Wajumbe wa Kamati ya Huduma za Jamii ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania walipotembelea ujenzi wa Kampasi mpya ya Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA) iliyopo Tunguu, nje kidogo ya mji wa Zanzibar hapo tarehe 7 Aprili, 2010. Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mheshimiwa Omari S. Kwaangw (katikati aliyefunga mikono) na Mheshimiwa Haroun A. Suleiman, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (mwenye suti nyeusi na kofia kati) walijumuika pamoja na Wajumbe wa Kamati hiyo na maofisa wengine wa Wizara na SUZA katika picha hii. Awamu ya kwanza ya ujenzi huo inategemewa kukamilika ifikapo mwezi Juni mwaka huu.
Home
Unlabelled
wajumbe wa kamati ya huduma ya jamii ya bunge watembelea ujenzi wa kampasi ya chuo kikuu cha SUZA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali wa Zanzibar. Mhe. Haroun A. Suleiman wa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar sio aliyevaa koti jeusi na kofia ila ni yule aliyesimama kulia kwa Mhe. Kwaangw'. Please correct me if I am wrong.
ReplyDelete