Habari kutoka Dodoma zinasema Mbunge wa Kasulu Mjini kupitia chama cha NCCR-Mageuzi, Mhe. Moses Machali (pichani), amelazwa katika hospitali ya mkoa ya Dodoma kuuguza majeraha aliyoyapata baada ya kushambuliwa na watu wasiojulikana usiku wa kuamkia leo mjini Dodoma.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi na Mbunge wa kuteuliwa, Mhe James Mbatia, watu takriban wanane hivi walimshambulia Mhe Machali mnamo saa mbili za usiku akielekea kupumzika baada ya kuhudhuria vikao vya Bunge.
Mhe Mbatia amesema leo mjini Dodoma kwamba amemtembelea Mhe. Machali asubuhi hii na kumkuta anaendelea vyema na matibabu.
Habari zaidi tutawaletea kwa kadri zitapopatikana.
Sitashangaa hapo tukiambiwa amejipiga mwenyewe! TUMEFIKA MAHALI YAANI HATA HAIFAHAMIKI MWENYE DHAMANA YA KULINDA WANANCHI NI NANI.
ReplyDeletePOLE MBUNGE
Mdau nakubaliana na wewe kabisa, baadhi ya watu wamekuwa si wakweli na hawayazungumzi ya ukweeli kabisa. Baadhi ya viongozi sikuhizi ni MAJANGAZ kabisa. visa vingi, wanapenda sifa, wanapenda kukejeli, wanapenda kusujudiwa na wana penda kuonewa huruma badala ya kuleta maendeleo nchini. POLE MBUNGE.
ReplyDelete