Timu ya Copa Coca-Cola iliyoshiriki katika michuano ya kimataifa ya Copa Coca-Cola nchini Afrika Kusini
wiki iliyopita ikiwasili kwenye Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam
Jumatatu jioni. Timu hiyo ilitolewa katika hatua ya makundi na Zimbabwe kuibuka mabingwa.
Afisa maendeleo wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Salum Madadi akiipokea timu ya vijana
ya Copa Coca-Cola iliyoshiriki katika michuano ya kimataifa ya Copa Coca-Cola nchini Afrika Kusini wiki
iliyopita. Timu hiyo ilitolewa katika hatua ya makundi na Zimbabwe kuibuka mabingwa.
Zimbabwe waliibuka mabingwa wa 2013 wa mashindano ya kimataifa ya COPA Coca-Cola kwa
kuwafunga Uganda 3-0 katika mchezo wa fainali iliyochezwa High Performance Center, Pretoria, Afrika
Kusini.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...