Waziri wa nchi katika ofisi ya Rais asiye na Wizara maalum Profesa Mark Mwandosya akila kiapo mbele ya Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete ikulu jijini Dar es Salaam leo asubuhi.Wapili kushoto ni Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue.Na watatu kulia ni Karani wa Baraza la Mawaziri Bwana Gerson Mdemu.
Profesa Mwandosya akipokea miongozo ya kazi baada ya kula kiapo ikulu leo asubuhi.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimpongeza na kumtakia mafanikio Profesa Mwandosya muda mfupi baada ya kumuapisha ikulu jijini Dar es Salaam leo.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimsaidiaWaziri wa nchi katika ofisi ya Rais asiye na Wizara maalumu Profesa Mark Mwandosya kushuka katika ngazi za ikulu baada ya kumuapisha leo asubuhi.
Waziri Profesa Mark Mwandosya akiwa katika mazungumzo na Rais Dkt.Jakaya Kikwete muda mfupi baada ya kula kiapo ikulu jijini Dar es Salaam leo asubuhi(picha na Freddy Maro)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 13 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 22, 2012

    hatimae kakubali hongera JK...napita tu siandiki zaidi.

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 22, 2012

    Mr.Prez please muache huyu mzee ajiuguze taratibu.hebu muondolee hayo majukumu yasiyo na wizara!!

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 22, 2012

    I see Mark Mwandosya as our Next President. Don't ask me where did i get this:) Just my opinion.

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 22, 2012

    Huyo anayesaidiwa kushuka pilika za ofisi ataziweza? Vijana wakiichukia CCM wanachama wanashangaa, watawapendeje wakati mnakumbatia wazee namna hii?

    ReplyDelete
  5. AnonymousMay 22, 2012

    Nimetokwa na machozi ......

    ReplyDelete
  6. AnonymousMay 22, 2012

    Hongera sana prof naona sasa umepona

    ReplyDelete
  7. AnonymousMay 22, 2012

    unastahili sifa mh rais utu wako umepitiliza kiwango mpende adui yako kama nafsi yako mungu akubariki mfano wa kuigwa

    ReplyDelete
  8. AnonymousMay 22, 2012

    Hivi huyu mwenye cheo cha "public" anaumwa kitu gani?

    ReplyDelete
  9. AnonymousMay 22, 2012

    Vazi la Taifa!

    Wanaume, vaeni ki-Mwandosya!

    Halafu tukazanie la akina mama.

    ReplyDelete
  10. AnonymousMay 23, 2012

    oooh Pole sana Mwandosya na mama Lucy tunakuombea utapona.sijaamini kushuka ngazi unasaidiwa!ila ni hatua kama umeweza kufika na kuapishwa maana yake kuna improvement.mungu akulinde

    ReplyDelete
  11. Mgonjwa atawezaje kufanya kazi jamani? Badilikeni!!!!!!

    ReplyDelete
  12. AnonymousMay 23, 2012

    kwanini isipite sheria ya kuongezewa muda wa uraisi tanzania huyu mh.kikwete hakuna wa kumfikia ana uwezo mkubwa wa kuongoza nchi yetu

    watanzania tukumbuke kuwa leo tutamuona hafai lakini tutakuja kumkumbuka sana mh.kikwete hakuna kama yeye kwa kila idara.

    ReplyDelete
  13. AnonymousMay 24, 2012

    Jamani Mhe. Raisi wetu JAKAYA MRISHO KIKWETE tutamkumbuka kwa mengi sana atakapomaliza muda wake.

    Ni wazi kwa sasa Serikali inafikika kuliko ilivyokuwa kabla.

    Ametumia ubinaadamu sana kumwacha Prof. Mwandosya Ofisini na kuwa hiyo Wizara isiyo kuwa na kazi Maalum ni kama amepewa mapumziko tu Mwandosya ili aweze kupata huduma za Mamlaka kuliko angetolewa ingesababisha ajione mpweke, engesononeka na ingeongeza kasi zaidi ya kuumwa kwake !

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...