira kufikisha elimu kwa wananchi mara kwa mara kwa kutumia redio, televisheni, magazeti na majukwaa ya kidijitali.

Ingawa umesalia muda mfupi wa kuelekea kwenye mkutano huo bado serikali na wadau wa mazingira wanayo nafasi ya kuzishirikisha jamii za vijijini kwa kuwapa elimu wakulima, wavuvi, wafugaji na wanawake kuhusu mbinu endelevu za uzalishaji zinazozingatia tabianchi sanjari na kufanya warsha na midahalo ya kijamii ili kubadilishana maarifa ya jadi na kisayansi.

Aidha ipo haja ya kuwajengea uwezo viongozi wa serikali za mitaa, mashirika ya kiraia (CSOs) na vyama vya wanahabari kuhusu maudhui ya COP30 na utekelezaji wa mikataba ya mazingira na kuanzisha mtandao wa mawasiliano unaounganisha sekta binafsi, mashirika ya kimataifa na serikali.

Katika mikakati ya muda mrefu ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi serikali na wadau wanaweza kuongeza nguvu katika kuwatumia vijana waliopo shuleni kama injini ya mabadiliko kwa kuwapa elimu ya mabadiliko ya tabianchi katika mitaala ya shule na vyuo, kukuza ubunifu wa vijana kupitia miradi ya kijani, sayansi na teknolojia rafiki kwa mazingira na kuandaa mashindano ya kitaifa ya ubunifu kuhusu masuala mbalimbali ya uokotaji na urejezaji wa taka ngumu kwa kuzifanya fursa badala ya tatizo.

Pamoja na mambo mengine kuna haja kwa serikali na wadau kuanzisha kampeni zenye lengo la kuonesha hatua ambazo taifa limepiga katika kutekeleza ahadi za NDCs, kulikuwa na haja kuitisha mijadala ya kitaifa juu ya mabadiliko ya tabia nchi kabla ya mkutano wa Brazil ili kujadili vipaumbele vya Tanzania na kutoa sauti ya wananchi itakayowakilishwa kimataifa.

Aidha serikali kupitia Ofisi ya Makamu wa Rais – Muungano na Mazingira ina wajibu mkubwa wa kuratibu juhudi za Wadau kama Chama cha Waandishi wa Habari za Mazingira Tanzania (JET), TMF, Oxford Policy Management (OPM), Climate Action Network Tanzania (CAN),UNDP, WWF, na Tanzania Climate Change Forum hawa wanaweza kuendesha kampeni za kitaifa za uhamasishaji.

Ushirikiano wa sekta binafsi pia ni muhimu katika kuwekeza kwenye teknolojia rafiki kwa mazingira kama nishati jadidifu na urejelezaji wa taka ngumu.

Uelewa wa wananchi kuhusu COP30 na mabadiliko ya tabianchi si suala la kubembeleza bali ni hitaji la msingi la kitaifa. Kupitia kampeni madhubuti za kuiandaa jamii, mwenendo huu utaisaidia nchi kujiweka kwenye nafasi nzuri ya kushiriki kikamilifu katika majadiliano ya kimataifa, kulinda maslahi yake ya kiuchumi na kijamii, na kuendeleza azma ya taifa ya “uchumi wa buluu” unaozingatia maendeleo endelevu.

Ripoti ya Mwongozo wa Kitaifa wa Kutambua Maeneo Hatari ya Plastiki na Kuunda Mikakati iliyooandaliwa na International Union for Conservation of Nature (IUCN) kwa kushirikiana na Mpango wa Umoja wa Mataifa wa Mazingira (UNEP) na taasisi ya Life Cycle Initiative (chini mradi wa MARPLASTICCs), inabainisha kuwa, Jiji la Dar es Salaam linachangia zaidi ya asilimi 50 ya taka zote za plastiki zinazoishia kwenye mito, maziwa na baharini.

Kulingana na ripoti hiyo mwaka 2018 zaidi ya tani 29,000 ziliingia kwenye maji (bahari, mito na maziwa). Uchafuzi huu unatajwa kuzidisha athari za mabadiliko ya tabianchi katika maeneo ya Pwani, huku umasikini wa wavuvi na wafanyabiashara wa samaki ukiongezeka.Kuelekea COP30, tuhamasike, tushirikiane, na tuwe sehemu ya suluhisho.



Na Mwandishi wetu, Karatu Arusha.

Siku chache baada  ya aliyekuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Isdor Mpango, kuzindua Makumbusho ya kisasa ya Jiopaki ya Ngorongoro-Lengai (Urithi Geo Museum) tarehe 16 Oktoba, 2025 wadau wameanza kuvutiwa na makumbusho hiyo na kuitembelea kwa lengo la kupata elimu kuhusu vivutio vya utalii, shughuli za uhifadhi wa maliasili na mambo kale.

