Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, imepokea taarifa kutoka Shirika la Afya
Duniani (WHO), tarehe 20 Oktoba, 2012 kuhusu ugonjwa wa Marburg ambao
umejitokeza katika nchi jirani ya Uganda. Maeneo yaliyokumbwa na ugonjwa huo ni
Wilaya ya Kabale, Kanda ya Kusini Magharibi ya nchi, na wilaya hii inapakana na
Rwanda. Mpaka tarehe 24 Oktoba 2012, takriban watu 13 wamepata maambukizo na 6
wamepoteza maisha..
Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii inapenda kutoa tahadhari ya Ugonjwa huu
kwa wananchi wote, katika mikoa yote ya Tanzania na hasa wale waliopo katika
mikoa ambayo inapakana na na nchi jirani ya Uganda (Mikoa ya Mara, Mwanza,
Kagera na Kigoma).
Marburg ni ugonjwa wa hatari unaofanana na Ebola na unasababishwa na virusi vijulikanavyo kwa lugha ya
kitaalam “Marburg Virus”. Ugonjwa huu ni miongoni mwa
magonjwa yajulikanayo kwa ujumla kama Homa za Virusi zinazosababisha kutokwa damu
mwilini, (Viral Haemorrhagic Fevers). Chanzo kamili cha virusi vya ugonjwa huu
hakijulikani. Hali inayosababisha mlipuko wake pia haijulikani. Ugonjwa huu hauna
tiba wala chanjo.
Dalili kuu za ugonjwa huu ni pamoja na Homa kali, inayoambatana na kutokwa damu katika matundu
yote ya mwili yaani pua, njia ya haja kubwa na ndogo, mdomoni, masikioni,
machoni, hali inayopelekea kifo kwa muda mfupi. Kipindi cha kuonekana kwa dalili za ugonjwa ni kati
ya siku 3 hadi 9 baada ya kupata maambukizi.
Ugonjwa huu unaenea kwa urahisi sana na haraka kutoka mtu
mmoja hadi mtu mwingine iwapo mtu atakuwa karibu na mgonjwa na kugusana na
mate, damu, mkojo, machozi, kamasi, maji maji mengine ya mwili, ikiwa ni pamoja
na jasho au kumgusa mtu aliyekufa kwa
ugonjwa wa Marburg.Ugonjwa
huu pia unaweza kuenezwa iwapo mtu atagusa nguo au mashuka ya mgonjwa wa
Marburg.
Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, imechukua hatua zifuatazo katika
kukabiliana na tishio la ugonjwa huu:
o Kutoa taarifa ya tahadhari ya ugonjwa huu kupitia kwa Waganga Wakuu wote wa
Mikoa na Wilaya. Aidha taarifa hii pia imejumuisha namna mgonjwa anavyoweza
kutambuliwa (Ainisho la Ugonjwa), “Fact
sheet” ya ugonjwa, Mwongozo kwa watumishi wa afya wa namna ya kuchukua sampuli
na vipeperushi vinavyoelezea ugonjwa huu.
o Kuimarisha ufuatiliaji wa ugonjwa huu kupitia kwa Wataalamu wa Afya katika
Mikoa, Wilaya na maeneo ya mipaka. Aidha watalaamu hawa wa Afya pia wanatoa
elimu kwa wananchi kuhusu dalili za ugonjwa huu ili endapo ugonjwa huo utatokea
uweze kutolewa taarifa mapema.
o Kupeleka vifaa kinga kwa ajili ya watumishi wa afya
Wananchi wanashauriwa kutokuwa na hofu kwani mpaka sasa hakuna mgonjwa
yeyote aliyeripotiwa nchini. Wananchi wanashauriwa kutoa taarifa kwenye kituo
cha huduma za afya kilicho karibu mara watakapoona mgonjwa yeyote atakayehisiwa
kuwa na dalili za ugonjwa huu.
Kitengo cha mawasiliano ya Serikali
Nashindwa kuelewa, mbona haya magonjwa hatari sana yanatokea Uganda??? Chanzo chake huko Uganda ni nini na kwa nini kisidhibitiwe kwa ushirikiano na nchi mbali mbali, hasa nchi jirani???
ReplyDeletewashausambaza wazungu ungonjwa huu sehemu kibao ambazo wanataka kuzi tawala kiuchumi kwa husda ya kuona uchumi upo
ReplyDeletehajishangainga waifrika kila siku sisi na kila kibaya ni chetu chao ni kizuri toka lini mkasikai magonjwa haya jeulizeni?
africa ni nchi tajiri kuliko zote duniani na wazungu na wenginewe wanakodolea macho uchumi wenu
kalaba bao kaeni hivyo hivyo kujiharibu akilizenu kwa mipombe na mibangi na madawa ya kulevyaa wenzenu pia wanataka mharibikiwe ili watukawaleni daimi maishani
poleni sana ugonjwa huu umeshafika tanzania chunguzeni mtaona kama nakudanganyeni
Lohhh kwa misongamano yetu Mijini hapa Afrika ya Mashariki ktk Masoko, kama Vivuko vya Feri kwenda Kigamboni rundo la watu, vyombo vya Usafiri kama mabasi makubwa ya Mchina njia za Mbagala, Gongo la Mboto na Tegeta, tutakiwisha sana dude hili likiingia Tanzania!
ReplyDeleteMUNGU TUSAIDIE!!!