Makao Makuu ya kituo cha habari na mawasiliano cha Redio ya jamii Sengerema Fm mkoani Mwanza kunakofanyika warsha ya wiki moja kwa redio za jamii nchini kwa ajili ya kuziandaa kuhubiri mijadala ya Amani na Demokrasia kuelekea uchaguzi wa mwaka 2015.
Meneja wa Kituo cha Habari na Mawasiliano cha Radio Sengerema mkoani Mwanza Bw. Felician Ncheye akiwakaribisha na kuwatambulisha wawezeshaji kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sayansi na Utamaduni (UNESCO) kwa Wakurugenzi na Mameneja wa redio za jamii nchini wanaohudhuria warsha ya wiki moja iliyoandaliwa na UNESCO kupitia mradi wa DEP kwa ajili ya kuwaanda kuhubiri mijadala ya Amani na Demokrasia kwa jamii kuelekea uchaguzi wa mwaka 2015.
Afisa Mipango Taifa wa Kitengo cha Mawasiliano na Habari UNESCO Yusuph Al Amin akizungumza na mameneja , wakurgenzi wa redio za jamii Tanzania nchini katika warsha ya wiki moja juu ya matayarisho ya mradi wa kuhubiri mijadala ya Amani na Demokrasia kwa jamii kuelekea uchaguzi wa mwaka 2015.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...