Watalii na wadau wanaotembelea jengo hilo wanapata elimu kuhusu muonekano wa dunia miaka milioni mia mbili iliyopita na ilivyo sasa, maumbile asilia yanayopatikana katika ukanda wa bonde la ufa,kujionea mwamba wenye umri wa miaka milioni tatu iliyopita unaopatikana hifadhi ya Jiolojia ya Ngorongoro-Lengai, kujifunza tamaduni za makabila ya  Wahadzabe, Wairaqw, Wadatoga na Wamasai pamoja, kupima uwezo wa kutambua sauti za wanyamapori, kushindana mbio kwa kutumia baiskeli na wanyamapori  ndani ya makumbusho na  vivutio vingine.

Miongoni wadau waliotembelea Makumbusho hiyo ni kundi la wanakwaya 22 wa KKKT Dayosisi ya kasikazini Jimbo la karatu usharika wa Qurus ambapo  wametembelea jengo la Makumbusho kwa lengo la kujifunza vitu vilivyopo na kurekodi wimbo wa kwaya kwa ajili ya albam yao inayoitwa "Tumetoka mbali" 

Kiongozi wa Kwaya hiyo Mwinjilisti Eliamani Kimay ameeleza kuwa kwaya hiyo kuamua kurekodi wimbo katika maeneo ya makumbusho hiyo ni kutokana na muonekano wa jengo hilo na maelezo ya vivutio vya utalii vilivyopo ndani ambapo kupitia kwaya hiyo wanatangaza injili kwa kutumia jengo hilo ambalo ndani yake kuna vioneshwa vya kipekee vinavyoashiria uumbaji wa Mungu 

Mmoja wa wanakwaya wa kundi hilo Bi. Mariam Emmanuel ameeleza kuwa uamuzi wa kwaya yao kurekodi katika jengo hilo  ni kuonesha vivutio vilivyopo Ngorongoro, kutangaza jengo hilo kupitia injili, kuonesha vivutio vilivyopo ndani ya makumbusho ili kuhamasisha wananchi wengi zaidi kupata elimu juu ya uumbaji wa Mungu, kufahamu masuala ya kijiolojia, urithi wa utamadani, malikale, historia ya chimbuko la binadamu ambayo kwa pamoja yanaashiria uumbaji wa Mungu.

Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro ilipewa hadhi ya kuwa eneo lenye utalii wa Miamba “Geopark” mwaka 2018  na kuwa Jiopaki pekee katika nchi za kusini mwa Jangwa la Sahara na ya  pili kwa Afrika ikitanguliwa na Morocco.











Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akishiriki Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini Mwa Afrika (SADC) kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, uliyofanyika kwa njia ya mtandao tarehe 07 Novemba 2025, Dodoma.


*Mkutano wa SADC wampongeza Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa ushindi katika Uchaguzi Mkuu Oktoba 2025.

MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amesema Serikali inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imechukua hatua za kurejesha utengamano katika nchi na kuhakikisha wananchi wanaishi katika utawala wa sheria.

Makamu wa Rais amesema hayo wakati akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini Mwa Afrika (SADC), uliyofanyika kwa njia ya mtandao, akiwa mkoani Dodoma.

Amesema dhamira ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuhakikisha mchakato wa mazungumzo ya maridhiano unafanikiwa ili kuwa na Taifa lenye amani na umoja na kuendelea kuwa mfano wa utulivu katika Afrika na Dunia kwa ujumla.

Halikadhalika, Makamu wa Rais amesema Tanzania ni salama na tulivu na ipo tayari kuendelea kupokea wageni kutoka duniani kote kwa manufaa ya nchi zote.

Aidha, Makamu wa Rais, amewashukuru viongozi wa SADC walioshiriki uapisho wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na wote waliotoa pongezi za dhati. Amesema jitihada zote zitatumika kuhakikisha Tanzania inapata maendeleo na amani kuendelezwa.

Mkutano huo umempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa ushindi aliyoupata na uchaguzi wenye mafanikio.

Mkutano huo ulilenga kujadili kujiondoa kwa nchi ya Madagascar kama nchi Mwenyekiti wa SADC, ambapo nchi ya Afrika Kusini imependekezwa kuwa Mwenyekiti kwa kipindi cha mpito mpaka kufikia mwezi Agosti 2026.

Mkutano huo umekubaliana kuendelea kutumia kauli mbiu ya Mkutano wa 45 wa SADC uliyofanyika nchini Madagascar ambayo ni “Kuimarisha Viwanda, Mapinduzi ya Kilimo, Mabadiliko ya Nishati kwa SADC yenye Uhimilivu”

Imetolewa na
Ofisi ya Makamu wa Rais
08 Novemba 2025
Dodoma.

