Jumuiya ya kimataifa ya hali ya hewa duniani kote inaadhimisha Siku ya Hali ya Hewa Duniani, ikiwa ni Siku ya kumbukumbu ya kuanzishwa kwa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) tarehe 23 Machi 1950. Tanzania pamoja na wanachama wengine 190 wa Shirika hili inaungana na jumuiya ya kimataifa kusherehekea siku hii kwa kuonesha mchango wa huduma za hali ya hewa katika kulinda usalama wa jamii.

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) ilianzishwa mnamo Desemba, 1999 baada ya Serikali kuchukua uamuzi wa kuboresha utoaji wa huduma kwa sekta mbali mbali muhimu chini ya sheria ya Wakala wa Serikali No. 30 ya 1997. Kabla ya TMA huduma hizi zilikuwa zikitolewa na iliyokuwa Idara Kuu ya Hali ya Hewa (DoM) chini ya iliyokuwa Wizara ya Mawasiliano na Uchukuzi. 

Katika kusherehekea Siku ya Hali ya Hewa Duniani ni desturi kuwa na kaulimbiu ya maadhimisho ya kila mwaka, hivyo kwa mwaka huu kaulimbiu ya maadhimisho haya ni “ Joto kali, Ukame, Mafuriko; Kabiliana na Mabadiliko”-“Hotter, Drier, Wetter - Face the Future’.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania Dkt. Agnes Kijazi akiwa sambamba na baadhi ya wafanyakazi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini, wakipanda miti katika eneo la TMA lililopo Sinza (kituo cha Simu 2000). Zoezi hili limefanyika katika maeneo ya mikoa yote nchini kupitia Ofisi za TMA na Wakala wa Misitu Tanzania Tarehe 23 Machi 2016.

 Kaulimbiu hii ni ya muhimu kwa kipindi hiki ambacho jamii nyingi nchini Tanzania na kwingineko duniani wanakabiliana na matukio ya hali mbaya ya hewa ikiwa ni pamoja na kuongezeka kwa joto kupita wastani na kubadilika kwa mifumo na misimu ya mvua. Hali hii ni dhahiri kwani jamii zetu nyingi zimeathirika kwa namna moja au nyingine kutokana na matukio haya ya hali mbaya ya hewa ambayo tafiti za kisayansi zimeyahusisha na mabadiliko ya hali ya hewa na tabia nchi.
 
Katika miongo ya hivi karibuni, mabadiliko ya hali ya hewa yameathiri mifumo ya asili na ya kibinadamu katika nchi nyingi. Mabadiliko ya matukio ya hali mbaya ya hewa ya muda mfupi na mrefu nidhahiri na hali hii inakaribia kuzoeleka na kuwa kama wastani mpya wa hali ya hewa katika nchi nyingi ikiwa pamoja na Tanzania. 

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania Dkt. Agnes Kijazi akipanda mti katika eneo la TMA lililopo Sinza (kituo cha Simu 2000). Zoezi hili limefanyika katika maeneo ya mikoa yote nchini kupitia Ofisi za TMA na Wakala wa Misitu Tanzania Tarehe 23 Machi 2016.

Katika miaka ya hivi karibuni Tanzania imeshuhudia athari za maafa yanayosababishwa na mabadiliko haya ya hali ya hewa yakiwa na sura mbalimbali. Mfano, tokea maadhimisho ya siku ya hali ya hewa ya mwaka uliopita tumeshuhudia matukio yaliyosababisha maafa yaliyotokana na mafuriko kwa mfano Mikoa ya kati ya nchi ambapo baadhi ya watu walipoteza maisha pamoja na mifugo na uharibifu wa mali. 

BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...