Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh. Paul Makonda akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam leo wakati alipozungumzia mpango wa kuwasafirishwa walimu bure jijini Dar es salaam wakati wa kwenda na kurudi kazini huku akiwa ameongozana na viongozi wa vyama vya usafirishaji wa abiria jijini Dar es salaam pamoja na viongozi wa Madereva wa Daladala jijini Dar es salaam.(Picha na Geofrey Adroph wa Pamoja Blog)
Mwenyekiti wa Chama Chama Wamiliki wa Daladala Mkoa wa Dar es salaam, Said Mabrouk(wa kwanza kushoto) akizungumzia mwitikio wa wamiliki hao kuhusu kuwasafirisha walimu ili kuunga mkono juhudi za Mkuu wa Wilaya ya Konondoni Mh. Paul makonda na Rais Dk. John Pombe Magufuli katika kutoa elimu bure hapa nchini, kutoka kulia ni Makamu mwenyekiti wa Umoja wa Madereva, Shabani Mdemu, wa pili kutoka kulia ni Mwenyekiti wa Umoja wa Wasafirishaji abiria Dar es Salaam, (UWADAR),William Masanja.
Mwenyekiti wa Umoja wa Wasafirishaji abiria Dar es Salaam, (UWADAR),William Masanja akizungumza na waandishi wa habari leo jijinni Dar es Salaam.
Baadhi ya waandishi wa habari wakiwa kazini

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.

WALIMU wa Shule ya Msingi na Sekondari Mkoa wa Dar es Salaam watasafiri na Daladala bure kuanzia Machi  7 mwaka huu.

Akizungumza na waadishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda amesema kuwa kutokana na changamoto za walimu ameona kuna umuhimu wao kusafiri bure waweze kupunguza makali ya nauli za kila siku wanapopanda daladala hizo.

Amesema kuwa walimu watasafiri kwa  usafiri huo kuanzia saa 11:30 hadi saa 2 kwa muda wa asubuhi na baada ya muda huo kupita watalipa nauli zao na nyakati za jioni watarudi majumbani mwao kwa kupanda daladala hizo kuanzia saa 9 hadi saa 12.Makonda amesema kuanzia kesho watatengeneza vitambulisho vya walimu wote wa serikali wa mkoa wa Dar es Salaam ambavyo wataonyesha kwa makondakta wa daladala vikiwa na saini ya mkuu mkuu wa Wilaya.

Amesema utaratibu huo utakuwa ukitumika kwa siku za kazi tu kwa walimu kupanda bure na sio vinginevyo na walimu wanaoishi mikoa mingine na wanafundisha Dar es Salaam watalipa nauli zao kufika katika vituo vyao vya kazi.

Aidha amesema kuwa walimu wataingia katika Daladala wasiopungua wawili na wengine watasubiri daladala zingingine kutokana na maoni ya wamliki wa vyombo vya usafiri.Nae Mwenyekiti wa Umoja wa Wamiliki wa Daladala Mkoa wa Dar es Salaam, Sabri Mabroock amesema kuwa wanaunga mkono sera ya elimu ya Rais  Dk.John Pombe Magufuli.

Amesema walimu wamekuwa na changamoto wakati mwingine wanashindwa kulipa hata nauli hivyo kupanda  bure watakuwa wamerahisisha maisha.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Nami naunga mkono. Ila tutawatambuaje? Uniform au ID tuu?

    ReplyDelete
  2. ila askari wote walipe. wao wana mishahara mikubwa wanaweza kumudu usafiri na pia wana mabasi yao na pikipiki, golf, n.k. walimu hawana vitu hivyo.

    ReplyDelete
  3. Credit to you Makonda. No wonder the president has complete confidence in you. Well done.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...