KIASI cha kasi cha mabadiliko katika teknolojia ya burudani kimetafuta njia mpya za kuwafurahisha wachezaji. Leo, wapenzi wa kasino wanataka zaidi ya mchezo wa kawaida, wanatafuta uzoefu wa kushirikisha akili, msisimko wa papo kwa papo, na nafasi za ushindi zinazogusa moja kwa moja hisia zao. Akizingatia haja hii, Meridianbet amechukua hatua ya kipekee kwa kumleta mtoa huduma mpya wa michezo ya kasino mtandaoni, iMoon, ili kuleta burudani isiyo na kifani kwa wateja wake.

Kuanzishwa kwa iMoon hakuishii kuifanya Meridianbet kuwa kiongozi wa kubashiri, bali pia inaonyesha uwezo wao wa kuleta mageuzi ya kweli katika tasnia ya kasino mtandaoni. Jukwaa hili jipya limeundwa kwa kuzingatia urahisi wa uchezaji, kasi ya matokeo, na ubora wa kimataifa wa maudhui, ikilenga kutoa uzoefu wa kipekee kwa kila mchezaji. Hii ni dalili ya dhamira yao ya kuimarisha kila kipengele cha burudani mtandaoni.

Michezo mipya inayopatikana kupitia iMoon, kama Crash Royale, inawakilisha mwelekeo mpya wa kasino mtandaoni. Crash Royale ni mchezo wa kasi na akili unaomtaka mchezaji kuondoa dau lake kwa wakati sahihi kabla ya kushuka, huku michezo mingine kama Plinko, Mines, TradeBlazer, na Crash Dragon Flare ikitumia teknolojia ya kisasa na mitindo ya kuvutia ili kuongeza uwezekano wa ushindi mkubwa.

Vilevile, meridianbet wana michezo mingi ya kasino mtandaoni na mechi za kimataifa za kubashiri zenye ushindani mkubwa wa odds. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Hatua hii ya Meridianbet ni kielelezo cha kuendeleza uongozi wao katika soko la michezo mtandaoni Tanzania. Uwekezaji huu wa kimkakati kwa iMoon unaonyesha kuwa Meridianbet wanathamini sio tu kuongeza idadi ya michezo, bali pia kuhakikisha kila mteja anapata burudani yenye thamani halisi ya muda na fedha yake. Ni ishara wazi ya kujitolea kwao katika kuleta mabadiliko chanya kwa wapenzi wa kasino.

Kwa wapenzi wa kasino wanaotafuta burudani ya kisasa, msisimko wa ushindi, na teknolojia isiyochosha, michezo ya iMoon ndani ya Meridianbet ni jibu sahihi. Sasa unaweza kufurahia michezo yenye thamani ya kweli na fursa za ushindi wa kweli. Jisajili leo kupitia Meridianbet, cheza michezo ya iMoon, na uanze safari yako ya ushindi.

HaloPesa Tamba na Bonasi imezidi kukiwasha zaidi katika soko la huduma za kifedha Tanzania, baada ya kufanikiwa kuwazawadia zaidi ya washindi 400 ndani ya kipindi cha mwezi mmoja tangu kuzinduliwa kwake.

Kupitia kampeni hii, wateja wa HaloPesa wamekuwa wakipata nafasi ya kujishindia bonasi mbalimbali kila wanapofanya miamala, ikiwemo kutuma pesa, kutoa pesa, kulipa bili, au kulipia bidhaa kupitia HaloPesa.

Miongoni mwa washindi waliobahatika kujinyakulia kitita cha shilingi milioni moja (1,000,000) kutoka kwa Mr Bonasi, Bw.Selemani Khalfan, ambaye amejishindia Bonasi ya shilingi Milioni 1, ikiwa ni sehemu ya mafanikio ya kampeni hii inayolenga kuwazawadia wateja wanaotumia HaloPesa katika shughuli zao za kila siku.

Akizungumza wakati wa kuwapongeza washindi hao, Afisa Masoko wa HaloPesa, Bi. Aidat Lwiza, alieleza kuwa kampeni ya Tamba na Bonasi ni sehemu ya jitihada za HaloPesa kuwashukuru wateja wake kwa kuendelea kutumia huduma zao, sambamba na kuhamasisha matumizi ya teknolojia rahisi katika miamala ya kifedha na kutimiza miaka 9 Tangu kuanzishwa kwa HaloPesa.


