Majambazi wawili wapora fedha maeneo ya kitumbini jijini Dar kwa kutumia silaha huku wakiwa na usafiri wa pikipiki,majambazi hayo yalikimbizwa na polisi pamoja na wana nchi hatimaye yalitelekeza pikipiki yao pamoja na bastola nakukimbia kwa kwa miguu polisi wali ichukua pikipiki hiyo na bastola hiyo.tukio hilo limetokea jioni ya leo majira saa kumi.
Askari Polisi wakiwa eneo la tukio huku mwingine akiikokota pikipiki iliyokuwa ikitumiwa na majambazi hayo.
Afande akiendelea kuikokota pikipiki hiyo.
Pikipiki iliyoachwa na majambazi hao ikiwa imepakiwa kwenye gari la polisi.
cheki huyo dada alivyo fiti
ReplyDeleteArobaini zao zilifika! Matukio kama hayo yanachorwa na watu waliofahamu kuna fedha zipo mahali. Safi sana Polisi na wasamaria wema. Tuwadhibiti hao wahalifu wanaotumia pikipiki!
ReplyDeleteMsamaria Mwema
jamani ndugu zangu wabongo wenzangu hebu chekini hii issue,askari anaharibu kabisa uchunguzi(investigation analyses) anashika pikipiki kwa mikono yake mikavu mikavu,jamani eeh tutafika sisi watanzania, hata gloves hatuna za kuhifadhi uchunguzi.wenzetu huku majuu,Ny wanatumia gloves kwenye eneo hili la uhalifu ili kupata finger print sasa leo watumia hizo number plate na kama ni number za feki itakuwaje yani acha tu lakin mungu atatusaidia si laumu sana ndo hali ya nchi uchumi na wakati kila leo tunatabiwa kuabiwa tanzania tabarare lakini tabarare kwa wachache wasio nacho kama miji mungu atusaidiye amen
ReplyDeleteDu, huyu dada askari ametulia, ila amekaa kiaskari zaid!
ReplyDeleteSasa wewe unasema finger prints, kwani kuna database gani ili wakatafute ni nani? Hilo ni tatizo la system ambayo haina vitambulisho, haina database ya fingerprints pamoja na kuwa kuna kila technolojia ya ku-support hayo yote. Askari hana kosa. Mwenye kosa ni serikali ambayo hajaliwekea hilo swala la finger prints kipaumbele.
ReplyDeletejamani mbona katika hii habari hamtuelezi hao majambazi walikamatwa au ndio walitelekeza pikipiki na wakakimbia na kutokomea bila kukamatwa kama kawaida ya polisi wetu siku zote huishia bila kumkamata mtu wao huibuka na vitu vilivyoachwa na majambazi tu
ReplyDeleteMiye huyo dada nampa 10/10 yupo gado hakuna mchezo...
ReplyDeleteNO NEED OF GLOVES MKUU!BONGO WATUMIA DNA TU MKUU
ReplyDeleteMdau wa alama za vidole... Alama za vidole zinakua dili kama una database ya hizo alama kwa utambuzi. Sidhani kama tuna hiyo database hapa bongo hivyo hata kama ukizipata alama za huyo mwizi utajuaje kama ni za nani? Hata hivyo wachache waliowahi kupata passport walichukuliwa alama za vidole na zitakua pale uhamiaji ingawa sina uhakika kama zipo kielekroniki. Pia pale KIA wameanzisha mtindo wa kuchukua alama za vidole ila nayo hii inawagusa sana watu wanaosafiri.
ReplyDeleteNadhani serikali inapaswa kufanyia kazi suala hili. Ukiangalia 24hrs ndo unaweza kuona jinsi gani polisi wetu wanafanya kazi katika mazingira magumu.
Mdau,
Ignorant
Hiiyetu bado iko nyuma kweli,yaani jeshi la police wanawafukuza majambazi hali yakuwa hawajava prof wamevaa ngwanda zao tu,ndio mana police hufariki ovyo kwa kupigwa risasi.
ReplyDeleteSerikali iwatafutie Prof za kukinga silaha katika vifua vyao hawa police wanapokuwa katika mabambano.
Hongereni kwa kazi nzuri