Kaimu Balozi wa Ubalozi wa Tanzania Roma nchini Italia, Bw. Salvator Marcus Mbilinyi (kushoto) akikabidhiwa baiskeli maalum za watu wenye ulemavu (wheelchairs) 100 (mia moja) kwa ajili ya watu wenye ulemavu nchini kutoka kwa Bw. Ziya Karahan, Konseli wa Heshima wa Tanzania mjini Istanbul, Uturuki. Baiskeli hizo zimepatikana kufutia mazungumzo kati ya Ubalozi na Konseli wa Heshima kuhusu njia za kuvipata vifaa hivyo ili kuwasaidia watanzania wenye ulemavu na hivyo kufanikiwa kupata 100. Baada ya makabidhiano hayo vifaa hivyo vitasafirishwa mara moja kwenda nchini Tanzania kwa ajili ya matumizi husika.
Home
Unlabelled
UBALOZI WA TANZANIA MJINI ROMA KUSAFIRISHA WHEELCHAIRS 100 KWA AJILI YA WATU WENYE ULEMAVU
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...