“Kupitia HaloPesa, tumerahisisha maisha ya wateja wetu. Wateja wetu waendelee kufanya miamala kwa urahisi, haraka na unafuu, huku wakiendelea kujipatia nafasi ya ushindi hadi Milioni 2 kutoka kwa Mr. Bonasi kila siku, kila wiki na kila mwezi. 

Kila muamala ni nafasi ya ushindi, aliongezea kwa kusema Halotel na HaloPesa itawasiliana na Wateja wake kupitia namba 100 pekee!” alisema Bi. Aidat Lwiza Afisa Masoko HaloPesa.

“HaloPesa, Tumerahisisha kwa makato nafuu zaidi!”








WAKALI wa ubashiri Tanzania, Meridianbet wanakwambia kuwa Wikendi hii ipo kwaajaili ya kuhakikisha hawakuachi patupu. ODDS KUBWA zipo kwenye mechi za leo hivyo bashiri sasa.

EPL pale mapema kabisa Tottenham Spurs watakipiga dhidi ya Manchester United ambapo tofauti kati yao ni magoli ya kufungwa na kufunga. Mara ya mwisho kukutana ilikuwa kwenye fainali ya Europa ambapo Spurs waliondoka na ushindi. Je United ya Amorim kulipa kisasi?. Bashiri hapa.

Nao vinara wa ligi Arsenal watakuwa ugenini kusaka ushindi dhidi ya Sunderland ambao wanaendelea kufanya vizuri msimu huu wakiwa na pointi 18 hadi sasa huku The Gunners wao wakiwa na pointi 25. Arteta anahitaji ushindi huu ili aendelee kujikita kileleni kwenye msimamo wa ligi. Je nani kushinda?. Jisajili hapa.

Kwa upande wa Chelsea wao watakuwa nyumbani pia kumenyana vikali dhidi ya Wolves ambao mpaka sasa hawana ushindi wowote kwenye ligi. Mechi hiyo inazikutanisha timu ambazo mara ya mwisho kukutana, The Blues walishinda. Je ni wakati wa wageni kulipa kisasi?. Beti sasa.

Cheza michezo ya kasino leo upige pesa kama vile Keno, Aviator, Poker, Roullette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

LALIGA kama kawaida kuna mechi za pesa kwani Sevilla ataumana dhidi ya CA Osasuna ambapo tofauti yao ni pointi 2 pekee. Kila timu inahitaji ushindi mkubwa kabisa. Hivyo tengeneza jamvi lako la uhakika siku ya leo.

Atletico Madrid ya Diego Simeone wao watakuwa kibaruani dhidi ya Levante amabo wamepanda daraja msimu huu wakiwa wameshinda 2 pekee huku wenyeji wao wakiwa wameshinda mechi 6. Je unajua kuwa kwenye mechi hii unaweza ukapasua mpunga wa maana?. Jisajili hapa.

Vilevile nao Espanyol Barcelona watakiwasha dhidi ya Villarreal ambao wapo nafasi ya 3 huku wenyeji wao wakiwa nafasi ya 6. Timu hizi mara ya mwisho kukutana, Nyambizi wa Njano aliondoka na ushindi mechi zote mbili. Je leo hii nani kuondoka na pointi 3?. Bashiri na Meridianbet mechi hii.

Pia kule Ujerumani, BUNDESLIGA nayo kuna mechi za pesa Bayer Leverkusen atacheza dhidi ya FC Heidenheim ambao wapo nafasi ya mwisho kwenye msimamo wa ligi. Wenyeji wao wapo nafasi ya 5 huku msimu uliopita kila mmoja akishinda mechi moja kati ya mbili walizokutana. Bashiri hapa.

Pia kwa upande wa RB Leipzig wao watakuwa ugenini kukipiga dhidi ya Hoffenheim ambao wanashika nafasi ya 6 kwenye msimamo wa ligi. RB yeye yupo nafasi ya 2 huku akiwa na malengo ya kupigani ubingwa msimu huu. Je nani kuondoka na ushindi?. Suka jamvi lako hapa.

Vinara wa ligi, Bayern Munich wao watapepetana dhidi ya Union Berlin ambapo mpaka sasa vijana wa Kompany wameshinda mechi zote kwenye mashindano yote. Nafasi kubwa ya kushinda mechi hii wamepewa Bayern pale Meridianbet. Je Berlin watakatiza mwendelezo wa ushindi wao?. Jisajili hapa.

Na Mwandishi wetu

Katika juhudi za kuendeleza  kutangaza fursa mbalimbali zilizopo kwenye mnyororo wa uongezaji thaman madini ya vito na metali za thamani, Kituo cha Jemolojia Tanzania (TGC) kimefungua vituo maalum vya kutangaza fursa zilizopo kwenye mnyororo wa uongezaji thamani madini nchini katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC) na katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA).

