Kaimu Balozi wa Ubalozi wa Tanzania Roma nchini Italia, Bw. Salvator Marcus Mbilinyi (kushoto) akikabidhiwa baiskeli maalum za watu wenye ulemavu (wheelchairs) 100 (mia moja) kwa ajili ya watu wenye ulemavu nchini kutoka kwa Bw. Ziya Karahan, Konseli wa Heshima wa Tanzania mjini Istanbul, Uturuki. Baiskeli  hizo zimepatikana kufutia mazungumzo kati ya Ubalozi na Konseli wa Heshima kuhusu njia za kuvipata vifaa hivyo ili kuwasaidia watanzania wenye ulemavu na hivyo kufanikiwa kupata 100. Baada ya makabidhiano hayo vifaa hivyo vitasafirishwa mara moja kwenda nchini Tanzania kwa ajili ya matumizi husika.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...