Hayo yamebainishwa leo Novemba 7, 2025 na Mkuu wa Kituo  hicho Mha. Ally  Maganga wakati akielezea namna vituo hivyo vitakavyotangaza fursa mbalimbali zilizopo kwenye mnyororo mzima wa thamani madini hususan kwa wageni wa ndani na nje ya nchi.

Akielezea kuhusu faida zitakazopatikana kupitia vituo hivyo  Mha. Maganga  amesema kuwa, lengo kubwa la kufungua vituo hivyo ni kutangaza, kuelimisha, kuhamasisha, kukuza uelewa kwa jamii kuhusu shughuli zinazofanywa na TGC. 

Sambamba na fursa za kimataifa, pia vituo hivyo vitafungua fursa za upatikanaji wa ajira na kuongeza  shughuli za ujasiriamali kwa vijana mbalimbali wenye ujuzi katika uongezaji thaman madini  hususan katika viwanda vya usonara.

Mha. Maganga amefafanua kuwa, mbali na fursa hizo, vituo hivyo  vitahamasisha na kuvutia uwekezaji katika mnyororo wa thamani wa madini itakayosaidia uanzishwaji wa viwanda vya kuchakata madini ya vito na utengenezaji wa bidhaa zitokanazo na rasilimali madini kama vile herein, pete, shanga , vinyago , mikufu na tuzo.

Akielezea kuhusu Utalii wa madini Mha. Maganga ameeleza kuwa,  faida nyingine  ni kukuza utalii wa madini   kupitia watalii wanatoka na kuingia nchini  kupitia kiwanja cha KIA na wageni watakaoshiriki mikutano ya kitaifa na kimataifa kupitia ukumbi wa  AICC.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyabiashara wa Kati wa Madini (Broker) Jeremiah Kituyo ameipongeza TGC kwa kupanua wigo wa fursa za kibiashara utakaohamasisha ushirikiano mzuri kati ya Sekta Binafsi na Serikali hasa kwenye mnyororo wa uongezaji thaman madini ya vito na metali za thamani (precious metals) kama Sera ya Madini ya Mwaka 2009 inavyoelekeza.



 

Dkt. Tulia Ackson ametangaza kujiondoa rasmi katika kugombea nafasi ya Uspika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) leo Novemba 07, 2025. Hii inamwachia nafasi Mussa Azzan Zungu na Stephen Julius Masele kuendelea na kinyang'anyiro hicho ndani ya CCM.

Kujiondoka kwa Dkt. Tulia Ackson kunatengeneza mazingira mapya ya kuteua mgombea wa CCM kwa nafasi hiyo muhimu. Mchakato wa kuteua mgombea bado unaendelea

MFANYABIASHARA Jennifer Bilikwija Jovin maarufu kama Niffer, amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akikabiliwa na mashtaka ya uhaini na kula njama.

Niffer anashtakiwa pamoja na wenzake 21 ambao ni Mwalimu, Lucianus Luchius (28), Paul Malima (28), Augustino Mulwale (30), Mohamed Kondo (30), John Mmena (26), Paul Shirima (23), Ramadhani Ramadhani (21), Levi Mkute (40), Esau Ernest Maarufu ‘Duduye’ (21), Leonard Mkonyi.

Wengine ni Fadhili Nyombi, Hamisi Hamisi, Abeid Kivuyo (24), Nicholous Shiduo (27),Abati Mwadini (27) Mika Chavala (32), Fatuma Mzengo (30), Dewji Ramji (19), Ruthmelda Silaa (21), Hilda Ngulu(22) na Yusuph Hussein(22)

Kwa mujibu wa hati ya mashtaka iliyosomwa mahakamani na wakili wa serikali Mwandamizi, Clemence Kato mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Aaron Lyamuya alidai washtakiwa wanakabiliwa na makosa matatu mbele ya mahakama hiyo la kwanza likiwa ni la kupanga njama na mengine mawili ni ya uhaini

Wakili Kato alidai katika tarehe tofauti kati ya Aprili na Agosti 2025, katika maeneo mbalimbali ndani ya Wilaya ya Ubungo, Mkoa wa Dar es Salaam washtakiwa walikula njama na kupanga kwa siri kufanya kosa la uhaini.

Aliendelea kudai kuwa shitaka la pili lilimuhusisha mshitakiwa wa pili hadi 21, ilidaiwa Oktoba 29, 2025, katika maeneo mbalimbali ndani ya Wilaya ya Ubungo Dar es Salaam, wakiwa chini ya utii kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, huku wakiwa ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, waliunda nia ya kuzuia Uchaguzi Mkuu wa 2025.

Alidai washitakiwa walifanya hivyo kwa lengo la kutishia mamlaka ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na walionyesha nia hiyo kwa kusababisha uharibifu mkubwa wa mali za Serikali zinazokusudiwa kutoa huduma muhimu.

Wakili Kato alidai shitaka la tatu linamuhusu Niffer peke yake ilidaiwa kati ya Agosti na Oktoba 2025, katika maeneo mbalimbali ndani ya Mkoa wa Dar es Salaam, akiwa chini ya utii kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, huku wakiwa ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, waliunda nia ya kushawishi umma kuzuiya Uchaguzi Mkuu wa 2025.

Alidai mshitakiwa alifanya hivyo kwa lengo la kutishia mamlaka ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na walionyesha nia hiyo kwa kuhamasisha umma kununua barakoa katika biashara yake kwa ajili ya kujikinga na mabomu ya machozi katika maandamano ya kupinga Uchaguzi Mkuu wa 2025.

Hata hivyo washtakiwa hawakuruhisiwa Hakimu kujibu kitu chochote kwa sababu mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza makosa ya uhaini.

Baada ya mahakama kueleza hayo jopo la Mawakili wa utetezi likiongozwa na Peter alidai anaomba hoja hizo ziingie katika rekodi Novemba 6,2025 mteja wake Niffer akiwa chini ya himaya ya jeshi la polisi katika kituo cha polisi Oysterbay alifanyiwa vitendo vya kikatili ikiwemo kupigwa na maofisa kadhaa ambao walimlazimisha asaini maelezo yanayosemekana kuwa ni ya onyo.

Alidai na ilikuwa hivyo kwa washtakiwa wengine kuanzia wa pili hadi wa 22 katika tarehe tofauti ambazo walichukuliwa maelezo yao, alidai aliomba ikae katika rekodi za mwenendo wa ukabidhi ili wakiibua pingamizi lolote la kisheria isionekanane kuwa hawakusema awali.

“Tunaomba mahakama hii itoe amri watakapokabidhiwa kwa uongozi wa magereza kwa sababu tunajua ina zahanati na hospitali ya serikali tunaomba wafanyiwe uchunguzi wa kitabibu juu ya majeraha hayo na ripoti hiyo chini ya uongozi wa magereza iletwe mahakamani,” alidai Kibatala.

Pia alidai kosa hilo lipo ndani ya mamlaka ya mahakama hiyo akisisitiza kuwa lilikuwepo kimakosa kwa sababukuwepo kwa sababu kuna kosa la pili na la tatu tayari, hivyo aliomba mahakama lifutiliwe mbali akisistiza hati ilikuwa na mapungufu.

Pia alidai ili mahakama iweze kufanya mwenendo wa ukabidhi unatakiwa kuwa na taarifa binafsi za washitakiwa lakini jamhuri walidai katika hati ya mashitaka zilikosekana taarifa za mshtakiwa wa 19 hadi 22, hivyo itapelekea mahakama kushindwa kuamua kwa usahihi.

Baada ya hoja hizo upande wa Jamhuri waliomba mahakama ahirisho ili kuweza kujiandaa na kuja kujibu hoja hizo za mawakili wa utetezi hapo jumatatu, Kibatala alipinga ombi hilo alidai kama ni marekebisho basi wapewe ahirisho la saa moja ili shauri liweze kuendelea na hakimu apate nafasi ya kwenda kuandika uamuzi.

Baada ya kusikiliza pande zote mbili Hakimu Lyamuya alisema kuhusu umri wa washtakiwa ni wazi kuwa washitakiwa hao watano ambao taarifa zao hazipo umri ni sawa.

“Mimi niliopo hapa nipo kwenye nafasi nzuri zaidi ya kuwaona kuliko waliosoma umri wao hakuna mtoto hapo na nimejiridhisha kuwa hakuna hoja ya umri tena,” alisema Hakimu.

Alisema kuhusu kuchunguzwa afya za washitakiwa alihitaji majibu ya serikali kwamba mshitakiwa yeyote anayehisi anatatizo la afya atoe taarifa kwa magerezwa na achunguzwe na ripoti upande wa magereza waipeleke mahakamani ili iwe sehemu ya mwenendo wa kesi.

Pande zote zilikubaliana shauri hilo kurudi Novemba 11, mwaka huu kwa ajili ya Jamhuri kujibu hoja na itasikilizwa kwa njia ya mtandao lakini siku ya uamuzi washitakiwa wote watafikishwa mahakamani.

Msingi wa Vurugu ni uharibifu. Hupofusha watu kwa sababu, huondoa huruma na badala yake hujaza uadui, na husababisha vitendo vya kuumiza na wakati mwingine hugharimu maisha ya Watu.

Vurugu mara nyingi zimekuwa chanzo cha baadhi ya matukio mabaya zaidi ya binadamu.

Kilichotokea Oktoba 29. Wananchi wachache waliongia barabarani walifanya uhalifu wa kutisha kwa kisingizio cha maandamano ya amani, wamechoma gari binafsi za watu, wameingia kwenye sehemu za starehe za watu binafsi na kuanza kunywa bia, wamechoma viwanda na zaidi kuiba mali mbalimbali za watu ikiwemo mavazi na simu kwenye maduka ya baadhi ya watu.

Mfano dhahiri ni uharibifu mkubwa wenye kugharimu zaidi ya Bilioni mbili uliofanywa kwenye Ofisi za The Voice Jijini Dar Es Salaam.Sababu kubwa za uharibifu huo ni waharibifu kuhusisha umiliki wa Klabu hiyo na familia za Viongozi wakuu wa serikali. Bahati mbaya taarifa hiyo ni potofu na imekanushwa na wamiliki wa eneo hilo.

"Walianza kushindwa kuelewa mgomvi wao halisi ni nani na hilo ndilo lilikuwa gape kubwa walilokosea. Mfano wamevamia sokoni na kuanza kuiba matunda ya Mama mwenye mtaji wa laki moja, je huyo mama unakuwa unemtetea au unamdhohofisha maisha.?Amehoji Mwandishi Aloyce Nyanda.

Msanii Juma Jux mwenye maduka ya mavazi ya chapa yake ya African Boy, Sharobaro wa Insta mwenye maduka ya mavazi Jijini Dar Es Salaam na mgahawa wa chakula wa Zena Yusuph Maarufu kama Shilole ama Shishifood na mwanamuziki Billnas ni miongoni pia mwa Vijana wanaotafuta kujikwamua kiuchumi ambao vitega uchumi vyao mbali ya kuharibiwa, vimechomwa moto na kuangamizwa kabisa. Sababu ikiwa ni ileile, vurugu zenye kutokana na upotoshaji na taarifa zisizo sahihi.

Katika dunia inayoonekana kugawanyika, ni muhimu Watanzania tukachagua mshikamano. Tukumbatie upendo, uelewano, na huruma kama kanuni zetu kuu. Chuki inaweza kuwa ugonjwa, lakini upendo ndio tiba.Tuvunje mzunguko wa mambo hasi na kupanda mbegu za mustakabali mwema na wa amani zaidi  kwa jamii yetu na Tanzania kwa ujumla.

 Na Mwandishi wa NCAA, Karatu.


Kamishna wa Uhifadhi wa Mamlaka ya hifadhi ya eneo la Ngorongoro (NCAA) Bw. Abdul-Razaq Badru ameeleza kuwa kusimamia na kuendeleza uhifadhi ni jukumu la msingi kwa mamlaka hiyo kwani uhifadhi ndiyo moyo katika ustawi wa utalii na maendeleo ya jamii.

Akizungumza na watumishi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro katika ofisi za makao makuu Karatu Arusha leo tarehe 7 Novermba, 2025 Kamishna Badru amesisitiza kuwa, usimamizi madhubuti wa rasilimali za wanyamapori, Misitu na Malikale zilizopo hifadhi ya Ngorongoro ni jambo la kufa na kupona na kueleza watumishi hao kuwahudumia wageni wanaotembelea hifadhi kwa wakati, ukarimu, uadilifu na nidhamu ili kuendelea kulinda chapa ya Ngorongoro (Brand) kama eneo bora la utalii wa kifahari (Premium Safari Destination)

“Jukumu la msingi kwa kila mtumishi wa Ngorongoro ni Uhifadhi kisha mengine yanafuata, uhifadhi na ulinzi wa rasilimali ni jambo la kufa na kupona, hivyo nawasisitiza kuhakikisha kila mmoja anakuwa mlinzi wa rasilimali hizo.

Akitoa taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya taasisi hiyo Naibu Kamishna anayeshughulikia uhifadhi,utalii na maendeleo ya jamii Joas Makwati ameeleza kuwa idadi ya watalii imeendelea kuongezeka ambapo robo ya kwanza iliyoishia Septemba 2025 zaidi ya watalii 350,000 wametembelea Ngorongoro.

Kwa upande wake Naibu Kamishna anayeshughulikia huduma za shirika Aidan Makalla amewataka watumishi kuwa wazi kuchangia maendeleo ya mamlaka kwa kuendelea kutoa ushauri,maoni na Mtazamo katika majukumu ya taasisi ili kuhakikisha huduma zinaendelea kuwa bora na endelevu.



Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Said Shaib Mussa ameshiriki Mkutano wa Dharura wa Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) uliofanyika kwa njia ya mtandao kutokea jijini Dodoma Novemba 07, 2025.

Mwenyekiti wa mkutano huo ambaye pia ni Waziri wa Uhusiano wa Kimataifa na Ushirikiano wa Afrika Kusini, Mhe. Ronald Lamola alisema mkutano huo ni mwendelezo wa umoja wa nchi za SADC kuitana pamoja kujadili masuala mbalimbali yanayohitaji maamuzi ya haraka.

Mkutano huo umejadili maandalizi ya mkutano wa Daharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali utakaofanyika kwa njia ya Mtandao jioni ya Novemba 07, 2025; masuala ya kibajeti ya ulinzi na usalama na uongozi wa SADC kufuatia kujitoa kwa Jamhuri ya Madagascar kuwa Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo kwa kipindi cha August 2025-August 2026.





 

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani, Jacobs Mwambegele (katikati) akiongoza kikao cha Tume kilichokutana Jijini Dodoma leo Novemba 7, 2025 na kupitisha majina ya wabunge wa viti maalum. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Tume , Mhe. Jaji wa Rufaa (Mst) Mbarouk Salim Mbarouk na kushoto ni Katibu wa Tume ambae pia ni Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume, Ndg. Ramadhani Kailima. 
Tume ikiwa katika kikao chake hii leo. 
**************

Kwa kuzingatia masharti ya Ibara ya 66(1)(b) na 78(1) za Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977 zikisomwe pamoja na kifungu cha 112 cha Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani Na. 1 ya Mwaka 2024, Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi katika kikao chake kilichofanyika leo tarehe 07 Novemba, 2025 imefanya uteuzi wa Wabunge Wanawake wa Viti Maalumu 115 kati ya idadi ya Wabunge 116 wanaopaswa kuteuliwa. 

Aidha, nafasi ya Mbunge mmoja uteuzi wake utafanyika baada ya kukamilisha uchaguzi wa Ubunge katika Jimbo la Fuoni - Tanzania Zazibar na Jimbo la Siha Tanzania Bara. Ifuatayo ni orodha ya Wabunge Wanawake wa Viti Maalumu 115 walioteuliwa:






 

 Mbinga, Ruvuma

Katika mwaka wa fedha 2024/2025, Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Wilaya ya Mbinga imepokea jumla ya shilingi milioni 403,772,750.00 kutoka serikali kuu kwa ajili ya kurejesha mawasiliano ya barabara zilizoharibiwa na mvua za masika pamoja na tetemeko la ardhi lililotokea mwezi Mei, 2024.

Meneja wa TARURA Wilaya ya Mbinga, Mhandisi Oscar Mussa, amesema kuwa fedha hizo zimetumika kutekeleza miradi miwili mikubwa ya ukarabati wa barabara ambazo zilikuwa muhimu kwa wakazi wa maeneo husika.

"Katika kipindi cha masika tulikumbwa na madhira makubwa yaliyosababisha kuporomoka kwa udongo na kuharibu miundombinu ya barabara. Serikali ilitupatia shilingi milioni 283,172,000.00 kwa ajili ya kurudisha mawasiliano katika barabara ya Langilo kuelekea mkoha," amesema Mhandisi Musa.

Barabara hiyo yenye urefu wa kilomita 7.2 inahudumia wakazi wa Kata ya Langilo, hususan kijiji cha Mkoha. Madhara makubwa yalitokea katika eneo la daraja la mto Makomba ambapo udongo uliporomoka na maeneo mengine yaliathiriwa na mawe yaliyoporomoka kwenye kona za barabara hiyo.

Amesema utekelezaji wa mradi huo ulianza mwezi Machi mwaka huu na unatarajiwa kukamilika mwezi Novemba na kuongeza kuwa kazi zilizokamilika hadi sasa ni pamoja na kurudisha tuta, kujenga mitaro ya maji ya mvua yenye urefu wa zaidi ya Km 1 na kuondoa mawe yaliyokuwa yameziba barabara.

Ametaja mradi wa pili ni ukarabati wa barabara ya Longa–Kipololo–Litoho, ambayo imepokea shilingi milioni 120,600,750.00 baada ya kuathiriwa na tetemeko la ardhi. “Eneo la Kalavati la mto Ntunduwalo, hususani katika barabara ya Longa liliporomoka tuta, lakini kwa sasa barabara hiyo imefunguliwa na inapitika kwa usalama”.

Mhandisi Mussa ameishukuru serikali kwa kuwezesha kupata fedha hizo kwani wananchi wa Mbinga wanaendelea kutoa shukrani kwa uwezeshaji huu ambao umeleta nafuu katika usafiri na usafirishaji pamoja na uchumi wa maeneo husika,









Top News